1st Ayah 1 الأية ١الأوليبِسْم ِ اللهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ
الم
Swahili
Alif Lam Mim (A.L.M.)
|
Ayah 31:2 الأية
تِلْكَ آيَاتُ الْكِتَابِ الْحَكِيمِ
Swahili
Hizi ni Aya za Kitabu chenye hikima.
|
Ayah 31:3 الأية
هُدًى وَرَحْمَةً لِّلْمُحْسِنِينَ
Swahili
Kuwa ni Uwongofu na Rehema kwa wafanyao wema,
|
Ayah 31:4 الأية
الَّذِينَ يُقِيمُونَ الصَّلَاةَ وَيُؤْتُونَ الزَّكَاةَ وَهُم بِالْآخِرَةِ هُمْ
يُوقِنُونَ
Swahili
Wanao shika Sala, na wanatoa Zaka, nao wana yakini na Akhera.
|
Ayah 31:5 الأية
أُولَٰئِكَ عَلَىٰ هُدًى مِّن رَّبِّهِمْ ۖ وَأُولَٰئِكَ هُمُ الْمُفْلِحُونَ
Swahili
Hao ndio walio na uwongofu utokao kwa Mola wao Mlezi, na hao ndio wenye
kufanikiwa.
|
Ayah 31:6 الأية
وَمِنَ النَّاسِ مَن يَشْتَرِي لَهْوَ الْحَدِيثِ لِيُضِلَّ عَن سَبِيلِ اللهِ
بِغَيْرِ عِلْمٍ وَيَتَّخِذَهَا هُزُوًا ۚ أُولَٰئِكَ لَهُمْ عَذَابٌ مُّهِينٌ
Swahili
Na miongoni mwa watu wapo wanao nunua maneno ya upuuzi, ili wawapoteze watu na
njia ya Mwenyezi Mungu pasipo kujua, na wanaichukulia ni maskhara. Hao watapata
adhabu ya kuwafedhehesha.
|
Ayah 31:7 الأية
وَإِذَا تُتْلَىٰ عَلَيْهِ آيَاتُنَا وَلَّىٰ مُسْتَكْبِرًا كَأَن لَّمْ
يَسْمَعْهَا كَأَنَّ فِي أُذُنَيْهِ وَقْرًا ۖ فَبَشِّرْهُ بِعَذَابٍ أَلِيمٍ
Swahili
Na (mtu kama huyo) anapo somewa Aya zetu huzipa mgongo kwa kujivuna, kama kwamba
hakuzisikia, kama kwamba masikioni mwake mna uziwi. Basi mbashirie kuwa atapata
adhabu chungu.
|
Ayah 31:8 الأية
إِنَّ الَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ لَهُمْ جَنَّاتُ النَّعِيمِ
Swahili
Hakika walio amini na wakatenda mema watakuwa nazo Bustani za neema.
|
Ayah 31:9 الأية
خَالِدِينَ فِيهَا ۖ وَعْدَ اللهِ حَقًّا ۚ وَهُوَ الْعَزِيزُ الْحَكِيمُ
Swahili
Watadumu humo - ni ahadi ya Mwenyezi Mungu ya kweli. Na Yeye ndiye Mwenye nguvu,
Mwenye hikima.
|
Ayah 31:10 الأية
خَلَقَ السَّمَاوَاتِ بِغَيْرِ عَمَدٍ تَرَوْنَهَا ۖ وَأَلْقَىٰ فِي الْأَرْضِ
رَوَاسِيَ أَن تَمِيدَ بِكُمْ وَبَثَّ فِيهَا مِن كُلِّ دَابَّةٍ ۚ وَأَنزَلْنَا
مِنَ السَّمَاءِ مَاءً فَأَنبَتْنَا فِيهَا مِن كُلِّ زَوْجٍ كَرِيمٍ
Swahili
Ameziumba mbingu bila ya nguzo mnazo ziona; na ameweka katika ardhi milima ili
ardhi isikuyumbisheni; na ametawanya humo kila namna ya wanyama; na tumeteremsha
maji kutoka mbinguni, na tukaotesha katika ardhi mimea mizuri ya kila namna.
|
Ayah 31:11 الأية
هَٰذَا خَلْقُ اللهِ فَأَرُونِي مَاذَا خَلَقَ الَّذِينَ مِن دُونِهِ ۚ بَلِ
الظَّالِمُونَ فِي ضَلَالٍ مُّبِينٍ
Swahili
Huu ni uumbaji wa Mwenyezi Mungu. Basi nionyesheni wameumba nini hao wasio kuwa
Yeye! Lakini madhaalimu wamo katika upotovu uliyo dhaahiri.
|
Ayah 31:12 الأية
وَلَقَدْ آتَيْنَا لُقْمَانَ الْحِكْمَةَ أَنِ اشْكُرْ لِلَّهِ ۚ وَمَن يَشْكُرْ
فَإِنَّمَا يَشْكُرُ لِنَفْسِهِ ۖ وَمَن كَفَرَ فَإِنَّ اللهَ غَنِيٌّ حَمِيدٌ
Swahili
Na tulimpa Luqman hikima, tukamwambia: Mshukuru Mwenyezi Mungu. Na mwenye
kushukuru basi hakika anashukuru kwa manufaa ya nafsi yake. Na aliye kufuru,
basi Mwenyezi Mungu ni Mkwasi, Msifiwa.
|
Ayah 31:13 الأية
وَإِذْ قَالَ لُقْمَانُ لِابْنِهِ وَهُوَ يَعِظُهُ يَا بُنَيَّ لَا تُشْرِكْ
بِاللهِ ۖ إِنَّ الشِّرْكَ لَظُلْمٌ عَظِيمٌ
Swahili
Na Luqman alipo mwambia mwanawe kwa kumpa mawaidha: Ewe mwanangu! Usimshirikishe
Mwenyezi Mungu. Kwani hakika ushirikina bila ya shaka ni dhulma iliyo kubwa.
|
Ayah 31:14 الأية
وَوَصَّيْنَا الْإِنسَانَ بِوَالِدَيْهِ حَمَلَتْهُ أُمُّهُ وَهْنًا عَلَىٰ وَهْنٍ
وَفِصَالُهُ فِي عَامَيْنِ أَنِ اشْكُرْ لِي وَلِوَالِدَيْكَ إِلَيَّ الْمَصِيرُ
Swahili
Na tumemuusia mtu kwa wazazi wake wawili. Mama yake ameichukua mimba yake kwa
udhaifu juu ya udhaifu, na kumwachisha ziwa baada ya miaka miwili. (Tumemuusia):
Nishukuru Mimi na wazazi wako. Ni kwangu Mimi ndiyo marudio.
|
Ayah 31:15 الأية
وَإِن جَاهَدَاكَ عَلَىٰ أَن تُشْرِكَ بِي مَا لَيْسَ لَكَ بِهِ عِلْمٌ فَلَا
تُطِعْهُمَا ۖ وَصَاحِبْهُمَا فِي الدُّنْيَا مَعْرُوفًا ۖ وَاتَّبِعْ سَبِيلَ مَنْ
أَنَابَ إِلَيَّ ۚ ثُمَّ إِلَيَّ مَرْجِعُكُمْ فَأُنَبِّئُكُم بِمَا كُنتُمْ
تَعْمَلُونَ
Swahili
Na pindi wakikushikilia kunishirikisha na ambayo huna ilimu nayo, basi
usiwat'ii. Lakini kaa nao kwa wema duniani, nawe ishike njia ya anaye elekea
kwangu. Kisha marejeo yenu ni kwangu Mimi, na Mimi nitakuambieni mliyo kuwa
mkiyatenda.
|
Ayah 31:16 الأية
يَا بُنَيَّ إِنَّهَا إِن تَكُ مِثْقَالَ حَبَّةٍ مِّنْ خَرْدَلٍ فَتَكُن فِي
صَخْرَةٍ أَوْ فِي السَّمَاوَاتِ أَوْ فِي الْأَرْضِ يَأْتِ بِهَا اللهُ ۚ إِنَّ
اللهَ لَطِيفٌ خَبِيرٌ
Swahili
Ewe mwanangu! Kikiwapo kitu cha uzito wa chembe ya khardali kikawa ndani ya
jabali au ndani ya mbingu au ndani ya ardhi, basi Mwenyezi Mungu atakileta.
Hakika Mwenyezi Mungu ni Mjuzi wa yaliyo fichika, Mwenye khabari za yote.
|
Ayah 31:17 الأية
يَا بُنَيَّ أَقِمِ الصَّلَاةَ وَأْمُرْ بِالْمَعْرُوفِ وَانْهَ عَنِ الْمُنكَرِ
وَاصْبِرْ عَلَىٰ مَا أَصَابَكَ ۖ إِنَّ ذَٰلِكَ مِنْ عَزْمِ الْأُمُورِ
Swahili
Ewe mwanangu! Shika Sala, na amrisha mema, na kataza maovu, na subiri kwa yanayo
kupata. Hayo ni katika mambo ya kuazimiwa..
|
Ayah 31:18 الأية
وَلَا تُصَعِّرْ خَدَّكَ لِلنَّاسِ وَلَا تَمْشِ فِي الْأَرْضِ مَرَحًا ۖ إِنَّ
اللهَ لَا يُحِبُّ كُلَّ مُخْتَالٍ فَخُورٍ
Swahili
Wala usiwabeuwe watu, wala usitembee katika nchi kwa maringo. Hakika Mwenyezi
Mungu hampendi kila anaye jivuna na kujifakhirisha.
|
Ayah 31:19 الأية
وَاقْصِدْ فِي مَشْيِكَ وَاغْضُضْ مِن صَوْتِكَ ۚ إِنَّ أَنكَرَ الْأَصْوَاتِ
لَصَوْتُ الْحَمِيرِ
Swahili
Na ushike mwendo wa katikati, na teremsha sauti yako. Hakika katika sauti mbaya
zote bila ya shaka iliyo zidi ni sauti ya punda.
|
Ayah 31:20 الأية
أَلَمْ تَرَوْا أَنَّ اللهَ سَخَّرَ لَكُم مَّا فِي السَّمَاوَاتِ وَمَا فِي
الْأَرْضِ وَأَسْبَغَ عَلَيْكُمْ نِعَمَهُ ظَاهِرَةً وَبَاطِنَةً ۗ وَمِنَ النَّاسِ
مَن يُجَادِلُ فِي اللهِ بِغَيْرِ عِلْمٍ وَلَا هُدًى وَلَا كِتَابٍ مُّنِيرٍ
Swahili
Kwani hamwoni ya kwamba Mwenyezi Mungu amevifanya vikutumikieni viliomo mbinguni
na kwenye ardhi, na akakujalizieni neema zake, za dhaahiri na za siri? Na
miongoni mwa watu wapo wanao bishana juu ya Mwenyezi Mungu pasipo ilimu, wala
uwongofu, wala Kitabu chenye nuru.
|
Ayah 31:21 الأية
وَإِذَا قِيلَ لَهُمُ اتَّبِعُوا مَا أَنزَلَ اللهُ قَالُوا بَلْ نَتَّبِعُ مَا
وَجَدْنَا عَلَيْهِ آبَاءَنَا ۚ أَوَلَوْ كَانَ الشَّيْطَانُ يَدْعُوهُمْ إِلَىٰ
عَذَابِ السَّعِيرِ
Swahili
Na wanapo ambiwa: Fuateni aliyo yateremsha Mwenyezi Mungu, husema: Bali
tunafuata tuliyo wakuta nayo baba zetu. Je! Ijapo kuwa Shet'ani anawaita kwenye
adhabu ya Moto uwakao?
|
Ayah 31:22 الأية
وَمَن يُسْلِمْ وَجْهَهُ إِلَى اللهِ وَهُوَ مُحْسِنٌ فَقَدِ اسْتَمْسَكَ
بِالْعُرْوَةِ الْوُثْقَىٰ ۗ وَإِلَى اللهِ عَاقِبَةُ الْأُمُورِ
Swahili
Na mwenye kuuelekeza uso wake kwa Mwenyezi Mungu, naye akawa anafanya wema, basi
huyo hakika amekwisha kamata fundo lilio madhubuti. Na mwisho wa mambo yote ni
kwa Mwenyezi Mungu.
|
Ayah 31:23 الأية
وَمَن كَفَرَ فَلَا يَحْزُنكَ كُفْرُهُ ۚ إِلَيْنَا مَرْجِعُهُمْ فَنُنَبِّئُهُم
بِمَا عَمِلُوا ۚ إِنَّ اللهَ عَلِيمٌ بِذَاتِ الصُّدُورِ
Swahili
Na anaye kufuru, isikuhuzunishe kufuru yake. Kwetu ndio marudio yao, na hapo
tutawaambia waliyo yatenda. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mjuzi wa yaliyomo vifuani.
|
Ayah 31:24 الأية
نُمَتِّعُهُمْ قَلِيلًا ثُمَّ نَضْطَرُّهُمْ إِلَىٰ عَذَابٍ غَلِيظٍ
Swahili
Tunawastarehesha kwa uchache, kisha tutawasukuma kwenye adhabu ngumu.
|
Ayah 31:25 الأية
وَلَئِن سَأَلْتَهُم مَّنْ خَلَقَ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضَ لَيَقُولُنَّ اللهُ
ۚ قُلِ الْحَمْدُ لِلَّهِ ۚ بَلْ أَكْثَرُهُمْ لَا يَعْلَمُونَ
Swahili
Na ukiwauliza: Nani aliye ziumba mbingu na ardhi? Bila ya shaka watasema:
Mwenyezi Mungu. Wewe sema: Alhamdulillahi! Sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu.
Lakini wengi wao hawajui.
|
Ayah 31:26 الأية
لِلَّهِ مَا فِي السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ ۚ إِنَّ اللهَ هُوَ الْغَنِيُّ
الْحَمِيدُ
Swahili
Ni vya Mwenyezi Mungu vyote viliomo mbinguni na katika ardhi. Hakika Mwenyezi
Mungu ndiye Mkwasi, Mwenye kusifiwa.
|
Ayah 31:27 الأية
وَلَوْ أَنَّمَا فِي الْأَرْضِ مِن شَجَرَةٍ أَقْلَامٌ وَالْبَحْرُ يَمُدُّهُ مِن
بَعْدِهِ سَبْعَةُ أَبْحُرٍ مَّا نَفِدَتْ كَلِمَاتُ اللهِ ۗ إِنَّ اللهَ
عَزِيزٌ حَكِيمٌ
Swahili
Na lau kuwa miti yote iliyomo duniani ikawa ni kalamu, na bahari (ikawa wino),
na ikaongezewa juu yake bahari nyengine saba, maneno ya Mwenyezi Mungu yasingeli
kwisha. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye nguvu, Mwenye hikima.
|
Ayah 31:28 الأية
مَّا خَلْقُكُمْ وَلَا بَعْثُكُمْ إِلَّا كَنَفْسٍ وَاحِدَةٍ ۗ إِنَّ اللهَ
سَمِيعٌ بَصِيرٌ
Swahili
Hakukuwa kuumbwa kwenu, wala kufufuliwa kwenu ila ni kama nafsi moja tu. Hakika
Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusikia Mwenye kuona.
|
Ayah 31:29 الأية
أَلَمْ تَرَ أَنَّ اللهَ يُولِجُ اللَّيْلَ فِي النَّهَارِ وَيُولِجُ النَّهَارَ
فِي اللَّيْلِ وَسَخَّرَ الشَّمْسَ وَالْقَمَرَ كُلٌّ يَجْرِي إِلَىٰ أَجَلٍ
مُّسَمًّى وَأَنَّ اللهَ بِمَا تَعْمَلُونَ خَبِيرٌ
Swahili
Kwani huoni kwamba Mwenyezi Mungu huuingiza usiku katika mchana, na huuingiza
mchana katika usiku, na amedhalilisha jua na mwezi? Vyote hivyo vinakwenda mpaka
wakati ulio wekwa. Na Mwenyezi Mungu anazo khabari za mnayo yatenda.
|
Ayah 31:30 الأية
ذَٰلِكَ بِأَنَّ اللهَ هُوَ الْحَقُّ وَأَنَّ مَا يَدْعُونَ مِن دُونِهِ
الْبَاطِلُ وَأَنَّ اللهَ هُوَ الْعَلِيُّ الْكَبِيرُ
Swahili
Hivi ni kwa sababu hakika Mwenyezi Mungu ndiye wa kweli, na hakika wanacho
kiomba ni cha uwongo. Na kwamba hakika Mwenyezi Mungu ndiye Mtukufu na ndiye
Mkubwa.
|
Ayah 31:31 الأية
أَلَمْ تَرَ أَنَّ الْفُلْكَ تَجْرِي فِي الْبَحْرِ بِنِعْمَتِ اللهِ لِيُرِيَكُم
مِّنْ آيَاتِهِ ۚ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَاتٍ لِّكُلِّ صَبَّارٍ شَكُورٍ
Swahili
Kwani huoni kwamba marikebu hupita baharini zikichukua neema za Mwenyezi Mungu,
ili kukuonyesheni baadhi ya Ishara zake? Hakika katika haya zipo Ishara kwa kila
mwenye kusubiri, mwenye kushukuru.
|
Ayah 31:32 الأية
وَإِذَا غَشِيَهُم مَّوْجٌ كَالظُّلَلِ دَعَوُا اللهَ مُخْلِصِينَ لَهُ الدِّينَ
فَلَمَّا نَجَّاهُمْ إِلَى الْبَرِّ فَمِنْهُم مُّقْتَصِدٌ ۚ وَمَا يَجْحَدُ
بِآيَاتِنَا إِلَّا كُلُّ خَتَّارٍ كَفُورٍ
Swahili
Na wimbi linapo wafunika kama wingu, wao humwomba Mwenyezi Mungu kwa kumsafia
dini. Lakini anapo waokoa wakafika nchi kavu, wapo baadhi yao huenda mwendo wa
sawa. Wala hazikanushi Ishara zetu ila aliye khaini kafiri mkubwa.
|
Ayah 31:33 الأية
يَا أَيُّهَا النَّاسُ اتَّقُوا رَبَّكُمْ وَاخْشَوْا يَوْمًا لَّا يَجْزِي وَالِدٌ
عَن وَلَدِهِ وَلَا مَوْلُودٌ هُوَ جَازٍ عَن وَالِدِهِ شَيْئًا ۚ إِنَّ وَعْدَ
اللهِ حَقٌّ ۖ فَلَا تَغُرَّنَّكُمُ الْحَيَاةُ الدُّنْيَا وَلَا يَغُرَّنَّكُم
بِاللهِ الْغَرُورُ
Swahili
Enyi watu! Mcheni Mola wenu Mlezi, na iogopeni siku ambayo mzazi hatamfaa mwana,
wala mwana hatamfaa mzazi kwa lolote. Hakika ahadi ya Mwenyezi Mungu ni ya
kweli. Basi yasikudanganyeni maisha ya dunia, wala asikudanganyeni na Mwenyezi
Mungu mdanganyifu.
|
Ayah 31:34 الأية
إِنَّ اللهَ عِندَهُ عِلْمُ السَّاعَةِ وَيُنَزِّلُ الْغَيْثَ وَيَعْلَمُ مَا فِي
الْأَرْحَامِ ۖ وَمَا تَدْرِي نَفْسٌ مَّاذَا تَكْسِبُ غَدًا ۖ وَمَا تَدْرِي
نَفْسٌ بِأَيِّ أَرْضٍ تَمُوتُ ۚ إِنَّ اللهَ عَلِيمٌ خَبِيرٌ
Swahili
Hakika kuijua Saa (ya Kiyama) kuko kwa Mwenyezi Mungu. Na Yeye ndiye anaye
iteremsha mvua. Na anavijua viliomo ndani ya matumbo ya uzazi. Na haijui nafsi
yoyote itachuma nini kesho. Wala nafsi yoyote haijui itafia nchi gani. Hakika
Mwenyezi Mungu ndiye Mwenye kujua, Mwenye khabari.
|
©
EsinIslam.Com Designed & produced by The Awqaf London. Please pray for us
|