Prev  

52. Surah At-Tûr سورة الطور

  Next  




Ayah  52:1  الأية
    +/- -/+  
بِسْم ِ اللهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ






Ayah  52:7  الأية
    +/- -/+  
إِنَّ عَذَابَ رَبِّكَ لَوَاقِعٌ
Swahili
 
Hakika adhabu ya Mola wako Mlezi hapana shaka itatokea.


Ayah  52:9  الأية
    +/- -/+  
يَوْمَ تَمُورُ السَّمَاءُ مَوْرًا
Swahili
 
Siku zitakapo tikisika mbingu kwa mtikiso,

Ayah  52:10  الأية
    +/- -/+  

Ayah  52:11  الأية
    +/- -/+  
فَوَيْلٌ يَوْمَئِذٍ لِّلْمُكَذِّبِينَ
Swahili
 
Basi ole wao siku hiyo hao wanao kadhibisha,

Ayah  52:12  الأية
    +/- -/+  
الَّذِينَ هُمْ فِي خَوْضٍ يَلْعَبُونَ
Swahili
 
Ambao wanacheza katika mambo ya upuuzi.

Ayah  52:13  الأية
    +/- -/+  
يَوْمَ يُدَعُّونَ إِلَىٰ نَارِ جَهَنَّمَ دَعًّا
Swahili
 
Siku watapo sukumwa kwenye Moto kwa msukumo wa nguvu,

Ayah  52:14  الأية
    +/- -/+  
هَٰذِهِ النَّارُ الَّتِي كُنتُم بِهَا تُكَذِّبُونَ
Swahili
 
(Waambiwe): Huu ndio ule Moto mlio kuwa mkiukanusha!

Ayah  52:15  الأية
    +/- -/+  
أَفَسِحْرٌ هَٰذَا أَمْ أَنتُمْ لَا تُبْصِرُونَ
Swahili
 
Je! Huu ni uchawi, au hamwoni tu?

Ayah  52:16  الأية
    +/- -/+  
اصْلَوْهَا فَاصْبِرُوا أَوْ لَا تَصْبِرُوا سَوَاءٌ عَلَيْكُمْ ۖ إِنَّمَا تُجْزَوْنَ مَا كُنتُمْ تَعْمَلُونَ
Swahili
 
Uingieni, mkistahamili au msistahamili - ni mamoja kwenu. Hakika mnalipwa kwa mliyo kuwa mkiyatenda.

Ayah  52:17  الأية
    +/- -/+  
إِنَّ الْمُتَّقِينَ فِي جَنَّاتٍ وَنَعِيمٍ
Swahili
 
Hakika wachamngu watakuwa katika Mabustani na neema,

Ayah  52:18  الأية
    +/- -/+  
فَاكِهِينَ بِمَا آتَاهُمْ رَبُّهُمْ وَوَقَاهُمْ رَبُّهُمْ عَذَابَ الْجَحِيمِ
Swahili
 
Wakifurahi kwa yale aliyo wapa Mola wao Mlezi. Na Mola wao Mlezi atawalinda na adhabu ya Motoni.

Ayah  52:19  الأية
    +/- -/+  
كُلُوا وَاشْرَبُوا هَنِيئًا بِمَا كُنتُمْ تَعْمَلُونَ
Swahili
 
Kuleni na kunyweni kwa raha kabisa kwa sababu ya mliyo kuwa mkiyatenda.

Ayah  52:20  الأية
    +/- -/+  
مُتَّكِئِينَ عَلَىٰ سُرُرٍ مَّصْفُوفَةٍ ۖ وَزَوَّجْنَاهُم بِحُورٍ عِينٍ
Swahili
 
Watakuwa wameegemea juu ya viti vya enzi vilivyo pangwa kwa safu. Na tutawaoza mahuru-l-aini.

Ayah  52:21  الأية
    +/- -/+  
وَالَّذِينَ آمَنُوا وَاتَّبَعَتْهُمْ ذُرِّيَّتُهُم بِإِيمَانٍ أَلْحَقْنَا بِهِمْ ذُرِّيَّتَهُمْ وَمَا أَلَتْنَاهُم مِّنْ عَمَلِهِم مِّن شَيْءٍ ۚ كُلُّ امْرِئٍ بِمَا كَسَبَ رَهِينٌ
Swahili
 
Na walio amini na dhuriya zao wakawafuata kwa Imani tutawakutanisha nao dhuriya zao, na wala hatutawapunja hata kidogo katika vitendo vyao. Kila mtu lazima atapata alicho kichuma.

Ayah  52:22  الأية
    +/- -/+  
وَأَمْدَدْنَاهُم بِفَاكِهَةٍ وَلَحْمٍ مِّمَّا يَشْتَهُونَ
Swahili
 
Na tutawapa matunda, na nyama kama watavyo penda.

Ayah  52:23  الأية
    +/- -/+  
يَتَنَازَعُونَ فِيهَا كَأْسًا لَّا لَغْوٌ فِيهَا وَلَا تَأْثِيمٌ
Swahili
 
Watapeana humo bilauri zisio na vinywaji vya kuleta maneno ya upuuzi wala dhambi.

Ayah  52:24  الأية
    +/- -/+  
وَيَطُوفُ عَلَيْهِمْ غِلْمَانٌ لَّهُمْ كَأَنَّهُمْ لُؤْلُؤٌ مَّكْنُونٌ
Swahili
 
Iwe wanawapitia watumishi wao kama kwamba ni lulu zilizomo katika chaza.

Ayah  52:25  الأية
    +/- -/+  
وَأَقْبَلَ بَعْضُهُمْ عَلَىٰ بَعْضٍ يَتَسَاءَلُونَ
Swahili
 
Wataelekeana wakiulizana.

Ayah  52:26  الأية
    +/- -/+  
قَالُوا إِنَّا كُنَّا قَبْلُ فِي أَهْلِنَا مُشْفِقِينَ
Swahili
 
Waseme: Tulikuwa zamani pamoja na ahali zetu tukiogopa;

Ayah  52:27  الأية
    +/- -/+  
فَمَنَّ اللهُ عَلَيْنَا وَوَقَانَا عَذَابَ السَّمُومِ
Swahili
 
Basi Mwenyezi Mungu akatufanyia hisani na akatulinda na adhabu ya upepo wa Moto.

Ayah  52:28  الأية
    +/- -/+  
إِنَّا كُنَّا مِن قَبْلُ نَدْعُوهُ ۖ إِنَّهُ هُوَ الْبَرُّ الرَّحِيمُ
Swahili
 
Hakika sisi zamani tulikuwa tukimwomba Yeye tu. Hakika Yeye ndiye Mwema Mwenye kurehemu.

Ayah  52:29  الأية
    +/- -/+  
فَذَكِّرْ فَمَا أَنتَ بِنِعْمَتِ رَبِّكَ بِكَاهِنٍ وَلَا مَجْنُونٍ
Swahili
 
Basi kumbusha! Kwani wewe, kwa neema ya Mola wako Mlezi, si kuhani wala mwendawazimu.

Ayah  52:30  الأية
    +/- -/+  
أَمْ يَقُولُونَ شَاعِرٌ نَّتَرَبَّصُ بِهِ رَيْبَ الْمَنُونِ
Swahili
 
Au wanasema: Huyu ni mtunga mashairi, tunamtarajia kupatilizwa na dahari.

Ayah  52:31  الأية
    +/- -/+  
قُلْ تَرَبَّصُوا فَإِنِّي مَعَكُم مِّنَ الْمُتَرَبِّصِينَ
Swahili
 
Sema: Tarajieni, na mimi pia ni pamoja nanyi katika kutarajia.

Ayah  52:32  الأية
    +/- -/+  
أَمْ تَأْمُرُهُمْ أَحْلَامُهُم بِهَٰذَا ۚ أَمْ هُمْ قَوْمٌ طَاغُونَ
Swahili
 
Au hizo akili zao ndio zinawaamrisha haya, au wao basi ni watu majeuri tu?

Ayah  52:33  الأية
    +/- -/+  
أَمْ يَقُولُونَ تَقَوَّلَهُ ۚ بَل لَّا يُؤْمِنُونَ
Swahili
 
Au ndio wanasema: Ameitunga hii! Bali basi tu hawaamini!

Ayah  52:34  الأية
    +/- -/+  
فَلْيَأْتُوا بِحَدِيثٍ مِّثْلِهِ إِن كَانُوا صَادِقِينَ
Swahili
 
Basi nawalete masimulizi kama haya ikiwa wao wanasema kweli.

Ayah  52:35  الأية
    +/- -/+  
أَمْ خُلِقُوا مِنْ غَيْرِ شَيْءٍ أَمْ هُمُ الْخَالِقُونَ
Swahili
 
Au wao wameumbwa pasipo kutokana na kitu chochote, au ni wao ndio waumbaji?

Ayah  52:36  الأية
    +/- -/+  
أَمْ خَلَقُوا السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضَ ۚ بَل لَّا يُوقِنُونَ
Swahili
 
Au wao wameziumba mbingu na ardhi? Bali hawana na yakini.

Ayah  52:37  الأية
    +/- -/+  
أَمْ عِندَهُمْ خَزَائِنُ رَبِّكَ أَمْ هُمُ الْمُصَيْطِرُونَ
Swahili
 
Au wanazo khazina za Mola wako Mlezi au wao ndio wenye madaraka?

Ayah  52:38  الأية
    +/- -/+  
أَمْ لَهُمْ سُلَّمٌ يَسْتَمِعُونَ فِيهِ ۖ فَلْيَأْتِ مُسْتَمِعُهُم بِسُلْطَانٍ مُّبِينٍ
Swahili
 
Au wanazo ngazi za kusikilizia? Basi huyo msikilizaji wao na alete hoja ilio wazi!

Ayah  52:39  الأية
    +/- -/+  
أَمْ لَهُ الْبَنَاتُ وَلَكُمُ الْبَنُونَ
Swahili
 
Au Yeye Mwenyezi Mungu ana wasichana, na nyinyi ndio mna wavulana?

Ayah  52:40  الأية
    +/- -/+  
أَمْ تَسْأَلُهُمْ أَجْرًا فَهُم مِّن مَّغْرَمٍ مُّثْقَلُونَ
Swahili
 
Au wewe unawaomba ujira, na kwa hivyo ndio wanaelemewa na uzito wa gharama?

Ayah  52:41  الأية
    +/- -/+  
أَمْ عِندَهُمُ الْغَيْبُ فَهُمْ يَكْتُبُونَ
Swahili
 
Au wanayo ilimu ya ghaibu, nao wameandika?

Ayah  52:42  الأية
    +/- -/+  
أَمْ يُرِيدُونَ كَيْدًا ۖ فَالَّذِينَ كَفَرُوا هُمُ الْمَكِيدُونَ
Swahili
 
Au wanataka kufanya vitimbi tu? Lakini hao walio kufuru ndio watakao tegeka.

Ayah  52:43  الأية
    +/- -/+  
أَمْ لَهُمْ إِلَٰهٌ غَيْرُ اللهِ ۚ سُبْحَانَ اللهِ عَمَّا يُشْرِكُونَ
Swahili
 
Au wanae mungu asiye kuwa Mwenyezi Mungu? Subhanallah! Ametaksika Mwenyezi Mungu na hao wanao washirikisha naye.

Ayah  52:44  الأية
    +/- -/+  
وَإِن يَرَوْا كِسْفًا مِّنَ السَّمَاءِ سَاقِطًا يَقُولُوا سَحَابٌ مَّرْكُومٌ
Swahili
 
Na hata wange ona pande linatoka mbinguni linaanguka wange sema: Ni mawingu yaliyo bebana.

Ayah  52:45  الأية
    +/- -/+  
فَذَرْهُمْ حَتَّىٰ يُلَاقُوا يَوْمَهُمُ الَّذِي فِيهِ يُصْعَقُونَ
Swahili
 
Basi waache mpaka wakutane na siku yao watakapo hilikishwa.

Ayah  52:46  الأية
    +/- -/+  
يَوْمَ لَا يُغْنِي عَنْهُمْ كَيْدُهُمْ شَيْئًا وَلَا هُمْ يُنصَرُونَ
Swahili
 
Siku ambayo hila zao hazitawafaa hata kidogo, wala wao hawatanusuriwa.

Ayah  52:47  الأية
    +/- -/+  
وَإِنَّ لِلَّذِينَ ظَلَمُوا عَذَابًا دُونَ ذَٰلِكَ وَلَٰكِنَّ أَكْثَرَهُمْ لَا يَعْلَمُونَ
Swahili
 
Na hakika walio dhulumu watapata adhabu nyengine isiyo kuwa hii, lakini wengi wao hawajui.

Ayah  52:48  الأية
    +/- -/+  
وَاصْبِرْ لِحُكْمِ رَبِّكَ فَإِنَّكَ بِأَعْيُنِنَا ۖ وَسَبِّحْ بِحَمْدِ رَبِّكَ حِينَ تَقُومُ
Swahili
 
Na ingojee hukumu ya Mola wako Mlezi. Kwani wewe hakika uko mbele ya macho yetu, na mtakase kwa kumsifu Mola wako Mlezi unapo simama,

Ayah  52:49  الأية
    +/- -/+  
وَمِنَ اللَّيْلِ فَسَبِّحْهُ وَإِدْبَارَ النُّجُومِ
Swahili
 
Na usiku pia mtakase, na zinapo kuchwa nyota.





© EsinIslam.Com Designed & produced by The Awqaf London. Please pray for us