1st Ayah 1 الأية ١الأوليبِسْم ِ اللهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ
الر ۚ تِلْكَ آيَاتُ الْكِتَابِ وَقُرْآنٍ مُّبِينٍ
Alif-lam-ra tilka ayatualkitabi waqur-anin mubeen
Swahili
Alif Lam Ra. (A.L.R). Hizi ni Aya za Kitabu na Qur'ani inayo bainisha.
|
Ayah 15:2 الأية
رُّبَمَا يَوَدُّ الَّذِينَ كَفَرُوا لَوْ كَانُوا مُسْلِمِينَ
Rubama yawaddu allatheenakafaroo law kanoo muslimeen
Swahili
HUENDA ikawa walio kufuru wakatamani wange kuwa Waislamu.
|
Ayah 15:3 الأية
ذَرْهُمْ يَأْكُلُوا وَيَتَمَتَّعُوا وَيُلْهِهِمُ الْأَمَلُ ۖ فَسَوْفَ
يَعْلَمُونَ
Tharhum ya/kuloo wayatamattaAAoowayulhihimu al-amalu fasawfa yaAAlamoon
Swahili
Waache wale, na wastarehe, na iwazuge tamaa. Watakuja jua.
|
Ayah 15:4 الأية
وَمَا أَهْلَكْنَا مِن قَرْيَةٍ إِلَّا وَلَهَا كِتَابٌ مَّعْلُومٌ
Wama ahlakna min qaryatin illawalaha kitabun maAAloom
Swahili
Na hatukuuangamiza mji wowote ule ila ulikuwa na muda wake maalumu.
|
Ayah 15:5 الأية
مَّا تَسْبِقُ مِنْ أُمَّةٍ أَجَلَهَا وَمَا يَسْتَأْخِرُونَ
Ma tasbiqu min ommatin ajalahawama yasta/khiroon
Swahili
Hawawezi watu wowote kuitangulia ajali yao, wala kuchelewa.
|
Ayah 15:6 الأية
وَقَالُوا يَا أَيُّهَا الَّذِي نُزِّلَ عَلَيْهِ الذِّكْرُ إِنَّكَ لَمَجْنُونٌ
Waqaloo ya ayyuha allatheenuzzila AAalayhi aththikru innaka lamajnoon
Swahili
Na walisema: Ewe uliyeteremshiwa Ukumbusho! Hakika wewe ni mwendawazimu.
|
Ayah 15:7 الأية
لَّوْ مَا تَأْتِينَا بِالْمَلَائِكَةِ إِن كُنتَ مِنَ الصَّادِقِينَ
Law ma ta/teena bilmala-ikatiin kunta mina assadiqeen
Swahili
Mbona hutuletei Malaika ikiwa wewe ni miongoni mwa wasemao kweli?
|
Ayah 15:8 الأية
مَا نُنَزِّلُ الْمَلَائِكَةَ إِلَّا بِالْحَقِّ وَمَا كَانُوا إِذًا مُّنظَرِينَ
Ma nunazzilu almala-ikata illabilhaqqi wama kanoo ithan munthareen
Swahili
Sisi hatuwateremshi Malaika ila kwa sababu ya haki, na hapo hawatapewa muhula.
|
Ayah 15:9 الأية
إِنَّا نَحْنُ نَزَّلْنَا الذِّكْرَ وَإِنَّا لَهُ لَحَافِظُونَ
Inna nahnu nazzalna aththikrawa-inna lahu lahafithoon
Swahili
Hakika Sisi ndio tulio teremsha Ukumbusho huu, na hakika Sisi ndio tutao ulinda.
|
Ayah 15:10 الأية
وَلَقَدْ أَرْسَلْنَا مِن قَبْلِكَ فِي شِيَعِ الْأَوَّلِينَ
Walaqad arsalna min qablika feeshiyaAAi al-awwaleen
Swahili
Na hakika tulikwisha watumia Mitume mataifa ya mwanzo.
|
Ayah 15:11 الأية
وَمَا يَأْتِيهِم مِّن رَّسُولٍ إِلَّا كَانُوا بِهِ يَسْتَهْزِئُونَ
Wama ya/teehim min rasoolin illakanoo bihi yastahzi-oon
Swahili
Na hakuwafikia Mtume ila walimkejeli.
|
Ayah 15:12 الأية
كَذَٰلِكَ نَسْلُكُهُ فِي قُلُوبِ الْمُجْرِمِينَ
Kathalika naslukuhu fee quloobialmujrimeen
Swahili
Na kama hivi ndivyo tunavyo ingiza katika nyoyo za wakosefu.
|
Ayah 15:13 الأية
لَا يُؤْمِنُونَ بِهِ ۖ وَقَدْ خَلَتْ سُنَّةُ الْأَوَّلِينَ
La yu/minoona bihi waqad khalatsunnatu al-awwaleen
Swahili
Hawayaamini haya, na hali ya kuwa umekwisha wapitia mfano wa watu wa kale.
|
Ayah 15:14 الأية
وَلَوْ فَتَحْنَا عَلَيْهِم بَابًا مِّنَ السَّمَاءِ فَظَلُّوا فِيهِ يَعْرُجُونَ
Walaw fatahna AAalayhim babanmina assama-i fathalloo feehiyaAArujoon
Swahili
Na lau tungeli wafungulia mlango wa mbingu, wakawa wanapanda,
|
Ayah 15:15 الأية
لَقَالُوا إِنَّمَا سُكِّرَتْ أَبْصَارُنَا بَلْ نَحْنُ قَوْمٌ مَّسْحُورُونَ
Laqaloo innama sukkirat absarunabal nahnu qawmun mashooroon
Swahili
Basi wangeli sema: Macho yetu yamelevywa, bali sisi wenyewe tumerogwa.
|
Ayah 15:16 الأية
وَلَقَدْ جَعَلْنَا فِي السَّمَاءِ بُرُوجًا وَزَيَّنَّاهَا لِلنَّاظِرِينَ
Walaqad jaAAalna fee assama-iburoojan wazayyannaha linnathireen
Swahili
Na hakika tumeweka katika mbingu vituo vya sayari, na tumezipamba kwa wenye
kuangalia.
|
Ayah 15:17 الأية
وَحَفِظْنَاهَا مِن كُلِّ شَيْطَانٍ رَّجِيمٍ
Wahafithnahamin kulli shaytanin rajeem
Swahili
Na tumezilinda na kila shetani afukuzwaye.
|
Ayah 15:18 الأية
إِلَّا مَنِ اسْتَرَقَ السَّمْعَ فَأَتْبَعَهُ شِهَابٌ مُّبِينٌ
Illa mani istaraqa assamAAafaatbaAAahu shihabun mubeen
Swahili
Isipo kuwa mwenye kusikiliza kwa kuibia, naye hufuatwa na kijinga cha moto
kinacho onekana.
|
Ayah 15:19 الأية
وَالْأَرْضَ مَدَدْنَاهَا وَأَلْقَيْنَا فِيهَا رَوَاسِيَ وَأَنبَتْنَا فِيهَا مِن
كُلِّ شَيْءٍ مَّوْزُونٍ
Wal-arda madadnahawaalqayna feeha rawasiya waanbatnafeeha min kulli shay-in
mawzoon
Swahili
Na ardhi tumeitandaza na humo tumeweka milima, na tumeotesha kila kitu kwa kiasi
chake.
|
Ayah 15:20 الأية
وَجَعَلْنَا لَكُمْ فِيهَا مَعَايِشَ وَمَن لَّسْتُمْ لَهُ بِرَازِقِينَ
WajaAAalna lakum feeha maAAayishawaman lastum lahu biraziqeen
Swahili
Na tumekujaalieni humo vitu vya maisha yenu, na ya hao ambao nyinyi sio wenye
kuwaruzuku.
|
Ayah 15:21 الأية
وَإِن مِّن شَيْءٍ إِلَّا عِندَنَا خَزَائِنُهُ وَمَا نُنَزِّلُهُ إِلَّا بِقَدَرٍ
مَّعْلُومٍ
Wa-in min shay-in illa AAindanakhaza-inuhu wama nunazziluhu illa
biqadarinmaAAloom
Swahili
Na hakuna chochote ila asili yake inatokana na Sisi; wala hatukiteremshi ila kwa
kipimo maalumu.
|
Ayah 15:22 الأية
وَأَرْسَلْنَا الرِّيَاحَ لَوَاقِحَ فَأَنزَلْنَا مِنَ السَّمَاءِ مَاءً
فَأَسْقَيْنَاكُمُوهُ وَمَا أَنتُمْ لَهُ بِخَازِنِينَ
Waarsalna arriyaha lawaqihafaanzalna mina assama-i maanfaasqaynakumoohu wama
antum lahu bikhazineen
Swahili
Na tunazipeleka pepo za kupandishia, na tunateremsha kutoka mbinguni maji, kisha
tukakunywesheni maji hayo. Wala si nyinyi mnayo yaweka.
|
Ayah 15:23 الأية
وَإِنَّا لَنَحْنُ نُحْيِي وَنُمِيتُ وَنَحْنُ الْوَارِثُونَ
Wa-inna lanahnu nuhyeewanumeetu wanahnu alwarithoon
Swahili
Na Sisi ndio tunao huisha na tunao fisha. Na Sisi ndio Warithi.
|
Ayah 15:24 الأية
وَلَقَدْ عَلِمْنَا الْمُسْتَقْدِمِينَ مِنكُمْ وَلَقَدْ عَلِمْنَا
الْمُسْتَأْخِرِينَ
Walaqad AAalimna almustaqdimeenaminkum walaqad AAalimna almusta/khireen
Swahili
Na tunawajua walio tangulia katika nyinyi, na tunawajua walio taakhari.
|
Ayah 15:25 الأية
وَإِنَّ رَبَّكَ هُوَ يَحْشُرُهُمْ ۚ إِنَّهُ حَكِيمٌ عَلِيمٌ
Wa-inna rabbaka huwa yahshuruhuminnahu hakeemun AAaleem
Swahili
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye atakaye wakusanya. Hakika Yeye ni Mwenye hikima
na Mjuzi.
|
Ayah 15:26 الأية
وَلَقَدْ خَلَقْنَا الْإِنسَانَ مِن صَلْصَالٍ مِّنْ حَمَإٍ مَّسْنُونٍ
Walaqad khalaqna al-insana minsalsalin min hama-in masnoon
Swahili
Na tulimuumba mtu kwa udongo unao toa sauti, unao tokana na matope yaliyo tiwa
sura.
|
Ayah 15:27 الأية
وَالْجَانَّ خَلَقْنَاهُ مِن قَبْلُ مِن نَّارِ السَّمُومِ
Waljanna khalaqnahumin qablu min nari assamoom
Swahili
Na majini tuliwaumba kabla kwa moto wa upepo umoto.
|
Ayah 15:28 الأية
وَإِذْ قَالَ رَبُّكَ لِلْمَلَائِكَةِ إِنِّي خَالِقٌ بَشَرًا مِّن صَلْصَالٍ مِّنْ
حَمَإٍ مَّسْنُونٍ
Wa-ith qala rabbuka lilmala-ikatiinnee khaliqun basharan min salsalin min
hama-inmasnoon
Swahili
Na Mola wako Mlezi alipo waambia Malaika: Hakika Mimi nitamuumba mtu kwa udongo
unao toa sauti, unao tokana na matope yaliyo tiwa sura.
|
Ayah 15:29 الأية
فَإِذَا سَوَّيْتُهُ وَنَفَخْتُ فِيهِ مِن رُّوحِي فَقَعُوا لَهُ سَاجِدِينَ
Fa-itha sawwaytuhu wanafakhtu feehimin roohee faqaAAoo lahu sajideen
Swahili
Basi nitakapo mkamilisha na nikampulizia roho yangu, basi mumwangukie
kumsujudia.
|
Ayah 15:30 الأية
فَسَجَدَ الْمَلَائِكَةُ كُلُّهُمْ أَجْمَعُونَ
Fasajada almala-ikatu kulluhumajmaAAoon
Swahili
Basi Malaika wote pamoja walimsujudia,
|
Ayah 15:31 الأية
إِلَّا إِبْلِيسَ أَبَىٰ أَن يَكُونَ مَعَ السَّاجِدِينَ
Illa ibleesa aba an yakoonamaAAa assajideen
Swahili
Isipo kuwa Iblisi. Yeye alikataa kuwa pamoja na walio sujudu.
|
Ayah 15:32 الأية
قَالَ يَا إِبْلِيسُ مَا لَكَ أَلَّا تَكُونَ مَعَ السَّاجِدِينَ
Qala ya ibleesu ma lakaalla takoona maAAa assajideen
Swahili
(Mwenyezi Mungu) akasema: Ewe Iblisi! Una nini hata hukuwa pamoja na walio
sujudu?
|
Ayah 15:33 الأية
قَالَ لَمْ أَكُن لِّأَسْجُدَ لِبَشَرٍ خَلَقْتَهُ مِن صَلْصَالٍ مِّنْ حَمَإٍ
مَّسْنُونٍ
Qala lam akun li-asjuda libasharinkhalaqtahu min salsalin min hama-in masnoon
Swahili
Akasema: Haiwi mimi nimsujudie mtu uliye muumba kwa udongo unao toa sauti, unao
tokana na matope yenye sura.
|
Ayah 15:34 الأية
قَالَ فَاخْرُجْ مِنْهَا فَإِنَّكَ رَجِيمٌ
Qala fakhruj minhafa-innaka rajeem
Swahili
(Mwenyezi Mungu) akasema: Basi toka humo, kwani hakika wewe ni maluuni!
|
Ayah 15:35 الأية
وَإِنَّ عَلَيْكَ اللَّعْنَةَ إِلَىٰ يَوْمِ الدِّينِ
Wa-inna AAalayka allaAAnata ila yawmiaddeen
Swahili
Na hakika juu yako ipo laana mpaka Siku ya Malipo.
|
Ayah 15:36 الأية
قَالَ رَبِّ فَأَنظِرْنِي إِلَىٰ يَوْمِ يُبْعَثُونَ
Qala rabbi faanthirneeila yawmi yubAAathoon
Swahili
Akasema (Iblisi): Mola wangu Mlezi! Nipe muhula mpaka siku watapo fufuliwa.
|
Ayah 15:37 الأية
قَالَ فَإِنَّكَ مِنَ الْمُنظَرِينَ
Qala fa-innaka mina almunthareen
Swahili
(Mwenyezi Mungu) akasema: Hakika wewe ni katika walio pewa muhula
|
Ayah 15:38 الأية
إِلَىٰ يَوْمِ الْوَقْتِ الْمَعْلُومِ
Ila yawmi alwaqti almaAAloom
Swahili
Mpaka siku ya wakati maalumu.
|
Ayah 15:39 الأية
قَالَ رَبِّ بِمَا أَغْوَيْتَنِي لَأُزَيِّنَنَّ لَهُمْ فِي الْأَرْضِ
وَلَأُغْوِيَنَّهُمْ أَجْمَعِينَ
Qala rabbi bima aghwaytaneelaozayyinanna lahum fee al-ardi
walaoghwiyannahumajmaAAeen
Swahili
Akasema: Mola wangu Mlezi! Ilivyo kuwa umenitia makosani, basi nahakikisha
nitawazaini hapa duniani na nitawapoteza wote,
|
Ayah 15:40 الأية
إِلَّا عِبَادَكَ مِنْهُمُ الْمُخْلَصِينَ
Illa AAibadaka minhumualmukhlaseen
Swahili
Ila waja wako walio safika.
|
Ayah 15:41 الأية
قَالَ هَٰذَا صِرَاطٌ عَلَيَّ مُسْتَقِيمٌ
Qala hatha siratunAAalayya mustaqeem
Swahili
Akasema: Hii Njia ya kujia kwangu Iliyo Nyooka.
|
Ayah 15:42 الأية
إِنَّ عِبَادِي لَيْسَ لَكَ عَلَيْهِمْ سُلْطَانٌ إِلَّا مَنِ اتَّبَعَكَ مِنَ
الْغَاوِينَ
Inna AAibadee laysa laka AAalayhimsultanun illa mani ittabaAAaka mina alghaween
Swahili
Hakika waja wangu, wewe hutakuwa na mamlaka juu yao, isipo kuwa wale wapotofu
walio kufuata.
|
Ayah 15:43 الأية
وَإِنَّ جَهَنَّمَ لَمَوْعِدُهُمْ أَجْمَعِينَ
Wa-inna jahannama lamawAAiduhum ajmaAAeen
Swahili
Na bila shaka Jahannamu ndipo pahali pao walipo ahidiwa wote.
|
Ayah 15:44 الأية
لَهَا سَبْعَةُ أَبْوَابٍ لِّكُلِّ بَابٍ مِّنْهُمْ جُزْءٌ مَّقْسُومٌ
Laha sabAAatu abwabin likullibabin minhum juz-on maqsoom
Swahili
Ina milango saba; na kwa kila mlango iko sehemu walio tengewa.
|
Ayah 15:45 الأية
إِنَّ الْمُتَّقِينَ فِي جَنَّاتٍ وَعُيُونٍ
Inna almuttaqeena fee jannatinwaAAuyoon
Swahili
Hakika wachamngu watakuwa katika Mabustani na chemchem.
|
Ayah 15:46 الأية
ادْخُلُوهَا بِسَلَامٍ آمِنِينَ
Odkhulooha bisalamin amineen
Swahili
(Wataambiwa:) Ingieni kwa salama na amani.
|
Ayah 15:47 الأية
وَنَزَعْنَا مَا فِي صُدُورِهِم مِّنْ غِلٍّ إِخْوَانًا عَلَىٰ سُرُرٍ
مُّتَقَابِلِينَ
WanazaAAna ma fee sudoorihimmin ghillin ikhwanan AAala sururin mutaqabileen
Swahili
Na tutaondoa chuki iliyo kuwamo vifuani mwao, wawe ndugu juu ya viti vya enzi
wameelekeana.
|
Ayah 15:48 الأية
لَا يَمَسُّهُمْ فِيهَا نَصَبٌ وَمَا هُم مِّنْهَا بِمُخْرَجِينَ
La yamassuhum feeha nasabunwama hum minha bimukhrajeen
Swahili
Humo hayatawagusa machofu, wala hawatatolewa humo.
|
Ayah 15:49 الأية
نَبِّئْ عِبَادِي أَنِّي أَنَا الْغَفُورُ الرَّحِيمُ
Nabbi/ AAibadee annee anaalghafooru arraheem
Swahili
Waambie waja wangu ya kwamba Mimi ndiye Mwenye kusamehe, Mwenye kurehemu.
|
Ayah 15:50 الأية
وَأَنَّ عَذَابِي هُوَ الْعَذَابُ الْأَلِيمُ
Waanna AAathabee huwa alAAathabual-aleem
Swahili
Na kwamba adhabu yangu ndio adhabu iliyo chungu!
|
Ayah 15:51 الأية
وَنَبِّئْهُمْ عَن ضَيْفِ إِبْرَاهِيمَ
Wanabbi/hum AAan dayfi ibraheem
Swahili
Na uwape khabari za wageni wa Ibrahim.
|
Ayah 15:52 الأية
إِذْ دَخَلُوا عَلَيْهِ فَقَالُوا سَلَامًا قَالَ إِنَّا مِنكُمْ وَجِلُونَ
Ith dakhaloo AAalayhi faqaloosalaman qala inna minkum wajiloon
Swahili
Walipo ingia kwake na wakasema: Salama! Yeye akasema: Hakika sisi tunakuogopeni.
|
Ayah 15:53 الأية
قَالُوا لَا تَوْجَلْ إِنَّا نُبَشِّرُكَ بِغُلَامٍ عَلِيمٍ
Qaloo la tawjal innanubashshiruka bighulamin AAaleem
Swahili
Wakasema: Usiogope. Sisi tunakubashiria kijana mwenye ujuzi.
|
Ayah 15:54 الأية
قَالَ أَبَشَّرْتُمُونِي عَلَىٰ أَن مَّسَّنِيَ الْكِبَرُ فَبِمَ تُبَشِّرُونَ
Qala abashshartumoonee AAalaan massaniya alkibaru fabima tubashshiroon
Swahili
Akasema: Mnanibashiria nami uzee umenishika! Basi kwa njia gani mnanibashiria?
|
Ayah 15:55 الأية
قَالُوا بَشَّرْنَاكَ بِالْحَقِّ فَلَا تَكُن مِّنَ الْقَانِطِينَ
Qaloo bashsharnaka bilhaqqifala takun mina alqaniteen
Swahili
Wakasema: Tunakubashiria kwa haki; basi usiwe miongoni mwa wanao kata tamaa.
|
Ayah 15:56 الأية
قَالَ وَمَن يَقْنَطُ مِن رَّحْمَةِ رَبِّهِ إِلَّا الضَّالُّونَ
Qala waman yaqnatu min rahmatirabbihi illa addalloon
Swahili
Akasema: Na nani anaye kata tamaa na rehema ya Mola wake Mlezi ila wale walio
potea?
|
Ayah 15:57 الأية
قَالَ فَمَا خَطْبُكُمْ أَيُّهَا الْمُرْسَلُونَ
Qala fama khatbukumayyuha almursaloon
Swahili
Akasema: Hebu nini amri yenu, enyi wajumbe?
|
Ayah 15:58 الأية
قَالُوا إِنَّا أُرْسِلْنَا إِلَىٰ قَوْمٍ مُّجْرِمِينَ
Qaloo inna orsilna ilaqawmin mujrimeen
Swahili
Wakasema: Hakika sisi tumetumwa kwa kaumu ya wakosefu!
|
Ayah 15:59 الأية
إِلَّا آلَ لُوطٍ إِنَّا لَمُنَجُّوهُمْ أَجْمَعِينَ
Illa ala lootin innalamunajjoohum ajmaAAeen
Swahili
Isipo kuwa walio mfuata Luut'i. Bila ya shaka sisi tutawaokoa hao wote.
|
Ayah 15:60 الأية
إِلَّا امْرَأَتَهُ قَدَّرْنَا ۙ إِنَّهَا لَمِنَ الْغَابِرِينَ
Illa imraatahu qaddarna innahalamina alghabireen
Swahili
Ila mkewe. Tunakadiria huyo atakuwa miongoni watao bakia nyuma.
|
Ayah 15:61 الأية
فَلَمَّا جَاءَ آلَ لُوطٍ الْمُرْسَلُونَ
Falamma jaa ala lootinalmursaloon
Swahili
Basi wale wajumbe walipo fika kwa Luut'i,
|
Ayah 15:62 الأية
قَالَ إِنَّكُمْ قَوْمٌ مُّنكَرُونَ
Qala innakum qawmun munkaroon
Swahili
Alisema (Luut'i): Hakika nyinyi ni watu msio juulikana.
|
Ayah 15:63 الأية
قَالُوا بَلْ جِئْنَاكَ بِمَا كَانُوا فِيهِ يَمْتَرُونَ
Qaloo bal ji/naka bimakanoo feehi yamtaroon
Swahili
Wakasema: Bali sisi tumekuletea yale waliyo kuwa wakiyafanyia shaka.
|
Ayah 15:64 الأية
وَأَتَيْنَاكَ بِالْحَقِّ وَإِنَّا لَصَادِقُونَ
Waataynaka bilhaqqiwa-inna lasadiqoon
Swahili
Na tumefika kwako kwa Haki, na hakika sisi tunasema kweli.
|
Ayah 15:65 الأية
فَأَسْرِ بِأَهْلِكَ بِقِطْعٍ مِّنَ اللَّيْلِ وَاتَّبِعْ أَدْبَارَهُمْ وَلَا
يَلْتَفِتْ مِنكُمْ أَحَدٌ وَامْضُوا حَيْثُ تُؤْمَرُونَ
Faasri bi-ahlika biqitAAin minaallayli wattabiAA adbarahum wala yaltafitminkum
ahadun wamdoo haythutu/maroon
Swahili
Basi ondoka na ahli zako usiku ungalipo, nawe ufuate nyuma yao, wala yeyote kati
yenu asigeuke nyuma. Na mwende mnapo amrishwa.
|
Ayah 15:66 الأية
وَقَضَيْنَا إِلَيْهِ ذَٰلِكَ الْأَمْرَ أَنَّ دَابِرَ هَٰؤُلَاءِ مَقْطُوعٌ
مُّصْبِحِينَ
Waqadayna ilayhi thalikaal-amra anna dabira haola-i maqtooAAunmusbiheen
Swahili
Na tukamfunulia hukumu hiyo, ya kwamba hata wa mwisho wao hao ikifika asubuhi
atakuwa kesha katiliwa mbali.
|
Ayah 15:67 الأية
وَجَاءَ أَهْلُ الْمَدِينَةِ يَسْتَبْشِرُونَ
Wajaa ahlu almadeenati yastabshiroon
Swahili
Na wakaja watu wa mji ule nao furahani.
|
Ayah 15:68 الأية
قَالَ إِنَّ هَٰؤُلَاءِ ضَيْفِي فَلَا تَفْضَحُونِ
Qala inna haola-i dayfeefala tafdahoon
Swahili
Akasema: Hakika hawa wageni wangu, basi msinifedheheshe.
|
Ayah 15:69 الأية
وَاتَّقُوا اللهَ وَلَا تُخْزُونِ
Wattaqoo Allaha walatukhzoon
Swahili
Na mcheni Mwenyezi Mungu, wala msinihizi.
|
Ayah 15:70 الأية
قَالُوا أَوَلَمْ نَنْهَكَ عَنِ الْعَالَمِينَ
Qaloo awa lam nanhaka AAani alAAalameen
Swahili
Wakasema: Sisi hatukukukataza usimkaribishe yeyote?
|
Ayah 15:71 الأية
قَالَ هَٰؤُلَاءِ بَنَاتِي إِن كُنتُمْ فَاعِلِينَ
Qala haola-i banateein kuntum faAAileen
Swahili
Akasema: Hawa binti zangu, ikiwa nyinyi ni watendaji.
|
Ayah 15:72 الأية
لَعَمْرُكَ إِنَّهُمْ لَفِي سَكْرَتِهِمْ يَعْمَهُونَ
LaAAamruka innahum lafee sakratihimyaAAmahoona
Swahili
Naapa kwa umri wako! Hakika hao walikuwa katika ulevi wao, wakihangaika ovyo.
|
Ayah 15:73 الأية
فَأَخَذَتْهُمُ الصَّيْحَةُ مُشْرِقِينَ
Faakhathat-humu assayhatumushriqeen
Swahili
Ukelele ukawatwaa wakipambaukiwa.
|
Ayah 15:74 الأية
فَجَعَلْنَا عَالِيَهَا سَافِلَهَا وَأَمْطَرْنَا عَلَيْهِمْ حِجَارَةً مِّن
سِجِّيلٍ
FajaAAalna AAaliyaha safilahawaamtarna AAalayhim hijaratan minsijjeel
Swahili
Na tukaigeuza nchi juu chini, na tukawanyeshea mvua ya mawe ya udongo wa Motoni.
|
Ayah 15:75 الأية
إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَاتٍ لِّلْمُتَوَسِّمِينَ
Inna fee thalika laayatinlilmutawassimeen
Swahili
Hakika katika hayo zipo ishara kwa waaguzi.
|
Ayah 15:76 الأية
وَإِنَّهَا لَبِسَبِيلٍ مُّقِيمٍ
Wa-innaha labisabeelin muqeem
Swahili
Na miji hii ipo kwenye njia inayo pitiwa.
|
Ayah 15:77 الأية
إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَةً لِّلْمُؤْمِنِينَ
Inna fee thalika laayatanlilmu/mineen
Swahili
Hakika katika hayo ipo ishara kwa Waumini.
|
Ayah 15:78 الأية
وَإِن كَانَ أَصْحَابُ الْأَيْكَةِ لَظَالِمِينَ
Wa-in kana as-habual-aykati lathalimeen
Swahili
Na hakika watu wa Kichakani walikuwa wenye kudhulumu.
|
Ayah 15:79 الأية
فَانتَقَمْنَا مِنْهُمْ وَإِنَّهُمَا لَبِإِمَامٍ مُّبِينٍ
Fantaqamna minhum wa-innahumalabi-imamin mubeen
Swahili
Kwa hivyo tukawaadhibu. Na nchi mbili hizi ziko kwenye njia ilio wazi.
|
Ayah 15:80 الأية
وَلَقَدْ كَذَّبَ أَصْحَابُ الْحِجْرِ الْمُرْسَلِينَ
Walaqad kaththaba as-habualhijri almursaleen
Swahili
Na bila ya shaka wakaazi wa Hijr waliwakanusha Mitume.
|
Ayah 15:81 الأية
وَآتَيْنَاهُمْ آيَاتِنَا فَكَانُوا عَنْهَا مُعْرِضِينَ
Waataynahum ayatinafakanoo AAanha muAArideen
Swahili
Na tuliwapa ishara zetu, nao wakazipuuza.
|
Ayah 15:82 الأية
وَكَانُوا يَنْحِتُونَ مِنَ الْجِبَالِ بُيُوتًا آمِنِينَ
Wakanoo yanhitoona mina aljibalibuyootan amineen
Swahili
Nao walikuwa wakichonga majumba katika milima kwa amani.
|
Ayah 15:83 الأية
فَأَخَذَتْهُمُ الصَّيْحَةُ مُصْبِحِينَ
Faakhathat-humu assayhatumusbiheen
Swahili
Basi ukelele ukawatwaa asubuhi.
|
Ayah 15:84 الأية
فَمَا أَغْنَىٰ عَنْهُم مَّا كَانُوا يَكْسِبُونَ
Fama aghna AAanhum ma kanooyaksiboon
Swahili
Hayakuwafaa waliyo kuwa wakiyachuma.
|
Ayah 15:85 الأية
وَمَا خَلَقْنَا السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضَ وَمَا بَيْنَهُمَا إِلَّا بِالْحَقِّ ۗ
وَإِنَّ السَّاعَةَ لَآتِيَةٌ ۖ فَاصْفَحِ الصَّفْحَ الْجَمِيلَ
Wama khalaqna assamawatiwal-arda wama baynahuma illabilhaqqi wa-inna assaAAata
laatiyatunfasfahi assafhaaljameel
Swahili
Na hatukuziumba mbingu na ardhi na vilivyomo ndani yake ila kwa ajili ya Haki.
Na hakika Kiyama kitafika. Basi samehe msamaha mzuri.
|
Ayah 15:86 الأية
إِنَّ رَبَّكَ هُوَ الْخَلَّاقُ الْعَلِيمُ
Inna rabbaka huwa alkhallaqualAAaleem
Swahili
Hakika Mola wako Mlezi ndiye Muumbaji Mjuzi.
|
Ayah 15:87 الأية
وَلَقَدْ آتَيْنَاكَ سَبْعًا مِّنَ الْمَثَانِي وَالْقُرْآنَ الْعَظِيمَ
Walaqad ataynaka sabAAan minaalmathanee walqur-ana alAAatheem
Swahili
Na tumekupa Aya saba zinazo somwa mara kwa mara, na Qur'ani Tukufu.
|
Ayah 15:88 الأية
لَا تَمُدَّنَّ عَيْنَيْكَ إِلَىٰ مَا مَتَّعْنَا بِهِ أَزْوَاجًا مِّنْهُمْ وَلَا
تَحْزَنْ عَلَيْهِمْ وَاخْفِضْ جَنَاحَكَ لِلْمُؤْمِنِينَ
La tamuddanna AAaynayka ila mamattaAAna bihi azwajan minhum wala tahzanAAalayhim
wakhfid janahaka lilmu/mineen
Swahili
Usivitumbulie macho yako vitu tulivyo waneemesha makundi fulani kati yao, wala
usiwahuzunikie. Na wainamishie bawa lako (la huruma) Waumini.
|
Ayah 15:89 الأية
وَقُلْ إِنِّي أَنَا النَّذِيرُ الْمُبِينُ
Waqul innee ana annatheerualmubeen
Swahili
Na sema: Hakika mimi ni mwonyaji mwenye kubainisha.
|
Ayah 15:90 الأية
كَمَا أَنزَلْنَا عَلَى الْمُقْتَسِمِينَ
Kama anzalna AAalaalmuqtasimeen
Swahili
Kama hivyo tuliwateremshia walio gawa,
|
Ayah 15:91 الأية
الَّذِينَ جَعَلُوا الْقُرْآنَ عِضِينَ
Allatheena jaAAaloo alqur-anaAAideen
Swahili
Ambao wakaifanya Qur'ani vipande vipande.
|
Ayah 15:92 الأية
فَوَرَبِّكَ لَنَسْأَلَنَّهُمْ أَجْمَعِينَ
Fawarabbika lanas-alannahum ajmaAAeen
Swahili
Basi Naapa kwa Mola wako Mlezi! Tutawahoji wote,
|
Ayah 15:93 الأية
عَمَّا كَانُوا يَعْمَلُونَ
AAamma kanoo yaAAmaloon
Swahili
Kwa waliyo kuwa wakiyatenda.
|
Ayah 15:94 الأية
فَاصْدَعْ بِمَا تُؤْمَرُ وَأَعْرِضْ عَنِ الْمُشْرِكِينَ
FasdaAA bima tu/maruwaaAArid AAani almushrikeen
Swahili
Basi wewe yatangaze uliyo amrishwa, na jitenge na washirikina.
|
Ayah 15:95 الأية
إِنَّا كَفَيْنَاكَ الْمُسْتَهْزِئِينَ
Inna kafaynaka almustahzi-een
Swahili
Hakika Sisi tunatosha kukukinga na wanao kejeli.
|
Ayah 15:96 الأية
الَّذِينَ يَجْعَلُونَ مَعَ اللهِ إِلَٰهًا آخَرَ ۚ فَسَوْفَ يَعْلَمُونَ
Allatheena yajAAaloona maAAa Allahiilahan akhara fasawfa yaAAlamoon
Swahili
Hao wanao fanya kuwa pamoja na Mwenyezi Mungu yupo mungu mwingine. Basi,
watakuja jua!
|
Ayah 15:97 الأية
وَلَقَدْ نَعْلَمُ أَنَّكَ يَضِيقُ صَدْرُكَ بِمَا يَقُولُونَ
Walaqad naAAlamu annaka yadeequ sadrukabima yaqooloon
Swahili
Na Sisi tunajua kwa hakika kuwa wewe kifua chako kinaona dhiki kwa hayo
wayasemayo.
|
Ayah 15:98 الأية
فَسَبِّحْ بِحَمْدِ رَبِّكَ وَكُن مِّنَ السَّاجِدِينَ
Fasabbih bihamdi rabbika wakunmina assajideen
Swahili
Basi mtakase Mola wako Mlezi kwa kumhimidi, na uwe miongoni wanao msujudia.
|
Ayah 15:99 الأية
وَاعْبُدْ رَبَّكَ حَتَّىٰ يَأْتِيَكَ الْيَقِينُ
WaAAbud rabbaka hattaya/tiyaka alyaqeen
Swahili
Na muabudu Mola wako Mlezi mpaka ikufikie Yakini.
|
©
EsinIslam.Com Designed & produced by The Awqaf London. Please pray for us
|