First Ayah 1 الأية الأوليبِسْم ِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ
يَا أَيُّهَا النَّاسُ اتَّقُوا رَبَّكُمْ ۚ إِنَّ زَلْزَلَةَ السَّاعَةِ شَيْءٌ
عَظِيمٌ
Ya ayyuha annasuittaqoo rabbakum inna zalzalata assaAAati shay-onAAatheem
Swahili
Enyi watu! Mcheni Mola wenu Mlezi. Hakika tetemeko la Saa (ya Kiyama) ni jambo
kuu.
|
Ayah 22:2 الأية
يَوْمَ تَرَوْنَهَا تَذْهَلُ كُلُّ مُرْضِعَةٍ عَمَّا أَرْضَعَتْ وَتَضَعُ كُلُّ
ذَاتِ حَمْلٍ حَمْلَهَا وَتَرَى النَّاسَ سُكَارَىٰ وَمَا هُم بِسُكَارَىٰ
وَلَٰكِنَّ عَذَابَ اللَّهِ شَدِيدٌ
Yawma tarawnaha tathhalu kullumurdiAAatin AAamma ardaAAat watadaAAukullu thati
hamlin hamlaha wataraannasa sukara wama hum bisukarawalakinna AAathaba Allahi
shadeed
Swahili
Siku mtapo iona, kila mwenye kunyonyesha atamsahau amnyonyeshaye, na kila mwenye
mimba ataharibu mimba yake. Na utaona watu wamelewa, na kumbe hawakulewa. Lakini
adhabu ya Mwenyezi Mungu ni kali.
|
Ayah 22:3 الأية
وَمِنَ النَّاسِ مَن يُجَادِلُ فِي اللَّهِ بِغَيْرِ عِلْمٍ وَيَتَّبِعُ كُلَّ
شَيْطَانٍ مَّرِيدٍ
Wamina annasi man yujadilufee Allahi bighayri AAilmin wayattabiAAu kulla
shaytaninmareed
Swahili
Na miongoni mwa watu wapo wanao bishana juu ya Mwenyezi Mungu bila ya ilimu, na
wanamfuata kila shet'ani aliye asi.
|
Ayah 22:4 الأية
كُتِبَ عَلَيْهِ أَنَّهُ مَن تَوَلَّاهُ فَأَنَّهُ يُضِلُّهُ وَيَهْدِيهِ إِلَىٰ
عَذَابِ السَّعِيرِ
Kutiba AAalayhi annahu man tawallahufaannahu yudilluhu wayahdeehi ila AAathabi
assaAAeer
Swahili
Ameandikiwa kwamba anaye mfanya kuwa rafiki, basi huyo hakika atampoteza na
atamwongoza kwenye adhabu ya Moto mkali.
|
Ayah 22:5 الأية
يَا أَيُّهَا النَّاسُ إِن كُنتُمْ فِي رَيْبٍ مِّنَ الْبَعْثِ فَإِنَّا
خَلَقْنَاكُم مِّن تُرَابٍ ثُمَّ مِن نُّطْفَةٍ ثُمَّ مِنْ عَلَقَةٍ ثُمَّ مِن
مُّضْغَةٍ مُّخَلَّقَةٍ وَغَيْرِ مُخَلَّقَةٍ لِّنُبَيِّنَ لَكُمْ ۚ وَنُقِرُّ فِي
الْأَرْحَامِ مَا نَشَاءُ إِلَىٰ أَجَلٍ مُّسَمًّى ثُمَّ نُخْرِجُكُمْ طِفْلًا
ثُمَّ لِتَبْلُغُوا أَشُدَّكُمْ ۖ وَمِنكُم مَّن يُتَوَفَّىٰ وَمِنكُم مَّن يُرَدُّ
إِلَىٰ أَرْذَلِ الْعُمُرِ لِكَيْلَا يَعْلَمَ مِن بَعْدِ عِلْمٍ شَيْئًا ۚ وَتَرَى
الْأَرْضَ هَامِدَةً فَإِذَا أَنزَلْنَا عَلَيْهَا الْمَاءَ اهْتَزَّتْ وَرَبَتْ
وَأَنبَتَتْ مِن كُلِّ زَوْجٍ بَهِيجٍ
Ya ayyuha annasuin kuntum fee raybin mina albaAAthi fa-inna khalaqnakummin
turabin thumma min nutfatin thumma minAAalaqatin thumma min mudghatin
mukhallaqatin waghayrimukhallaqatin linubayyina lakum wanuqirru fee al-arhami
manashao ila ajalin musamman thumma nukhrijukum tiflanthumma litablughoo
ashuddakum waminkum man yutawaffawaminkum man yuraddu ila arthali alAAumuri
likaylayaAAlama min baAAdi AAilmin shay-an watara al-ardahamidatan fa-itha
anzalna AAalayhaalmaa ihtazzat warabat waanbatat min kulli zawjin baheej
Swahili
Enyi watu! Ikiwa nyinyi mna shaka ya kufufuliwa basi kwa hakika Sisi
tulikuumbeni kutokana na udongo, kisha kutokana na manii, kisha kutokana na
kipande cha damu ilio gandana, kisha kutokana na kipande cha nyama chenye umbo
na kisicho kuwa na umbo, ili tukubainishieni. Nasi tunakiweka katika matumbo ya
uzazi tunacho kitaka mpaka muda ulio wekwa. Kisha tunakutoeni kwa hali ya mtoto
mchanga, kisha mfikie kutimia akili. Na wapo katika nyinyi wanao kufa, na wapo
katika nyinyi wanao rudishwa kwenye umri wa unyonge kabisa, hata mtu awe hajui
kitu baada ya kuwa anakijua. Na unaiona ardhi imetulia kimya, lakini tunapo
yateremsha maji juu yake husisimka na kututumka, na kumea kila namna ya mimea
mizuri.
|
Ayah 22:6 الأية
ذَٰلِكَ بِأَنَّ اللَّهَ هُوَ الْحَقُّ وَأَنَّهُ يُحْيِي الْمَوْتَىٰ وَأَنَّهُ
عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ
Thalika bi-anna Allaha huwa alhaqquwaannahu yuhyee almawta waannahu AAala
kullishay-in qadeer
Swahili
Hayo ni kwa sababu hakika Mwenyezi Mungu ndiye Haki, na kwamba hakika Yeye ndiye
mwenye kuhuisha wafu, na kwamba hakika Yeye ni Muweza wa kila kitu.
|
Ayah 22:7 الأية
وَأَنَّ السَّاعَةَ آتِيَةٌ لَّا رَيْبَ فِيهَا وَأَنَّ اللَّهَ يَبْعَثُ مَن فِي
الْقُبُورِ
Waanna assaAAata atiyatunla rayba feeha waanna Allaha yabAAathu manfee alquboor
Swahili
Na kwamba hakika Saa itakuja hapana shaka kwa hilo, na kwamba hakika Mwenyezi
Mungu atawafufua walio makaburini.
|
Ayah 22:8 الأية
وَمِنَ النَّاسِ مَن يُجَادِلُ فِي اللَّهِ بِغَيْرِ عِلْمٍ وَلَا هُدًى وَلَا
كِتَابٍ مُّنِيرٍ
Wamina annasi man yujadilufee Allahi bighayri AAilmin wala hudan walakitabin
muneer
Swahili
Na katika watu wapo wanao bishana juu ya Mwenyezi Mungu bila ya ilimu, wala
uwongofu, wala Kitabu chenye nuru.
|
Ayah 22:9 الأية
ثَانِيَ عِطْفِهِ لِيُضِلَّ عَن سَبِيلِ اللَّهِ ۖ لَهُ فِي الدُّنْيَا خِزْيٌ ۖ
وَنُذِيقُهُ يَوْمَ الْقِيَامَةِ عَذَابَ الْحَرِيقِ
Thaniya AAitfihi liyudillaAAan sabeeli Allahi lahu fee addunyakhizyun
wanutheequhu yawma alqiyamati AAathabaalhareeq
Swahili
Anaye geuza shingo yake ili kupoteza watu waache Njia ya Mwenyezi Mungu. Duniani
atapata hizaya, na Siku ya Kiyama tutamwonjesha adhabu ya kuungua.
|
Ayah 22:10 الأية
ذَٰلِكَ بِمَا قَدَّمَتْ يَدَاكَ وَأَنَّ اللَّهَ لَيْسَ بِظَلَّامٍ لِّلْعَبِيدِ
Thalika bima qaddamat yadakawaanna Allaha laysa bithallaminlilAAabeed
Swahili
(Ataambiwa): Hayo ni kwa sababu ya iliyo tanguliza mikono yako. Na hakika
Mwenyezi Mungu si dhaalimu kwa waja.
|
Ayah 22:11 الأية
وَمِنَ النَّاسِ مَن يَعْبُدُ اللَّهَ عَلَىٰ حَرْفٍ ۖ فَإِنْ أَصَابَهُ خَيْرٌ
اطْمَأَنَّ بِهِ ۖ وَإِنْ أَصَابَتْهُ فِتْنَةٌ انقَلَبَ عَلَىٰ وَجْهِهِ خَسِرَ
الدُّنْيَا وَالْآخِرَةَ ۚ ذَٰلِكَ هُوَ الْخُسْرَانُ الْمُبِينُ
Wamina annasi man yaAAbuduAllaha AAala harfin fa-in asabahukhayrun itmaanna bihi
wa-in asabat-hu fitnatuninqalaba AAala wajhihi khasira addunya
wal-akhiratathalika huwa alkhusranu almubeen
Swahili
Na katika watu wapo wanao muabudu Mwenyezi Mungu kwa ukingoni. Ikimfikia kheri
hutulia kwayo, na ukimfikia msukosuko hugeuza uso wake. Amekhasiri dunia na
Akhera; hiyo ndiyo khasara iliyo wazi.
|
Ayah 22:12 الأية
يَدْعُو مِن دُونِ اللَّهِ مَا لَا يَضُرُّهُ وَمَا لَا يَنفَعُهُ ۚ ذَٰلِكَ هُوَ
الضَّلَالُ الْبَعِيدُ
YadAAoo min dooni Allahi ma layadurruhu wama la yanfaAAuhu thalikahuwa addalalu
albaAAeed
Swahili
Badala ya Mwenyezi Mungu, yeye huomba kisicho mdhuru wala kumnufaisha. Huko
ndiko kupotolea mbali!
|
Ayah 22:13 الأية
يَدْعُو لَمَن ضَرُّهُ أَقْرَبُ مِن نَّفْعِهِ ۚ لَبِئْسَ الْمَوْلَىٰ وَلَبِئْسَ
الْعَشِيرُ
YadAAoo laman darruhu aqrabu minnafAAihi labi/sa almawla walabi/sa alAAasheer
Swahili
Humuomba yule ambaye bila ya shaka dhara yake ipo karibu zaidi kuliko nafuu
yake. Kwa hakika huyo ni mlinzi muovu, na rafiki muovu.
|
Ayah 22:14 الأية
إِنَّ اللَّهَ يُدْخِلُ الَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ جَنَّاتٍ
تَجْرِي مِن تَحْتِهَا الْأَنْهَارُ ۚ إِنَّ اللَّهَ يَفْعَلُ مَا يُرِيدُ
Inna Allaha yudkhilu allatheenaamanoo waAAamiloo assalihati jannatintajree min
tahtiha al-anharu inna AllahayafAAalu ma yureed
Swahili
Hakika Mwenyezi Mungu atawaingiza walio amini na wakatenda mema katika Bustani
zipitazo mito kati yake. Hakika Mwenyezi Mungu hutenda atakayo.
|
Ayah 22:15 الأية
مَن كَانَ يَظُنُّ أَن لَّن يَنصُرَهُ اللَّهُ فِي الدُّنْيَا وَالْآخِرَةِ
فَلْيَمْدُدْ بِسَبَبٍ إِلَى السَّمَاءِ ثُمَّ لْيَقْطَعْ فَلْيَنظُرْ هَلْ
يُذْهِبَنَّ كَيْدُهُ مَا يَغِيظُ
Man kana yathunnu anlan yansurahu Allahu fee addunya wal-akhiratifalyamdud
bisababin ila assama-i thummaliyaqtaAA falyanthur hal yuthhibannakayduhu ma
yagheeth
Swahili
Anaye dhani kwamba Mwenyezi Mungu hatamnusuru (Mtume) katika dunia na Akhera na
afunge kamba kwenye dari kisha aikate. Atazame je hila yake itaondoa hayo yaliyo
mkasirisha?
|
Ayah 22:16 الأية
وَكَذَٰلِكَ أَنزَلْنَاهُ آيَاتٍ بَيِّنَاتٍ وَأَنَّ اللَّهَ يَهْدِي مَن يُرِيدُ
Wakathalika anzalnahu ayatinbayyinatin waanna Allaha yahdee man yureed
Swahili
Na namna hivi tumeiteremsha (Qur'ani) kuwa ni Aya zilizo wazi, na hakika
Mwenyezi Mungu humwongoa amtakaye.
|
Ayah 22:17 الأية
إِنَّ الَّذِينَ آمَنُوا وَالَّذِينَ هَادُوا وَالصَّابِئِينَ وَالنَّصَارَىٰ
وَالْمَجُوسَ وَالَّذِينَ أَشْرَكُوا إِنَّ اللَّهَ يَفْصِلُ بَيْنَهُمْ يَوْمَ
الْقِيَامَةِ ۚ إِنَّ اللَّهَ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ شَهِيدٌ
Inna allatheena amanoo wallatheenahadoo wassabi-eena wannasarawalmajoosa
wallatheena ashrakoo inna Allahayafsilu baynahum yawma alqiyamati inna
AllahaAAala kulli shay-in shaheed
Swahili
Hakika walio amini, na ambao ni Mayahudi na Wasabai na Wakristo na Majusi na
wale walio shiriki - hakika Mwenyezi Mungu atawapambanua baina yao Siku ya
Kiyama. Hakika Mwenyezi Mungu ni Shahidi wa kila kitu.
|
Ayah 22:18 الأية
أَلَمْ تَرَ أَنَّ اللَّهَ يَسْجُدُ لَهُ مَن فِي السَّمَاوَاتِ وَمَن فِي
الْأَرْضِ وَالشَّمْسُ وَالْقَمَرُ وَالنُّجُومُ وَالْجِبَالُ وَالشَّجَرُ
وَالدَّوَابُّ وَكَثِيرٌ مِّنَ النَّاسِ ۖ وَكَثِيرٌ حَقَّ عَلَيْهِ الْعَذَابُ ۗ
وَمَن يُهِنِ اللَّهُ فَمَا لَهُ مِن مُّكْرِمٍ ۚ إِنَّ اللَّهَ يَفْعَلُ مَا
يَشَاءُ ۩
Alam tara anna Allaha yasjudu lahuman fee assamawati waman fee al-ardiwashshamsu
walqamaru wannujoomu waljibaluwashshajaru waddawabbu wakatheerun minaannasi
wakatheerun haqqa AAalayhi alAAathabuwaman yuhini Allahu fama lahu min mukrimin
inna AllahayafAAalu ma yasha/
Swahili
Je! Huoni kwamba vinamsujudia Mwenyezi Mungu viliomo mbinguni na viliomo katika
ardhi, na jua, na mwezi, na nyota, na milima, na miti, na wanyama, na wengi
miongoni mwa watu. Na wengi imewastahiki adhabu. Na anaye fedheheshwa na
Mwenyezi Mungu hana wa kumhishimu. Hakika Mwenyezi Mungu hutenda apendayo.
|
Ayah 22:19 الأية
هَٰذَانِ خَصْمَانِ اخْتَصَمُوا فِي رَبِّهِمْ ۖ فَالَّذِينَ كَفَرُوا قُطِّعَتْ
لَهُمْ ثِيَابٌ مِّن نَّارٍ يُصَبُّ مِن فَوْقِ رُءُوسِهِمُ الْحَمِيمُ
Hathani khasmani ikhtasamoofee rabbihim fallatheena kafaroo quttiAAatlahum
thiyabun min narin yusabbu min fawqiruoosihimu alhameem
Swahili
Hawa wagomvi wawili walio gombana kwa ajili ya Mola wao Mlezi. Basi walio kufuru
watakatiwa nguo za moto, na yatamiminwa juu ya vichwa vyao maji yanayo chemka.
|
Ayah 22:20 الأية
يُصْهَرُ بِهِ مَا فِي بُطُونِهِمْ وَالْجُلُودُ
Yusharu bihi ma fee butoonihimwaljulood
Swahili
Kwa maji hayo vitayayushwa viliomo matumboni mwao, na ngozi zao pia.
|
Ayah 22:21 الأية
وَلَهُم مَّقَامِعُ مِنْ حَدِيدٍ
Walahum maqamiAAu min hadeed
Swahili
Na kwa ajili yao yatakuwapo marungu ya chuma.
|
Ayah 22:22 الأية
كُلَّمَا أَرَادُوا أَن يَخْرُجُوا مِنْهَا مِنْ غَمٍّ أُعِيدُوا فِيهَا وَذُوقُوا
عَذَابَ الْحَرِيقِ
Kullama aradoo an yakhrujoominha min ghammin oAAeedoo feeha wathooqooAAathaba
alhareeq
Swahili
Kila wakitaka kutoka humo kwa sababu ya uchungu watarudishwa humo humo, na
wataambiwa: Onjeni adhabu ya kuungua!
|
Ayah 22:23 الأية
إِنَّ اللَّهَ يُدْخِلُ الَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ جَنَّاتٍ
تَجْرِي مِن تَحْتِهَا الْأَنْهَارُ يُحَلَّوْنَ فِيهَا مِنْ أَسَاوِرَ مِن ذَهَبٍ
وَلُؤْلُؤًا ۖ وَلِبَاسُهُمْ فِيهَا حَرِيرٌ
Inna Allaha yudkhilu allatheenaamanoo waAAamiloo assalihati jannatintajree min
tahtiha al-anharu yuhallawnafeeha min asawira min thahabin walu/lu-anwalibasuhum
feeha hareer
Swahili
Hakika Mwenyezi Mungu atawaingiza walio amini na wakatenda mema katika Bustani
zipitiwazo na mito kati yake. Watapambwa humo kwa mapambo ya mikononi ya dhahabu
na lulu. Na mavazi yao humo ni hariri.
|
Ayah 22:24 الأية
وَهُدُوا إِلَى الطَّيِّبِ مِنَ الْقَوْلِ وَهُدُوا إِلَىٰ صِرَاطِ الْحَمِيدِ
Wahudoo ila attayyibimina alqawli wahudoo ila sirati alhameed
Swahili
Na wataongozwa kwenye maneno mazuri, na wataongozwa kwenye Njia ya Msifiwa.
|
Ayah 22:25 الأية
إِنَّ الَّذِينَ كَفَرُوا وَيَصُدُّونَ عَن سَبِيلِ اللَّهِ وَالْمَسْجِدِ
الْحَرَامِ الَّذِي جَعَلْنَاهُ لِلنَّاسِ سَوَاءً الْعَاكِفُ فِيهِ وَالْبَادِ ۚ
وَمَن يُرِدْ فِيهِ بِإِلْحَادٍ بِظُلْمٍ نُّذِقْهُ مِنْ عَذَابٍ أَلِيمٍ
Inna allatheena kafaroo wayasuddoonaAAan sabeeli Allahi walmasjidi
alharamiallathee jaAAalnahu linnasi sawaanalAAakifu feehi walbadi waman yurid
feehibi-ilhadin bithulmin nuthiqhu min AAathabinaleem
Swahili
Hakika wale walio kufuru na wakazuilia Njia ya Mwenyezi Mungu na Msikiti
Mtakatifu, ambao tumeufanya kwa ajili ya watu wote sawasawa, kwa wakaao humo na
wageni. Na kila atakaye taka kufanya upotofu humo kwa dhulma, basi tutamwonjesha
adhabu chungu.
|
Ayah 22:26 الأية
وَإِذْ بَوَّأْنَا لِإِبْرَاهِيمَ مَكَانَ الْبَيْتِ أَن لَّا تُشْرِكْ بِي شَيْئًا
وَطَهِّرْ بَيْتِيَ لِلطَّائِفِينَ وَالْقَائِمِينَ وَالرُّكَّعِ السُّجُودِ
Wa-ith bawwa/na li-ibraheemamakana albayti an la tushrik bee shay-an
watahhirbaytiya litta-ifeena walqa-imeenawarrukkaAAi assujood
Swahili
Na pale tulipomweka Ibrahim pahala penye ile Nyumba tukamwambia: Usinishirikishe
na chochote; na isafishe Nyumba yangu kwa ajili ya wanao izunguka kwa kut'ufu,
na wanao kaa hapo kwa ibada, na wanao rukuu, na wanao sujudu.
|
Ayah 22:27 الأية
وَأَذِّن فِي النَّاسِ بِالْحَجِّ يَأْتُوكَ رِجَالًا وَعَلَىٰ كُلِّ ضَامِرٍ
يَأْتِينَ مِن كُلِّ فَجٍّ عَمِيقٍ
Waaththin fee annasibilhajji ya/tooka rijalan waAAalakulli damirin ya/teena min
kulli fajjin AAameeq
Swahili
Na watangazie watu Hija; watakujia kwa miguu na juu ya kila ngamia aliye konda,
wakija kutoka katika kila njia ya mbali.
|
Ayah 22:28 الأية
لِّيَشْهَدُوا مَنَافِعَ لَهُمْ وَيَذْكُرُوا اسْمَ اللَّهِ فِي أَيَّامٍ
مَّعْلُومَاتٍ عَلَىٰ مَا رَزَقَهُم مِّن بَهِيمَةِ الْأَنْعَامِ ۖ فَكُلُوا
مِنْهَا وَأَطْعِمُوا الْبَائِسَ الْفَقِيرَ
Liyashhadoo manafiAAa lahum wayathkurooisma Allahi fee ayyamin maAAloomatin
AAalama razaqahum min baheemati al-anAAami fakuloo minhawaatAAimoo alba-isa
alfaqeer
Swahili
Ili washuhudie manufaa yao na walitaje jina la Mwenyezi Mungu katika siku
maalumu juu ya nyama hoa alio waruzuku. Basi kuleni katika hao na mlisheni
mwenye shida aliye fakiri.
|
Ayah 22:29 الأية
ثُمَّ لْيَقْضُوا تَفَثَهُمْ وَلْيُوفُوا نُذُورَهُمْ وَلْيَطَّوَّفُوا بِالْبَيْتِ
الْعَتِيقِ
Thumma lyaqdoo tafathahum walyoofoonuthoorahum walyattawwafoo bilbaytialAAateeq
Swahili
Kisha wajisafishe taka zao, na waondoe nadhiri zao, na waizunguke Nyumba ya
Kale.
|
Ayah 22:30 الأية
ذَٰلِكَ وَمَن يُعَظِّمْ حُرُمَاتِ اللَّهِ فَهُوَ خَيْرٌ لَّهُ عِندَ رَبِّهِ ۗ
وَأُحِلَّتْ لَكُمُ الْأَنْعَامُ إِلَّا مَا يُتْلَىٰ عَلَيْكُمْ ۖ فَاجْتَنِبُوا
الرِّجْسَ مِنَ الْأَوْثَانِ وَاجْتَنِبُوا قَوْلَ الزُّورِ
Thalika waman yuAAaththimhurumati Allahi fahuwa khayrun lahu AAindarabbihi
waohillat lakumu al-anAAamu illa mayutla AAalaykum fajtaniboo arrijsa
minaal-awthani wajtaniboo qawla azzoor
Swahili
Ndio hivyo iwe! Na anaye vitukuza vitakatifu vya Mwenyezi Mungu basi hayo ndiyo
kheri yake mbele ya Mola wake Mlezi. Na mmehalalishiwa nyama hoa ila wale mlio
somewa. Basi jiepusheni na uchafu wa masanamu, na jiepusheni na usemi wa uwongo.
|
Ayah 22:31 الأية
حُنَفَاءَ لِلَّهِ غَيْرَ مُشْرِكِينَ بِهِ ۚ وَمَن يُشْرِكْ بِاللَّهِ
فَكَأَنَّمَا خَرَّ مِنَ السَّمَاءِ فَتَخْطَفُهُ الطَّيْرُ أَوْ تَهْوِي بِهِ
الرِّيحُ فِي مَكَانٍ سَحِيقٍ
Hunafaa lillahi ghayramushrikeena bihi waman yushrik billahi fakaannamakharra
mina assama-i fatakhtafuhu attayruaw tahwee bihi arreehu fee makanin saheeq
Swahili
Kwa kumtakasikia Imani Mwenyezi Mungu, bila ya kumshirikisha. Na anaye
mshirikisha Mwenyezi Mungu ni kama kwamba ameporomoka kutoka mbinguni, kisha
ndege wakamnyakua au upepo ukamtupa pahala mbali.
|
Ayah 22:32 الأية
ذَٰلِكَ وَمَن يُعَظِّمْ شَعَائِرَ اللَّهِ فَإِنَّهَا مِن تَقْوَى الْقُلُوبِ
Thalika waman yuAAaththimshaAAa-ira Allahi fa-innaha min taqwaalquloob
Swahili
Ndio hivyo! Na anayetukuza ibada za Mwenyezi Mungu, basi hayo ni katika
unyenyekevu wa nyoyo.
|
Ayah 22:33 الأية
لَكُمْ فِيهَا مَنَافِعُ إِلَىٰ أَجَلٍ مُّسَمًّى ثُمَّ مَحِلُّهَا إِلَى الْبَيْتِ
الْعَتِيقِ
Lakum feeha manafiAAu ilaajalin musamman thumma mahilluha ila albaytialAAateeq
Swahili
Katika hao nyinyi mna manufaa mpaka muda maalumu. Kisha pahala pa kuchinjiwa
kwake ni kwenye Nyumba ya Kale.
|
Ayah 22:34 الأية
وَلِكُلِّ أُمَّةٍ جَعَلْنَا مَنسَكًا لِّيَذْكُرُوا اسْمَ اللَّهِ عَلَىٰ مَا
رَزَقَهُم مِّن بَهِيمَةِ الْأَنْعَامِ ۗ فَإِلَٰهُكُمْ إِلَٰهٌ وَاحِدٌ فَلَهُ
أَسْلِمُوا ۗ وَبَشِّرِ الْمُخْبِتِينَ
Walikulli ommatin jaAAalna mansakanliyathkuroo isma Allahi AAala marazaqahum min
baheemati al-anAAami fa-ilahukum ilahunwahidun falahu aslimoo wabashshiri
almukhbiteen
Swahili
Na kila umma tumewafanyia mahala pa kuchinjia mihanga ya ibada ili walitaje jina
la Mwenyezi Mungu juu ya vile walivyo ruzukiwa katika wanyama wa mifugo. Basi
Mungu wenu ni Mungu Mmoja tu. Jisalimishieni kwake tu, na wabashirie
wanyenyekevu,
|
Ayah 22:35 الأية
الَّذِينَ إِذَا ذُكِرَ اللَّهُ وَجِلَتْ قُلُوبُهُمْ وَالصَّابِرِينَ عَلَىٰ مَا
أَصَابَهُمْ وَالْمُقِيمِي الصَّلَاةِ وَمِمَّا رَزَقْنَاهُمْ يُنفِقُونَ
Allatheena itha thukiraAllahu wajilat quloobuhum wassabireenaAAala ma asabahum
walmuqeemee assalatiwamimma razaqnahum yunfiqoon
Swahili
Ambao, anapo tajwa Mwenyezi Mungu nyoyo zao hutetemeka, na wanao vumilia kwa
yanao wasibu, na wanao shika Sala, na wanatoa katika tulivyo waruzuku.
|
Ayah 22:36 الأية
وَالْبُدْنَ جَعَلْنَاهَا لَكُم مِّن شَعَائِرِ اللَّهِ لَكُمْ فِيهَا خَيْرٌ ۖ
فَاذْكُرُوا اسْمَ اللَّهِ عَلَيْهَا صَوَافَّ ۖ فَإِذَا وَجَبَتْ جُنُوبُهَا
فَكُلُوا مِنْهَا وَأَطْعِمُوا الْقَانِعَ وَالْمُعْتَرَّ ۚ كَذَٰلِكَ
سَخَّرْنَاهَا لَكُمْ لَعَلَّكُمْ تَشْكُرُونَ
Walbudna jaAAalnahalakum min shaAAa-iri Allahi lakum feehakhayrun fathkuroo isma
Allahi AAalayhasawaffa fa-itha wajabat junoobuhafakuloo minha waatAAimoo
alqaniAAa walmuAAtarrakathalika sakhkharnaha lakum laAAallakumtashkuroon
Swahili
Na ngamia wa sadaka tumekufanyieni kuwa ni kudhihirisha matukuzo kwa Mwenyezi
Mungu; kwa hao mna kheri nyingi. Basi litajeni jina la Mwenyezi Mungu juu yao
wanapo simama kwa safu. Na waangukapo ubavu kuleni katika hao na walisheni walio
kinai na wanao lazimika kuomba. Ndio kama hivi tumewafanya hawa wanyama dhalili
kwenu ili mpate kushukuru.
|
Ayah 22:37 الأية
لَن يَنَالَ اللَّهَ لُحُومُهَا وَلَا دِمَاؤُهَا وَلَٰكِن يَنَالُهُ التَّقْوَىٰ
مِنكُمْ ۚ كَذَٰلِكَ سَخَّرَهَا لَكُمْ لِتُكَبِّرُوا اللَّهَ عَلَىٰ مَا هَدَاكُمْ
ۗ وَبَشِّرِ الْمُحْسِنِينَ
Lan yanala Allaha luhoomuhawala dimaoha walakin yanaluhuattaqwa minkum kathalika
sakhkharahalakum litukabbiroo Allaha AAala ma hadakumwabashshiri almuhsineen
Swahili
Nyama zao hazimfikii Mwenyezi Mungu wala damu zao, lakini unamfikia uchamngu
wenu. Namna hivi tumewadhalilisha kwenu ili mumtukuze Mwenyezi Mungu kwa alivyo
kuongoeni. Na wabashirie wafanyao mema.
|
Ayah 22:38 الأية
إِنَّ اللَّهَ يُدَافِعُ عَنِ الَّذِينَ آمَنُوا ۗ إِنَّ اللَّهَ لَا يُحِبُّ كُلَّ
خَوَّانٍ كَفُورٍ
Inna Allaha yudafiAAu AAaniallatheena amanoo inna Allaha la yuhibbukulla
khawwanin kafoor
Swahili
Hakika Mwenyezi Mungu huwakinga walio amini. Hakika Mwenyezi Mungu hampendi kila
khaini mwingi wa kukanya mema.
|
Ayah 22:39 الأية
أُذِنَ لِلَّذِينَ يُقَاتَلُونَ بِأَنَّهُمْ ظُلِمُوا ۚ وَإِنَّ اللَّهَ عَلَىٰ
نَصْرِهِمْ لَقَدِيرٌ
Othina lillatheena yuqataloonabi-annahum thulimoo wa-inna Allaha AAalanasrihim
laqadeer
Swahili
Wameruhusiwa kupigana wale wanao pigwa vita kwa sababu wamedhulumiwa - na kwa
yakini Mwenyezi Mungu ni Muweza wa kuwasaidia -
|
Ayah 22:40 الأية
الَّذِينَ أُخْرِجُوا مِن دِيَارِهِم بِغَيْرِ حَقٍّ إِلَّا أَن يَقُولُوا رَبُّنَا
اللَّهُ ۗ وَلَوْلَا دَفْعُ اللَّهِ النَّاسَ بَعْضَهُم بِبَعْضٍ لَّهُدِّمَتْ
صَوَامِعُ وَبِيَعٌ وَصَلَوَاتٌ وَمَسَاجِدُ يُذْكَرُ فِيهَا اسْمُ اللَّهِ
كَثِيرًا ۗ وَلَيَنصُرَنَّ اللَّهُ مَن يَنصُرُهُ ۗ إِنَّ اللَّهَ لَقَوِيٌّ
عَزِيزٌ
Allatheena okhrijoo min diyarihimbighayri haqqin illa an yaqooloo rabbuna
Allahuwalawla dafAAu Allahi annasa baAAdahumbibaAAdin lahuddimat sawamiAAu
wabiyaAAun wasalawatunwamasajidu yuthkaru feeha ismu Allahikatheeran
walayansuranna Allahu man yansuruhuinna Allaha laqawiyyun AAazeez
Swahili
Wale ambao wametolewa majumbani mwao pasipo haki, ila kwa kuwa wanasema: Mola
wetu Mlezi ni Mwenyezi Mungu! Na lau kuwa Mwenyezi Mungu hawakingi watu kwa
watu, basi hapana shaka zingeli vunjwa nymba za wat'awa, na makanisa, na
masinagogi, na misikiti, ambamo ndani yake jina la Mwenyezi Mungu linatajwa kwa
wingi. Na bila ya shaka Mwenyezi Mungu humsaidia yule anaye msaidia Yeye. Hakika
Mwenyezi Mungu ni Mwenye nguvu Mtukufu.
|
Ayah 22:41 الأية
الَّذِينَ إِن مَّكَّنَّاهُمْ فِي الْأَرْضِ أَقَامُوا الصَّلَاةَ وَآتَوُا
الزَّكَاةَ وَأَمَرُوا بِالْمَعْرُوفِ وَنَهَوْا عَنِ الْمُنكَرِ ۗ وَلِلَّهِ
عَاقِبَةُ الْأُمُورِ
Allatheena in makkannahum feeal-ardi aqamoo assalata waatawooazzakata waamaroo
bilmaAAroofi wanahawAAani almunkari walillahi AAaqibatu al-omoor
Swahili
Wale ambao tukiwapa madaraka katika nchi husimamisha Sala, na wakatoa Zaka, na
wakaamrisha mema, na wakakataza mabaya. Na kwa Mwenyezi Mungu ndio marejeo ya
mambo yote.
|
Ayah 22:42 الأية
وَإِن يُكَذِّبُوكَ فَقَدْ كَذَّبَتْ قَبْلَهُمْ قَوْمُ نُوحٍ وَعَادٌ وَثَمُودُ
Wa-in yukaththibooka faqad kaththabatqablahum qawmu noohin waAAadun wathamood
Swahili
Na wakikukanusha basi walikwisha kanusha kabla yao watu wa Nuhu, na kina A'ad na
kina Thamud,
|
Ayah 22:43 الأية
وَقَوْمُ إِبْرَاهِيمَ وَقَوْمُ لُوطٍ
Waqawmu ibraheema waqawmu loot
Swahili
Na watu wa Ibrahim na watu wa Lut'i
|
Ayah 22:44 الأية
وَأَصْحَابُ مَدْيَنَ ۖ وَكُذِّبَ مُوسَىٰ فَأَمْلَيْتُ لِلْكَافِرِينَ ثُمَّ
أَخَذْتُهُمْ ۖ فَكَيْفَ كَانَ نَكِيرِ
Waas-habu madyana wakuththibamoosa faamlaytu lilkafireena thumma
akhathtuhumfakayfa kana nakeer
Swahili
Na watu wa Madiana. Na Musa pia alikanushwa. Nikawapa muda makafiri, kisha
nikawatia mkononi. Basi ilikuwaje adhabu yangu!
|
Ayah 22:45 الأية
فَكَأَيِّن مِّن قَرْيَةٍ أَهْلَكْنَاهَا وَهِيَ ظَالِمَةٌ فَهِيَ خَاوِيَةٌ عَلَىٰ
عُرُوشِهَا وَبِئْرٍ مُّعَطَّلَةٍ وَقَصْرٍ مَّشِيدٍ
Fakaayyin min qaryatin ahlaknahawahiya thalimatun fahiya khawiyatunAAala
AAurooshiha wabi/rin muAAattalatinwaqasrin masheed
Swahili
Miji mingapi tuliiangamiza iliyo kuwa ikidhulumu, ikawa imebaki magofu, na
visima vilivyo achwa, na majumba yaliyo kuwa madhubuti?
|
Ayah 22:46 الأية
أَفَلَمْ يَسِيرُوا فِي الْأَرْضِ فَتَكُونَ لَهُمْ قُلُوبٌ يَعْقِلُونَ بِهَا أَوْ
آذَانٌ يَسْمَعُونَ بِهَا ۖ فَإِنَّهَا لَا تَعْمَى الْأَبْصَارُ وَلَٰكِن تَعْمَى
الْقُلُوبُ الَّتِي فِي الصُّدُورِ
Afalam yaseeroo fee al-ardi fatakoonalahum quloobun yaAAqiloona biha aw
athanunyasmaAAoona biha fa-innaha la taAAmaal-absaru walakin taAAma alquloobu
allateefee assudoor
Swahili
Je! Hawatembei katika ardhi ili wapate kuwa na nyoyo zao za kuzingatia, au
masikio ya kusikilia? Kwani hakika si macho yanayo pofuka, lakini zinazo pofuka
ni nyoyo ziliomo vifuani.
|
Ayah 22:47 الأية
وَيَسْتَعْجِلُونَكَ بِالْعَذَابِ وَلَن يُخْلِفَ اللَّهُ وَعْدَهُ ۚ وَإِنَّ
يَوْمًا عِندَ رَبِّكَ كَأَلْفِ سَنَةٍ مِّمَّا تَعُدُّونَ
WayastaAAjiloonaka bilAAathabiwalan yukhlifa Allahu waAAdahu wa-inna yawman
AAindarabbika kaalfi sanatin mimma taAAuddoon
Swahili
Na wanakuhimiza ulete adhabu, lakini Mwenyezi Mungu hatakwenda kinyume na ahadi
yake kabisa. Na hakika siku moja kwa Mola wako Mlezi ni kama miaka elfu mnavyo
hisabu nyinyi.
|
Ayah 22:48 الأية
وَكَأَيِّن مِّن قَرْيَةٍ أَمْلَيْتُ لَهَا وَهِيَ ظَالِمَةٌ ثُمَّ أَخَذْتُهَا
وَإِلَيَّ الْمَصِيرُ
Wakaayyin min qaryatin amlaytu lahawahiya thalimatun thumma akhathtuhawa-ilayya
almaseer
Swahili
Na miji mingapi niliipa muda na hali ilikuwa imedhulumu, na kisha nikaitia
mkononi? Na kwangu Mimi ndio marudio yote.
|
Ayah 22:49 الأية
قُلْ يَا أَيُّهَا النَّاسُ إِنَّمَا أَنَا لَكُمْ نَذِيرٌ مُّبِينٌ
Qul ya ayyuha annasuinnama ana lakum natheerun mubeen
Swahili
Sema: Enyi watu! Hakika mimi ni mwonyaji kwenu niliye dhaahiri.
|
Ayah 22:50 الأية
فَالَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ لَهُم مَّغْفِرَةٌ وَرِزْقٌ كَرِيمٌ
Fallatheena amanoowaAAamiloo assalihati lahum maghfiratunwarizqun kareem
Swahili
Basi walio amini na wakatenda mema watapata maghfira na riziki za ukarimu.
|
Ayah 22:51 الأية
وَالَّذِينَ سَعَوْا فِي آيَاتِنَا مُعَاجِزِينَ أُولَٰئِكَ أَصْحَابُ الْجَحِيمِ
Wallatheena saAAaw fee ayatinamuAAajizeena ola-ika as-habu aljaheem
Swahili
Na wanao jitahidi kuzipinga Aya zetu hao ndio watu wa Motoni.
|
Ayah 22:52 الأية
وَمَا أَرْسَلْنَا مِن قَبْلِكَ مِن رَّسُولٍ وَلَا نَبِيٍّ إِلَّا إِذَا تَمَنَّىٰ
أَلْقَى الشَّيْطَانُ فِي أُمْنِيَّتِهِ فَيَنسَخُ اللَّهُ مَا يُلْقِي
الشَّيْطَانُ ثُمَّ يُحْكِمُ اللَّهُ آيَاتِهِ ۗ وَاللَّهُ عَلِيمٌ حَكِيمٌ
Wama arsalna min qablika minrasoolin wala nabiyyin illa itha tamannaalqa
ashshaytanu fee omniyyatihi fayansakhuAllahu ma yulqee ashshaytanu thummayuhkimu
Allahu ayatihi wallahuAAaleemun hakeem
Swahili
Na hatukumtuma kabla yako Mtume wala Nabii ila anapo soma, Shet'ani hutumbukiza
katika masomo yake. Lakini Mwenyezi Mungu huyaondoa anayo yatia Shet'ani; kisha
Mwenyezi Mungu huzithibitisha Aya zake. Na Mwenyezi Mungu ni Mjuzi Mwenye
hikima.
|
Ayah 22:53 الأية
لِّيَجْعَلَ مَا يُلْقِي الشَّيْطَانُ فِتْنَةً لِّلَّذِينَ فِي قُلُوبِهِم مَّرَضٌ
وَالْقَاسِيَةِ قُلُوبُهُمْ ۗ وَإِنَّ الظَّالِمِينَ لَفِي شِقَاقٍ بَعِيدٍ
LiyajAAala ma yulqee ashshaytanufitnatan lillatheena fee quloobihim maradun
walqasiyatiquloobuhum wa-inna aththalimeenalafee shiqaqin baAAeed
Swahili
Hayo ni ili alifanye lile analo litia Shet'ani liwe ni fitna kwa wale wenye
maradhi ndani ya nyoyo zao, na wale ambao nyoyo zao ni ngumu. Na hakika
madhaalimu wamo katika mfarakano wa mbali.
|
Ayah 22:54 الأية
وَلِيَعْلَمَ الَّذِينَ أُوتُوا الْعِلْمَ أَنَّهُ الْحَقُّ مِن رَّبِّكَ
فَيُؤْمِنُوا بِهِ فَتُخْبِتَ لَهُ قُلُوبُهُمْ ۗ وَإِنَّ اللَّهَ لَهَادِ
الَّذِينَ آمَنُوا إِلَىٰ صِرَاطٍ مُّسْتَقِيمٍ
WaliyaAAlama allatheena ootooalAAilma annahu alhaqqu min rabbika fayu/minoo
bihifatukhbita lahu quloobuhum wa-inna Allaha lahadiallatheena amanoo ila
siratinmustaqeem
Swahili
Na ili walio pewa ilimu wajue kuwa hayo ni Haki itokayo kwa Mola wako Mlezi na
waamini, na zipate kutua nyoyo zao. Na hakika Mwenyezi Mungu ndiye anaye waongoa
wenye kuamini kwenye Njia Iliyo Nyooka.
|
Ayah 22:55 الأية
وَلَا يَزَالُ الَّذِينَ كَفَرُوا فِي مِرْيَةٍ مِّنْهُ حَتَّىٰ تَأْتِيَهُمُ
السَّاعَةُ بَغْتَةً أَوْ يَأْتِيَهُمْ عَذَابُ يَوْمٍ عَقِيمٍ
Wala yazalu allatheenakafaroo fee miryatin minhu hatta ta/tiyahumu
assaAAatubaghtatan aw ya/tiyahum AAathabu yawmin AAaqeem
Swahili
Na walio kufuru hawatoacha kuwa katika wasiwasi kwa hilo mpaka Saa iwafikie
ghafla, au iwafikie adhabu ya Siku Tasa.
|
Ayah 22:56 الأية
الْمُلْكُ يَوْمَئِذٍ لِّلَّهِ يَحْكُمُ بَيْنَهُمْ ۚ فَالَّذِينَ آمَنُوا
وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ فِي جَنَّاتِ النَّعِيمِ
Almulku yawma-ithin lillahi yahkumubaynahum fallatheena amanoo waAAamiloo
assalihatifee jannati annaAAeem
Swahili
Ufalme wote siku hiyo utakuwa wa Mwenyezi Mungu. Atahukumu baina yao. Basi walio
amini na wakatenda mema watakuwa katika Bustani zenye neema.
|
Ayah 22:57 الأية
وَالَّذِينَ كَفَرُوا وَكَذَّبُوا بِآيَاتِنَا فَأُولَٰئِكَ لَهُمْ عَذَابٌ
مُّهِينٌ
Wallatheena kafaroo wakaththaboobi-ayatina faola-ika lahum AAathabunmuheen
Swahili
Na walio kufuru na kuzikanusha Ishara zetu, basi hao watapata adhabu ya
kufedhehesha.
|
Ayah 22:58 الأية
وَالَّذِينَ هَاجَرُوا فِي سَبِيلِ اللَّهِ ثُمَّ قُتِلُوا أَوْ مَاتُوا
لَيَرْزُقَنَّهُمُ اللَّهُ رِزْقًا حَسَنًا ۚ وَإِنَّ اللَّهَ لَهُوَ خَيْرُ
الرَّازِقِينَ
Wallatheena hajaroofee sabeeli Allahi thumma qutiloo aw matoolayarzuqannahumu
Allahu rizqan hasanan wa-inna Allahalahuwa khayru arraziqeen
Swahili
Na walio hama kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, kisha wakauwawa au wakafa, bila ya
shaka Mwenyezi Mungu atawaruzuku riziki njema. Na hakika Mwenyezi Mungu ni Mbora
wa wanao ruzuku.
|
Ayah 22:59 الأية
لَيُدْخِلَنَّهُم مُّدْخَلًا يَرْضَوْنَهُ ۗ وَإِنَّ اللَّهَ لَعَلِيمٌ حَلِيمٌ
Layudkhilannahum mudkhalan yardawnahuwa-inna Allaha laAAaleemun haleem
Swahili
BIla ya shaka atawaingiza pahala watakapo paridhia. Na hakika Mwenyezi Mungu ni
Mjuzi na Mpole.
|
Ayah 22:60 الأية
ذَٰلِكَ وَمَنْ عَاقَبَ بِمِثْلِ مَا عُوقِبَ بِهِ ثُمَّ بُغِيَ عَلَيْهِ
لَيَنصُرَنَّهُ اللَّهُ ۗ إِنَّ اللَّهَ لَعَفُوٌّ غَفُورٌ
Thalika waman AAaqaba bimithlima AAooqiba bihi thumma bughiya AAalayhi
layansurannahuAllahu inna Allaha laAAafuwwun ghafoor
Swahili
Ndio namna hivi. Na anaye lipiza mfano wa alivyo adhibiwa, kisha akadhulumiwa,
basi hapana shaka Mwenyezi Mungu atamsaidia. Hakika Mwenyezi Mungu ni Msamehevu
Mwenye maghfira.
|
Ayah 22:61 الأية
ذَٰلِكَ بِأَنَّ اللَّهَ يُولِجُ اللَّيْلَ فِي النَّهَارِ وَيُولِجُ النَّهَارَ
فِي اللَّيْلِ وَأَنَّ اللَّهَ سَمِيعٌ بَصِيرٌ
Thalika bi-anna Allaha yoolijuallayla fee annahari wayooliju annaharafee allayli
waanna Allaha sameeAAun baseer
Swahili
Hayo ni kwa kuwa Mwenyezi Mungu huingiza usiku katika mchana, na huuingiza
mchana katika usiku, na ya kwamba Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusikia Mwenye kuona.
|
Ayah 22:62 الأية
ذَٰلِكَ بِأَنَّ اللَّهَ هُوَ الْحَقُّ وَأَنَّ مَا يَدْعُونَ مِن دُونِهِ هُوَ
الْبَاطِلُ وَأَنَّ اللَّهَ هُوَ الْعَلِيُّ الْكَبِيرُ
Thalika bi-anna Allaha huwa alhaqquwaanna ma yadAAoona min doonihi huwa
albatiluwaanna Allaha huwa alAAaliyyu alkabeer
Swahili
Hayo ni kwa kuwa Mwenyezi Mungu ndiye Wa Kweli, na kwamba wale wanao waomba
badala yake, ni baat'ili, na hakika Mwenyezi Mungu ndiye Aliye Juu na ndiye
Mkubwa.
|
Ayah 22:63 الأية
أَلَمْ تَرَ أَنَّ اللَّهَ أَنزَلَ مِنَ السَّمَاءِ مَاءً فَتُصْبِحُ الْأَرْضُ
مُخْضَرَّةً ۗ إِنَّ اللَّهَ لَطِيفٌ خَبِيرٌ
Alam tara anna Allaha anzala mina assama-imaan fatusbihu al-ardu
mukhdarrataninna Allaha lateefun khabeer
Swahili
Je! Huoni kwamba Mwenyezi Mungu huteremsha maji kutoka mbinguni, na mara ardhi
inakuwa chanikiwiti? Hakika Mwenyezi Mungu ni Mpole na Mwenye kujua.
|
Ayah 22:64 الأية
لَّهُ مَا فِي السَّمَاوَاتِ وَمَا فِي الْأَرْضِ ۗ وَإِنَّ اللَّهَ لَهُوَ
الْغَنِيُّ الْحَمِيدُ
Lahu ma fee assamawatiwama fee al-ardi wa-inna Allaha lahuwaalghaniyyu alhameed
Swahili
Ni vyake viliomo mbinguni na viliomo katika ardhi. Na hakika Mwenyezi Mungu ni
Mwenye kujitosha na Mwenye kusifiwa.
|
Ayah 22:65 الأية
أَلَمْ تَرَ أَنَّ اللَّهَ سَخَّرَ لَكُم مَّا فِي الْأَرْضِ وَالْفُلْكَ تَجْرِي
فِي الْبَحْرِ بِأَمْرِهِ وَيُمْسِكُ السَّمَاءَ أَن تَقَعَ عَلَى الْأَرْضِ إِلَّا
بِإِذْنِهِ ۗ إِنَّ اللَّهَ بِالنَّاسِ لَرَءُوفٌ رَّحِيمٌ
Alam tara anna Allaha sakhkhara lakumma fee al-ardi walfulka tajree fee
albahribi-amrihi wayumsiku assamaa an taqaAAa AAalaal-ardi illa bi-ithnihi inna
Allahabinnasi laraoofun raheem
Swahili
Je! Huoni kwamba Mwenyezi Mungu amevidhalilisha kwenu viliomo katika ardhi, na
marikebu zipitazo baharini kwa amri yake, na amezishika mbingu zisianguke juu ya
ardhi ila kwa idhini yake. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye huruma kwa watu,
Mwenye kurehemu.
|
Ayah 22:66 الأية
وَهُوَ الَّذِي أَحْيَاكُمْ ثُمَّ يُمِيتُكُمْ ثُمَّ يُحْيِيكُمْ ۗ إِنَّ
الْإِنسَانَ لَكَفُورٌ
Wahuwa allathee ahyakumthumma yumeetukum thumma yuhyeekum inna al-insanalakafoor
Swahili
Na Yeye ndiye aliye kuhuisheni kisha akakufisheni, na kisha atakufufueni. Hakika
mwanaadamu hana fadhila.
|
Ayah 22:67 الأية
لِّكُلِّ أُمَّةٍ جَعَلْنَا مَنسَكًا هُمْ نَاسِكُوهُ ۖ فَلَا يُنَازِعُنَّكَ فِي
الْأَمْرِ ۚ وَادْعُ إِلَىٰ رَبِّكَ ۖ إِنَّكَ لَعَلَىٰ هُدًى مُّسْتَقِيمٍ
Likulli ommatin jaAAalna mansakan humnasikoohu fala yunaziAAunnaka fee al-amri
wadAAuila rabbika innaka laAAala hudan mustaqeem
Swahili
Kila umma tumewajaalia na ibada zao wanazo zishika. Basi wasizozane nawe katika
jambo hili. Na waite watu kwendea kwa Mola wako Mlezi. Hakika wewe uko kwenye
Uwongofu Ulio Nyooka.
|
Ayah 22:68 الأية
وَإِن جَادَلُوكَ فَقُلِ اللَّهُ أَعْلَمُ بِمَا تَعْمَلُونَ
Wa-in jadalooka faquli AllahuaAAlamu bima taAAmaloon
Swahili
Na wakikujadili basi sema: Mwenyezi Mungu anajua zaidi mnayo yatenda.
|
Ayah 22:69 الأية
اللَّهُ يَحْكُمُ بَيْنَكُمْ يَوْمَ الْقِيَامَةِ فِيمَا كُنتُمْ فِيهِ
تَخْتَلِفُونَ
Allahu yahkumu baynakum yawmaalqiyamati feema kuntum feehi takhtalifoon
Swahili
Mwenyezi Mungu atahukumu baina yenu Siku ya Kiyama katika hayo mnayo
khitalifiana.
|
Ayah 22:70 الأية
أَلَمْ تَعْلَمْ أَنَّ اللَّهَ يَعْلَمُ مَا فِي السَّمَاءِ وَالْأَرْضِ ۗ إِنَّ
ذَٰلِكَ فِي كِتَابٍ ۚ إِنَّ ذَٰلِكَ عَلَى اللَّهِ يَسِيرٌ
Alam taAAlam anna Allaha yaAAlamu mafee assama-i wal-ardi inna thalikafee
kitabin inna thalika AAala Allahiyaseer
Swahili
Je! Hujui kwamba Mwenyezi Mungu anayajua yaliomo mbinguni na katika ardhi?
Hakika hayo yamo Kitabuni. Hakika hayo kwa Mwenyezi Mungu ni mepesi.
|
Ayah 22:71 الأية
وَيَعْبُدُونَ مِن دُونِ اللَّهِ مَا لَمْ يُنَزِّلْ بِهِ سُلْطَانًا وَمَا لَيْسَ
لَهُم بِهِ عِلْمٌ ۗ وَمَا لِلظَّالِمِينَ مِن نَّصِيرٍ
WayaAAbudoona min dooni Allahi malam yunazzil bihi sultanan wama laysa lahum
bihiAAilmun wama liththalimeenamin naseer
Swahili
Na wanaabudu badala ya Mwenyezi Mungu ambavyo hakuviteremshia ushahidi, na
ambavyo hawana ujuzi navyo. Na madhaalimu hawatakuwa na wa kuwasaidia.
|
Ayah 22:72 الأية
وَإِذَا تُتْلَىٰ عَلَيْهِمْ آيَاتُنَا بَيِّنَاتٍ تَعْرِفُ فِي وُجُوهِ الَّذِينَ
كَفَرُوا الْمُنكَرَ ۖ يَكَادُونَ يَسْطُونَ بِالَّذِينَ يَتْلُونَ عَلَيْهِمْ
آيَاتِنَا ۗ قُلْ أَفَأُنَبِّئُكُم بِشَرٍّ مِّن ذَٰلِكُمُ ۗ النَّارُ وَعَدَهَا
اللَّهُ الَّذِينَ كَفَرُوا ۖ وَبِئْسَ الْمَصِيرُ
Wa-itha tutla AAalayhim ayatunabayyinatin taAArifu fee wujoohi allatheena
kafarooalmunkara yakadoona yastoona billatheenayatloona AAalayhim ayatina
qulafaonabbi-okum bisharrin min thalikum annaruwaAAadaha Allahu allatheena
kafaroo wabi/saalmaseer
Swahili
Na wanapo somewa Aya zetu zilizo wazi utaona chuki katika nyuso za walio kufuru.
Hukaribia kuwavamia wale wanao wasomea hizo Aya zetu. Sema: Je! Nikwambieni
yaliyo mabaya zaidi kuliko haya? Ni Moto. Mwenyezi Mungu amewaahidi walio
kufuru, na ni marudio mabaya hayo.
|
Ayah 22:73 الأية
يَا أَيُّهَا النَّاسُ ضُرِبَ مَثَلٌ فَاسْتَمِعُوا لَهُ ۚ إِنَّ الَّذِينَ
تَدْعُونَ مِن دُونِ اللَّهِ لَن يَخْلُقُوا ذُبَابًا وَلَوِ اجْتَمَعُوا لَهُ ۖ
وَإِن يَسْلُبْهُمُ الذُّبَابُ شَيْئًا لَّا يَسْتَنقِذُوهُ مِنْهُ ۚ ضَعُفَ
الطَّالِبُ وَالْمَطْلُوبُ
Ya ayyuha annasuduriba mathalun fastamiAAoo lahu inna allatheenatadAAoona min
dooni Allahi lan yakhluqoo thubabanwalawi ijtamaAAoo lahu wa-in yaslubuhumu
aththubabushay-an la yastanqithoohu minhu daAAufa attalibuwalmatloob
Swahili
Enyi watu! Unapigwa mfano, basi usikilizeni. Hakika wale mnao waomba badala ya
Mwenyezi Mungu, hawatoumba hata nzi ijapo kuwa watajumuika kwa hilo. Na nzi
akiwapokonya kitu hawawezi kukipata kwake. Amedhoofika kweli huyo mwenye kutaka
na mwenye kutakiwa.
|
Ayah 22:74 الأية
مَا قَدَرُوا اللَّهَ حَقَّ قَدْرِهِ ۗ إِنَّ اللَّهَ لَقَوِيٌّ عَزِيزٌ
Ma qadaroo Allaha haqqaqadrihi inna Allaha laqawiyyun AAazeez
Swahili
Hawakumuadhimisha Mwenyezi Mungu anavyo stahiki kuadhimishwa. Hakika Mwenyezi
Mungu bila ya shaka ni Mwenye kushinda.
|
Ayah 22:75 الأية
اللَّهُ يَصْطَفِي مِنَ الْمَلَائِكَةِ رُسُلًا وَمِنَ النَّاسِ ۚ إِنَّ اللَّهَ
سَمِيعٌ بَصِيرٌ
Allahu yastafee mina almala-ikatirusulan wamina annasi inna Allaha
sameeAAunbaseer
Swahili
Mwenyezi Mungu huteuwa Wajumbe miongoni mwa Malaika na miongoni mwa watu. Hakika
Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusikia, Mwenye kuona.
|
Ayah 22:76 الأية
يَعْلَمُ مَا بَيْنَ أَيْدِيهِمْ وَمَا خَلْفَهُمْ ۗ وَإِلَى اللَّهِ تُرْجَعُ
الْأُمُورُ
YaAAlamu ma bayna aydeehim wamakhalfahum wa-ila Allahi turjaAAu al-omoor
Swahili
Anayajua yaliyo mbele yao na yaliyo nyuma yao. Na kwa Mwenyezi Mungu
yatarejeshwa mambo yote.
|
Ayah 22:77 الأية
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا ارْكَعُوا وَاسْجُدُوا وَاعْبُدُوا رَبَّكُمْ
وَافْعَلُوا الْخَيْرَ لَعَلَّكُمْ تُفْلِحُونَ ۩
Ya ayyuha allatheena amanooirkaAAoo wasjudoo waAAbudoo rabbakum
wafAAalooalkhayra laAAallakum tuflihoon
Swahili
Enyi mlio amini! Rukuuni na msujudu, na muabuduni Mola wenu Mlezi, na tendeni
mema, ili mfanikiwe.
|
Ayah 22:78 الأية
وَجَاهِدُوا فِي اللَّهِ حَقَّ جِهَادِهِ ۚ هُوَ اجْتَبَاكُمْ وَمَا جَعَلَ
عَلَيْكُمْ فِي الدِّينِ مِنْ حَرَجٍ ۚ مِّلَّةَ أَبِيكُمْ إِبْرَاهِيمَ ۚ هُوَ
سَمَّاكُمُ الْمُسْلِمِينَ مِن قَبْلُ وَفِي هَٰذَا لِيَكُونَ الرَّسُولُ شَهِيدًا
عَلَيْكُمْ وَتَكُونُوا شُهَدَاءَ عَلَى النَّاسِ ۚ فَأَقِيمُوا الصَّلَاةَ وَآتُوا
الزَّكَاةَ وَاعْتَصِمُوا بِاللَّهِ هُوَ مَوْلَاكُمْ ۖ فَنِعْمَ الْمَوْلَىٰ
وَنِعْمَ النَّصِيرُ
Wajahidoo fee Allahi haqqajihadihi huwa ijtabakum wama jaAAalaAAalaykum fee
addeeni min harajin millata abeekumibraheema huwa sammakumu almuslimeena min
qabluwafee hatha liyakoona arrasoolu shaheedanAAalaykum watakoonoo shuhadaa
AAala annasifaaqeemoo assalata waatoo azzakatawaAAtasimoo billahi huwa
mawlakumfaniAAma almawla waniAAma annaseer
Swahili
Na fanyeni juhudi kwa ajili ya Mwenyezi Mungu kama inavyo stahiki jihadi yake.
Yeye amekuteueni. Wala hakuweka juu yenu mambo mazito katika Dini. Nayo ni mila
ya baba yenu Ibrahim. Yeye (Mwenyezi Mungu) alikuiteni Waislamu tangu zamani, na
katika hii (Qur'ani) pia, ili awe Mtume shahidi juu yenu, na nyinyi muwe
mashahidi kwa watu. Basi shikeni Sala na toeni Zaka na shikamaneni na Mwenyezi
Mungu. Yeye ndiye Mlinzi wenu, Mlinzi bora kabisa, na Msaidizi bora kabisa.
|
©
EsinIslam.Com Designed & produced by The Awqaf London. Please pray for us
|