First Ayah 1 الأية الأوليبِسْم ِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ
طس ۚ تِلْكَ آيَاتُ الْقُرْآنِ وَكِتَابٍ مُّبِينٍ
Ta-seen tilka ayatualqur-ani wakitabin mubeen
Swahili
T'aa Siin. (T'.S.), Hizi ni Aya za Qur'ani na Kitabu kinacho bainisha;
|
Ayah 27:2 الأية
هُدًى وَبُشْرَىٰ لِلْمُؤْمِنِينَ
Hudan wabushra lilmu/mineen
Swahili
Uwongofu na bishara kwa Waumini,
|
Ayah 27:3 الأية
الَّذِينَ يُقِيمُونَ الصَّلَاةَ وَيُؤْتُونَ الزَّكَاةَ وَهُم بِالْآخِرَةِ هُمْ
يُوقِنُونَ
Allatheena yuqeemoona assalatawayu/toona azzakata wahum bil-akhiratihum
yooqinoon
Swahili
Ambao wanashika Sala, na wanatoa Zaka, na Akhera wana yakini nayo.
|
Ayah 27:4 الأية
إِنَّ الَّذِينَ لَا يُؤْمِنُونَ بِالْآخِرَةِ زَيَّنَّا لَهُمْ أَعْمَالَهُمْ
فَهُمْ يَعْمَهُونَ
Inna allatheena la yu/minoonabil-akhirati zayyanna lahum aAAmalahumfahum
yaAAmahoon
Swahili
Kwa hakika wale wasio iamini Akhera tumewapambia vitendo vyao, kwa hivyo
wanatangatanga ovyo.
|
Ayah 27:5 الأية
أُولَٰئِكَ الَّذِينَ لَهُمْ سُوءُ الْعَذَابِ وَهُمْ فِي الْآخِرَةِ هُمُ
الْأَخْسَرُونَ
Ola-ika allatheena lahum soo-oalAAathabi wahum fee al-akhirati humu al-akhsaroon
Swahili
Hao ndio watapata adhabu mbaya kabisa, na hao katika Akhera ndio watapata
khasara zaidi.
|
Ayah 27:6 الأية
وَإِنَّكَ لَتُلَقَّى الْقُرْآنَ مِن لَّدُنْ حَكِيمٍ عَلِيمٍ
Wa-innaka latulaqqa alqur-anamin ladun hakeemin AAaleem
Swahili
Na hakika wewe unafundishwa Qur'ani inayo tokana kwake Mwenye hikima Mwenye
kujua.
|
Ayah 27:7 الأية
إِذْ قَالَ مُوسَىٰ لِأَهْلِهِ إِنِّي آنَسْتُ نَارًا سَآتِيكُم مِّنْهَا بِخَبَرٍ
أَوْ آتِيكُم بِشِهَابٍ قَبَسٍ لَّعَلَّكُمْ تَصْطَلُونَ
Ith qala moosa li-ahlihiinnee anastu naran saateekum minhabikhabarin aw ateekum
bishihabin qabasinlaAAallakum tastaloon
Swahili
(Kumbuka) Musa alipo waambia ahali zake: Hakika nimeona moto, nitakwenda
nikuleteeni khabari, au nitakuleteeni kijinga kinacho waka ili mpate kuota moto.
|
Ayah 27:8 الأية
فَلَمَّا جَاءَهَا نُودِيَ أَن بُورِكَ مَن فِي النَّارِ وَمَنْ حَوْلَهَا
وَسُبْحَانَ اللَّهِ رَبِّ الْعَالَمِينَ
Falamma jaaha noodiya anboorika man fee annari waman hawlahawasubhana Allahi
rabbi alAAalameen
Swahili
Basi alipo fika ilinadiwa: Amebarikiwa aliomo katika moto huu na walioko
pembezoni mwake. Na ametakasika Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wa walimwengu wote.
|
Ayah 27:9 الأية
يَا مُوسَىٰ إِنَّهُ أَنَا اللَّهُ الْعَزِيزُ الْحَكِيمُ
Ya moosa innahu ana AllahualAAazeezu alhakeem
Swahili
Ewe Musa! Hakika Mimi ndiye Mwenyezi Mungu, Mwenye nguvu, Mwenye hikima.
|
Ayah 27:10 الأية
وَأَلْقِ عَصَاكَ ۚ فَلَمَّا رَآهَا تَهْتَزُّ كَأَنَّهَا جَانٌّ وَلَّىٰ مُدْبِرًا
وَلَمْ يُعَقِّبْ ۚ يَا مُوسَىٰ لَا تَخَفْ إِنِّي لَا يَخَافُ لَدَيَّ
الْمُرْسَلُونَ
Waalqi AAasaka falamma raahatahtazzu kaannaha jannun walla mudbiranwalam
yuAAaqqib ya moosa la takhaf innee layakhafu ladayya almursaloon
Swahili
Na itupe fimbo yako! Alipo iona ikitikisika kama nyoka, aligeuka nyuma wala
hakungoja. Ewe Musa! Usikhofu! Hakika hawakhofu mbele yangu Mitume.
|
Ayah 27:11 الأية
إِلَّا مَن ظَلَمَ ثُمَّ بَدَّلَ حُسْنًا بَعْدَ سُوءٍ فَإِنِّي غَفُورٌ رَّحِيمٌ
Illa man thalama thummabaddala husnan baAAda soo-in fa-innee ghafoorun raheem
Swahili
Lakini aliye dhulumu, kisha akabadilisha wema baada ya ubaya, basi Mimi ni
Mwenye kusamehe Mwenye kurehemu.
|
Ayah 27:12 الأية
وَأَدْخِلْ يَدَكَ فِي جَيْبِكَ تَخْرُجْ بَيْضَاءَ مِنْ غَيْرِ سُوءٍ ۖ فِي تِسْعِ
آيَاتٍ إِلَىٰ فِرْعَوْنَ وَقَوْمِهِ ۚ إِنَّهُمْ كَانُوا قَوْمًا فَاسِقِينَ
Waadkhil yadaka fee jaybika takhruj baydaamin ghayri soo-in fee tisAAi ayatin
ilafirAAawna waqawmihi innahum kanoo qawman fasiqeen
Swahili
Na ingiza mkono wako katika mfuko wako, utatoka mweupe bila ya maradhi. Ni
katika Ishara tisa za kumpelekea Firauni na kaumu yake. Hakika hao walikuwa watu
waovu.
|
Ayah 27:13 الأية
فَلَمَّا جَاءَتْهُمْ آيَاتُنَا مُبْصِرَةً قَالُوا هَٰذَا سِحْرٌ مُّبِينٌ
Falamma jaat-hum ayatunamubsiratan qaloo hatha sihrun mubeen
Swahili
Basi zilipo wafikia Ishara zetu hizo zenye kuonyesha, wakasema: Huu ni uchawi
dhaahiri.
|
Ayah 27:14 الأية
وَجَحَدُوا بِهَا وَاسْتَيْقَنَتْهَا أَنفُسُهُمْ ظُلْمًا وَعُلُوًّا ۚ فَانظُرْ
كَيْفَ كَانَ عَاقِبَةُ الْمُفْسِدِينَ
Wajahadoo biha wastayqanat-haanfusuhum thulman waAAuluwwan fanthurkayfa kana
AAaqibatu almufsideen
Swahili
Na wakazikataa kwa dhulma na kujivuna, na hali ya kuwa nafsi zao zina yakini
nazo. Basi angalia ulikuwaje mwisho wa mafisadi!
|
Ayah 27:15 الأية
وَلَقَدْ آتَيْنَا دَاوُودَ وَسُلَيْمَانَ عِلْمًا ۖ وَقَالَا الْحَمْدُ لِلَّهِ
الَّذِي فَضَّلَنَا عَلَىٰ كَثِيرٍ مِّنْ عِبَادِهِ الْمُؤْمِنِينَ
Walaqad atayna dawoodawasulaymana AAilman waqala alhamdulillahi allathee
faddalana AAalakatheerin min AAibadihi almu/mineen
Swahili
Na hakika tuliwapa Daudi na Sulaiman ilimu, na wakasema: Alhamdu Lillahi,
Kuhimidiwa kote ni kwa Mwenyezi Mungu aliye tufadhilisha kuliko wengi katika
waja wake Waumini.
|
Ayah 27:16 الأية
وَوَرِثَ سُلَيْمَانُ دَاوُودَ ۖ وَقَالَ يَا أَيُّهَا النَّاسُ عُلِّمْنَا مَنطِقَ
الطَّيْرِ وَأُوتِينَا مِن كُلِّ شَيْءٍ ۖ إِنَّ هَٰذَا لَهُوَ الْفَضْلُ
الْمُبِينُ
Wawaritha sulaymanu dawoodawaqala ya ayyuha annasuAAullimna mantiqa attayri
waooteenamin kulli shay-in inna hatha lahuwa alfadlualmubeen
Swahili
Na Sulaiman alimrithi Daudi, na akasema: Enyi watu! Tumefunzwa usemi wa ndege,
na tumepewa kila kitu. Hakika hii ni fadhila iliyo dhaahiri.
|
Ayah 27:17 الأية
وَحُشِرَ لِسُلَيْمَانَ جُنُودُهُ مِنَ الْجِنِّ وَالْإِنسِ وَالطَّيْرِ فَهُمْ
يُوزَعُونَ
Wahushira lisulaymanajunooduhu mina aljinni wal-insi wattayrifahum yoozaAAoon
Swahili
Na alikusanyiwa Sulaiman majeshi yake ya majini, na watu, na ndege; nayo
yakapangwa kwa nidhamu.
|
Ayah 27:18 الأية
حَتَّىٰ إِذَا أَتَوْا عَلَىٰ وَادِ النَّمْلِ قَالَتْ نَمْلَةٌ يَا أَيُّهَا
النَّمْلُ ادْخُلُوا مَسَاكِنَكُمْ لَا يَحْطِمَنَّكُمْ سُلَيْمَانُ وَجُنُودُهُ
وَهُمْ لَا يَشْعُرُونَ
Hatta itha ataw AAalawadi annamli qalat namlatun ya ayyuhaannamlu odkhuloo
masakinakum la yahtimannakumsulaymanu wajunooduhu wahum la yashAAuroon
Swahili
Mpaka walipo fika kwenye bonde la wadudu chungu, alisema mdudu chungu mmoja:
Enyi wadudu chungu! Ingieni majumbani mwenu, asikupondeni Sulaiman na majeshi
yake bila ya wao kutambua.
|
Ayah 27:19 الأية
فَتَبَسَّمَ ضَاحِكًا مِّن قَوْلِهَا وَقَالَ رَبِّ أَوْزِعْنِي أَنْ أَشْكُرَ
نِعْمَتَكَ الَّتِي أَنْعَمْتَ عَلَيَّ وَعَلَىٰ وَالِدَيَّ وَأَنْ أَعْمَلَ
صَالِحًا تَرْضَاهُ وَأَدْخِلْنِي بِرَحْمَتِكَ فِي عِبَادِكَ الصَّالِحِينَ
Fatabassama dahikan min qawlihawaqala rabbi awziAAnee an ashkura niAAmataka
allateeanAAamta AAalayya waAAala walidayya waan aAAmala salihantardahu
waadkhilnee birahmatika fee AAibadikaassaliheen
Swahili
Basi (Sulaiman) akatabasamu akacheka kwa neno hili, na akasema: Ee Mola wangu
Mlezi! Nizindue niishukuru neema yako uliyo nineemesha mimi na wazazi wangu, na
nipate kutenda mema uyapendayo, na uniingize kwa rehema yako katika waja wako
wema.
|
Ayah 27:20 الأية
وَتَفَقَّدَ الطَّيْرَ فَقَالَ مَا لِيَ لَا أَرَى الْهُدْهُدَ أَمْ كَانَ مِنَ
الْغَائِبِينَ
Watafaqqada attayra faqalama liya la ara alhudhuda am kana minaalgha-ibeen
Swahili
Na akawakagua ndege, na akasema: Imekuwaje, mbona simwoni Hud-hud, au amekuwa
miongoni mwa walio ghibu?
|
Ayah 27:21 الأية
لَأُعَذِّبَنَّهُ عَذَابًا شَدِيدًا أَوْ لَأَذْبَحَنَّهُ أَوْ لَيَأْتِيَنِّي
بِسُلْطَانٍ مُّبِينٍ
LaoAAaththibannahu AAathabanshadeedan aw laathbahannahu aw laya/tiyannee
bisultaninmubeen
Swahili
Kwa yakini nitamuadhibu kwa adhabu kali, au nitamchinja, au aniletee hoja ya
kutosha.
|
Ayah 27:22 الأية
فَمَكَثَ غَيْرَ بَعِيدٍ فَقَالَ أَحَطتُ بِمَا لَمْ تُحِطْ بِهِ وَجِئْتُكَ مِن
سَبَإٍ بِنَبَإٍ يَقِينٍ
Famakatha ghayra baAAeedin faqala ahattubima lam tuhit bihi waji/tuka min
saba-inbinaba-in yaqeen
Swahili
Basi (Hud-hud) akakaa si mbali na akasema: Nimegundua usilo gundua wewe, na
ninakujia hivi kutoka nchi ya Sabai, na nakuletea khabari za yakini.
|
Ayah 27:23 الأية
إِنِّي وَجَدتُّ امْرَأَةً تَمْلِكُهُمْ وَأُوتِيَتْ مِن كُلِّ شَيْءٍ وَلَهَا
عَرْشٌ عَظِيمٌ
Innee wajadtu imraatan tamlikuhum waootiyatmin kulli shay-in walaha AAarshun
AAatheem
Swahili
Hakika mimi nimemkuta mwanamke anawatawala, naye amepewa kila kitu, na anacho
kiti cha enzi kikubwa.
|
Ayah 27:24 الأية
وَجَدتُّهَا وَقَوْمَهَا يَسْجُدُونَ لِلشَّمْسِ مِن دُونِ اللَّهِ وَزَيَّنَ
لَهُمُ الشَّيْطَانُ أَعْمَالَهُمْ فَصَدَّهُمْ عَنِ السَّبِيلِ فَهُمْ لَا
يَهْتَدُونَ
Wajadtuha waqawmaha yasjudoonalishshamsi min dooni Allahi wazayyana lahumu
ashshaytanuaAAmalahum fasaddahum AAani assabeeli fahumla yahtadoon
Swahili
Nimemkuta yeye na watu wake wanalisujudia jua badala ya Mwenyezi Mungu; na
Shet'ani amewapambia vitendo vyao na akawazuilia Njia. Kwa hivyo hawakuongoka,
|
Ayah 27:25 الأية
أَلَّا يَسْجُدُوا لِلَّهِ الَّذِي يُخْرِجُ الْخَبْءَ فِي السَّمَاوَاتِ
وَالْأَرْضِ وَيَعْلَمُ مَا تُخْفُونَ وَمَا تُعْلِنُونَ
Alla yasjudoo lillahi allatheeyukhriju alkhabaa fee assamawati
wal-ardiwayaAAlamu ma tukhfoona wama tuAAlinoon
Swahili
Na hawamsujudii Mwenyezi Mungu ambaye huyatoa yaliyo fichikana katika mbingu na
ardhi, na anayajua mnayo yaficha na mnayo yatangaza.
|
Ayah 27:26 الأية
اللَّهُ لَا إِلَٰهَ إِلَّا هُوَ رَبُّ الْعَرْشِ الْعَظِيمِ ۩
Allahu la ilaha illahuwa rabbu alAAarshi alAAatheem
Swahili
Mwenyezi Mungu - hapana mungu ila Yeye, Mola Mlezi wa A'rshi tukufu..
|
Ayah 27:27 الأية
قَالَ سَنَنظُرُ أَصَدَقْتَ أَمْ كُنتَ مِنَ الْكَاذِبِينَ
Qala sananthuru asadaqtaam kunta mina alkathibeen
Swahili
Akasema (Sulaiman): Tutatazama umesema kweli au wewe ni miongoni mwa waongo.
|
Ayah 27:28 الأية
اذْهَب بِّكِتَابِي هَٰذَا فَأَلْقِهْ إِلَيْهِمْ ثُمَّ تَوَلَّ عَنْهُمْ فَانظُرْ
مَاذَا يَرْجِعُونَ
Ithhab bikitabee hathafaalqih ilayhim thumma tawalla AAanhum fanthurmatha
yarjiAAoon
Swahili
Nenda na barua yangu hii na uwafikishie, kisha waache na utazame watarejesha
nini.
|
Ayah 27:29 الأية
قَالَتْ يَا أَيُّهَا الْمَلَأُ إِنِّي أُلْقِيَ إِلَيَّ كِتَابٌ كَرِيمٌ
Qalat ya ayyuha almalaoinnee olqiya ilayya kitabun kareem
Swahili
(Malkia) akasema: Enyi wahishimiwa! Hakika nimeletewa barua tukufu.
|
Ayah 27:30 الأية
إِنَّهُ مِن سُلَيْمَانَ وَإِنَّهُ بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ
Innahu min sulaymana wa-innahu bismiAllahi arrahmani arraheem
Swahili
Imetoka kwa Sulaiman nayo ni: Kwa jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa rehema,
Mwenye kurehemu.
|
Ayah 27:31 الأية
أَلَّا تَعْلُوا عَلَيَّ وَأْتُونِي مُسْلِمِينَ
Alla taAAloo AAalayya wa/tooneemuslimeen
Swahili
Msinifanyie jeuri, na fikeni kwangu nanyi mmekwisha kuwa wenye kusalimu amri.
|
Ayah 27:32 الأية
قَالَتْ يَا أَيُّهَا الْمَلَأُ أَفْتُونِي فِي أَمْرِي مَا كُنتُ قَاطِعَةً
أَمْرًا حَتَّىٰ تَشْهَدُونِ
Qalat ya ayyuha almalaoaftoonee fee amree ma kuntu qatiAAatan amran
hattatashhadoon
Swahili
Akasema: Enyi wahishimiwa! Nipeni shauri katika jambo langu hili, kwani mimi
sikati shauri yoyote mpaka mhudhurie.
|
Ayah 27:33 الأية
قَالُوا نَحْنُ أُولُو قُوَّةٍ وَأُولُو بَأْسٍ شَدِيدٍ وَالْأَمْرُ إِلَيْكِ
فَانظُرِي مَاذَا تَأْمُرِينَ
Qaloo nahnu oloo quwwatinwaoloo ba/sin shadeedin wal-amru ilayki fanthureematha
ta/mureen
Swahili
Wakasema: Sisi ni wenye nguvu na wakali kwa vita; na amri iko kwako, basi tazama
ni nini unaamrisha.
|
Ayah 27:34 الأية
قَالَتْ إِنَّ الْمُلُوكَ إِذَا دَخَلُوا قَرْيَةً أَفْسَدُوهَا وَجَعَلُوا
أَعِزَّةَ أَهْلِهَا أَذِلَّةً ۖ وَكَذَٰلِكَ يَفْعَلُونَ
Qalat inna almulooka ithadakhaloo qaryatan afsadooha wajaAAaloo aAAizzata
ahlihaathillatan wakathalika yafAAaloon
Swahili
Akasema: Hakika wafalme wanapo uingia mji wanauharibu, na wanawafanya wale
watukufu wake kuwa wanyonge. Na hivyo ndivyo watendavyo.
|
Ayah 27:35 الأية
وَإِنِّي مُرْسِلَةٌ إِلَيْهِم بِهَدِيَّةٍ فَنَاظِرَةٌ بِمَ يَرْجِعُ
الْمُرْسَلُونَ
Wa-innee mursilatun ilayhim bihadiyyatin fanathiratunbima yarjiAAu almursaloon
Swahili
Lakini mimi nitawapelekea zawadi, nami nitangoja watakayo rudi nayo wajumbe.
|
Ayah 27:36 الأية
فَلَمَّا جَاءَ سُلَيْمَانَ قَالَ أَتُمِدُّونَنِ بِمَالٍ فَمَا آتَانِيَ اللَّهُ
خَيْرٌ مِّمَّا آتَاكُم بَلْ أَنتُم بِهَدِيَّتِكُمْ تَفْرَحُونَ
Falamma jaa sulaymana qalaatumiddoonani bimalin fama ataniyaAllahu khayrun mimma
atakum bal antumbihadiyyatikum tafrahoon
Swahili
Basi alipo fika (mjumbe) kwa Sulaiman, alisema (Sulaiman): Hivyo ndio nyinyi
mnanisaidia kwa mali? Aliyo nipa Mwenyezi Mungu ni bora zaidi kuliko aliyo
kupeni nyinyi. Lakini nyinyi mnafurahia hii zawadi yenu.
|
Ayah 27:37 الأية
ارْجِعْ إِلَيْهِمْ فَلَنَأْتِيَنَّهُم بِجُنُودٍ لَّا قِبَلَ لَهُم بِهَا
وَلَنُخْرِجَنَّهُم مِّنْهَا أَذِلَّةً وَهُمْ صَاغِرُونَ
IrjiAA ilayhim falana/tiyannahum bijunoodinla qibala lahum biha
walanukhrijannahum minhaathillatan wahum saghiroon
Swahili
Rejea kwao! Kwa yakini sisi tutawajia kwa majeshi wasio yaweza kuyakabili. Na
hakika tutawatoa humo na hali wao wamekuwa madhalili na wanyonge.
|
Ayah 27:38 الأية
قَالَ يَا أَيُّهَا الْمَلَأُ أَيُّكُمْ يَأْتِينِي بِعَرْشِهَا قَبْلَ أَن
يَأْتُونِي مُسْلِمِينَ
Qala ya ayyuha almalaoayyukum ya/teenee biAAarshiha qabla an ya/toonee muslimeen
Swahili
Akasema: Enyi wahishimiwa! Ni nani kati yenu atakaye niletea kiti chake cha enzi
kabla hawajanijia nao wamekwisha salimu amri.
|
Ayah 27:39 الأية
قَالَ عِفْرِيتٌ مِّنَ الْجِنِّ أَنَا آتِيكَ بِهِ قَبْلَ أَن تَقُومَ مِن
مَّقَامِكَ ۖ وَإِنِّي عَلَيْهِ لَقَوِيٌّ أَمِينٌ
Qala AAifreetun mina aljinni anaateeka bihi qabla an taqooma min maqamika
wa-inneAAalayhi laqawiyyun ameen
Swahili
Akasema: Afriti, katika majini: Mimi nitakuletea kabla hujainuka pahala pako
hapo. Na mimi kwa hakika nina nguvu na muaminifu.
|
Ayah 27:40 الأية
قَالَ الَّذِي عِندَهُ عِلْمٌ مِّنَ الْكِتَابِ أَنَا آتِيكَ بِهِ قَبْلَ أَن
يَرْتَدَّ إِلَيْكَ طَرْفُكَ ۚ فَلَمَّا رَآهُ مُسْتَقِرًّا عِندَهُ قَالَ هَٰذَا
مِن فَضْلِ رَبِّي لِيَبْلُوَنِي أَأَشْكُرُ أَمْ أَكْفُرُ ۖ وَمَن شَكَرَ
فَإِنَّمَا يَشْكُرُ لِنَفْسِهِ ۖ وَمَن كَفَرَ فَإِنَّ رَبِّي غَنِيٌّ كَرِيمٌ
Qala allathee AAindahu AAilmunmina alkitabi ana ateeka bihi qabla anyartadda
ilayka tarfuka falamma raahumustaqirran AAindahu qala hatha min fadlirabbee
liyabluwanee aashkuru am akfuru waman shakara fa-innamayashkuru linafsihi waman
kafara fa-inna rabbee ghaniyyun kareem
Swahili
Akasema mwenye ilimu ya Kitabu: Mimi nitakuletea kabla ya kupepesa jicho lako.
Basi alipo kiona kimewekwa mbele yake, akasema: Haya ni katika fadhila zake Mola
wangu Mlezi, ili anijaribu nitashukuru au nitakufuru. Na mwenye kushukuru, kwa
hakika, anashukuru kwa manufaa ya nafsi yake; na anaye kufuru, kwa hakika Mola
wangu Mlezi ni Mkwasi na Karimu.
|
Ayah 27:41 الأية
قَالَ نَكِّرُوا لَهَا عَرْشَهَا نَنظُرْ أَتَهْتَدِي أَمْ تَكُونُ مِنَ الَّذِينَ
لَا يَهْتَدُونَ
Qala nakkiroo laha AAarshahananthur atahtadee am takoonu mina allatheenala
yahtadoon
Swahili
Akasema: Mgeuzieni kiti chake cha enzi hiki, tuone ataongoka, au atakuwa
miongoni mwa wasio ongoka.
|
Ayah 27:42 الأية
فَلَمَّا جَاءَتْ قِيلَ أَهَٰكَذَا عَرْشُكِ ۖ قَالَتْ كَأَنَّهُ هُوَ ۚ
وَأُوتِينَا الْعِلْمَ مِن قَبْلِهَا وَكُنَّا مُسْلِمِينَ
Falamma jaat qeela ahakathaAAarshuki qalat kaannahu huwa waooteena alAAilmamin
qabliha wakunna muslimeen
Swahili
Basi (Malkia) alipo fika akaambiwa: Je! Kiti chako cha enzi ni kama hiki?
Akasema: Kama kwamba ndicho hichi. (Sulaiman na watu wake wakasema): Na sisi
tumepewa ilimu kabla yake (Malkia), na tukawa Waislamu.
|
Ayah 27:43 الأية
وَصَدَّهَا مَا كَانَت تَّعْبُدُ مِن دُونِ اللَّهِ ۖ إِنَّهَا كَانَتْ مِن قَوْمٍ
كَافِرِينَ
Wasaddaha ma kanattaAAbudu min dooni Allahi innaha kanat minqawmin kafireen
Swahili
Na yale aliyo kuwa akiyaabudu badala ya Mwenyezi Mungu yalimzuilia. Hakika yeye
(Malkia) alikuwa katika kaumu ya makafiri.
|
Ayah 27:44 الأية
قِيلَ لَهَا ادْخُلِي الصَّرْحَ ۖ فَلَمَّا رَأَتْهُ حَسِبَتْهُ لُجَّةً وَكَشَفَتْ
عَن سَاقَيْهَا ۚ قَالَ إِنَّهُ صَرْحٌ مُّمَرَّدٌ مِّن قَوَارِيرَ ۗ قَالَتْ رَبِّ
إِنِّي ظَلَمْتُ نَفْسِي وَأَسْلَمْتُ مَعَ سُلَيْمَانَ لِلَّهِ رَبِّ
الْعَالَمِينَ
Qeela laha odkhulee assarhafalamma raat-hu hasibat-hu lujjatan wakashafat
AAansaqayha qala innahu sarhunmumarradun min qawareera qalat rabbi innee
thalamtunafsee waaslamtu maAAa sulaymana lillahi rabbi alAAalameen
Swahili
Akaambiwa: Liingie behewa la hili jumba. Alipo liona alidhani ni maji, na
akapandisha nguo mpaka kwenye miundi yake. (Sulaiman) akasema: Hakika hilo ni
behewa lilio sakafiwa kwa viyoo! Akasema (Malkia): Mola wangu Mlezi! Mimi
nimejidhulumu nafsi yangu, na sasa nanyenyekea pamoja na Sulaiman kwa Mwenyezi
Mungu, Mola Mlezi wa walimwengu wote.
|
Ayah 27:45 الأية
وَلَقَدْ أَرْسَلْنَا إِلَىٰ ثَمُودَ أَخَاهُمْ صَالِحًا أَنِ اعْبُدُوا اللَّهَ
فَإِذَا هُمْ فَرِيقَانِ يَخْتَصِمُونَ
Walaqad arsalna ila thamoodaakhahum salihan ani oAAbudoo Allahafa-itha hum
fareeqani yakhtasimoon
Swahili
Na kwa kina Thamud tulimtuma ndugu yao Saleh kuwaambia: Muabuduni Mwenyezi
Mungu. Basi wakawa makundi mawili yanayo gombana.
|
Ayah 27:46 الأية
قَالَ يَا قَوْمِ لِمَ تَسْتَعْجِلُونَ بِالسَّيِّئَةِ قَبْلَ الْحَسَنَةِ ۖ
لَوْلَا تَسْتَغْفِرُونَ اللَّهَ لَعَلَّكُمْ تُرْحَمُونَ
Qala ya qawmi limatastaAAjiloona bissayyi-ati qabla alhasanati
lawlatastaghfiroona Allaha laAAallakum turhamoon
Swahili
Akasema: Enyi watu wangu! Kwa nini mnauhimiza uwovu kabla ya wema? Kwa nini
hamuombi msamaha kwa Mwenyezi Mungu ili mrehemewe?
|
Ayah 27:47 الأية
قَالُوا اطَّيَّرْنَا بِكَ وَبِمَن مَّعَكَ ۚ قَالَ طَائِرُكُمْ عِندَ اللَّهِ ۖ
بَلْ أَنتُمْ قَوْمٌ تُفْتَنُونَ
Qaloo ittayyarna bikawabiman maAAaka qala ta-irukum AAinda Allahibal antum
qawmun tuftanoon
Swahili
Wakasema: Tuna kisirani nawe na wale walio pamoja nawe. Yeye akasema: Uaguzi wa
ukorofi wenu uko kwa Mwenyezi Mungu; lakini nyinyi ni watu mnao jaribiwa.
|
Ayah 27:48 الأية
وَكَانَ فِي الْمَدِينَةِ تِسْعَةُ رَهْطٍ يُفْسِدُونَ فِي الْأَرْضِ وَلَا
يُصْلِحُونَ
Wakana fee almadeenati tisAAatu rahtinyufsidoona fee al-ardi wala yuslihoon
Swahili
Na walikuwamo mjini watu tisa wakifanya ufisadi katika nchi wala hawafanyi la
maslaha.
|
Ayah 27:49 الأية
قَالُوا تَقَاسَمُوا بِاللَّهِ لَنُبَيِّتَنَّهُ وَأَهْلَهُ ثُمَّ لَنَقُولَنَّ
لِوَلِيِّهِ مَا شَهِدْنَا مَهْلِكَ أَهْلِهِ وَإِنَّا لَصَادِقُونَ
Qaloo taqasamoo billahilanubayyitannahu waahlahu thumma lanaqoolanna liwaliyyihi
mashahidna mahlika ahlihi wa-inna lasadiqoon
Swahili
Wakasema: Apishaneni kwa Mwenyezi Mungu tutamshambulia usiku yeye na ahali zake;
kisha tutamwambia mrithi wake: Sisi hatukuona maangamizo ya watu wake, na sisi
bila ya shaka tunasema kweli.
|
Ayah 27:50 الأية
وَمَكَرُوا مَكْرًا وَمَكَرْنَا مَكْرًا وَهُمْ لَا يَشْعُرُونَ
Wamakaroo makran wamakarna makranwahum la yashAAuroon
Swahili
Basi wakapanga mipango yao, na Sisi tukapanga mipango yetu, na wao hawatambui.
|
Ayah 27:51 الأية
فَانظُرْ كَيْفَ كَانَ عَاقِبَةُ مَكْرِهِمْ أَنَّا دَمَّرْنَاهُمْ وَقَوْمَهُمْ
أَجْمَعِينَ
Fanthur kayfa kanaAAaqibatu makrihim anna dammarnahumwaqawmahum ajmaAAeen
Swahili
Basi angalia ulivyo kuwa mwisho wa mipango yao, ya kwamba tuliwaangamiza wao
pamoja na watu wao wote.
|
Ayah 27:52 الأية
فَتِلْكَ بُيُوتُهُمْ خَاوِيَةً بِمَا ظَلَمُوا ۗ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَةً
لِّقَوْمٍ يَعْلَمُونَ
Fatilka buyootuhum khawiyatan bimathalamoo inna fee thalika laayatanliqawmin
yaAAlamoon
Swahili
Basi hizo nyumba zao ni tupu kwa sababu ya walivyo dhulumu. Hakika bila ya shaka
katika hayo ipo Ishara kwa watu wanao jua.
|
Ayah 27:53 الأية
وَأَنجَيْنَا الَّذِينَ آمَنُوا وَكَانُوا يَتَّقُونَ
Waanjayna allatheena amanoowakanoo yattaqoon
Swahili
Na tukawaokoa wale walio amini na walio kuwa wanamchamngu.
|
Ayah 27:54 الأية
وَلُوطًا إِذْ قَالَ لِقَوْمِهِ أَتَأْتُونَ الْفَاحِشَةَ وَأَنتُمْ تُبْصِرُونَ
Walootan ith qalaliqawmihi ata/toona alfahishata waantum tubsiroon
Swahili
Na Lut'i alipo waambia watu wake: Je! Mnafanya uchafu nanyi mnaona?
|
Ayah 27:55 الأية
أَئِنَّكُمْ لَتَأْتُونَ الرِّجَالَ شَهْوَةً مِّن دُونِ النِّسَاءِ ۚ بَلْ أَنتُمْ
قَوْمٌ تَجْهَلُونَ
A-innakum lata/toona arrijalashahwatan min dooni annisa-i bal antum
qawmuntajhaloon
Swahili
Hivyo nyinyi mnawaingilia wanaume kwa matamanio badala ya wanawake? Hakika
nyinyi ni watu mnao fanya ujinga kabisa!
|
Ayah 27:56 الأية
فَمَا كَانَ جَوَابَ قَوْمِهِ إِلَّا أَن قَالُوا أَخْرِجُوا آلَ لُوطٍ مِّن
قَرْيَتِكُمْ ۖ إِنَّهُمْ أُنَاسٌ يَتَطَهَّرُونَ
Fama kana jawabaqawmihi illa an qaloo akhrijoo ala lootinmin qaryatikum innahum
onasun yatatahharoon
Swahili
Basi haikuwa jawabu ya watu wake ila ni kusema: Wafukuzeni wafwasi wa Lut'i
katika mji wenu. Hao ni watu wanao jitia usafi.
|
Ayah 27:57 الأية
فَأَنجَيْنَاهُ وَأَهْلَهُ إِلَّا امْرَأَتَهُ قَدَّرْنَاهَا مِنَ الْغَابِرِينَ
Faanjaynahu waahlahu illaimraatahu qaddarnaha mina alghabireen
Swahili
Basi tukamwokoa yeye na ahali zake, isipo kuwa mkewe; tukamkadiria katika walio
baki nyuma.
|
Ayah 27:58 الأية
وَأَمْطَرْنَا عَلَيْهِم مَّطَرًا ۖ فَسَاءَ مَطَرُ الْمُنذَرِينَ
Waamtarna AAalayhim mataranfasaa mataru almunthareen
Swahili
Na tukawanyeshea mvua. Ni ovu kweli kweli hiyo mvua ya walio kwisha onywa.
|
Ayah 27:59 الأية
قُلِ الْحَمْدُ لِلَّهِ وَسَلَامٌ عَلَىٰ عِبَادِهِ الَّذِينَ اصْطَفَىٰ ۗ آللَّهُ
خَيْرٌ أَمَّا يُشْرِكُونَ
Quli alhamdu lillahi wasalamunAAala AAibadihi allatheena istafaallahu khayrun
amma yushrikoon
Swahili
Sema: Alhamdu Lillahi! Kuhimidiwa ni kwa Mwenyezi Mungu! Na amani ishuke juu ya
waja wake alio wateuwa. Je! Mwenyezi Mungu ni bora, au wale wanao washirikisha
naye?
|
Ayah 27:60 الأية
أَمَّنْ خَلَقَ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضَ وَأَنزَلَ لَكُم مِّنَ السَّمَاءِ مَاءً
فَأَنبَتْنَا بِهِ حَدَائِقَ ذَاتَ بَهْجَةٍ مَّا كَانَ لَكُمْ أَن تُنبِتُوا
شَجَرَهَا ۗ أَإِلَٰهٌ مَّعَ اللَّهِ ۚ بَلْ هُمْ قَوْمٌ يَعْدِلُونَ
Amman khalaqa assamawatiwal-arda waanzala lakum mina assama-imaan faanbatna bihi
hada-iqa thatabahjatin ma kana lakum an tunbitoo shajarahaa-ilahun maAAa Allahi
bal hum qawmun yaAAdiloon
Swahili
AU NANI yule aliye ziumba mbingu na ardhi, na akakuteremshieni maji kutoka
mbinguni, na kwa hayo tukaziotesha bustani zenye kupendeza? Nyinyi hamna uwezo
wa kuiotesha miti yake. Je! Yupo mungu pamoja na Mwenyezi Mungu? Bali hao ni
watu walio potoka.
|
Ayah 27:61 الأية
أَمَّن جَعَلَ الْأَرْضَ قَرَارًا وَجَعَلَ خِلَالَهَا أَنْهَارًا وَجَعَلَ لَهَا
رَوَاسِيَ وَجَعَلَ بَيْنَ الْبَحْرَيْنِ حَاجِزًا ۗ أَإِلَٰهٌ مَّعَ اللَّهِ ۚ
بَلْ أَكْثَرُهُمْ لَا يَعْلَمُونَ
Amman jaAAala al-arda qararanwajaAAala khilalaha anharan wajaAAala laharawasiya
wajaAAala bayna albahrayni hajizana-ilahun maAAa Allahi bal aktharuhum
layaAAlamoon
Swahili
Au nani yule aliye ifanya ardhi mahali pa kutua, na akajaalia ndani yake mito,
na akaweka milima? Na akaweka baina ya bahari mbili kiziwizi? Je! Yupo mungu
pamoja na Mwenyezi Mungu? Bali wengi wao hawajui.
|
Ayah 27:62 الأية
أَمَّن يُجِيبُ الْمُضْطَرَّ إِذَا دَعَاهُ وَيَكْشِفُ السُّوءَ وَيَجْعَلُكُمْ
خُلَفَاءَ الْأَرْضِ ۗ أَإِلَٰهٌ مَّعَ اللَّهِ ۚ قَلِيلًا مَّا تَذَكَّرُونَ
Amman yujeebu almudtarra ithadaAAahu wayakshifu assoo-a wayajAAalukum
khulafaaal-ardi a-ilahun maAAa Allahi qaleelan matathakkaroon
Swahili
Au nani yule anaye mjibu mwenye shida pale anapo mwomba, na akaiondoa dhiki, na
akakufanyeni warithi wa ardhi? Je! Yupo mungu pamoja na Mwenyezi Mungu? Ni
machache mnayo yazingatia.
|
Ayah 27:63 الأية
أَمَّن يَهْدِيكُمْ فِي ظُلُمَاتِ الْبَرِّ وَالْبَحْرِ وَمَن يُرْسِلُ الرِّيَاحَ
بُشْرًا بَيْنَ يَدَيْ رَحْمَتِهِ ۗ أَإِلَٰهٌ مَّعَ اللَّهِ ۚ تَعَالَى اللَّهُ
عَمَّا يُشْرِكُونَ
Amman yahdeekum fee thulumatialbarri walbahri waman yursilu arriyahabushran
bayna yaday rahmatihi a-ilahun maAAa AllahitaAAala Allahu AAamma yushrikoon
Swahili
Au nani yule anaye kuongoeni katika giza la bara na bahari, na akazipeleka pepo
kuleta bishara kabla ya rehema zake? Je! Yupo mungu pamoja na Mwenyezi Mungu?
Ametukuka Mwenyezi Mungu juu ya wanao washirikisha naye.
|
Ayah 27:64 الأية
أَمَّن يَبْدَأُ الْخَلْقَ ثُمَّ يُعِيدُهُ وَمَن يَرْزُقُكُم مِّنَ السَّمَاءِ
وَالْأَرْضِ ۗ أَإِلَٰهٌ مَّعَ اللَّهِ ۚ قُلْ هَاتُوا بُرْهَانَكُمْ إِن كُنتُمْ
صَادِقِينَ
Amman yabdao alkhalqa thumma yuAAeeduhuwaman yarzuqukum mina assama-i
wal-ardia-ilahun maAAa Allahi qul hatoo burhanakumin kuntum sadiqeen
Swahili
Au nani anaye uanzisha uumbaji, kisha akaurejesha? Na nani anaye kuruzukuni
kutoka mbinguni na kwenye ardhi? Je! Yupo mungu pamoja na Mwenyezi Mungu? Sema:
Leteni hoja zenu kama nyinyi ni wasema kweli.
|
Ayah 27:65 الأية
قُل لَّا يَعْلَمُ مَن فِي السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ الْغَيْبَ إِلَّا اللَّهُ ۚ
وَمَا يَشْعُرُونَ أَيَّانَ يُبْعَثُونَ
Qul la yaAAlamu man fee assamawatiwal-ardi alghayba illa Allahu wamayashAAuroona
ayyana yubAAathoon
Swahili
Sema: Hapana katika mbingu na ardhi ajuaye ya ghaibu isipo kuwa Mwenyezi Mungu.
Wala wao hawajui lini watafufuliwa.
|
Ayah 27:66 الأية
بَلِ ادَّارَكَ عِلْمُهُمْ فِي الْآخِرَةِ ۚ بَلْ هُمْ فِي شَكٍّ مِّنْهَا ۖ بَلْ
هُم مِّنْهَا عَمُونَ
Bali iddaraka AAilmuhum fee al-akhiratibal hum fee shakkin minha bal hum minha
AAamoon
Swahili
Kwani huo ujuzi wao umefikilia kuijua Akhera? Bali wao wamo katika shaka nayo
tu, bali wao ni vipofu nayo.
|
Ayah 27:67 الأية
وَقَالَ الَّذِينَ كَفَرُوا أَإِذَا كُنَّا تُرَابًا وَآبَاؤُنَا أَئِنَّا
لَمُخْرَجُونَ
Waqala allatheena kafaroo a-ithakunna turaban waabaona a-innalamukhrajoon
Swahili
Na wakasema walio kufuru: Tutapo kuwa mchanga, sisi na baba zetu, hivyo kweli
tutakuja tolewa?
|
Ayah 27:68 الأية
لَقَدْ وُعِدْنَا هَٰذَا نَحْنُ وَآبَاؤُنَا مِن قَبْلُ إِنْ هَٰذَا إِلَّا
أَسَاطِيرُ الْأَوَّلِينَ
Laqad wuAAidna hatha nahnuwaabaona min qablu in hatha illaasateeru al-awwaleen
Swahili
Haya haya tuliahidiwa sisi na baba zetu zamani. Hayakuwa haya ila ni hadithi za
uwongo za watu wa kale.
|
Ayah 27:69 الأية
قُلْ سِيرُوا فِي الْأَرْضِ فَانظُرُوا كَيْفَ كَانَ عَاقِبَةُ الْمُجْرِمِينَ
Qul seeroo fee al-ardi fanthurookayfa kana AAaqibatu almujrimeen
Swahili
Sema: Nendeni katika ardhi, na tazameni ulikuwaje mwisho wa wakosefu.
|
Ayah 27:70 الأية
وَلَا تَحْزَنْ عَلَيْهِمْ وَلَا تَكُن فِي ضَيْقٍ مِّمَّا يَمْكُرُونَ
Wala tahzan AAalayhim walatakun fee dayqin mimma yamkuroon
Swahili
Wala usiwahuzunukie wala usiwe katika dhiki kwa sababu ya hila zao wanazo
zifanya.
|
Ayah 27:71 الأية
وَيَقُولُونَ مَتَىٰ هَٰذَا الْوَعْدُ إِن كُنتُمْ صَادِقِينَ
Wayaqooloona mata hathaalwaAAdu in kuntum sadiqeen
Swahili
Na wanasema: Ahadi hii itatokea lini, ikiwa mnasema kweli?
|
Ayah 27:72 الأية
قُلْ عَسَىٰ أَن يَكُونَ رَدِفَ لَكُم بَعْضُ الَّذِي تَسْتَعْجِلُونَ
Qul AAasa an yakoona radifa lakumbaAAdu allathee tastaAAjiloon
Swahili
Sema: Asaa ni karibu kukufikieni sehemu ya yale mnayo yahimiza.
|
Ayah 27:73 الأية
وَإِنَّ رَبَّكَ لَذُو فَضْلٍ عَلَى النَّاسِ وَلَٰكِنَّ أَكْثَرَهُمْ لَا
يَشْكُرُونَ
Wa-inna rabbaka lathoo fadlinAAala annasi walakinna aktharahum layashkuroon
Swahili
Na hakika Mola wako Mlezi ni Mwenye fadhila kwa watu, lakini wengi wao
hawashukuru.
|
Ayah 27:74 الأية
وَإِنَّ رَبَّكَ لَيَعْلَمُ مَا تُكِنُّ صُدُورُهُمْ وَمَا يُعْلِنُونَ
Wa-inna rabbaka layaAAlamu ma tukinnusudooruhum wama yuAAlinoon
Swahili
Na hakika Mola wako Mlezi anayajua yanayo ficha vifua vyao na wanayo yatangaza.
|
Ayah 27:75 الأية
وَمَا مِنْ غَائِبَةٍ فِي السَّمَاءِ وَالْأَرْضِ إِلَّا فِي كِتَابٍ مُّبِينٍ
Wama min gha-ibatin fee assama-iwal-ardi illa fee kitabin mubeen
Swahili
Na hakuna siri katika mbingu na ardhi ila imo katika Kitabu kinacho bainisha.
|
Ayah 27:76 الأية
إِنَّ هَٰذَا الْقُرْآنَ يَقُصُّ عَلَىٰ بَنِي إِسْرَائِيلَ أَكْثَرَ الَّذِي هُمْ
فِيهِ يَخْتَلِفُونَ
Inna hatha alqur-ana yaqussuAAala banee isra-eela akthara allathee humfeehi
yakhtalifoon
Swahili
Hakika Qur'ani hii inawasimulia Wana wa Israili mengi wanayo khitalifiana nayo.
|
Ayah 27:77 الأية
وَإِنَّهُ لَهُدًى وَرَحْمَةٌ لِّلْمُؤْمِنِينَ
Wa-innahu lahudan warahmatunlilmu/mineen
Swahili
Nayo hakika ni Uwongofu na Rehema kwa Waumini.
|
Ayah 27:78 الأية
إِنَّ رَبَّكَ يَقْضِي بَيْنَهُم بِحُكْمِهِ ۚ وَهُوَ الْعَزِيزُ الْعَلِيمُ
Inna rabbaka yaqdee baynahum bihukmihiwahuwa alAAazeezu alAAaleem
Swahili
Hakika Mola wako Mlezi atawahukumu kwa hukumu yake, naye ni Mwenye nguvu Mjuzi.
|
Ayah 27:79 الأية
فَتَوَكَّلْ عَلَى اللَّهِ ۖ إِنَّكَ عَلَى الْحَقِّ الْمُبِينِ
Fatawakkal AAala Allahi innakaAAala alhaqqi almubeen
Swahili
Basi mtegemee Mweneyezi Mungu; hakika wewe uko juu ya Haki iliyo wazi.
|
Ayah 27:80 الأية
إِنَّكَ لَا تُسْمِعُ الْمَوْتَىٰ وَلَا تُسْمِعُ الصُّمَّ الدُّعَاءَ إِذَا
وَلَّوْا مُدْبِرِينَ
Innaka la tusmiAAu almawta walatusmiAAu assumma adduAAaa ithawallaw mudbireen
Swahili
Kwa hakika wewe huwezi kuwafanya maiti wasikie, wala kuwafanya viziwi wasikie
wito, wanapo kwisha geuka kwenda zao.
|
Ayah 27:81 الأية
وَمَا أَنتَ بِهَادِي الْعُمْيِ عَن ضَلَالَتِهِمْ ۖ إِن تُسْمِعُ إِلَّا مَن
يُؤْمِنُ بِآيَاتِنَا فَهُم مُّسْلِمُونَ
Wama anta bihadee alAAumyiAAan dalalatihim in tusmiAAu illa manyu/minu
bi-ayatina fahum muslimoon
Swahili
Wala huwezi kuwaongoa vipofu waache upotovu wao. Huwezi kuwafanya wasikie isipo
kuwa wenye kuziamini Ishara zetu; na hao ndio wat'iifu.
|
Ayah 27:82 الأية
وَإِذَا وَقَعَ الْقَوْلُ عَلَيْهِمْ أَخْرَجْنَا لَهُمْ دَابَّةً مِّنَ الْأَرْضِ
تُكَلِّمُهُمْ أَنَّ النَّاسَ كَانُوا بِآيَاتِنَا لَا يُوقِنُونَ
Wa-itha waqaAAa alqawlu AAalayhimakhrajna lahum dabbatan mina
al-arditukallimuhum anna annasa kanoo bi-ayatinala yooqinoon
Swahili
Na itapo waangukia kauli juu yao, tutawatolea mnyama katika ardhi atakaye
wasemeza, ya kuwa watu walikuwa hawana na yakini na Ishara zetu.
|
Ayah 27:83 الأية
وَيَوْمَ نَحْشُرُ مِن كُلِّ أُمَّةٍ فَوْجًا مِّمَّن يُكَذِّبُ بِآيَاتِنَا فَهُمْ
يُوزَعُونَ
Wayawma nahshuru min kulli ommatinfawjan mimman yukaththibu bi-ayatinafahum
yoozaAAoon
Swahili
Na Siku tutapo kusanya kutoka kila umma kundi katika wanao kadhibisha Ishara
zetu, nao watagawanywa mafungu mafungu.
|
Ayah 27:84 الأية
حَتَّىٰ إِذَا جَاءُوا قَالَ أَكَذَّبْتُم بِآيَاتِي وَلَمْ تُحِيطُوا بِهَا
عِلْمًا أَمَّاذَا كُنتُمْ تَعْمَلُونَ
Hatta itha jaooqala akaththabtum bi-ayatee walam tuheetoobiha AAilman ammatha
kuntum taAAmaloon
Swahili
Hata watakapo fika, atasema (Mwenyezi Mungu): Je! Nyinyi si mlizikanusha Ishara
zangu pasipo kuzijua vyema? Au mlikuwa mkifanya nini?
|
Ayah 27:85 الأية
وَوَقَعَ الْقَوْلُ عَلَيْهِم بِمَا ظَلَمُوا فَهُمْ لَا يَنطِقُونَ
WawaqaAAa alqawlu AAalayhim bima thalamoofahum la yantiqoon
Swahili
Na kauli itawaangukia juu yao kwa vile walivyo dhulumu. Basi hao hawatasema
lolote.
|
Ayah 27:86 الأية
أَلَمْ يَرَوْا أَنَّا جَعَلْنَا اللَّيْلَ لِيَسْكُنُوا فِيهِ وَالنَّهَارَ
مُبْصِرًا ۚ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَاتٍ لِّقَوْمٍ يُؤْمِنُونَ
Alam yaraw anna jaAAalnaallayla liyaskunoo feehi wannahara mubsiraninna fee
thalika laayatin liqawmin yu/minoon
Swahili
Je! Hawaoni kwamba sisi tumeufanya usiku ili watulie, na mchana wa kuangaza.
Hakika katika hayo zipo Ishara kwa watu wanao amini.
|
Ayah 27:87 الأية
وَيَوْمَ يُنفَخُ فِي الصُّورِ فَفَزِعَ مَن فِي السَّمَاوَاتِ وَمَن فِي الْأَرْضِ
إِلَّا مَن شَاءَ اللَّهُ ۚ وَكُلٌّ أَتَوْهُ دَاخِرِينَ
Wayawma yunfakhu fee assoorifafaziAAa man fee assamawati waman feeal-ardi illa
man shaa Allahu wakullunatawhu dakhireen
Swahili
Na Siku litapo pulizwa baragumu, watahangaika waliomo mbinguni na katika ardhi,
ila amtakaye Mwenyezi Mungu. Na wote watamfikia nao ni wanyonge.
|
Ayah 27:88 الأية
وَتَرَى الْجِبَالَ تَحْسَبُهَا جَامِدَةً وَهِيَ تَمُرُّ مَرَّ السَّحَابِ ۚ
صُنْعَ اللَّهِ الَّذِي أَتْقَنَ كُلَّ شَيْءٍ ۚ إِنَّهُ خَبِيرٌ بِمَا تَفْعَلُونَ
Watara aljibala tahsabuhajamidatan wahiya tamurru marra assahabi sunAAaAllahi
allathee atqana kulla shay-in innahukhabeerun bima tafAAaloon
Swahili
Na unaiona milima unaidhunia imetulia; nayo inakwenda kama mwendo wa mawingu.
Huo ndio ufundi wa Mwenyezi Mungu aliye tengeneza vilivyo kila kitu. Hakika Yeye
anazo khabari za yote myatendayo.
|
Ayah 27:89 الأية
مَن جَاءَ بِالْحَسَنَةِ فَلَهُ خَيْرٌ مِّنْهَا وَهُم مِّن فَزَعٍ يَوْمَئِذٍ
آمِنُونَ
Man jaa bilhasanatifalahu khayrun minha wahum min fazaAAin yawma-ithinaminoon
Swahili
Watakao kuja na mema, watapata bora kuliko hayo. Nao watasalimika na mahangaiko
ya Siku hiyo.
|
Ayah 27:90 الأية
وَمَن جَاءَ بِالسَّيِّئَةِ فَكُبَّتْ وُجُوهُهُمْ فِي النَّارِ هَلْ تُجْزَوْنَ
إِلَّا مَا كُنتُمْ تَعْمَلُونَ
Waman jaa bissayyi-atifakubbat wujoohuhum fee annari hal tujzawna illama kuntum
taAAmaloon
Swahili
Na watakao kuja na uovu, basi zitasunukishwa nyuso zao Motoni. Je! Kwani
mnalipwa isipo kuwa mliyo kuwa mkiyatenda?
|
Ayah 27:91 الأية
إِنَّمَا أُمِرْتُ أَنْ أَعْبُدَ رَبَّ هَٰذِهِ الْبَلْدَةِ الَّذِي حَرَّمَهَا
وَلَهُ كُلُّ شَيْءٍ ۖ وَأُمِرْتُ أَنْ أَكُونَ مِنَ الْمُسْلِمِينَ
Innama omirtu an aAAbuda rabba hathihialbaldati allathee harramaha walahu
kullushay-in waomirtu an akoona mina almuslimeen
Swahili
Ama mimi nimeamrishwa nimuabudu Mola Mlezi wa mji huu aliye ufanya ni mtakatifu;
na ni vyake Yeye tu vitu vyote. Na nimeamrishwa niwe miongoni mwa Waislamu,
wenye kunyenyekea.
|
Ayah 27:92 الأية
وَأَنْ أَتْلُوَ الْقُرْآنَ ۖ فَمَنِ اهْتَدَىٰ فَإِنَّمَا يَهْتَدِي لِنَفْسِهِ ۖ
وَمَن ضَلَّ فَقُلْ إِنَّمَا أَنَا مِنَ الْمُنذِرِينَ
Waan atluwa alqur-ana famani ihtadafa-innama yahtadee linafsihi waman dalla
faqulinnama ana mina almunthireen
Swahili
Na niisome Qur'ani. Na mwenye kuongoka, basi ameongoka kwa faida ya nafsi yake;
na aliye potea - basi sema: Hakika mimi ni miongoni mwa waonyaji.
|
Ayah 27:93 الأية
وَقُلِ الْحَمْدُ لِلَّهِ سَيُرِيكُمْ آيَاتِهِ فَتَعْرِفُونَهَا ۚ وَمَا رَبُّكَ
بِغَافِلٍ عَمَّا تَعْمَلُونَ
Waquli alhamdu lillahisayureekum ayatihi fataAArifoonaha wamarabbuka bighafilin
AAamma taAAmaloon
Swahili
Na sema: Alhamdu Lillahi, Sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu. Yeye
atakuonyesheni Ishara zake, na mtazijua. Na Mola wako Mlezi si mwenye
kughafilika na myatendayo.
|
©
EsinIslam.Com Designed & produced by The Awqaf London. Please pray for us
|