First Ayah 1 الأية الأوليبِسْم ِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ
حم
Ha-meem
Swahili
H'A MIM
|
Ayah 46:2 الأية
تَنزِيلُ الْكِتَابِ مِنَ اللَّهِ الْعَزِيزِ الْحَكِيمِ
Tanzeelu alkitabi mina AllahialAAazeezi alhakeem
Swahili
Uteremsho wa Kitabu umetoka kwa Mwenyezi Mungu, Mwenye nguvu, Mwenye hikima.
|
Ayah 46:3 الأية
مَا خَلَقْنَا السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضَ وَمَا بَيْنَهُمَا إِلَّا بِالْحَقِّ
وَأَجَلٍ مُّسَمًّى ۚ وَالَّذِينَ كَفَرُوا عَمَّا أُنذِرُوا مُعْرِضُونَ
Ma khalaqna assamawatiwal-arda wama baynahuma illabilhaqqi waajalin musamman
wallatheenakafaroo AAamma onthiroo muAAridoon
Swahili
Hatukuziumba mbingu na ardhi wala yaliyomo baina yake ila kwa haki na kwa muda
maalumu. Na walio kufuru wanayapuuza yale wanayo onywa.
|
Ayah 46:4 الأية
قُلْ أَرَأَيْتُم مَّا تَدْعُونَ مِن دُونِ اللَّهِ أَرُونِي مَاذَا خَلَقُوا مِنَ
الْأَرْضِ أَمْ لَهُمْ شِرْكٌ فِي السَّمَاوَاتِ ۖ ائْتُونِي بِكِتَابٍ مِّن قَبْلِ
هَٰذَا أَوْ أَثَارَةٍ مِّنْ عِلْمٍ إِن كُنتُمْ صَادِقِينَ
Qul araaytum ma tadAAoona min dooniAllahi aroonee matha khalaqoo mina al-ardiam
lahum shirkun fee assamawati eetooneebikitabin min qabli hatha aw atharatin
minAAilmin in kuntum sadiqeen
Swahili
Je! Mwawaona wale mnao waomba badala ya Mwenyezi Mungu? Nionyesheni wameumba
nini katika ardhi; au hao wanayo shirika katika mbingu? Nileteeni Kitabu kilicho
kuwa kabla ya hiki, au alama yoyote ya ilimu, ikiwa mnasema kweli.
|
Ayah 46:5 الأية
وَمَنْ أَضَلُّ مِمَّن يَدْعُو مِن دُونِ اللَّهِ مَن لَّا يَسْتَجِيبُ لَهُ إِلَىٰ
يَوْمِ الْقِيَامَةِ وَهُمْ عَن دُعَائِهِمْ غَافِلُونَ
Waman adallu mimman yadAAoo min dooniAllahi man la yastajeebu lahu ila
yawmialqiyamati wahum AAan duAAa-ihim ghafiloon
Swahili
Na nani mpotofu mkubwa kuliko hao wanao waomba, badala ya Mwenyezi Mungu, ambao
hawatawaitikia mpaka Siku ya Kiyama, na wala hawatambui maombi yao.
|
Ayah 46:6 الأية
وَإِذَا حُشِرَ النَّاسُ كَانُوا لَهُمْ أَعْدَاءً وَكَانُوا بِعِبَادَتِهِمْ
كَافِرِينَ
Wa-itha hushira annasukanoo lahum aAAdaan wakanoo biAAibadatihimkafireen
Swahili
Na ambao watu watakapo kusanywa watakuwa maadui zao, na wataikataa ibada yao.
|
Ayah 46:7 الأية
وَإِذَا تُتْلَىٰ عَلَيْهِمْ آيَاتُنَا بَيِّنَاتٍ قَالَ الَّذِينَ كَفَرُوا
لِلْحَقِّ لَمَّا جَاءَهُمْ هَٰذَا سِحْرٌ مُّبِينٌ
Wa-itha tutla AAalayhim ayatunabayyinatin qala allatheena kafaroo lilhaqqilamma
jaahum hatha sihrun mubeen
Swahili
Na wanapo somewa Aya zetu zilizo wazi, walio kufuru husema juu ya haki inapo
wajia: Huu ni uchawi dhaahiri.
|
Ayah 46:8 الأية
أَمْ يَقُولُونَ افْتَرَاهُ ۖ قُلْ إِنِ افْتَرَيْتُهُ فَلَا تَمْلِكُونَ لِي مِنَ
اللَّهِ شَيْئًا ۖ هُوَ أَعْلَمُ بِمَا تُفِيضُونَ فِيهِ ۖ كَفَىٰ بِهِ شَهِيدًا
بَيْنِي وَبَيْنَكُمْ ۖ وَهُوَ الْغَفُورُ الرَّحِيمُ
Am yaqooloona iftarahu qul iniiftaraytuhu fala tamlikoona lee mina Allahi
shay-anhuwa aAAlamu bima tufeedoona feehi kafa bihishaheedan baynee wabaynakum
wahuwa alghafooru arraheem
Swahili
Au wanasema: Ameizua mwenyewe! Sema: Ikiwa nimeizua mimi, basi nyinyi hamwezi
kunifaa chochote mbele ya Mwenyezi Mungu. Yeye anajua zaidi hayo mnayo ropokwa;
anatosha kuwa shahidi baina yangu na nyinyi. Na Yeye ndiye Mwenye kusamehe,
Mwenye kurehemu.
|
Ayah 46:9 الأية
قُلْ مَا كُنتُ بِدْعًا مِّنَ الرُّسُلِ وَمَا أَدْرِي مَا يُفْعَلُ بِي وَلَا
بِكُمْ ۖ إِنْ أَتَّبِعُ إِلَّا مَا يُوحَىٰ إِلَيَّ وَمَا أَنَا إِلَّا نَذِيرٌ
مُّبِينٌ
Qul ma kuntu bidAAan mina arrusuliwama adree ma yufAAalu bee wala bikum
inattabiAAu illa ma yooha ilayya wamaana illa natheerun mubeen
Swahili
Sema: Mimi si kiroja miongoni mwa Mitume. Wala sijui nitakavyo fanywa wala
nyinyi. Mimi nafuata niliyo funuliwa tu kwa Wahyi, wala mimi si chochote ila ni
mwonyaji mwenye kudhihirisha wazi.
|
Ayah 46:10 الأية
قُلْ أَرَأَيْتُمْ إِن كَانَ مِنْ عِندِ اللَّهِ وَكَفَرْتُم بِهِ وَشَهِدَ شَاهِدٌ
مِّن بَنِي إِسْرَائِيلَ عَلَىٰ مِثْلِهِ فَآمَنَ وَاسْتَكْبَرْتُمْ ۖ إِنَّ
اللَّهَ لَا يَهْدِي الْقَوْمَ الظَّالِمِينَ
Qul araaytum in kana min AAindi Allahiwakafartum bihi washahida shahidun min
banee isra-eelaAAala mithlihi faamana wastakbartum innaAllaha la yahdee alqawma
aththalimeen
Swahili
Sema: Mwaonaje yakiwa haya ni kweli yametoka kwa Mwenyezi Mungu, nanyi
mmeyakataa, na akashuhudia shahidi miongoni mwa Wana wa Israili juu ya mfano wa
haya, na akaamini, na nyinyi mnafanya kiburi? Hakika Mwenyezi Mungu hawaongoi
watu wenye kudhulumu.
|
Ayah 46:11 الأية
وَقَالَ الَّذِينَ كَفَرُوا لِلَّذِينَ آمَنُوا لَوْ كَانَ خَيْرًا مَّا سَبَقُونَا
إِلَيْهِ ۚ وَإِذْ لَمْ يَهْتَدُوا بِهِ فَسَيَقُولُونَ هَٰذَا إِفْكٌ قَدِيمٌ
Waqala allatheena kafaroolillatheena amanoo law kana khayran masabaqoona ilayhi
wa-ith lam yahtadoo bihifasayaqooloona hatha ifkun qadeem
Swahili
Na walio kufuru waliwaambia walio amini: Lau kuwa hii ni kheri, wasingeli
tutangulia. Na walipo kosa kuongoka wakasema: Huu ni uzushi wa zamani.
|
Ayah 46:12 الأية
وَمِن قَبْلِهِ كِتَابُ مُوسَىٰ إِمَامًا وَرَحْمَةً ۚ وَهَٰذَا كِتَابٌ مُّصَدِّقٌ
لِّسَانًا عَرَبِيًّا لِّيُنذِرَ الَّذِينَ ظَلَمُوا وَبُشْرَىٰ لِلْمُحْسِنِينَ
Wamin qablihi kitabu moosa imamanwarahmatan wahatha kitabun musaddiqunlisanan
AAarabiyyan liyunthira allatheena thalamoowabushra lilmuhsineen
Swahili
Na kabla yake kilikuwapo Kitabu cha Musa, kuwa chenye uwongozi na rehema. Na
hichi ni Kitabu cha kusadikisha na kilicho kuja kwa lugha ya Kiarabu, ili
kiwaonye walio dhulumu, na kiwe ni bishara kwa watendao mema.
|
Ayah 46:13 الأية
إِنَّ الَّذِينَ قَالُوا رَبُّنَا اللَّهُ ثُمَّ اسْتَقَامُوا فَلَا خَوْفٌ
عَلَيْهِمْ وَلَا هُمْ يَحْزَنُونَ
Inna allatheena qaloo rabbunaAllahu thumma istaqamoo fala khawfunAAalayhim wala
hum yahzanoon
Swahili
Hakika walio sema: Mola wetu Mlezi ni Mwenyezi Mungu; kisha wakatengenea,
hawatakuwa na khofu, wala hawatahuzunika.
|
Ayah 46:14 الأية
أُولَٰئِكَ أَصْحَابُ الْجَنَّةِ خَالِدِينَ فِيهَا جَزَاءً بِمَا كَانُوا
يَعْمَلُونَ
Ola-ika as-habualjannati khalideena feeha jazaan bimakanoo yaAAmaloon
Swahili
Hao ndio watu wa Peponi, watadumu humo, kuwa ni malipo kwa waliyo kuwa
wakiyatenda.
|
Ayah 46:15 الأية
وَوَصَّيْنَا الْإِنسَانَ بِوَالِدَيْهِ إِحْسَانًا ۖ حَمَلَتْهُ أُمُّهُ كُرْهًا
وَوَضَعَتْهُ كُرْهًا ۖ وَحَمْلُهُ وَفِصَالُهُ ثَلَاثُونَ شَهْرًا ۚ حَتَّىٰ إِذَا
بَلَغَ أَشُدَّهُ وَبَلَغَ أَرْبَعِينَ سَنَةً قَالَ رَبِّ أَوْزِعْنِي أَنْ
أَشْكُرَ نِعْمَتَكَ الَّتِي أَنْعَمْتَ عَلَيَّ وَعَلَىٰ وَالِدَيَّ وَأَنْ
أَعْمَلَ صَالِحًا تَرْضَاهُ وَأَصْلِحْ لِي فِي ذُرِّيَّتِي ۖ إِنِّي تُبْتُ
إِلَيْكَ وَإِنِّي مِنَ الْمُسْلِمِينَ
Wawassayna al-insanabiwalidayhi ihsanan hamalat-hu ommuhukurhan wawadaAAat-hu
kurhan wahamluhu wafisaluhuthalathoona shahran hatta ithabalagha ashuddahu
wabalagha arbaAAeena sanatan qala rabbiawziAAnee an ashkura niAAmataka allatee
anAAamta AAalayya waAAalawalidayya waan aAAmala salihan tardahuwaaslih lee fee
thurriyyatee innee tubtuilayka wa-innee mina almuslimeen
Swahili
Na tumemuusia mwanaadamu awatendee wema wazazi wake wawili. Mama yake amechukua
mimba yake kwa taabu, na akamzaa kwa taabu. Na kuchukua mimba kwake hata
kumwachisha ziwa ni miezi thalathini. Hata anapo fika utu uzima wake, na
akafikilia miaka arubaini, husema: Mola wangu Mlezi! Niwezeshe nishukuru neema
zako ulizo nineemesha mimi na wazazi wangu, na nitende mema unayo yapenda. Na
unitengenezee dhuriya zangu. Hakika mimi nimetubu kwako, na mimi ni miongoni mwa
Waislamu.
|
Ayah 46:16 الأية
أُولَٰئِكَ الَّذِينَ نَتَقَبَّلُ عَنْهُمْ أَحْسَنَ مَا عَمِلُوا وَنَتَجَاوَزُ
عَن سَيِّئَاتِهِمْ فِي أَصْحَابِ الْجَنَّةِ ۖ وَعْدَ الصِّدْقِ الَّذِي كَانُوا
يُوعَدُونَ
Ola-ika allatheena nataqabbaluAAanhum ahsana ma AAamiloo wanatajawazu
AAansayyi-atihim fee as-habi aljannati waAAda assidqiallathee kanoo yooAAadoon
Swahili
Hao ndio tunao wapokelea bora ya vitendo vyao walivyo vitenda, na tunayasamehe
makosa yao. Watakuwa miongoni mwa watu wa Peponi. Miadi ya kweli hiyo walio
ahidiwa.
|
Ayah 46:17 الأية
وَالَّذِي قَالَ لِوَالِدَيْهِ أُفٍّ لَّكُمَا أَتَعِدَانِنِي أَنْ أُخْرَجَ وَقَدْ
خَلَتِ الْقُرُونُ مِن قَبْلِي وَهُمَا يَسْتَغِيثَانِ اللَّهَ وَيْلَكَ آمِنْ
إِنَّ وَعْدَ اللَّهِ حَقٌّ فَيَقُولُ مَا هَٰذَا إِلَّا أَسَاطِيرُ الْأَوَّلِينَ
Wallathee qala liwalidayhioffin lakuma ataAAidaninee an okhraja waqad
khalatialquroonu min qablee wahuma yastagheethani Allahawaylaka amin inna waAAda
Allahi haqqunfayaqoolu ma hatha illa asateerual-awwaleen
Swahili
Na ambaye amewafyonya wazazi wake na akawaambia: Ati ndio mnanitisha kuwa
nitafufuliwa, na hali vizazi vingi vimekwisha pita kabla yangu! Na hao wazazi
humwomba msaada Mwenyezi Mungu (na humwambia mtoto wao): Ole wako! Amini! Hakika
ahadi ya Mwenyezi Mungu ni kweli. Na yeye husema: Hayakuwa haya ila ni visa vya
watu wa kale.
|
Ayah 46:18 الأية
أُولَٰئِكَ الَّذِينَ حَقَّ عَلَيْهِمُ الْقَوْلُ فِي أُمَمٍ قَدْ خَلَتْ مِن
قَبْلِهِم مِّنَ الْجِنِّ وَالْإِنسِ ۖ إِنَّهُمْ كَانُوا خَاسِرِينَ
Ola-ika allatheena haqqaAAalayhimu alqawlu fee umamin qad khalat min qablihim
minaaljinni wal-insi innahum kanoo khasireen
Swahili
Hao ndio ambao imehakikikishwa hukumu juu yao kama mataifa yaliyo kwisha pita
kabla yao miongoni mwa majini na watu. Hakika hao wamekuwa wenye kukhasiri.
|
Ayah 46:19 الأية
وَلِكُلٍّ دَرَجَاتٌ مِّمَّا عَمِلُوا ۖ وَلِيُوَفِّيَهُمْ أَعْمَالَهُمْ وَهُمْ
لَا يُظْلَمُونَ
Walikullin darajatun mimmaAAamiloo waliyuwaffiyahum aAAmalahum wahum la
yuthlamoon
Swahili
Na wote watakuwa na daraja zao mbali mbali kwa waliyo yatenda, na ili awalipe
kwa vitendo vyao, na wala hawatadhulumiwa.
|
Ayah 46:20 الأية
وَيَوْمَ يُعْرَضُ الَّذِينَ كَفَرُوا عَلَى النَّارِ أَذْهَبْتُمْ طَيِّبَاتِكُمْ
فِي حَيَاتِكُمُ الدُّنْيَا وَاسْتَمْتَعْتُم بِهَا فَالْيَوْمَ تُجْزَوْنَ عَذَابَ
الْهُونِ بِمَا كُنتُمْ تَسْتَكْبِرُونَ فِي الْأَرْضِ بِغَيْرِ الْحَقِّ وَبِمَا
كُنتُمْ تَفْسُقُونَ
Wayawma yuAAradu allatheenakafaroo AAala annari athhabtum tayyibatikumfee
hayatikumu addunya wastamtaAAtumbiha falyawma tujzawna AAathaba alhooni
bimakuntum tastakbiroona fee al-ardi bighayri alhaqqiwabima kuntum tafsuqoon
Swahili
Na siku watakapo letwa walio kufuru kwenye Moto wataambiwa: Nyinyi mlitwaa vitu
vyenu vizuri katika uhai wa duniani, na mkastareheshwa navyo. Basi leo ndio
mnalipwa adhabu ya fedheha kwa mlivyo kuwa mkitakabari katika ardhi bila ya
haki, na kwa sababu mlikuwa mkifanya upotovu.
|
Ayah 46:21 الأية
وَاذْكُرْ أَخَا عَادٍ إِذْ أَنذَرَ قَوْمَهُ بِالْأَحْقَافِ وَقَدْ خَلَتِ
النُّذُرُ مِن بَيْنِ يَدَيْهِ وَمِنْ خَلْفِهِ أَلَّا تَعْبُدُوا إِلَّا اللَّهَ
إِنِّي أَخَافُ عَلَيْكُمْ عَذَابَ يَوْمٍ عَظِيمٍ
Wathkur akha AAadinith anthara qawmahu bil-ahqafiwaqad khalati annuthuru min
bayni yadayhi waminkhalfihi alla taAAbudoo illa Allaha inneeakhafu AAalaykum
AAathaba yawmin AAatheem
Swahili
Na mtaje ndugu wa kina A'di, alipo waonya watu wake kwenye vilima vya mchanga.
Na kwa yakini waonyaji wengi walitokea kabla yake na baada yake kuwaambia:
Msimuabudu isipo kuwa Mwenyezi Mungu. Hakika mimi nakukhofieni isikupateni
adhabu ya siku iliyo kuu.
|
Ayah 46:22 الأية
قَالُوا أَجِئْتَنَا لِتَأْفِكَنَا عَنْ آلِهَتِنَا فَأْتِنَا بِمَا تَعِدُنَا إِن
كُنتَ مِنَ الصَّادِقِينَ
Qaloo aji/tana lita/fikanaAAan alihatina fa/tina bima taAAidunain kunta mina
assadiqeen
Swahili
Wakasema: Je! Umetujia ili ututenge mbali na miungu yetu? Basi tuletee hayo
unayo tuahidi ikiwa wewe ni miongoni mwa wasemao kweli.
|
Ayah 46:23 الأية
قَالَ إِنَّمَا الْعِلْمُ عِندَ اللَّهِ وَأُبَلِّغُكُم مَّا أُرْسِلْتُ بِهِ
وَلَٰكِنِّي أَرَاكُمْ قَوْمًا تَجْهَلُونَ
Qala innama alAAilmu AAindaAllahi waoballighukum ma orsiltu bihi
walakinneearakum qawman tajhaloon
Swahili
Akasema: Hakika ujuzi uko kwa Mwenyezi Mungu. Mimi nakufikishieni niliyo tumwa.
Lakini nakuoneni kuwa nyinyi mnafanya ujinga.
|
Ayah 46:24 الأية
فَلَمَّا رَأَوْهُ عَارِضًا مُّسْتَقْبِلَ أَوْدِيَتِهِمْ قَالُوا هَٰذَا عَارِضٌ
مُّمْطِرُنَا ۚ بَلْ هُوَ مَا اسْتَعْجَلْتُم بِهِ ۖ رِيحٌ فِيهَا عَذَابٌ أَلِيمٌ
Falamma raawhu AAaridanmustaqbila awdiyatihim qaloo hatha AAaridunmumtiruna bal
huwa ma istaAAjaltum bihi reehunfeeha AAathabun aleem
Swahili
Basi walipo liona wingu likielekea kwenye mabonde yao, walisema: Wingu hili la
kutunyeshea mvua! Kumbe sivyo, haya ni hayo mliyo yahimiza, upepo ambao ndani
yake imo adhabu chungu!
|
Ayah 46:25 الأية
تُدَمِّرُ كُلَّ شَيْءٍ بِأَمْرِ رَبِّهَا فَأَصْبَحُوا لَا يُرَىٰ إِلَّا
مَسَاكِنُهُمْ ۚ كَذَٰلِكَ نَجْزِي الْقَوْمَ الْمُجْرِمِينَ
Tudammiru kulla shay-in bi-amri rabbihafaasbahoo la yura illa
masakinuhumkathalika najzee alqawma almujrimeen
Swahili
Unaangamiza kila kitu kwa amri ya Mola wake Mlezi. Wakawa hawaonekani ila nyumba
zao tu. Hivyo ndivyo tuwalipavyo wakosefu!
|
Ayah 46:26 الأية
وَلَقَدْ مَكَّنَّاهُمْ فِيمَا إِن مَّكَّنَّاكُمْ فِيهِ وَجَعَلْنَا لَهُمْ
سَمْعًا وَأَبْصَارًا وَأَفْئِدَةً فَمَا أَغْنَىٰ عَنْهُمْ سَمْعُهُمْ وَلَا
أَبْصَارُهُمْ وَلَا أَفْئِدَتُهُم مِّن شَيْءٍ إِذْ كَانُوا يَجْحَدُونَ بِآيَاتِ
اللَّهِ وَحَاقَ بِهِم مَّا كَانُوا بِهِ يَسْتَهْزِئُونَ
Walaqad makkannahum feema inmakkannakum feehi wajaAAalna lahum samAAan
waabsaranwaaf-idatan fama aghna AAanhum samAAuhum walaabsaruhum wala af-idatuhum
min shay-in ith kanooyajhadoona bi-ayati Allahi wahaqabihim ma kanoo bihi
yastahzi-oon
Swahili
Na bila ya shaka tuliwaweka vizuri sio kama tulivyo kuwekeni nyinyi; na tuliwapa
masikio, na macho, na nyoyo. Na hayakuwafaa kitu masikio yao, wala macho yao,
wala nyoyo zao kwa lolote. Kwani hao walikuwa wakizikataa Ishara za Mwenyezi
Mungu, na yale waliyo kuwa wakiyafanyia maskhara ndiyo yakawazunguka.
|
Ayah 46:27 الأية
وَلَقَدْ أَهْلَكْنَا مَا حَوْلَكُم مِّنَ الْقُرَىٰ وَصَرَّفْنَا الْآيَاتِ
لَعَلَّهُمْ يَرْجِعُونَ
Walaqad ahlakna ma hawlakummina alqura wasarrafna al-ayatilaAAallahum yarjiAAoon
Swahili
Na hakika tuliiangamiza miji ilio jirani zenu, na tulizitumia Ishara ili wapate
kurejea.
|
Ayah 46:28 الأية
فَلَوْلَا نَصَرَهُمُ الَّذِينَ اتَّخَذُوا مِن دُونِ اللَّهِ قُرْبَانًا آلِهَةً ۖ
بَلْ ضَلُّوا عَنْهُمْ ۚ وَذَٰلِكَ إِفْكُهُمْ وَمَا كَانُوا يَفْتَرُونَ
Falawla nasarahumu allatheenaittakhathoo min dooni Allahi qurbanan alihatanbal
dalloo AAanhum wathalika ifkuhum wama kanooyaftaroon
Swahili
Basi mbona wale walio washika badala ya Mwenyezi Mungu, kuwa ati hao ndio
wawakurubishe, hawakuwanusuru? Bali waliwapotea! Na huo ndio uwongo walio kuwa
wakiuzua.
|
Ayah 46:29 الأية
وَإِذْ صَرَفْنَا إِلَيْكَ نَفَرًا مِّنَ الْجِنِّ يَسْتَمِعُونَ الْقُرْآنَ
فَلَمَّا حَضَرُوهُ قَالُوا أَنصِتُوا ۖ فَلَمَّا قُضِيَ وَلَّوْا إِلَىٰ قَوْمِهِم
مُّنذِرِينَ
Wa-ith sarafna ilaykanafaran mina aljinni yastamiAAoona alqur-ana
falammahadaroohu qaloo ansitoo falammaqudiya wallaw ila qawmihim munthireen
Swahili
Na wakati tulipo waleta kundi la majini kuja kwako kusikiliza Qur'ani. Basi
walipo ihudhuria walisema: Sikilizeni! Na ilipo kwisha somwa, walirudi kwa kaumu
yao kwenda kuwaonya.
|
Ayah 46:30 الأية
قَالُوا يَا قَوْمَنَا إِنَّا سَمِعْنَا كِتَابًا أُنزِلَ مِن بَعْدِ مُوسَىٰ
مُصَدِّقًا لِّمَا بَيْنَ يَدَيْهِ يَهْدِي إِلَى الْحَقِّ وَإِلَىٰ طَرِيقٍ
مُّسْتَقِيمٍ
Qaloo ya qawmana innasamiAAna kitaban onzila min baAAdi moosa musaddiqanlima
bayna yadayhi yahdee ila alhaqqi wa-ilatareeqin mustaqeem
Swahili
Wakasema: Enyi kaumu yetu! Sisi tumesikia Kitabu kilicho teremshwa baada ya
Musa, kinacho sadikisha yaliyo kuwa kabla yake, na kinacho ongoza kwenye Haki na
kwenye Njia Iliyo Nyooka.
|
Ayah 46:31 الأية
يَا قَوْمَنَا أَجِيبُوا دَاعِيَ اللَّهِ وَآمِنُوا بِهِ يَغْفِرْ لَكُم مِّن
ذُنُوبِكُمْ وَيُجِرْكُم مِّنْ عَذَابٍ أَلِيمٍ
Ya qawmana ajeeboo daAAiyaAllahi waaminoo bihi yaghfir lakum min
thunoobikumwayujirkum min AAathabin aleem
Swahili
Enyi kaumu yetu! Muitikieni Mwenye kuitia kwa Mwenyezi Mungu, na muaminini,
Mwenyezi Mungu atakusameheni, na atakukingeni na adhabu chungu.
|
Ayah 46:32 الأية
وَمَن لَّا يُجِبْ دَاعِيَ اللَّهِ فَلَيْسَ بِمُعْجِزٍ فِي الْأَرْضِ وَلَيْسَ
لَهُ مِن دُونِهِ أَوْلِيَاءُ ۚ أُولَٰئِكَ فِي ضَلَالٍ مُّبِينٍ
Waman la yujib daAAiya Allahifalaysa bimuAAjizin fee al-ardi walaysa lahu min
doonihiawliyaa ola-ika fee dalalin mubeen
Swahili
Na wasio mwitikia Mwitaji wa Mwenyezi Mungu basi hao hawatashinda katika ardhi,
wala hawatakuwa na walinzi mbele yake. Hao wamo katika upotovu ulio dhaahiri.
|
Ayah 46:33 الأية
أَوَلَمْ يَرَوْا أَنَّ اللَّهَ الَّذِي خَلَقَ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضَ وَلَمْ
يَعْيَ بِخَلْقِهِنَّ بِقَادِرٍ عَلَىٰ أَن يُحْيِيَ الْمَوْتَىٰ ۚ بَلَىٰ إِنَّهُ
عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ
Awa lam yaraw anna Allaha allatheekhalaqa assamawati wal-ardawalam yaAAya
bikhalqihinna biqadirin AAala an yuhyiyaalmawta bala innahu AAala kulli
shay-inqadeer
Swahili
Je! Hawaoni ya kwamba Mwenyezi Mungu, aliye ziumba mbingu na ardhi, na hakuchoka
kwa kuziumba, kuwa ni Muweza wa kuwafufua wafu? Kwani? Hakika Yeye ni Muweza wa
kila kitu.
|
Ayah 46:34 الأية
وَيَوْمَ يُعْرَضُ الَّذِينَ كَفَرُوا عَلَى النَّارِ أَلَيْسَ هَٰذَا بِالْحَقِّ ۖ
قَالُوا بَلَىٰ وَرَبِّنَا ۚ قَالَ فَذُوقُوا الْعَذَابَ بِمَا كُنتُمْ تَكْفُرُونَ
Wayawma yuAAradu allatheenakafaroo AAala annari alaysa hatha bilhaqqiqaloo bala
warabbina qala fathooqooalAAathaba bima kuntum takfuroon
Swahili
Na siku watakapo letwa makafiri Motoni wakaambiwa: Je! Haya si kweli? Watasema:
Kwani? Tunaapa kwa Mola wetu Mlezi, ni kweli! Atasema: Basi onjeni adhabu kwa
sababu ya kule kukataa kwenu.
|
Ayah 46:35 الأية
فَاصْبِرْ كَمَا صَبَرَ أُولُو الْعَزْمِ مِنَ الرُّسُلِ وَلَا تَسْتَعْجِل لَّهُمْ
ۚ كَأَنَّهُمْ يَوْمَ يَرَوْنَ مَا يُوعَدُونَ لَمْ يَلْبَثُوا إِلَّا سَاعَةً مِّن
نَّهَارٍ ۚ بَلَاغٌ ۚ فَهَلْ يُهْلَكُ إِلَّا الْقَوْمُ الْفَاسِقُونَ
Fasbir kama sabaraoloo alAAazmi mina arrusuli wala tastaAAjil lahumkaannahum
yawma yarawna ma yooAAadoona lam yalbathoo illasaAAatan min naharin balaghun
fahal yuhlakuilla alqawmu alfasiqoon
Swahili
Basi subiri, kama walivyo subiri Mitume wenye stahmala kubwa, wala usiwafanyie
haraka. Siku watakayo yaona waliyo ahidiwa itakuwa kama kwamba hawakukaa
ulimwenguni ila saa moja ya mchana. Huu ndio ufikisho! Kwani huangamizwa wengine
isipo kuwa walio waovu tu?
|
©
EsinIslam.Com Designed & produced by The Awqaf London. Please pray for us
|