First Ayah 1 الأية الأوليبِسْم ِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تُقَدِّمُوا بَيْنَ يَدَيِ اللَّهِ وَرَسُولِهِ
ۖ وَاتَّقُوا اللَّهَ ۚ إِنَّ اللَّهَ سَمِيعٌ عَلِيمٌ
Ya ayyuha allatheena amanoola tuqaddimoo bayna yadayi Allahi warasoolihi
wattaqooAllaha inna Allaha sameeAAun AAaleem
Swahili
Enyi mlio amini! Msitangulie mbele ya Mwenyezi Mungu na Mtume wake, na mcheni
Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusikia, Mwenye kujua.
|
Ayah 49:2 الأية
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تَرْفَعُوا أَصْوَاتَكُمْ فَوْقَ صَوْتِ
النَّبِيِّ وَلَا تَجْهَرُوا لَهُ بِالْقَوْلِ كَجَهْرِ بَعْضِكُمْ لِبَعْضٍ أَن
تَحْبَطَ أَعْمَالُكُمْ وَأَنتُمْ لَا تَشْعُرُونَ
Ya ayyuha allatheena amanoola tarfaAAoo aswatakum fawqa sawti annabiyyiwala
tajharoo lahu bilqawli kajahri baAAdikumlibaAAdin an tahbata aAAmalukumwaantum
la tashAAuroon
Swahili
Enyi mlio amini! Msinyanyue sauti zenu kuliko sauti ya Nabii, wala msiseme naye
kwa kelele kama mnavyo semezana nyinyi kwa nyinyi, visije vitendo vyenu
vikaharibika, na hali hamtambui.
|
Ayah 49:3 الأية
إِنَّ الَّذِينَ يَغُضُّونَ أَصْوَاتَهُمْ عِندَ رَسُولِ اللَّهِ أُولَٰئِكَ
الَّذِينَ امْتَحَنَ اللَّهُ قُلُوبَهُمْ لِلتَّقْوَىٰ ۚ لَهُم مَّغْفِرَةٌ
وَأَجْرٌ عَظِيمٌ
Inna allatheena yaghuddoona aswatahumAAinda rasooli Allahi ola-ika
allatheenaimtahana Allahu quloobahum littaqwalahum maghfiratun waajrun AAatheem
Swahili
Kwa hakika wanao teremsha sauti zao mbele ya Mtume wa Mwenyezi Mungu, hao ndio
Mwenyezi Mungu amezisafisha nyoyo zao kwa uchamngu. Hao watakuwa na maghfira na
ujira mkubwa.
|
Ayah 49:4 الأية
إِنَّ الَّذِينَ يُنَادُونَكَ مِن وَرَاءِ الْحُجُرَاتِ أَكْثَرُهُمْ لَا
يَعْقِلُونَ
Inna allatheena yunadoonaka minwara-i alhujurati aktharuhum layaAAqiloon
Swahili
Hakika hao wanao kuita nawe uko nyuma ya vyumba, wengi wao hawana akili.
|
Ayah 49:5 الأية
وَلَوْ أَنَّهُمْ صَبَرُوا حَتَّىٰ تَخْرُجَ إِلَيْهِمْ لَكَانَ خَيْرًا لَّهُمْ ۚ
وَاللَّهُ غَفُورٌ رَّحِيمٌ
Walaw annahum sabaroo hattatakhruja ilayhim lakana khayran lahum
wallahughafoorun raheem
Swahili
Na lau wao wangeli ngojea mpaka uwatokee ingeli kuwa kheri kwao. Na Mwenyezi
Mungu ni Mwenye maghfira, Mwenye kurehemu.
|
Ayah 49:6 الأية
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا إِن جَاءَكُمْ فَاسِقٌ بِنَبَإٍ فَتَبَيَّنُوا أَن
تُصِيبُوا قَوْمًا بِجَهَالَةٍ فَتُصْبِحُوا عَلَىٰ مَا فَعَلْتُمْ نَادِمِينَ
Ya ayyuha allatheena amanooin jaakum fasiqun binaba-in fatabayyanoo an
tuseebooqawman bijahalatin fatusbihoo AAala mafaAAaltum nadimeen
Swahili
Enyi mlio amini! Akikujieni mpotovu na khabari yoyote, ichunguzeni, msije
mkawasibu watu kwa kuto jua, na mkawa tena wenye kujuta kwa mliyo yatenda.
|
Ayah 49:7 الأية
وَاعْلَمُوا أَنَّ فِيكُمْ رَسُولَ اللَّهِ ۚ لَوْ يُطِيعُكُمْ فِي كَثِيرٍ مِّنَ
الْأَمْرِ لَعَنِتُّمْ وَلَٰكِنَّ اللَّهَ حَبَّبَ إِلَيْكُمُ الْإِيمَانَ
وَزَيَّنَهُ فِي قُلُوبِكُمْ وَكَرَّهَ إِلَيْكُمُ الْكُفْرَ وَالْفُسُوقَ
وَالْعِصْيَانَ ۚ أُولَٰئِكَ هُمُ الرَّاشِدُونَ
WaAAlamoo anna feekum rasoola Allahilaw yuteeAAukum fee katheerin mina al-amri
laAAanittum walakinnaAllaha habbaba ilaykumu al-eemanawazayyanahu fee quloobikum
wakarraha ilaykumu alkufra walfusooqawalAAisyana ola-ika humu arrashidoon
Swahili
Na jueni kuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu yuko nanyi. Lau angeli kut'iini katika
mambo mengi, bila ya shaka mngeli taabika. Lakini Mwenyezi Mungu amekupendezeeni
Imani, na akaipamba katika nyoyo zenu, na amekufanyeni muuchukie ukafiri, na
upotovu, na uasi. Hao ndio walio ongoka,
|
Ayah 49:8 الأية
فَضْلًا مِّنَ اللَّهِ وَنِعْمَةً ۚ وَاللَّهُ عَلِيمٌ حَكِيمٌ
Fadlan mina Allahi waniAAmatanwallahu AAaleemun hakeem
Swahili
Kwa fadhila za Mwenyezi Mungu na neema zake. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kujua,
Mwenye hikima.
|
Ayah 49:9 الأية
وَإِن طَائِفَتَانِ مِنَ الْمُؤْمِنِينَ اقْتَتَلُوا فَأَصْلِحُوا بَيْنَهُمَا ۖ
فَإِن بَغَتْ إِحْدَاهُمَا عَلَى الْأُخْرَىٰ فَقَاتِلُوا الَّتِي تَبْغِي حَتَّىٰ
تَفِيءَ إِلَىٰ أَمْرِ اللَّهِ ۚ فَإِن فَاءَتْ فَأَصْلِحُوا بَيْنَهُمَا
بِالْعَدْلِ وَأَقْسِطُوا ۖ إِنَّ اللَّهَ يُحِبُّ الْمُقْسِطِينَ
Wa-in ta-ifatani minaalmu/mineena iqtataloo faaslihoo baynahumafa-in baghat
ihdahuma AAala al-okhrafaqatiloo allatee tabghee hatta tafee-a ilaamri Allahi
fa-in faat faaslihoobaynahuma bilAAadli waaqsitoo inna Allahayuhibbu almuqsiteen
Swahili
Na ikiwa makundi mawili katika Waumini yanapigana, basi yapatanisheni. Na likiwa
moja la hao linamdhulumu mwenzie, basi lipigeni linalo dhulumu mpaka lirejee
kwenye amri ya Mwenyezi Mungu. Na likirudi basi yapatanisheni kwa uadilifu. Na
hukumuni kwa haki. Hakika Mwenyezi Mungu anawapenda wanao hukumu kwa haki.
|
Ayah 49:10 الأية
إِنَّمَا الْمُؤْمِنُونَ إِخْوَةٌ فَأَصْلِحُوا بَيْنَ أَخَوَيْكُمْ ۚ وَاتَّقُوا
اللَّهَ لَعَلَّكُمْ تُرْحَمُونَ
Innama almu/minoona ikhwatun faaslihoobayna akhawaykum wattaqoo Allaha
laAAallakum turhamoon
Swahili
Hakika Waumini ni ndugu, basi patanisheni baina ya ndugu zenu, na mcheni
Mwenyezi Mungu ili mrehemewe.
|
Ayah 49:11 الأية
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا يَسْخَرْ قَوْمٌ مِّن قَوْمٍ عَسَىٰ أَن
يَكُونُوا خَيْرًا مِّنْهُمْ وَلَا نِسَاءٌ مِّن نِّسَاءٍ عَسَىٰ أَن يَكُنَّ
خَيْرًا مِّنْهُنَّ ۖ وَلَا تَلْمِزُوا أَنفُسَكُمْ وَلَا تَنَابَزُوا
بِالْأَلْقَابِ ۖ بِئْسَ الِاسْمُ الْفُسُوقُ بَعْدَ الْإِيمَانِ ۚ وَمَن لَّمْ
يَتُبْ فَأُولَٰئِكَ هُمُ الظَّالِمُونَ
Ya ayyuha allatheena amanoola yaskhar qawmun min qawmin AAasa an yakoonookhayran
minhum wala nisaon min nisa-in AAasaan yakunna khayran minhunna wala talmizoo
anfusakum walatanabazoo bil-alqabi bi/sa al-ismualfusooqu baAAda al-eemani waman
lam yatub faola-ikahumu aththalimoon
Swahili
Enyi mlio amini! Wanaume wasiwadharau wanaume wenzao, wala wanawake wasiwadharau
wanawake wenzao. Huenda hao wakawa bora kuliko wao. Wala msivunjiane hishima,
wala msiitane kwa majina ya kejeli. Ni uovu kutumia jina baya baada ya kwisha
amini. Na wasio tubu, hao ndio wenye kudhulumu.
|
Ayah 49:12 الأية
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اجْتَنِبُوا كَثِيرًا مِّنَ الظَّنِّ إِنَّ بَعْضَ
الظَّنِّ إِثْمٌ ۖ وَلَا تَجَسَّسُوا وَلَا يَغْتَب بَّعْضُكُم بَعْضًا ۚ أَيُحِبُّ
أَحَدُكُمْ أَن يَأْكُلَ لَحْمَ أَخِيهِ مَيْتًا فَكَرِهْتُمُوهُ ۚ وَاتَّقُوا
اللَّهَ ۚ إِنَّ اللَّهَ تَوَّابٌ رَّحِيمٌ
Ya ayyuha allatheena amanooijtaniboo katheeran mina aththanni innabaAAda
aththanni ithmun walatajassasoo wala yaghtab baAAdukum baAAdanayuhibbu ahadukum
an ya/kula lahma akheehimaytan fakarihtumoohu wattaqoo Allaha inna
Allahatawwabun raheem
Swahili
Enyi mlio amini! Jiepusheni na dhana nyingi, kwani baadhi ya dhana ni dhambi.
Wala msipelelezane, wala msisengenyane nyinyi kwa nyinyi. Je! Yupo katika nyinyi
anaye penda kuila nyama ya nduguye aliye kufa? Mnalichukia hilo! Na mcheni
Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye kupokea toba, Mwenye kurehemu.
|
Ayah 49:13 الأية
يَا أَيُّهَا النَّاسُ إِنَّا خَلَقْنَاكُم مِّن ذَكَرٍ وَأُنثَىٰ وَجَعَلْنَاكُمْ
شُعُوبًا وَقَبَائِلَ لِتَعَارَفُوا ۚ إِنَّ أَكْرَمَكُمْ عِندَ اللَّهِ
أَتْقَاكُمْ ۚ إِنَّ اللَّهَ عَلِيمٌ خَبِيرٌ
Ya ayyuha annasuinna khalaqnakum min thakarin waonthawajaAAalnakum shuAAooban
waqaba-ila litaAAarafooinna akramakum AAinda Allahi atqakum inna AllahaAAaleemun
khabeer
Swahili
Enyi watu! Hakika Sisi tumekuumbeni kutokana na mwanamume na mwanamke. Na
tumekujaalieni kuwa ni mataifa na makabila ili mjuane. Hakika aliye mtukufu
zaidi kati yenu kwa Mwenyezi Mungu ni huyo aliye mchamngu zaidi katika nyinyi.
Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye kujua, Mwenye khabari.
|
Ayah 49:14 الأية
قَالَتِ الْأَعْرَابُ آمَنَّا ۖ قُل لَّمْ تُؤْمِنُوا وَلَٰكِن قُولُوا أَسْلَمْنَا
وَلَمَّا يَدْخُلِ الْإِيمَانُ فِي قُلُوبِكُمْ ۖ وَإِن تُطِيعُوا اللَّهَ
وَرَسُولَهُ لَا يَلِتْكُم مِّنْ أَعْمَالِكُمْ شَيْئًا ۚ إِنَّ اللَّهَ غَفُورٌ
رَّحِيمٌ
Qalati al-aAArabu amannaqul lam tu/minoo walakin qooloo aslamna walammayadkhuli
al-eemanu fee quloobikum wa-in tuteeAAooAllaha warasoolahu la yalitkum min
aAAmalikumshay-an inna Allaha ghafoorun raheem
Swahili
Mabedui wamesema: Tumeamini. Sema: Hamjaamini, lakini semeni: Tumesilimu. Kwani
Imani haijaingia katika nyoyo zenu. Na mkimt'ii Mwenyezi Mungu na Mtume wake,
hatakupunguzieni chochote katika vitendo vyenu. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye
kusamehe, Mwenye kurehemu.
|
Ayah 49:15 الأية
إِنَّمَا الْمُؤْمِنُونَ الَّذِينَ آمَنُوا بِاللَّهِ وَرَسُولِهِ ثُمَّ لَمْ
يَرْتَابُوا وَجَاهَدُوا بِأَمْوَالِهِمْ وَأَنفُسِهِمْ فِي سَبِيلِ اللَّهِ ۚ
أُولَٰئِكَ هُمُ الصَّادِقُونَ
Innama almu/minoona allatheenaamanoo billahi warasoolihi thumma lam
yartaboowajahadoo bi-amwalihim waanfusihim fee sabeeli Allahiola-ika humu
assadiqoon
Swahili
Hakika Waumini ni wale walio muamini Mwenyezi Mungu na Mtume wake tena wasitie
shaka kabisa, na wakapigana Jihadi katika Njia ya Mwenyezi Mungu kwa mali yao na
nafsi zao. Hao ndio wakweli.
|
Ayah 49:16 الأية
قُلْ أَتُعَلِّمُونَ اللَّهَ بِدِينِكُمْ وَاللَّهُ يَعْلَمُ مَا فِي السَّمَاوَاتِ
وَمَا فِي الْأَرْضِ ۚ وَاللَّهُ بِكُلِّ شَيْءٍ عَلِيمٌ
Qul atuAAallimoona Allaha bideenikumwallahu yaAAlamu ma fee assamawatiwama fee
al-ardi wallahu bikullishay-in AAaleem
Swahili
Sema: Ati ndio mnamfundisha Mwenyezi Mungu Dini yenu, na hali Mwenyezi Mungu
anayajua ya katika mbingu na ardhi, na Mwenyezi Mungu anajua kila kitu?
|
Ayah 49:17 الأية
يَمُنُّونَ عَلَيْكَ أَنْ أَسْلَمُوا ۖ قُل لَّا تَمُنُّوا عَلَيَّ إِسْلَامَكُم ۖ
بَلِ اللَّهُ يَمُنُّ عَلَيْكُمْ أَنْ هَدَاكُمْ لِلْإِيمَانِ إِن كُنتُمْ
صَادِقِينَ
Yamunnoona AAalayka an aslamoo qul latamunnoo AAalayya islamakum bali Allahu
yamunnuAAalaykum an hadakum lil-eemani in kuntum sadiqeen
Swahili
Wanakusimbulia kuwa wamesilimu! Sema: Msinisimbulie kwa kusilimu kwenu. Bali
Mwenyezi Mungu ndiye aliye kufanyieni hisani kwa kukuongoeni kwenye Imani, ikiwa
nyinyi ni wakweli.
|
Ayah 49:18 الأية
إِنَّ اللَّهَ يَعْلَمُ غَيْبَ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ ۚ وَاللَّهُ بَصِيرٌ
بِمَا تَعْمَلُونَ
Inna Allaha yaAAlamu ghayba assamawatiwal-ardi wallahu baseerunbima taAAmaloon
Swahili
Hakika Mwenyezi Mungu anajua siri za mbingu na ardhi. Na Mwenyezi Mungu anayaona
myatendayo.
|
©
EsinIslam.Com Designed & produced by The Awqaf London. Please pray for us
|