1st Ayah 1 الأية ١الأوليبِسْم ِ اللهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا أَوْفُوا بِالْعُقُودِ ۚ أُحِلَّتْ لَكُم بَهِيمَةُ
الْأَنْعَامِ إِلَّا مَا يُتْلَىٰ عَلَيْكُمْ غَيْرَ مُحِلِّي الصَّيْدِ وَأَنتُمْ
حُرُمٌ ۗ إِنَّ اللهَ يَحْكُمُ مَا يُرِيدُ
Ya ayyuha allatheena amanooawfoo bilAAuqoodi ohillat lakum baheematu
al-anAAamiilla ma yutla AAalaykum ghayra muhilleeassaydi waantum hurumun inna
Allahayahkumu ma yureed
Swahili
Enyi mlio amini! Timizeni ahadi. Mmehalalishiwa wanyama wa mifugo, ila wale mnao
tajiwa. Lakini msihalalishe kuwinda nanyi mmo katika Hija. Hakika Mwenyezi Mungu
anahukumu apendavyo.
|
Ayah 5:2 الأية
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تُحِلُّوا شَعَائِرَ اللهِ وَلَا الشَّهْرَ
الْحَرَامَ وَلَا الْهَدْيَ وَلَا الْقَلَائِدَ وَلَا آمِّينَ الْبَيْتَ الْحَرَامَ
يَبْتَغُونَ فَضْلًا مِّن رَّبِّهِمْ وَرِضْوَانًا ۚ وَإِذَا حَلَلْتُمْ
فَاصْطَادُوا ۚ وَلَا يَجْرِمَنَّكُمْ شَنَآنُ قَوْمٍ أَن صَدُّوكُمْ عَنِ
الْمَسْجِدِ الْحَرَامِ أَن تَعْتَدُوا ۘ وَتَعَاوَنُوا عَلَى الْبِرِّ
وَالتَّقْوَىٰ ۖ وَلَا تَعَاوَنُوا عَلَى الْإِثْمِ وَالْعُدْوَانِ ۚ وَاتَّقُوا
اللهَ ۖ إِنَّ اللهَ شَدِيدُ الْعِقَابِ
Ya ayyuha allatheena amanoola tuhilloo shaAAa-ira Allahi walaashshahra alharama
wala alhadya walaalqala-ida wala ammeena albayta alharamayabtaghoona fadlan min
rabbihim waridwananwa-itha halaltum fastadoo walayajrimannakum shanaanu qawmin
an saddookum AAanialmasjidi alharami an taAAtadoo wataAAawanooAAala albirri
wattaqwa wala taAAawanooAAala al-ithmi walAAudwani wattaqooAllaha inna Allaha
shadeedu alAAiqab
Swahili
Enyi mlio amini! Msivunje hishima ya alama ya Dini ya Mwenyezi Mungu wala mwezi
mtakatifu, wala wanyama wanao pelekwa Makka kuchinjwa, wala vigwe vyao, wala
wanao elekea kwendea Nyumba Takatifu, wakitafuta fadhila na radhi za Mola wao
Mlezi. Na mkisha toka Hija yenu basi windeni. Wala kuwachukia watu kwa kuwa
wali- kuzuilieni kufika Msikiti mtakatifu kusikupelekeeni kuwafanyia uadui. Na
saidianeni katika wema na uchamngu. Wala msisaidiane katika dhambi na uadui. Na
mcheni Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mkali wa kuadhibu.
|
Ayah 5:3 الأية
حُرِّمَتْ عَلَيْكُمُ الْمَيْتَةُ وَالدَّمُ وَلَحْمُ الْخِنزِيرِ وَمَا أُهِلَّ
لِغَيْرِ اللهِ بِهِ وَالْمُنْخَنِقَةُ وَالْمَوْقُوذَةُ وَالْمُتَرَدِّيَةُ
وَالنَّطِيحَةُ وَمَا أَكَلَ السَّبُعُ إِلَّا مَا ذَكَّيْتُمْ وَمَا ذُبِحَ عَلَى
النُّصُبِ وَأَن تَسْتَقْسِمُوا بِالْأَزْلَامِ ۚ ذَٰلِكُمْ فِسْقٌ ۗ الْيَوْمَ
يَئِسَ الَّذِينَ كَفَرُوا مِن دِينِكُمْ فَلَا تَخْشَوْهُمْ وَاخْشَوْنِ ۚ
الْيَوْمَ أَكْمَلْتُ لَكُمْ دِينَكُمْ وَأَتْمَمْتُ عَلَيْكُمْ نِعْمَتِي
وَرَضِيتُ لَكُمُ الْإِسْلَامَ دِينًا ۚ فَمَنِ اضْطُرَّ فِي مَخْمَصَةٍ غَيْرَ
مُتَجَانِفٍ لِّإِثْمٍ ۙ فَإِنَّ اللهَ غَفُورٌ رَّحِيمٌ
Hurrimat AAalaykumu almaytatu waddamuwalahmu alkhinzeeri wama ohilla lighayri
Allahibihi walmunkhaniqatu walmawqoothatu walmutaraddiyatuwannateehatu wama
akala assabuAAuilla ma thakkaytum wama thubihaAAala annusubi waan tastaqsimoo
bil-azlamithalikum fisqun alyawma ya-isa allatheena kafaroomin deenikum fala
takhshawhum wakhshawni alyawmaakmaltu lakum deenakum waatmamtu AAalaykum
niAAmatee waradeetulakumu al-islama deenan famani idturra fee makhmasatinghayra
mutajanifin li-ithmin fa-inna Allahaghafoorun raheem
Swahili
Mmeharimishiwa nyamafu, na damu, na nyama ya nguruwe, na mnyama aliye chinjwa si
kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, na aliye kufa kwa kunyongeka koo, na aliye kufa kwa
kupigwa, na aliye kufa kwa kuanguka, na aliye kufa kwa kupigwa pembe, aliye liwa
na mnyama, ila mkimdiriki kumchinja. Na pia ni haramu kula nyama aliye chinjiwa
masanamu. Na ni haramu kupiga ramli. Hayo yote ni upotovu. Leo walio kufuru
wamekata tamaa na Dini yenu; basi msiwaogope, bali niogopeni Mimi. Leo
nimekukamiliishieni Dini yenu, na nimekutimizieni neema yangu, na
nimekupendeleeni UISLAMU uwe ndiyo Dini. Na mwenye kushurutishwa na njaa, bila
ya kupendelea dhambi, basi hakika Mwenyezi Mungu ni Msamehevu na Mwenye
kurehemu.
|
Ayah 5:4 الأية
يَسْأَلُونَكَ مَاذَا أُحِلَّ لَهُمْ ۖ قُلْ أُحِلَّ لَكُمُ الطَّيِّبَاتُ ۙ وَمَا
عَلَّمْتُم مِّنَ الْجَوَارِحِ مُكَلِّبِينَ تُعَلِّمُونَهُنَّ مِمَّا عَلَّمَكُمُ
اللهُ ۖ فَكُلُوا مِمَّا أَمْسَكْنَ عَلَيْكُمْ وَاذْكُرُوا اسْمَ اللهِ
عَلَيْهِ ۖ وَاتَّقُوا اللهَ ۚ إِنَّ اللهَ سَرِيعُ الْحِسَابِ
Yas-aloonaka matha ohilla lahumqul ohilla lakumu attayyibatu wamaAAallamtum mina
aljawarihi mukallibeenatuAAallimoonahunna mimma AAallamakumu Allahufakuloo mimma
amsakna AAalaykum wathkurooisma Allahi AAalayhi wattaqoo Allaha innaAllaha
sareeAAu alhisab
Swahili
Wanakuuliza wamehalalishiwa nini? Sema: Mmehalalishiwa kila vilivyo vizuri na
mlicho wafundisha wanyama kukiwinda. Mnawafundisha alivyo kufunzeni Mwenyezi
Mungu. Basi kuleni walicho kukamatieni, na mkisomee jina la Mwenyezi Mungu. Na
mcheni Mwenyezi Mungu; hakika Mwenyezi Mungu ni Mwepesi wa kuhisabu.
|
Ayah 5:5 الأية
الْيَوْمَ أُحِلَّ لَكُمُ الطَّيِّبَاتُ ۖ وَطَعَامُ الَّذِينَ أُوتُوا الْكِتَابَ
حِلٌّ لَّكُمْ وَطَعَامُكُمْ حِلٌّ لَّهُمْ ۖ وَالْمُحْصَنَاتُ مِنَ الْمُؤْمِنَاتِ
وَالْمُحْصَنَاتُ مِنَ الَّذِينَ أُوتُوا الْكِتَابَ مِن قَبْلِكُمْ إِذَا
آتَيْتُمُوهُنَّ أُجُورَهُنَّ مُحْصِنِينَ غَيْرَ مُسَافِحِينَ وَلَا مُتَّخِذِي
أَخْدَانٍ ۗ وَمَن يَكْفُرْ بِالْإِيمَانِ فَقَدْ حَبِطَ عَمَلُهُ وَهُوَ فِي
الْآخِرَةِ مِنَ الْخَاسِرِينَ
Alyawma ohilla lakumu attayyibatuwataAAamu allatheena ootoo alkitaba hillunlakum
wataAAamukum hillun lahum walmuhsanatumina almu/minati walmuhsanatu
minaallatheena ootoo alkitaba min qablikum itha ataytumoohunnaojoorahunna
muhsineena ghayra musafiheenawala muttakhithee akhdanin waman yakfur
bil-eemanifaqad habita AAamaluhu wahuwa fee al-akhiratimina alkhasireen
Swahili
Leo mmehalalishiwa kila vilivyo vizuri. Na chakula cha walio pewa Kitabu ni
halali kwenu, na chakula chenu ni halali kwao. Na pia wanawake wema miongoni mwa
Waumini, na wanawake wema miongoni mwa walio pewa Kitabu kabla yenu, mtakapo
wapa mahari yao, mkafunga nao ndoa, bila ya kufanya uhasharati wala kuwaweka
kinyumba. Na anaye kataa kuamini bila shaka a'mali yake imepotea, naye katika
Akhera atakuwa miongoni mwa wenye khasara.
|
Ayah 5:6 الأية
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا إِذَا قُمْتُمْ إِلَى الصَّلَاةِ فَاغْسِلُوا
وُجُوهَكُمْ وَأَيْدِيَكُمْ إِلَى الْمَرَافِقِ وَامْسَحُوا بِرُءُوسِكُمْ
وَأَرْجُلَكُمْ إِلَى الْكَعْبَيْنِ ۚ وَإِن كُنتُمْ جُنُبًا فَاطَّهَّرُوا ۚ وَإِن
كُنتُم مَّرْضَىٰ أَوْ عَلَىٰ سَفَرٍ أَوْ جَاءَ أَحَدٌ مِّنكُم مِّنَ الْغَائِطِ
أَوْ لَامَسْتُمُ النِّسَاءَ فَلَمْ تَجِدُوا مَاءً فَتَيَمَّمُوا صَعِيدًا
طَيِّبًا فَامْسَحُوا بِوُجُوهِكُمْ وَأَيْدِيكُم مِّنْهُ ۚ مَا يُرِيدُ اللهُ
لِيَجْعَلَ عَلَيْكُم مِّنْ حَرَجٍ وَلَٰكِن يُرِيدُ لِيُطَهِّرَكُمْ وَلِيُتِمَّ
نِعْمَتَهُ عَلَيْكُمْ لَعَلَّكُمْ تَشْكُرُونَ
Ya ayyuha allatheena amanooitha qumtum ila assalati faghsiloowujoohakum
waaydiyakum ila almarafiqi wamsahoobiruoosikum waarjulakum ila alkaAAbayni wa-in
kuntumjunuban fattahharoo wa-in kuntum marda awAAala safarin aw jaa ahadun
minkum mina algha-itiaw lamastumu annisaa falam tajidoo maanfatayammamoo
saAAeedan tayyiban famsahoobiwujoohikum waaydeekum minhu ma yureedu
AllahuliyajAAala AAalaykum min harajin walakin yureeduliyutahhirakum waliyutimma
niAAmatahu AAalaykumlaAAallakum tashkuroon
Swahili
Enyi mlio amini! Mnapo simama kwa ajili ya Sala basi osheni nyuso zenu, na
mikono yenu mpaka vifundoni, na mpake vichwa vyenu, na osheni miguu yenu mpaka
vifundoni. Na mkiwa na janaba basi ogeni. Na mkiwa wagonjwa au mmo safarini, au
mmoja wenu ametoka chooni au mmewagusa wanawake, na hamkupata maji, basi
tayamamuni vumbi lilio safi, na mpake nyuso zenu na mikono yenu. Hapendi
Mwenyezi Mungu kukutieni katika taabu; bali anataka kukutakaseni na kutimiza
neema yake juu yenu ili mpate kushukuru.
|
Ayah 5:7 الأية
وَاذْكُرُوا نِعْمَةَ اللهِ عَلَيْكُمْ وَمِيثَاقَهُ الَّذِي وَاثَقَكُم بِهِ
إِذْ قُلْتُمْ سَمِعْنَا وَأَطَعْنَا ۖ وَاتَّقُوا اللهَ ۚ إِنَّ اللهَ عَلِيمٌ
بِذَاتِ الصُّدُورِ
Wathkuroo niAAmata AllahiAAalaykum wameethaqahu allathee wathaqakumbihi ith
qultum samiAAna waataAAna wattaqooAllaha inna Allaha AAaleemun bithati assudoor
Swahili
Na kumbukeni neema ya Mwenyezi Mungu iliyo juu yenu, na ahadi yake aliyo
fungamana nanyi mlipo sema: Tumesikia na tumet'ii. Na mcheni Mwenyezi Mungu.
Hakika Mwenyezi Mungu ni Mjuzi sana wa yaliyomo vifuani.
|
Ayah 5:8 الأية
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا كُونُوا قَوَّامِينَ لِلَّهِ شُهَدَاءَ بِالْقِسْطِ
ۖ وَلَا يَجْرِمَنَّكُمْ شَنَآنُ قَوْمٍ عَلَىٰ أَلَّا تَعْدِلُوا ۚ اعْدِلُوا هُوَ
أَقْرَبُ لِلتَّقْوَىٰ ۖ وَاتَّقُوا اللهَ ۚ إِنَّ اللهَ خَبِيرٌ بِمَا
تَعْمَلُونَ
Ya ayyuha allatheena amanookoonoo qawwameena lillahi shuhadaa bilqistiwala
yajrimannakum shanaanu qawmin AAala allataAAdiloo iAAdiloo huwa aqrabu littaqwa
wattaqooAllaha inna Allaha khabeerun bima taAAmaloon
Swahili
Enyi mlio amini! Kuweni wasimamizi madhubuti kwa ajili ya Mwenyezi Mungu mkitoa
ushahidi kwa haki. Wala kuchukiana na watu kusikupelekeeni kutofanya uadilifu.
Fanyeni uadilifu. Hivyo ndio kuwa karibu mno na uchamngu. Na mcheni Mwenyezi
Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu anazo khabari za mnayo yatenda.
|
Ayah 5:9 الأية
وَعَدَ اللهُ الَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ ۙ لَهُم مَّغْفِرَةٌ
وَأَجْرٌ عَظِيمٌ
WaAAada Allahu allatheena amanoowaAAamiloo assalihati lahum maghfiratunwaajrun
AAatheem
Swahili
Mwenyezi Mungu amewaahidi walio muamini na wakatenda mema kwamba watapata
maghfira na malipo makubwa.
|
Ayah 5:10 الأية
وَالَّذِينَ كَفَرُوا وَكَذَّبُوا بِآيَاتِنَا أُولَٰئِكَ أَصْحَابُ الْجَحِيمِ
Wallatheena kafaroo wakaththaboobi-ayatina ola-ika as-habualjaheem
Swahili
Na wale walio kufuru na wakakanusha Ishara zetu, hao ndio watu wa Motoni.
|
Ayah 5:11 الأية
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اذْكُرُوا نِعْمَتَ اللهِ عَلَيْكُمْ إِذْ هَمَّ
قَوْمٌ أَن يَبْسُطُوا إِلَيْكُمْ أَيْدِيَهُمْ فَكَفَّ أَيْدِيَهُمْ عَنكُمْ ۖ
وَاتَّقُوا اللهَ ۚ وَعَلَى اللهِ فَلْيَتَوَكَّلِ الْمُؤْمِنُونَ
Ya ayyuha allatheena amanooothkuroo niAAmata Allahi AAalaykum ith hammaqawmun an
yabsutoo ilaykum aydiyahum fakaffa aydiyahumAAankum wattaqoo Allaha waAAala
Allahifalyatawakkali almu/minoon
Swahili
Enyi mlio amini! Kumbukeni neema za Mwenyezi Mungu zilizo juu yenu, walipo taka
watu kukunyooshieni mikono, naye akaizuilia mikono yao kukufikieni. Na mcheni
Mwenyezi Mungu. Na Waumini wamtegemee Mwenyezi Mungu tu.
|
Ayah 5:12 الأية
وَلَقَدْ أَخَذَ اللهُ مِيثَاقَ بَنِي إِسْرَائِيلَ وَبَعَثْنَا مِنْهُمُ اثْنَيْ
عَشَرَ نَقِيبًا ۖ وَقَالَ اللهُ إِنِّي مَعَكُمْ ۖ لَئِنْ أَقَمْتُمُ الصَّلَاةَ
وَآتَيْتُمُ الزَّكَاةَ وَآمَنتُم بِرُسُلِي وَعَزَّرْتُمُوهُمْ وَأَقْرَضْتُمُ
اللهَ قَرْضًا حَسَنًا لَّأُكَفِّرَنَّ عَنكُمْ سَيِّئَاتِكُمْ
وَلَأُدْخِلَنَّكُمْ جَنَّاتٍ تَجْرِي مِن تَحْتِهَا الْأَنْهَارُ ۚ فَمَن كَفَرَ
بَعْدَ ذَٰلِكَ مِنكُمْ فَقَدْ ضَلَّ سَوَاءَ السَّبِيلِ
Walaqad akhatha Allahu meethaqabanee isra-eela wabaAAathna minhumu ithnay
AAasharanaqeeban waqala Allahu innee maAAakum la-inaqamtumu assalata waataytumu
azzakatawaamantum birusulee waAAazzartumoohum waaqradtumuAllaha qardan hasanan
laokaffiranna AAankumsayyi-atikum walaodkhilannakum jannatin tajree mintahtiha
al-anharu faman kafara baAAda thalikaminkum faqad dalla sawaa assabeel
Swahili
Na Mwenyezi Mungu alifanya agano na Wana wa Israili. Na tukawateulia kutokana
nao wakuu kumi na mbili. Na Mwenyezi Mungu akasema: Kwa yakini Mimi ni pamoja
nanyi. Mkisali, na mkatoa Zaka, na mkawaamini Mitume wangu, na mkawasaidia, na
mkamkopesha Mwenyezi Mungu mkopo mwema, hapana shaka nitakufutieni maovu yenu na
nitakuingizeni katika mabustani yapitayo mito kati yake. Lakini atakaye kufuru
miongoni mwenu baada ya hayo bila ya shaka atakuwa amepotea njia iliyo sawa.
|
Ayah 5:13 الأية
فَبِمَا نَقْضِهِم مِّيثَاقَهُمْ لَعَنَّاهُمْ وَجَعَلْنَا قُلُوبَهُمْ قَاسِيَةً ۖ
يُحَرِّفُونَ الْكَلِمَ عَن مَّوَاضِعِهِ ۙ وَنَسُوا حَظًّا مِّمَّا ذُكِّرُوا بِهِ
ۚ وَلَا تَزَالُ تَطَّلِعُ عَلَىٰ خَائِنَةٍ مِّنْهُمْ إِلَّا قَلِيلًا مِّنْهُمْ ۖ
فَاعْفُ عَنْهُمْ وَاصْفَحْ ۚ إِنَّ اللهَ يُحِبُّ الْمُحْسِنِينَ
Fabima naqdihim meethaqahumlaAAannahum wajaAAalna quloobahum
qasiyatanyuharrifoona alkalima AAan mawadiAAihi wanasoo haththanmimma thukkiroo
bihi wala tazalu tattaliAAuAAala kha-inatin minhum illa qaleelan minhumfaAAfu
AAanhum wasfah inna Allahayuhibbu almuhsineen
Swahili
Basi kwa sababu ya kuvunja agano lao tuliwalaani, na tukazifanya nyoyo zao kuwa
ngumu. Wanayabadilisha maneno kutoka pahala pake, na wamesahau sehemu ya yale
waliyo kumbushwa. Na huachi kuvumbua khiana kutokana nao, isipo kuwa wachache
miongoni mwao. Basi wasamehe na waache. Hakika Mwenyezi Mungu huwapenda wafanyao
wema.
|
Ayah 5:14 الأية
وَمِنَ الَّذِينَ قَالُوا إِنَّا نَصَارَىٰ أَخَذْنَا مِيثَاقَهُمْ فَنَسُوا حَظًّا
مِّمَّا ذُكِّرُوا بِهِ فَأَغْرَيْنَا بَيْنَهُمُ الْعَدَاوَةَ وَالْبَغْضَاءَ
إِلَىٰ يَوْمِ الْقِيَامَةِ ۚ وَسَوْفَ يُنَبِّئُهُمُ اللهُ بِمَا كَانُوا
يَصْنَعُونَ
Wamina allatheena qaloo innanasara akhathna meethaqahumfanasoo haththan mimma
thukkiroobihi faaghrayna baynahumu alAAadawata walbaghdaaila yawmi alqiyamati
wasawfa yunabbi-ohumu Allahubima kanoo yasnaAAoon
Swahili
Na kutoka kwa wale walio sema: Sisi ni Manasara, tulichukua ahadi yao, lakini
wakasahau sehemu ya waliyo kumbushwa. Kwa hivyo tukaweka kati yao uadui na chuki
mpaka Siku ya Kiyama. Na hapo Mwenyezi Mungu atawaambia waliyo kuwa wakiyafanya.
|
Ayah 5:15 الأية
يَا أَهْلَ الْكِتَابِ قَدْ جَاءَكُمْ رَسُولُنَا يُبَيِّنُ لَكُمْ كَثِيرًا
مِّمَّا كُنتُمْ تُخْفُونَ مِنَ الْكِتَابِ وَيَعْفُو عَن كَثِيرٍ ۚ قَدْ جَاءَكُم
مِّنَ اللهِ نُورٌ وَكِتَابٌ مُّبِينٌ
Ya ahla alkitabi qad jaakumrasooluna yubayyinu lakum katheeran mimma
kuntumtukhfoona mina alkitabi wayaAAfoo AAan katheerin qad jaakummina Allahi
noorun wakitabun mubeen
Swahili
Enyi Watu wa Kitabu! Amekwisha kujieni Mtume wetu anaye kufichulieni mengi mliyo
kuwa mkiyaficha katika Kitabu, na anaye samehe mengi. Bila shaka imekujieni
kutoka kwa Mwenyezi Mungu nuru na Kitabu kinacho bainisha.
|
Ayah 5:16 الأية
يَهْدِي بِهِ اللهُ مَنِ اتَّبَعَ رِضْوَانَهُ سُبُلَ السَّلَامِ وَيُخْرِجُهُم
مِّنَ الظُّلُمَاتِ إِلَى النُّورِ بِإِذْنِهِ وَيَهْدِيهِمْ إِلَىٰ صِرَاطٍ
مُّسْتَقِيمٍ
Yahdee bihi Allahu mani ittabaAAa ridwanahusubula assalami wayukhrijuhum mina
aththulumatiila annoori bi-ithnihi wayahdeehim ilasiratin mustaqeem
Swahili
Mwenyezi Mungu huwaongoa wenye kufuata radhi yake katika njia za salama, na
huwatoa katika giza kuwapeleka kwenye nuru kwa amri yake, na huwaongoa kwenye
njia iliyo nyooka.
|
Ayah 5:17 الأية
لَّقَدْ كَفَرَ الَّذِينَ قَالُوا إِنَّ اللهَ هُوَ الْمَسِيحُ ابْنُ مَرْيَمَ ۚ
قُلْ فَمَن يَمْلِكُ مِنَ اللهِ شَيْئًا إِنْ أَرَادَ أَن يُهْلِكَ الْمَسِيحَ
ابْنَ مَرْيَمَ وَأُمَّهُ وَمَن فِي الْأَرْضِ جَمِيعًا ۗ وَلِلَّهِ مُلْكُ
السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَمَا بَيْنَهُمَا ۚ يَخْلُقُ مَا يَشَاءُ ۚ وَاللهُ
عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ
Laqad kafara allatheena qalooinna Allaha huwa almaseehu ibnu maryama qul
famanyamliku mina Allahi shay-an in arada an yuhlikaalmaseeha ibna maryama
waommahu waman fee al-ardijameeAAan walillahi mulku assamawatiwal-ardi wama
baynahuma yakhluqu mayashao wallahu AAala kulli shay-inqadeer
Swahili
Hakika wamekufuru walio sema: Mwenyezi Mungu ni Masihi mwana wa Maryamu. Sema:
Ni nani mwenye kumiliki cho chote mbele ya Mwenyezi Mungu ikiwa Yeye angetaka
kumuangamiza Masihi mwana wa Maryamu, na mama yake, na wote waliomo katika
ardhi? Na mamlaka ya mbingu na ardhi na vilivyomo ndani yake ni vya Mwenyezi
Mungu. Huumba apendavyo. Na Mwenyezi Mungu anao uweza juu ya kila kitu.
|
Ayah 5:18 الأية
وَقَالَتِ الْيَهُودُ وَالنَّصَارَىٰ نَحْنُ أَبْنَاءُ اللهِ وَأَحِبَّاؤُهُ ۚ
قُلْ فَلِمَ يُعَذِّبُكُم بِذُنُوبِكُم ۖ بَلْ أَنتُم بَشَرٌ مِّمَّنْ خَلَقَ ۚ
يَغْفِرُ لِمَن يَشَاءُ وَيُعَذِّبُ مَن يَشَاءُ ۚ وَلِلَّهِ مُلْكُ السَّمَاوَاتِ
وَالْأَرْضِ وَمَا بَيْنَهُمَا ۖ وَإِلَيْهِ الْمَصِيرُ
Waqalati alyahoodu wannasaranahnu abnao Allahi waahibbaohuqul falima
yuAAaththibukum bithunoobikum bal antumbasharun mimman khalaqa yaghfiru liman
yashao wayuAAaththibuman yashao walillahi mulku assamawatiwal-ardi wama
baynahuma wa-ilayhialmaseer
Swahili
Na Mayahudi na Wakristo wanasema: Sisi ni wana wa Mwenyezi Mungu na vipenzi
vyake. Sema: Basi kwa nini anakuadhibuni kwa ajili ya dhambi zenu? Bali nyinyi
ni watu tu kama wale wengine alio waumba. Humsamehe amtakaye na humuadhibu
amtakaye. Na ni wa Mwenyezi Mungu tu ufalme wa mbingu na ardhi. Na marejeo ni
kwake Yeye.
|
Ayah 5:19 الأية
يَا أَهْلَ الْكِتَابِ قَدْ جَاءَكُمْ رَسُولُنَا يُبَيِّنُ لَكُمْ عَلَىٰ فَتْرَةٍ
مِّنَ الرُّسُلِ أَن تَقُولُوا مَا جَاءَنَا مِن بَشِيرٍ وَلَا نَذِيرٍ ۖ فَقَدْ
جَاءَكُم بَشِيرٌ وَنَذِيرٌ ۗ وَاللهُ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ
Ya ahla alkitabi qad jaakumrasooluna yubayyinu lakum AAala fatratin mina
arrusulian taqooloo ma jaana min basheerin walanatheerin faqad jaakum basheerun
wanatheerunwallahu AAala kulli shay-in qadeer
Swahili
Enyi Watu wa Kitabu! Bila ya shaka amekujilieni Mtume wetu akikubainishieni
katika wakati usio kuwa na Mitume, msije mkasema: Hakufika kwetu mbashiri wala
mwonyaji. Basi amekujieni mbashiri na mwonyaji. Na Mwenyezi Mungu anao uweza wa
kila kitu.
|
Ayah 5:20 الأية
وَإِذْ قَالَ مُوسَىٰ لِقَوْمِهِ يَا قَوْمِ اذْكُرُوا نِعْمَةَ اللهِ عَلَيْكُمْ
إِذْ جَعَلَ فِيكُمْ أَنبِيَاءَ وَجَعَلَكُم مُّلُوكًا وَآتَاكُم مَّا لَمْ يُؤْتِ
أَحَدًا مِّنَ الْعَالَمِينَ
Wa-ith qala moosaliqawmihi ya qawmi othkuroo niAAmata AllahiAAalaykum ith
jaAAala feekum anbiyaa wajaAAalakummulookan waatakum ma lam yu/ti ahadanmina
alAAalameen
Swahili
Na pale Musa alipo waambia watu wake: Enyi watu wangu! Kumbukeni neema za
Mwenyezi Mungu zilizo juu yenu, alipo wateuwa Manabii kati yenu, na akakufanyeni
watawala, na akakupeni ambayo hakuwapa wowote katika walimwengu.
|
Ayah 5:21 الأية
يَا قَوْمِ ادْخُلُوا الْأَرْضَ الْمُقَدَّسَةَ الَّتِي كَتَبَ اللهُ لَكُمْ
وَلَا تَرْتَدُّوا عَلَىٰ أَدْبَارِكُمْ فَتَنقَلِبُوا خَاسِرِينَ
Ya qawmi odkhuloo al-ardaalmuqaddasata allatee kataba Allahu lakum walatartaddoo
AAala adbarikum fatanqaliboo khasireen
Swahili
Enyi watu wangu! Ingieni katika nchi takatifu ambayo Mwenyezi Mungu
amekuandikieni. Wala msirudi nyuma, msije mkawa wenye kukhasirika.
|
Ayah 5:22 الأية
قَالُوا يَا مُوسَىٰ إِنَّ فِيهَا قَوْمًا جَبَّارِينَ وَإِنَّا لَن نَّدْخُلَهَا
حَتَّىٰ يَخْرُجُوا مِنْهَا فَإِن يَخْرُجُوا مِنْهَا فَإِنَّا دَاخِلُونَ
Qaloo ya moosa innafeeha qawman jabbareena wa-inna lannadkhulaha hatta yakhrujoo
minhafa-in yakhrujoo minha fa-inna dakhiloon
Swahili
Wakasema: Ewe Musa! Huko wako watu majabari. Nasi hatutaingia huko mpaka wao
watoke humo. Wakitoka humo hapo tutaingia.
|
Ayah 5:23 الأية
قَالَ رَجُلَانِ مِنَ الَّذِينَ يَخَافُونَ أَنْعَمَ اللهُ عَلَيْهِمَا ادْخُلُوا
عَلَيْهِمُ الْبَابَ فَإِذَا دَخَلْتُمُوهُ فَإِنَّكُمْ غَالِبُونَ ۚ وَعَلَى
اللهِ فَتَوَكَّلُوا إِن كُنتُم مُّؤْمِنِينَ
Qala rajulani mina allatheenayakhafoona anAAama Allahu AAalayhimaodkhuloo
AAalayhimu albaba fa-itha dakhaltumoohufa-innakum ghaliboona waAAala
Allahifatawakkaloo in kuntum mu/mineen
Swahili
Watu wawili miongoni mwa wachamngu ambao Mwenyezi Mungu amewaneemesha, walisema:
Waingilieni kwa mlangoni. Mtakapo waingilia basi kwa yakini nyinyi mtashinda. Na
mtegemeeni Mwenyezi Mungu ikiwa nyinyi ni Waumini.
|
Ayah 5:24 الأية
قَالُوا يَا مُوسَىٰ إِنَّا لَن نَّدْخُلَهَا أَبَدًا مَّا دَامُوا فِيهَا ۖ
فَاذْهَبْ أَنتَ وَرَبُّكَ فَقَاتِلَا إِنَّا هَاهُنَا قَاعِدُونَ
Qaloo ya moosa innalan nadkhulaha abadan ma damoo feehafa-ithhab anta warabbuka
faqatila innahahuna qaAAidoon
Swahili
Wakasema: Ewe Musa! Sisi hatutaingia humo kamwe maadamu wao wamo humo. Basi
nenda wewe na Mola wako Mlezi mkapigane. Sisi tutakaa hapa hapa.
|
Ayah 5:25 الأية
قَالَ رَبِّ إِنِّي لَا أَمْلِكُ إِلَّا نَفْسِي وَأَخِي ۖ فَافْرُقْ بَيْنَنَا
وَبَيْنَ الْقَوْمِ الْفَاسِقِينَ
Qala rabbi innee la amliku illanafsee waakhee fafruq baynana wabayna alqawmi
alfasiqeen
Swahili
Akasema: Mola wangu Mlezi! Hakika mimi similiki ila nafsi yangu na ndugu yangu.
Basi tutenge na hawa watu wapotovu.
|
Ayah 5:26 الأية
قَالَ فَإِنَّهَا مُحَرَّمَةٌ عَلَيْهِمْ ۛ أَرْبَعِينَ سَنَةً ۛ يَتِيهُونَ فِي
الْأَرْضِ ۚ فَلَا تَأْسَ عَلَى الْقَوْمِ الْفَاسِقِينَ
Qala fa-innaha muharramatunAAalayhim arbaAAeena sanatan yateehoona fee al-ardi
falata/sa AAala alqawmi alfasiqeen
Swahili
(Mwenyezi Mungu) akasema: Basi nchi hiyo wameharimishiwa muda wa miaka arubaini,
watakuwa wakitanga-tanga katika ardhi. Basi wewe usiwasikitikie watu wapotovu.
|
Ayah 5:27 الأية
وَاتْلُ عَلَيْهِمْ نَبَأَ ابْنَيْ آدَمَ بِالْحَقِّ إِذْ قَرَّبَا قُرْبَانًا
فَتُقُبِّلَ مِنْ أَحَدِهِمَا وَلَمْ يُتَقَبَّلْ مِنَ الْآخَرِ قَالَ
لَأَقْتُلَنَّكَ ۖ قَالَ إِنَّمَا يَتَقَبَّلُ اللهُ مِنَ الْمُتَّقِينَ
Watlu AAalayhim nabaa ibnay adamabilhaqqi ith qarraba qurbananfatuqubbila min
ahadihima walam yutaqabbal mina al-akhariqala laaqtulannaka qala innama
yataqabbaluAllahu mina almuttaqeen
Swahili
Na wasomee khabari za wana wawili wa Adam kwa kweli. Walipo toa mhanga,
ukakubaliwa wa mmoja wao, na wa mwengine haukukubaliwa. Akasema: Nitakuuwa.
Akasema mwengine: Mwenyezi Mungu huwapokelea wachamngu.
|
Ayah 5:28 الأية
لَئِن بَسَطتَ إِلَيَّ يَدَكَ لِتَقْتُلَنِي مَا أَنَا بِبَاسِطٍ يَدِيَ إِلَيْكَ
لِأَقْتُلَكَ ۖ إِنِّي أَخَافُ اللهَ رَبَّ الْعَالَمِينَ
La-in basatta ilayya yadakalitaqtulanee ma ana bibasitin yadiyailayka
li-aqtulaka innee akhafu Allaha rabba alAAalameen
Swahili
Ukininyooshea mkono wako kuniuwa, mimi sitakunyooshea mkono wangu kukuuwa.
Hakika mimi namwogopa Mwenyezi Mungu, Mola wa walimwengu wote.
|
Ayah 5:29 الأية
إِنِّي أُرِيدُ أَن تَبُوءَ بِإِثْمِي وَإِثْمِكَ فَتَكُونَ مِنْ أَصْحَابِ
النَّارِ ۚ وَذَٰلِكَ جَزَاءُ الظَّالِمِينَ
Innee oreedu an taboo-a bi-ithmee wa-ithmikafatakoona min as-habi annari
wathalikajazao aththalimeen
Swahili
Mimi nataka ubebe dhambi zangu na dhambi zako, kwani wewe utakuwa miongoni mwa
watu wa Motoni. Na hayo ndiyo malipo ya wenye kudhulumu.
|
Ayah 5:30 الأية
فَطَوَّعَتْ لَهُ نَفْسُهُ قَتْلَ أَخِيهِ فَقَتَلَهُ فَأَصْبَحَ مِنَ
الْخَاسِرِينَ
FatawwaAAat lahu nafsuhu qatlaakheehi faqatalahu faasbaha mina alkhasireen
Swahili
Basi nafsi yake ikampelekea kumuuwa nduguye, akamuuwa na akawa miongoni mwa
wenye kukhasirika.
|
Ayah 5:31 الأية
فَبَعَثَ اللهُ غُرَابًا يَبْحَثُ فِي الْأَرْضِ لِيُرِيَهُ كَيْفَ يُوَارِي
سَوْءَةَ أَخِيهِ ۚ قَالَ يَا وَيْلَتَا أَعَجَزْتُ أَنْ أَكُونَ مِثْلَ هَٰذَا
الْغُرَابِ فَأُوَارِيَ سَوْءَةَ أَخِي ۖ فَأَصْبَحَ مِنَ النَّادِمِينَ
FabaAAatha Allahu ghuraban yabhathufee al-ardi liyuriyahu kayfa yuwaree
saw-ataakheehi qala ya waylata aAAajaztu an akoonamithla hatha alghurabi
faowariya saw-ataakhee faasbaha mina annadimeen
Swahili
Hapo Mwenyezi Mungu akamleta kunguru anaye fukua katika ardhi ili amwonyeshe
vipi kumsitiri nduguye. Akasema: Ole wangu! Nimeshindwa kuwa kama kunguru huyu
nikamsitiri ndugu yangu? Basi akawa miongoni mwa wenye kujuta.
|
Ayah 5:32 الأية
مِنْ أَجْلِ ذَٰلِكَ كَتَبْنَا عَلَىٰ بَنِي إِسْرَائِيلَ أَنَّهُ مَن قَتَلَ
نَفْسًا بِغَيْرِ نَفْسٍ أَوْ فَسَادٍ فِي الْأَرْضِ فَكَأَنَّمَا قَتَلَ النَّاسَ
جَمِيعًا وَمَنْ أَحْيَاهَا فَكَأَنَّمَا أَحْيَا النَّاسَ جَمِيعًا ۚ وَلَقَدْ
جَاءَتْهُمْ رُسُلُنَا بِالْبَيِّنَاتِ ثُمَّ إِنَّ كَثِيرًا مِّنْهُم بَعْدَ
ذَٰلِكَ فِي الْأَرْضِ لَمُسْرِفُونَ
Min ajli thalika katabna AAalabanee isra-eela annahu man qatala nafsan bighayri
nafsinaw fasadin fee al-ardi fakaannama qatala annasajameeAAan waman ahyaha
fakaannama ahyaannasa jameeAAan walaqad jaat-hum rusulunabilbayyinati thumma
inna katheeran minhum baAAda thalikafee al-ardi lamusrifoon
Swahili
Kwa sababu ya hayo tuliwaandikia Wana wa Israili ya kwamba aliye muuwa mtu bila
ya yeye kuuwa, au kufanya uchafuzi katika nchi, basi ni kama amewauwa watu wote.
Na mwenye kumuokoa mtu na mauti ni kama amewaokoa watu wote. Na hakika waliwajia
Mitume wetu na hoja zilizo wazi. Kisha wengi katika wao baada ya haya wakawa
waharibifu katika nchi.
|
Ayah 5:33 الأية
إِنَّمَا جَزَاءُ الَّذِينَ يُحَارِبُونَ اللهَ وَرَسُولَهُ وَيَسْعَوْنَ فِي
الْأَرْضِ فَسَادًا أَن يُقَتَّلُوا أَوْ يُصَلَّبُوا أَوْ تُقَطَّعَ أَيْدِيهِمْ
وَأَرْجُلُهُم مِّنْ خِلَافٍ أَوْ يُنفَوْا مِنَ الْأَرْضِ ۚ ذَٰلِكَ لَهُمْ خِزْيٌ
فِي الدُّنْيَا ۖ وَلَهُمْ فِي الْآخِرَةِ عَذَابٌ عَظِيمٌ
Innama jazao allatheenayuhariboona Allaha warasoolahu wayasAAawna feeal-ardi
fasadan an yuqattaloo aw yusallabooaw tuqattaAAa aydeehim waarjuluhum min
khilafin awyunfaw mina al-ardi thalika lahum khizyun fee addunyawalahum fee
al-akhirati AAathabun AAatheem
Swahili
Basi malipo ya wale wanao mpiga vita Mwenyezi Mungu na Mtume wake na wakawania
kufanya uchafuzi katika nchi, ni kuuwawa, au kusalibiwa, au kukatwa mikono yao
na miguu yao kwa mabadilisho, au kutolewa nchi. Hii ndiyo hizaya yao katika
dunia; na katika Akhera watapata adhabu kubwa.
|
Ayah 5:34 الأية
إِلَّا الَّذِينَ تَابُوا مِن قَبْلِ أَن تَقْدِرُوا عَلَيْهِمْ ۖ فَاعْلَمُوا
أَنَّ اللهَ غَفُورٌ رَّحِيمٌ
Illa allatheena taboomin qabli an taqdiroo AAalayhim faAAlamoo anna
Allahaghafoorun raheem
Swahili
Isipo kuwa wale walio tubu kabla hamjawatia nguvuni. Na jueni kwamba Mwenyezi
Mungu ni Mwenye maghfira na Mwenye kurehemu.
|
Ayah 5:35 الأية
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اتَّقُوا اللهَ وَابْتَغُوا إِلَيْهِ
الْوَسِيلَةَ وَجَاهِدُوا فِي سَبِيلِهِ لَعَلَّكُمْ تُفْلِحُونَ
Ya ayyuha allatheena amanooittaqoo Allaha wabtaghoo ilayhi alwaseelata
wajahidoofee sabeelihi laAAallakum tuflihoon
Swahili
Enyi mlio amini! Mcheni Mwenyezi Mungu, na tafuteni njia ya kumfikilia. Na
wanieni kwa juhudi kwa ajili yake ili mpate kuokoka.
|
Ayah 5:36 الأية
إِنَّ الَّذِينَ كَفَرُوا لَوْ أَنَّ لَهُم مَّا فِي الْأَرْضِ جَمِيعًا وَمِثْلَهُ
مَعَهُ لِيَفْتَدُوا بِهِ مِنْ عَذَابِ يَوْمِ الْقِيَامَةِ مَا تُقُبِّلَ مِنْهُمْ
ۖ وَلَهُمْ عَذَابٌ أَلِيمٌ
Inna allatheena kafaroo law annalahum ma fee al-ardi jameeAAan wamithlahu
maAAahuliyaftadoo bihi min AAathabi yawmi alqiyamati matuqubbila minhum walahum
AAathabun aleem
Swahili
Hakika walio kufuru lau wange kuwa na yote yaliyomo duniani, na mengine kama
hayo, ili watoe fidia ya kuepukana na adhabu ya Siku ya Kiyama, yasingeli
pokelewa kwao; na watapata adhabu chungu.
|
Ayah 5:37 الأية
يُرِيدُونَ أَن يَخْرُجُوا مِنَ النَّارِ وَمَا هُم بِخَارِجِينَ مِنْهَا ۖ
وَلَهُمْ عَذَابٌ مُّقِيمٌ
Yureedoona an yakhrujoo mina annariwama hum bikharijeena minha walahum
AAathabunmuqeem
Swahili
Watataka watoke Motoni, lakini hawatatoka humo, na watakuwa na adhabu inayo
dumu.
|
Ayah 5:38 الأية
وَالسَّارِقُ وَالسَّارِقَةُ فَاقْطَعُوا أَيْدِيَهُمَا جَزَاءً بِمَا كَسَبَا
نَكَالًا مِّنَ اللهِ ۗ وَاللهُ عَزِيزٌ حَكِيمٌ
Wassariqu wassariqatufaqtaAAoo aydiyahuma jazaan bimakasaba nakalan mina Allahi
wallahuAAazeezun hakeem
Swahili
Na mwizi mwanamume na mwizi mwanamke, ikateni mikono yao, hayo ni malipo ya
waliyo yachuma, ndiyo adhabu ya mfano itokayo kwa Mwenyezi Mungu. Na Mwenyezi
Mungu ni Mwenye nguvu na Mwenye hikima.
|
Ayah 5:39 الأية
فَمَن تَابَ مِن بَعْدِ ظُلْمِهِ وَأَصْلَحَ فَإِنَّ اللهَ يَتُوبُ عَلَيْهِ ۗ
إِنَّ اللهَ غَفُورٌ رَّحِيمٌ
Faman taba min baAAdi thulmihiwaaslaha fa-inna Allaha yatoobu AAalayhiinna
Allaha ghafoorun raheem
Swahili
Lakini mwenye kutubia baada ya dhulma yake, na akatengenea, basi Mwenyezi Mungu
atapokea toba yake. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye maghfira na Mwenye kurehemu.
|
Ayah 5:40 الأية
أَلَمْ تَعْلَمْ أَنَّ اللهَ لَهُ مُلْكُ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ يُعَذِّبُ
مَن يَشَاءُ وَيَغْفِرُ لِمَن يَشَاءُ ۗ وَاللهُ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ
Alam taAAlam anna Allaha lahu mulku assamawatiwal-ardi yuAAaththibu man
yashaowayaghfiru liman yashao wallahu AAalakulli shay-in qadeer
Swahili
Hujui ya kwamba Mwenyezi Mungu anao ufalme wa mbingu na ardhi? Humuadhibu
amtakaye, na humsamehe amtakaye. Na Mwenyezi Mungu ni Muweza wa kila kitu.
|
Ayah 5:41 الأية
يَا أَيُّهَا الرَّسُولُ لَا يَحْزُنكَ الَّذِينَ يُسَارِعُونَ فِي الْكُفْرِ مِنَ
الَّذِينَ قَالُوا آمَنَّا بِأَفْوَاهِهِمْ وَلَمْ تُؤْمِن قُلُوبُهُمْ ۛ وَمِنَ
الَّذِينَ هَادُوا ۛ سَمَّاعُونَ لِلْكَذِبِ سَمَّاعُونَ لِقَوْمٍ آخَرِينَ لَمْ
يَأْتُوكَ ۖ يُحَرِّفُونَ الْكَلِمَ مِن بَعْدِ مَوَاضِعِهِ ۖ يَقُولُونَ إِنْ
أُوتِيتُمْ هَٰذَا فَخُذُوهُ وَإِن لَّمْ تُؤْتَوْهُ فَاحْذَرُوا ۚ وَمَن يُرِدِ
اللهُ فِتْنَتَهُ فَلَن تَمْلِكَ لَهُ مِنَ اللهِ شَيْئًا ۚ أُولَٰئِكَ
الَّذِينَ لَمْ يُرِدِ اللهُ أَن يُطَهِّرَ قُلُوبَهُمْ ۚ لَهُمْ فِي الدُّنْيَا
خِزْيٌ ۖ وَلَهُمْ فِي الْآخِرَةِ عَذَابٌ عَظِيمٌ
Ya ayyuha arrasoolu layahzunka allatheena yusariAAoona fee alkufrimina
allatheena qaloo amanna bi-afwahihimwalam tu/min quloobuhum wamina allatheena
hadoosammaAAoona lilkathibi sammaAAoona liqawmin akhareenalam ya/tooka
yuharrifoona alkalima min baAAdi mawadiAAihiyaqooloona in ooteetum hatha
fakhuthoohu wa-in lamtu/tawhu fahtharoo waman yuridi Allahufitnatahu falan
tamlika lahu mina Allahi shay-an ola-ikaallatheena lam yuridi Allahu an
yutahhiraquloobahum lahum fee addunya khizyun walahum feeal-akhirati AAathabun
AAatheem
Swahili
Ewe Mtume! Wasikuhuzunishe wa fanyao haraka kukufuru, miongoni mwa wanao sema
kwa vinywa vyao: Tumeamini, na hali nyoyo zao hazikuamini, na miongoni mwa
Mayahudi, wanao sikiliza kwa ajili ya uwongo, wanao sikiliza kwa ajili ya watu
wengine wasio kufikia. Wao huyabadilisha maneno kutoka pahala pake. Wanasema:
Mkipewa haya basi yashikeni, na msipo pewa haya tahadharini. Na mtu ambaye
Mwenyezi Mungu anataka kumfitini huwezi kuwa na madaraka naye mbele ya Mwenyezi
Mungu. Hao ndio ambao Mwenyezi Mungu hataki kuzitakasa nyoyo zao. Watakuwa na
hizaya duniani, na Akhera watakuwa na adhabu kubwa.
|
Ayah 5:42 الأية
سَمَّاعُونَ لِلْكَذِبِ أَكَّالُونَ لِلسُّحْتِ ۚ فَإِن جَاءُوكَ فَاحْكُم
بَيْنَهُمْ أَوْ أَعْرِضْ عَنْهُمْ ۖ وَإِن تُعْرِضْ عَنْهُمْ فَلَن يَضُرُّوكَ
شَيْئًا ۖ وَإِنْ حَكَمْتَ فَاحْكُم بَيْنَهُم بِالْقِسْطِ ۚ إِنَّ اللهَ يُحِبُّ
الْمُقْسِطِينَ
SammaAAoona lilkathibi akkaloonalissuhti fa-in jaooka fahkumbaynahum aw aAArid
AAanhum wa-in tuAArid AAanhumfalan yadurrooka shay-an wa-in hakamta
fahkumbaynahum bilqisti inna Allaha yuhibbualmuqsiteen
Swahili
Hao ni wasikilizaji kwa ajili ya kusema uwongo, na ni walaji mno vya haramu!
Basi wakikujia, wahukumu baina yao au jipuuze nao. Na ukijipuuza nao, basi wao
hawatakudhuru kitu. Na ukiwahukumu, basi hukumu baina yao kwa uadilifu. Hakika
Mwenyezi Mungu anawapenda waadilifu.
|
Ayah 5:43 الأية
وَكَيْفَ يُحَكِّمُونَكَ وَعِندَهُمُ التَّوْرَاةُ فِيهَا حُكْمُ اللهِ ثُمَّ
يَتَوَلَّوْنَ مِن بَعْدِ ذَٰلِكَ ۚ وَمَا أُولَٰئِكَ بِالْمُؤْمِنِينَ
Wakayfa yuhakkimoonaka waAAindahumu attawratufeeha hukmu Allahi thumma
yatawallawna minbaAAdi thalika wama ola-ika bilmu/mineen
Swahili
Na huwaje wakufanye wewe hakimu nao wanayo Taurati yenye hukumu za Mwenyezi
Mungu? Kisha baada ya hayo wanageuka. Na hao si wenye kuamini.
|
Ayah 5:44 الأية
إِنَّا أَنزَلْنَا التَّوْرَاةَ فِيهَا هُدًى وَنُورٌ ۚ يَحْكُمُ بِهَا
النَّبِيُّونَ الَّذِينَ أَسْلَمُوا لِلَّذِينَ هَادُوا وَالرَّبَّانِيُّونَ
وَالْأَحْبَارُ بِمَا اسْتُحْفِظُوا مِن كِتَابِ اللهِ وَكَانُوا عَلَيْهِ
شُهَدَاءَ ۚ فَلَا تَخْشَوُا النَّاسَ وَاخْشَوْنِ وَلَا تَشْتَرُوا بِآيَاتِي
ثَمَنًا قَلِيلًا ۚ وَمَن لَّمْ يَحْكُم بِمَا أَنزَلَ اللهُ فَأُولَٰئِكَ هُمُ
الْكَافِرُونَ
Inna anzalna attawratafeeha hudan wanoorun yahkumu biha annabiyyoonaallatheena
aslamoo lillatheena hadoo warrabbaniyyoonawal-ahbaru bima istuhfithoomin kitabi
Allahi wakanoo AAalayhi shuhadaafala takhshawoo annasa wakhshawniwala tashtaroo
bi-ayatee thamanan qaleelanwaman lam yahkum bima anzala Allahu faola-ikahumu
alkafiroon
Swahili
Hakika Sisi tuliteremsha Taurati yenye uwongofu na nuru, ambayo kwayo Manabii
walio nyenyekea kiislamu, na wachamngu, na wanazuoni, waliwahukumu Mayahudi;
kwani walikabidhiwa kukihifadhi Kitabu cha Mwenyezi Mungu. Nao wakawa ni
mashahidi juu yake. Basi msiwaogope watu, bali niogopeni Mimi. Wala msibadilishe
Aya zangu kwa thamani chache. Na wasio hukumu kwa aliyo teremsha Mwenyezi Mungu,
basi hao ndio makafiri.
|
Ayah 5:45 الأية
وَكَتَبْنَا عَلَيْهِمْ فِيهَا أَنَّ النَّفْسَ بِالنَّفْسِ وَالْعَيْنَ
بِالْعَيْنِ وَالْأَنفَ بِالْأَنفِ وَالْأُذُنَ بِالْأُذُنِ وَالسِّنَّ بِالسِّنِّ
وَالْجُرُوحَ قِصَاصٌ ۚ فَمَن تَصَدَّقَ بِهِ فَهُوَ كَفَّارَةٌ لَّهُ ۚ وَمَن
لَّمْ يَحْكُم بِمَا أَنزَلَ اللهُ فَأُولَٰئِكَ هُمُ الظَّالِمُونَ
Wakatabna AAalayhim feeha annaannafsa binnafsi walAAayna bilAAayniwal-anfa
bil-anfi walothuna bilothuniwassinna bissinni waljurooha qisasunfaman tasaddaqa
bihi fahuwa kaffaratun lahu wamanlam yahkum bima anzala Allahu faola-ikahumu
aththalimoon
Swahili
Na humo tuliwaandikia ya kwamba roho kwa roho, na jicho kwa jicho, na pua kwa
pua, na sikio kwa sikio, na jino kwa jino, na kwa majaraha kisasi. Lakini
atakaye samehe basi itakuwa ni kafara kwake. Na wasio hukumu kwa yale aliyo
yateremsha Mwenyezi Mungu, basi hao ndio madhaalimu.
|
Ayah 5:46 الأية
وَقَفَّيْنَا عَلَىٰ آثَارِهِم بِعِيسَى ابْنِ مَرْيَمَ مُصَدِّقًا لِّمَا بَيْنَ
يَدَيْهِ مِنَ التَّوْرَاةِ ۖ وَآتَيْنَاهُ الْإِنجِيلَ فِيهِ هُدًى وَنُورٌ
وَمُصَدِّقًا لِّمَا بَيْنَ يَدَيْهِ مِنَ التَّوْرَاةِ وَهُدًى وَمَوْعِظَةً
لِّلْمُتَّقِينَ
Waqaffayna AAala atharihimbiAAeesa ibni maryama musaddiqan lima baynayadayhi
mina attawrati waataynahual-injeela feehi hudan wanoorun wamusaddiqan limabayna
yadayhi mina attawrati wahudan wamawAAithatanlilmuttaqeen
Swahili
Na tukawafuatishia hao Isa bin Maryamu kuyahakikisha yaliyo kuwa kabla yake
katika Taurati, na tukampa Injili iliyomo ndani yake uwongofu, na nuru na inayo
sadikisha yaliyo kuwa kabla yake katika Taurati, na uwongofu na mawaidha kwa
wachamngu.
|
Ayah 5:47 الأية
وَلْيَحْكُمْ أَهْلُ الْإِنجِيلِ بِمَا أَنزَلَ اللهُ فِيهِ ۚ وَمَن لَّمْ
يَحْكُم بِمَا أَنزَلَ اللهُ فَأُولَٰئِكَ هُمُ الْفَاسِقُونَ
Walyahkum ahlu al-injeeli bimaanzala Allahu feehi waman lam yahkum bimaanzala
Allahu faola-ika humu alfasiqoon
Swahili
Na wahukumu Watu wa Injili kwa yale aliyo teremsha Mwenyezi Mungu ndani yake. Na
wasio hukumu kwa yale aliyo yateremsha Mwenyezi Mungu basi hao ndio wapotofu.
|
Ayah 5:48 الأية
وَأَنزَلْنَا إِلَيْكَ الْكِتَابَ بِالْحَقِّ مُصَدِّقًا لِّمَا بَيْنَ يَدَيْهِ
مِنَ الْكِتَابِ وَمُهَيْمِنًا عَلَيْهِ ۖ فَاحْكُم بَيْنَهُم بِمَا أَنزَلَ
اللهُ ۖ وَلَا تَتَّبِعْ أَهْوَاءَهُمْ عَمَّا جَاءَكَ مِنَ الْحَقِّ ۚ لِكُلٍّ
جَعَلْنَا مِنكُمْ شِرْعَةً وَمِنْهَاجًا ۚ وَلَوْ شَاءَ اللهُ لَجَعَلَكُمْ
أُمَّةً وَاحِدَةً وَلَٰكِن لِّيَبْلُوَكُمْ فِي مَا آتَاكُمْ ۖ فَاسْتَبِقُوا
الْخَيْرَاتِ ۚ إِلَى اللهِ مَرْجِعُكُمْ جَمِيعًا فَيُنَبِّئُكُم بِمَا كُنتُمْ
فِيهِ تَخْتَلِفُونَ
Waanzalna ilayka alkitaba bilhaqqimusaddiqan lima bayna yadayhi mina
alkitabiwamuhayminan AAalayhi fahkum baynahum bimaanzala Allahu wala tattabiAA
ahwaahum AAammajaaka mina alhaqqi likullin jaAAalna minkumshirAAatan waminhajan
walaw shaa AllahulajaAAalakum ommatan wahidatan walakin liyabluwakumfeema atakum
fastabiqoo alkhayratiila Allahi marjiAAukum jameeAAan fayunabbi-okum bimakuntum
feehi takhtalifoon
Swahili
Na tumekuteremshia wewe, kwa haki, Kitabu hichi kinacho sadikisha yaliyo kuwa
kabla yake katika Vitabu na kuyalinda. Basi hukumu baina yao kwa aliyo
yateremsha Mwenyezi Mungu, wala usifuate matamanio yao ukaacha Haki iliyo kujia.
Kila mmoja katika nyinyi tumemwekea sharia yake na njia yake. Na lau kuwa
Mwenyezi Mungu angeli taka ange kufanyeni nyote umma mmoja, lakini ni
kukujaribuni kwa aliyo kupeni. Basi shindaneni kwa mambo ya kheri. Kwa Mwenyezi
Mungu ndio marejeo yenu nyote, na atakuja kuwaambieni yale mliyo kuwa
mkikhitalifiana.
|
Ayah 5:49 الأية
وَأَنِ احْكُم بَيْنَهُم بِمَا أَنزَلَ اللهُ وَلَا تَتَّبِعْ أَهْوَاءَهُمْ
وَاحْذَرْهُمْ أَن يَفْتِنُوكَ عَن بَعْضِ مَا أَنزَلَ اللهُ إِلَيْكَ ۖ فَإِن
تَوَلَّوْا فَاعْلَمْ أَنَّمَا يُرِيدُ اللهُ أَن يُصِيبَهُم بِبَعْضِ
ذُنُوبِهِمْ ۗ وَإِنَّ كَثِيرًا مِّنَ النَّاسِ لَفَاسِقُونَ
Waani ohkum baynahum bimaanzala Allahu wala tattabiAA ahwaahum wahtharhuman
yaftinooka AAan baAAdi ma anzala Allahuilayka fa-in tawallaw faAAlam annama
yureedu Allahuan yuseebahum bibaAAdi thunoobihim wa-innakatheeran mina annasi
lafasiqoon
Swahili
Na wahukumu baina yao kwa aliyo yateremsha Mwenyezi Mungu, wala usifuate
matamanio yao. Nawe tahadhari nao wasije kukufitini ukaacha baadhi ya aliyo
kuteremshia Mwenyezi Mungu. Na wakigeuka, basi jua kwamba hakika Mwenyezi Mungu
anataka kuwasibu kwa baadhi ya dhambi zao. Na hakika wengi wa watu ni wapotofu.
|
Ayah 5:50 الأية
أَفَحُكْمَ الْجَاهِلِيَّةِ يَبْغُونَ ۚ وَمَنْ أَحْسَنُ مِنَ اللهِ حُكْمًا
لِّقَوْمٍ يُوقِنُونَ
Afahukma aljahiliyyatiyabghoona waman ahsanu mina Allahu hukmanliqawmin
yooqinoon
Swahili
Je, wao wanataka hukumu za Kijahiliya? Na nani aliye mwema zaidi katika kuhukumu
kuliko Mwenyezi Mungu kwa watu wenye yakini?
|
Ayah 5:51 الأية
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تَتَّخِذُوا الْيَهُودَ وَالنَّصَارَىٰ
أَوْلِيَاءَ ۘ بَعْضُهُمْ أَوْلِيَاءُ بَعْضٍ ۚ وَمَن يَتَوَلَّهُم مِّنكُمْ
فَإِنَّهُ مِنْهُمْ ۗ إِنَّ اللهَ لَا يَهْدِي الْقَوْمَ الظَّالِمِينَ
Ya ayyuha allatheena amanoola tattakhithoo alyahooda wannasaraawliyaa baAAduhum
awliyao baAAdinwaman yatawallahum minkum fa-innahu minhum inna Allaha layahdee
alqawma aththalimeen
Swahili
Enyi mlio amini! Msiwafanye Mayahudi na Wakristo kuwa ni marafiki. Wao ni
marafiki wao kwa wao. Na miongoni mwenu mwenye kufanya urafiki nao, basi huyo ni
katika wao. Hakika Mwenyezi Mungu hawaongoi watu wenye kudhulumu.
|
Ayah 5:52 الأية
فَتَرَى الَّذِينَ فِي قُلُوبِهِم مَّرَضٌ يُسَارِعُونَ فِيهِمْ يَقُولُونَ
نَخْشَىٰ أَن تُصِيبَنَا دَائِرَةٌ ۚ فَعَسَى اللهُ أَن يَأْتِيَ بِالْفَتْحِ
أَوْ أَمْرٍ مِّنْ عِندِهِ فَيُصْبِحُوا عَلَىٰ مَا أَسَرُّوا فِي أَنفُسِهِمْ
نَادِمِينَ
Fatara allatheena feequloobihim maradun yusariAAoona feehim yaqooloonanakhsha an
tuseebana da-iratun faAAasaAllahu an ya/tiya bilfathi aw amrin minAAindihi
fayusbihoo AAala ma asarroofee anfusihim nadimeen
Swahili
Utawaona wale wenye maradhi nyoyoni mwao wanakimbilia kwao wakisema: Tunakhofu
yasitusibu mabadiliko. Huenda Mwenyezi Mungu akaleta ushindi au jambo jingine
litokalo kwake wakawa wenye kujuta kwa waliyo yaficha katika nafsi zao.
|
Ayah 5:53 الأية
وَيَقُولُ الَّذِينَ آمَنُوا أَهَٰؤُلَاءِ الَّذِينَ أَقْسَمُوا بِاللهِ جَهْدَ
أَيْمَانِهِمْ ۙ إِنَّهُمْ لَمَعَكُمْ ۚ حَبِطَتْ أَعْمَالُهُمْ فَأَصْبَحُوا
خَاسِرِينَ
Wayaqoolu allatheena amanoo ahaola-iallatheena aqsamoo billahi jahda
aymanihiminnahum lamaAAakum habitat aAAmaluhum faasbahookhasireen
Swahili
Na walio amini watasema: Hivyo hawa ndio wale walio apa ukomo wa viapo vyao kuwa
wao wa pamoja nanyi? Vitendo vyao vitapotea bure, na wataamkia kuwa wenye
kukhasirika.
|
Ayah 5:54 الأية
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا مَن يَرْتَدَّ مِنكُمْ عَن دِينِهِ فَسَوْفَ
يَأْتِي اللهُ بِقَوْمٍ يُحِبُّهُمْ وَيُحِبُّونَهُ أَذِلَّةٍ عَلَى
الْمُؤْمِنِينَ أَعِزَّةٍ عَلَى الْكَافِرِينَ يُجَاهِدُونَ فِي سَبِيلِ اللهِ
وَلَا يَخَافُونَ لَوْمَةَ لَائِمٍ ۚ ذَٰلِكَ فَضْلُ اللهِ يُؤْتِيهِ مَن يَشَاءُ
ۚ وَاللهُ وَاسِعٌ عَلِيمٌ
Ya ayyuha allatheena amanooman yartadda minkum AAan deenihi fasawfa ya/tee
Allahubiqawmin yuhibbuhum wayuhibboonahu athillatinAAala almu/mineena aAAizzatin
AAala alkafireenayujahidoona fee sabeeli Allahi wala yakhafoonalawmata la-imin
thalika fadlu Allahiyu/teehi man yashao wallahu wasiAAunAAaleem
Swahili
Enyi mlio amini! Atakaye iacha miongoni mwenu Dini yake, basi Mwenyezi Mungu
atakuja leta watu anao wapenda nao wanampenda, wanyenyekevu kwa Waumini na wenye
nguvu juu ya makafiri, wanapigania Jihadi katika Njia ya Mwenyezi Mungu, wala
hawaogopi lawama ya anaye laumu. Hiyo ndiyo fadhila ya Mwenyezi Mungu, humpa
amtakaye. Na Mwenyezi Mungu ni Mkunjufu na Mwenye kujua.
|
Ayah 5:55 الأية
إِنَّمَا وَلِيُّكُمُ اللهُ وَرَسُولُهُ وَالَّذِينَ آمَنُوا الَّذِينَ
يُقِيمُونَ الصَّلَاةَ وَيُؤْتُونَ الزَّكَاةَ وَهُمْ رَاكِعُونَ
Innama waliyyukumu Allahuwarasooluhu wallatheena amanoo allatheenayuqeemoona
assalata wayu/toona azzakatawahum rakiAAoon
Swahili
Hakika rafiki yenu mlinzi ni Mwenyezi Mungu na Mtume wake na walio amini, ambao
hushika Sala na hutoa Zaka nao wananyenyekea.
|
Ayah 5:56 الأية
وَمَن يَتَوَلَّ اللهَ وَرَسُولَهُ وَالَّذِينَ آمَنُوا فَإِنَّ حِزْبَ اللهِ
هُمُ الْغَالِبُونَ
Waman yatawalla Allaha warasoolahu wallatheenaamanoo fa-inna hizba Allahi humu
alghaliboon
Swahili
Na atakaye fanya urafiki na Mwenyezi Mungu na Mtume wake na walio amini, basi
hakika kundi la Mwenyezi Mungu ndilo lenye kushinda.
|
Ayah 5:57 الأية
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تَتَّخِذُوا الَّذِينَ اتَّخَذُوا دِينَكُمْ
هُزُوًا وَلَعِبًا مِّنَ الَّذِينَ أُوتُوا الْكِتَابَ مِن قَبْلِكُمْ
وَالْكُفَّارَ أَوْلِيَاءَ ۚ وَاتَّقُوا اللهَ إِن كُنتُم مُّؤْمِنِينَ
Ya ayyuha allatheena amanoola tattakhithoo allatheena ittakhathoodeenakum
huzuwan walaAAiban mina allatheena ootoo alkitabamin qablikum walkuffara awliyaa
wattaqooAllaha in kuntum mu/mineen
Swahili
Enyi mlio amini! Msiwafanye marafiki wale walio ifanyia kejeli na mchezo Dini
yenu miongoni mwa walio pewa Kitabu kabla yenu, na makafiri wengine. Na mcheni
Mwenyezi Mungu kama nyinyi ni wenye kuamini.
|
Ayah 5:58 الأية
وَإِذَا نَادَيْتُمْ إِلَى الصَّلَاةِ اتَّخَذُوهَا هُزُوًا وَلَعِبًا ۚ ذَٰلِكَ
بِأَنَّهُمْ قَوْمٌ لَّا يَعْقِلُونَ
Wa-itha nadaytum ila assalatiittakhathooha huzuwan walaAAiban thalikabi-annahum
qawmun la yaAAqiloon
Swahili
Na mnapo adhinia Sala wao wanaichukulia maskhara na mchezo. Hayo ni kwa sababu
wao ni watu wasio na akili.
|
Ayah 5:59 الأية
قُلْ يَا أَهْلَ الْكِتَابِ هَلْ تَنقِمُونَ مِنَّا إِلَّا أَنْ آمَنَّا بِاللهِ
وَمَا أُنزِلَ إِلَيْنَا وَمَا أُنزِلَ مِن قَبْلُ وَأَنَّ أَكْثَرَكُمْ فَاسِقُونَ
Qul ya ahla alkitabi haltanqimoona minna illa an amanna billahiwama onzila
ilayna wama onzila min qabluwaanna aktharakum fasiqoon
Swahili
Sema: Enyi Watu wa Kitabu! Hivyo mnatuchukia kwa kuwa tumemuamini Mwenyezi Mungu
na tuliyo teremshiwa na yaliyo teremshwa kabla, na kwa kuwa wengi katika nyinyi
ni wapotofu?
|
Ayah 5:60 الأية
قُلْ هَلْ أُنَبِّئُكُم بِشَرٍّ مِّن ذَٰلِكَ مَثُوبَةً عِندَ اللهِ ۚ مَن
لَّعَنَهُ اللهُ وَغَضِبَ عَلَيْهِ وَجَعَلَ مِنْهُمُ الْقِرَدَةَ
وَالْخَنَازِيرَ وَعَبَدَ الطَّاغُوتَ ۚ أُولَٰئِكَ شَرٌّ مَّكَانًا وَأَضَلُّ عَن
سَوَاءِ السَّبِيلِ
Qul hal onabbi-okum bisharrin min thalikamathoobatan AAinda Allahi man laAAanahu
Allahuwaghadiba AAalayhi wajaAAala minhumu alqiradata walkhanazeerawaAAabada
attaghooti ola-ika sharrun makananwaadallu AAan sawa-i assabeel
Swahili
Sema: Je! Nikwambieni yule ambaye ni mwenye malipo mabaya zaidi kuliko hayo
mbele ya Mwenyezi Mungu? Ni yule ambaye Mwenyezi Mungu amemlaani na
amemkasirikia, na amewafanya miongoni mwao manyani na nguruwe, na wakamuabudu
Shet'ani. Hao ndio wenye mahali pabaya na wamepotea zaidi njia iliyo sawa.
|
Ayah 5:61 الأية
وَإِذَا جَاءُوكُمْ قَالُوا آمَنَّا وَقَد دَّخَلُوا بِالْكُفْرِ وَهُمْ قَدْ
خَرَجُوا بِهِ ۚ وَاللهُ أَعْلَمُ بِمَا كَانُوا يَكْتُمُونَ
Wa-itha jaookum qaloo amannawaqad dakhaloo bilkufri wahum qad kharajoo bihi
wallahuaAAlamu bima kanoo yaktumoon
Swahili
Na wanapo kujieni husema: Tumeamini. Lakini hakika wao wameingia na ukafiri wao,
na wametoka nao pia. Na Mwenyezi Mungu ni Mjuzi kabisa wa yote wanayo yaficha.
|
Ayah 5:62 الأية
وَتَرَىٰ كَثِيرًا مِّنْهُمْ يُسَارِعُونَ فِي الْإِثْمِ وَالْعُدْوَانِ
وَأَكْلِهِمُ السُّحْتَ ۚ لَبِئْسَ مَا كَانُوا يَعْمَلُونَ
Watara katheeran minhum yusariAAoonafee al-ithmi walAAudwani waaklihimu
assuhtalabi/sa ma kanoo yaAAmaloon
Swahili
Na utawaona wengi katika wao wanakimbilia kwenye dhambi, na uadui, na ulaji wao
vya haramu. Ni maovu mno hayo wayatendayo!
|
Ayah 5:63 الأية
لَوْلَا يَنْهَاهُمُ الرَّبَّانِيُّونَ وَالْأَحْبَارُ عَن قَوْلِهِمُ الْإِثْمَ
وَأَكْلِهِمُ السُّحْتَ ۚ لَبِئْسَ مَا كَانُوا يَصْنَعُونَ
Lawla yanhahumu arrabbaniyyoonawal-ahbaru AAan qawlihimu al-ithmawaaklihimu
assuhta labi/sa ma kanooyasnaAAoon
Swahili
Mbona hao wanazuoni na makohani wao hawawakatazi maneno yao ya dhambi, na ulaji
wao vya haramu? Ni maovu mno hayo wayafanyayo!
|
Ayah 5:64 الأية
وَقَالَتِ الْيَهُودُ يَدُ اللهِ مَغْلُولَةٌ ۚ غُلَّتْ أَيْدِيهِمْ وَلُعِنُوا
بِمَا قَالُوا ۘ بَلْ يَدَاهُ مَبْسُوطَتَانِ يُنفِقُ كَيْفَ يَشَاءُ ۚ
وَلَيَزِيدَنَّ كَثِيرًا مِّنْهُم مَّا أُنزِلَ إِلَيْكَ مِن رَّبِّكَ طُغْيَانًا
وَكُفْرًا ۚ وَأَلْقَيْنَا بَيْنَهُمُ الْعَدَاوَةَ وَالْبَغْضَاءَ إِلَىٰ يَوْمِ
الْقِيَامَةِ ۚ كُلَّمَا أَوْقَدُوا نَارًا لِّلْحَرْبِ أَطْفَأَهَا اللهُ ۚ
وَيَسْعَوْنَ فِي الْأَرْضِ فَسَادًا ۚ وَاللهُ لَا يُحِبُّ الْمُفْسِدِينَ
Waqalati alyahoodu yadu Allahimaghloolatun ghullat aydeehim waluAAinoo bima
qaloobal yadahu mabsootatani yunfiqu kayfa yashaowalayazeedanna katheeran minhum
ma onzila ilayka minrabbika tughyanan wakufran waalqaynabaynahumu alAAadawata
walbaghdaa ilayawmi alqiyamati kullama awqadoo naran lilharbiatfaaha Allahu
wayasAAawna fee al-ardifasadan wallahu la yuhibbualmufsideen
Swahili
Na Mayahudi walisema: Mkono wa Mwenyezi Mungu umefumba. Mikono yao ndiyo iliyo
fumba, na wamelaaniwa kwa sababu ya waliyo yasema. Bali mikono yake iwazi. Hutoa
apendavyo. Kwa yakini yaliyo teremshwa kwako kutoka kwa Mola wako Mlezi
yatawazidisha wengi katika wao uasi na kufuru. Na Sisi tumewatilia uadui na
chuki baina yao mpaka Siku ya Kiyama. Kila mara wanapo washa moto wa vita,
Mwenyezi Mungu anauzima. Na wanajitahidi kuleta uharibifu katika ardhi. Na
Mwenyezi Mungu hawapendi waharibifu.
|
Ayah 5:65 الأية
وَلَوْ أَنَّ أَهْلَ الْكِتَابِ آمَنُوا وَاتَّقَوْا لَكَفَّرْنَا عَنْهُمْ
سَيِّئَاتِهِمْ وَلَأَدْخَلْنَاهُمْ جَنَّاتِ النَّعِيمِ
Walaw anna ahla alkitabi amanoowattaqaw lakaffarna AAanhum
sayyi-atihimwalaadkhalnahum jannati annaAAeem
Swahili
Na lau kuwa Watu wa Kitabu wangeli amini na wakachamngu hapana shaka tungeli
wafutia makosa yao, na tungeli waingiza katika Bustani zenye neema.
|
Ayah 5:66 الأية
وَلَوْ أَنَّهُمْ أَقَامُوا التَّوْرَاةَ وَالْإِنجِيلَ وَمَا أُنزِلَ إِلَيْهِم
مِّن رَّبِّهِمْ لَأَكَلُوا مِن فَوْقِهِمْ وَمِن تَحْتِ أَرْجُلِهِم ۚ مِّنْهُمْ
أُمَّةٌ مُّقْتَصِدَةٌ ۖ وَكَثِيرٌ مِّنْهُمْ سَاءَ مَا يَعْمَلُونَ
Walaw annahum aqamoo attawratawal-injeela wama onzila ilayhim min
rabbihimlaakaloo min fawqihim wamin tahti arjulihim minhum ommatunmuqtasidatun
wakatheerun minhum saa mayaAAmaloon
Swahili
Na lau kuwa wangeli ishika Taurati na Injili na yote waliyo teremshiwa kutokana
na Mola wao Mlezi, basi hapana shaka wangeli kula vya juu yao na vya chini ya
miguu yao. Wapo watu miongoni mwao walio sawa, lakini wengi wao wanayo yafanya
ni mabaya mno.
|
Ayah 5:67 الأية
يَا أَيُّهَا الرَّسُولُ بَلِّغْ مَا أُنزِلَ إِلَيْكَ مِن رَّبِّكَ ۖ وَإِن لَّمْ
تَفْعَلْ فَمَا بَلَّغْتَ رِسَالَتَهُ ۚ وَاللهُ يَعْصِمُكَ مِنَ النَّاسِ ۗ
إِنَّ اللهَ لَا يَهْدِي الْقَوْمَ الْكَافِرِينَ
Ya ayyuha arrasooluballigh ma onzila ilayka min rabbika wa-in lam tafAAal
famaballaghta risalatahu wallahu yaAAsimukamina annasi inna Allaha la
yahdeealqawma alkafireen
Swahili
Ewe Mtume! Fikisha uliyo teremshiwa kutoka kwa Mola wako Mlezi. Na ikiwa
hukufanya hayo basi hukufikisha ujumbe wake. Na Mwenyezi Mungu atakulinda na
watu. Hakika Mwenyezi Mungu hawaongoi watu makafiri.
|
Ayah 5:68 الأية
قُلْ يَا أَهْلَ الْكِتَابِ لَسْتُمْ عَلَىٰ شَيْءٍ حَتَّىٰ تُقِيمُوا التَّوْرَاةَ
وَالْإِنجِيلَ وَمَا أُنزِلَ إِلَيْكُم مِّن رَّبِّكُمْ ۗ وَلَيَزِيدَنَّ كَثِيرًا
مِّنْهُم مَّا أُنزِلَ إِلَيْكَ مِن رَّبِّكَ طُغْيَانًا وَكُفْرًا ۖ فَلَا تَأْسَ
عَلَى الْقَوْمِ الْكَافِرِينَ
Qul ya ahla alkitabi lastumAAala shay-in hatta tuqeemoo attawratawal-injeela
wama onzila ilaykum min rabbikumwalayazeedanna katheeran minhum ma onzila ilayka
minrabbika tughyanan wakufran fala ta/sa AAalaalqawmi alkafireen
Swahili
Sema: Enyi Watu wa Kitabu! Hamna lenu jambo mpaka muishike Taurati na Injili na
yote mlio teremshiwa kutokana na Mola wenu Mlezi. Na hakika ulio teremshiwa wewe
kutokana na Mola wako Mlezi yatawazidishia wengi katika wao uasi na ukafiri.
Basi usiwasikitikie watu makafiri.
|
Ayah 5:69 الأية
إِنَّ الَّذِينَ آمَنُوا وَالَّذِينَ هَادُوا وَالصَّابِئُونَ وَالنَّصَارَىٰ مَنْ
آمَنَ بِاللهِ وَالْيَوْمِ الْآخِرِ وَعَمِلَ صَالِحًا فَلَا خَوْفٌ عَلَيْهِمْ
وَلَا هُمْ يَحْزَنُونَ
Inna allatheena amanoo wallatheenahadoo wassabi-oona wannasaraman amana billahi
walyawmi al-akhiriwaAAamila salihan fala khawfun AAalayhim walahum yahzanoon
Swahili
Hakika walio amini, na Mayahudi na Masabii na Wakristo, walio muamini Mwenyezi
Mungu, na Siku ya mwisho, na wakatenda mema, basi hawatakuwa na khofu wala
hawatahuzunika.
|
Ayah 5:70 الأية
لَقَدْ أَخَذْنَا مِيثَاقَ بَنِي إِسْرَائِيلَ وَأَرْسَلْنَا إِلَيْهِمْ رُسُلًا ۖ
كُلَّمَا جَاءَهُمْ رَسُولٌ بِمَا لَا تَهْوَىٰ أَنفُسُهُمْ فَرِيقًا كَذَّبُوا
وَفَرِيقًا يَقْتُلُونَ
Laqad akhathna meethaqabanee isra-eela waarsalna ilayhim rusulan kullamajaahum
rasoolun bima la tahwaanfusuhum fareeqan kaththaboo wafareeqan yaqtuloon
Swahili
Tulifanya agano na Wana wa Israili, na tukawatumia Mitume. Kila alipo wajia
Mtume kwa wasio yapenda nafsi zao wengine waliwakanusha na wengine wakawauwa.
|
Ayah 5:71 الأية
وَحَسِبُوا أَلَّا تَكُونَ فِتْنَةٌ فَعَمُوا وَصَمُّوا ثُمَّ تَابَ اللهُ
عَلَيْهِمْ ثُمَّ عَمُوا وَصَمُّوا كَثِيرٌ مِّنْهُمْ ۚ وَاللهُ بَصِيرٌ بِمَا
يَعْمَلُونَ
Wahasiboo alla takoonafitnatun faAAamoo wasammoo thumma taba AllahuAAalayhim
thumma AAamoo wasammoo katheerun minhum wallahubaseerun bima yaAAmaloon
Swahili
Na wakadhani kuwa hapatakuwa majaribio; basi wakawa vipofu na viziwi. Kisha
Mwenyezi Mungu akawapokelea toba zao. Kisha tena wengi katika wao wakawa vipofu
na viziwi. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kuyaona hayo wayatendayo.
|
Ayah 5:72 الأية
لَقَدْ كَفَرَ الَّذِينَ قَالُوا إِنَّ اللهَ هُوَ الْمَسِيحُ ابْنُ مَرْيَمَ ۖ
وَقَالَ الْمَسِيحُ يَا بَنِي إِسْرَائِيلَ اعْبُدُوا اللهَ رَبِّي وَرَبَّكُمْ ۖ
إِنَّهُ مَن يُشْرِكْ بِاللهِ فَقَدْ حَرَّمَ اللهُ عَلَيْهِ الْجَنَّةَ
وَمَأْوَاهُ النَّارُ ۖ وَمَا لِلظَّالِمِينَ مِنْ أَنصَارٍ
Laqad kafara allatheena qalooinna Allaha huwa almaseehu ibnu maryama
waqalaalmaseehu ya banee isra-eela oAAbudoo Allaharabbee warabbakum innahu man
yushrik billahi faqadharrama Allahu AAalayhi aljannata wama/wahuannaru wama
liththalimeenamin ansar
Swahili
Hakika wamekufuru walio sema: Mwenyezi Mungu ni Masihi mwana wa Maryamu! Na hali
Masihi mwenyewe alisema: Enyi Wana wa Israili! Muabuduni Mwenyezi Mungu, Mola
wangu Mlezi na Mola wenu Mlezi. Kwani anaye mshirikisha Mwenyezi Mungu, hakika
Mwenyezi Mungu atamharimishia Pepo, na mahala pake ni Motoni. Na walio dhulumu
hawatakuwa na wa kuwanusuru.
|
Ayah 5:73 الأية
لَّقَدْ كَفَرَ الَّذِينَ قَالُوا إِنَّ اللهَ ثَالِثُ ثَلَاثَةٍ ۘ وَمَا مِنْ
إِلَٰهٍ إِلَّا إِلَٰهٌ وَاحِدٌ ۚ وَإِن لَّمْ يَنتَهُوا عَمَّا يَقُولُونَ
لَيَمَسَّنَّ الَّذِينَ كَفَرُوا مِنْهُمْ عَذَابٌ أَلِيمٌ
Laqad kafara allatheena qalooinna Allaha thalithu thalathatin wamamin ilahin
illa ilahun wahidun wa-inlam yantahoo AAamma yaqooloona layamassanna
allatheenakafaroo minhum AAathabun aleem
Swahili
Kwa hakika wamekufuru walio sema: Mwenyezi Mungu ni wa tatu wa Utatu. Hali
hakuna mungu ila Mungu Mmoja. Na ikiwa hawaachi hayo wanayo yasema, kwa yakini
itawakamata adhabu chungu wale wanao kufuru.
|
Ayah 5:74 الأية
أَفَلَا يَتُوبُونَ إِلَى اللهِ وَيَسْتَغْفِرُونَهُ ۚ وَاللهُ غَفُورٌ
رَّحِيمٌ
Afala yatooboona ila Allahiwayastaghfiroonahu wallahu ghafoorun raheem
Swahili
Je! Hawatubu kwa Mwenyezi Mungu na wakamwomba msamaha? Na Mwenyezi Mungu ni
Mwenye maghfira na Mwenye kurehemu.
|
Ayah 5:75 الأية
مَّا الْمَسِيحُ ابْنُ مَرْيَمَ إِلَّا رَسُولٌ قَدْ خَلَتْ مِن قَبْلِهِ الرُّسُلُ
وَأُمُّهُ صِدِّيقَةٌ ۖ كَانَا يَأْكُلَانِ الطَّعَامَ ۗ انظُرْ كَيْفَ نُبَيِّنُ
لَهُمُ الْآيَاتِ ثُمَّ انظُرْ أَنَّىٰ يُؤْفَكُونَ
Ma almaseehu ibnu maryama illarasoolun qad khalat min qablihi arrusulu waommuhu
siddeeqatunkana ya/kulani attaAAamaonthur kayfa nubayyinu lahumu al-ayatithumma
onthur anna yu/fakoon
Swahili
Masihi mwana wa Maryam si chochote ila ni Mtume. Wamekwisha pita Mitume kabla
yake. Na mama yake ni mwanamke mkweli. Wote wawili walikuwa wakila chakula.
Angalia jinsi tunavyo wabainishia Aya, kisha angalia vipi wanavyo geuzwa.
|
Ayah 5:76 الأية
قُلْ أَتَعْبُدُونَ مِن دُونِ اللهِ مَا لَا يَمْلِكُ لَكُمْ ضَرًّا وَلَا
نَفْعًا ۚ وَاللهُ هُوَ السَّمِيعُ الْعَلِيمُ
Qul ataAAbudoona min dooni Allahi mala yamliku lakum darran wala nafAAan
wallahuhuwa assameeAAu alAAaleem
Swahili
Sema: Je! Mnawaabudu, badala ya Mwenyezi Mungu, wale ambao hawawezi kukudhuruni
wala kukufaeni? Na Mwenyezi Mungu ndiye Mwenye kusikia, Mwenye kujua.
|
Ayah 5:77 الأية
قُلْ يَا أَهْلَ الْكِتَابِ لَا تَغْلُوا فِي دِينِكُمْ غَيْرَ الْحَقِّ وَلَا
تَتَّبِعُوا أَهْوَاءَ قَوْمٍ قَدْ ضَلُّوا مِن قَبْلُ وَأَضَلُّوا كَثِيرًا
وَضَلُّوا عَن سَوَاءِ السَّبِيلِ
Qul ya ahla alkitabi lataghloo fee deenikum ghayra alhaqqi wala tattabiAAooahwaa
qawmin qad dalloo min qablu waadallookatheeran wadalloo AAan sawa-i assabeel
Swahili
Sema: Enyi Watu wa Kitabu! Msipite kiasi katika dini yenu bila ya haki. Wala
msifuate matamanio ya watu walio kwisha potea tangu zamani, na wakawapoteza
wengi, na wenyewe wakapotea njia iliyo sawa.
|
Ayah 5:78 الأية
لُعِنَ الَّذِينَ كَفَرُوا مِن بَنِي إِسْرَائِيلَ عَلَىٰ لِسَانِ دَاوُودَ
وَعِيسَى ابْنِ مَرْيَمَ ۚ ذَٰلِكَ بِمَا عَصَوا وَّكَانُوا يَعْتَدُونَ
LuAAina allatheena kafaroo min baneeisra-eela AAala lisani dawoodawaAAeesa ibni
maryama thalika bima AAasawwakanoo yaAAtadoon
Swahili
Walilaaniwa walio kufuru miongoni mwa Wana wa Israili kwa ulimi wa Daud na wa
Isa mwana wa Maryamu. Hayo ni kwa sababu waliasi na wakawa wanapindukia mipaka.
|
Ayah 5:79 الأية
كَانُوا لَا يَتَنَاهَوْنَ عَن مُّنكَرٍ فَعَلُوهُ ۚ لَبِئْسَ مَا كَانُوا
يَفْعَلُونَ
Kanoo la yatanahawnaAAan munkarin faAAaloohu labi/sa ma kanooyafAAaloon
Swahili
Walikuwa hawakatazani maovu waliyo kuwa wakiyafanya. Hakika ni maovu yalioje
mambo waliyo kuwa wakiyafanya!
|
Ayah 5:80 الأية
تَرَىٰ كَثِيرًا مِّنْهُمْ يَتَوَلَّوْنَ الَّذِينَ كَفَرُوا ۚ لَبِئْسَ مَا
قَدَّمَتْ لَهُمْ أَنفُسُهُمْ أَن سَخِطَ اللهُ عَلَيْهِمْ وَفِي الْعَذَابِ هُمْ
خَالِدُونَ
Tara katheeran minhum yatawallawnaallatheena kafaroo labi/sa ma qaddamat
lahumanfusuhum an sakhita Allahu AAalayhim wafee alAAathabihum khalidoon
Swahili
Utawaona wengi wao wanafanya urafiki na walio kufuru. Hakika ni maovu yaliyo
tangulizwa na nafsi zao hata Mwenyezi Mungu amewakasirikia, nao watadumu katika
adhabu.
|
Ayah 5:81 الأية
وَلَوْ كَانُوا يُؤْمِنُونَ بِاللهِ وَالنَّبِيِّ وَمَا أُنزِلَ إِلَيْهِ مَا
اتَّخَذُوهُمْ أَوْلِيَاءَ وَلَٰكِنَّ كَثِيرًا مِّنْهُمْ فَاسِقُونَ
Walaw kanoo yu/minoona billahiwannabiyyi wama onzila ilayhi ma
ittakhathoohumawliyaa walakinna katheeran minhum fasiqoon
Swahili
Na lau wangeli kuwa wanamuamini Mwenyezi Mungu, na huyu Nabii, na yaliyo
teremshwa kwake, wasingeli wafanya hao marafiki. Lakini wengi katika wao ni
wapotofu.
|
Ayah 5:82 الأية
لَتَجِدَنَّ أَشَدَّ النَّاسِ عَدَاوَةً لِّلَّذِينَ آمَنُوا الْيَهُودَ
وَالَّذِينَ أَشْرَكُوا ۖ وَلَتَجِدَنَّ أَقْرَبَهُم مَّوَدَّةً لِّلَّذِينَ
آمَنُوا الَّذِينَ قَالُوا إِنَّا نَصَارَىٰ ۚ ذَٰلِكَ بِأَنَّ مِنْهُمْ
قِسِّيسِينَ وَرُهْبَانًا وَأَنَّهُمْ لَا يَسْتَكْبِرُونَ
Latajidanna ashadda annasiAAadawatan lillatheena amanoo alyahooda
wallatheenaashrakoo walatajidanna aqrabahum mawaddatan lillatheena
amanooallatheena qaloo inna nasara thalikabi-anna minhum qisseeseena waruhbanan
waannahum layastakbiroon
Swahili
Hakika utawakuta walio shadidi kuliko watu wote katika uadui kwa walio amini ni
Mayahudi na washirikina. Na utawakuta walio karibu mno kwa mapenzi ni wale wanao
sema: Sisi ni Manasara. Hayo ni kwa sababu wapo miongoni mwao makasisi na
wamonaki, na kwa sababu wao hawafanyi kiburi.
|
Ayah 5:83 الأية
وَإِذَا سَمِعُوا مَا أُنزِلَ إِلَى الرَّسُولِ تَرَىٰ أَعْيُنَهُمْ تَفِيضُ مِنَ
الدَّمْعِ مِمَّا عَرَفُوا مِنَ الْحَقِّ ۖ يَقُولُونَ رَبَّنَا آمَنَّا
فَاكْتُبْنَا مَعَ الشَّاهِدِينَ
Wa-itha samiAAoo ma onzila ilaarrasooli tara aAAyunahum tafeedu mina
addamAAimimma AAarafoo mina alhaqqi yaqooloona rabbanaamanna faktubna maAAa
ashshahideen
Swahili
NA WANAPO SIKIA yaliyo teremshwa kwa Mtume utaona macho yao yanachururika
machozi kwa sababu ya Haki waliyo itambua. Wanasema: Mola wetu Mlezi! Tumeamini.
Basi tuandike pamoja na wanao shuhudia.
|
Ayah 5:84 الأية
وَمَا لَنَا لَا نُؤْمِنُ بِاللهِ وَمَا جَاءَنَا مِنَ الْحَقِّ وَنَطْمَعُ أَن
يُدْخِلَنَا رَبُّنَا مَعَ الْقَوْمِ الصَّالِحِينَ
Wama lana la nu/minu billahiwama jaana mina alhaqqi wanatmaAAuan yudkhilana
rabbuna maAAa alqawmi assaliheen
Swahili
Na kwa nini tusimuamini Mwenyezi Mungu na Haki iliyo tujia, na hali tunatumai
Mola wetu Mlezi atuingize pamoja na watu wema?
|
Ayah 5:85 الأية
فَأَثَابَهُمُ اللهُ بِمَا قَالُوا جَنَّاتٍ تَجْرِي مِن تَحْتِهَا الْأَنْهَارُ
خَالِدِينَ فِيهَا ۚ وَذَٰلِكَ جَزَاءُ الْمُحْسِنِينَ
Faathabahumu Allahu bimaqaloo jannatin tajree min tahtihaal-anharu khalideena
feeha wathalikajazao almuhsineen
Swahili
Basi Mwenyezi Mungu atawalipa, kwa yale waliyo yasema, Bustani zipitazo mito
katika yake; humo watadumu. Na haya ndiyo malipo ya wafanyao wema.
|
Ayah 5:86 الأية
وَالَّذِينَ كَفَرُوا وَكَذَّبُوا بِآيَاتِنَا أُولَٰئِكَ أَصْحَابُ الْجَحِيمِ
Wallatheena kafaroo wakaththaboobi-ayatina ola-ika as-habualjaheem
Swahili
Na wale walio kufuru na wakazikanusha Ishara zetu, hao ndio watu wa Motoni.
|
Ayah 5:87 الأية
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تُحَرِّمُوا طَيِّبَاتِ مَا أَحَلَّ اللهُ
لَكُمْ وَلَا تَعْتَدُوا ۚ إِنَّ اللهَ لَا يُحِبُّ الْمُعْتَدِينَ
Ya ayyuha allatheena amanoola tuharrimoo tayyibati ma ahallaAllahu lakum wala
taAAtadoo inna Allaha layuhibbu almuAAtadeen
Swahili
Enyi mlio amini! Msiharimishe vizuri alivyo kuhalalishieni Mwenyezi Mungu, wala
msikiuke mipaka. Hakika Mwenyezi Mungu hawapendi wakiukao mipaka.
|
Ayah 5:88 الأية
وَكُلُوا مِمَّا رَزَقَكُمُ اللهُ حَلَالًا طَيِّبًا ۚ وَاتَّقُوا اللهَ
الَّذِي أَنتُم بِهِ مُؤْمِنُونَ
Wakuloo mimma razaqakumu Allahuhalalan tayyiban wattaqoo Allahaallathee antum
bihi mu/minoon
Swahili
Na kuleni katika alivyo kuruzukuni Mwenyezi Mungu, halali na vizuri. Na mcheni
Mwenyezi Mungu ambaye mnamuamini.
|
Ayah 5:89 الأية
لَا يُؤَاخِذُكُمُ اللهُ بِاللَّغْوِ فِي أَيْمَانِكُمْ وَلَٰكِن يُؤَاخِذُكُم
بِمَا عَقَّدتُّمُ الْأَيْمَانَ ۖ فَكَفَّارَتُهُ إِطْعَامُ عَشَرَةِ مَسَاكِينَ
مِنْ أَوْسَطِ مَا تُطْعِمُونَ أَهْلِيكُمْ أَوْ كِسْوَتُهُمْ أَوْ تَحْرِيرُ
رَقَبَةٍ ۖ فَمَن لَّمْ يَجِدْ فَصِيَامُ ثَلَاثَةِ أَيَّامٍ ۚ ذَٰلِكَ كَفَّارَةُ
أَيْمَانِكُمْ إِذَا حَلَفْتُمْ ۚ وَاحْفَظُوا أَيْمَانَكُمْ ۚ كَذَٰلِكَ يُبَيِّنُ
اللهُ لَكُمْ آيَاتِهِ لَعَلَّكُمْ تَشْكُرُونَ
La yu-akhithukumu Allahubillaghwi fee aymanikum walakin yu-akhithukumbima
AAaqqadtumu al-aymana fakaffaratuhu itAAamuAAasharati masakeena min awsati ma
tutAAimoonaahleekum aw kiswatuhum aw tahreeru raqabatin faman lamyajid fasiyamu
thalathati ayyamin thalikakaffaratu aymanikum itha halaftum wahfathooaymanakum
kathalika yubayyinu Allahu lakum ayatihilaAAallakum tashkuroon
Swahili
Mwenyezi Mungu hatakushikeni kwa viapo vyenu vya upuuzi, lakini atakushikeni kwa
mnavyo apa kweli kweli kwa makusudio. Basi kafara yake ni kuwalisha masikini
kumi kwa chakula cha wastani mnacho walisha ahali zenu, au kuwavisha, au
kumkomboa mtumwa. Asiye pata hayo, basi afunge siku tatu. Hii ndiyo kafara ya
viapo vyenu mnapo apa. Na hifadhini yamini zenu. Namna hivyo Mwenyezi Mungu
anakubainishieni Aya zake ili mpate kushukuru.
|
Ayah 5:90 الأية
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا إِنَّمَا الْخَمْرُ وَالْمَيْسِرُ وَالْأَنصَابُ
وَالْأَزْلَامُ رِجْسٌ مِّنْ عَمَلِ الشَّيْطَانِ فَاجْتَنِبُوهُ لَعَلَّكُمْ
تُفْلِحُونَ
Ya ayyuha allatheena amanooinnama alkhamru walmaysiru wal-ansabuwal-azlamu
rijsun min AAamali ashshaytanifajtaniboohu laAAallakum tuflihoon
Swahili
Enyi mlio amini! Bila ya shaka ulevi, na kamari, na kuabudu masanamu, na kupiga
ramli, ni uchafu katika kazi ya Shet'ani. Basi jiepusheni navyo, ili mpate
kufanikiwa.
|
Ayah 5:91 الأية
إِنَّمَا يُرِيدُ الشَّيْطَانُ أَن يُوقِعَ بَيْنَكُمُ الْعَدَاوَةَ وَالْبَغْضَاءَ
فِي الْخَمْرِ وَالْمَيْسِرِ وَيَصُدَّكُمْ عَن ذِكْرِ اللهِ وَعَنِ الصَّلَاةِ ۖ
فَهَلْ أَنتُم مُّنتَهُونَ
Innama yureedu ashshaytanuan yooqiAAa baynakumu alAAadawata walbaghdaafee
alkhamri walmaysiri wayasuddakum AAan thikriAllahi waAAani assalati fahal
antummuntahoon
Swahili
Hakika Shet'ani anataka kutia kati yenu uadui na chuki kwa ulevi na kamari, na
akuzuieni kumkumbuka Mwenyezi Mungu na kusali. Basi je, mmeacha?
|
Ayah 5:92 الأية
وَأَطِيعُوا اللهَ وَأَطِيعُوا الرَّسُولَ وَاحْذَرُوا ۚ فَإِن تَوَلَّيْتُمْ
فَاعْلَمُوا أَنَّمَا عَلَىٰ رَسُولِنَا الْبَلَاغُ الْمُبِينُ
WaateeAAoo Allaha waateeAAooarrasoola wahtharoo fa-in tawallaytum
faAAlamooannama AAala rasoolina albalaghualmubeen
Swahili
Na mt'iini Mwenyezi Mungu, na mt'iini Mtume, na tahadharini. Na ikiwa mtageuka
basi jueni ya kuwa juu ya Mtume wetu ni kufikisha ujumbe tu ulio wazi.
|
Ayah 5:93 الأية
لَيْسَ عَلَى الَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ جُنَاحٌ فِيمَا طَعِمُوا
إِذَا مَا اتَّقَوا وَّآمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ ثُمَّ اتَّقَوا وَّآمَنُوا
ثُمَّ اتَّقَوا وَّأَحْسَنُوا ۗ وَاللهُ يُحِبُّ الْمُحْسِنِينَ
Laysa AAala allatheena amanoowaAAamiloo assalihati junahun feemataAAimoo itha ma
ittaqaw waamanoowaAAamiloo assalihati thumma ittaqaw waamanoothumma ittaqaw
waahsanoo wallahu yuhibbualmuhsineen
Swahili
Si dhambi juu ya walio amini na wakatenda mema kwa walivyo vila (zamani) maadamu
wakichamngu na wakiamini na wakitenda mema, kisha wakachamngu, na wakaamini,
kisha wakachamngu na wakafanya mazuri. Na Mwenyezi Mungu huwapenda wafanyao
mazuri.
|
Ayah 5:94 الأية
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَيَبْلُوَنَّكُمُ اللهُ بِشَيْءٍ مِّنَ
الصَّيْدِ تَنَالُهُ أَيْدِيكُمْ وَرِمَاحُكُمْ لِيَعْلَمَ اللهُ مَن يَخَافُهُ
بِالْغَيْبِ ۚ فَمَنِ اعْتَدَىٰ بَعْدَ ذَٰلِكَ فَلَهُ عَذَابٌ أَلِيمٌ
Ya ayyuha allatheena amanoolayabluwannakumu Allahu bishay-in mina
assayditanaluhu aydeekum warimahukum liyaAAlama Allahuman yakhafuhu bilghaybi
famani iAAtadabaAAda thalika falahu AAathabun aleem
Swahili
Enyi mlio amini! Mwenyezi Mungu atakujaribuni kidogo kwa wanyama wa kuwinda
inayo wafikia mikono yenu na mikuki yenu, ili Mwenyezi Mungu amjue nani anaye
mkhofu kwa ghaibu. Basi atakaye ruka mipaka baada ya hayo atapata adhabu kali.
|
Ayah 5:95 الأية
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تَقْتُلُوا الصَّيْدَ وَأَنتُمْ حُرُمٌ ۚ وَمَن
قَتَلَهُ مِنكُم مُّتَعَمِّدًا فَجَزَاءٌ مِّثْلُ مَا قَتَلَ مِنَ النَّعَمِ
يَحْكُمُ بِهِ ذَوَا عَدْلٍ مِّنكُمْ هَدْيًا بَالِغَ الْكَعْبَةِ أَوْ كَفَّارَةٌ
طَعَامُ مَسَاكِينَ أَوْ عَدْلُ ذَٰلِكَ صِيَامًا لِّيَذُوقَ وَبَالَ أَمْرِهِ ۗ
عَفَا اللهُ عَمَّا سَلَفَ ۚ وَمَنْ عَادَ فَيَنتَقِمُ اللهُ مِنْهُ ۗ
وَاللهُ عَزِيزٌ ذُو انتِقَامٍ
Ya ayyuha allatheena amanoola taqtuloo assayda waantum hurumunwaman qatalahu
minkum mutaAAammidan fajazaon mithlu maqatala mina annaAAami yahkumu bihi
thawaAAadlin minkum hadyan baligha alkaAAbati aw kaffaratuntaAAamu masakeena aw
AAadlu thalika siyamanliyathooqa wabala amrihi AAafa AllahuAAamma salafa waman
AAada fayantaqimu Allahuminhu wallahu AAazeezun thoo intiqam
Swahili
Enyi mlio amini! Msiue wanyama wa kuwinda nanyi mmeharimia katika Hija. Na
miongoni mwenu atakaye muuwa makusudi, basi malipo yake yatakuwa kwa kuchinja
kilicho sawa na alicho kiuwa, katika mifugo, kama wanavyo hukumu waadilifu
wawili miongoni mwenu. Mnyama huyo apelekwe kwenye Al Kaaba, au kutoa kafara kwa
kuwalisha masikini; au badala ya hayo ni kufunga, ili aonje ubaya wa jambo lake
hili. Mwenyezi Mungu amekwisha yafuta yaliyo pita; lakini atakaye fanya tena
Mwenyezi Mungu atampa adhabu. Na Mwenyezi Mungu ndiye Mwenye nguvu na Mwenye
kuadhibu.
|
Ayah 5:96 الأية
أُحِلَّ لَكُمْ صَيْدُ الْبَحْرِ وَطَعَامُهُ مَتَاعًا لَّكُمْ وَلِلسَّيَّارَةِ ۖ
وَحُرِّمَ عَلَيْكُمْ صَيْدُ الْبَرِّ مَا دُمْتُمْ حُرُمًا ۗ وَاتَّقُوا اللهَ
الَّذِي إِلَيْهِ تُحْشَرُونَ
Ohilla lakum saydu albahriwataAAamuhu mataAAan lakum walissayyaratiwahurrima
AAalaykum saydu albarri ma dumtum hurumanwattaqoo Allaha allathee ilayhi
tuhsharoon
Swahili
Nyinyi mmehalalishiwa kuvua vinyama vya baharini na kuvila, kwa faida yenu na
kwa wasafiri. Na mmeharimishiwa mawindo ya wanyama wa bara maadamu mmeharimia
Hija. Na mcheni Mwenyezi Mungu ambaye mtakusanywa kwake.
|
Ayah 5:97 الأية
جَعَلَ اللهُ الْكَعْبَةَ الْبَيْتَ الْحَرَامَ قِيَامًا لِّلنَّاسِ وَالشَّهْرَ
الْحَرَامَ وَالْهَدْيَ وَالْقَلَائِدَ ۚ ذَٰلِكَ لِتَعْلَمُوا أَنَّ اللهَ
يَعْلَمُ مَا فِي السَّمَاوَاتِ وَمَا فِي الْأَرْضِ وَأَنَّ اللهَ بِكُلِّ
شَيْءٍ عَلِيمٌ
JaAAala Allahu alkaAAbata albayta alharamaqiyaman linnasi washshahra
alharamawalhadya walqala-ida thalikalitaAAlamoo anna Allaha yaAAlamu ma fee
assamawatiwama fee al-ardi waanna Allaha bikullishay-in AAaleem
Swahili
Mwenyezi Mungu ameifanya Al Kaaba, hii Nyumba Tukufu, ni simamio la watu, na
kadhaalika Miezi Mitukufu, na wanyama wa dhabihu, na vigwe. Hayo ili mjue ya
kwamba Mwenyezi Mungu anayajua yaliyomo mbinguni na yaliyomo katika ardhi, na ya
kwamba Mwenyezi Mungu ni Mjuzi wa kila kitu.
|
Ayah 5:98 الأية
اعْلَمُوا أَنَّ اللهَ شَدِيدُ الْعِقَابِ وَأَنَّ اللهَ غَفُورٌ رَّحِيمٌ
IAAlamoo anna Allaha shadeedu alAAiqabiwaanna Allaha ghafoorun raheem
Swahili
Jueni kwamba Mwenyezi Mungu ni Mkali wa kuadhibu, na ya kwamba Mwenyezi Mungu ni
Mwenye maghfira, na Mwenye kurehemu.
|
Ayah 5:99 الأية
مَّا عَلَى الرَّسُولِ إِلَّا الْبَلَاغُ ۗ وَاللهُ يَعْلَمُ مَا تُبْدُونَ وَمَا
تَكْتُمُونَ
Ma AAala arrasooli illaalbalaghu wallahu yaAAlamu matubdoona wama taktumoon
Swahili
Haimlazimu Mtume ila kufikisha ujumbe tu. Na Mwenyezi Mungu anajua mnacho
kidhihirisha na mnacho kificha.
|
Ayah 5:100 الأية
قُل لَّا يَسْتَوِي الْخَبِيثُ وَالطَّيِّبُ وَلَوْ أَعْجَبَكَ كَثْرَةُ الْخَبِيثِ
ۚ فَاتَّقُوا اللهَ يَا أُولِي الْأَلْبَابِ لَعَلَّكُمْ تُفْلِحُونَ
Qul la yastawee alkhabeethu wattayyibuwalaw aAAjabaka kathratu alkhabeethi
fattaqoo Allahaya olee al-albabi laAAallakum tuflihoon
Swahili
Sema: Haviwi sawa viovu na vyema ujapo kupendeza wingi wa viovu. Basi mcheni
Mwenyezi Mungu, enyi wenye akili, ili mpate kufanikiwa.
|
Ayah 5:101 الأية
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تَسْأَلُوا عَنْ أَشْيَاءَ إِن تُبْدَ لَكُمْ
تَسُؤْكُمْ وَإِن تَسْأَلُوا عَنْهَا حِينَ يُنَزَّلُ الْقُرْآنُ تُبْدَ لَكُمْ
عَفَا اللهُ عَنْهَا ۗ وَاللهُ غَفُورٌ حَلِيمٌ
Ya ayyuha allatheena amanoola tas-aloo AAan ashyaa in tubda lakum tasu/kumwa-in
tas-aloo AAanha heena yunazzalu alqur-anutubda lakum AAafa Allahu AAanha
wallahughafoorun haleem
Swahili
Enyi mlio amini! Msiulize mambo ambayo mkidhihirishiwa yatakuchukizeni. Na
mkiyauliza inapo teremshwa Qur'ani mtabainishiwa. Mwenyezi Mungu amesamehe hayo.
Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye maghfira Mpole.
|
Ayah 5:102 الأية
قَدْ سَأَلَهَا قَوْمٌ مِّن قَبْلِكُمْ ثُمَّ أَصْبَحُوا بِهَا كَافِرِينَ
Qad saalaha qawmun min qablikumthumma asbahoo biha kafireen
Swahili
Waliyauliza hayo watu wa kabla yenu, kisha wakawa wenye kuyakataa.
|
Ayah 5:103 الأية
مَا جَعَلَ اللهُ مِن بَحِيرَةٍ وَلَا سَائِبَةٍ وَلَا وَصِيلَةٍ وَلَا حَامٍ ۙ
وَلَٰكِنَّ الَّذِينَ كَفَرُوا يَفْتَرُونَ عَلَى اللهِ الْكَذِبَ ۖ
وَأَكْثَرُهُمْ لَا يَعْقِلُونَ
Ma jaAAala Allahu min baheeratinwala sa-ibatin wala waseelatin walahamin
walakinna allatheena kafarooyaftaroona AAala Allahi alkathibawaaktharuhum la
yaAAqiloon
Swahili
Mwenyezi Mungu hakujaalia uharamu wowote juu ya "Bahira" wala "Saiba" wala
"Wasila" wala "Hami". Lakini walio kufuru humzulia uwongo Mwenyezi Mungu, na
wengi wao hawatumii akili.
|
Ayah 5:104 الأية
وَإِذَا قِيلَ لَهُمْ تَعَالَوْا إِلَىٰ مَا أَنزَلَ اللهُ وَإِلَى الرَّسُولِ
قَالُوا حَسْبُنَا مَا وَجَدْنَا عَلَيْهِ آبَاءَنَا ۚ أَوَلَوْ كَانَ آبَاؤُهُمْ
لَا يَعْلَمُونَ شَيْئًا وَلَا يَهْتَدُونَ
Wa-itha qeela lahum taAAalawila ma anzala Allahu wa-ila arrasooliqaloo hasbuna
ma wajadnaAAalayhi abaana awa law kana abaohumla yaAAlamoona shay-an wala
yahtadoon
Swahili
Na wanapo ambiwa: Njooni kwenye yale aliyo yateremsha Mwenyezi Mungu, na kwa
Mtume, husema: Yanatutosha tuliyo wakuta nayo baba zetu. Je, hata ikiwa baba zao
walikuwa hawajui kitu wala hawakuongoka?
|
Ayah 5:105 الأية
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا عَلَيْكُمْ أَنفُسَكُمْ ۖ لَا يَضُرُّكُم مَّن
ضَلَّ إِذَا اهْتَدَيْتُمْ ۚ إِلَى اللهِ مَرْجِعُكُمْ جَمِيعًا فَيُنَبِّئُكُم
بِمَا كُنتُمْ تَعْمَلُونَ
Ya ayyuha allatheena amanooAAalaykum anfusakum la yadurrukum man dallaitha
ihtadaytum ila Allahi marjiAAukumjameeAAan fayunabbi-okum bima kuntum taAAmaloon
Swahili
Enyi mlio amini! Kilicho lazima juu yenu ni nafsi zenu. Hawakudhuruni walio
potoka ikiwa nyinyi mmeongoka. Ni kwa Mwenyezi Mungu ndio marudio yenu nyote;
basi atakwambieni yale mliyo kuwa mkiyatenda.
|
Ayah 5:106 الأية
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا شَهَادَةُ بَيْنِكُمْ إِذَا حَضَرَ أَحَدَكُمُ
الْمَوْتُ حِينَ الْوَصِيَّةِ اثْنَانِ ذَوَا عَدْلٍ مِّنكُمْ أَوْ آخَرَانِ مِنْ
غَيْرِكُمْ إِنْ أَنتُمْ ضَرَبْتُمْ فِي الْأَرْضِ فَأَصَابَتْكُم مُّصِيبَةُ
الْمَوْتِ ۚ تَحْبِسُونَهُمَا مِن بَعْدِ الصَّلَاةِ فَيُقْسِمَانِ بِاللهِ إِنِ
ارْتَبْتُمْ لَا نَشْتَرِي بِهِ ثَمَنًا وَلَوْ كَانَ ذَا قُرْبَىٰ ۙ وَلَا
نَكْتُمُ شَهَادَةَ اللهِ إِنَّا إِذًا لَّمِنَ الْآثِمِينَ
Ya ayyuha allatheena amanooshahadatu baynikum itha hadara ahadakumualmawtu heena
alwasiyyati ithnani thawaAAadlin minkum aw akharani min ghayrikum in antum
darabtumfee al-ardi faasabatkum museebatu almawti tahbisoonahumamin baAAdi
assalati fayuqsimani billahiini irtabtum la nashtaree bihi thamanan walaw kana
thaqurba wala naktumu shahadata Allahiinna ithan lamina al-athimeen
Swahili
Enyi mlio amini! Yanapo mfikia mauti mmoja wenu na akataka kutoa wasia, basi
wawepo mashahidi wawili miongoni mwenu ambao ni waadilifu. Na mnapo kuwa
safarini, na msiba wa mauti ukakusibuni, basi washuhudie wengineo wawili wasio
kuwa katika nyinyi. Mtawazuia wawili hao baada ya Sala na waape kwa Mwenyezi
Mungu, mkitilia shaka, wakisema: Hatutopokea thamani yoyote kwa haya hata kwa
ajili ya jamaa; na wala hatutaficha ushahidi wa Mwenyezi Mungu; hakika hapo
tutakuwa miongoni mwa wenye dhambi.
|
Ayah 5:107 الأية
فَإِنْ عُثِرَ عَلَىٰ أَنَّهُمَا اسْتَحَقَّا إِثْمًا فَآخَرَانِ يَقُومَانِ
مَقَامَهُمَا مِنَ الَّذِينَ اسْتَحَقَّ عَلَيْهِمُ الْأَوْلَيَانِ فَيُقْسِمَانِ
بِاللهِ لَشَهَادَتُنَا أَحَقُّ مِن شَهَادَتِهِمَا وَمَا اعْتَدَيْنَا إِنَّا
إِذًا لَّمِنَ الظَّالِمِينَ
Fa-in AAuthira AAala annahumaistahaqqa ithman faakharani yaqoomanimaqamahuma
mina allatheena istahaqqaAAalayhimu al-awlayani fayuqsimani billahilashahadatuna
ahaqqu min shahadatihimawama iAAtadayna inna ithan lamina aththalimeen
Swahili
Ikigundulikana kuwa wawili hao wamestahiki dhambi, basi wawili wengineo kutokana
na warithi wenye kudai haki washike makamo ya wa mwanzo. Nao waape kwa Mwenyezi
Mungu wakisema: Hakika ushahidi wetu ni wa haki zaidi kuliko ushahidi wa wale.
Na sisi hatujafanya dhambi; hakika hapo tutakuwa miongoni mwa walio dhulumu.
|
Ayah 5:108 الأية
ذَٰلِكَ أَدْنَىٰ أَن يَأْتُوا بِالشَّهَادَةِ عَلَىٰ وَجْهِهَا أَوْ يَخَافُوا أَن
تُرَدَّ أَيْمَانٌ بَعْدَ أَيْمَانِهِمْ ۗ وَاتَّقُوا اللهَ وَاسْمَعُوا ۗ
وَاللهُ لَا يَهْدِي الْقَوْمَ الْفَاسِقِينَ
Thalika adna an ya/too bishshahadatiAAala wajhiha aw yakhafoo an turadda
aymanunbaAAda aymanihim wattaqoo Allaha wasmaAAoowallahu la yahdee alqawma
alfasiqeen
Swahili
Hivi inaelekea zaidi ya kwamba watatoa ushahidi ulio sawa au wataogopa visije
vikaletwa viapo vingine baada ya viapo vyao. Na mcheni Mwenyezi Mungu na msikie.
Na hakika Mwenyezi Mungu hawaongoi wapotofu.
|
Ayah 5:109 الأية
يَوْمَ يَجْمَعُ اللهُ الرُّسُلَ فَيَقُولُ مَاذَا أُجِبْتُمْ ۖ قَالُوا لَا
عِلْمَ لَنَا ۖ إِنَّكَ أَنتَ عَلَّامُ الْغُيُوبِ
Yawma yajmaAAu Allahu arrusulafayaqoolu matha ojibtum qaloo la AAilma lanainnaka
anta AAallamu alghuyoob
Swahili
Ile siku ambayo Mwenyezi Mungu atapo wakusanya Mitume awaambie: Mlijibiwa nini?
Watasema: Hatuna ujuzi; hakika Wewe ndiye Mjuzi Mkubwa wa yote yaliyo fichikana.
|
Ayah 5:110 الأية
إِذْ قَالَ اللهُ يَا عِيسَى ابْنَ مَرْيَمَ اذْكُرْ نِعْمَتِي عَلَيْكَ وَعَلَىٰ
وَالِدَتِكَ إِذْ أَيَّدتُّكَ بِرُوحِ الْقُدُسِ تُكَلِّمُ النَّاسَ فِي الْمَهْدِ
وَكَهْلًا ۖ وَإِذْ عَلَّمْتُكَ الْكِتَابَ وَالْحِكْمَةَ وَالتَّوْرَاةَ
وَالْإِنجِيلَ ۖ وَإِذْ تَخْلُقُ مِنَ الطِّينِ كَهَيْئَةِ الطَّيْرِ بِإِذْنِي
فَتَنفُخُ فِيهَا فَتَكُونُ طَيْرًا بِإِذْنِي ۖ وَتُبْرِئُ الْأَكْمَهَ
وَالْأَبْرَصَ بِإِذْنِي ۖ وَإِذْ تُخْرِجُ الْمَوْتَىٰ بِإِذْنِي ۖ وَإِذْ
كَفَفْتُ بَنِي إِسْرَائِيلَ عَنكَ إِذْ جِئْتَهُم بِالْبَيِّنَاتِ فَقَالَ
الَّذِينَ كَفَرُوا مِنْهُمْ إِنْ هَٰذَا إِلَّا سِحْرٌ مُّبِينٌ
Ith qala Allahu yaAAeesa ibna maryama othkur niAAmatee AAalaykawaAAala
walidatika ith ayyadtuka biroohialqudusi tukallimu annasa fee almahdi
wakahlanwa-ith AAallamtuka alkitaba walhikmatawattawrata wal-injeela
wa-ithtakhluqu mina atteeni kahay-ati attayribi-ithnee fatanfukhu feeha
fatakoonu tayranbi-ithnee watubri-o al-akmaha wal-abrasabi-ithnee wa-ith
tukhriju almawta bi-ithneewa-ith kafaftu banee isra-eela AAanka ithji/tahum
bilbayyinati faqala allatheenakafaroo minhum in hatha illa sihrun mubeen
Swahili
Na pale Mwenyezi Mungu atapo sema: Ewe Isa bin Maryamu! Kumbuka neema yangu juu
yako, na juu ya mama yako, nilipo kutia nguvu kwa Roho Takatifu, ukazungumza na
watu katika utoto na utuuzimani. Na nilivyo kufunza kuandika na hikima na
Taurati na Injili. Na ulipo tengeneza udongo sura ya ndege, kwa idhini yangu,
kisha ukapuliza ikawa ndege kwa idhini yangu; na ulipo waponesha vipofu na
wakoma kwa idhini yangu; na ulipo wafufua wafu kwa idhini yangu; na nilipo
kukinga na Wana wa Israili ulipo wajia na hoja zilizo wazi, na wakasema walio
kufuru miongoni mwao: Haya si lolote ila ni uchawi mtupu!
|
Ayah 5:111 الأية
وَإِذْ أَوْحَيْتُ إِلَى الْحَوَارِيِّينَ أَنْ آمِنُوا بِي وَبِرَسُولِي قَالُوا
آمَنَّا وَاشْهَدْ بِأَنَّنَا مُسْلِمُونَ
Wa-ith awhaytu ila alhawariyyeenaan aminoo bee wabirasoolee qaloo amannawashhad
bi-annana muslimoon
Swahili
Na nilipo wafunulia Wanafunzi kwamba waniamini Mimi na Mtume wangu, wakasema:
Tumeamini na shuhudia kuwa sisi ni Waislamu.
|
Ayah 5:112 الأية
إِذْ قَالَ الْحَوَارِيُّونَ يَا عِيسَى ابْنَ مَرْيَمَ هَلْ يَسْتَطِيعُ رَبُّكَ
أَن يُنَزِّلَ عَلَيْنَا مَائِدَةً مِّنَ السَّمَاءِ ۖ قَالَ اتَّقُوا اللهَ إِن
كُنتُم مُّؤْمِنِينَ
Ith qala alhawariyyoonaya AAeesa ibna maryama hal yastateeAAurabbuka an
yunazzila AAalayna ma-idatan mina assama-iqala ittaqoo Allaha in kuntum
mu/mineen
Swahili
Wanafunzi walipo sema: Ewe Isa bin Maryamu! Je, Mola wako Mlezi anaweza
kututeremshia chakula kutoka mbinguni? Akasema: Mcheni Mwenyezi Mungu ikiwa
nyinyi ni Waumini.
|
Ayah 5:113 الأية
قَالُوا نُرِيدُ أَن نَّأْكُلَ مِنْهَا وَتَطْمَئِنَّ قُلُوبُنَا وَنَعْلَمَ أَن
قَدْ صَدَقْتَنَا وَنَكُونَ عَلَيْهَا مِنَ الشَّاهِدِينَ
Qaloo nureedu an na/kula minhawatatma-inna quloobuna wanaAAlama an qad
sadaqtanawanakoona AAalayha mina ashshahideen
Swahili
Wakasema: Tunataka kukila chakula hicho, na nyoyo zetu zitue, na tujue kwamba
umetuambia kweli, na tuwe miongoni mwa wanao shuhudia.
|
Ayah 5:114 الأية
قَالَ عِيسَى ابْنُ مَرْيَمَ اللهُمَّ رَبَّنَا أَنزِلْ عَلَيْنَا مَائِدَةً
مِّنَ السَّمَاءِ تَكُونُ لَنَا عِيدًا لِّأَوَّلِنَا وَآخِرِنَا وَآيَةً مِّنكَ ۖ
وَارْزُقْنَا وَأَنتَ خَيْرُ الرَّازِقِينَ
Qala AAeesa ibnu maryama allahummarabbana anzil AAalayna ma-idatan mina
assama-itakoonu lana AAeedan li-awwalina waakhirinawaayatan minka warzuqna
waanta khayru arraziqeen
Swahili
Akasema Isa bin Maryamu: Ewe Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wetu! Tuteremshia
chakula kutoka mbinguni ili kiwe Sikukuu kwa ajili ya wa mwanzo wetu na wa
mwisho wetu, na kiwe ni Ishara itokayo kwako. Basi turuzuku, kwani Wewe ndiye
mbora wa wanao ruzuku.
|
Ayah 5:115 الأية
قَالَ اللهُ إِنِّي مُنَزِّلُهَا عَلَيْكُمْ ۖ فَمَن يَكْفُرْ بَعْدُ مِنكُمْ
فَإِنِّي أُعَذِّبُهُ عَذَابًا لَّا أُعَذِّبُهُ أَحَدًا مِّنَ الْعَالَمِينَ
Qala Allahu innee munazziluhaAAalaykum faman yakfur baAAdu minkum fa-innee
oAAaththibuhuAAathaban la oAAaththibuhu ahadanmina alAAalameen
Swahili
Mwenyezi Mungu akasema: Hakika Mimi nitakuteremshieni hicho. Lakini yeyote
katika nyinyi atakaye kanya baadae, basi hakika Mimi nitampa adhabu nisiyopata
kumpa yeyote katika walimwengu.
|
Ayah 5:116 الأية
وَإِذْ قَالَ اللهُ يَا عِيسَى ابْنَ مَرْيَمَ أَأَنتَ قُلْتَ لِلنَّاسِ
اتَّخِذُونِي وَأُمِّيَ إِلَٰهَيْنِ مِن دُونِ اللهِ ۖ قَالَ سُبْحَانَكَ مَا
يَكُونُ لِي أَنْ أَقُولَ مَا لَيْسَ لِي بِحَقٍّ ۚ إِن كُنتُ قُلْتُهُ فَقَدْ
عَلِمْتَهُ ۚ تَعْلَمُ مَا فِي نَفْسِي وَلَا أَعْلَمُ مَا فِي نَفْسِكَ ۚ إِنَّكَ
أَنتَ عَلَّامُ الْغُيُوبِ
Wa-ith qala Allahu yaAAeesa ibna maryama aanta qulta linnasiittakhithoonee
waommiya ilahayni min dooni Allahiqala subhanaka ma yakoonu lee an aqoola
malaysa lee bihaqqin in kuntu qultuhu faqad AAalimtahutaAAlamu ma fee nafsee
wala aAAlamu ma feenafsika innaka anta AAallamu alghuyoob
Swahili
Na pale Mwenyezi Mungu atakapo sema: Ewe Isa bin Maryamu! Ati wewe uliwaambia
watu: Nifanyeni mimi na mama yangu kuwa ni miungu badala ya Mwenyezi Mungu? (Na
Isa) atasema: Subhanaka, Wewe umetakasika! Hainifalii mimi kusema ambayo si haki
yangu. Ikiwa nilisema basi bila ya shaka umekwisha yajua. Wewe unayajua yaliyo
ndani ya nafsi yangu, lakini mimi siyajui yaliyo katika nafsi yako. Hakika Wewe
ndiye Mjuzi mkubwa wa yaliyo fichikana.
|
Ayah 5:117 الأية
مَا قُلْتُ لَهُمْ إِلَّا مَا أَمَرْتَنِي بِهِ أَنِ اعْبُدُوا اللهَ رَبِّي
وَرَبَّكُمْ ۚ وَكُنتُ عَلَيْهِمْ شَهِيدًا مَّا دُمْتُ فِيهِمْ ۖ فَلَمَّا
تَوَفَّيْتَنِي كُنتَ أَنتَ الرَّقِيبَ عَلَيْهِمْ ۚ وَأَنتَ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ
شَهِيدٌ
Ma qultu lahum illa maamartanee bihi ani oAAbudoo Allaha rabbee
warabbakumwakuntu AAalayhim shaheedan ma dumtu feehim falammatawaffaytanee kunta
anta arraqeeba AAalayhim waanta AAalakulli shay-in shaheed
Swahili
Sikuwaambia lolote ila uliyo niamrisha, nayo ni: Muabuduni Mwenyezi Mungu, Mola
wangu Mlezi na Mola wenu Mlezi. Na mimi nilikuwa shahidi juu yao nilipo kuwa
nao. Na ulipo nifisha ukawa Wewe ndiye Muangalizi juu yao. Na Wewe ni shahidi
juu ya kila kitu.
|
|