First Ayah 1 الأية الأوليبِسْم ِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ
اقْتَرَبَتِ السَّاعَةُ وَانشَقَّ الْقَمَرُ
Iqtarabati assaAAatu wanshaqqaalqamar
Swahili
Saa imekaribia, na mwezi umepasuka!
|
Ayah 54:2 الأية
وَإِن يَرَوْا آيَةً يُعْرِضُوا وَيَقُولُوا سِحْرٌ مُّسْتَمِرٌّ
Wa-in yaraw ayatan yuAAridoowayaqooloo sihrun mustamirr
Swahili
Na wakiona Ishara hugeuka upande na husema: Huu uchawi tu unazidi kuendelea.
|
Ayah 54:3 الأية
وَكَذَّبُوا وَاتَّبَعُوا أَهْوَاءَهُمْ ۚ وَكُلُّ أَمْرٍ مُّسْتَقِرٌّ
Wakaththaboo wattabaAAoo ahwaahumwakullu amrin mustaqirr
Swahili
Na wamekanusha na wamefuata matamanio yao. Na kila jambo ni lenye kuthibiti.
|
Ayah 54:4 الأية
وَلَقَدْ جَاءَهُم مِّنَ الْأَنبَاءِ مَا فِيهِ مُزْدَجَرٌ
Walaqad jaahum mina al-anba-i mafeehi muzdajar
Swahili
Na bila ya shaka zimewajia khabari zenye makaripio.
|
Ayah 54:5 الأية
حِكْمَةٌ بَالِغَةٌ ۖ فَمَا تُغْنِ النُّذُرُ
Hikmatun balighatun famatughnee annuthur
Swahili
Hikima kaamili; lakini maonyo hayafai kitu!
|
Ayah 54:6 الأية
فَتَوَلَّ عَنْهُمْ ۘ يَوْمَ يَدْعُ الدَّاعِ إِلَىٰ شَيْءٍ نُّكُرٍ
Fatawalla AAanhum yawma yadAAu addaAAiila shay-in nukur
Swahili
Basi jiepushe nao. Siku atakapo ita mwitaji kuliendea jambo linalo chusha;
|
Ayah 54:7 الأية
خُشَّعًا أَبْصَارُهُمْ يَخْرُجُونَ مِنَ الْأَجْدَاثِ كَأَنَّهُمْ جَرَادٌ
مُّنتَشِرٌ
KhushshaAAan absaruhum yakhrujoonamina al-ajdathi kaannahum jaradun muntashir
Swahili
Macho yao yatainama; watatoka makaburini kama nzige walio tawanyika,
|
Ayah 54:8 الأية
مُّهْطِعِينَ إِلَى الدَّاعِ ۖ يَقُولُ الْكَافِرُونَ هَٰذَا يَوْمٌ عَسِرٌ
MuhtiAAeena ila addaAAiyaqoolu alkafiroona hatha yawmun AAasir
Swahili
Wanamkimbilia mwitaji, na makafiri wanasema: Hii ni siku ngumu.
|
Ayah 54:9 الأية
كَذَّبَتْ قَبْلَهُمْ قَوْمُ نُوحٍ فَكَذَّبُوا عَبْدَنَا وَقَالُوا مَجْنُونٌ
وَازْدُجِرَ
Kaththabat qablahum qawmu noohinfakaththaboo AAabdana waqaloo majnoonun wazdujir
Swahili
Kabla yao kaumu ya Nuhu walikanusha; wakamkanusha mja wetu, na wakasema ni
mwendawazimu, na akakaripiwa.
|
Ayah 54:10 الأية
فَدَعَا رَبَّهُ أَنِّي مَغْلُوبٌ فَانتَصِرْ
FadaAAa rabbahu annee maghloobun fantasir
Swahili
Basi akamwomba Mola wake Mlezi akasema: Kwa hakika mimi nimeshindwa, basi
ninusuru!
|
Ayah 54:11 الأية
فَفَتَحْنَا أَبْوَابَ السَّمَاءِ بِمَاءٍ مُّنْهَمِرٍ
Fafatahna abwaba assama-ibima-in munhamir
Swahili
Basi tukaifungua milango ya mbingu kwa maji yanayo miminika.
|
Ayah 54:12 الأية
وَفَجَّرْنَا الْأَرْضَ عُيُونًا فَالْتَقَى الْمَاءُ عَلَىٰ أَمْرٍ قَدْ قُدِرَ
Wafajjarna al-arda AAuyoonanfaltaqa almao AAala amrin qad qudir
Swahili
Na tukazipasua ardhi kwa chemchem, yakakutana maji kwa jambo lilio kadiriwa.
|
Ayah 54:13 الأية
وَحَمَلْنَاهُ عَلَىٰ ذَاتِ أَلْوَاحٍ وَدُسُرٍ
Wahamalnahu AAala thatialwahin wadusur
Swahili
Na tukamchukua kwenye safina ya mbao na kamba.
|
Ayah 54:14 الأية
تَجْرِي بِأَعْيُنِنَا جَزَاءً لِّمَن كَانَ كُفِرَ
Tajree bi-aAAyunina jazaanliman kana kufir
Swahili
Ikawa inakwenda kwa nadhari yetu, kuwa ni malipo kwa alivyo kuwa amekanushwa.
|
Ayah 54:15 الأية
وَلَقَد تَّرَكْنَاهَا آيَةً فَهَلْ مِن مُّدَّكِرٍ
Walaqad taraknaha ayatanfahal min muddakir
Swahili
Na bila ya shaka tuliiacha iwe ni Ishara. Lakini je, yupo anaye kumbuka?
|
Ayah 54:16 الأية
فَكَيْفَ كَانَ عَذَابِي وَنُذُرِ
Fakayfa kana AAathabee wanuthur
Swahili
Basi ilikuwaje adhabu yangu, na maonyo yangu.
|
Ayah 54:17 الأية
وَلَقَدْ يَسَّرْنَا الْقُرْآنَ لِلذِّكْرِ فَهَلْ مِن مُّدَّكِرٍ
Walaqad yassarna alqur-ana liththikrifahal min muddakir
Swahili
Na bila ya shaka Sisi tumeifanya Qur'ani iwe nyepesi kufahamika. Lakini yupo
anaye kumbuka?
|
Ayah 54:18 الأية
كَذَّبَتْ عَادٌ فَكَيْفَ كَانَ عَذَابِي وَنُذُرِ
Kaththabat AAadun fakayfa kanaAAathabee wanuthur
Swahili
Kina A'di walikanusha. Basi ilikuwaje adhabu yangu na maonyo yangu?
|
Ayah 54:19 الأية
إِنَّا أَرْسَلْنَا عَلَيْهِمْ رِيحًا صَرْصَرًا فِي يَوْمِ نَحْسٍ مُّسْتَمِرٍّ
Inna arsalna AAalayhim reehansarsaran fee yawmi nahsin mustamirr
Swahili
Hakika Sisi tuliwapelekea upepo wa kimbunga katika siku korofi mfululizo,
|
Ayah 54:20 الأية
تَنزِعُ النَّاسَ كَأَنَّهُمْ أَعْجَازُ نَخْلٍ مُّنقَعِرٍ
TanziAAu annasa kaannahumaAAjazu nakhlin munqaAAir
Swahili
Ukiwang'oa watu kama vigogo vya mitende vilio ng'olewa.
|
Ayah 54:21 الأية
فَكَيْفَ كَانَ عَذَابِي وَنُذُرِ
Fakayfa kana AAathabee wanuthur
Swahili
Basi ilikuwaje adhabu yangu na maonyo yangu?
|
Ayah 54:22 الأية
وَلَقَدْ يَسَّرْنَا الْقُرْآنَ لِلذِّكْرِ فَهَلْ مِن مُّدَّكِرٍ
Walaqad yassarna alqur-ana liththikrifahal min muddakir
Swahili
Na bila ya shaka Sisi tumeifanya Qur'ani nyepesi kufahamika; lakini yupo anaye
kumbuka?
|
Ayah 54:23 الأية
كَذَّبَتْ ثَمُودُ بِالنُّذُرِ
Kaththabat thamoodu binnuthur
Swahili
Thamudi waliwakanusha Waonyaji.
|
Ayah 54:24 الأية
فَقَالُوا أَبَشَرًا مِّنَّا وَاحِدًا نَّتَّبِعُهُ إِنَّا إِذًا لَّفِي ضَلَالٍ
وَسُعُرٍ
Faqaloo abasharan minna wahidannattabiAAuhu inna ithan lafee dalalinwasuAAur
Swahili
Wakasema: Ati tumfuate binaadamu mmoja katika sisi? Basi hivyo sisi tutakuwa
katika upotofu na kichaa!
|
Ayah 54:25 الأية
أَأُلْقِيَ الذِّكْرُ عَلَيْهِ مِن بَيْنِنَا بَلْ هُوَ كَذَّابٌ أَشِرٌ
Aolqiya aththikru AAalayhimin baynina bal huwa kaththabun ashir
Swahili
Ni yeye tu aliye teremshiwa huo ukumbusho kati yetu sote? Bali huyu ni mwongo
mwenye kiburi!
|
Ayah 54:26 الأية
سَيَعْلَمُونَ غَدًا مَّنِ الْكَذَّابُ الْأَشِرُ
SayaAAlamoona ghadan mani alkaththabual-ashir
Swahili
Kesho watajua ni nani huyo mwongo mwenye kiburi.
|
Ayah 54:27 الأية
إِنَّا مُرْسِلُو النَّاقَةِ فِتْنَةً لَّهُمْ فَارْتَقِبْهُمْ وَاصْطَبِرْ
Inna mursiloo annaqatifitnatan lahum fartaqibhum wastabir
Swahili
Hakika Sisi tutawapelekea ngamia jike ili kuwajaribu, basi watazame tu na
ustahamili.
|
Ayah 54:28 الأية
وَنَبِّئْهُمْ أَنَّ الْمَاءَ قِسْمَةٌ بَيْنَهُمْ ۖ كُلُّ شِرْبٍ مُّحْتَضَرٌ
Wanabbi/hum anna almaa qismatunbaynahum kullu shirbin muhtadar
Swahili
Na waambie kwamba maji yatagawanywa baina yao; kila sehemu ya maji itahudhuriwa
na aliye khusika.
|
Ayah 54:29 الأية
فَنَادَوْا صَاحِبَهُمْ فَتَعَاطَىٰ فَعَقَرَ
Fanadaw sahibahum fataAAatafaAAaqar
Swahili
Basi wakamwita mtu wao akaja akamchinja.
|
Ayah 54:30 الأية
فَكَيْفَ كَانَ عَذَابِي وَنُذُرِ
Fakayfa kana AAathabee wanuthur
Swahili
Basi ilikuwaje adhabu yangu na maonyo yangu!
|
Ayah 54:31 الأية
إِنَّا أَرْسَلْنَا عَلَيْهِمْ صَيْحَةً وَاحِدَةً فَكَانُوا كَهَشِيمِ
الْمُحْتَظِرِ
Inna arsalna AAalayhim sayhatanwahidatan fakanoo kahasheemi almuhtathir
Swahili
Hakika Sisi tuliwapelekea ukelele mmoja tu, wakawa kama mabuwa ya kujengea uwa.
|
Ayah 54:32 الأية
وَلَقَدْ يَسَّرْنَا الْقُرْآنَ لِلذِّكْرِ فَهَلْ مِن مُّدَّكِرٍ
Walaqad yassarna alqur-ana liththikrifahal min muddakir
Swahili
Na bila ya shaka Sisi tumeifanya Qur'ani iwe nyepesi kwa kukumbuka, lakini yupo
akumbukaye?
|
Ayah 54:33 الأية
كَذَّبَتْ قَوْمُ لُوطٍ بِالنُّذُرِ
Kaththabat qawmu lootin binnuthur
Swahili
Kaumu Lut'i nao waliwakadhibisha Waonyaji.
|
Ayah 54:34 الأية
إِنَّا أَرْسَلْنَا عَلَيْهِمْ حَاصِبًا إِلَّا آلَ لُوطٍ ۖ نَّجَّيْنَاهُم
بِسَحَرٍ
Inna arsalna AAalayhim hasibanilla ala lootin najjaynahum bisahar
Swahili
Hakika Sisi tukawapelekea kimbunga cha vijiwe, isipo kuwa wafuasi wa Lut'i. Hao
tuliwaokoa karibu na alfajiri.
|
Ayah 54:35 الأية
نِّعْمَةً مِّنْ عِندِنَا ۚ كَذَٰلِكَ نَجْزِي مَن شَكَرَ
NiAAmatan min AAindina kathalikanajzee man shakar
Swahili
Kwa neema inayo toka kwetu. Hivyo ndivyo tumlipavyo anaye shukuru.
|
Ayah 54:36 الأية
وَلَقَدْ أَنذَرَهُم بَطْشَتَنَا فَتَمَارَوْا بِالنُّذُرِ
Walaqad antharahum batshatanafatamaraw binnuthur
Swahili
Na hakika yeye aliwaonya adhabu yetu; lakini wao waliyatilia shaka hayo maonyo.
|
Ayah 54:37 الأية
وَلَقَدْ رَاوَدُوهُ عَن ضَيْفِهِ فَطَمَسْنَا أَعْيُنَهُمْ فَذُوقُوا عَذَابِي
وَنُذُرِ
Walaqad rawadoohu AAan dayfihifatamasna aAAyunahum fathooqoo AAathabeewanuthur
Swahili
Na walimtaka awape wageni wake. Tukayapofua macho yao, na tukawaambia: Onjeni
basi adhabu na maonyo yangu!
|
Ayah 54:38 الأية
وَلَقَدْ صَبَّحَهُم بُكْرَةً عَذَابٌ مُّسْتَقِرٌّ
Walaqad sabbahahum bukratanAAathabun mustaqirr
Swahili
Na iliwafikia wakati wa asubuhi adhabu yangu ya kuendelea.
|
Ayah 54:39 الأية
فَذُوقُوا عَذَابِي وَنُذُرِ
Fathooqoo AAathabee wanuthur
Swahili
Basi onjeni adhabu na maonyo yangu!
|
Ayah 54:40 الأية
وَلَقَدْ يَسَّرْنَا الْقُرْآنَ لِلذِّكْرِ فَهَلْ مِن مُّدَّكِرٍ
Walaqad yassarna alqur-ana liththikrifahal min muddakir
Swahili
Na hakika tumeisahilisha Qur'ani kuikumbuka. Lakini yupo anaye kumbuka?
|
Ayah 54:41 الأية
وَلَقَدْ جَاءَ آلَ فِرْعَوْنَ النُّذُرُ
Walaqad jaa ala firAAawna annuthur
Swahili
Na Waonyaji waliwafikia watu wa Firauni.
|
Ayah 54:42 الأية
كَذَّبُوا بِآيَاتِنَا كُلِّهَا فَأَخَذْنَاهُمْ أَخْذَ عَزِيزٍ مُّقْتَدِرٍ
Kaththaboo bi-ayatinakulliha faakhathnahum akhthaAAazeezin muqtadir
Swahili
Walizikadhibisha Ishara zetu zote, nasi tukawashika kama anavyo shika Mwenye
nguvu Mwenye uweza.
|
Ayah 54:43 الأية
أَكُفَّارُكُمْ خَيْرٌ مِّنْ أُولَٰئِكُمْ أَمْ لَكُم بَرَاءَةٌ فِي الزُّبُرِ
Akuffarukum khayrun min ola-ikumam lakum baraatun fee azzubur
Swahili
Je! Makafiri wenu ni bora kuliko hao, au yameandikwa vitabuni kuwa nyinyi
hamtiwi makosani?
|
Ayah 54:44 الأية
أَمْ يَقُولُونَ نَحْنُ جَمِيعٌ مُّنتَصِرٌ
Am yaqooloona nahnu jameeAAun muntasir
Swahili
Au ndio wanasema: Sisi ni wengi tutashinda tu.
|
Ayah 54:45 الأية
سَيُهْزَمُ الْجَمْعُ وَيُوَلُّونَ الدُّبُرَ
Sayuhzamu aljamAAu wayuwalloona addubur
Swahili
Wingi wao huu utashindwa, na wao watasukumwa nyuma.
|
Ayah 54:46 الأية
بَلِ السَّاعَةُ مَوْعِدُهُمْ وَالسَّاعَةُ أَدْهَىٰ وَأَمَرُّ
Bali assaAAatu mawAAiduhum wassaAAatuadha waamar
Swahili
Bali Saa ya Kiyama ndio miadi yao, na Saa hiyo ni nzito zaidi na chungu zaidi.
|
Ayah 54:47 الأية
إِنَّ الْمُجْرِمِينَ فِي ضَلَالٍ وَسُعُرٍ
Inna almujrimeena fee dalalinwasuAAur
Swahili
Hakika wakosefu wamo katika upotofu na wazimu.
|
Ayah 54:48 الأية
يَوْمَ يُسْحَبُونَ فِي النَّارِ عَلَىٰ وُجُوهِهِمْ ذُوقُوا مَسَّ سَقَرَ
Yawma yushaboona fee annariAAala wujoohihim thooqoo massa saqar
Swahili
Siku watakapo kokotwa Motoni kifudifudi waambiwe: Onjeni mguso wa Jahannamu!
|
Ayah 54:49 الأية
إِنَّا كُلَّ شَيْءٍ خَلَقْنَاهُ بِقَدَرٍ
Inna kulla shay-in khalaqnahubiqadar
Swahili
Kwa hakika Sisi tumekiumba kila kitu kwa kipimo.
|
Ayah 54:50 الأية
وَمَا أَمْرُنَا إِلَّا وَاحِدَةٌ كَلَمْحٍ بِالْبَصَرِ
Wama amruna illa wahidatunkalamhin bilbasar
Swahili
Na amri yetu haikuwa ila ni moja tu, kama kupepesa jicho.
|
Ayah 54:51 الأية
وَلَقَدْ أَهْلَكْنَا أَشْيَاعَكُمْ فَهَلْ مِن مُّدَّكِرٍ
Walaqad ahlakna ashyaAAakumfahal min muddakir
Swahili
Na bila ya shaka tumekwisha waangamiza wenzenu. Lakini yupo anaye kumbuka?
|
Ayah 54:52 الأية
وَكُلُّ شَيْءٍ فَعَلُوهُ فِي الزُّبُرِ
Wakullu shay-in faAAaloohu fee azzubur
Swahili
Na kila jambo walilo lifanya limo vitabuni.
|
Ayah 54:53 الأية
وَكُلُّ صَغِيرٍ وَكَبِيرٍ مُّسْتَطَرٌ
Wakullu sagheerin wakabeerin mustatar
Swahili
Na kila kidogo na kikubwa kimeandikwa.
|
Ayah 54:54 الأية
إِنَّ الْمُتَّقِينَ فِي جَنَّاتٍ وَنَهَرٍ
Inna almuttaqeena fee jannatinwanahar
Swahili
Hakika wachamngu watakuwa katika Mabustani na mito.
|
Ayah 54:55 الأية
فِي مَقْعَدِ صِدْقٍ عِندَ مَلِيكٍ مُّقْتَدِرٍ
Fee maqAAadi sidqin AAinda maleekinmuqtadir
Swahili
Katika makalio ya haki kwa Mfalme Mwenye uweza.
|
©
EsinIslam.Com Designed & produced by The Awqaf London. Please pray for us
|