1st Ayah 1 الأية ١الأوليبِسْم ِ اللهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ
إِذَا وَقَعَتِ الْوَاقِعَةُ
Itha waqaAAati alwaqiAAat
Swahili
Litakapo tukia hilo Tukio
|
Ayah 56:2 الأية
لَيْسَ لِوَقْعَتِهَا كَاذِبَةٌ
Laysa liwaqAAatiha kathiba
Swahili
Hapana cha kukanusha kutukia kwake.
|
Ayah 56:3 الأية
خَافِضَةٌ رَّافِعَةٌ
Khafidatun rafiAAa
Swahili
Literemshalo linyanyualo,
|
Ayah 56:4 الأية
إِذَا رُجَّتِ الْأَرْضُ رَجًّا
Itha rujjati al-ardu rajja
Swahili
Itakapo tikiswa ardhi kwa mtikiso,
|
Ayah 56:5 الأية
وَبُسَّتِ الْجِبَالُ بَسًّا
Wabussati aljibalu bassa
Swahili
Na milima itapo sagwasagwa,
|
Ayah 56:6 الأية
فَكَانَتْ هَبَاءً مُّنبَثًّا
Fakanat habaan munbaththa
Swahili
Iwe mavumbi yanayo peperushwa,
|
Ayah 56:7 الأية
وَكُنتُمْ أَزْوَاجًا ثَلَاثَةً
Wakuntum azwajan thalatha
Swahili
Na nyinyi mtakuwa namna tatu:-
|
Ayah 56:8 الأية
فَأَصْحَابُ الْمَيْمَنَةِ مَا أَصْحَابُ الْمَيْمَنَةِ
Faas-habu almaymanati maas-habu almaymanat
Swahili
Basi watakuwepo wa kuliani; je, ni wepi wa kuliani?
|
Ayah 56:9 الأية
وَأَصْحَابُ الْمَشْأَمَةِ مَا أَصْحَابُ الْمَشْأَمَةِ
Waas-habu almash-amati maas-habu almash-amat
Swahili
Na wa kushotoni; je, ni wepi wa kushotoni?
|
Ayah 56:10 الأية
وَالسَّابِقُونَ السَّابِقُونَ
Wassabiqoona assabiqoon
Swahili
Na wa mbele watakuwa mbele.
|
Ayah 56:11 الأية
أُولَٰئِكَ الْمُقَرَّبُونَ
Ola-ika almuqarraboon
Swahili
Hao ndio watakao karibishwa
|
Ayah 56:12 الأية
فِي جَنَّاتِ النَّعِيمِ
Fee jannati annaAAeem
Swahili
Katika Bustani zenye neema.
|
Ayah 56:13 الأية
ثُلَّةٌ مِّنَ الْأَوَّلِينَ
Thullatun mina al-awwaleen
Swahili
Fungu kubwa katika wa mwanzo,
|
Ayah 56:14 الأية
وَقَلِيلٌ مِّنَ الْآخِرِينَ
Waqaleelun mina al-akhireena
Swahili
Na wachache katika wa mwisho.
|
Ayah 56:15 الأية
عَلَىٰ سُرُرٍ مَّوْضُونَةٍ
AAala sururin mawdoona
Swahili
Watakuwa juu ya viti vya fakhari vilivyo tonewa.
|
Ayah 56:16 الأية
مُّتَّكِئِينَ عَلَيْهَا مُتَقَابِلِينَ
Muttaki-eena AAalayha mutaqabileen
Swahili
Wakiviegemea wakielekeana.
|
Ayah 56:17 الأية
يَطُوفُ عَلَيْهِمْ وِلْدَانٌ مُّخَلَّدُونَ
Yatoofu AAalayhim wildanunmukhalladoon
Swahili
Wakitumikiwa na wavulana wa ujana wa milele,
|
Ayah 56:18 الأية
بِأَكْوَابٍ وَأَبَارِيقَ وَكَأْسٍ مِّن مَّعِينٍ
Bi-akwabin waabareeqa waka/sinmin maAAeen
Swahili
Kwa vikombe na mabirika na bilauri za vinywaji kutoka chemchem safi.
|
Ayah 56:19 الأية
لَّا يُصَدَّعُونَ عَنْهَا وَلَا يُنزِفُونَ
La yusaddaAAoona AAanhawala yunzifoon
Swahili
Hawataumwa kichwa kwa vinywaji hivyo wala hawatoleweshwa.
|
Ayah 56:20 الأية
وَفَاكِهَةٍ مِّمَّا يَتَخَيَّرُونَ
Wafakihatin mimmayatakhayyaroon
Swahili
Na matunda wayapendayo,
|
Ayah 56:21 الأية
وَلَحْمِ طَيْرٍ مِّمَّا يَشْتَهُونَ
Walahmi tayrin mimmayashtahoon
Swahili
Na nyama za ndege kama wanavyo tamani.
|
Ayah 56:22 الأية
وَحُورٌ عِينٌ
Wahoorun AAeen
Swahili
Na Mahurulaini,
|
Ayah 56:23 الأية
كَأَمْثَالِ اللُّؤْلُؤِ الْمَكْنُونِ
Kaamthali allu/lui almaknoon
Swahili
Walio kama mfano wa lulu zilio hifadhiwa.
|
Ayah 56:24 الأية
جَزَاءً بِمَا كَانُوا يَعْمَلُونَ
Jazaan bima kanooyaAAmaloon
Swahili
Ni malipo kwa waliyo kuwa wakiyatenda.
|
Ayah 56:25 الأية
لَا يَسْمَعُونَ فِيهَا لَغْوًا وَلَا تَأْثِيمًا
La yasmaAAoona feeha laghwanwala ta/theema
Swahili
Humo hawatasikia porojo wala maneno ya dhambi,
|
Ayah 56:26 الأية
إِلَّا قِيلًا سَلَامًا سَلَامًا
Illa qeelan salaman salama
Swahili
Isipo kuwa maneno ya Salama, Salama.
|
Ayah 56:27 الأية
وَأَصْحَابُ الْيَمِينِ مَا أَصْحَابُ الْيَمِينِ
Waas-habu alyameeni maas-habu alyameen
Swahili
Na wale wa mkono wa kulia, ni yepi yatakuwa ya wa kuliani?
|
Ayah 56:28 الأية
فِي سِدْرٍ مَّخْضُودٍ
Fee sidrin makhdood
Swahili
Katika mikunazi isiyo na miba,
|
Ayah 56:29 الأية
وَطَلْحٍ مَّنضُودٍ
Watalhin mandood
Swahili
Na migomba iliyo pangiliwa,
|
Ayah 56:30 الأية
وَظِلٍّ مَّمْدُودٍ
Wathillin mamdood
Swahili
Na kivuli kilicho tanda,
|
Ayah 56:31 الأية
وَمَاءٍ مَّسْكُوبٍ
Wama-in maskoob
Swahili
Na maji yanayo miminika,
|
Ayah 56:32 الأية
وَفَاكِهَةٍ كَثِيرَةٍ
Wafakihatin katheera
Swahili
Na matunda mengi,
|
Ayah 56:33 الأية
لَّا مَقْطُوعَةٍ وَلَا مَمْنُوعَةٍ
La maqtooAAatin walamamnooAAa
Swahili
Hayatindikii wala hayakatazwi,
|
Ayah 56:34 الأية
وَفُرُشٍ مَّرْفُوعَةٍ
Wafurushin marfooAAa
Swahili
Na matandiko yaliyo nyanyuliwa.
|
Ayah 56:35 الأية
إِنَّا أَنشَأْنَاهُنَّ إِنشَاءً
Inna ansha/nahunna inshaa
Swahili
Hakika Sisi tutawaumba (Mahurulaini) upya,
|
Ayah 56:36 الأية
فَجَعَلْنَاهُنَّ أَبْكَارًا
FajaAAalnahunna abkara
Swahili
Na tutawafanya vijana,
|
Ayah 56:37 الأية
عُرُبًا أَتْرَابًا
AAuruban atraba
Swahili
Wanapendana na waume zao, hirimu moja.
|
Ayah 56:38 الأية
لِّأَصْحَابِ الْيَمِينِ
Li-as-habi alyameen
Swahili
Kwa ajili ya watu wa kuliani.
|
Ayah 56:39 الأية
ثُلَّةٌ مِّنَ الْأَوَّلِينَ
Thullatun mina al-awwaleen
Swahili
Fungu kubwa katika wa mwanzo,
|
Ayah 56:40 الأية
وَثُلَّةٌ مِّنَ الْآخِرِينَ
Wathullatun mina al-akhireen
Swahili
Na fungu kubwa katika wa mwisho.
|
Ayah 56:41 الأية
وَأَصْحَابُ الشِّمَالِ مَا أَصْحَابُ الشِّمَالِ
Waas-habu ashshimalima as-habu ashshimal
Swahili
Na watu wa kushotoni; je ni yepi ya wa kushotoni?
|
Ayah 56:42 الأية
فِي سَمُومٍ وَحَمِيمٍ
Fee samoomin wahameem
Swahili
Katika upepo wa moto, na maji yanayo chemka,
|
Ayah 56:43 الأية
وَظِلٍّ مِّن يَحْمُومٍ
Wathillin min yahmoom
Swahili
Na kivuli cha moshi mweusi,
|
Ayah 56:44 الأية
لَّا بَارِدٍ وَلَا كَرِيمٍ
La baridin wala kareem
Swahili
Si cha kuburudisha wala kustarehesha.
|
Ayah 56:45 الأية
إِنَّهُمْ كَانُوا قَبْلَ ذَٰلِكَ مُتْرَفِينَ
Innahum kanoo qabla thalikamutrafeen
Swahili
Hakika hao walikuwa kabla ya haya wakiishi maisha ya anasa.
|
Ayah 56:46 الأية
وَكَانُوا يُصِرُّونَ عَلَى الْحِنثِ الْعَظِيمِ
Wakanoo yusirroona AAalaalhinthi alAAatheem
Swahili
Na walikuwa wakishikilia kufanya madhambi makubwa,
|
Ayah 56:47 الأية
وَكَانُوا يَقُولُونَ أَئِذَا مِتْنَا وَكُنَّا تُرَابًا وَعِظَامًا أَإِنَّا
لَمَبْعُوثُونَ
Wakanoo yaqooloona a-itha mitnawakunna turaban waAAithamana-inna lamabAAoothoon
Swahili
Na walikuwa wakisema: Tutakapo kufa na tukawa udongo na mafupa, ati ndio
tutafufuliwa?
|
Ayah 56:48 الأية
أَوَآبَاؤُنَا الْأَوَّلُونَ
Awa abaona al-awwaloon
Swahili
Au baba zetu wa zamani?
|
Ayah 56:49 الأية
قُلْ إِنَّ الْأَوَّلِينَ وَالْآخِرِينَ
Qul inna al-awwaleena wal-akhireen
Swahili
Sema: Hakika wa zamani na wa mwisho
|
Ayah 56:50 الأية
لَمَجْمُوعُونَ إِلَىٰ مِيقَاتِ يَوْمٍ مَّعْلُومٍ
LamajmooAAoona ila meeqatiyawmin maAAloom
Swahili
Bila ya shaka watakusanywa kwa wakati wa siku maalumu.
|
Ayah 56:51 الأية
ثُمَّ إِنَّكُمْ أَيُّهَا الضَّالُّونَ الْمُكَذِّبُونَ
Thumma innakum ayyuha addalloonaalmukaththiboon
Swahili
Kisha nyinyi, mlio potea, mnao kanusha,
|
Ayah 56:52 الأية
لَآكِلُونَ مِن شَجَرٍ مِّن زَقُّومٍ
Laakiloona min shajarin min zaqqoom
Swahili
Kwa yakini mtakula mti wa Zaqqumu.
|
Ayah 56:53 الأية
فَمَالِئُونَ مِنْهَا الْبُطُونَ
Famali-oona minha albutoon
Swahili
Na kwa mti huo mtajaza matumbo.
|
Ayah 56:54 الأية
فَشَارِبُونَ عَلَيْهِ مِنَ الْحَمِيمِ
Fashariboona AAalayhi mina alhameem
Swahili
Na juu yake mtakunywa maji yanayo chemka.
|
Ayah 56:55 الأية
فَشَارِبُونَ شُرْبَ الْهِيمِ
Fashariboona shurba alheem
Swahili
Tena mtakunywa kama wanavyo kunywa ngamia wenye kiu.
|
Ayah 56:56 الأية
هَٰذَا نُزُلُهُمْ يَوْمَ الدِّينِ
Hatha nuzuluhum yawma addeen
Swahili
Hiyo ndiyo karamu yao Siku ya Malipo.
|
Ayah 56:57 الأية
نَحْنُ خَلَقْنَاكُمْ فَلَوْلَا تُصَدِّقُونَ
Nahnu khalaqnakum falawlatusaddiqoon
Swahili
Sisi tumekuumbeni; basi hamsadiki?
|
Ayah 56:58 الأية
أَفَرَأَيْتُم مَّا تُمْنُونَ
Afaraaytum ma tumnoon
Swahili
Je! Mnaiona mbegu ya uzazi mnayo idondokeza?
|
Ayah 56:59 الأية
أَأَنتُمْ تَخْلُقُونَهُ أَمْ نَحْنُ الْخَالِقُونَ
Aantum takhluqoonahu am nahnu alkhaliqoon
Swahili
Je! Mnaiumba nyinyi, au ni Sisi ndio Waumbaji?
|
Ayah 56:60 الأية
نَحْنُ قَدَّرْنَا بَيْنَكُمُ الْمَوْتَ وَمَا نَحْنُ بِمَسْبُوقِينَ
Nahnu qaddarna baynakumualmawta wama nahnu bimasbooqeen
Swahili
Sisi tumekuwekeeni mauti; na wala Sisi hatushindwi
|
Ayah 56:61 الأية
عَلَىٰ أَن نُّبَدِّلَ أَمْثَالَكُمْ وَنُنشِئَكُمْ فِي مَا لَا تَعْلَمُونَ
AAala an nubaddila amthalakumwanunshi-akum fee ma la taAAlamoon
Swahili
Kuwaleta wengine badala yenu na kukuumbeni nyinyi kwa umbo msilo lijua.
|
Ayah 56:62 الأية
وَلَقَدْ عَلِمْتُمُ النَّشْأَةَ الْأُولَىٰ فَلَوْلَا تَذَكَّرُونَ
Walaqad AAalimtumu annash-ata al-oolafalawla tathakkaroon
Swahili
Na bila ya shaka mlikwisha jua umbo la kwanza, basi kwa nini hamkumbuki?
|
Ayah 56:63 الأية
أَفَرَأَيْتُم مَّا تَحْرُثُونَ
Afaraaytum ma tahruthoon
Swahili
Je! Mnaona makulima mnayo yapanda?
|
Ayah 56:64 الأية
أَأَنتُمْ تَزْرَعُونَهُ أَمْ نَحْنُ الزَّارِعُونَ
Aantum tazraAAoonahu am nahnu azzariAAoon
Swahili
Je! Ni nyinyi mnayo yaotesha au ni Sisi ndio wenye kuotesha?
|
Ayah 56:65 الأية
لَوْ نَشَاءُ لَجَعَلْنَاهُ حُطَامًا فَظَلْتُمْ تَفَكَّهُونَ
Law nashao lajaAAalnahu hutamanfathaltum tafakkahoon
Swahili
Tungeli taka tungeli yafanya yakawa mapepe, mkabaki mnastaajabu,
|
Ayah 56:66 الأية
إِنَّا لَمُغْرَمُونَ
Inna lamughramoon
Swahili
Mkisema: Hakika sisi tumegharimika;
|
Ayah 56:67 الأية
بَلْ نَحْنُ مَحْرُومُونَ
Bal nahnu mahroomoon
Swahili
Bali sisi tumenyimwa.
|
Ayah 56:68 الأية
أَفَرَأَيْتُمُ الْمَاءَ الَّذِي تَشْرَبُونَ
Afaraaytumu almaa allatheetashraboon
Swahili
Je! Mnayaona maji mnayo yanywa?
|
Ayah 56:69 الأية
أَأَنتُمْ أَنزَلْتُمُوهُ مِنَ الْمُزْنِ أَمْ نَحْنُ الْمُنزِلُونَ
Aantum anzaltumoohu mina almuzni am nahnualmunziloon
Swahili
Je! Ni nyinyi mnayo yateremsha kutoka mawinguni au ni Sisi ndio wenye
kuyateremsha?
|
Ayah 56:70 الأية
لَوْ نَشَاءُ جَعَلْنَاهُ أُجَاجًا فَلَوْلَا تَشْكُرُونَ
Law nashao jaAAalnahu ojajanfalawla tashkuroon
Swahili
Tungeli penda tungeli yafanya ya chumvi. Basi mbona hamshukuru?
|
Ayah 56:71 الأية
أَفَرَأَيْتُمُ النَّارَ الَّتِي تُورُونَ
Afaraaytumu annara allateetooroon
Swahili
Je! Mnauona moto mnao uwasha?
|
Ayah 56:72 الأية
أَأَنتُمْ أَنشَأْتُمْ شَجَرَتَهَا أَمْ نَحْنُ الْمُنشِئُونَ
Aantum ansha/tum shajarataha am nahnualmunshi-oon
Swahili
Ni nyinyi mlio uumba mti wake au Sisi ndio Waumbaji?
|
Ayah 56:73 الأية
نَحْنُ جَعَلْنَاهَا تَذْكِرَةً وَمَتَاعًا لِّلْمُقْوِينَ
Nahnu jaAAalnaha tathkiratanwamataAAan lilmuqween
Swahili
Sisi tumeufanya uwe ni ukumbusho na manufaa kwa walioko nyikani.
|
Ayah 56:74 الأية
فَسَبِّحْ بِاسْمِ رَبِّكَ الْعَظِيمِ
Fasabbih bismi rabbika alAAatheem
Swahili
Basi litakase jina la Mola wako Mlezi aliye Mkuu.
|
Ayah 56:75 الأية
فَلَا أُقْسِمُ بِمَوَاقِعِ النُّجُومِ
Fala oqsimu bimawaqiAAi annujoom
Swahili
Basi naapa kwa maanguko ya nyota,
|
Ayah 56:76 الأية
وَإِنَّهُ لَقَسَمٌ لَّوْ تَعْلَمُونَ عَظِيمٌ
Wa-innahu laqasamun law taAAlamoona AAatheem
Swahili
Na hakika bila ya shaka hichi ni kiapo kikubwa, laiti mngeli jua!
|
Ayah 56:77 الأية
إِنَّهُ لَقُرْآنٌ كَرِيمٌ
Innahu laqur-anun kareem
Swahili
Hakika hii bila ya shaka ni Qur'ani Tukufu,
|
Ayah 56:78 الأية
فِي كِتَابٍ مَّكْنُونٍ
Fee kitabin maknoon
Swahili
Katika Kitabu kilicho hifadhiwa.
|
Ayah 56:79 الأية
لَّا يَمَسُّهُ إِلَّا الْمُطَهَّرُونَ
La yamassuhu illa almutahharoon
Swahili
Hapana akigusaye ila walio takaswa.
|
Ayah 56:80 الأية
تَنزِيلٌ مِّن رَّبِّ الْعَالَمِينَ
Tanzeelun min rabbi alAAalameen
Swahili
Ni uteremsho unao toka kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
|
Ayah 56:81 الأية
أَفَبِهَٰذَا الْحَدِيثِ أَنتُم مُّدْهِنُونَ
Afabihatha alhadeethi antummudhinoon
Swahili
Ni maneno haya ndiyo nyinyi mnayapuuza?
|
Ayah 56:82 الأية
وَتَجْعَلُونَ رِزْقَكُمْ أَنَّكُمْ تُكَذِّبُونَ
WatajAAaloona rizqakum annakum tukaththiboon
Swahili
Na badala ya kushukuru kwa riziki yenu mnafanya kuwa mnakadhibisha?
|
Ayah 56:83 الأية
فَلَوْلَا إِذَا بَلَغَتِ الْحُلْقُومَ
Falawla itha balaghati alhulqoom
Swahili
Yawaje basi itakapo fika roho kwenye koo,
|
Ayah 56:84 الأية
وَأَنتُمْ حِينَئِذٍ تَنظُرُونَ
Waantum heena-ithin tanthuroona
Swahili
Na nyinyi wakati huo mnatazama!
|
Ayah 56:85 الأية
وَنَحْنُ أَقْرَبُ إِلَيْهِ مِنكُمْ وَلَٰكِن لَّا تُبْصِرُونَ
Wanahnu aqrabu ilayhi minkum walakinla tubsiroon
Swahili
Na Sisi tuko karibu zaidi naye kuliko nyinyi.
|
Ayah 56:86 الأية
فَلَوْلَا إِن كُنتُمْ غَيْرَ مَدِينِينَ
Falawla in kuntum ghayra madeeneen
Swahili
Na lau kuwa nyinyi hamumo katika mamlaka yangu,
|
Ayah 56:87 الأية
تَرْجِعُونَهَا إِن كُنتُمْ صَادِقِينَ
TarjiAAoonaha in kuntum sadiqeen
Swahili
Kwanini hamuirudishi hiyo roho, ikiwa nyinyi mnasema kweli?
|
Ayah 56:88 الأية
فَأَمَّا إِن كَانَ مِنَ الْمُقَرَّبِينَ
Faamma in kana minaalmuqarrabeen
Swahili
Basi akiwa miongoni mwa walio karibishwa,
|
Ayah 56:89 الأية
فَرَوْحٌ وَرَيْحَانٌ وَجَنَّتُ نَعِيمٍ
Farawhun warayhanun wajannatunaAAeem
Swahili
Basi ni raha, na manukato, na Bustani zenye neema.
|
Ayah 56:90 الأية
وَأَمَّا إِن كَانَ مِنْ أَصْحَابِ الْيَمِينِ
Waamma in kana min as-habialyameen
Swahili
Na akiwa katika watu wa upande wa kulia,
|
Ayah 56:91 الأية
فَسَلَامٌ لَّكَ مِنْ أَصْحَابِ الْيَمِينِ
Fasalamun laka min as-habialyameen
Swahili
Basi ni Salamu kwako uliye miongoni mwa watu wa upande wa kulia.
|
Ayah 56:92 الأية
وَأَمَّا إِن كَانَ مِنَ الْمُكَذِّبِينَ الضَّالِّينَ
Waamma in kana mina almukaththibeenaaddalleen
Swahili
Na ama akiwa katika walio kadhibisha wapotovu,
|
Ayah 56:93 الأية
فَنُزُلٌ مِّنْ حَمِيمٍ
Fanuzulun min hameem
Swahili
Basi karamu yake ni maji yanayo chemka,
|
Ayah 56:94 الأية
وَتَصْلِيَةُ جَحِيمٍ
Watasliyatu jaheem
Swahili
Na kutiwa Motoni.
|
Ayah 56:95 الأية
إِنَّ هَٰذَا لَهُوَ حَقُّ الْيَقِينِ
Inna hatha lahuwa haqqualyaqeen
Swahili
Hakika hii ndiyo haki yenye yakini.
|
Ayah 56:96 الأية
فَسَبِّحْ بِاسْمِ رَبِّكَ الْعَظِيمِ
Fasabbih bismi rabbika alAAatheem
Swahili
Basi litakase jina la Mola wako Mlezi aliye Mkubwa.
|
©
EsinIslam.Com Designed & produced by The Awqaf London. Please pray for us
|