Prev  

56. Surah Al-Wâqi'ah سورة الواقعة

  Next  




1st Ayah  1  الأية ١الأولي
بِسْم ِ اللهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ
إِذَا وَقَعَتِ الْوَاقِعَةُ
Itha waqaAAati alwaqiAAat

Swahili
 
Litakapo tukia hilo Tukio

Ayah  56:2  الأية
لَيْسَ لِوَقْعَتِهَا كَاذِبَةٌ
Laysa liwaqAAatiha kathiba

Swahili
 
Hapana cha kukanusha kutukia kwake.

Ayah  56:3  الأية
خَافِضَةٌ رَّافِعَةٌ
Khafidatun rafiAAa

Swahili
 
Literemshalo linyanyualo,

Ayah  56:4  الأية
إِذَا رُجَّتِ الْأَرْضُ رَجًّا
Itha rujjati al-ardu rajja

Swahili
 
Itakapo tikiswa ardhi kwa mtikiso,

Ayah  56:5  الأية
وَبُسَّتِ الْجِبَالُ بَسًّا
Wabussati aljibalu bassa

Swahili
 
Na milima itapo sagwasagwa,

Ayah  56:6  الأية
فَكَانَتْ هَبَاءً مُّنبَثًّا
Fakanat habaan munbaththa

Swahili
 
Iwe mavumbi yanayo peperushwa,

Ayah  56:7  الأية
وَكُنتُمْ أَزْوَاجًا ثَلَاثَةً
Wakuntum azwajan thalatha

Swahili
 
Na nyinyi mtakuwa namna tatu:-

Ayah  56:8  الأية
فَأَصْحَابُ الْمَيْمَنَةِ مَا أَصْحَابُ الْمَيْمَنَةِ
Faas-habu almaymanati maas-habu almaymanat

Swahili
 
Basi watakuwepo wa kuliani; je, ni wepi wa kuliani?

Ayah  56:9  الأية
وَأَصْحَابُ الْمَشْأَمَةِ مَا أَصْحَابُ الْمَشْأَمَةِ
Waas-habu almash-amati maas-habu almash-amat

Swahili
 
Na wa kushotoni; je, ni wepi wa kushotoni?

Ayah  56:10  الأية
وَالسَّابِقُونَ السَّابِقُونَ
Wassabiqoona assabiqoon

Swahili
 
Na wa mbele watakuwa mbele.

Ayah  56:11  الأية
أُولَٰئِكَ الْمُقَرَّبُونَ
Ola-ika almuqarraboon

Swahili
 
Hao ndio watakao karibishwa

Ayah  56:12  الأية
فِي جَنَّاتِ النَّعِيمِ
Fee jannati annaAAeem

Swahili
 
Katika Bustani zenye neema.

Ayah  56:13  الأية
ثُلَّةٌ مِّنَ الْأَوَّلِينَ
Thullatun mina al-awwaleen

Swahili
 
Fungu kubwa katika wa mwanzo,

Ayah  56:14  الأية
وَقَلِيلٌ مِّنَ الْآخِرِينَ
Waqaleelun mina al-akhireena

Swahili
 
Na wachache katika wa mwisho.

Ayah  56:15  الأية
عَلَىٰ سُرُرٍ مَّوْضُونَةٍ
AAala sururin mawdoona

Swahili
 
Watakuwa juu ya viti vya fakhari vilivyo tonewa.

Ayah  56:16  الأية
مُّتَّكِئِينَ عَلَيْهَا مُتَقَابِلِينَ
Muttaki-eena AAalayha mutaqabileen

Swahili
 
Wakiviegemea wakielekeana.

Ayah  56:17  الأية
يَطُوفُ عَلَيْهِمْ وِلْدَانٌ مُّخَلَّدُونَ
Yatoofu AAalayhim wildanunmukhalladoon

Swahili
 
Wakitumikiwa na wavulana wa ujana wa milele,

Ayah  56:18  الأية
بِأَكْوَابٍ وَأَبَارِيقَ وَكَأْسٍ مِّن مَّعِينٍ
Bi-akwabin waabareeqa waka/sinmin maAAeen

Swahili
 
Kwa vikombe na mabirika na bilauri za vinywaji kutoka chemchem safi.

Ayah  56:19  الأية
لَّا يُصَدَّعُونَ عَنْهَا وَلَا يُنزِفُونَ
La yusaddaAAoona AAanhawala yunzifoon

Swahili
 
Hawataumwa kichwa kwa vinywaji hivyo wala hawatoleweshwa.

Ayah  56:20  الأية
وَفَاكِهَةٍ مِّمَّا يَتَخَيَّرُونَ
Wafakihatin mimmayatakhayyaroon

Swahili
 
Na matunda wayapendayo,

Ayah  56:21  الأية
وَلَحْمِ طَيْرٍ مِّمَّا يَشْتَهُونَ
Walahmi tayrin mimmayashtahoon

Swahili
 
Na nyama za ndege kama wanavyo tamani.

Ayah  56:22  الأية
وَحُورٌ عِينٌ
Wahoorun AAeen

Swahili
 
Na Mahurulaini,

Ayah  56:23  الأية
كَأَمْثَالِ اللُّؤْلُؤِ الْمَكْنُونِ
Kaamthali allu/lui almaknoon

Swahili
 
Walio kama mfano wa lulu zilio hifadhiwa.

Ayah  56:24  الأية
جَزَاءً بِمَا كَانُوا يَعْمَلُونَ
Jazaan bima kanooyaAAmaloon

Swahili
 
Ni malipo kwa waliyo kuwa wakiyatenda.

Ayah  56:25  الأية
لَا يَسْمَعُونَ فِيهَا لَغْوًا وَلَا تَأْثِيمًا
La yasmaAAoona feeha laghwanwala ta/theema

Swahili
 
Humo hawatasikia porojo wala maneno ya dhambi,

Ayah  56:26  الأية
إِلَّا قِيلًا سَلَامًا سَلَامًا
Illa qeelan salaman salama

Swahili
 
Isipo kuwa maneno ya Salama, Salama.

Ayah  56:27  الأية
وَأَصْحَابُ الْيَمِينِ مَا أَصْحَابُ الْيَمِينِ
Waas-habu alyameeni maas-habu alyameen

Swahili
 
Na wale wa mkono wa kulia, ni yepi yatakuwa ya wa kuliani?

Ayah  56:28  الأية
فِي سِدْرٍ مَّخْضُودٍ
Fee sidrin makhdood

Swahili
 
Katika mikunazi isiyo na miba,

Ayah  56:29  الأية
وَطَلْحٍ مَّنضُودٍ
Watalhin mandood

Swahili
 
Na migomba iliyo pangiliwa,

Ayah  56:30  الأية
وَظِلٍّ مَّمْدُودٍ
Wathillin mamdood

Swahili
 
Na kivuli kilicho tanda,

Ayah  56:31  الأية
وَمَاءٍ مَّسْكُوبٍ
Wama-in maskoob

Swahili
 
Na maji yanayo miminika,

Ayah  56:32  الأية
وَفَاكِهَةٍ كَثِيرَةٍ
Wafakihatin katheera

Swahili
 
Na matunda mengi,

Ayah  56:33  الأية
لَّا مَقْطُوعَةٍ وَلَا مَمْنُوعَةٍ
La maqtooAAatin walamamnooAAa

Swahili
 
Hayatindikii wala hayakatazwi,

Ayah  56:34  الأية
وَفُرُشٍ مَّرْفُوعَةٍ
Wafurushin marfooAAa

Swahili
 
Na matandiko yaliyo nyanyuliwa.

Ayah  56:35  الأية
إِنَّا أَنشَأْنَاهُنَّ إِنشَاءً
Inna ansha/nahunna inshaa

Swahili
 
Hakika Sisi tutawaumba (Mahurulaini) upya,

Ayah  56:36  الأية
فَجَعَلْنَاهُنَّ أَبْكَارًا
FajaAAalnahunna abkara

Swahili
 
Na tutawafanya vijana,

Ayah  56:37  الأية
عُرُبًا أَتْرَابًا
AAuruban atraba

Swahili
 
Wanapendana na waume zao, hirimu moja.

Ayah  56:38  الأية
لِّأَصْحَابِ الْيَمِينِ
Li-as-habi alyameen

Swahili
 
Kwa ajili ya watu wa kuliani.

Ayah  56:39  الأية
ثُلَّةٌ مِّنَ الْأَوَّلِينَ
Thullatun mina al-awwaleen

Swahili
 
Fungu kubwa katika wa mwanzo,

Ayah  56:40  الأية
وَثُلَّةٌ مِّنَ الْآخِرِينَ
Wathullatun mina al-akhireen

Swahili
 
Na fungu kubwa katika wa mwisho.

Ayah  56:41  الأية
وَأَصْحَابُ الشِّمَالِ مَا أَصْحَابُ الشِّمَالِ
Waas-habu ashshimalima as-habu ashshimal

Swahili
 
Na watu wa kushotoni; je ni yepi ya wa kushotoni?

Ayah  56:42  الأية
فِي سَمُومٍ وَحَمِيمٍ
Fee samoomin wahameem

Swahili
 
Katika upepo wa moto, na maji yanayo chemka,

Ayah  56:43  الأية
وَظِلٍّ مِّن يَحْمُومٍ
Wathillin min yahmoom

Swahili
 
Na kivuli cha moshi mweusi,

Ayah  56:44  الأية
لَّا بَارِدٍ وَلَا كَرِيمٍ
La baridin wala kareem

Swahili
 
Si cha kuburudisha wala kustarehesha.

Ayah  56:45  الأية
إِنَّهُمْ كَانُوا قَبْلَ ذَٰلِكَ مُتْرَفِينَ
Innahum kanoo qabla thalikamutrafeen

Swahili
 
Hakika hao walikuwa kabla ya haya wakiishi maisha ya anasa.

Ayah  56:46  الأية
وَكَانُوا يُصِرُّونَ عَلَى الْحِنثِ الْعَظِيمِ
Wakanoo yusirroona AAalaalhinthi alAAatheem

Swahili
 
Na walikuwa wakishikilia kufanya madhambi makubwa,

Ayah  56:47  الأية
وَكَانُوا يَقُولُونَ أَئِذَا مِتْنَا وَكُنَّا تُرَابًا وَعِظَامًا أَإِنَّا لَمَبْعُوثُونَ
Wakanoo yaqooloona a-itha mitnawakunna turaban waAAithamana-inna lamabAAoothoon

Swahili
 
Na walikuwa wakisema: Tutakapo kufa na tukawa udongo na mafupa, ati ndio tutafufuliwa?

Ayah  56:48  الأية
أَوَآبَاؤُنَا الْأَوَّلُونَ
Awa abaona al-awwaloon

Swahili
 
Au baba zetu wa zamani?

Ayah  56:49  الأية
قُلْ إِنَّ الْأَوَّلِينَ وَالْآخِرِينَ
Qul inna al-awwaleena wal-akhireen

Swahili
 
Sema: Hakika wa zamani na wa mwisho

Ayah  56:50  الأية
لَمَجْمُوعُونَ إِلَىٰ مِيقَاتِ يَوْمٍ مَّعْلُومٍ
LamajmooAAoona ila meeqatiyawmin maAAloom

Swahili
 
Bila ya shaka watakusanywa kwa wakati wa siku maalumu.

Ayah  56:51  الأية
ثُمَّ إِنَّكُمْ أَيُّهَا الضَّالُّونَ الْمُكَذِّبُونَ
Thumma innakum ayyuha addalloonaalmukaththiboon

Swahili
 
Kisha nyinyi, mlio potea, mnao kanusha,

Ayah  56:52  الأية
لَآكِلُونَ مِن شَجَرٍ مِّن زَقُّومٍ
Laakiloona min shajarin min zaqqoom

Swahili
 
Kwa yakini mtakula mti wa Zaqqumu.

Ayah  56:53  الأية
فَمَالِئُونَ مِنْهَا الْبُطُونَ
Famali-oona minha albutoon

Swahili
 
Na kwa mti huo mtajaza matumbo.

Ayah  56:54  الأية
فَشَارِبُونَ عَلَيْهِ مِنَ الْحَمِيمِ
Fashariboona AAalayhi mina alhameem

Swahili
 
Na juu yake mtakunywa maji yanayo chemka.

Ayah  56:55  الأية
فَشَارِبُونَ شُرْبَ الْهِيمِ
Fashariboona shurba alheem

Swahili
 
Tena mtakunywa kama wanavyo kunywa ngamia wenye kiu.

Ayah  56:56  الأية
هَٰذَا نُزُلُهُمْ يَوْمَ الدِّينِ
Hatha nuzuluhum yawma addeen

Swahili
 
Hiyo ndiyo karamu yao Siku ya Malipo.

Ayah  56:57  الأية
نَحْنُ خَلَقْنَاكُمْ فَلَوْلَا تُصَدِّقُونَ
Nahnu khalaqnakum falawlatusaddiqoon

Swahili
 
Sisi tumekuumbeni; basi hamsadiki?

Ayah  56:58  الأية
أَفَرَأَيْتُم مَّا تُمْنُونَ
Afaraaytum ma tumnoon

Swahili
 
Je! Mnaiona mbegu ya uzazi mnayo idondokeza?

Ayah  56:59  الأية
أَأَنتُمْ تَخْلُقُونَهُ أَمْ نَحْنُ الْخَالِقُونَ
Aantum takhluqoonahu am nahnu alkhaliqoon

Swahili
 
Je! Mnaiumba nyinyi, au ni Sisi ndio Waumbaji?

Ayah  56:60  الأية
نَحْنُ قَدَّرْنَا بَيْنَكُمُ الْمَوْتَ وَمَا نَحْنُ بِمَسْبُوقِينَ
Nahnu qaddarna baynakumualmawta wama nahnu bimasbooqeen

Swahili
 
Sisi tumekuwekeeni mauti; na wala Sisi hatushindwi

Ayah  56:61  الأية
عَلَىٰ أَن نُّبَدِّلَ أَمْثَالَكُمْ وَنُنشِئَكُمْ فِي مَا لَا تَعْلَمُونَ
AAala an nubaddila amthalakumwanunshi-akum fee ma la taAAlamoon

Swahili
 
Kuwaleta wengine badala yenu na kukuumbeni nyinyi kwa umbo msilo lijua.

Ayah  56:62  الأية
وَلَقَدْ عَلِمْتُمُ النَّشْأَةَ الْأُولَىٰ فَلَوْلَا تَذَكَّرُونَ
Walaqad AAalimtumu annash-ata al-oolafalawla tathakkaroon

Swahili
 
Na bila ya shaka mlikwisha jua umbo la kwanza, basi kwa nini hamkumbuki?

Ayah  56:63  الأية
أَفَرَأَيْتُم مَّا تَحْرُثُونَ
Afaraaytum ma tahruthoon

Swahili
 
Je! Mnaona makulima mnayo yapanda?

Ayah  56:64  الأية
أَأَنتُمْ تَزْرَعُونَهُ أَمْ نَحْنُ الزَّارِعُونَ
Aantum tazraAAoonahu am nahnu azzariAAoon

Swahili
 
Je! Ni nyinyi mnayo yaotesha au ni Sisi ndio wenye kuotesha?

Ayah  56:65  الأية
لَوْ نَشَاءُ لَجَعَلْنَاهُ حُطَامًا فَظَلْتُمْ تَفَكَّهُونَ
Law nashao lajaAAalnahu hutamanfathaltum tafakkahoon

Swahili
 
Tungeli taka tungeli yafanya yakawa mapepe, mkabaki mnastaajabu,

Ayah  56:66  الأية
إِنَّا لَمُغْرَمُونَ
Inna lamughramoon

Swahili
 
Mkisema: Hakika sisi tumegharimika;

Ayah  56:67  الأية
بَلْ نَحْنُ مَحْرُومُونَ
Bal nahnu mahroomoon

Swahili
 
Bali sisi tumenyimwa.

Ayah  56:68  الأية
أَفَرَأَيْتُمُ الْمَاءَ الَّذِي تَشْرَبُونَ
Afaraaytumu almaa allatheetashraboon

Swahili
 
Je! Mnayaona maji mnayo yanywa?

Ayah  56:69  الأية
أَأَنتُمْ أَنزَلْتُمُوهُ مِنَ الْمُزْنِ أَمْ نَحْنُ الْمُنزِلُونَ
Aantum anzaltumoohu mina almuzni am nahnualmunziloon

Swahili
 
Je! Ni nyinyi mnayo yateremsha kutoka mawinguni au ni Sisi ndio wenye kuyateremsha?

Ayah  56:70  الأية
لَوْ نَشَاءُ جَعَلْنَاهُ أُجَاجًا فَلَوْلَا تَشْكُرُونَ
Law nashao jaAAalnahu ojajanfalawla tashkuroon

Swahili
 
Tungeli penda tungeli yafanya ya chumvi. Basi mbona hamshukuru?

Ayah  56:71  الأية
أَفَرَأَيْتُمُ النَّارَ الَّتِي تُورُونَ
Afaraaytumu annara allateetooroon

Swahili
 
Je! Mnauona moto mnao uwasha?

Ayah  56:72  الأية
أَأَنتُمْ أَنشَأْتُمْ شَجَرَتَهَا أَمْ نَحْنُ الْمُنشِئُونَ
Aantum ansha/tum shajarataha am nahnualmunshi-oon

Swahili
 
Ni nyinyi mlio uumba mti wake au Sisi ndio Waumbaji?

Ayah  56:73  الأية
نَحْنُ جَعَلْنَاهَا تَذْكِرَةً وَمَتَاعًا لِّلْمُقْوِينَ
Nahnu jaAAalnaha tathkiratanwamataAAan lilmuqween

Swahili
 
Sisi tumeufanya uwe ni ukumbusho na manufaa kwa walioko nyikani.

Ayah  56:74  الأية
فَسَبِّحْ بِاسْمِ رَبِّكَ الْعَظِيمِ
Fasabbih bismi rabbika alAAatheem

Swahili
 
Basi litakase jina la Mola wako Mlezi aliye Mkuu.

Ayah  56:75  الأية
فَلَا أُقْسِمُ بِمَوَاقِعِ النُّجُومِ
Fala oqsimu bimawaqiAAi annujoom

Swahili
 
Basi naapa kwa maanguko ya nyota,

Ayah  56:76  الأية
وَإِنَّهُ لَقَسَمٌ لَّوْ تَعْلَمُونَ عَظِيمٌ
Wa-innahu laqasamun law taAAlamoona AAatheem

Swahili
 
Na hakika bila ya shaka hichi ni kiapo kikubwa, laiti mngeli jua!

Ayah  56:77  الأية
إِنَّهُ لَقُرْآنٌ كَرِيمٌ
Innahu laqur-anun kareem

Swahili
 
Hakika hii bila ya shaka ni Qur'ani Tukufu,

Ayah  56:78  الأية
فِي كِتَابٍ مَّكْنُونٍ
Fee kitabin maknoon

Swahili
 
Katika Kitabu kilicho hifadhiwa.

Ayah  56:79  الأية
لَّا يَمَسُّهُ إِلَّا الْمُطَهَّرُونَ
La yamassuhu illa almutahharoon

Swahili
 
Hapana akigusaye ila walio takaswa.

Ayah  56:80  الأية
تَنزِيلٌ مِّن رَّبِّ الْعَالَمِينَ
Tanzeelun min rabbi alAAalameen

Swahili
 
Ni uteremsho unao toka kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.

Ayah  56:81  الأية
أَفَبِهَٰذَا الْحَدِيثِ أَنتُم مُّدْهِنُونَ
Afabihatha alhadeethi antummudhinoon

Swahili
 
Ni maneno haya ndiyo nyinyi mnayapuuza?

Ayah  56:82  الأية
وَتَجْعَلُونَ رِزْقَكُمْ أَنَّكُمْ تُكَذِّبُونَ
WatajAAaloona rizqakum annakum tukaththiboon

Swahili
 
Na badala ya kushukuru kwa riziki yenu mnafanya kuwa mnakadhibisha?

Ayah  56:83  الأية
فَلَوْلَا إِذَا بَلَغَتِ الْحُلْقُومَ
Falawla itha balaghati alhulqoom

Swahili
 
Yawaje basi itakapo fika roho kwenye koo,

Ayah  56:84  الأية
وَأَنتُمْ حِينَئِذٍ تَنظُرُونَ
Waantum heena-ithin tanthuroona

Swahili
 
Na nyinyi wakati huo mnatazama!

Ayah  56:85  الأية
وَنَحْنُ أَقْرَبُ إِلَيْهِ مِنكُمْ وَلَٰكِن لَّا تُبْصِرُونَ
Wanahnu aqrabu ilayhi minkum walakinla tubsiroon

Swahili
 
Na Sisi tuko karibu zaidi naye kuliko nyinyi.

Ayah  56:86  الأية
فَلَوْلَا إِن كُنتُمْ غَيْرَ مَدِينِينَ
Falawla in kuntum ghayra madeeneen

Swahili
 
Na lau kuwa nyinyi hamumo katika mamlaka yangu,

Ayah  56:87  الأية
تَرْجِعُونَهَا إِن كُنتُمْ صَادِقِينَ
TarjiAAoonaha in kuntum sadiqeen

Swahili
 
Kwanini hamuirudishi hiyo roho, ikiwa nyinyi mnasema kweli?

Ayah  56:88  الأية
فَأَمَّا إِن كَانَ مِنَ الْمُقَرَّبِينَ
Faamma in kana minaalmuqarrabeen

Swahili
 
Basi akiwa miongoni mwa walio karibishwa,

Ayah  56:89  الأية
فَرَوْحٌ وَرَيْحَانٌ وَجَنَّتُ نَعِيمٍ
Farawhun warayhanun wajannatunaAAeem

Swahili
 
Basi ni raha, na manukato, na Bustani zenye neema.

Ayah  56:90  الأية
وَأَمَّا إِن كَانَ مِنْ أَصْحَابِ الْيَمِينِ
Waamma in kana min as-habialyameen

Swahili
 
Na akiwa katika watu wa upande wa kulia,

Ayah  56:91  الأية
فَسَلَامٌ لَّكَ مِنْ أَصْحَابِ الْيَمِينِ
Fasalamun laka min as-habialyameen

Swahili
 
Basi ni Salamu kwako uliye miongoni mwa watu wa upande wa kulia.

Ayah  56:92  الأية
وَأَمَّا إِن كَانَ مِنَ الْمُكَذِّبِينَ الضَّالِّينَ
Waamma in kana mina almukaththibeenaaddalleen

Swahili
 
Na ama akiwa katika walio kadhibisha wapotovu,

Ayah  56:93  الأية
فَنُزُلٌ مِّنْ حَمِيمٍ
Fanuzulun min hameem

Swahili
 
Basi karamu yake ni maji yanayo chemka,

Ayah  56:94  الأية
وَتَصْلِيَةُ جَحِيمٍ
Watasliyatu jaheem

Swahili
 
Na kutiwa Motoni.

Ayah  56:95  الأية
إِنَّ هَٰذَا لَهُوَ حَقُّ الْيَقِينِ
Inna hatha lahuwa haqqualyaqeen

Swahili
 
Hakika hii ndiyo haki yenye yakini.

Ayah  56:96  الأية
فَسَبِّحْ بِاسْمِ رَبِّكَ الْعَظِيمِ
Fasabbih bismi rabbika alAAatheem

Swahili
 
Basi litakase jina la Mola wako Mlezi aliye Mkubwa.





© EsinIslam.Com Designed & produced by The Awqaf London. Please pray for us