1st Ayah 1 الأية ١الأوليبِسْم ِ اللهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ
سَبَّحَ لِلَّهِ مَا فِي السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ ۖ وَهُوَ الْعَزِيزُ الْحَكِيمُ
Sabbaha lillahi ma fee assamawatiwal-ardi wahuwa alAAazeezu alhakeem
Swahili
Kinamsabihi kumtakasa Mwenyezi Mungu kila kiliomo ndani ya mbingu na ardhi. Na
Yeye ndiye Mwenye nguvu, Mwenye hikima.
|
Ayah 57:2 الأية
لَهُ مُلْكُ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ ۖ يُحْيِي وَيُمِيتُ ۖ وَهُوَ عَلَىٰ كُلِّ
شَيْءٍ قَدِيرٌ
Lahu mulku assamawatiwal-ardi yuhyee wayumeetu wahuwa AAalakulli shay-in qadeer
Swahili
Yeye ndiye Mwenye ufalme wa mbingu na ardhi. Anahuisha na anafisha. Na Yeye ni
Mwenye uweza wa kila kitu.
|
Ayah 57:3 الأية
هُوَ الْأَوَّلُ وَالْآخِرُ وَالظَّاهِرُ وَالْبَاطِنُ ۖ وَهُوَ بِكُلِّ شَيْءٍ
عَلِيمٌ
Huwa al-awwalu wal-akhiru waththahiruwalbatinu wahuwa bikulli shay-in AAaleem
Swahili
Yeye ndiye wa Mwanzo na ndiye wa Mwisho, naye ndiye wa Dhaahiri na wa Siri, naye
ndiye Mjuzi wa kila kitu.
|
Ayah 57:4 الأية
هُوَ الَّذِي خَلَقَ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضَ فِي سِتَّةِ أَيَّامٍ ثُمَّ
اسْتَوَىٰ عَلَى الْعَرْشِ ۚ يَعْلَمُ مَا يَلِجُ فِي الْأَرْضِ وَمَا يَخْرُجُ
مِنْهَا وَمَا يَنزِلُ مِنَ السَّمَاءِ وَمَا يَعْرُجُ فِيهَا ۖ وَهُوَ مَعَكُمْ
أَيْنَ مَا كُنتُمْ ۚ وَاللهُ بِمَا تَعْمَلُونَ بَصِيرٌ
Huwa allathee khalaqa assamawatiwal-arda fee sittati ayyamin thumma istawaAAala
alAAarshi yaAAlamu ma yaliju fee al-ardiwama yakhruju minha wama yanzilu mina
assama-iwama yaAAruju feeha wahuwa maAAakum ayna makuntum wallahu bima
taAAmaloona baseer
Swahili
Yeye ndiye aliye ziumba mbingu na ardhi katika siku sita; kisha akakaa vyema juu
ya enzi. Anayajua yanayo ingia katika ardhi na yanayo toka humo, na yanayo
teremka kutoka mbinguni, na yanayo panda humo. Naye yu pamoja nanyi popote
mlipo. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kuyaona mnayo yatenda.
|
Ayah 57:5 الأية
لَّهُ مُلْكُ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ ۚ وَإِلَى اللهِ تُرْجَعُ الْأُمُورُ
Lahu mulku assamawatiwal-ardi wa-ila Allahi turjaAAual-omoor
Swahili
Ufalme wa mbingu na ardhi ni wake. Na mambo yote yanarejeshwa kwa Mwenyezi
Mungu.
|
Ayah 57:6 الأية
يُولِجُ اللَّيْلَ فِي النَّهَارِ وَيُولِجُ النَّهَارَ فِي اللَّيْلِ ۚ وَهُوَ
عَلِيمٌ بِذَاتِ الصُّدُورِ
Yooliju allayla fee annahariwayooliju annahara fee allayi wahuwa AAaleemun
bithatiassudoor
Swahili
Anaingiza usiku katika mchana, na anaingiza mchana katika usiku. Na Yeye ni
Mwenye kuyajua yaliomo vifuani.
|
Ayah 57:7 الأية
آمِنُوا بِاللهِ وَرَسُولِهِ وَأَنفِقُوا مِمَّا جَعَلَكُم مُّسْتَخْلَفِينَ
فِيهِ ۖ فَالَّذِينَ آمَنُوا مِنكُمْ وَأَنفَقُوا لَهُمْ أَجْرٌ كَبِيرٌ
Aminoo billahiwarasoolihi waanfiqoo mimma jaAAalakum mustakhlafeenafeehi
fallatheena amanoo minkum waanfaqoolahum ajrun kabeer
Swahili
Muaminini Mwenyezi Mungu na Mtume wake; na toeni katika alivyo kufanyeni nyinyi
kuwa ni waangalizi wake. Basi walio amini miongoni mwenu, na wakatoa, wana
malipo makubwa.
|
Ayah 57:8 الأية
وَمَا لَكُمْ لَا تُؤْمِنُونَ بِاللهِ ۙ وَالرَّسُولُ يَدْعُوكُمْ لِتُؤْمِنُوا
بِرَبِّكُمْ وَقَدْ أَخَذَ مِيثَاقَكُمْ إِن كُنتُم مُّؤْمِنِينَ
Wama lakum la tu/minoona billahiwarrasoolu yadAAookum litu/minoo birabbikum
waqad akhathameethaqakum in kuntum mu/mineen
Swahili
Na mna nini hata hamumuamini Mwenyezi Mungu na hali Mtume anakuiteni mumuamini
Mola wenu Mlezi? Naye amekwisha chukua ahadi yenu, ikiwa nyinyi ni Waumini.
|
Ayah 57:9 الأية
هُوَ الَّذِي يُنَزِّلُ عَلَىٰ عَبْدِهِ آيَاتٍ بَيِّنَاتٍ لِّيُخْرِجَكُم مِّنَ
الظُّلُمَاتِ إِلَى النُّورِ ۚ وَإِنَّ اللهَ بِكُمْ لَرَءُوفٌ رَّحِيمٌ
Huwa allathee yunazzilu AAalaAAabdihi ayatin bayyinatin liyukhrijakummina
aththulumati ila annooriwa-inna Allaha bikum laraoofun raheem
Swahili
Yeye ndiye anaye mteremshia mja wake Aya zinazo bainisha wazi ili akutoeni
gizani muingie kwenye nuru. Na hakika Mwenyezi Mungu kwenu ni Mpole, Mwenye
kurehemu.
|
Ayah 57:10 الأية
وَمَا لَكُمْ أَلَّا تُنفِقُوا فِي سَبِيلِ اللهِ وَلِلَّهِ مِيرَاثُ
السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ ۚ لَا يَسْتَوِي مِنكُم مَّنْ أَنفَقَ مِن قَبْلِ
الْفَتْحِ وَقَاتَلَ ۚ أُولَٰئِكَ أَعْظَمُ دَرَجَةً مِّنَ الَّذِينَ أَنفَقُوا مِن
بَعْدُ وَقَاتَلُوا ۚ وَكُلًّا وَعَدَ اللهُ الْحُسْنَىٰ ۚ وَاللهُ بِمَا
تَعْمَلُونَ خَبِيرٌ
Wama lakum alla tunfiqoo feesabeeli Allahi walillahi meerathu assamawatiwal-ardi
la yastawee minkum man anfaqa minqabli alfathi waqatala ola-ika
aAAthamudarajatan mina allatheena anfaqoo min baAAdu waqataloowakullan waAAada
Allahu alhusna wallahubima taAAmaloona khabeer
Swahili
Na mna nini hata hamtoi katika Njia ya Mwenyezi Mungu, na hali urithi wa mbingu
na ardhi ni wa Mwenyezi Mungu? Hawawi sawa miongoni mwenu wenye kutoa kabla ya
Ushindi na wakapigana vita. Hao wana daraja kubwa zaidi kuliko wale ambao walio
toa baadae na wakapigana. Na wote hao Mwenyezi Mungu amewaahidia wema. Na
Mwenyezi Mungu anazo khabari za mnayo yatenda.
|
Ayah 57:11 الأية
مَّن ذَا الَّذِي يُقْرِضُ اللهَ قَرْضًا حَسَنًا فَيُضَاعِفَهُ لَهُ وَلَهُ
أَجْرٌ كَرِيمٌ
Man tha allathee yuqriduAllaha qardan hasanan fayudaAAifahulahu walahu ajrun
kareem
Swahili
Ni nani atakaye mkopesha Mwenyezi Mungu mkopo mwema, ili amrudishie mardufu, na
apate malipo ya ukarimu.
|
Ayah 57:12 الأية
يَوْمَ تَرَى الْمُؤْمِنِينَ وَالْمُؤْمِنَاتِ يَسْعَىٰ نُورُهُم بَيْنَ
أَيْدِيهِمْ وَبِأَيْمَانِهِم بُشْرَاكُمُ الْيَوْمَ جَنَّاتٌ تَجْرِي مِن
تَحْتِهَا الْأَنْهَارُ خَالِدِينَ فِيهَا ۚ ذَٰلِكَ هُوَ الْفَوْزُ الْعَظِيمُ
Yawma tara almu/mineena walmu/minatiyasAAa nooruhum bayna aydeehim
wabi-aymanihim bushrakumualyawma jannatun tajree min tahtiha al-anharukhalideena
feeha thalika huwa alfawzu alAAatheem
Swahili
Siku utakapo waona Waumini wanaume na Waumini wanawake, nuru yao iko mbele yao,
na kuliani kwao: Furaha yenu leo - Bustani zipitazo mito kati yake mtakaa humo
milele. Huko ndiko kufuzu kukubwa.
|
Ayah 57:13 الأية
يَوْمَ يَقُولُ الْمُنَافِقُونَ وَالْمُنَافِقَاتُ لِلَّذِينَ آمَنُوا انظُرُونَا
نَقْتَبِسْ مِن نُّورِكُمْ قِيلَ ارْجِعُوا وَرَاءَكُمْ فَالْتَمِسُوا نُورًا
فَضُرِبَ بَيْنَهُم بِسُورٍ لَّهُ بَابٌ بَاطِنُهُ فِيهِ الرَّحْمَةُ وَظَاهِرُهُ
مِن قِبَلِهِ الْعَذَابُ
Yawma yaqoolu almunafiqoona walmunafiqatulillatheena amanoo onthuroonanaqtabis
min noorikum qeela irjiAAoo waraakum faltamisoonooran faduriba baynahum bisoorin
lahu babun batinuhufeehi arrahmatu wathahiruhumin qibalihi alAAathab
Swahili
Siku wanaafiki wanaume na wanaafiki wanawake watapo waambia walio amini:
Tungojeni ili tupate mwangaza katika nuru yenu. Waambiwe: Rejeeni nyuma yenu
mkaitafute nuru! Utiwe baina yao ukuta wenye mlango - ndani yake mna rehema, na
nje upande wake wa mbele kuna adhabu.
|
Ayah 57:14 الأية
يُنَادُونَهُمْ أَلَمْ نَكُن مَّعَكُمْ ۖ قَالُوا بَلَىٰ وَلَٰكِنَّكُمْ فَتَنتُمْ
أَنفُسَكُمْ وَتَرَبَّصْتُمْ وَارْتَبْتُمْ وَغَرَّتْكُمُ الْأَمَانِيُّ حَتَّىٰ
جَاءَ أَمْرُ اللهِ وَغَرَّكُم بِاللهِ الْغَرُورُ
Yunadoonahum alam nakun maAAakum qaloobala walakinnakum fatantum anfusakum
watarabbastumwartabtum wagharratkumu al-amaniyyu hattajaa amru Allahi
wagharrakum billahialgharoor
Swahili
Watawaita wawaambie: Kwani vile hatukuwa pamoja nanyi? Watawaambia: Ndiyo,
lakini mlijifitini wenyewe, na mkasitasita, na mkatia shaka, na matamanio ya
nafsi zenu yakakudanganyeni. mpaka ilipo kuja amri ya Mwenyezi Mungu, na
mdanganyifu akakudanganyeni msimfuate Mwenyezi Mungu.
|
Ayah 57:15 الأية
فَالْيَوْمَ لَا يُؤْخَذُ مِنكُمْ فِدْيَةٌ وَلَا مِنَ الَّذِينَ كَفَرُوا ۚ
مَأْوَاكُمُ النَّارُ ۖ هِيَ مَوْلَاكُمْ ۖ وَبِئْسَ الْمَصِيرُ
Falyawma la yu/khathuminkum fidyatun wala mina allatheena kafaroo
ma/wakumuannaru hiya mawlakum wabi/sa almaseer
Swahili
Basi leo haitapokelewa kwenu fidia, wala kwa wale walio kufuru. Makaazi yenu ni
Motoni, ndio bora kwenu; na ni marejeo maovu yalioje!
|
Ayah 57:16 الأية
أَلَمْ يَأْنِ لِلَّذِينَ آمَنُوا أَن تَخْشَعَ قُلُوبُهُمْ لِذِكْرِ اللهِ وَمَا
نَزَلَ مِنَ الْحَقِّ وَلَا يَكُونُوا كَالَّذِينَ أُوتُوا الْكِتَابَ مِن قَبْلُ
فَطَالَ عَلَيْهِمُ الْأَمَدُ فَقَسَتْ قُلُوبُهُمْ ۖ وَكَثِيرٌ مِّنْهُمْ
فَاسِقُونَ
Alam ya/ni lillatheena amanooan takhshaAAa quloobuhum lithikri Allahi wamanazala
mina alhaqqi wala yakoonoo kallatheenaootoo alkitaba min qablu fatala AAalayhimu
al-amadufaqasat quloobuhum wakatheerun minhum fasiqoon
Swahili
Je! Wakati haujafika bado kwa walio amini zikanyenyekea nyoyo zao kwa kumkumbuka
Mwenyezi Mungu na haki iliyo teremka? Wala wasiwe kama walio pewa Kitabu kabla
yao, muda wao ukawa mrefu, kwa hivyo nyoyo zao zikawa ngumu, na wengi wao wakawa
wapotovu.
|
Ayah 57:17 الأية
اعْلَمُوا أَنَّ اللهَ يُحْيِي الْأَرْضَ بَعْدَ مَوْتِهَا ۚ قَدْ بَيَّنَّا
لَكُمُ الْآيَاتِ لَعَلَّكُمْ تَعْقِلُونَ
IAAlamoo anna Allaha yuhyeeal-arda baAAda mawtiha qad bayyanna lakumual-ayati
laAAallakum taAAqiloon
Swahili
Jueni kwamba Mwenyezi Mungu huifufua ardhi baada ya kufa kwake.
Tumekubainishieni Ishara ili mpate kuzingatia.
|
Ayah 57:18 الأية
إِنَّ الْمُصَّدِّقِينَ وَالْمُصَّدِّقَاتِ وَأَقْرَضُوا اللهَ قَرْضًا حَسَنًا
يُضَاعَفُ لَهُمْ وَلَهُمْ أَجْرٌ كَرِيمٌ
Inna almussaddiqeena walmussaddiqatiwaaqradoo Allaha qardan hasanan
yudaAAafulahum walahum ajrun kareem
Swahili
Kwa hakika wanaume wanao toa sadaka, na wanawake wanao toa sadaka, na
wakamkopesha Mwenyezi Mungu mkopo mwema, watazidishiwa mardufu na watapata
malipo ya ukarimu.
|
Ayah 57:19 الأية
وَالَّذِينَ آمَنُوا بِاللهِ وَرُسُلِهِ أُولَٰئِكَ هُمُ الصِّدِّيقُونَ ۖ
وَالشُّهَدَاءُ عِندَ رَبِّهِمْ لَهُمْ أَجْرُهُمْ وَنُورُهُمْ ۖ وَالَّذِينَ
كَفَرُوا وَكَذَّبُوا بِآيَاتِنَا أُولَٰئِكَ أَصْحَابُ الْجَحِيمِ
Wallatheena amanoo billahiwarusulihi ola-ika humu assiddeeqoona
washshuhadaoAAinda rabbihim lahum ajruhum wanooruhum wallatheenakafaroo
wakaththaboo bi-ayatina ola-ikaas-habu aljaheem
Swahili
Na walio muamini Mwenyezi Mungu na Mitume wake, hao ndio Masidiqi na Mashahidi
mbele ya Mola wao Mlezi. Wao watapata malipo yao na nuru yao. Na walio kufuru na
wakakadhibisha Ishara zetu, hao ndio watu wa Motoni.
|
Ayah 57:20 الأية
اعْلَمُوا أَنَّمَا الْحَيَاةُ الدُّنْيَا لَعِبٌ وَلَهْوٌ وَزِينَةٌ وَتَفَاخُرٌ
بَيْنَكُمْ وَتَكَاثُرٌ فِي الْأَمْوَالِ وَالْأَوْلَادِ ۖ كَمَثَلِ غَيْثٍ
أَعْجَبَ الْكُفَّارَ نَبَاتُهُ ثُمَّ يَهِيجُ فَتَرَاهُ مُصْفَرًّا ثُمَّ يَكُونُ
حُطَامًا ۖ وَفِي الْآخِرَةِ عَذَابٌ شَدِيدٌ وَمَغْفِرَةٌ مِّنَ اللهِ
وَرِضْوَانٌ ۚ وَمَا الْحَيَاةُ الدُّنْيَا إِلَّا مَتَاعُ الْغُرُورِ
IAAlamoo annama alhayatuaddunya laAAibun walahwun wazeenatun
watafakhurunbaynakum watakathurun fee al-amwali wal-awladikamathali ghaythin
aAAjaba alkuffara nabatuhuthumma yaheeju fatarahu musfarran thumma yakoonu
hutamanwafee al-akhirati AAathabun shadeedun wamaghfiratunmina Allahi waridwanun
wama alhayatuaddunya illa mataAAu alghuroor
Swahili
Jueni ya kwamba maisha ya dunia ni mchezo, na pumbao, na pambo, na
kujifakhirisha baina yenu na kushindana kwa wingi wa mali na watoto. Mfano wake
ni kama mvua ambayo huwafurahisha wakulima mimea yake, kisha hunyauka ukayaona
yamepiga manjano kisha yakawa mabua. Na akhera kuna adhabu kali na maghfira
kutoka kwa Mwenyezi Mungu na radhi. Na maisha ya dunia si chochote ila ni
starehe ya udanganyifu.
|
Ayah 57:21 الأية
سَابِقُوا إِلَىٰ مَغْفِرَةٍ مِّن رَّبِّكُمْ وَجَنَّةٍ عَرْضُهَا كَعَرْضِ
السَّمَاءِ وَالْأَرْضِ أُعِدَّتْ لِلَّذِينَ آمَنُوا بِاللهِ وَرُسُلِهِ ۚ
ذَٰلِكَ فَضْلُ اللهِ يُؤْتِيهِ مَن يَشَاءُ ۚ وَاللهُ ذُو الْفَضْلِ
الْعَظِيمِ
Sabiqoo ila maghfiratin minrabbikum wajannatin AAarduha kaAAardi
assama-iwal-ardi oAAiddat lillatheena amanoobillahi warusulihi thalika fadlu
Allahiyu/teehi man yashao wallahu thooalfadli alAAatheem
Swahili
Kimbilieni msamaha wa Mola wenu Mlezi, na Pepo ambayo upana wake ni kama upana
wa mbingu na ardhi, iliyo wekewa walio muamini Mwenyezi Mungu na Mitume wake.
Hiyo ndiyo fadhila ya Mwenyezi Mungu, humpa amtakaye. Na Mwenyezi Mungu ni
Mwenye fadhila kuu.
|
Ayah 57:22 الأية
مَا أَصَابَ مِن مُّصِيبَةٍ فِي الْأَرْضِ وَلَا فِي أَنفُسِكُمْ إِلَّا فِي
كِتَابٍ مِّن قَبْلِ أَن نَّبْرَأَهَا ۚ إِنَّ ذَٰلِكَ عَلَى اللهِ يَسِيرٌ
Ma asaba min museebatinfee al-ardi wala fee anfusikum illa fee kitabinmin qabli
an nabraaha inna thalika AAala Allahiyaseer
Swahili
Hautokei msiba katika ardhi wala katika nafsi zenu ila umekwisha andikwa katika
Kitabu kabla hatujauumba. Hakika hayo kwa Mwenyezi Mungu ni mepesi.
|
Ayah 57:23 الأية
لِّكَيْلَا تَأْسَوْا عَلَىٰ مَا فَاتَكُمْ وَلَا تَفْرَحُوا بِمَا آتَاكُمْ ۗ
وَاللهُ لَا يُحِبُّ كُلَّ مُخْتَالٍ فَخُورٍ
Likayla ta/saw AAala mafatakum wala tafrahoo bima atakumwallahu la yuhibbu kulla
mukhtalinfakhoor
Swahili
Ili msihuzunike kwa kilicho kupoteeni, wala msijitape kwa alicho kupeni. Na
Mwenyezi Mungu hampendi kila anaye jivuna akajifakhirisha.
|
Ayah 57:24 الأية
الَّذِينَ يَبْخَلُونَ وَيَأْمُرُونَ النَّاسَ بِالْبُخْلِ ۗ وَمَن يَتَوَلَّ
فَإِنَّ اللهَ هُوَ الْغَنِيُّ الْحَمِيدُ
Allatheena yabkhaloona waya/muroona annasabilbukhli waman yatawalla fa-inna
Allaha huwaalghaniyyu alhameed
Swahili
Ambao wanafanya ubakhili, na wanaamrisha watu wafanye ubakhili. Na anaye geuka,
basi Mwenyezi Mungu ni Mwenye kujitosha, Msifiwa.
|
Ayah 57:25 الأية
لَقَدْ أَرْسَلْنَا رُسُلَنَا بِالْبَيِّنَاتِ وَأَنزَلْنَا مَعَهُمُ الْكِتَابَ
وَالْمِيزَانَ لِيَقُومَ النَّاسُ بِالْقِسْطِ ۖ وَأَنزَلْنَا الْحَدِيدَ فِيهِ
بَأْسٌ شَدِيدٌ وَمَنَافِعُ لِلنَّاسِ وَلِيَعْلَمَ اللهُ مَن يَنصُرُهُ
وَرُسُلَهُ بِالْغَيْبِ ۚ إِنَّ اللهَ قَوِيٌّ عَزِيزٌ
Laqad arsalna rusulana bilbayyinatiwaanzalna maAAahumu alkitaba
walmeezanaliyaqooma annasu bilqisti waanzalnaalhadeeda feehi ba/sun shadeedun
wamanafiAAu linnasiwaliyaAAlama Allahu man yansuruhu warusulahu bilghaybiinna
Allaha qawiyyun AAazeez
Swahili
Kwa hakika tuliwatuma Mitume wetu kwa dalili waziwazi, na tukateremsha Kitabu
pamoja nao na Mizani, ili watu wasimamie uadilifu, na tumeteremsha chuma chenye
nguvu nyingi na manufaa kwa watu, na ili Mwenyezi Mungu amjue anaye mnusuru Yeye
na Mitume wake kwa ghaibu. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye nguvu Mwenye
kushinda.
|
Ayah 57:26 الأية
وَلَقَدْ أَرْسَلْنَا نُوحًا وَإِبْرَاهِيمَ وَجَعَلْنَا فِي ذُرِّيَّتِهِمَا
النُّبُوَّةَ وَالْكِتَابَ ۖ فَمِنْهُم مُّهْتَدٍ ۖ وَكَثِيرٌ مِّنْهُمْ فَاسِقُونَ
Walaqad arsalna noohan wa-ibraheemawajaAAalna fee thurriyyatihima
annubuwwatawalkitaba faminhum muhtadin wakatheerun minhum fasiqoon
Swahili
Na bila ya shaka tulimtuma Nuhu na Ibrahim, na tukaweka katika dhuriya zao
Unabii na Kitabu. Basi wapo miongoni mwao walio ongoka, na wengi katika wao ni
wapotovu.
|
Ayah 57:27 الأية
ثُمَّ قَفَّيْنَا عَلَىٰ آثَارِهِم بِرُسُلِنَا وَقَفَّيْنَا بِعِيسَى ابْنِ
مَرْيَمَ وَآتَيْنَاهُ الْإِنجِيلَ وَجَعَلْنَا فِي قُلُوبِ الَّذِينَ اتَّبَعُوهُ
رَأْفَةً وَرَحْمَةً وَرَهْبَانِيَّةً ابْتَدَعُوهَا مَا كَتَبْنَاهَا عَلَيْهِمْ
إِلَّا ابْتِغَاءَ رِضْوَانِ اللهِ فَمَا رَعَوْهَا حَقَّ رِعَايَتِهَا ۖ
فَآتَيْنَا الَّذِينَ آمَنُوا مِنْهُمْ أَجْرَهُمْ ۖ وَكَثِيرٌ مِّنْهُمْ
فَاسِقُونَ
Thumma qaffayna AAala atharihimbirusulina waqaffayna biAAeesa ibni
maryamawaataynahu al-injeela wajaAAalna fee quloobiallatheena ittabaAAoohu
ra/fatan warahmatan warahbaniyyatanibtadaAAooha ma katabnaha AAalayhimilla
ibtighaa ridwani Allahifama raAAawha haqqa riAAayatihafaatayna allatheena amanoo
minhumajrahum wakatheerun minhum fasiqoon
Swahili
Tena tukafuatisha nyuma yao Mitume wengine, na tukamfuatisha Isa bin Mariamu, na
tukampa Injili. Na tukajaalia katika nyoyo za walio mfuata upole na rehema. Na
umonaki (utawa wa mapadri) wameuzua wao. Sisi hatukuwaandikia hayo, ila kutafuta
radhi za Mwenyezi Mungu. Lakini hawakuufuata inavyo takiwa kuufuata. Basi wale
walio amini katika wao tuliwapa ujira wao. Na wengi wao ni wapotovu.
|
Ayah 57:28 الأية
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اتَّقُوا اللهَ وَآمِنُوا بِرَسُولِهِ يُؤْتِكُمْ
كِفْلَيْنِ مِن رَّحْمَتِهِ وَيَجْعَل لَّكُمْ نُورًا تَمْشُونَ بِهِ وَيَغْفِرْ
لَكُمْ ۚ وَاللهُ غَفُورٌ رَّحِيمٌ
Ya ayyuha allatheena amanooittaqoo Allaha waaminoo birasoolihi yu/tikumkiflayni
min rahmatihi wayajAAal lakum nooran tamshoonabihi wayaghfir lakum wallahu
ghafoorun raheem
Swahili
Enyi mlio amini! Mcheni Mwenyezi Mungu, na muaminini Mtume wake, atakupeni
sehemu mbili katika rehema yake, na atakujaalieni muwe na nuru ya kwenda nayo.
Na atakusameheni. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusamehe, Mwenye kurehemu.
|
Ayah 57:29 الأية
لِّئَلَّا يَعْلَمَ أَهْلُ الْكِتَابِ أَلَّا يَقْدِرُونَ عَلَىٰ شَيْءٍ مِّن
فَضْلِ اللهِ ۙ وَأَنَّ الْفَضْلَ بِيَدِ اللهِ يُؤْتِيهِ مَن يَشَاءُ ۚ
وَاللهُ ذُو الْفَضْلِ الْعَظِيمِ
Li-alla yaAAlama ahlu alkitabialla yaqdiroona AAala shay-in min fadli
Allahiwaanna alfadla biyadi Allahi yu/teehi man yashaowallahu thoo alfadli
alAAatheem
Swahili
Ili watu wa Kitabu wajue kwamba wao hawana uweza wowote juu ya fadhila za
Mwenyezi Mungu. Na fadhila zote zimo mikononi mwa Mwenyezi Mungu. Humpa
amtakaye. Na Mwenyezi Mungu ndiye Mwenye fadhila kuu.
|
©
EsinIslam.Com Designed & produced by The Awqaf London. Please pray for us
|