1st Ayah 1 الأية ١الأوليبِسْم ِ اللهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ
سَبَّحَ لِلَّهِ مَا فِي السَّمَاوَاتِ وَمَا فِي الْأَرْضِ ۖ وَهُوَ الْعَزِيزُ
الْحَكِيمُ
Sabbaha lillahi ma fee assamawatiwama fee al-ardi wahuwa alAAazeezu alhakeem
Swahili
Vinamsabihi, Vinamtakasa Mwenyezi Mungu viliomo katika mbingu na viliomo katika
ardhi. Naye ni Mwenye nguvu, Mwenye hikima.
|
Ayah 59:2 الأية
هُوَ الَّذِي أَخْرَجَ الَّذِينَ كَفَرُوا مِنْ أَهْلِ الْكِتَابِ مِن دِيَارِهِمْ
لِأَوَّلِ الْحَشْرِ ۚ مَا ظَنَنتُمْ أَن يَخْرُجُوا ۖ وَظَنُّوا أَنَّهُم
مَّانِعَتُهُمْ حُصُونُهُم مِّنَ اللهِ فَأَتَاهُمُ اللهُ مِنْ حَيْثُ لَمْ
يَحْتَسِبُوا ۖ وَقَذَفَ فِي قُلُوبِهِمُ الرُّعْبَ ۚ يُخْرِبُونَ بُيُوتَهُم
بِأَيْدِيهِمْ وَأَيْدِي الْمُؤْمِنِينَ فَاعْتَبِرُوا يَا أُولِي الْأَبْصَارِ
Huwa allathee akhraja allatheenakafaroo min ahli alkitabi min diyarihim
li-awwalialhashri ma thanantum an yakhrujoo wathannooannahum maniAAatuhum
husoonuhum mina Allahifaatahumu Allahu min haythu lam yahtasiboowaqathafa fee
quloobihimu arruAAba yukhriboonabuyootahum bi-aydeehim waaydee almu/mineena
faAAtabiroo yaolee al-absar
Swahili
Yeye ndiye aliye watoa walio kufuru miongoni mwa Watu wa Kitabu katika nyumba
zao wakati wa uhamisho wa kwanza. Hamkudhani kuwa watatoka, nao walidhani kuwa
ngome zao zitawalinda na Mwenyezi Mungu. Lakini Mwenyezi Mungu aliwafikia kwa
mahali wasipo patazamia, na akatia woga katika nyoyo zao. Wakawa wanazibomoa
nyumba zao kwa mikono yao na mikono ya Waumini. Basi zingatieni enyi wenye
macho!
|
Ayah 59:3 الأية
وَلَوْلَا أَن كَتَبَ اللهُ عَلَيْهِمُ الْجَلَاءَ لَعَذَّبَهُمْ فِي الدُّنْيَا
ۖ وَلَهُمْ فِي الْآخِرَةِ عَذَابُ النَّارِ
Walawla an kataba AllahuAAalayhimu aljalaa laAAaththabahum fee addunyawalahum
fee al-akhirati AAathabu annar
Swahili
Na lau kuwa Mwenyezi Mungu asingeli waandikia kutoka, angeli waadhibu katika
dunia. Na katika Akhera watapata adhabu ya Moto.
|
Ayah 59:4 الأية
ذَٰلِكَ بِأَنَّهُمْ شَاقُّوا اللهَ وَرَسُولَهُ ۖ وَمَن يُشَاقِّ اللهَ
فَإِنَّ اللهَ شَدِيدُ الْعِقَابِ
Thalika bi-annahum shaqqoo Allahawarasoolahu waman yushaqqi Allaha fa-inna
Allahashadeedu alAAiqab
Swahili
Hayo ni kwa sababu walimpinga Mwenyezi Mungu na Mtume wake. Na mwenye kumpinga
Mwenyezi Mungu, basi hakika Mwenyezi Mungu ni Mkali wa kuadhibu.
|
Ayah 59:5 الأية
مَا قَطَعْتُم مِّن لِّينَةٍ أَوْ تَرَكْتُمُوهَا قَائِمَةً عَلَىٰ أُصُولِهَا
فَبِإِذْنِ اللهِ وَلِيُخْزِيَ الْفَاسِقِينَ
Ma qataAAtum min leenatin awtaraktumooha qa-imatan AAala osoolihafabi-ithni
Allahi waliyukhziya alfasiqeen
Swahili
Mtende wowote mlio ukata au mlio uacha unasimama vile vile juu ya mashina yake,
basi ni kwa idhini ya Mwenyezi Mungu, na kwa kuwahizi wapotovu.
|
Ayah 59:6 الأية
وَمَا أَفَاءَ اللهُ عَلَىٰ رَسُولِهِ مِنْهُمْ فَمَا أَوْجَفْتُمْ عَلَيْهِ مِنْ
خَيْلٍ وَلَا رِكَابٍ وَلَٰكِنَّ اللهَ يُسَلِّطُ رُسُلَهُ عَلَىٰ مَن يَشَاءُ ۚ
وَاللهُ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ
Wama afaa Allahu AAalarasoolihi minhum fama awjaftum AAalayhi min khaylin
walarikabin walakinna Allaha yusalliturusulahu AAala man yashao wallahuAAala
kulli shay-in qadeer
Swahili
Na mali aliyo leta Mwenyezi Mungu kwa Mtume wake kutoka kwao hamkuyakimbilia
mbio kwa farasi wala ngamia. Lakini Mwenyezi Mungu huwapa mamlaka Mitume wake
juu ya wowote awatakao. Na Mwenyezi Mungu ni Muweza juu ya kila kitu.
|
Ayah 59:7 الأية
مَّا أَفَاءَ اللهُ عَلَىٰ رَسُولِهِ مِنْ أَهْلِ الْقُرَىٰ فَلِلَّهِ
وَلِلرَّسُولِ وَلِذِي الْقُرْبَىٰ وَالْيَتَامَىٰ وَالْمَسَاكِينِ وَابْنِ
السَّبِيلِ كَيْ لَا يَكُونَ دُولَةً بَيْنَ الْأَغْنِيَاءِ مِنكُمْ ۚ وَمَا
آتَاكُمُ الرَّسُولُ فَخُذُوهُ وَمَا نَهَاكُمْ عَنْهُ فَانتَهُوا ۚ وَاتَّقُوا
اللهَ ۖ إِنَّ اللهَ شَدِيدُ الْعِقَابِ
Ma afaa Allahu AAalarasoolihi min ahli alqura falillahi walirrasooliwalithee
alqurba walyatama walmasakeeniwabni assabeeli kay la yakoona doolatanbayna
al-aghniya-i minkum wama atakumuarrasoolu fakhuthoohu wama nahakumAAanhu
fantahoo wattaqoo Allaha inna Allahashadeedu alAAiqab
Swahili
Mali aliyo leta Mwenyezi Mungu kwa Mtume wake kutoka kwa watu wa hivi vijiji ni
kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, na kwa ajili ya Mtume, na jamaa, na mayatima, na
masikini, na msafiri, ili yasiwe yakizunguka baina ya matajiri tu miongoni
mwenu. Na anacho kupeni Mtume chukueni, na anacho kukatazeni jiepusheni nacho.
Na mcheni Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mkali wa kuadhibu.
|
Ayah 59:8 الأية
لِلْفُقَرَاءِ الْمُهَاجِرِينَ الَّذِينَ أُخْرِجُوا مِن دِيَارِهِمْ
وَأَمْوَالِهِمْ يَبْتَغُونَ فَضْلًا مِّنَ اللهِ وَرِضْوَانًا وَيَنصُرُونَ
اللهَ وَرَسُولَهُ ۚ أُولَٰئِكَ هُمُ الصَّادِقُونَ
Lilfuqara-i almuhajireena allatheenaokhrijoo min diyarihim waamwalihim
yabtaghoona fadlanmina Allahi waridwanan wayansuroonaAllaha warasoolahu ola-ika
humu assadiqoon
Swahili
Wapewe mafakiri Wahajiri walio tolewa majumbani mwao na mali yao kwa ajili ya
kutafuta fadhila kutoka kwa Mwenyezi Mungu na radhi zake, na wanamsaidia
Mwenyezi Mungu na Mtume wake. Hao ndio wa kweli.
|
Ayah 59:9 الأية
وَالَّذِينَ تَبَوَّءُوا الدَّارَ وَالْإِيمَانَ مِن قَبْلِهِمْ يُحِبُّونَ مَنْ
هَاجَرَ إِلَيْهِمْ وَلَا يَجِدُونَ فِي صُدُورِهِمْ حَاجَةً مِّمَّا أُوتُوا
وَيُؤْثِرُونَ عَلَىٰ أَنفُسِهِمْ وَلَوْ كَانَ بِهِمْ خَصَاصَةٌ ۚ وَمَن يُوقَ
شُحَّ نَفْسِهِ فَأُولَٰئِكَ هُمُ الْمُفْلِحُونَ
Wallatheena tabawwaoo addarawal-eemana min qablihim yuhibboona man hajarailayhim
wala yajidoona fee sudoorihim hajatanmimma ootoo wayu/thiroona AAala anfusihim
walaw kanabihim khasasatun waman yooqa shuhha nafsihi faola-ikahumu almuflihoon
Swahili
Na walio na maskani zao na Imani yao kabla yao, wanawapenda walio hamia kwao,
wala hawaoni choyo katika vifua vyao kwa walivyo pewa (Wahajiri), bali
wanawapendelea kuliko nafsi zao, ingawa wao wenyewe ni wahitaji. Na mwenye
kuepushwa uchoyo wa nafsi yake, basi hao ndio wenye kufanikiwa.
|
Ayah 59:10 الأية
وَالَّذِينَ جَاءُوا مِن بَعْدِهِمْ يَقُولُونَ رَبَّنَا اغْفِرْ لَنَا
وَلِإِخْوَانِنَا الَّذِينَ سَبَقُونَا بِالْإِيمَانِ وَلَا تَجْعَلْ فِي
قُلُوبِنَا غِلًّا لِّلَّذِينَ آمَنُوا رَبَّنَا إِنَّكَ رَءُوفٌ رَّحِيمٌ
Wallatheena jaoo minbaAAdihim yaqooloona rabbana ighfir lana
wali-ikhwaninaallatheena sabaqoona bil-eemani walatajAAal fee quloobina ghillan
lillatheena amanoorabbana innaka raoofun raheem
Swahili
Na walio kuja baada yao wanasema: Mola wetu Mlezi! Tughufirie sisi na ndugu zetu
walio tutangulia kwa Imani, wala usijaalie ndani ya nyoyo zetu undani kwa walio
amini. Mola wetu Mlezi! Hakika Wewe ni Mpole na Mwenye kurehemu.
|
Ayah 59:11 الأية
أَلَمْ تَرَ إِلَى الَّذِينَ نَافَقُوا يَقُولُونَ لِإِخْوَانِهِمُ الَّذِينَ
كَفَرُوا مِنْ أَهْلِ الْكِتَابِ لَئِنْ أُخْرِجْتُمْ لَنَخْرُجَنَّ مَعَكُمْ وَلَا
نُطِيعُ فِيكُمْ أَحَدًا أَبَدًا وَإِن قُوتِلْتُمْ لَنَنصُرَنَّكُمْ وَاللهُ
يَشْهَدُ إِنَّهُمْ لَكَاذِبُونَ
Alam tara ila allatheena nafaqooyaqooloona li-ikhwanihimu allatheena kafaroo
minahli alkitabi la-in okhrijtum lanakhrujanna maAAakum walanuteeAAu feekum
ahadan abadan wa-in qootiltum lanansurannakumwallahu yashhadu innahum
lakathiboon
Swahili
Huwaoni wanao fanya unaafiki wanawaambia ndugu zao walio kufuru katika Watu wa
Kitabu: Mkitolewa na sisi lazima tutatoka pamoja nanyi, wala hatutamt'ii yeyote
kabisa dhidi yenu. Na mkipigwa vita lazima tutakusaidieni. Na Mwenyezi Mungu
anashuhudia kuwa hao hakika bila ya shaka ni waongo.
|
Ayah 59:12 الأية
لَئِنْ أُخْرِجُوا لَا يَخْرُجُونَ مَعَهُمْ وَلَئِن قُوتِلُوا لَا يَنصُرُونَهُمْ
وَلَئِن نَّصَرُوهُمْ لَيُوَلُّنَّ الْأَدْبَارَ ثُمَّ لَا يُنصَرُونَ
La-in okhrijoo la yakhrujoonamaAAahum wala-in qootiloo la yansuroonahum
wala-innasaroohum layuwallunna al-adbara thumma layunsaroon
Swahili
Pindi wakitolewa hawatatoka pamoja nao, na wakipigwa vita hawatawasaidia. Na
kama wakiwasaidia basi watageuza migongo; kisha hawatanusuriwa.
|
Ayah 59:13 الأية
لَأَنتُمْ أَشَدُّ رَهْبَةً فِي صُدُورِهِم مِّنَ اللهِ ۚ ذَٰلِكَ بِأَنَّهُمْ
قَوْمٌ لَّا يَفْقَهُونَ
Laantum ashaddu rahbatan fee sudoorihimmina Allahi thalika bi-annahum qawmun
layafqahoon
Swahili
Hakika nyinyi ni kitisho zaidi katika vifua vyao kuliko Mwenyezi Mungu. Hayo ni
kwa kuwa hao ni watu wasio fahamu kitu.
|
Ayah 59:14 الأية
لَا يُقَاتِلُونَكُمْ جَمِيعًا إِلَّا فِي قُرًى مُّحَصَّنَةٍ أَوْ مِن وَرَاءِ
جُدُرٍ ۚ بَأْسُهُم بَيْنَهُمْ شَدِيدٌ ۚ تَحْسَبُهُمْ جَمِيعًا وَقُلُوبُهُمْ
شَتَّىٰ ۚ ذَٰلِكَ بِأَنَّهُمْ قَوْمٌ لَّا يَعْقِلُونَ
La yuqatiloonakum jameeAAanilla fee quran muhassanatin aw min wara-ijudurin
ba/suhum baynahum shadeedun tahsabuhum jameeAAanwaquloobuhum shatta thalika
bi-annahum qawmun layaAAqiloon
Swahili
Hawatapigana nanyi kwa mkusanyiko isipo kuwa katika vijiji vilivyo zatitiwa kwa
ngome, au nyuma ya kuta. Wao kwa wao vita vyao ni vikali. Utawadhania kuwa wako
pamoja, kumbe nyoyo zao ni mbali mbali. Hayo ni kwa kuwa wao ni watu wasio na
akili.
|
Ayah 59:15 الأية
كَمَثَلِ الَّذِينَ مِن قَبْلِهِمْ قَرِيبًا ۖ ذَاقُوا وَبَالَ أَمْرِهِمْ وَلَهُمْ
عَذَابٌ أَلِيمٌ
Kamathali allatheena min qablihimqareeban thaqoo wabala amrihim walahum
AAathabunaleem
Swahili
Ni kama mfano wa walio kuwa kabla yao hivi karibuni. Walionja uovu wa mambo yao.
Nao watapata adhabu iliyo chungu.
|
Ayah 59:16 الأية
كَمَثَلِ الشَّيْطَانِ إِذْ قَالَ لِلْإِنسَانِ اكْفُرْ فَلَمَّا كَفَرَ قَالَ
إِنِّي بَرِيءٌ مِّنكَ إِنِّي أَخَافُ اللهَ رَبَّ الْعَالَمِينَ
Kamathali ashshaytani ithqala lil-insani okfur falamma kafara qalainnee baree-on
minka innee akhafu Allaha rabba alAAalameen
Swahili
Ni kama mfano wa Shetani anapo mwambia mtu: Kufuru. Na akikufuru humwambia: Mimi
si pamoja nawe. Hakika mimi namwogopa Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wa walimwengu
wote.
|
Ayah 59:17 الأية
فَكَانَ عَاقِبَتَهُمَا أَنَّهُمَا فِي النَّارِ خَالِدَيْنِ فِيهَا ۚ وَذَٰلِكَ
جَزَاءُ الظَّالِمِينَ
Fakana AAaqibatahumaannahuma fee annari khalidayni feehawathalika jazao
aththalimeen
Swahili
Basi ikawa mwisho wa wote wawili hao ni kuingia Motoni, wadumu humo daima; na
hiyo ndiyo jaza ya madhaalimu.
|
Ayah 59:18 الأية
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اتَّقُوا اللهَ وَلْتَنظُرْ نَفْسٌ مَّا
قَدَّمَتْ لِغَدٍ ۖ وَاتَّقُوا اللهَ ۚ إِنَّ اللهَ خَبِيرٌ بِمَا تَعْمَلُونَ
Ya ayyuha allatheena amanooittaqoo Allaha waltanthur nafsun maqaddamat lighadin
wattaqoo Allaha inna Allahakhabeerun bima taAAmaloon
Swahili
Enyi mlio amini! Mcheni Mwenyezi Mungu, na kila nafsi iangalie inayo yatanguliza
kwa ajili ya Kesho. Na mcheni Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu anazo
khabari ya mnayo yatenda.
|
Ayah 59:19 الأية
وَلَا تَكُونُوا كَالَّذِينَ نَسُوا اللهَ فَأَنسَاهُمْ أَنفُسَهُمْ ۚ أُولَٰئِكَ
هُمُ الْفَاسِقُونَ
Wala takoonoo kallatheenanasoo Allaha faansahum anfusahum ola-ikahumu alfasiqoon
Swahili
Wala msiwe kama wale walio msahau Mwenyezi Mungu, na Yeye akawasahaulisha nafsi
zao. Hao ndio wapotovu.
|
Ayah 59:20 الأية
لَا يَسْتَوِي أَصْحَابُ النَّارِ وَأَصْحَابُ الْجَنَّةِ ۚ أَصْحَابُ الْجَنَّةِ
هُمُ الْفَائِزُونَ
La yastawee as-habu annariwaas-habu aljannati as-habu aljannatihumu alfa-izoon
Swahili
Hawawi sawa watu wa Motoni na watu wa Peponi. Watu wa Peponi ndio wenye kufuzu.
|
Ayah 59:21 الأية
لَوْ أَنزَلْنَا هَٰذَا الْقُرْآنَ عَلَىٰ جَبَلٍ لَّرَأَيْتَهُ خَاشِعًا
مُّتَصَدِّعًا مِّنْ خَشْيَةِ اللهِ ۚ وَتِلْكَ الْأَمْثَالُ نَضْرِبُهَا
لِلنَّاسِ لَعَلَّهُمْ يَتَفَكَّرُونَ
Law anzalna hatha alqur-anaAAala jabalin laraaytahu khashiAAan mutasaddiAAanmin
khashyati Allahi watilka al-amthalu nadribuhalinnasi laAAallahum yatafakkaroon
Swahili
Lau kuwa tumeiteremsha hii Qur'ani juu ya mlima, basi bila ya shaka ungeli uona
ukinyenyekea, ukipasuka kwa khofu ya Mwenyezi Mungu. Na hiyo mifano tunawapigia
watu ili wafikiri.
|
Ayah 59:22 الأية
هُوَ اللهُ الَّذِي لَا إِلَٰهَ إِلَّا هُوَ ۖ عَالِمُ الْغَيْبِ وَالشَّهَادَةِ
ۖ هُوَ الرَّحْمَٰنُ الرَّحِيمُ
Huwa Allahu allathee lailaha illa huwa AAalimu alghaybi washshahadatihuwa
arrahmanu arraheem
Swahili
Yeye ndiye Mwenyezi Mungu, ambaye hapana mungu isipo kuwa Yeye tu. Mwenye
kuyajua yaliyo fichikana na yanayo onekana. Yeye ndiye Mwingi wa rehema, Mwenye
kurehemu.
|
Ayah 59:23 الأية
هُوَ اللهُ الَّذِي لَا إِلَٰهَ إِلَّا هُوَ الْمَلِكُ الْقُدُّوسُ السَّلَامُ
الْمُؤْمِنُ الْمُهَيْمِنُ الْعَزِيزُ الْجَبَّارُ الْمُتَكَبِّرُ ۚ سُبْحَانَ
اللهِ عَمَّا يُشْرِكُونَ
Huwa Allahu allathee lailaha illa huwa almaliku alquddoosu assalamualmu/minu
almuhayminu alAAazeezu aljabbaru almutakabbirusubhana Allahi AAamma yushrikoon
Swahili
Yeye ndiye Mwenyezi Mungu ambaye hapana mungu isipo kuwa Yeye tu. Mfalme,
Mtakatifu, Mwenye salama, Mtoaji wa amani, Mwenye kuyaendesha Mwenyewe mambo
yake, Mwenye nguvu, Anaye fanya analo litaka, Mkubwa, Ametakasika Mwenyezi Mungu
na hayo wanayo mshirikisha nayo.
|
Ayah 59:24 الأية
هُوَ اللهُ الْخَالِقُ الْبَارِئُ الْمُصَوِّرُ ۖ لَهُ الْأَسْمَاءُ الْحُسْنَىٰ
ۚ يُسَبِّحُ لَهُ مَا فِي السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ ۖ وَهُوَ الْعَزِيزُ
الْحَكِيمُ
Huwa Allahu alkhaliqu albari-oalmusawwiru lahu al-asmao alhusnayusabbihu lahu ma
fee assamawatiwal-ardi wahuwa alAAazeezu alhakeem
Swahili
Yeye ndiye Mwenyezi Mungu, Muumbaji, Mtengenezaji, Mtia sura, Mwenye majina
mazuri kabisa. Kila kilioko katika mbingu na ardhi kinamtakasa, naye ni Mwenye
kushinda, Mwenye hikima.
|
©
EsinIslam.Com Designed & produced by The Awqaf London. Please pray for us
|