1st Ayah 1 الأية ١الأوليبِسْم ِ اللهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تَتَّخِذُوا عَدُوِّي وَعَدُوَّكُمْ
أَوْلِيَاءَ تُلْقُونَ إِلَيْهِم بِالْمَوَدَّةِ وَقَدْ كَفَرُوا بِمَا جَاءَكُم
مِّنَ الْحَقِّ يُخْرِجُونَ الرَّسُولَ وَإِيَّاكُمْ ۙ أَن تُؤْمِنُوا بِاللهِ
رَبِّكُمْ إِن كُنتُمْ خَرَجْتُمْ جِهَادًا فِي سَبِيلِي وَابْتِغَاءَ مَرْضَاتِي ۚ
تُسِرُّونَ إِلَيْهِم بِالْمَوَدَّةِ وَأَنَا أَعْلَمُ بِمَا أَخْفَيْتُمْ وَمَا
أَعْلَنتُمْ ۚ وَمَن يَفْعَلْهُ مِنكُمْ فَقَدْ ضَلَّ سَوَاءَ السَّبِيلِ
Ya ayyuha allatheena amanoola tattakhithoo AAaduwwee waAAaduwwakum
awliyaatulqoona ilayhim bilmawaddati waqad kafaroo bima jaakummina alhaqqi
yukhrijoona arrasoola wa-iyyakuman tu/minoo billahi rabbikum in kuntum
kharajtumjihadan fee sabeelee wabtighaa mardateetusirroona ilayhim bilmawaddati
waana aAAlamu bimaakhfaytum wama aAAlantum waman yafAAalhu minkum faqad
dallasawaa assabeel
Swahili
Enyi mlio amini! Msiwafanye adui zangu na adui zenu kuwa marafiki mkiwapa
mapenzi, na hali wao wamekwisha ikataa haki iliyo kujieni, wakamfukuza Mtume na
nyinyi kwa sababu mnamuamini Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wenu. Mnapotoka kwa
ajili ya Jihadi katika Njia yangu na kutafuta radhi yangu, mnafanya urafiki nao
kwa siri, na Mimi nayajua mnayo yaficha na mnayo dhihirisha. Na mwenye kufanya
hayo kati yenu basi ameipotea njia ya sawa.
|
Ayah 60:2 الأية
إِن يَثْقَفُوكُمْ يَكُونُوا لَكُمْ أَعْدَاءً وَيَبْسُطُوا إِلَيْكُمْ
أَيْدِيَهُمْ وَأَلْسِنَتَهُم بِالسُّوءِ وَوَدُّوا لَوْ تَكْفُرُونَ
In yathqafookum yakoonoo lakam aAAdaanwayabsutoo ilaykum aydiyahum waalsinatahum
bissoo-iwawaddoo law takfuroon
Swahili
Wakikuwezeni wanakuwa maadui zenu, na wanakukunjulieni mikono yao na ndimi zao
kwa uovu. Na wanapenda muwe makafiri.
|
Ayah 60:3 الأية
لَن تَنفَعَكُمْ أَرْحَامُكُمْ وَلَا أَوْلَادُكُمْ ۚ يَوْمَ الْقِيَامَةِ يَفْصِلُ
بَيْنَكُمْ ۚ وَاللهُ بِمَا تَعْمَلُونَ بَصِيرٌ
Lan tanfaAAakum arhamukum walaawladukum yawma alqiyamati yafsilu baynakumwallahu
bima taAAmaloona baseer
Swahili
Hawatakufaeni jamaa zenu, wala watoto wenu Siku ya Kiyama. Mwenyezi Mungu
atapambanua baina yenu, na Mwenyezi Mungu anayaona mnayo yatenda.
|
Ayah 60:4 الأية
قَدْ كَانَتْ لَكُمْ أُسْوَةٌ حَسَنَةٌ فِي إِبْرَاهِيمَ وَالَّذِينَ مَعَهُ إِذْ
قَالُوا لِقَوْمِهِمْ إِنَّا بُرَآءُ مِنكُمْ وَمِمَّا تَعْبُدُونَ مِن دُونِ
اللهِ كَفَرْنَا بِكُمْ وَبَدَا بَيْنَنَا وَبَيْنَكُمُ الْعَدَاوَةُ
وَالْبَغْضَاءُ أَبَدًا حَتَّىٰ تُؤْمِنُوا بِاللهِ وَحْدَهُ إِلَّا قَوْلَ
إِبْرَاهِيمَ لِأَبِيهِ لَأَسْتَغْفِرَنَّ لَكَ وَمَا أَمْلِكُ لَكَ مِنَ اللهِ
مِن شَيْءٍ ۖ رَّبَّنَا عَلَيْكَ تَوَكَّلْنَا وَإِلَيْكَ أَنَبْنَا وَإِلَيْكَ
الْمَصِيرُ
Qad kanat lakum oswatun hasanatunfee ibraheema wallatheena maAAahu ithqaloo
liqawmihim inna buraao minkum wamimmataAAbudoona min dooni Allahi kafarna bikum
wabadabaynana wabaynakumu alAAadawatu walbaghdaoabadan hatta tu/minoo billahi
wahdahuilla qawla ibraheema li-abeehi laastaghfiranna lakawama amliku laka mina
Allahi min shay-in rabbanaAAalayka tawakkalna wa-ilayka anabna wa-ilayka
almaseer
Swahili
Hakika nyinyi mna mfano mzuri kwenu kwa Ibrahim na wale walio kuwa pamoja naye,
walipo waambia watu wao: Hakika sisi tumejitenga nanyi na hayo mnayo yaabudu
badala ya Mwenyezi Mungu. Tunakukataeni; na umekwisha dhihiri uadui na chuki
baina yetu na nyinyi mpaka mtakapo muamini Mwenyezi Mungu peke yake. Isipo kuwa
kauli ya Ibrahim kumwambia baba yake: Hakika nitakuombea msamaha, wala similiki
chochote kwa ajili yako mbele ya Mwenyezi Mungu. Mola wetu Mlezi! Juu yako
tumetegemea, na kwako tumeelekea, na kwako ndio marejeo.
|
Ayah 60:5 الأية
رَبَّنَا لَا تَجْعَلْنَا فِتْنَةً لِّلَّذِينَ كَفَرُوا وَاغْفِرْ لَنَا رَبَّنَا
ۖ إِنَّكَ أَنتَ الْعَزِيزُ الْحَكِيمُ
Rabbana la tajAAalnafitnatan lillatheena kafaroo waghfir lanarabbana innaka anta
alAAazeezu alhakeem
Swahili
Mola wetu Mlezi! Usitufanyie mtihani kwa walio kufuru. Na tusamehe, Mola wetu
Mlezi. Hakika Wewe ndiye Mwenye nguvu, Mwenye hikima.
|
Ayah 60:6 الأية
لَقَدْ كَانَ لَكُمْ فِيهِمْ أُسْوَةٌ حَسَنَةٌ لِّمَن كَانَ يَرْجُو اللهَ
وَالْيَوْمَ الْآخِرَ ۚ وَمَن يَتَوَلَّ فَإِنَّ اللهَ هُوَ الْغَنِيُّ
الْحَمِيدُ
Laqad kana lakum feehim oswatun hasanatunliman kana yarjoo Allaha walyawma
al-akhirawaman yatawalla fa-inna Allaha huwa alghanniyyu alhameed
Swahili
Kwa yakini umekuwa mfano mzuri kwenu katika mwendo wao, kwa anaye mtarajia
Mwenyezi Mungu na Siku ya Mwisho. Na mwenye kugeuka basi hakika Mwnyezi Mungu ni
Mwenye kujitosha, Msifiwa.
|
Ayah 60:7 الأية
عَسَى اللهُ أَن يَجْعَلَ بَيْنَكُمْ وَبَيْنَ الَّذِينَ عَادَيْتُم مِّنْهُم
مَّوَدَّةً ۚ وَاللهُ قَدِيرٌ ۚ وَاللهُ غَفُورٌ رَّحِيمٌ
AAasa Allahu an yajAAalabaynakum wabayna allatheena AAadaytum minhummawaddatan
wallahu qadeerun wallahughafoorun raheem
Swahili
Asaa Mwenyezi Mungu akatia mapenzi baina yenu na hao maadui zenu, na Mwenyezi
Mungu ni Mweza, na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusamehe, Mwenye kurehemu.
|
Ayah 60:8 الأية
لَّا يَنْهَاكُمُ اللهُ عَنِ الَّذِينَ لَمْ يُقَاتِلُوكُمْ فِي الدِّينِ وَلَمْ
يُخْرِجُوكُم مِّن دِيَارِكُمْ أَن تَبَرُّوهُمْ وَتُقْسِطُوا إِلَيْهِمْ ۚ إِنَّ
اللهَ يُحِبُّ الْمُقْسِطِينَ
La yanhakumu AllahuAAani allatheena lam yuqatilookum fee addeeniwalam
yukhrijookum min diyarikum an tabarroohum watuqsitooilayhim inna Allaha yuhibbu
almuqsiteen
Swahili
Mwenyezi Mungu hakukatazini kuwafanyia wema na uadilifu wale ambao
hawakukupigeni vita, wala hawakukutoeni makwenu. Hakika Mwenyezi Mungu huwapenda
wafanyao uadilifu.
|
Ayah 60:9 الأية
إِنَّمَا يَنْهَاكُمُ اللهُ عَنِ الَّذِينَ قَاتَلُوكُمْ فِي الدِّينِ
وَأَخْرَجُوكُم مِّن دِيَارِكُمْ وَظَاهَرُوا عَلَىٰ إِخْرَاجِكُمْ أَن
تَوَلَّوْهُمْ ۚ وَمَن يَتَوَلَّهُمْ فَأُولَٰئِكَ هُمُ الظَّالِمُونَ
Innama yanhakumu AllahuAAani allatheena qatalookum fee addeeniwaakhrajookum min
diyarikum wathaharooAAala ikhrajikum an tawallawhum waman yatawallahumfaola-ika
humu aththalimoon
Swahili
Hakika Mwenyezi Mungu anakukatazeni kufanya urafiki na wale walio kupigeni vita,
na wakakutoeni makwenu, na wakasaidia katika kufukuzwa kwenu. Na wanao wafanya
hao marafiki basi hao ndio madhaalimu.
|
Ayah 60:10 الأية
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا إِذَا جَاءَكُمُ الْمُؤْمِنَاتُ مُهَاجِرَاتٍ
فَامْتَحِنُوهُنَّ ۖ اللهُ أَعْلَمُ بِإِيمَانِهِنَّ ۖ فَإِنْ عَلِمْتُمُوهُنَّ
مُؤْمِنَاتٍ فَلَا تَرْجِعُوهُنَّ إِلَى الْكُفَّارِ ۖ لَا هُنَّ حِلٌّ لَّهُمْ
وَلَا هُمْ يَحِلُّونَ لَهُنَّ ۖ وَآتُوهُم مَّا أَنفَقُوا ۚ وَلَا جُنَاحَ
عَلَيْكُمْ أَن تَنكِحُوهُنَّ إِذَا آتَيْتُمُوهُنَّ أُجُورَهُنَّ ۚ وَلَا
تُمْسِكُوا بِعِصَمِ الْكَوَافِرِ وَاسْأَلُوا مَا أَنفَقْتُمْ وَلْيَسْأَلُوا مَا
أَنفَقُوا ۚ ذَٰلِكُمْ حُكْمُ اللهِ ۖ يَحْكُمُ بَيْنَكُمْ ۚ وَاللهُ عَلِيمٌ
حَكِيمٌ
Ya ayyuha allatheena amanooitha jaakumu almu/minatu muhajiratinfamtahinoohunna
Allahu aAAlamu bi-eemanihinnafa-in AAalimtumoohunna mu/minatin
falatarjiAAoohunna ila alkuffari la hunna hillunlahum wala hum yahilloona
lahunna waatoohumma anfaqoo wala junaha AAalaykum an tankihoohunnaitha
ataytumoohunna ojoorahunna walatumsikoo biAAisami alkawafiri was-aloo maanfaqtum
walyas-aloo ma anfaqoo thalikum hukmuAllahi yahkumu baynakum wallahuAAaleemun
hakeem
Swahili
Enyi mlio amini! Wakikujilieni wanawake Waumini walio hama, basi wafanyieni
mtihani - Mwenyezi Mungu ndiye Mwenye kujua zaidi Imani yao. Mkiwa mnawajua kuwa
ni Waumini basi msiwarudishe kwa makafiri. Wanawake hao si halali kwa hao
makafiri, wala hao makafiri hawahalalikii wanawake Waumini. Na wapeni hao
wanaume mahari walio toa. Wala hapana makosa kwenu kuwaoa mkiwapa mahari yao.
Wala msiwaweke wanawake makafiri katika kifungo cha ndoa zenu. Na takeni mlicho
kitoa, na wao watake walicho kitoa. Hiyo ndiyo hukumu ya Mwenyezi Mungu anayo
kuhukumuni. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kujua, Mwenye hikima.
|
Ayah 60:11 الأية
وَإِن فَاتَكُمْ شَيْءٌ مِّنْ أَزْوَاجِكُمْ إِلَى الْكُفَّارِ فَعَاقَبْتُمْ
فَآتُوا الَّذِينَ ذَهَبَتْ أَزْوَاجُهُم مِّثْلَ مَا أَنفَقُوا ۚ وَاتَّقُوا
اللهَ الَّذِي أَنتُم بِهِ مُؤْمِنُونَ
Wa-in fatakum shay-on min azwajikumila alkuffari faAAaqabtum faatoo
allatheenathahabat azwajuhum mithla ma anfaqoo wattaqooAllaha allathee antum
bihi mu/minoon
Swahili
Na akitoroka yeyote katika wake zenu kwenda kwa makafiri, tena ikatokea mkapata
ngawira, basi wapeni walio kimbiwa na wake zao kiasi cha mahari waliyo yatoa. Na
mcheni Mwenyezi Mungu ambaye mnamuamini.
|
Ayah 60:12 الأية
يَا أَيُّهَا النَّبِيُّ إِذَا جَاءَكَ الْمُؤْمِنَاتُ يُبَايِعْنَكَ عَلَىٰ أَن
لَّا يُشْرِكْنَ بِاللهِ شَيْئًا وَلَا يَسْرِقْنَ وَلَا يَزْنِينَ وَلَا
يَقْتُلْنَ أَوْلَادَهُنَّ وَلَا يَأْتِينَ بِبُهْتَانٍ يَفْتَرِينَهُ بَيْنَ
أَيْدِيهِنَّ وَأَرْجُلِهِنَّ وَلَا يَعْصِينَكَ فِي مَعْرُوفٍ ۙ فَبَايِعْهُنَّ
وَاسْتَغْفِرْ لَهُنَّ اللهَ ۖ إِنَّ اللهَ غَفُورٌ رَّحِيمٌ
Ya ayyuha annabiyyu ithajaaka almu/minatu yubayiAAnaka AAalaan la yushrikna
billahi shay-an walayasriqna wala yazneena wala yaqtulna awladahunnawala
ya/teena bibuhtanin yaftareenahu baynaaydeehinna waarjulihinna wala yaAAseenaka
feemaAAroofin fabayiAAhunna wastaghfir lahunna Allahainna Allaha ghafoorun
raheem
Swahili
Ewe Nabii! Watakapo kujia wanawake Waumini wanakuahidi ya kwamba
hawatamshirikisha Mwenyezi Mungu na chochote, wala hawataiba, wala hawatazini,
wala hawatawauwa watoto wao, wala hawataleta uzushi wanao uzua tu wenyewe baina
ya mikono yao na miguu yao, wala hawatakuasi katika jambo jema, basi peana nao
ahadi, na uwatakie maghfira kwa Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwingi
maghfira, Mwenye kurehemu.
|
Ayah 60:13 الأية
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تَتَوَلَّوْا قَوْمًا غَضِبَ اللهُ
عَلَيْهِمْ قَدْ يَئِسُوا مِنَ الْآخِرَةِ كَمَا يَئِسَ الْكُفَّارُ مِنْ أَصْحَابِ
الْقُبُورِ
Ya ayyuha allatheena amanoola tatawallaw qawman ghadiba AllahuAAalayhim qad
ya-isoo mina al-akhirati kama ya-isaalkuffaru min as-habi alquboor
Swahili
Enyi mlio amini! Msiwafanye rafiki zenu watu ambao Mwenyezi Mungu
amewakasirikia. Hao wamekwisha kata tamaa ya Akhera, kama makafiri walivyo
wakatia tamaa watu wa makaburini.
|
©
EsinIslam.Com Designed & produced by The Awqaf London. Please pray for us
|