First Ayah 1 الأية الأولي
بَرَاءَةٌ مِّنَ اللَّهِ وَرَسُولِهِ إِلَى الَّذِينَ عَاهَدتُّم مِّنَ
الْمُشْرِكِينَ
Baraatun mina Allahiwarasoolihi ila allatheena AAahadtum minaalmushrikeen
Swahili
Huku ni kujitoa Mwenyezi Mungu na Mtume wake kwenye jukumu la maagano na mlio
ahidiana nao katika washirikina.
|
Ayah 9:2 الأية
فَسِيحُوا فِي الْأَرْضِ أَرْبَعَةَ أَشْهُرٍ وَاعْلَمُوا أَنَّكُمْ غَيْرُ
مُعْجِزِي اللَّهِ ۙ وَأَنَّ اللَّهَ مُخْزِي الْكَافِرِينَ
Faseehoo fee al-ardi arbaAAataashhurin waAAlamoo annakum ghayru muAAjizee
Allahiwaanna Allaha mukhzee alkafireen
Swahili
Basi tembeeni katika nchi miezi mine, na jueni kwamba nyinyi hamwezi kumshinda
Mwenyezi Mung, na kwamba Mwenyezi Mungu ndiye anaye wahizi makafiri.
|
Ayah 9:3 الأية
وَأَذَانٌ مِّنَ اللَّهِ وَرَسُولِهِ إِلَى النَّاسِ يَوْمَ الْحَجِّ الْأَكْبَرِ
أَنَّ اللَّهَ بَرِيءٌ مِّنَ الْمُشْرِكِينَ ۙ وَرَسُولُهُ ۚ فَإِن تُبْتُمْ فَهُوَ
خَيْرٌ لَّكُمْ ۖ وَإِن تَوَلَّيْتُمْ فَاعْلَمُوا أَنَّكُمْ غَيْرُ مُعْجِزِي
اللَّهِ ۗ وَبَشِّرِ الَّذِينَ كَفَرُوا بِعَذَابٍ أَلِيمٍ
Waathanun mina Allahiwarasoolihi ila annasi yawma alhajjial-akbari anna Allaha
baree-on mina almushrikeenawarasooluhu fa-in tubtum fahuwa khayrun lakum wa-in
tawallaytumfaAAlamoo annakum ghayru muAAjizee Allahiwabashshiri allatheena
kafaroo biAAathabin aleem
Swahili
Na ni tangazo kutokana na Mwenyezi Mungu na Mtume wake kwa wote siku ya Hija
Kubwa kwamba Mwenyezi Mungu na Mtume wake hawana jukumu lolote kwa washirikina.
Basi mkitubu itakuwa kheri kwenu, na mkigeuka basi jueni kuwa nyinyi hamumshindi
Mwenyezi Mungu. Na wabashirie makafiri kuwa watapata adhabu chungu.
|
Ayah 9:4 الأية
إِلَّا الَّذِينَ عَاهَدتُّم مِّنَ الْمُشْرِكِينَ ثُمَّ لَمْ يَنقُصُوكُمْ شَيْئًا
وَلَمْ يُظَاهِرُوا عَلَيْكُمْ أَحَدًا فَأَتِمُّوا إِلَيْهِمْ عَهْدَهُمْ إِلَىٰ
مُدَّتِهِمْ ۚ إِنَّ اللَّهَ يُحِبُّ الْمُتَّقِينَ
Illa allatheena AAahadtummina almushrikeena thumma lam yanqusookum shay-an walam
yuthahirooAAalaykum ahadan faatimmoo ilayhim AAahdahum ilamuddatihim inna Allaha
yuhibbu almuttaqeen
Swahili
Isipo kuwa washirikina ambao mliahidiana nao kisha wasikupunguzieni chochote,
wala hawakumsaidia yeyote dhidi yenu, basi hao watimizieni ahadi yao mpaka muda
wao. Hakika Mwenyezi Mungu huwapenda wacha-Mungu.
|
Ayah 9:5 الأية
فَإِذَا انسَلَخَ الْأَشْهُرُ الْحُرُمُ فَاقْتُلُوا الْمُشْرِكِينَ حَيْثُ
وَجَدتُّمُوهُمْ وَخُذُوهُمْ وَاحْصُرُوهُمْ وَاقْعُدُوا لَهُمْ كُلَّ مَرْصَدٍ ۚ
فَإِن تَابُوا وَأَقَامُوا الصَّلَاةَ وَآتَوُا الزَّكَاةَ فَخَلُّوا سَبِيلَهُمْ ۚ
إِنَّ اللَّهَ غَفُورٌ رَّحِيمٌ
Fa-itha insalakha al-ashhuru alhurumufaqtuloo almushrikeena haythu wajadtumoohum
wakhuthoohumwahsuroohum waqAAudoo lahum kulla marsadinfa-in taboo waaqamoo
assalatawaatawoo azzakata fakhalloo sabeelahum innaAllaha ghafoorun raheem
Swahili
Na ikisha miezi mitukufu basi wauweni washirikina popote mwakutapo, na washikeni
na wazungukeni, na wavizieni katika kila njia. Lakini wakitubu, wakashika Sala,
na wakatoa Zaka, basi waachilieni. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusamehe
Mwenye kurehemu.
|
Ayah 9:6 الأية
وَإِنْ أَحَدٌ مِّنَ الْمُشْرِكِينَ اسْتَجَارَكَ فَأَجِرْهُ حَتَّىٰ يَسْمَعَ
كَلَامَ اللَّهِ ثُمَّ أَبْلِغْهُ مَأْمَنَهُ ۚ ذَٰلِكَ بِأَنَّهُمْ قَوْمٌ لَّا
يَعْلَمُونَ
Wa-in ahadun mina almushrikeena istajarakafaajirhu hatta yasmaAAa kalama
Allahithumma ablighhu ma/manahu thalika bi-annahum qawmun layaAAlamoon
Swahili
Na ikiwa mmoja wapo katika washirikina akikuomba ulinzi, basi mpe ulinzi apate
kusikia maneno ya Mwenyezi Mungu. Kisha mfikishe pahala pake pa amani. Haya ni
kwa kuwa hao ni watu wasiojua kitu.
|
Ayah 9:7 الأية
كَيْفَ يَكُونُ لِلْمُشْرِكِينَ عَهْدٌ عِندَ اللَّهِ وَعِندَ رَسُولِهِ إِلَّا
الَّذِينَ عَاهَدتُّمْ عِندَ الْمَسْجِدِ الْحَرَامِ ۖ فَمَا اسْتَقَامُوا لَكُمْ
فَاسْتَقِيمُوا لَهُمْ ۚ إِنَّ اللَّهَ يُحِبُّ الْمُتَّقِينَ
Kayfa yakoonu lilmushrikeena AAahdun AAindaAllahi waAAinda rasoolihi illa
allatheena AAahadtumAAinda almasjidi alharami fama istaqamoolakum fastaqeemoo
lahum inna Allaha yuhibbualmuttaqeen
Swahili
Itakuwaje iwepo ahadi na washirikina mbele ya Mwenyezi Mungu na mbele ya Mtume
wake, ila wale mlio ahidiana nao kwenye Msikiti Mtakatifu? Basi maadamu
wanakwenda nanyi sawa, nanyi pia nendeni sawa nao. Hakika Mwenyezi Mungu
huwapenda wachamngu
|
Ayah 9:8 الأية
كَيْفَ وَإِن يَظْهَرُوا عَلَيْكُمْ لَا يَرْقُبُوا فِيكُمْ إِلًّا وَلَا ذِمَّةً ۚ
يُرْضُونَكُم بِأَفْوَاهِهِمْ وَتَأْبَىٰ قُلُوبُهُمْ وَأَكْثَرُهُمْ فَاسِقُونَ
Kayfa wa-in yathharoo AAalaykumla yarquboo feekum illan wala thimmatan
yurdoonakumbi-afwahihim wata/ba quloobuhum waaktharuhum fasiqoon
Swahili
Itakuwaje! Nao wakikushindeni hawatazami kwenu udugu wala ahadi.
Wanakufurahisheni kwa midomo yao tu, na nyoyo zao zinakataa hayo. Na wengi wao
ni wapotovu.
|
Ayah 9:9 الأية
اشْتَرَوْا بِآيَاتِ اللَّهِ ثَمَنًا قَلِيلًا فَصَدُّوا عَن سَبِيلِهِ ۚ إِنَّهُمْ
سَاءَ مَا كَانُوا يَعْمَلُونَ
Ishtaraw bi-ayati Allahithamanan qaleelan fasaddoo AAan sabeelihi innahum saama
kanoo yaAAmaloon
Swahili
Wamenunua thamani ndogo kwa Ishara za Mwenyezi Mungu, na wakazuilia watu na Njia
yake. Hakika hao ni maovu waliyo kuwa wakiyatenda.
|
Ayah 9:10 الأية
لَا يَرْقُبُونَ فِي مُؤْمِنٍ إِلًّا وَلَا ذِمَّةً ۚ وَأُولَٰئِكَ هُمُ
الْمُعْتَدُونَ
La yarquboona fee mu/minin illan walathimmatan waola-ika humu almuAAtadoon
Swahili
Hawatazami kwa Muumini udugu wala ahadi; basi hao ndio warukao mipaka.
|
Ayah 9:11 الأية
فَإِن تَابُوا وَأَقَامُوا الصَّلَاةَ وَآتَوُا الزَّكَاةَ فَإِخْوَانُكُمْ فِي
الدِّينِ ۗ وَنُفَصِّلُ الْآيَاتِ لِقَوْمٍ يَعْلَمُونَ
Fa-in taboo waaqamoo assalatawaatawoo azzakata fa-ikhwanukum feeaddeeni
wanufassilu al-ayatiliqawmin yaAAlamoon
Swahili
Basi wakitubu na wakashika Sala na wakatoa Zaka, basi ni ndugu zenu katika Dini.
Na tunazichambua Aya kwa watu wajuao.
|
Ayah 9:12 الأية
وَإِن نَّكَثُوا أَيْمَانَهُم مِّن بَعْدِ عَهْدِهِمْ وَطَعَنُوا فِي دِينِكُمْ
فَقَاتِلُوا أَئِمَّةَ الْكُفْرِ ۙ إِنَّهُمْ لَا أَيْمَانَ لَهُمْ لَعَلَّهُمْ
يَنتَهُونَ
Wa-in nakathoo aymanahum min baAAdiAAahdihim wataAAanoo fee deenikum
faqatilooa-immata alkufri innahum la aymana lahumlaAAallahum yantahoon
Swahili
Na wakivunja viapo vyao baada ya kuahidi kwao, na wakatukana Dini yenu, basi
piganeni na waongozi wa ukafiri. Hakika hao hawana viapo vya kweli. Huenda (kwa
hayo) wakaacha.
|
Ayah 9:13 الأية
أَلَا تُقَاتِلُونَ قَوْمًا نَّكَثُوا أَيْمَانَهُمْ وَهَمُّوا بِإِخْرَاجِ
الرَّسُولِ وَهُم بَدَءُوكُمْ أَوَّلَ مَرَّةٍ ۚ أَتَخْشَوْنَهُمْ ۚ فَاللَّهُ
أَحَقُّ أَن تَخْشَوْهُ إِن كُنتُم مُّؤْمِنِينَ
Ala tuqatiloona qawmannakathoo aymanahum wahammoo bi-ikhraji arrasooliwahum
badaookum awwala marratin atakhshawnahum fallahuahaqqu an takhshawhu in kuntum
mu/mineen
Swahili
Je, hamtapigana na watu walio vunja viapo vyao na wakawa na hamu ya kumfukuza
Mtume, nao ndio walio kuanzeni mara ya kwanza? Je, mnawaogopa? Basi Mwenyezi
Mungu anastahiki zaidi mumwogope, ikiwa nyinyi ni Waumini.
|
Ayah 9:14 الأية
قَاتِلُوهُمْ يُعَذِّبْهُمُ اللَّهُ بِأَيْدِيكُمْ وَيُخْزِهِمْ وَيَنصُرْكُمْ
عَلَيْهِمْ وَيَشْفِ صُدُورَ قَوْمٍ مُّؤْمِنِينَ
Qatiloohum yuAAaththibhumu Allahubi-aydeekum wayukhzihim wayansurkum AAalayhim
wayashfi sudooraqawmin mu/mineen
Swahili
Piganeni nao, Mwenyezi Mungu awaadhibu kwa mikono yenu, na awahizi na
akunusuruni muwashinde, na avipoze vifua vya kaumu ya Waumini,
|
Ayah 9:15 الأية
وَيُذْهِبْ غَيْظَ قُلُوبِهِمْ ۗ وَيَتُوبُ اللَّهُ عَلَىٰ مَن يَشَاءُ ۗ وَاللَّهُ
عَلِيمٌ حَكِيمٌ
Wayuthhib ghaythaquloobihim wayatoobu Allahu AAala man yashaowallahu AAaleemun
hakeem
Swahili
Na aondoe hasira ya nyoyo zao. Na Mwenyezi Mungu humkubalia toba ya amtakaye. Na
Mwenyezi Mungu ni Mwenye kujua Mwenye hikima.
|
Ayah 9:16 الأية
أَمْ حَسِبْتُمْ أَن تُتْرَكُوا وَلَمَّا يَعْلَمِ اللَّهُ الَّذِينَ جَاهَدُوا
مِنكُمْ وَلَمْ يَتَّخِذُوا مِن دُونِ اللَّهِ وَلَا رَسُولِهِ وَلَا
الْمُؤْمِنِينَ وَلِيجَةً ۚ وَاللَّهُ خَبِيرٌ بِمَا تَعْمَلُونَ
Am hasibtum an tutrakoo walammayaAAlami Allahu allatheena jahadoo minkumwalam
yattakhithoo min dooni Allahi walarasoolihi wala almu/mineena waleejatan
wallahukhabeerun bima taAAmaloon
Swahili
Je, mlidhani kuwa mtaachwa tu, bila ya Mwenyezi Mungu kuwajuulisha wale walio
pigana Jihadi kati yenu, na wala hawakumfanya mwendani wao isipo kuwa Mwenyezi
Mungu na Mtume wake na Waumini wenziwe? Na Mwenyezi Mungu anazo khabari za yote
mnayo yatenda.
|
Ayah 9:17 الأية
مَا كَانَ لِلْمُشْرِكِينَ أَن يَعْمُرُوا مَسَاجِدَ اللَّهِ شَاهِدِينَ عَلَىٰ
أَنفُسِهِم بِالْكُفْرِ ۚ أُولَٰئِكَ حَبِطَتْ أَعْمَالُهُمْ وَفِي النَّارِ هُمْ
خَالِدُونَ
Ma kana lilmushrikeena anyaAAmuroo masajida Allahi shahideena AAalaanfusihim
bilkufri ola-ika habitataAAmaluhum wafee annari hum khalidoon
Swahili
Haiwi kuwa makafiri ndio waamirishe misikiti ya Mwenyezi Mungu, hali
wanajishuhudishia wenyewe ukafiri. Hao ndio ambao vitendo vyao vimeharibika, na
katika Moto watadumu.
|
Ayah 9:18 الأية
إِنَّمَا يَعْمُرُ مَسَاجِدَ اللَّهِ مَنْ آمَنَ بِاللَّهِ وَالْيَوْمِ الْآخِرِ
وَأَقَامَ الصَّلَاةَ وَآتَى الزَّكَاةَ وَلَمْ يَخْشَ إِلَّا اللَّهَ ۖ فَعَسَىٰ
أُولَٰئِكَ أَن يَكُونُوا مِنَ الْمُهْتَدِينَ
Innama yaAAmuru masajida Allahiman amana billahi walyawmi al-akhiriwaaqama
assalata waataazzakata walam yakhsha illa AllahafaAAasa ola-ika an yakoonoo mina
almuhtadeen
Swahili
Hakika wanao amirisha misikiti ya Mwenyezi Mungu ni wale wanao muamini Mwenyezi
Mungu, na Siku ya Mwisho, na wakashika Sala, na wakatoa Zaka, na wala hawamchi
ila Mwenyezi Mungu. Basi huenda hao wakawa katika waongofu.
|
Ayah 9:19 الأية
أَجَعَلْتُمْ سِقَايَةَ الْحَاجِّ وَعِمَارَةَ الْمَسْجِدِ الْحَرَامِ كَمَنْ آمَنَ
بِاللَّهِ وَالْيَوْمِ الْآخِرِ وَجَاهَدَ فِي سَبِيلِ اللَّهِ ۚ لَا يَسْتَوُونَ
عِندَ اللَّهِ ۗ وَاللَّهُ لَا يَهْدِي الْقَوْمَ الظَّالِمِينَ
AjaAAaltum siqayata alhajjiwaAAimarata almasjidi alharami kaman amanabillahi
walyawmi al-akhiri wajahadafee sabeeli Allahi la yastawoona AAinda Allahiwallahu
la yahdee alqawma aththalimeen
Swahili
Je, mnafanya kuwanywesha maji Mahujaji na kuamirisha Msikiti Mtakatifu ni sawa
na mwenye kumuamini Mwenyezi Mungu, na Siku ya Mwisho, na akapigana Jihadi
katika Njia ya Mwenyezi Mungu? Hawawi sawa mbele ya Mwenyezi Mungu. Na Mwenyezi
Mungu hawaongoi watu madhaalimu.
|
Ayah 9:20 الأية
الَّذِينَ آمَنُوا وَهَاجَرُوا وَجَاهَدُوا فِي سَبِيلِ اللَّهِ بِأَمْوَالِهِمْ
وَأَنفُسِهِمْ أَعْظَمُ دَرَجَةً عِندَ اللَّهِ ۚ وَأُولَٰئِكَ هُمُ الْفَائِزُونَ
Allatheena amanoo wahajaroowajahadoo fee sabeeli Allahi bi-amwalihimwaanfusihim
aAAthamu darajatan AAinda Allahiwaola-ika humu alfa-izoon
Swahili
Wale walio amini, na wakahama, na wakapigana Jihadi katika Njia ya Mwenyezi
Mungu kwa mali yao na nafsi zao, hao wana cheo kikubwa zaidi mbele ya Mwenyezi
Mungu. Na hao ndio wenye kufuzu.
|
Ayah 9:21 الأية
يُبَشِّرُهُمْ رَبُّهُم بِرَحْمَةٍ مِّنْهُ وَرِضْوَانٍ وَجَنَّاتٍ لَّهُمْ فِيهَا
نَعِيمٌ مُّقِيمٌ
Yubashshiruhum rabbuhum birahmatinminhu waridwanin wajannatin lahum
feehanaAAeemun muqeem
Swahili
Mola wao Mlezi anawabashiria rehema zitokazo kwake, na radhi, na Bustani ambazo
humo watapata neema za kudumu.
|
Ayah 9:22 الأية
خَالِدِينَ فِيهَا أَبَدًا ۚ إِنَّ اللَّهَ عِندَهُ أَجْرٌ عَظِيمٌ
Khalideena feeha abadan innaAllaha AAindahu ajrun AAatheem
Swahili
Watadumu humo milele. Hakika kwa Mwenyezi Mungu yapo malipo makubwa.
|
Ayah 9:23 الأية
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تَتَّخِذُوا آبَاءَكُمْ وَإِخْوَانَكُمْ
أَوْلِيَاءَ إِنِ اسْتَحَبُّوا الْكُفْرَ عَلَى الْإِيمَانِ ۚ وَمَن يَتَوَلَّهُم
مِّنكُمْ فَأُولَٰئِكَ هُمُ الظَّالِمُونَ
Ya ayyuha allatheena amanoola tattakhithoo abaakum wa-ikhwanakumawliyaa ini
istahabboo alkufra AAala al-eemaniwaman yatawallahum minkum faola-ika humu
aththalimoon
Swahili
Enyi mlio amini! Msiwafanye baba zenu na ndugu zenu kuwa vipenzi vyenu ikiwa
wanastahabu ukafiri kuliko Imani. Na katika nyinyi atakaye wafanya hao ndio
vipenzi vyake, basi hao ndio madhaalimu.
|
Ayah 9:24 الأية
قُلْ إِن كَانَ آبَاؤُكُمْ وَأَبْنَاؤُكُمْ وَإِخْوَانُكُمْ وَأَزْوَاجُكُمْ
وَعَشِيرَتُكُمْ وَأَمْوَالٌ اقْتَرَفْتُمُوهَا وَتِجَارَةٌ تَخْشَوْنَ كَسَادَهَا
وَمَسَاكِنُ تَرْضَوْنَهَا أَحَبَّ إِلَيْكُم مِّنَ اللَّهِ وَرَسُولِهِ وَجِهَادٍ
فِي سَبِيلِهِ فَتَرَبَّصُوا حَتَّىٰ يَأْتِيَ اللَّهُ بِأَمْرِهِ ۗ وَاللَّهُ لَا
يَهْدِي الْقَوْمَ الْفَاسِقِينَ
Qul in kana abaokumwaabnaokum wa-ikhwanukum waazwajukumwaAAasheeratukum
waamwalun iqtaraftumooha watijaratuntakhshawna kasadaha wamasakinu
tardawnahaahabba ilaykum mina Allahi warasoolihi wajihadinfee sabeelihi
fatarabbasoo hatta ya/tiya Allahubi-amrihi wallahu la yahdee alqawma alfasiqeen
Swahili
Sema: Ikiwa baba zenu, na wenenu, na ndugu zenu, na wake zenu, na jamaa zenu, na
mali mliyo yachuma, na biashara mnazo ogopa kuharibika, na majumba mnayo
yapenda, ni vipenzi zaidi kwenu kuliko Mwenyezi Mungu na Mtume wake na Jihadi
katika Njia yake, basi ngojeni mpaka Mwenyezi Mungu alete amri yake. Na Mwenyezi
Mungu hawaongoi watu wapotovu.
|
Ayah 9:25 الأية
لَقَدْ نَصَرَكُمُ اللَّهُ فِي مَوَاطِنَ كَثِيرَةٍ ۙ وَيَوْمَ حُنَيْنٍ ۙ إِذْ
أَعْجَبَتْكُمْ كَثْرَتُكُمْ فَلَمْ تُغْنِ عَنكُمْ شَيْئًا وَضَاقَتْ عَلَيْكُمُ
الْأَرْضُ بِمَا رَحُبَتْ ثُمَّ وَلَّيْتُم مُّدْبِرِينَ
Laqad nasarakumu Allahu feemawatina katheeratin wayawma hunaynin ithaAAjabatkum
kathratukum falam tughni AAankum shay-an wadaqatAAalaykumu al-ardu bima rahubat
thummawallaytum mudbireen
Swahili
Hakika Mwenyezi Mungu amekunusuruni katika mapigano mengi, na siku ya Hunayni
ambapo wingi wenu ulikupandisheni kichwa, lakini haukukufaeni kitu. Na ardhi
ikawa dhiki kwenu juu ya upana wake. Kisha mkageuka mkarudi nyuma.
|
Ayah 9:26 الأية
ثُمَّ أَنزَلَ اللَّهُ سَكِينَتَهُ عَلَىٰ رَسُولِهِ وَعَلَى الْمُؤْمِنِينَ
وَأَنزَلَ جُنُودًا لَّمْ تَرَوْهَا وَعَذَّبَ الَّذِينَ كَفَرُوا ۚ وَذَٰلِكَ
جَزَاءُ الْكَافِرِينَ
Thumma anzala Allahu sakeenatahu AAalarasoolihi waAAala almu/mineena waanzala
junoodan lamtarawha waAAaththaba allatheena kafaroo wathalikajazao alkafireen
Swahili
Kisha Mwenyezi Mungu akateremsha utulivu wake juu ya Mtume wake na juu ya
Waumini. Na akateremsha majeshi ambayo hamkuyaona, na akawaadhibu wale walio
kufuru. Na hayo ndiyo malipo ya makafiri.
|
Ayah 9:27 الأية
ثُمَّ يَتُوبُ اللَّهُ مِن بَعْدِ ذَٰلِكَ عَلَىٰ مَن يَشَاءُ ۗ وَاللَّهُ غَفُورٌ
رَّحِيمٌ
Thumma yatoobu Allahu min baAAdi thalikaAAala man yashao wallahu ghafoorunraheem
Swahili
Kisha baada ya hayo Mwenyezi Mungu atawasamehe awatakao. Na Mwenyezi Mungu ni
Mwenye kusamehe Mwenye kurehemu.
|
Ayah 9:28 الأية
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا إِنَّمَا الْمُشْرِكُونَ نَجَسٌ فَلَا يَقْرَبُوا
الْمَسْجِدَ الْحَرَامَ بَعْدَ عَامِهِمْ هَٰذَا ۚ وَإِنْ خِفْتُمْ عَيْلَةً
فَسَوْفَ يُغْنِيكُمُ اللَّهُ مِن فَضْلِهِ إِن شَاءَ ۚ إِنَّ اللَّهَ عَلِيمٌ
حَكِيمٌ
Ya ayyuha allatheena amanooinnama almushrikoona najasun fala yaqrabooalmasjida
alharama baAAda AAamihim hathawa-in khiftum AAaylatan fasawfa yughneekumu Allahu
min fadlihiin shaa inna Allaha AAaleemun hakeem
Swahili
Enyi mlio amini! Hakika washirikina ni najsi, kwa hivyo wasiukaribie Msikiti
Mtakatifu baada ya mwaka wao huu. Na ikiwa mnakhofia umasikini, basi Mwenyezi
Mungu atakutajirisheni kwa fadhila yake akipenda. Hakika Mwenyezi Mungu ni
Mwenye kujua Mwenye hikima.
|
Ayah 9:29 الأية
قَاتِلُوا الَّذِينَ لَا يُؤْمِنُونَ بِاللَّهِ وَلَا بِالْيَوْمِ الْآخِرِ وَلَا
يُحَرِّمُونَ مَا حَرَّمَ اللَّهُ وَرَسُولُهُ وَلَا يَدِينُونَ دِينَ الْحَقِّ
مِنَ الَّذِينَ أُوتُوا الْكِتَابَ حَتَّىٰ يُعْطُوا الْجِزْيَةَ عَن يَدٍ وَهُمْ
صَاغِرُونَ
Qatiloo allatheena layu/minoona billahi wala bilyawmial-akhiri wala yuharrimoona
ma harramaAllahu warasooluhu wala yadeenoona deena alhaqqimina allatheena ootoo
alkitaba hattayuAAtoo aljizyata AAan yadin wahum saghiroon
Swahili
Piganeni na wasio muamini Mwenyezi Mungu wala Siku ya Mwisho, wala hawaharimishi
alivyo harimisha Mwenyezi Mungu na Mtume, wala hawashiki Dini ya Haki, miongoni
mwa walio pewa Kitabu, mpaka watoe kodi kwa khiari yao, hali wamet'ii.
|
Ayah 9:30 الأية
وَقَالَتِ الْيَهُودُ عُزَيْرٌ ابْنُ اللَّهِ وَقَالَتِ النَّصَارَى الْمَسِيحُ
ابْنُ اللَّهِ ۖ ذَٰلِكَ قَوْلُهُم بِأَفْوَاهِهِمْ ۖ يُضَاهِئُونَ قَوْلَ
الَّذِينَ كَفَرُوا مِن قَبْلُ ۚ قَاتَلَهُمُ اللَّهُ ۚ أَنَّىٰ يُؤْفَكُونَ
Waqalati alyahoodu AAuzayrun ibnu Allahiwaqalati annasara almaseehuibnu Allahi
thalika qawluhum bi-afwahihim yudahi-oonaqawla allatheena kafaroo min qablu
qatalahumu Allahuanna yu/fakoon
Swahili
Na Mayahudi wanasema: Uzeir ni mwana wa Mungu. Na Wakristo wanasema: Masihi ni
mwana wa Mungu. Hiyo ndiyo kauli yao kwa vinywa vyao. Wanayaiga maneno ya walio
kufuru kabla yao. Mwenyezi Mungu awaangamize! Wanageuzwa namna gani hawa!
|
Ayah 9:31 الأية
اتَّخَذُوا أَحْبَارَهُمْ وَرُهْبَانَهُمْ أَرْبَابًا مِّن دُونِ اللَّهِ
وَالْمَسِيحَ ابْنَ مَرْيَمَ وَمَا أُمِرُوا إِلَّا لِيَعْبُدُوا إِلَٰهًا وَاحِدًا
ۖ لَّا إِلَٰهَ إِلَّا هُوَ ۚ سُبْحَانَهُ عَمَّا يُشْرِكُونَ
Ittakhathoo ahbarahumwaruhbanahum arbaban min dooni Allahi walmaseehaibna
maryama wama omiroo illa liyaAAbudoo ilahanwahidan la ilaha illa huwa
subhanahuAAamma yushrikoon
Swahili
Wamewafanya makuhani wao na wamonaki wao kuwa ni marabi badala ya Mwenyezi
Mungu, na pia Masihi bin Maryamu. Na wala hawakuamrishwa isipo kuwa wamuabudu
Mungu Mmoja, hapana mungu ila Yeye. Subhanahu, Ametakasika na hayo wanayo
mshirikisha nayo.
|
Ayah 9:32 الأية
يُرِيدُونَ أَن يُطْفِئُوا نُورَ اللَّهِ بِأَفْوَاهِهِمْ وَيَأْبَى اللَّهُ إِلَّا
أَن يُتِمَّ نُورَهُ وَلَوْ كَرِهَ الْكَافِرُونَ
Yureedoona an yutfi-oo noora Allahibi-afwahihim waya/ba Allahu illa anyutimma
noorahu walaw kariha alkafiroon
Swahili
Wanataka kuizima Nuru ya Mwenyezi Mungu kwa vinywa vyao, na Mwenyezi Mungu
anakataa ila aitimize Nuru yake ijapo kuwa makafiri watachukia.
|
Ayah 9:33 الأية
هُوَ الَّذِي أَرْسَلَ رَسُولَهُ بِالْهُدَىٰ وَدِينِ الْحَقِّ لِيُظْهِرَهُ عَلَى
الدِّينِ كُلِّهِ وَلَوْ كَرِهَ الْمُشْرِكُونَ
Huwa allathee arsala rasoolahu bilhudawadeeni alhaqqi liyuthhirahu AAala
addeenikullihi walaw kariha almushrikoon
Swahili
Yeye ndiye aliye mtuma Mtume wake kwa uwongofu na Dini ya Haki ipate kushinda
dini zote, ijapo kuwa washirikina watachukia.
|
Ayah 9:34 الأية
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا إِنَّ كَثِيرًا مِّنَ الْأَحْبَارِ وَالرُّهْبَانِ
لَيَأْكُلُونَ أَمْوَالَ النَّاسِ بِالْبَاطِلِ وَيَصُدُّونَ عَن سَبِيلِ اللَّهِ ۗ
وَالَّذِينَ يَكْنِزُونَ الذَّهَبَ وَالْفِضَّةَ وَلَا يُنفِقُونَهَا فِي سَبِيلِ
اللَّهِ فَبَشِّرْهُم بِعَذَابٍ أَلِيمٍ
Ya ayyuha allatheena amanooinna katheeran mina al-ahbari warruhbanilaya/kuloona
amwala annasi bilbatiliwayasuddoona AAan sabeeli Allahi wallatheenayaknizoona
aththahaba walfiddatawala yunfiqoonaha fee sabeeli Allahifabashshirhum
biAAathabin aleem
Swahili
Enyi mlio amini! Hakika wengi katika makuhani na wamonaki wanakula mali za watu
kwa baat'ili na wanazuilia Njia ya Mwenyezi Mungu. Na wanao kusanya dhahabu na
fedha, wala hawazitumii katika Njia ya Mwenyezi Mungu, wabashirie khabari ya
adhabu iliyo chungu.
|
Ayah 9:35 الأية
يَوْمَ يُحْمَىٰ عَلَيْهَا فِي نَارِ جَهَنَّمَ فَتُكْوَىٰ بِهَا جِبَاهُهُمْ
وَجُنُوبُهُمْ وَظُهُورُهُمْ ۖ هَٰذَا مَا كَنَزْتُمْ لِأَنفُسِكُمْ فَذُوقُوا مَا
كُنتُمْ تَكْنِزُونَ
Yawma yuhma AAalayhafee nari jahannama fatukwa biha jibahuhumwajunoobuhum
wathuhooruhum hatha makanaztum li-anfusikum fathooqoo ma kuntum taknizoon
Swahili
Siku zitapo tiwa moto katika Moto wa Jahannamu, na kwazo vikachomwa vipaji vya
nyuso zao na mbavu zao na migongo yao, wakaambiwa: Haya ndiyo mlio jilimbikia
nafsi zenu, basi onjeni mliyo kuwa mkilimbika.
|
Ayah 9:36 الأية
إِنَّ عِدَّةَ الشُّهُورِ عِندَ اللَّهِ اثْنَا عَشَرَ شَهْرًا فِي كِتَابِ اللَّهِ
يَوْمَ خَلَقَ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضَ مِنْهَا أَرْبَعَةٌ حُرُمٌ ۚ ذَٰلِكَ
الدِّينُ الْقَيِّمُ ۚ فَلَا تَظْلِمُوا فِيهِنَّ أَنفُسَكُمْ ۚ وَقَاتِلُوا
الْمُشْرِكِينَ كَافَّةً كَمَا يُقَاتِلُونَكُمْ كَافَّةً ۚ وَاعْلَمُوا أَنَّ
اللَّهَ مَعَ الْمُتَّقِينَ
Inna AAiddata ashshuhoori AAinda Allahiithna AAashara shahran fee kitabi
Allahiyawma khalaqa assamawati wal-ardaminha arbaAAatun hurumun thalika
addeenualqayyimu fala tathlimoo feehinna anfusakumwaqatiloo almushrikeena
kaffatan kama yuqatiloonakumkaffatan waAAlamoo anna Allaha maAAaalmuttaqeen
Swahili
Hakika idadi ya miezi kwa Mwenyezi Mungu ni miezi kumi na mbili katika hukumu ya
Mwenyezi Mungu tangu alipo umba mbingu na ardhi. Katika hiyo iko mine
mitakatifu. Hiyo ndiyo Dini iliyo sawa. Basi msidhulumu nafsi zenu humo. Na
piganeni na washirikina wote kama wao wnavyo pigana nanyi nyote. Na jueni kuwa
Mwenyezi Mungu yu pamoja na wachamngu.
|
Ayah 9:37 الأية
إِنَّمَا النَّسِيءُ زِيَادَةٌ فِي الْكُفْرِ ۖ يُضَلُّ بِهِ الَّذِينَ كَفَرُوا
يُحِلُّونَهُ عَامًا وَيُحَرِّمُونَهُ عَامًا لِّيُوَاطِئُوا عِدَّةَ مَا حَرَّمَ
اللَّهُ فَيُحِلُّوا مَا حَرَّمَ اللَّهُ ۚ زُيِّنَ لَهُمْ سُوءُ أَعْمَالِهِمْ ۗ
وَاللَّهُ لَا يَهْدِي الْقَوْمَ الْكَافِرِينَ
Innama annasee-o ziyadatunfee alkufri yudallu bihi allatheena kafaroo
yuhilloonahuAAaman wayuharrimoonahu AAaman liyuwati-ooAAiddata ma harrama Allahu
fayuhillooma harrama Allahu zuyyina lahum soo-o aAAmalihimwallahu la yahdee
alqawma alkafireen
Swahili
Bila ya shaka kuakhirisha (miezi) ni kuzidi katika kukufuru; kwa hayo hupotezwa
walio kufuru. Wanauhalalisha mwaka mmoja na kuharimisha mwaka mwingine, ili
wafanye kuwa sawa idadi ya ile (miezi) aliyo itukuza Mwenyezi Mungu. Kwa hivyo
huhalalisha alivyo viharimisha Mwenyezi Mungu. Wamepambiwa ubaya wa vitendo vyao
hivi. Na Mwenyezi Mungu hawaongoi watu makafiri.
|
Ayah 9:38 الأية
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا مَا لَكُمْ إِذَا قِيلَ لَكُمُ انفِرُوا فِي
سَبِيلِ اللَّهِ اثَّاقَلْتُمْ إِلَى الْأَرْضِ ۚ أَرَضِيتُم بِالْحَيَاةِ
الدُّنْيَا مِنَ الْآخِرَةِ ۚ فَمَا مَتَاعُ الْحَيَاةِ الدُّنْيَا فِي الْآخِرَةِ
إِلَّا قَلِيلٌ
Ya ayyuha allatheena amanooma lakum itha qeela lakumu infiroo fee sabeeli
Allahiiththaqaltum ila al-ardi aradeetum bilhayatiaddunya mina al-akhirati fama
mataAAualhayati addunya fee al-akhiratiilla qaleel
Swahili
Enyi mlio amini! Mna nini mnapo ambiwa: Nendeni katika Njia ya Mwenyezi Mungu,
mnajitia uzito katika ardhi? Je, mmeridhia maisha ya dunia kuliko ya Akhera?
Lakini starehe za maisha ya dunia kulinganisha na ya Akhera ni chache.
|
Ayah 9:39 الأية
إِلَّا تَنفِرُوا يُعَذِّبْكُمْ عَذَابًا أَلِيمًا وَيَسْتَبْدِلْ قَوْمًا
غَيْرَكُمْ وَلَا تَضُرُّوهُ شَيْئًا ۗ وَاللَّهُ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ
Illa tanfiroo yuAAaththibkumAAathaban aleeman wayastabdil qawman ghayrakum
walatadurroohu shay-an wallahu AAalakulli shay-in qadeer
Swahili
Kama hamwendi atakuadhibuni adhabu chungu, na atawaleta watu wengine, wala
nyinyi hamtamdhuru chochote. Na Mwenyezi Mungu ni Muweza wa kila kitu.
|
Ayah 9:40 الأية
إِلَّا تَنصُرُوهُ فَقَدْ نَصَرَهُ اللَّهُ إِذْ أَخْرَجَهُ الَّذِينَ كَفَرُوا
ثَانِيَ اثْنَيْنِ إِذْ هُمَا فِي الْغَارِ إِذْ يَقُولُ لِصَاحِبِهِ لَا تَحْزَنْ
إِنَّ اللَّهَ مَعَنَا ۖ فَأَنزَلَ اللَّهُ سَكِينَتَهُ عَلَيْهِ وَأَيَّدَهُ
بِجُنُودٍ لَّمْ تَرَوْهَا وَجَعَلَ كَلِمَةَ الَّذِينَ كَفَرُوا السُّفْلَىٰ ۗ
وَكَلِمَةُ اللَّهِ هِيَ الْعُلْيَا ۗ وَاللَّهُ عَزِيزٌ حَكِيمٌ
Illa tansuroohu faqad nasarahuAllahu ith akhrajahu allatheena kafaroo
thaniyaithnayni ith huma fee alghari ithyaqoolu lisahibihi la tahzan inna
AllahamaAAana faanzala Allahu sakeenatahu AAalayhiwaayyadahu bijunoodin lam
tarawha wajaAAala kalimata allatheenakafaroo assufla wakalimatu Allahi
hiyaalAAulya wallahu AAazeezun hakeem
Swahili
Ikiwa nyinyi hamtamnusuru Mtume, basi Mwenyezi Mungu alikwisha mnusuru walipo
mtoa walio kufuru, naye ni wa pili katika wawili walipo kuwa katika pango, naye
akamwambia sahibu yake: Usihuzunike. Hakika Mwenyezi Mungu yu pamoja nasi.
Mwenyezi Mungu akamteremshia utulivu wake, na akamuunga mkono kwa majeshi msiyo
yaona, na akalifanya neno la walio kufuru kuwa chini, na Neno la Mwenyezi Mungu
kuwa ndilo juu. Na Mwenyezi Mungu ndiye Mwenye nguvu Mwenye hikima.
|
Ayah 9:41 الأية
انفِرُوا خِفَافًا وَثِقَالًا وَجَاهِدُوا بِأَمْوَالِكُمْ وَأَنفُسِكُمْ فِي
سَبِيلِ اللَّهِ ۚ ذَٰلِكُمْ خَيْرٌ لَّكُمْ إِن كُنتُمْ تَعْلَمُونَ
Infiroo khifafan wathiqalanwajahidoo bi-amwalikum waanfusikum fee sabeeli
Allahithalikum khayrun lakum in kuntum taAAlamoon
Swahili
Nendeni mtoke, mkiwa wepesi na wazito, na piganeni Jihadi kwa mali yenu na nafsi
zenu katika Njia ya Mwenyezi Mungu. Haya ni kheri kwenu mkiwa mnajua.
|
Ayah 9:42 الأية
لَوْ كَانَ عَرَضًا قَرِيبًا وَسَفَرًا قَاصِدًا لَّاتَّبَعُوكَ وَلَٰكِن بَعُدَتْ
عَلَيْهِمُ الشُّقَّةُ ۚ وَسَيَحْلِفُونَ بِاللَّهِ لَوِ اسْتَطَعْنَا لَخَرَجْنَا
مَعَكُمْ يُهْلِكُونَ أَنفُسَهُمْ وَاللَّهُ يَعْلَمُ إِنَّهُمْ لَكَاذِبُونَ
Law kana AAaradan qareebanwasafaran qasidan lattabaAAooka walakinbaAAudat
AAalayhimu ashshuqqatu wasayahlifoona billahilawi istataAAna lakharajna
maAAakumyuhlikoona anfusahum wallahu yaAAlamu innahum lakathiboon
Swahili
Na lau ingeli kuwa ipo faida ya papo kwa papo, na safari yenyewe ni fupi,
wangeli kufuata. Lakini wameona ni mbali na kuna mashaka. Nao wataapa kwa
Mwenyezi Mungu: Tungeli weza bila ya shaka tungeli toka pamoja nanyi.
Wanaziangamiza nafsi zao. Na Mwenyezi Mungu anajua kuwa hakika hao ni waongo.
|
Ayah 9:43 الأية
عَفَا اللَّهُ عَنكَ لِمَ أَذِنتَ لَهُمْ حَتَّىٰ يَتَبَيَّنَ لَكَ الَّذِينَ
صَدَقُوا وَتَعْلَمَ الْكَاذِبِينَ
AAafa Allahu AAanka lima athintalahum hatta yatabayyana laka allatheena
sadaqoowataAAlama alkathibeen
Swahili
Mwenyezi Mungu amekusamehe! Kwa nini ukawapa ruhusa kabla ya kubainikia kwako
wanao sema kweli, na ukawajua waongo?
|
Ayah 9:44 الأية
لَا يَسْتَأْذِنُكَ الَّذِينَ يُؤْمِنُونَ بِاللَّهِ وَالْيَوْمِ الْآخِرِ أَن
يُجَاهِدُوا بِأَمْوَالِهِمْ وَأَنفُسِهِمْ ۗ وَاللَّهُ عَلِيمٌ بِالْمُتَّقِينَ
La yasta/thinuka allatheenayu/minoona billahi walyawmi al-akhirian yujahidoo
bi-amwalihim waanfusihim wallahuAAaleemun bilmuttaqeen
Swahili
Hawatakuomba ruhusa wale wanao muamini Mwenyezi Mungu na Siku ya Mwisho, wasende
kupigana Jihadi kwa mali yao na nafsi zao. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kuwajua
wachamngu.
|
Ayah 9:45 الأية
إِنَّمَا يَسْتَأْذِنُكَ الَّذِينَ لَا يُؤْمِنُونَ بِاللَّهِ وَالْيَوْمِ الْآخِرِ
وَارْتَابَتْ قُلُوبُهُمْ فَهُمْ فِي رَيْبِهِمْ يَتَرَدَّدُونَ
Innama yasta/thinuka allatheenala yu/minoona billahi walyawmi al-akhiriwartabat
quloobuhum fahum fee raybihimyataraddadoon
Swahili
Wasio muamini Mwenyezi Mungu na Siku ya Mwisho na nyoyo zao zikatia shaka, hao
tu ndio wanao kutaka ruhusa. Basi hao wanataradadi katika shaka zao.
|
Ayah 9:46 الأية
وَلَوْ أَرَادُوا الْخُرُوجَ لَأَعَدُّوا لَهُ عُدَّةً وَلَٰكِن كَرِهَ اللَّهُ
انبِعَاثَهُمْ فَثَبَّطَهُمْ وَقِيلَ اقْعُدُوا مَعَ الْقَاعِدِينَ
Walaw aradoo alkhurooja laaAAaddoolahu AAuddatan walakin kariha Allahu
inbiAAathahumfathabbatahum waqeela oqAAudoo maAAa alqaAAideen
Swahili
Na ingeli kuwa kweli walitaka kutoka bila ya shaka wangeli jiandalia maandalio,
lakini Mwenyezi Mungu kachukia kutoka kwao, na kwa hivyo akawazuia na ikasemwa:
Kaeni pamoja na wanao kaa!
|
Ayah 9:47 الأية
لَوْ خَرَجُوا فِيكُم مَّا زَادُوكُمْ إِلَّا خَبَالًا وَلَأَوْضَعُوا خِلَالَكُمْ
يَبْغُونَكُمُ الْفِتْنَةَ وَفِيكُمْ سَمَّاعُونَ لَهُمْ ۗ وَاللَّهُ عَلِيمٌ
بِالظَّالِمِينَ
Law kharajoo feekum ma zadookumilla khabalan walaawdaAAoo
khilalakumyabghoonakumu alfitnata wafeekum sammaAAoona lahum wallahuAAaleemun
biththalimeen
Swahili
Lau wangeli toka nanyi wasingeli kuzidishieni ila mchafuko, na wange tanga tanga
kati yenu kukutilieni fitna. Na miongoni mwenu wapo wanao wasikiliza. Na
Mwenyezi Mungu anawajua madhaalimu.
|
Ayah 9:48 الأية
لَقَدِ ابْتَغَوُا الْفِتْنَةَ مِن قَبْلُ وَقَلَّبُوا لَكَ الْأُمُورَ حَتَّىٰ
جَاءَ الْحَقُّ وَظَهَرَ أَمْرُ اللَّهِ وَهُمْ كَارِهُونَ
Laqadi ibtaghawoo alfitnata min qabluwaqallaboo laka al-omoora hatta jaa
alhaqquwathahara amru Allahi wahum karihoon
Swahili
Tangu zamani walitaka kukutilieni fitna, na wakakupindulia mambo juu chini,
mpaka ikaja Haki na ikadhihirika amri ya Mwenyezi Mungu, na wao wamechukia.
|
Ayah 9:49 الأية
وَمِنْهُم مَّن يَقُولُ ائْذَن لِّي وَلَا تَفْتِنِّي ۚ أَلَا فِي الْفِتْنَةِ
سَقَطُوا ۗ وَإِنَّ جَهَنَّمَ لَمُحِيطَةٌ بِالْكَافِرِينَ
Waminhum man yaqoolu i/than lee walataftinnee ala fee alfitnati saqatoo
wa-innajahannama lamuheetatun bilkafireen
Swahili
Na miongoni mwao wapo wanao sema: Niruhusu wala usinitie katika fitina. Kwa
yakini wao hivyo wamekwisha tumbukia katika fitina. Na hakika Jahannamu
imewazunguka.
|
Ayah 9:50 الأية
إِن تُصِبْكَ حَسَنَةٌ تَسُؤْهُمْ ۖ وَإِن تُصِبْكَ مُصِيبَةٌ يَقُولُوا قَدْ
أَخَذْنَا أَمْرَنَا مِن قَبْلُ وَيَتَوَلَّوا وَّهُمْ فَرِحُونَ
In tusibka hasanatun tasu/humwa-in tusibka museebatun yaqooloo qad
akhathnaamrana min qablu wayatawallaw wahum farihoon
Swahili
Ukikupata wema unawachukiza, na ukikusibu msiba, wao husema: Sisi tuliangalia
mambo yetu vizuri tangu kwanza. Na hugeuka kwenda zao nao wamefurahi.
|
Ayah 9:51 الأية
قُل لَّن يُصِيبَنَا إِلَّا مَا كَتَبَ اللَّهُ لَنَا هُوَ مَوْلَانَا ۚ وَعَلَى
اللَّهِ فَلْيَتَوَكَّلِ الْمُؤْمِنُونَ
Qul lan yuseebana illama kataba Allahu lana huwa mawlanawaAAala Allahi
falyatawakkali almu/minoon
Swahili
Sema: Halitusibu ila alilo tuandikia Mwenyezi Mungu. Yeye ndiye Mola wetu
Mlinzi. Na Waumini wamtegemee Mwenyezi Mungu tu!
|
Ayah 9:52 الأية
قُلْ هَلْ تَرَبَّصُونَ بِنَا إِلَّا إِحْدَى الْحُسْنَيَيْنِ ۖ وَنَحْنُ
نَتَرَبَّصُ بِكُمْ أَن يُصِيبَكُمُ اللَّهُ بِعَذَابٍ مِّنْ عِندِهِ أَوْ
بِأَيْدِينَا ۖ فَتَرَبَّصُوا إِنَّا مَعَكُم مُّتَرَبِّصُونَ
Qul hal tarabbasoona bina illaihda alhusnayayni wanahnu natarabbasubikum an
yuseebakumu Allahu biAAathabin minAAindihi aw bi-aydeena fatarabbasoo
innamaAAakum mutarabbisoon
Swahili
Sema: Hivyo mnatutazamia litupate lolote isipo kuwa moja katika mema mawili? Na
sisi tunakutazamieni kuwa Mwenyezi Mungu akufikishieni adhabu itokayo kwake, au
kutokana na mikono yetu. Basi ngojeni, nasi tunangoja pamoja nanyi.
|
Ayah 9:53 الأية
قُلْ أَنفِقُوا طَوْعًا أَوْ كَرْهًا لَّن يُتَقَبَّلَ مِنكُمْ ۖ إِنَّكُمْ كُنتُمْ
قَوْمًا فَاسِقِينَ
Qul anfiqoo tawAAan aw karhan lanyutaqabbala minkum innakum kuntum qawman
fasiqeen
Swahili
Sema: Toeni mkipenda msipende. Hakitopokelewa kitu kwenu, kwani nyinyi ni watu
wapotovu.
|
Ayah 9:54 الأية
وَمَا مَنَعَهُمْ أَن تُقْبَلَ مِنْهُمْ نَفَقَاتُهُمْ إِلَّا أَنَّهُمْ كَفَرُوا
بِاللَّهِ وَبِرَسُولِهِ وَلَا يَأْتُونَ الصَّلَاةَ إِلَّا وَهُمْ كُسَالَىٰ وَلَا
يُنفِقُونَ إِلَّا وَهُمْ كَارِهُونَ
Wama manaAAahum an tuqbala minhumnafaqatuhum illa annahum kafaroo
billahiwabirasoolihi wala ya/toona assalatailla wahum kusala wala yunfiqoona
illawahum karihoon
Swahili
Na hawakuzuiliwa kukubaliwa michango yao ila kwa kuwa walimkataa Mwenyezi Mungu
na Mtume wake, wala hawaji kwenye Sala ila kwa uvivu, wala hawatoi michango ila
nao wamechukia.
|
Ayah 9:55 الأية
فَلَا تُعْجِبْكَ أَمْوَالُهُمْ وَلَا أَوْلَادُهُمْ ۚ إِنَّمَا يُرِيدُ اللَّهُ
لِيُعَذِّبَهُم بِهَا فِي الْحَيَاةِ الدُّنْيَا وَتَزْهَقَ أَنفُسُهُمْ وَهُمْ
كَافِرُونَ
Fala tuAAjibka amwaluhum walaawladuhum innama yureedu Allahu
liyuAAaththibahumbiha fee alhayati addunyawatazhaqa anfusuhum wahum kafiroon
Swahili
Yasikufurahishe mali yao wala wana wao. Hakika Mwenyezi Mungu anataka kuwaadhibu
kwayo hapa duniani, na zitoke roho zao na hali wao ni makafiri.
|
Ayah 9:56 الأية
وَيَحْلِفُونَ بِاللَّهِ إِنَّهُمْ لَمِنكُمْ وَمَا هُم مِّنكُمْ وَلَٰكِنَّهُمْ
قَوْمٌ يَفْرَقُونَ
Wayahlifoona billahiinnahum laminkum wama hum minkum walakinnahumqawmun
yafraqoon
Swahili
Na wanaapa kwa Mwenyezi Mungu kwamba wao ni katika nyinyi, wala wao si katika
nyinyi. Lakini ni watu wanao ogopa.
|
Ayah 9:57 الأية
لَوْ يَجِدُونَ مَلْجَأً أَوْ مَغَارَاتٍ أَوْ مُدَّخَلًا لَّوَلَّوْا إِلَيْهِ
وَهُمْ يَجْمَحُونَ
Law yajidoona maljaan aw magharatinaw muddakhalan lawallaw ilayhi wahum
yajmahoon
Swahili
Lau kama wangeli pata pa kukimbilia au mapango au pahala pa kuingia basi wangeli
fyatuka mbio kuelekea huko.
|
Ayah 9:58 الأية
وَمِنْهُم مَّن يَلْمِزُكَ فِي الصَّدَقَاتِ فَإِنْ أُعْطُوا مِنْهَا رَضُوا وَإِن
لَّمْ يُعْطَوْا مِنْهَا إِذَا هُمْ يَسْخَطُونَ
Waminhum man yalmizuka fee assadaqatifa-in oAAtoo minha radoo wa-in lam
yuAAtawminha itha hum yaskhatoon
Swahili
Na miongoni mwao wapo wanao kusengenya katika kugawa sadaka. Wanapo pewa wao
huridhika. Na wakito pewa hukasirika.
|
Ayah 9:59 الأية
وَلَوْ أَنَّهُمْ رَضُوا مَا آتَاهُمُ اللَّهُ وَرَسُولُهُ وَقَالُوا حَسْبُنَا
اللَّهُ سَيُؤْتِينَا اللَّهُ مِن فَضْلِهِ وَرَسُولُهُ إِنَّا إِلَى اللَّهِ
رَاغِبُونَ
Walaw annahum radoo ma atahumuAllahu warasooluhu waqaloo hasbunaAllahu
sayu/teena Allahu min fadlihiwarasooluhu inna ila Allahi raghiboon
Swahili
Na laiti wao wangeli ridhia kile alicho wapa Mwenyezi Mungu na Mtume wake, na
wakasema: Mwenyezi Mungu anatutosheleza, Mwenyezi Mungu atatupa katika fadhila
yake - na pia Mtume wake; hakika sisi ni wenye kumtaka Mwenyezi Mungu!
|
Ayah 9:60 الأية
إِنَّمَا الصَّدَقَاتُ لِلْفُقَرَاءِ وَالْمَسَاكِينِ وَالْعَامِلِينَ عَلَيْهَا
وَالْمُؤَلَّفَةِ قُلُوبُهُمْ وَفِي الرِّقَابِ وَالْغَارِمِينَ وَفِي سَبِيلِ
اللَّهِ وَابْنِ السَّبِيلِ ۖ فَرِيضَةً مِّنَ اللَّهِ ۗ وَاللَّهُ عَلِيمٌ حَكِيمٌ
Innama assadaqatulilfuqara-i walmasakeeni walAAamileenaAAalayha walmu-allafati
quloobuhum wafee arriqabiwalgharimeena wafee sabeeli Allahi wabniassabeeli
fareedatan mina Allahi wallahuAAaleemun hakeemun
Swahili
Wa kupewa sadaka ni mafakiri, na masikini, na wanao zitumikia, na wa kutiwa
nguvu nyoyo zao, na katika kukomboa watumwa, na wenye madeni, na katika Njia ya
Mwenyezi Mungu, na wasafiri. Huu ni waajibu ulio faridhiwa na Mwenyezi Mungu. Na
Mwenyezi Mungu ni Mwenye kujua Mwenye hikima.
|
Ayah 9:61 الأية
وَمِنْهُمُ الَّذِينَ يُؤْذُونَ النَّبِيَّ وَيَقُولُونَ هُوَ أُذُنٌ ۚ قُلْ أُذُنُ
خَيْرٍ لَّكُمْ يُؤْمِنُ بِاللَّهِ وَيُؤْمِنُ لِلْمُؤْمِنِينَ وَرَحْمَةٌ
لِّلَّذِينَ آمَنُوا مِنكُمْ ۚ وَالَّذِينَ يُؤْذُونَ رَسُولَ اللَّهِ لَهُمْ
عَذَابٌ أَلِيمٌ
Waminhumu allatheena yu/thoonaannabiyya wayaqooloona huwa othunun qul
othunukhayrin lakum yu/minu billahi wayu/minulilmu/mineena warahmatun
lillatheena amanoominkum wallatheena yu/thoona rasoola Allahilahum AAathabun
aleem
Swahili
Na miongoni mwao wapo wanao muudhi Nabii na kusema: Yeye huyu ni sikio tu. Sema:
Basi ni sikio la kheri kwenu. Anamuamini Mwenyezi Mungu, na ana imani na
Waumini, naye ni rehema kwa wanao amini miongoni mwenu. Na wanao muudhi Mtume wa
Mwenyezi Mungu watapata adhabu chungu.
|
Ayah 9:62 الأية
يَحْلِفُونَ بِاللَّهِ لَكُمْ لِيُرْضُوكُمْ وَاللَّهُ وَرَسُولُهُ أَحَقُّ أَن
يُرْضُوهُ إِن كَانُوا مُؤْمِنِينَ
Yahlifoona billahilakum liyurdookum wallahu warasooluhu ahaqquan yurdoohu in
kanoo mu/mineen
Swahili
Wanakuapieni Mwenyezi Mungu ili kukuridhisheni nyinyi, hali ya kuwa wanao
stahiki zaidi kuridhishwa ni Mwenyezi Mungu na Mtume wake, lau kama wao ni
Waumini.
|
Ayah 9:63 الأية
أَلَمْ يَعْلَمُوا أَنَّهُ مَن يُحَادِدِ اللَّهَ وَرَسُولَهُ فَأَنَّ لَهُ نَارَ
جَهَنَّمَ خَالِدًا فِيهَا ۚ ذَٰلِكَ الْخِزْيُ الْعَظِيمُ
Alam yaAAlamoo annahu man yuhadidiAllaha warasoolahu faanna lahu nara jahannama
khalidanfeeha thalika alkhizyu alAAatheem
Swahili
Je, hawajui ya kwamba anaye shindana na Mwenyezi Mungu na Mtume wake, basi huyo
atapata Moto wa Jahannamu adumu humo? Hiyo ndiyo hizaya kubwa.
|
Ayah 9:64 الأية
يَحْذَرُ الْمُنَافِقُونَ أَن تُنَزَّلَ عَلَيْهِمْ سُورَةٌ تُنَبِّئُهُم بِمَا فِي
قُلُوبِهِمْ ۚ قُلِ اسْتَهْزِئُوا إِنَّ اللَّهَ مُخْرِجٌ مَّا تَحْذَرُونَ
Yahtharu almunafiqoona antunazzala AAalayhim sooratun tunabbi-ohum bima
feequloobihim quli istahzi-oo inna Allaha mukhrijun matahtharoon
Swahili
Wanaafiki wanaogopa isije teremshwa Sura itakayo watajia yaliyomo katika nyoyo
zao. Sema: Fanyeni mzaha! Hakika Mwenyezi Mungu atayatoa nje hayo mnayo yaogopa.
|
Ayah 9:65 الأية
وَلَئِن سَأَلْتَهُمْ لَيَقُولُنَّ إِنَّمَا كُنَّا نَخُوضُ وَنَلْعَبُ ۚ قُلْ
أَبِاللَّهِ وَآيَاتِهِ وَرَسُولِهِ كُنتُمْ تَسْتَهْزِئُونَ
Wala-in saaltahum layaqoolunna innamakunna nakhoodu wanalAAabu qul
abillahiwaayatihi warasoolihi kuntum tastahzi-oon
Swahili
Na ukiwauliza, wanasema: Sisi tulikuwa tukipiga porojo na kucheza tu. Sema:
Mlikuwa mkimfanyia maskhara Mwenyezi Mungu na Ishara zake na Mtume wake?
|
Ayah 9:66 الأية
لَا تَعْتَذِرُوا قَدْ كَفَرْتُم بَعْدَ إِيمَانِكُمْ ۚ إِن نَّعْفُ عَن طَائِفَةٍ
مِّنكُمْ نُعَذِّبْ طَائِفَةً بِأَنَّهُمْ كَانُوا مُجْرِمِينَ
La taAAtathiroo qad kafartumbaAAda eemanikum in naAAfu AAan ta-ifatin
minkumnuAAaththib ta-ifatan bi-annahum kanoomujrimeen
Swahili
Msitoe udhuru; mmekwisha kufuru baada ya kuamini kwenu! Tukilisamehe kundi moja
kati yenu, tutaliadhibu kundi jingine kwa kuwa wao ni wakosefu.
|
Ayah 9:67 الأية
الْمُنَافِقُونَ وَالْمُنَافِقَاتُ بَعْضُهُم مِّن بَعْضٍ ۚ يَأْمُرُونَ
بِالْمُنكَرِ وَيَنْهَوْنَ عَنِ الْمَعْرُوفِ وَيَقْبِضُونَ أَيْدِيَهُمْ ۚ نَسُوا
اللَّهَ فَنَسِيَهُمْ ۗ إِنَّ الْمُنَافِقِينَ هُمُ الْفَاسِقُونَ
Almunafiqoona walmunafiqatubaAAduhum min baAAdin ya/muroona bilmunkariwayanhawna
AAani almaAAroofi wayaqbidoona aydiyahum nasooAllaha fanasiyahum inna
almunafiqeena humu alfasiqoon
Swahili
Wanaume wanaafiki na wanawake wanaafiki, wote ni hali moja. Huamrisha maovu na
huyakataza mema, na huifumba mikono yao. Wamemsahau Mwenyezi Mungu, basi na Yeye
pia amewasahau. Hakika wanaafiki ndio wapotofu.
|
Ayah 9:68 الأية
وَعَدَ اللَّهُ الْمُنَافِقِينَ وَالْمُنَافِقَاتِ وَالْكُفَّارَ نَارَ جَهَنَّمَ
خَالِدِينَ فِيهَا ۚ هِيَ حَسْبُهُمْ ۚ وَلَعَنَهُمُ اللَّهُ ۖ وَلَهُمْ عَذَابٌ
مُّقِيمٌ
WaAAada Allahu almunafiqeenawalmunafiqati walkuffara narajahannama khalideena
feeha hiya hasbuhumwalaAAanahumu Allahu walahum AAathabun muqeem
Swahili
Mwenyezi Mungu amewaahidi wanaafiki wanaume na wanaafiki wanawake na makafiri
Moto wa Jahannamu kudumu humo. Hayo yanawatosha, na Mwenyezi Mungu amewalaani;
nao wana adhabu milele.
|
Ayah 9:69 الأية
كَالَّذِينَ مِن قَبْلِكُمْ كَانُوا أَشَدَّ مِنكُمْ قُوَّةً وَأَكْثَرَ أَمْوَالًا
وَأَوْلَادًا فَاسْتَمْتَعُوا بِخَلَاقِهِمْ فَاسْتَمْتَعْتُم بِخَلَاقِكُمْ كَمَا
اسْتَمْتَعَ الَّذِينَ مِن قَبْلِكُم بِخَلَاقِهِمْ وَخُضْتُمْ كَالَّذِي خَاضُوا ۚ
أُولَٰئِكَ حَبِطَتْ أَعْمَالُهُمْ فِي الدُّنْيَا وَالْآخِرَةِ ۖ وَأُولَٰئِكَ
هُمُ الْخَاسِرُونَ
Kallatheena min qablikum kanooashadda minkum quwwatan waakthara amwalan
waawladanfastamtaAAoo bikhalaqihim fastamtaAAtumbikhalaqikum kama istamtaAAa
allatheena minqablikum bikhalaqihim wakhudtum kallatheekhadoo ola-ika habitat
aAAmaluhumfee addunya wal-akhirati waola-ikahumu alkhasiroon
Swahili
Ni kama wale walio kuwa kabla yenu. Walikuwa wana nguvu na mali na watoto zaidi
kuliko nyinyi. Basi walistarehea fungu lao, na nyinyi mnastarehea fungu lenu,
kama walivyo starehe kwa fungu lao wale walio kuwa kabla yenu. Na nyinyi mkazama
katika maovu kama wao walivyo zama. Hao ndio ambao vitendo vyao vimeharibika
katika dunia na Akhera; na hao ndio walio khasiri.
|
Ayah 9:70 الأية
أَلَمْ يَأْتِهِمْ نَبَأُ الَّذِينَ مِن قَبْلِهِمْ قَوْمِ نُوحٍ وَعَادٍ وَثَمُودَ
وَقَوْمِ إِبْرَاهِيمَ وَأَصْحَابِ مَدْيَنَ وَالْمُؤْتَفِكَاتِ ۚ أَتَتْهُمْ
رُسُلُهُم بِالْبَيِّنَاتِ ۖ فَمَا كَانَ اللَّهُ لِيَظْلِمَهُمْ وَلَٰكِن كَانُوا
أَنفُسَهُمْ يَظْلِمُونَ
Alam ya/tihim nabao allatheena minqablihim qawmi noohin waAAadin wathamooda
waqawmiibraheema waas-habi madyana walmu/tafikatiatat-hum rusuluhum bilbayyinati
fama kanaAllahu liyathlimahum walakin kanooanfusahum yathlimoon
Swahili
Je, hazikuwafikia khabari za walio kuwa kabla yao - kaumu ya Nuhu, na A'ad, na
Thamud, na kaumu ya Ibrahim, na watu wa Madyana, na miji iliyo pinduliwa chini
juu? Mitume wao waliwafikia kwa hoja zilizo wazi. Basi Mwenyezi Mungu hakuwa
mwenye kuwadhulumu, walakini wao walikuwa wakijidhulumu wenyewe.
|
Ayah 9:71 الأية
وَالْمُؤْمِنُونَ وَالْمُؤْمِنَاتُ بَعْضُهُمْ أَوْلِيَاءُ بَعْضٍ ۚ يَأْمُرُونَ
بِالْمَعْرُوفِ وَيَنْهَوْنَ عَنِ الْمُنكَرِ وَيُقِيمُونَ الصَّلَاةَ وَيُؤْتُونَ
الزَّكَاةَ وَيُطِيعُونَ اللَّهَ وَرَسُولَهُ ۚ أُولَٰئِكَ سَيَرْحَمُهُمُ اللَّهُ
ۗ إِنَّ اللَّهَ عَزِيزٌ حَكِيمٌ
Walmu/minoona walmu/minatubaAAduhum awliyao baAAdin ya/muroona
bilmaAAroofiwayanhawna AAani almunkari wayuqeemoona assalatawayu/toona azzakata
wayuteeAAoona Allahawarasoolahu ola-ika sayarhamuhumu Allahuinna Allaha
AAazeezun hakeem
Swahili
Na Waumini wanaume na Waumini wanawake wao kwa wao ni marafiki walinzi.
Huamrisha mema na hukataza maovu, na hushika Sala, na hutoa Zaka, na humt'ii
Mwenyezi Mungu na Mtume wake. Hao Mwenyezi Mungu atawarehemu. Hakika Mwenyezi
Mungu ni Mtukufu Mwenye nguvu, Mwenye hikima.
|
Ayah 9:72 الأية
وَعَدَ اللَّهُ الْمُؤْمِنِينَ وَالْمُؤْمِنَاتِ جَنَّاتٍ تَجْرِي مِن تَحْتِهَا
الْأَنْهَارُ خَالِدِينَ فِيهَا وَمَسَاكِنَ طَيِّبَةً فِي جَنَّاتِ عَدْنٍ ۚ
وَرِضْوَانٌ مِّنَ اللَّهِ أَكْبَرُ ۚ ذَٰلِكَ هُوَ الْفَوْزُ الْعَظِيمُ
WaAAada Allahu almu/mineena walmu/minatijannatin tajree min tahtiha
al-anharukhalideena feeha wamasakina tayyibatanfee jannati AAadnin waridwanun
mina Allahiakbaru thalika huwa alfawzu alAAatheem
Swahili
Mwenyezi Mungu amewaahidi Waumini wanaume na Waumini wanawake Bustani zipitazo
mito kati yake, wadumu humo. Na makaazi mema katika Bustani za kudumu, na Radhi
za Mwenyezi Mungu ndio kubwa kuliko yote. Huko ndiko kufuzu kukubwa.
|
Ayah 9:73 الأية
يَا أَيُّهَا النَّبِيُّ جَاهِدِ الْكُفَّارَ وَالْمُنَافِقِينَ وَاغْلُظْ
عَلَيْهِمْ ۚ وَمَأْوَاهُمْ جَهَنَّمُ ۖ وَبِئْسَ الْمَصِيرُ
Ya ayyuha annabiyyu jahidialkuffara walmunafiqeena waghluthAAalayhim wama/wahum
jahannamu wabi/sa almaseer
Swahili
Ewe Nabii! Pambana na makafiri na wanaafiki, na wakazanie. Na makaazi yao ni
Jahannamu, na huo ndio mwisho mbaya.
|
Ayah 9:74 الأية
يَحْلِفُونَ بِاللَّهِ مَا قَالُوا وَلَقَدْ قَالُوا كَلِمَةَ الْكُفْرِ وَكَفَرُوا
بَعْدَ إِسْلَامِهِمْ وَهَمُّوا بِمَا لَمْ يَنَالُوا ۚ وَمَا نَقَمُوا إِلَّا أَنْ
أَغْنَاهُمُ اللَّهُ وَرَسُولُهُ مِن فَضْلِهِ ۚ فَإِن يَتُوبُوا يَكُ خَيْرًا
لَّهُمْ ۖ وَإِن يَتَوَلَّوْا يُعَذِّبْهُمُ اللَّهُ عَذَابًا أَلِيمًا فِي
الدُّنْيَا وَالْآخِرَةِ ۚ وَمَا لَهُمْ فِي الْأَرْضِ مِن وَلِيٍّ وَلَا نَصِيرٍ
Yahlifoona billahi maqaloo walaqad qaloo kalimata alkufri wakafaroobaAAda
islamihim wahammoo bima lam yanaloowama naqamoo illa an aghnahumu
Allahuwarasooluhu min fadlihi fa-in yatooboo yaku khayran lahumwa-in yatawallaw
yuAAaththibhumu Allahu AAathabanaleeman fee addunya wal-akhiratiwama lahum fee
al-ardi min waliyyin wala naseer
Swahili
Wanaapa kwa Mwenyezi Mungu kuwa hawakusema; nao wamekwisha sema neno la ukafiri,
na wakakufuru baada ya kusilimu kwao. Na wakajihimu kufanya ambayo hawakuweza
kuyafikia. Na hawakuchukia ila kuwa Mwenyezi Mungu na Mtume wake amewatajirisha
kutokana na fadhila zake. Wakitubu itakuwa kheri kwao, na wakigeuka Mwenyezi
Mungu atawaadhibu adhabu chungu duniani na Akhera. Na wala hawana katika ardhi
mlinzi wala wa kuwanusuru.
|
Ayah 9:75 الأية
وَمِنْهُم مَّنْ عَاهَدَ اللَّهَ لَئِنْ آتَانَا مِن فَضْلِهِ لَنَصَّدَّقَنَّ
وَلَنَكُونَنَّ مِنَ الصَّالِحِينَ
Waminhum man AAahada Allahala-in atana min fadlihi lanassaddaqannawalanakoonanna
mina assaliheen
Swahili
Na miongoni mwao wapo walio muahidi Mwenyezi Mungu kwa kusema: Akitupa katika
fadhila yake hapana shaka tutatoa sadaka, na tutakuwa katika watendao mema.
|
Ayah 9:76 الأية
فَلَمَّا آتَاهُم مِّن فَضْلِهِ بَخِلُوا بِهِ وَتَوَلَّوا وَّهُم مُّعْرِضُونَ
Falamma atahum min fadlihibakhiloo bihi watawallaw wahum muAAridoon
Swahili
Alipo wapa katika fadhila yake wakaifanyia ubakhili na wakageuka, na huku
wakipuuza.
|
Ayah 9:77 الأية
فَأَعْقَبَهُمْ نِفَاقًا فِي قُلُوبِهِمْ إِلَىٰ يَوْمِ يَلْقَوْنَهُ بِمَا
أَخْلَفُوا اللَّهَ مَا وَعَدُوهُ وَبِمَا كَانُوا يَكْذِبُونَ
FaaAAqabahum nifaqan fee quloobihimila yawmi yalqawnahu bima akhlafoo Allaha
mawaAAadoohu wabima kanoo yakthiboon
Swahili
Basi akawalipa unaafiki kuutia nyoyoni mwao mpaka Siku watapo kutana naye, kwa
sababu ya kuwa walimkhalifu Mwenyezi Mungu katika yale waliyo muahidi, na kwa
sababu ya kusema kwao uwongo.
|
Ayah 9:78 الأية
أَلَمْ يَعْلَمُوا أَنَّ اللَّهَ يَعْلَمُ سِرَّهُمْ وَنَجْوَاهُمْ وَأَنَّ اللَّهَ
عَلَّامُ الْغُيُوبِ
Alam yaAAlamoo anna Allaha yaAAlamusirrahum wanajwahum waanna Allaha
AAallamualghuyoob
Swahili
Je, hawajui kwamba Mwenyezi Mungu anajua siri zao na minong'ono yao, na kwamba
Mwenyezi Mungu ni Mwenye kuyajua sana ya ghaibu?
|
Ayah 9:79 الأية
الَّذِينَ يَلْمِزُونَ الْمُطَّوِّعِينَ مِنَ الْمُؤْمِنِينَ فِي الصَّدَقَاتِ
وَالَّذِينَ لَا يَجِدُونَ إِلَّا جُهْدَهُمْ فَيَسْخَرُونَ مِنْهُمْ ۙ سَخِرَ
اللَّهُ مِنْهُمْ وَلَهُمْ عَذَابٌ أَلِيمٌ
Allatheena yalmizoona almuttawwiAAeenamina almu/mineena fee assadaqati
wallatheenala yajidoona illa juhdahum fayaskharoona minhumsakhira Allahu minhum
walahum AAathabun aleem
Swahili
Wale wanao wabeuwa Waumini wanao toa sadaka nyingi na wasio nacho cha kutoa ila
kadri ya juhudi yao, basi huwakejeli. Mwenyezi Mungu atawakejeli wao! Nao
watapata adhabu chungu!
|
Ayah 9:80 الأية
اسْتَغْفِرْ لَهُمْ أَوْ لَا تَسْتَغْفِرْ لَهُمْ إِن تَسْتَغْفِرْ لَهُمْ
سَبْعِينَ مَرَّةً فَلَن يَغْفِرَ اللَّهُ لَهُمْ ۚ ذَٰلِكَ بِأَنَّهُمْ كَفَرُوا
بِاللَّهِ وَرَسُولِهِ ۗ وَاللَّهُ لَا يَهْدِي الْقَوْمَ الْفَاسِقِينَ
Istaghfir lahum aw la tastaghfirlahum in tastaghfir lahum sabAAeena marratan
falan yaghfira Allahulahum thalika bi-annahum kafaroo billahiwarasoolihi wallahu
la yahdee alqawma alfasiqeen
Swahili
Waombee msamaha au usiwaombee. Hata ukiwaombea msamaha mara sabiini, Mwenyezi
Mungu hatawasamehe. Hayo ni kwa sababu ya kuwa wao wamemkataa Mwenyezi Mungu na
Mtume wake. Na Mwenyezi Mungu hawaongoi watu wapotofu.
|
Ayah 9:81 الأية
فَرِحَ الْمُخَلَّفُونَ بِمَقْعَدِهِمْ خِلَافَ رَسُولِ اللَّهِ وَكَرِهُوا أَن
يُجَاهِدُوا بِأَمْوَالِهِمْ وَأَنفُسِهِمْ فِي سَبِيلِ اللَّهِ وَقَالُوا لَا
تَنفِرُوا فِي الْحَرِّ ۗ قُلْ نَارُ جَهَنَّمَ أَشَدُّ حَرًّا ۚ لَّوْ كَانُوا
يَفْقَهُونَ
Fariha almukhallafoona bimaqAAadihimkhilafa rasooli Allahi wakarihoo an
yujahidoobi-amwalihim waanfusihim fee sabeeli Allahi waqaloola tanfiroo fee
alharri qul naru jahannamaashaddu harran law kanoo yafqahoon
Swahili
Walifurahi walio achwa nyuma kwa kule kubakia kwao nyuma na kumuacha Mtume wa
Mwenyezi Mungu. Na walichukia kupigana Jihadi kwa mali zao na nafsi zao, na
wakasema: Msitoke nje katika joto! Sema: Moto wa Jahannamu una joto zaidi, laiti
wangeli fahamu!
|
Ayah 9:82 الأية
فَلْيَضْحَكُوا قَلِيلًا وَلْيَبْكُوا كَثِيرًا جَزَاءً بِمَا كَانُوا يَكْسِبُونَ
Falyadhakoo qaleelan walyabkookatheeran jazaan bima kanoo yaksiboon
Swahili
Basi nawacheke kidogo; watalia sana. Hayo ni malipo ya yale waliyo kuwa
wakiyachuma.
|
Ayah 9:83 الأية
فَإِن رَّجَعَكَ اللَّهُ إِلَىٰ طَائِفَةٍ مِّنْهُمْ فَاسْتَأْذَنُوكَ لِلْخُرُوجِ
فَقُل لَّن تَخْرُجُوا مَعِيَ أَبَدًا وَلَن تُقَاتِلُوا مَعِيَ عَدُوًّا ۖ
إِنَّكُمْ رَضِيتُم بِالْقُعُودِ أَوَّلَ مَرَّةٍ فَاقْعُدُوا مَعَ الْخَالِفِينَ
Fa-in rajaAAaka Allahu ila ta-ifatinminhum fasta/thanooka lilkhurooji faqul
lantakhrujoo maAAiya abadan walan tuqatiloo maAAiya AAaduwwaninnakum radeetum
bilquAAoodi awwala marratin faqAAudoomaAAa alkhalifeen
Swahili
Basi Mwenyezi Mungu akikurudisha kwenye kikundi kimoja miongoni mwao - na
wakakutaka idhini ya kutoka - sema: Nyinyi hamtatoka pamoja nami kabisa, wala
hamtapigana na adui pamoja nami. Nyinyi mliridhia kukaa nyuma mara ya kwanza,
basi kaeni pamoja na hao watakao bakia nyuma.
|
Ayah 9:84 الأية
وَلَا تُصَلِّ عَلَىٰ أَحَدٍ مِّنْهُم مَّاتَ أَبَدًا وَلَا تَقُمْ عَلَىٰ قَبْرِهِ
ۖ إِنَّهُمْ كَفَرُوا بِاللَّهِ وَرَسُولِهِ وَمَاتُوا وَهُمْ فَاسِقُونَ
Wala tusalli AAala ahadinminhum mata abadan wala taqum AAala qabrihiinnahum
kafaroo billahi warasoolihi wamatoowahum fasiqoon
Swahili
Wala usimsalie kabisa yeyote katika wao akifa, wala usisimame kaburini kwake.
Hakika hao wamemkataa Mwenyezi Mungu na Mtume wake, na wakafa na hali ni
wapotofu.
|
Ayah 9:85 الأية
وَلَا تُعْجِبْكَ أَمْوَالُهُمْ وَأَوْلَادُهُمْ ۚ إِنَّمَا يُرِيدُ اللَّهُ أَن
يُعَذِّبَهُم بِهَا فِي الدُّنْيَا وَتَزْهَقَ أَنفُسُهُمْ وَهُمْ كَافِرُونَ
Wala tuAAjibka amwaluhum waawladuhuminnama yureedu Allahu an yuAAaththibahum
bihafee addunya watazhaqa anfusuhum wahum kafiroon
Swahili
Wala zisikushitue mali zao na watoto wao. Mwenyezi Mungu anataka kuwaadhibu kwa
hayo katika dunia; na zitoke roho zao na hali wao ni makafiri.
|
Ayah 9:86 الأية
وَإِذَا أُنزِلَتْ سُورَةٌ أَنْ آمِنُوا بِاللَّهِ وَجَاهِدُوا مَعَ رَسُولِهِ
اسْتَأْذَنَكَ أُولُو الطَّوْلِ مِنْهُمْ وَقَالُوا ذَرْنَا نَكُن مَّعَ
الْقَاعِدِينَ
Wa-itha onzilat sooratun an aminoobillahi wajahidoo maAAa rasoolihi
ista/thanakaoloo attawli minhum waqaloo tharnanakun maAAa alqaAAideen
Swahili
Na inapo teremshwa Sura isemayo: Muaminini Mwenyezi Mungu na piganeni Jihadi
pamoja na Mtume wake, wale wenye nguvu miongoni mwao hukutaka ruhusa na husema:
Tuache tuwe pamoja na wanao kaa nyuma!
|
Ayah 9:87 الأية
رَضُوا بِأَن يَكُونُوا مَعَ الْخَوَالِفِ وَطُبِعَ عَلَىٰ قُلُوبِهِمْ فَهُمْ لَا
يَفْقَهُونَ
Radoo bi-an yakoonoo maAAa alkhawalifiwatubiAAa AAala quloobihim fahum
layafqahoon
Swahili
Wameridhia kuwa pamoja na wabakiao nyuma, na nyoyo zao zikapigwa muhuri; kwa
hivyo hawafahamu.
|
Ayah 9:88 الأية
لَٰكِنِ الرَّسُولُ وَالَّذِينَ آمَنُوا مَعَهُ جَاهَدُوا بِأَمْوَالِهِمْ
وَأَنفُسِهِمْ ۚ وَأُولَٰئِكَ لَهُمُ الْخَيْرَاتُ ۖ وَأُولَٰئِكَ هُمُ
الْمُفْلِحُونَ
Lakini arrasoolu wallatheenaamanoo maAAahu jahadoo bi-amwalihimwaanfusihim
waola-ika lahumu alkhayratu waola-ikahumu almuflihoon
Swahili
Lakini Mtume na wale walio amini pamoja naye waliwania Jihadi kwa mali zao na
nafsi zao. Hao ndio watakao pata kheri nyingi, na hao ndio wenye kufanikiwa.
|
Ayah 9:89 الأية
أَعَدَّ اللَّهُ لَهُمْ جَنَّاتٍ تَجْرِي مِن تَحْتِهَا الْأَنْهَارُ خَالِدِينَ
فِيهَا ۚ ذَٰلِكَ الْفَوْزُ الْعَظِيمُ
aAAadda Allahu lahum jannatintajree min tahtiha al-anharu khalideenafeeha
thalika alfawzu alAAatheem
Swahili
Mwenyezi Mungu amewatengenezea Bustani zipitazo mito kati yake, wadumu humo.
Huko ndiko kufuzu kukubwa.
|
Ayah 9:90 الأية
وَجَاءَ الْمُعَذِّرُونَ مِنَ الْأَعْرَابِ لِيُؤْذَنَ لَهُمْ وَقَعَدَ الَّذِينَ
كَذَبُوا اللَّهَ وَرَسُولَهُ ۚ سَيُصِيبُ الَّذِينَ كَفَرُوا مِنْهُمْ عَذَابٌ
أَلِيمٌ
Wajaa almuAAaththiroona minaal-aAArabi liyu/thana lahum waqaAAada
allatheenakathaboo Allaha warasoolahu sayuseebu allatheenakafaroo minhum
AAathabun aleem
Swahili
Na walikuja wenye kutoa udhuru katika Mabedui ili wapewe ruhusa, na wakakaa wale
walio mwambia Mwenyezi Mungu na Mtume wake uwongo. Itawafika walio kufuru katika
wao adhabu chungu.
|
Ayah 9:91 الأية
لَّيْسَ عَلَى الضُّعَفَاءِ وَلَا عَلَى الْمَرْضَىٰ وَلَا عَلَى الَّذِينَ لَا
يَجِدُونَ مَا يُنفِقُونَ حَرَجٌ إِذَا نَصَحُوا لِلَّهِ وَرَسُولِهِ ۚ مَا عَلَى
الْمُحْسِنِينَ مِن سَبِيلٍ ۚ وَاللَّهُ غَفُورٌ رَّحِيمٌ
Laysa AAala adduAAafa-iwala AAala almarda wala AAalaallatheena la yajidoona ma
yunfiqoona harajunitha nasahoo lillahi warasoolihi maAAala almuhsineena min
sabeelin wallahughafoorun raheem
Swahili
Hapana lawama kwa wanyonge, wagonjwa, na wasio pata cha kutumia, maadamu
wanamsafia niya Mwenyezi Mungu na Mtume wake. Hapana njia ya kuwalaumu wanao
fanya wema. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusamehe Mwenye kurehemu.
|
Ayah 9:92 الأية
وَلَا عَلَى الَّذِينَ إِذَا مَا أَتَوْكَ لِتَحْمِلَهُمْ قُلْتَ لَا أَجِدُ مَا
أَحْمِلُكُمْ عَلَيْهِ تَوَلَّوا وَّأَعْيُنُهُمْ تَفِيضُ مِنَ الدَّمْعِ حَزَنًا
أَلَّا يَجِدُوا مَا يُنفِقُونَ
Wala AAala allatheena ithama atawka litahmilahum qulta la ajidu maahmilukum
AAalayhi tawallaw waaAAyunuhum tafeedumina addamAAi hazanan alla yajidoo
mayunfiqoon
Swahili
Wala wale walio kujia ili uwachukue ukasema: Sina kipando cha kukuchukueni. Tena
wakarudi na macho yao yanamiminika machozi kwa huzuni ya kukosa cha kutoa.
|
Ayah 9:93 الأية
إِنَّمَا السَّبِيلُ عَلَى الَّذِينَ يَسْتَأْذِنُونَكَ وَهُمْ أَغْنِيَاءُ ۚ
رَضُوا بِأَن يَكُونُوا مَعَ الْخَوَالِفِ وَطَبَعَ اللَّهُ عَلَىٰ قُلُوبِهِمْ
فَهُمْ لَا يَعْلَمُونَ
Innama assabeelu AAalaallatheena yasta/thinoonaka wahum aghniyaoradoo bi-an
yakoonoo maAAa alkhawalifi watabaAAaAllahu AAala quloobihim fahum la yaAAlamoon
Swahili
Ipo njia ya kuwalaumu wale wanao kuomba ruhusa wasende vitani na hali wao ni
matajiri. Wameridhia kuwa pamoja na wanao bakia nyuma. Na Mwenyezi Mungu
amewapiga muhuri juu ya nyoyo zao. Kwa hivyo hawajui.
|
Ayah 9:94 الأية
يَعْتَذِرُونَ إِلَيْكُمْ إِذَا رَجَعْتُمْ إِلَيْهِمْ ۚ قُل لَّا تَعْتَذِرُوا لَن
نُّؤْمِنَ لَكُمْ قَدْ نَبَّأَنَا اللَّهُ مِنْ أَخْبَارِكُمْ ۚ وَسَيَرَى اللَّهُ
عَمَلَكُمْ وَرَسُولُهُ ثُمَّ تُرَدُّونَ إِلَىٰ عَالِمِ الْغَيْبِ وَالشَّهَادَةِ
فَيُنَبِّئُكُم بِمَا كُنتُمْ تَعْمَلُونَ
YaAAtathiroona ilaykum itharajaAAtum ilayhim qul la taAAtathiroo lan
nu/minalakum qad nabbaana Allahu min akhbarikumwasayara Allahu AAamalakum
warasooluhu thummaturaddoona ila AAalimi alghaybi washshahadatifayunabbi-okum
bima kuntum taAAmaloon
Swahili
WATAKUTOLEENI UDHURU mtapo warudia. Sema: Msitoe udhuru; hatukuaminini. Mwenyezi
Mungu amekwisha tueleza khabari zenu. Na Mwenyezi Mungu na Mtume wake wataviona
vitendo vyenu. Kisha mtarudishwa kwa Mjuzi wa ya siri na ya dhaahiri; naye
atakuambieni mliyo kuwa mkiyatenda.
|
Ayah 9:95 الأية
سَيَحْلِفُونَ بِاللَّهِ لَكُمْ إِذَا انقَلَبْتُمْ إِلَيْهِمْ لِتُعْرِضُوا
عَنْهُمْ ۖ فَأَعْرِضُوا عَنْهُمْ ۖ إِنَّهُمْ رِجْسٌ ۖ وَمَأْوَاهُمْ جَهَنَّمُ
جَزَاءً بِمَا كَانُوا يَكْسِبُونَ
Sayahlifoona billahilakum itha inqalabtum ilayhim lituAAridoo AAanhumfaaAAridoo
AAanhum innahum rijsun wama/wahumjahannamu jazaan bima kanoo yaksiboon
Swahili
Watakuapieni kwa Mwenyezi Mungu mtakapo rudi kwao ili muwaachilie mbali. Basi
waachilieni mbali. Hakika hao ni najsi, na makaazi yao ni Jahannamu, kuwa ni
malipo kwa waliyo kuwa wakiyachuma.
|
Ayah 9:96 الأية
يَحْلِفُونَ لَكُمْ لِتَرْضَوْا عَنْهُمْ ۖ فَإِن تَرْضَوْا عَنْهُمْ فَإِنَّ
اللَّهَ لَا يَرْضَىٰ عَنِ الْقَوْمِ الْفَاسِقِينَ
Yahlifoona lakum litardawAAanhum fa-in tardaw AAanhum fa-inna Allaha layarda
AAani alqawmi alfasiqeen
Swahili
Wanakuapieni ili muwe radhi nao. Basi hata mkiwa radhi nao nyiye, Mwenyezi Mungu
hawi radhi na watu wapotofu.
|
Ayah 9:97 الأية
الْأَعْرَابُ أَشَدُّ كُفْرًا وَنِفَاقًا وَأَجْدَرُ أَلَّا يَعْلَمُوا حُدُودَ مَا
أَنزَلَ اللَّهُ عَلَىٰ رَسُولِهِ ۗ وَاللَّهُ عَلِيمٌ حَكِيمٌ
Al-aAArabu ashaddu kufran wanifaqanwaajdaru alla yaAAlamoo hudooda ma
anzalaAllahu AAala rasoolihi wallahuAAaleemun hakeem
Swahili
Mabedui wamezidi sana katika ukafiri na unaafiki, na wameelekea zaidi kutojua
mipaka ya aliyo yateremsha Mwenyezi Mungu juu ya Mtume wake. Na Mwenyezi Mungu
ni Mjuzi Mwenye hikima.
|
Ayah 9:98 الأية
وَمِنَ الْأَعْرَابِ مَن يَتَّخِذُ مَا يُنفِقُ مَغْرَمًا وَيَتَرَبَّصُ بِكُمُ
الدَّوَائِرَ ۚ عَلَيْهِمْ دَائِرَةُ السَّوْءِ ۗ وَاللَّهُ سَمِيعٌ عَلِيمٌ
Wamina al-aAArabi man yattakhithuma yunfiqu maghraman wayatarabbasu bikumu
addawa-iraAAalayhim da-iratu assaw-i wallahusameeAAun AAaleem
Swahili
Na katika Mabedui hao wapo wanao fikiri kuwa wanayo yatoa ni gharama ya bure, na
wanakungojeleeni mambo yakugeukieni. Mageuko maovu yatakuwa juu yao! Na Mwenyezi
Mungu ni Mwenye kusikia Mwenye kujua.
|
Ayah 9:99 الأية
وَمِنَ الْأَعْرَابِ مَن يُؤْمِنُ بِاللَّهِ وَالْيَوْمِ الْآخِرِ وَيَتَّخِذُ مَا
يُنفِقُ قُرُبَاتٍ عِندَ اللَّهِ وَصَلَوَاتِ الرَّسُولِ ۚ أَلَا إِنَّهَا قُرْبَةٌ
لَّهُمْ ۚ سَيُدْخِلُهُمُ اللَّهُ فِي رَحْمَتِهِ ۗ إِنَّ اللَّهَ غَفُورٌ رَّحِيمٌ
Wamina al-aAArabi man yu/minu billahiwalyawmi al-akhiri wayattakhithu mayunfiqu
qurubatin AAinda Allahi wasalawatiarrasooli ala innaha qurbatun
lahumsayudkhiluhumu Allahu fee rahmatihi inna Allahaghafoorun raheem
Swahili
Na katika Mabedui wapo wanao muamini Mwenyezi Mungu na Siku ya Mwisho, na
wanaitakidi kuwa wanayo yatoa ndiyo ya kuwasogeza kwa Mwenyezi Mungu na ya
kuwapatia dua za Mtume. Naam! Hayo ni kweli mambo ya kuwasogeza. Mwenyezi Mungu
atawaingiza katika rehema yake. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye maghfira Mwenye
kurehemu.
|
Ayah 9:100 الأية
وَالسَّابِقُونَ الْأَوَّلُونَ مِنَ الْمُهَاجِرِينَ وَالْأَنصَارِ وَالَّذِينَ
اتَّبَعُوهُم بِإِحْسَانٍ رَّضِيَ اللَّهُ عَنْهُمْ وَرَضُوا عَنْهُ وَأَعَدَّ
لَهُمْ جَنَّاتٍ تَجْرِي تَحْتَهَا الْأَنْهَارُ خَالِدِينَ فِيهَا أَبَدًا ۚ
ذَٰلِكَ الْفَوْزُ الْعَظِيمُ
Wassabiqoona al-awwaloonamina almuhajireena wal-ansari wallatheenaittabaAAoohum
bi-ihsanin radiya AllahuAAanhum waradoo AAanhu waaAAadda lahum jannatintajree
tahtaha al-anharu khalideenafeeha abadan thalika alfawzu alAAatheem
Swahili
Na wale walio tangulia, wa kwanza, katika Wahajiri na Ansari, na walio wafuata
kwa wema, Mwenyezi Mungu ameridhika nao, na wao wameridhika naye; na
amewaandalia Bustani zipitazo mito kati yake, wadumu humo milele. Huko ndiko
kufuzu kukubwa.
|
Ayah 9:101 الأية
وَمِمَّنْ حَوْلَكُم مِّنَ الْأَعْرَابِ مُنَافِقُونَ ۖ وَمِنْ أَهْلِ الْمَدِينَةِ
ۖ مَرَدُوا عَلَى النِّفَاقِ لَا تَعْلَمُهُمْ ۖ نَحْنُ نَعْلَمُهُمْ ۚ
سَنُعَذِّبُهُم مَّرَّتَيْنِ ثُمَّ يُرَدُّونَ إِلَىٰ عَذَابٍ عَظِيمٍ
Wamimman hawlakum mina al-aAArabimunafiqoona wamin ahli almadeenati maradoo
AAala annifaqila taAAlamuhum nahnu naAAlamuhum sanuAAaththibuhummarratayni
thumma yuraddoona ila AAathabin AAatheem
Swahili
Na katika mabedui walio jirani zenu wamo wanaafiki; na katika wenyeji wa Madina
pia wapo walio bobea katika unaafiki. Wewe huwajui. Sisi tunawajua. Tutawaadhibu
mara mbili, kisha watarudishwa kwenye adhabu kubwa.
|
Ayah 9:102 الأية
وَآخَرُونَ اعْتَرَفُوا بِذُنُوبِهِمْ خَلَطُوا عَمَلًا صَالِحًا وَآخَرَ سَيِّئًا
عَسَى اللَّهُ أَن يَتُوبَ عَلَيْهِمْ ۚ إِنَّ اللَّهَ غَفُورٌ رَّحِيمٌ
Waakharoona iAAtarafoo bithunoobihimkhalatoo AAamalan salihan waakharasayyi-an
AAasa Allahu an yatooba AAalayhim inna Allahaghafoorun raheem
Swahili
Na wengine walikiri dhambi zao, wakachanganya vitendo vyema na vingine viovu.
Asaa Mwenyezi Mungu akapokea toba zao. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusamehe
Mwenye kurehemu.
|
Ayah 9:103 الأية
خُذْ مِنْ أَمْوَالِهِمْ صَدَقَةً تُطَهِّرُهُمْ وَتُزَكِّيهِم بِهَا وَصَلِّ
عَلَيْهِمْ ۖ إِنَّ صَلَاتَكَ سَكَنٌ لَّهُمْ ۗ وَاللَّهُ سَمِيعٌ عَلِيمٌ
Khuth min amwalihim sadaqatantutahhiruhum watuzakkeehim biha wasalliAAalayhim
inna salataka sakanun lahum wallahusameeAAun AAaleem
Swahili
Chukua sadaka katika mali zao, uwasafishe na uwatakase kwazo, na uwaombee
rehema. Hakika maombi yako ni utulivu kwao. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusikia
Mwenye kujua.
|
Ayah 9:104 الأية
أَلَمْ يَعْلَمُوا أَنَّ اللَّهَ هُوَ يَقْبَلُ التَّوْبَةَ عَنْ عِبَادِهِ
وَيَأْخُذُ الصَّدَقَاتِ وَأَنَّ اللَّهَ هُوَ التَّوَّابُ الرَّحِيمُ
Alam yaAAlamoo anna Allaha huwayaqbalu attawbata AAan AAibadihi
waya/khuthuassadaqati waanna Allaha huwa attawwabuarraheem
Swahili
Je! Hawajui ya kwamba Mwenyezi Mungu anapokea toba ya waja wake, na anazikubali
sadaka, na kwamba Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa kupokea toba na Mwenye kurehemu?
|
Ayah 9:105 الأية
وَقُلِ اعْمَلُوا فَسَيَرَى اللَّهُ عَمَلَكُمْ وَرَسُولُهُ وَالْمُؤْمِنُونَ ۖ
وَسَتُرَدُّونَ إِلَىٰ عَالِمِ الْغَيْبِ وَالشَّهَادَةِ فَيُنَبِّئُكُم بِمَا
كُنتُمْ تَعْمَلُونَ
Waquli iAAmaloo fasayara AllahuAAamalakum warasooluhu walmu/minoona
wasaturaddoona ilaAAalimi alghaybi washshahadatifayunabbi-okum bima kuntum
taAAmaloon
Swahili
Na sema: Tendeni vitendo. Na Mwenyezi Mungu, na Mtume wake, na Waumini wataviona
vitendo vyenu. Na mtarudishwa kwa Mwenye kujua siri na dhaahiri; naye
atakuambieni mliyo kuwa mkiyatenda.
|
Ayah 9:106 الأية
وَآخَرُونَ مُرْجَوْنَ لِأَمْرِ اللَّهِ إِمَّا يُعَذِّبُهُمْ وَإِمَّا يَتُوبُ
عَلَيْهِمْ ۗ وَاللَّهُ عَلِيمٌ حَكِيمٌ
Waakharoona murjawna li-amri Allahiimma yuAAaththibuhum wa-imma yatoobuAAalayhim
wallahu AAaleemun hakeem
Swahili
Na wapo wengine wanangojea amri ya Mwenyezi Mungu - ama atawaadhibu au
atawasamehe. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kujua Mwenye hikima.
|
Ayah 9:107 الأية
وَالَّذِينَ اتَّخَذُوا مَسْجِدًا ضِرَارًا وَكُفْرًا وَتَفْرِيقًا بَيْنَ
الْمُؤْمِنِينَ وَإِرْصَادًا لِّمَنْ حَارَبَ اللَّهَ وَرَسُولَهُ مِن قَبْلُ ۚ
وَلَيَحْلِفُنَّ إِنْ أَرَدْنَا إِلَّا الْحُسْنَىٰ ۖ وَاللَّهُ يَشْهَدُ إِنَّهُمْ
لَكَاذِبُونَ
Wallatheena ittakhathoomasjidan diraran wakufran watafreeqan baynaalmu/mineena
wa-irsadan liman haraba Allahawarasoolahu min qablu walayahlifunna in aradna
illaalhusna wallahu yashhadu innahum lakathiboon
Swahili
Na wapo walio jenga msikiti kwa ajili ya madhara na ukafiri na kuwafarikisha
Waumini, na pa kuvizia kwa walio mpiga vita Mwenyezi Mungu na Mtume wake hapo
kabla. Na bila ya shaka wataapa kwamba: Hatukukusudia ila wema tu. Na Mwenyezi
Mungu anashuhudia kuwa wao ni waongo.
|
Ayah 9:108 الأية
لَا تَقُمْ فِيهِ أَبَدًا ۚ لَّمَسْجِدٌ أُسِّسَ عَلَى التَّقْوَىٰ مِنْ أَوَّلِ
يَوْمٍ أَحَقُّ أَن تَقُومَ فِيهِ ۚ فِيهِ رِجَالٌ يُحِبُّونَ أَن يَتَطَهَّرُوا ۚ
وَاللَّهُ يُحِبُّ الْمُطَّهِّرِينَ
La taqum feehi abadan lamasjidunossisa AAala attaqwa min awwali yawmin ahaqquan
taqooma feehi feehi rijalun yuhibboona an yatatahharoowallahu yuhibbu
almuttahhireen
Swahili
Usisimame kwenye msikiti huo kabisa. Msikiti ulio jengwa juu ya msingi wa
uchamngu tangu siku ya mwanzo unastahiki zaidi wewe usimame ndani yake. Humo
wamo watu wanao penda kujitakasa. Na Mwenyezi Mungu anawapenda wanao jitakasa.
|
Ayah 9:109 الأية
أَفَمَنْ أَسَّسَ بُنْيَانَهُ عَلَىٰ تَقْوَىٰ مِنَ اللَّهِ وَرِضْوَانٍ خَيْرٌ أَم
مَّنْ أَسَّسَ بُنْيَانَهُ عَلَىٰ شَفَا جُرُفٍ هَارٍ فَانْهَارَ بِهِ فِي نَارِ
جَهَنَّمَ ۗ وَاللَّهُ لَا يَهْدِي الْقَوْمَ الظَّالِمِينَ
Afaman assasa bunyanahu AAalataqwa mina Allahi waridwanin khayrunam man assasa
bunyanahu AAala shafa jurufinharin fanhara bihi fee narijahannama wallahu la
yahdee alqawma aththalimeen
Swahili
Je! Mwenye kuweka msingi wa jengo lake juu ya kumcha Mwenyezi Mungu na radhi
zake ni bora au mwenye kuweka msingi wa jengo lake juu ya ukingo wa shimo linalo
burugunyika, na likaburugunyika naye katika Moto wa Jahannamu? Na Mwenyezi Mungu
hawaongoi watu madhaalimu.
|
Ayah 9:110 الأية
لَا يَزَالُ بُنْيَانُهُمُ الَّذِي بَنَوْا رِيبَةً فِي قُلُوبِهِمْ إِلَّا أَن
تَقَطَّعَ قُلُوبُهُمْ ۗ وَاللَّهُ عَلِيمٌ حَكِيمٌ
La yazalu bunyanuhumuallathee banaw reebatan fee quloobihim illa an
taqattaAAaquloobuhum wallahu AAaleemun hakeem
Swahili
Na jengo lao hilo walilo lijenga litakuwa sababu ya kutia wasiwasi nyoyoni mwao
mpaka nyoyo zao hizo zikatike vipande vipande. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kujua
Mwenye hikima.
|
Ayah 9:111 الأية
إِنَّ اللَّهَ اشْتَرَىٰ مِنَ الْمُؤْمِنِينَ أَنفُسَهُمْ وَأَمْوَالَهُم بِأَنَّ
لَهُمُ الْجَنَّةَ ۚ يُقَاتِلُونَ فِي سَبِيلِ اللَّهِ فَيَقْتُلُونَ وَيُقْتَلُونَ
ۖ وَعْدًا عَلَيْهِ حَقًّا فِي التَّوْرَاةِ وَالْإِنجِيلِ وَالْقُرْآنِ ۚ وَمَنْ
أَوْفَىٰ بِعَهْدِهِ مِنَ اللَّهِ ۚ فَاسْتَبْشِرُوا بِبَيْعِكُمُ الَّذِي
بَايَعْتُم بِهِ ۚ وَذَٰلِكَ هُوَ الْفَوْزُ الْعَظِيمُ
Inna Allaha ishtara minaalmu/mineena anfusahum waamwalahum bi-anna
lahumualjannata yuqatiloona fee sabeeli Allahifayaqtuloona wayuqtaloona waAAdan
AAalayhi haqqan fee attawratiwal-injeeli walqur-ani waman awfabiAAahdihi mina
Allahi fastabshiroo bibayAAikumuallathee bayaAAtum bihi wathalika huwaalfawzu
alAAatheem
Swahili
Hakika Mwenyezi Mungu amenunua kwa Waumini nafsi zao na mali zao kwa kuwa wao
watapata Pepo. Wanapigana katika Njia ya Mwenyezi Mungu - wanauwa na wanauwawa.
Hii ni ahadi aliyo jilazimisha kwa Haki katika Taurati na Injili na Qur'ani. Na
nani atimizae ahadi kuliko Mwenyezi Mungu? Basi furahini kwa biashara yenu mliyo
fanya naye. Na huko ndiko kufuzu kukubwa,
|
Ayah 9:112 الأية
التَّائِبُونَ الْعَابِدُونَ الْحَامِدُونَ السَّائِحُونَ الرَّاكِعُونَ
السَّاجِدُونَ الْآمِرُونَ بِالْمَعْرُوفِ وَالنَّاهُونَ عَنِ الْمُنكَرِ
وَالْحَافِظُونَ لِحُدُودِ اللَّهِ ۗ وَبَشِّرِ الْمُؤْمِنِينَ
Atta-iboona alAAabidoonaalhamidoona assa-ihoona arrakiAAoonaassajidoona
al-amiroona bilmaAAroofiwannahoona AAani almunkari walhafithoonalihudoodi Allahi
wabashshiri almu/mineen
Swahili
(Kwa) wanao tubia, wanao abudu, wanao himidi, wanao kimbilia kheri, wanao rukuu,
wanao sujudu, wanao amrisha mema na wanao kataza maovu, na wanao linda mipaka ya
Mwenyezi Mungu. Na wabashirie Waumini.
|
Ayah 9:113 الأية
مَا كَانَ لِلنَّبِيِّ وَالَّذِينَ آمَنُوا أَن يَسْتَغْفِرُوا لِلْمُشْرِكِينَ
وَلَوْ كَانُوا أُولِي قُرْبَىٰ مِن بَعْدِ مَا تَبَيَّنَ لَهُمْ أَنَّهُمْ
أَصْحَابُ الْجَحِيمِ
Ma kana linnabiyyi wallatheenaamanoo an yastaghfiroo lilmushrikeena walaw
kanooolee qurba min baAAdi ma tabayyana lahum annahum as-habualjaheem
Swahili
Haimpasii Nabii na wale walio amini kuwatakia msamaha washirikina, ijapo kuwa ni
jamaa zao, baada ya kwisha bainika kuwa hao ni watu wa Motoni.
|
Ayah 9:114 الأية
وَمَا كَانَ اسْتِغْفَارُ إِبْرَاهِيمَ لِأَبِيهِ إِلَّا عَن مَّوْعِدَةٍ وَعَدَهَا
إِيَّاهُ فَلَمَّا تَبَيَّنَ لَهُ أَنَّهُ عَدُوٌّ لِّلَّهِ تَبَرَّأَ مِنْهُ ۚ
إِنَّ إِبْرَاهِيمَ لَأَوَّاهٌ حَلِيمٌ
Wama kana istighfaruibraheema li-abeehi illa AAan mawAAidatin waAAadahaiyyahu
falamma tabayyana lahu annahu AAaduwwun lillahitabarraa minhu inna ibraheema
laawwahun haleem
Swahili
Wala haikuwa Ibrahim kumtakia msamaha baba yake ila kwa sababu wa ahadi aliyo
fanya naye. Lakini ilipo mbainikia kwamba yeye ni adui ya Mwenyezi Mungu,
alijiepusha naye. Hakika Ibrahim alikuwa mwingi wa kuomba, mnyenyekevu,
mvumilivu.
|
Ayah 9:115 الأية
وَمَا كَانَ اللَّهُ لِيُضِلَّ قَوْمًا بَعْدَ إِذْ هَدَاهُمْ حَتَّىٰ يُبَيِّنَ
لَهُم مَّا يَتَّقُونَ ۚ إِنَّ اللَّهَ بِكُلِّ شَيْءٍ عَلِيمٌ
Wama kana Allahu liyudillaqawman baAAda ith hadahum hattayubayyina lahum ma
yattaqoona inna Allaha bikullishay-in AAaleem
Swahili
Na haiwi kwa Mwenyezi Mungu kuwahisabu watu kuwa wamepotea baada ya kwisha
waongoza mpaka awabainishie ya kujiepusha nayo. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye
kujua kila kitu.
|
Ayah 9:116 الأية
إِنَّ اللَّهَ لَهُ مُلْكُ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ ۖ يُحْيِي وَيُمِيتُ ۚ وَمَا
لَكُم مِّن دُونِ اللَّهِ مِن وَلِيٍّ وَلَا نَصِيرٍ
Inna Allaha lahu mulku assamawatiwal-ardi yuhyee wayumeetu wama lakummin dooni
Allahi min waliyyin wala naseer
Swahili
Hakika Mwenyezi Mungu anao ufalme wa mbingu na ardhi; huhuisha na hufisha. Nanyi
hamna Mlinzi wala Msaidizi isipo kuwa Mwenyezi Mungu.
|
|