First Ayah 1 الأية الأوليبِسْم ِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ
الم
Swahili
Alif Lam Mim.
|
Ayah 2:2 الأية
ذَٰلِكَ الْكِتَابُ لَا رَيْبَ ۛ فِيهِ ۛ هُدًى لِّلْمُتَّقِينَ
Swahili
Hiki ni Kitabu kisichokuwa na shaka ndani yake; ni uwongofu kwa wachamungu,
|
Ayah 2:3 الأية
الَّذِينَ يُؤْمِنُونَ بِالْغَيْبِ وَيُقِيمُونَ الصَّلَاةَ وَمِمَّا رَزَقْنَاهُمْ
يُنفِقُونَ
Swahili
Ambao huyaamini ya ghaibu na hushika Sala, na hutoa katika tuliyo wapa.
|
Ayah 2:4 الأية
وَالَّذِينَ يُؤْمِنُونَ بِمَا أُنزِلَ إِلَيْكَ وَمَا أُنزِلَ مِن قَبْلِكَ
وَبِالْآخِرَةِ هُمْ يُوقِنُونَ
Swahili
Na ambao wanayaamini yaliyo teremshwa kwako, na yaliyo teremshwa kabla yako; na
Akhera wana yakini nayo.
|
Ayah 2:5 الأية
أُولَٰئِكَ عَلَىٰ هُدًى مِّن رَّبِّهِمْ ۖ وَأُولَٰئِكَ هُمُ الْمُفْلِحُونَ
Swahili
Hao wapo juu ya uwongofu utokao kwa Mola wao Mlezi, na hao ndio walio fanikiwa.
|
Ayah 2:6 الأية
إِنَّ الَّذِينَ كَفَرُوا سَوَاءٌ عَلَيْهِمْ أَأَنذَرْتَهُمْ أَمْ لَمْ تُنذِرْهُمْ
لَا يُؤْمِنُونَ
Swahili
Hakika wale walio kufuru ni sawa kwao ukiwaonya au usiwaonye, hawaamini.
|
Ayah 2:7 الأية
خَتَمَ اللَّهُ عَلَىٰ قُلُوبِهِمْ وَعَلَىٰ سَمْعِهِمْ ۖ وَعَلَىٰ أَبْصَارِهِمْ
غِشَاوَةٌ ۖ وَلَهُمْ عَذَابٌ عَظِيمٌ
Swahili
Mwenyezi Mungu amepiga muhuri juu ya nyoyo zao na juu ya masikio yao, na juu ya
macho yao pana kifuniko. Basi watapata adhabu kubwa.
|
Ayah 2:8 الأية
وَمِنَ النَّاسِ مَن يَقُولُ آمَنَّا بِاللَّهِ وَبِالْيَوْمِ الْآخِرِ وَمَا هُم
بِمُؤْمِنِينَ
Swahili
Na katika watu, wako wasemao: Tumemwamini Mwenyezi Mungu na Siku ya Mwisho, wala
wao si wenye kuamini.
|
Ayah 2:9 الأية
يُخَادِعُونَ اللَّهَ وَالَّذِينَ آمَنُوا وَمَا يَخْدَعُونَ إِلَّا أَنفُسَهُمْ
وَمَا يَشْعُرُونَ
Swahili
Wanatafuta kumdanganya Mwenyezi Mungu na wale walio amini, lakini hawadanganyi
ila nafsi zao; nao hawatambui.
|
Ayah 2:10 الأية
فِي قُلُوبِهِم مَّرَضٌ فَزَادَهُمُ اللَّهُ مَرَضًا ۖ وَلَهُمْ عَذَابٌ أَلِيمٌ
بِمَا كَانُوا يَكْذِبُونَ
Swahili
Nyoyoni mwao mna maradhi, na Mwenyezi Mungu amewazidishia maradhi. Basi watakuwa
na adhabu chungu kwa sababu ya kusema kwao uwongo.
|
Ayah 2:11 الأية
وَإِذَا قِيلَ لَهُمْ لَا تُفْسِدُوا فِي الْأَرْضِ قَالُوا إِنَّمَا نَحْنُ
مُصْلِحُونَ
Swahili
Na wanapo ambiwa: Msifanye uharibifu ulimwenguni. Husema: Bali sisi ni
watengenezaji.
|
Ayah 2:12 الأية
أَلَا إِنَّهُمْ هُمُ الْمُفْسِدُونَ وَلَٰكِن لَّا يَشْعُرُونَ
Swahili
Hakika wao ndio waharibifu, lakini hawatambui.
|
Ayah 2:13 الأية
وَإِذَا قِيلَ لَهُمْ آمِنُوا كَمَا آمَنَ النَّاسُ قَالُوا أَنُؤْمِنُ كَمَا آمَنَ
السُّفَهَاءُ ۗ أَلَا إِنَّهُمْ هُمُ السُّفَهَاءُ وَلَٰكِن لَّا يَعْلَمُونَ
Swahili
Na wanapo ambiwa: Aminini kama walivyo amini watu. Husema: Tuamini kama walivyo
amini wapumbavu? Hakika wao ndio wapumbavu, lakini hawajui tu.
|
Ayah 2:14 الأية
وَإِذَا لَقُوا الَّذِينَ آمَنُوا قَالُوا آمَنَّا وَإِذَا خَلَوْا إِلَىٰ
شَيَاطِينِهِمْ قَالُوا إِنَّا مَعَكُمْ إِنَّمَا نَحْنُ مُسْتَهْزِئُونَ
Swahili
Na wanapo kutana na walio amini husema: Tumeamini. Na wanapo kuwa peke yao na
mashet'ani wao husema: Hakika sisi tu pamoja nanyi. Hakika sisi tunawadhihaki tu.
|
Ayah 2:15 الأية
اللَّهُ يَسْتَهْزِئُ بِهِمْ وَيَمُدُّهُمْ فِي طُغْيَانِهِمْ يَعْمَهُونَ
Swahili
Mwenyezi Mungu atawadhihaki wao na atawawacha katika upotofu wao wakitangatanga
ovyo.
|
Ayah 2:16 الأية
أُولَٰئِكَ الَّذِينَ اشْتَرَوُا الضَّلَالَةَ بِالْهُدَىٰ فَمَا رَبِحَت
تِّجَارَتُهُمْ وَمَا كَانُوا مُهْتَدِينَ
Swahili
Hao ndio walio nunua upotofu kwa uwongofu; lakini biashara yao haikupata tija,
wala hawakuwa wenye kuongoka.
|
Ayah 2:17 الأية
مَثَلُهُمْ كَمَثَلِ الَّذِي اسْتَوْقَدَ نَارًا فَلَمَّا أَضَاءَتْ مَا حَوْلَهُ
ذَهَبَ اللَّهُ بِنُورِهِمْ وَتَرَكَهُمْ فِي ظُلُمَاتٍ لَّا يُبْصِرُونَ
Swahili
Mfano wao ni kama mfano wa aliye koka moto, na ulipo tanda mwangaza wake kote
kote Mwenyezi Mungu aliiondoa nuru yao na akawawacha katika giza, hawaoni.
|
Ayah 2:18 الأية
صُمٌّ بُكْمٌ عُمْيٌ فَهُمْ لَا يَرْجِعُونَ
Swahili
Viziwi, mabubu, vipofu; kwa hivyo hawatarejea.
|
Ayah 2:19 الأية
أَوْ كَصَيِّبٍ مِّنَ السَّمَاءِ فِيهِ ظُلُمَاتٌ وَرَعْدٌ وَبَرْقٌ يَجْعَلُونَ
أَصَابِعَهُمْ فِي آذَانِهِم مِّنَ الصَّوَاعِقِ حَذَرَ الْمَوْتِ ۚ وَاللَّهُ
مُحِيطٌ بِالْكَافِرِينَ
Swahili
Au ni kama mvua kubwa itokayo mbinguni, ina giza na radi na umeme; wakawa
wakitia vidole vyao masikioni mwao kwa ajili ya mingurumo, kwa kuogopa kufa. Na
Mwenyezi Mungu amewazunguka makafiri.
|
Ayah 2:20 الأية
يَكَادُ الْبَرْقُ يَخْطَفُ أَبْصَارَهُمْ ۖ كُلَّمَا أَضَاءَ لَهُم مَّشَوْا فِيهِ
وَإِذَا أَظْلَمَ عَلَيْهِمْ قَامُوا ۚ وَلَوْ شَاءَ اللَّهُ لَذَهَبَ بِسَمْعِهِمْ
وَأَبْصَارِهِمْ ۚ إِنَّ اللَّهَ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ
Swahili
Unakaribia umeme kunyakua macho yao. Kila ukiwatolea mwangaza huenda, na unapo
wafanyia giza husimama. Na angelitaka Mwenyezi Mungu angeliondoa kusikia kwao na
kuona kwao. Hakika Mwenyezi Mungu ni Muweza wa kila kitu.
|
Ayah 2:21 الأية
يَا أَيُّهَا النَّاسُ اعْبُدُوا رَبَّكُمُ الَّذِي خَلَقَكُمْ وَالَّذِينَ مِن
قَبْلِكُمْ لَعَلَّكُمْ تَتَّقُونَ
Swahili
Enyi watu! Muabuduni Mola wenu Mlezi aliye kuumbeni nyinyi na wale wa kabla yenu,
ili mpate kuokoka.
|
Ayah 2:22 الأية
الَّذِي جَعَلَ لَكُمُ الْأَرْضَ فِرَاشًا وَالسَّمَاءَ بِنَاءً وَأَنزَلَ مِنَ
السَّمَاءِ مَاءً فَأَخْرَجَ بِهِ مِنَ الثَّمَرَاتِ رِزْقًا لَّكُمْ ۖ فَلَا
تَجْعَلُوا لِلَّهِ أَندَادًا وَأَنتُمْ تَعْلَمُونَ
Swahili
(Mwenyezi Mungu) ambaye amekufanyieni hii ardhi kuwa kama tandiko, na mbingu
kama paa, na akateremsha maji kutoka mbinguni, na kwayo akatoa matunda yawe
riziki zenu. Basi msimfanyizie Mwenyezi Mungu washirika, na hali nyinyi mnajua.
|
Ayah 2:23 الأية
وَإِن كُنتُمْ فِي رَيْبٍ مِّمَّا نَزَّلْنَا عَلَىٰ عَبْدِنَا فَأْتُوا بِسُورَةٍ
مِّن مِّثْلِهِ وَادْعُوا شُهَدَاءَكُم مِّن دُونِ اللَّهِ إِن كُنتُمْ صَادِقِينَ
Swahili
Na ikiwa mna shaka kwa hayo tuliyo mteremshia mja wetu basi leteni sura moja ya
mfano wake, na muwaite mashahidi wenu badala ya Mwenyezi Mungu, ikiwa mnasema
kweli.
|
Ayah 2:24 الأية
فَإِن لَّمْ تَفْعَلُوا وَلَن تَفْعَلُوا فَاتَّقُوا النَّارَ الَّتِي وَقُودُهَا
النَّاسُ وَالْحِجَارَةُ ۖ أُعِدَّتْ لِلْكَافِرِينَ
Swahili
Na mkitofanya - na wala hamtofanya kamwe - basi uogopeni moto ambao kuni zake ni
watu na mawe walio andaliwa hao wanao kanusha.
|
Ayah 2:25 الأية
وَبَشِّرِ الَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ أَنَّ لَهُمْ جَنَّاتٍ
تَجْرِي مِن تَحْتِهَا الْأَنْهَارُ ۖ كُلَّمَا رُزِقُوا مِنْهَا مِن ثَمَرَةٍ
رِّزْقًا ۙ قَالُوا هَٰذَا الَّذِي رُزِقْنَا مِن قَبْلُ ۖ وَأُتُوا بِهِ
مُتَشَابِهًا ۖ وَلَهُمْ فِيهَا أَزْوَاجٌ مُّطَهَّرَةٌ ۖ وَهُمْ فِيهَا خَالِدُونَ
Swahili
Na wabashirie walio amini na wakatenda mema kwamba watapata mabustani yapitayo
mito kati yake; kila watapo pewa matunda humo, watasema: Haya ndiyo kama tuliyo
pewa mbele. Na wataletewa matunda yaliyo fanana; na humo watakuwa na wake walio
takasika; na wao humo watadumu.
|
Ayah 2:26 الأية
إِنَّ اللَّهَ لَا يَسْتَحْيِي أَن يَضْرِبَ مَثَلًا مَّا بَعُوضَةً فَمَا
فَوْقَهَا ۚ فَأَمَّا الَّذِينَ آمَنُوا فَيَعْلَمُونَ أَنَّهُ الْحَقُّ مِن
رَّبِّهِمْ ۖ وَأَمَّا الَّذِينَ كَفَرُوا فَيَقُولُونَ مَاذَا أَرَادَ اللَّهُ
بِهَٰذَا مَثَلًا ۘ يُضِلُّ بِهِ كَثِيرًا وَيَهْدِي بِهِ كَثِيرًا ۚ وَمَا يُضِلُّ
بِهِ إِلَّا الْفَاسِقِينَ
Swahili
Hakika Mwenyezi Mungu haoni haya kutoa mfano hata wa mbu na ulio wa zaidi yake.
Ama wale walio amini hujua ya kwamba hiyo ni haki iliyo toka kwa Mola wao Mlezi,
lakini wale walio kufuru husema: Ni nini analo kusudia Mwenyezi Mungu kwa mfano
huu? Kwa mfano huu huwapoteza wengi na huwaongoa wengi; lakini hawapotezi ila
wale wapotovu,
|
Ayah 2:27 الأية
الَّذِينَ يَنقُضُونَ عَهْدَ اللَّهِ مِن بَعْدِ مِيثَاقِهِ وَيَقْطَعُونَ مَا
أَمَرَ اللَّهُ بِهِ أَن يُوصَلَ وَيُفْسِدُونَ فِي الْأَرْضِ ۚ أُولَٰئِكَ هُمُ
الْخَاسِرُونَ
Swahili
Wanao vunja ahadi ya Mwenyezi Mungu baada ya kwisha ifunga, na wakayakata aliyo
amrisha Mwenyezi Mungu kuungwa, na wakafanya uharibifu katika nchi; hao ndio
wenye khasara.
|
Ayah 2:28 الأية
كَيْفَ تَكْفُرُونَ بِاللَّهِ وَكُنتُمْ أَمْوَاتًا فَأَحْيَاكُمْ ۖ ثُمَّ
يُمِيتُكُمْ ثُمَّ يُحْيِيكُمْ ثُمَّ إِلَيْهِ تُرْجَعُونَ
Swahili
Vipi mnamkanusha Mwenyezi Mungu na hali mlikuwa wafu akakufufueni! Kisha
atakufisheni, tena atakufufueni, kisha kwake mtarejeshwa?.
|
Ayah 2:29 الأية
هُوَ الَّذِي خَلَقَ لَكُم مَّا فِي الْأَرْضِ جَمِيعًا ثُمَّ اسْتَوَىٰ إِلَى
السَّمَاءِ فَسَوَّاهُنَّ سَبْعَ سَمَاوَاتٍ ۚ وَهُوَ بِكُلِّ شَيْءٍ عَلِيمٌ
Swahili
Yeye ndiye aliye kuumbieni vyote vilivyomo katika ardhi. Tena akazielekea mbingu,
na akazifanya mbingu saba. Naye ndiye Mjuzi wa kila kitu.
|
Ayah 2:30 الأية
وَإِذْ قَالَ رَبُّكَ لِلْمَلَائِكَةِ إِنِّي جَاعِلٌ فِي الْأَرْضِ خَلِيفَةً ۖ
قَالُوا أَتَجْعَلُ فِيهَا مَن يُفْسِدُ فِيهَا وَيَسْفِكُ الدِّمَاءَ وَنَحْنُ
نُسَبِّحُ بِحَمْدِكَ وَنُقَدِّسُ لَكَ ۖ قَالَ إِنِّي أَعْلَمُ مَا لَا تَعْلَمُونَ
Swahili
Na pale Mola wako Mlezi alipo waambia Malaika: Mimi nitamweka katika ardhi
Khalifa (mfwatizi), wakasema: Utaweka humo atakaye fanya uharibifu humo na
kumwaga damu, hali sisi tunakutakasa kwa sifa zako na tunakutaja kwa utakatifu
wako? Akasema: Hakika Mimi nayajua msiyo yajua.
|
Ayah 2:31 الأية
وَعَلَّمَ آدَمَ الْأَسْمَاءَ كُلَّهَا ثُمَّ عَرَضَهُمْ عَلَى الْمَلَائِكَةِ
فَقَالَ أَنبِئُونِي بِأَسْمَاءِ هَٰؤُلَاءِ إِن كُنتُمْ صَادِقِينَ
Swahili
Na akamfundisha Adam majina ya vitu vyote, kisha akaviweka mbele ya Malaika, na
akasema: Niambieni majina ya hivi ikiwa mnasema kweli.
|
Ayah 2:32 الأية
قَالُوا سُبْحَانَكَ لَا عِلْمَ لَنَا إِلَّا مَا عَلَّمْتَنَا ۖ إِنَّكَ أَنتَ
الْعَلِيمُ الْحَكِيمُ
Swahili
Wakasema: Subhanaka, Wewe umetakasika! Hatuna ujuzi isipokuwa kwa uliyo tufunza
Wewe. Hakika Wewe ndiye Mjuzi Mwenye hikima.
|
Ayah 2:33 الأية
قَالَ يَا آدَمُ أَنبِئْهُم بِأَسْمَائِهِمْ ۖ فَلَمَّا أَنبَأَهُم بِأَسْمَائِهِمْ
قَالَ أَلَمْ أَقُل لَّكُمْ إِنِّي أَعْلَمُ غَيْبَ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ
وَأَعْلَمُ مَا تُبْدُونَ وَمَا كُنتُمْ تَكْتُمُونَ
Swahili
Akasema: Ewe Adam! Waambie majina yake. Basi alipo waambia majina yake alisema:
Sikukwambieni kwamba Mimi ninajua siri za mbinguni na za duniani, na ninayajua
mnayo yadhihirisha na mliyo kuwa mnayaficha?
|
Ayah 2:34 الأية
وَإِذْ قُلْنَا لِلْمَلَائِكَةِ اسْجُدُوا لِآدَمَ فَسَجَدُوا إِلَّا إِبْلِيسَ
أَبَىٰ وَاسْتَكْبَرَ وَكَانَ مِنَ الْكَافِرِينَ
Swahili
Na tulipo waambia Malaika: Msujudieni Adam, wakamsujudia wote isipo kuwa Iblis,
alikataa na akajivuna na akawa katika makafiri.
|
Ayah 2:35 الأية
وَقُلْنَا يَا آدَمُ اسْكُنْ أَنتَ وَزَوْجُكَ الْجَنَّةَ وَكُلَا مِنْهَا رَغَدًا
حَيْثُ شِئْتُمَا وَلَا تَقْرَبَا هَٰذِهِ الشَّجَرَةَ فَتَكُونَا مِنَ
الظَّالِمِينَ
Swahili
Na tulisema: Ewe Adam! Kaa wewe na mkeo katika Bustani, na kuleni humo maridhawa
popote mpendapo, lakini msiukaribie mti huu tu; mkawa katika wale walio dhulumu.
|
Ayah 2:36 الأية
فَأَزَلَّهُمَا الشَّيْطَانُ عَنْهَا فَأَخْرَجَهُمَا مِمَّا كَانَا فِيهِ ۖ
وَقُلْنَا اهْبِطُوا بَعْضُكُمْ لِبَعْضٍ عَدُوٌّ ۖ وَلَكُمْ فِي الْأَرْضِ
مُسْتَقَرٌّ وَمَتَاعٌ إِلَىٰ حِينٍ
Swahili
Lakini Shet'ani aliwatelezesha hao wawili na akawatoa katika waliyo kuwamo, na
tukasema: Shukeni, nanyi ni maadui nyinyi kwa nyinyi. Katika ardhi yatakuwa
makaazi yenu na starehe kwa muda.
|
Ayah 2:37 الأية
فَتَلَقَّىٰ آدَمُ مِن رَّبِّهِ كَلِمَاتٍ فَتَابَ عَلَيْهِ ۚ إِنَّهُ هُوَ
التَّوَّابُ الرَّحِيمُ
Swahili
Kisha Adam akapokea maneno kwa Mola wake Mlezi, na Mola wake Mlezi alimkubalia
toba yake; hakika Yeye ndiye Mwingi wa kukubali toba na Mwenye kurehemu.
|
Ayah 2:38 الأية
قُلْنَا اهْبِطُوا مِنْهَا جَمِيعًا ۖ فَإِمَّا يَأْتِيَنَّكُم مِّنِّي هُدًى فَمَن
تَبِعَ هُدَايَ فَلَا خَوْفٌ عَلَيْهِمْ وَلَا هُمْ يَحْزَنُونَ
Swahili
Tukasema: Shukeni nyote; na kama ukikufikieni uwongofu utokao kwangu, basi
watakao fuata uwongofu wangu huo haitakuwa khofu juu yao wala hawatahuzunika.
|
Ayah 2:39 الأية
وَالَّذِينَ كَفَرُوا وَكَذَّبُوا بِآيَاتِنَا أُولَٰئِكَ أَصْحَابُ النَّارِ ۖ
هُمْ فِيهَا خَالِدُونَ
Swahili
Na wenye kukufuru na kuzikanusha ishara zetu, hao ndio watakao kuwa watu wa
Motoni, humo watadumu.
|
Ayah 2:40 الأية
يَا بَنِي إِسْرَائِيلَ اذْكُرُوا نِعْمَتِيَ الَّتِي أَنْعَمْتُ عَلَيْكُمْ
وَأَوْفُوا بِعَهْدِي أُوفِ بِعَهْدِكُمْ وَإِيَّايَ فَارْهَبُونِ
Swahili
Enyi Wana wa Israili! Kumbukeni neema yangu niliyo kuneemesheni, na timizeni
ahadi yangu, na Mimi nitatimiza ahadi yenu, na niogopeni Mimi tu.
|
Ayah 2:41 الأية
وَآمِنُوا بِمَا أَنزَلْتُ مُصَدِّقًا لِّمَا مَعَكُمْ وَلَا تَكُونُوا أَوَّلَ
كَافِرٍ بِهِ ۖ وَلَا تَشْتَرُوا بِآيَاتِي ثَمَنًا قَلِيلًا وَإِيَّايَ
فَاتَّقُونِ
Swahili
Na aminini niliyo yateremsha ambayo yanasadikisha mliyo nayo, wala msiwe wa
kwanza kuyakataa. Wala msiuze Ishara zangu kwa thamani ndogo. Na niogopeni Mimi
tu.
|
Ayah 2:42 الأية
وَلَا تَلْبِسُوا الْحَقَّ بِالْبَاطِلِ وَتَكْتُمُوا الْحَقَّ وَأَنتُمْ
تَعْلَمُونَ
Swahili
Wala msichanganye kweli na uwongo na mkaificha kweli nanyi mnajua.
|
Ayah 2:43 الأية
وَأَقِيمُوا الصَّلَاةَ وَآتُوا الزَّكَاةَ وَارْكَعُوا مَعَ الرَّاكِعِينَ
Swahili
Na shikeni Sala, na toeni Zaka, na inameni pamoja na wanao inama.
|
Ayah 2:44 الأية
أَتَأْمُرُونَ النَّاسَ بِالْبِرِّ وَتَنسَوْنَ أَنفُسَكُمْ وَأَنتُمْ تَتْلُونَ
الْكِتَابَ ۚ أَفَلَا تَعْقِلُونَ
Swahili
Je! Mnawaamrisha watu mema na mnajisahau nafsi zenu, na hali nyinyi mnasoma
Kitabu? Basi je, hamzingatii?
|
Ayah 2:45 الأية
وَاسْتَعِينُوا بِالصَّبْرِ وَالصَّلَاةِ ۚ وَإِنَّهَا لَكَبِيرَةٌ إِلَّا عَلَى
الْخَاشِعِينَ
Swahili
Na tafuteni msaada kwa kusubiri na kwa kusali; na kwa hakika jambo hilo ni gumu
isipokuwa kwa wanyenyekevu,
|
Ayah 2:46 الأية
الَّذِينَ يَظُنُّونَ أَنَّهُم مُّلَاقُو رَبِّهِمْ وَأَنَّهُمْ إِلَيْهِ
رَاجِعُونَ
Swahili
Ambao wana yakini kuwa hakika watakutana na Mola wao Mlezi na ya kuwa hakika
watarejea kwake.
|
Ayah 2:47 الأية
يَا بَنِي إِسْرَائِيلَ اذْكُرُوا نِعْمَتِيَ الَّتِي أَنْعَمْتُ عَلَيْكُمْ
وَأَنِّي فَضَّلْتُكُمْ عَلَى الْعَالَمِينَ
Swahili
Enyi Wana wa Israili! Kumbukeni zile neema zangu nilizo kuneemesheni, na
nikakuteuweni kuliko wote wengineo.
|
Ayah 2:48 الأية
وَاتَّقُوا يَوْمًا لَّا تَجْزِي نَفْسٌ عَن نَّفْسٍ شَيْئًا وَلَا يُقْبَلُ
مِنْهَا شَفَاعَةٌ وَلَا يُؤْخَذُ مِنْهَا عَدْلٌ وَلَا هُمْ يُنصَرُونَ
Swahili
Na iogopeni Siku ambayo mtu hatomfaa mtu kwa lolote, wala hayatakubaliwa kwake
maombezi, wala hakitapokewa kikomboleo kwake; wala hawatanusuriwa.
|
Ayah 2:49 الأية
وَإِذْ نَجَّيْنَاكُم مِّنْ آلِ فِرْعَوْنَ يَسُومُونَكُمْ سُوءَ الْعَذَابِ
يُذَبِّحُونَ أَبْنَاءَكُمْ وَيَسْتَحْيُونَ نِسَاءَكُمْ ۚ وَفِي ذَٰلِكُم بَلَاءٌ
مِّن رَّبِّكُمْ عَظِيمٌ
Swahili
Na vile tulipo kuokoeni kwa watu wa Firauni walio kupeni adhabu mbaya,
wakiwachinja wana wenu wa kiume na wakawawacha hai wanawake; na katika hayo
ulikuwa ni mtihani mkubwa ulio toka kwa Mola wenu Mlezi.
|
Ayah 2:50 الأية
وَإِذْ فَرَقْنَا بِكُمُ الْبَحْرَ فَأَنجَيْنَاكُمْ وَأَغْرَقْنَا آلَ فِرْعَوْنَ
وَأَنتُمْ تَنظُرُونَ
Swahili
Na tulipo ipasua bahari kwa ajili yenu na tukakuokoeni, tukawazamisha watu wa
Firauni, na huku mnatazama.
|
Ayah 2:51 الأية
وَإِذْ وَاعَدْنَا مُوسَىٰ أَرْبَعِينَ لَيْلَةً ثُمَّ اتَّخَذْتُمُ الْعِجْلَ مِن
بَعْدِهِ وَأَنتُمْ ظَالِمُونَ
Swahili
Na tulipo muahidi Musa masiku arubaini, kisha mkachukua ndama (mkamuabudu) baada
yake, na mkawa wenye kudhulumu.
|
Ayah 2:52 الأية
ثُمَّ عَفَوْنَا عَنكُم مِّن بَعْدِ ذَٰلِكَ لَعَلَّكُمْ تَشْكُرُونَ
Swahili
Kisha tukakusameheni baada ya hayo, ili mpate kushukuru.
|
Ayah 2:53 الأية
وَإِذْ آتَيْنَا مُوسَى الْكِتَابَ وَالْفُرْقَانَ لَعَلَّكُمْ تَهْتَدُونَ
Swahili
Na tulipo mpa Musa Kitabu na pambanuo ili mpate kuongoka.
|
Ayah 2:54 الأية
وَإِذْ قَالَ مُوسَىٰ لِقَوْمِهِ يَا قَوْمِ إِنَّكُمْ ظَلَمْتُمْ أَنفُسَكُم
بِاتِّخَاذِكُمُ الْعِجْلَ فَتُوبُوا إِلَىٰ بَارِئِكُمْ فَاقْتُلُوا أَنفُسَكُمْ
ذَٰلِكُمْ خَيْرٌ لَّكُمْ عِندَ بَارِئِكُمْ فَتَابَ عَلَيْكُمْ ۚ إِنَّهُ هُوَ
التَّوَّابُ الرَّحِيمُ
Swahili
Na Musa alipo waambia watu wake: Enyi watu wangu! Hakika nyinyi mmezidhulumu
nafsi zenu kwa kuchukua kwenu ndama (kumuabudu). Basi tubuni kwa Muumba wenu na
ziueni nafsi zenu. Haya ni bora kwenu mbele ya Muumba wenu. Naye akapokea toba
yenu. Hakika Yeye ndiye apokeaye toba na Mwenye kurehemu.
|
Ayah 2:55 الأية
وَإِذْ قُلْتُمْ يَا مُوسَىٰ لَن نُّؤْمِنَ لَكَ حَتَّىٰ نَرَى اللَّهَ جَهْرَةً
فَأَخَذَتْكُمُ الصَّاعِقَةُ وَأَنتُمْ تَنظُرُونَ
Swahili
Na mlipo sema: Ewe Musa! Hatutakuamini mpaka tumwone Mwenyezi Mungu waziwazi.
Ikakunyakueni radi nanyi mnaangalia.
|
Ayah 2:56 الأية
ثُمَّ بَعَثْنَاكُم مِّن بَعْدِ مَوْتِكُمْ لَعَلَّكُمْ تَشْكُرُونَ
Swahili
Kisha tukakufufueni baada ya kufa kwenu, ili mpate kushukuru.
|
Ayah 2:57 الأية
وَظَلَّلْنَا عَلَيْكُمُ الْغَمَامَ وَأَنزَلْنَا عَلَيْكُمُ الْمَنَّ
وَالسَّلْوَىٰ ۖ كُلُوا مِن طَيِّبَاتِ مَا رَزَقْنَاكُمْ ۖ وَمَا ظَلَمُونَا
وَلَٰكِن كَانُوا أَنفُسَهُمْ يَظْلِمُونَ
Swahili
Na tukakutilieni kivuli kwa mawingu na tukakuteremshieni Manna na Salwa;
tukakwambieni: Kuleni vitu vizuri hivi tulivyo kuruzukuni. Nao hawakutudhulumu
Sisi lakini walikuwa wanajidhulumu nafsi zao.
|
Ayah 2:58 الأية
وَإِذْ قُلْنَا ادْخُلُوا هَٰذِهِ الْقَرْيَةَ فَكُلُوا مِنْهَا حَيْثُ شِئْتُمْ
رَغَدًا وَادْخُلُوا الْبَابَ سُجَّدًا وَقُولُوا حِطَّةٌ نَّغْفِرْ لَكُمْ
خَطَايَاكُمْ ۚ وَسَنَزِيدُ الْمُحْسِنِينَ
Swahili
Na tulipo sema: Ingieni mji huu, na humo mle mpendapo maridhawa, na ingieni
katika mlango wake kwa unyenyekevu, na semeni: Tusamehe! Tutakusameheni makosa
yenu, na tutawazidishia wema wafanyao wema.
|
Ayah 2:59 الأية
فَبَدَّلَ الَّذِينَ ظَلَمُوا قَوْلًا غَيْرَ الَّذِي قِيلَ لَهُمْ فَأَنزَلْنَا
عَلَى الَّذِينَ ظَلَمُوا رِجْزًا مِّنَ السَّمَاءِ بِمَا كَانُوا يَفْسُقُونَ
Swahili
Lakini walio dhulumu waliibadili kauli isiyo kuwa waliyo ambiwa. Kwa hivyo
tukaiteremsha juu ya wale walio dhulumu adhabu kutoka mbinguni kwa sababu ya
walivyo kuwa wamepotoka.
|
Ayah 2:60 الأية
وَإِذِ اسْتَسْقَىٰ مُوسَىٰ لِقَوْمِهِ فَقُلْنَا اضْرِب بِّعَصَاكَ الْحَجَرَ ۖ
فَانفَجَرَتْ مِنْهُ اثْنَتَا عَشْرَةَ عَيْنًا ۖ قَدْ عَلِمَ كُلُّ أُنَاسٍ
مَّشْرَبَهُمْ ۖ كُلُوا وَاشْرَبُوا مِن رِّزْقِ اللَّهِ وَلَا تَعْثَوْا فِي
الْأَرْضِ مُفْسِدِينَ
Swahili
Na Musa alipo omba maji kwa ajili ya watu wake, tulimwambia: Lipige jiwe kwa
fimbo yako. Mara zikatimbuka chemchem kumi na mbili; kila kabila ikajua mahali
pake pa kunywea. Tukawaambia: Kuleni na mnywe riziki ya Mwenyezi Mungu, wala
msiasi katika nchi mkafanya uharibifu.
|
Ayah 2:61 الأية
وَإِذْ قُلْتُمْ يَا مُوسَىٰ لَن نَّصْبِرَ عَلَىٰ طَعَامٍ وَاحِدٍ فَادْعُ لَنَا
رَبَّكَ يُخْرِجْ لَنَا مِمَّا تُنبِتُ الْأَرْضُ مِن بَقْلِهَا وَقِثَّائِهَا
وَفُومِهَا وَعَدَسِهَا وَبَصَلِهَا ۖ قَالَ أَتَسْتَبْدِلُونَ الَّذِي هُوَ
أَدْنَىٰ بِالَّذِي هُوَ خَيْرٌ ۚ اهْبِطُوا مِصْرًا فَإِنَّ لَكُم مَّا سَأَلْتُمْ
ۗ وَضُرِبَتْ عَلَيْهِمُ الذِّلَّةُ وَالْمَسْكَنَةُ وَبَاءُوا بِغَضَبٍ مِّنَ
اللَّهِ ۗ ذَٰلِكَ بِأَنَّهُمْ كَانُوا يَكْفُرُونَ بِآيَاتِ اللَّهِ وَيَقْتُلُونَ
النَّبِيِّينَ بِغَيْرِ الْحَقِّ ۗ ذَٰلِكَ بِمَا عَصَوا وَّكَانُوا يَعْتَدُونَ
Swahili
Na mlipo sema: Ewe Musa! Hatuwezi kuvumilia chakula cha namna moja tu, basi
tuombee kwa Mola wako Mlezi atutolee vile vinavyo mea katika ardhi, kama mboga
zake, na matango yake, na thom zake, na adesi zake, na vitunguu vyake. Akasema:
Mnabadili kilicho duni kwa kilicho bora? Shukeni mjini, huko mtapata mlivyo
viomba. Na wakapigwa na unyonge,na umasikini, na wakastahili ghadhabu ya
Mwenyezi Mungu. Na haya ni kwa sababu walikuwa wakiyakataa maneno ya Mwenyezi
Mungu, na wakiwauwa Manabii pasipo haki. Hayo ni kwa walivyo asi na wakapindukia
mipaka.
|
Ayah 2:62 الأية
إِنَّ الَّذِينَ آمَنُوا وَالَّذِينَ هَادُوا وَالنَّصَارَىٰ وَالصَّابِئِينَ مَنْ
آمَنَ بِاللَّهِ وَالْيَوْمِ الْآخِرِ وَعَمِلَ صَالِحًا فَلَهُمْ أَجْرُهُمْ عِندَ
رَبِّهِمْ وَلَا خَوْفٌ عَلَيْهِمْ وَلَا هُمْ يَحْزَنُونَ
Swahili
Hakika Walio amini, na Mayahudi na Wakristo, na Wasabai; yeyote atakaye muamini
Mwenyezi Mungu na Siku ya Mwisho na akatenda mema basi watapata malipwa yao kwa
Mola wao Mlezi, wala haitakuwa khofu juu yao, wala hawatahuzunika.
|
Ayah 2:63 الأية
وَإِذْ أَخَذْنَا مِيثَاقَكُمْ وَرَفَعْنَا فَوْقَكُمُ الطُّورَ خُذُوا مَا
آتَيْنَاكُم بِقُوَّةٍ وَاذْكُرُوا مَا فِيهِ لَعَلَّكُمْ تَتَّقُونَ
Swahili
Na tulipo chukua ahadi yenu, na tukaunyanyua mlima juu yenu (tukakwambieni):
Shikeni kwa nguvu haya tuliyo kupeni, na yakumbukeni yaliyomo ndani yake ili
mpate kujilinda.
|
Ayah 2:64 الأية
ثُمَّ تَوَلَّيْتُم مِّن بَعْدِ ذَٰلِكَ ۖ فَلَوْلَا فَضْلُ اللَّهِ عَلَيْكُمْ
وَرَحْمَتُهُ لَكُنتُم مِّنَ الْخَاسِرِينَ
Swahili
Kisha mligeuka baada ya haya. Na lau kuwa si fadhila za Mwenyezi Mungu juu yenu
na rehema zake, mngeli kuwa miongoni mwa wenye kukhasirika.
|
Ayah 2:65 الأية
وَلَقَدْ عَلِمْتُمُ الَّذِينَ اعْتَدَوْا مِنكُمْ فِي السَّبْتِ فَقُلْنَا لَهُمْ
كُونُوا قِرَدَةً خَاسِئِينَ
Swahili
Na hakika mlikwisha yajua ya wale miongoni mwenu walio ivunja Sabato,(siku ya
mapumziko, Jumaa Mosi) na tukawaambia: Kuweni manyani wadhalilifu.
|
Ayah 2:66 الأية
فَجَعَلْنَاهَا نَكَالًا لِّمَا بَيْنَ يَدَيْهَا وَمَا خَلْفَهَا وَمَوْعِظَةً
لِّلْمُتَّقِينَ
Swahili
Kwa hivyo tukayafanya hayo kuwa onyo kwa wale walio kuwa katika zama zao na
walio kuja baada yao, na mawaidha kwa wachamngu.
|
Ayah 2:67 الأية
وَإِذْ قَالَ مُوسَىٰ لِقَوْمِهِ إِنَّ اللَّهَ يَأْمُرُكُمْ أَن تَذْبَحُوا
بَقَرَةً ۖ قَالُوا أَتَتَّخِذُنَا هُزُوًا ۖ قَالَ أَعُوذُ بِاللَّهِ أَنْ أَكُونَ
مِنَ الْجَاهِلِينَ
Swahili
Na Musa alipo waambia watu wake: Hakika Mwenyezi Mungu anakuamrisheni mchinje
ng'ombe. Wakasema: Je! Unatufanyia mzaha? Akasema: Audhubil lahi! Najikinga kwa
Mwenyezi Mungu nisiwe miongoni mwa wajinga.
|
Ayah 2:68 الأية
قَالُوا ادْعُ لَنَا رَبَّكَ يُبَيِّن لَّنَا مَا هِيَ ۚ قَالَ إِنَّهُ يَقُولُ
إِنَّهَا بَقَرَةٌ لَّا فَارِضٌ وَلَا بِكْرٌ عَوَانٌ بَيْنَ ذَٰلِكَ ۖ فَافْعَلُوا
مَا تُؤْمَرُونَ
Swahili
Wakasema: Tuombee kwa Mola wako Mlezi atupambanulie ni ng'ombe gani? Akasema:
Hakika Yeye anasema kwamba ng'ombe huyo si mpevu, wala si kinda, bali ni wa
katikati baina ya hao. Basi fanyeni mnavyo amrishwa.
|
Ayah 2:69 الأية
قَالُوا ادْعُ لَنَا رَبَّكَ يُبَيِّن لَّنَا مَا لَوْنُهَا ۚ قَالَ إِنَّهُ
يَقُولُ إِنَّهَا بَقَرَةٌ صَفْرَاءُ فَاقِعٌ لَّوْنُهَا تَسُرُّ النَّاظِرِينَ
Swahili
Wakasema: Tuombee kwa Mola wako atupambanulie nini rangi yake? Akasema: Yeye
anasema, kuwa ng'ombe huyo ni wa manjano, na rangi yake imekoza, huwapendeza
wanao mtazama.
|
Ayah 2:70 الأية
قَالُوا ادْعُ لَنَا رَبَّكَ يُبَيِّن لَّنَا مَا هِيَ إِنَّ الْبَقَرَ تَشَابَهَ
عَلَيْنَا وَإِنَّا إِن شَاءَ اللَّهُ لَمُهْتَدُونَ
Swahili
Wakasema: Tuombee kwa Mola wako Mlezi atupambanulie ni yupi? Hakika tunaona
ng'ombe wamefanana. Na kwa yakini, Inshaallah, Mwenyezi Mungu akipenda,
tutaongoka.
|
Ayah 2:71 الأية
قَالَ إِنَّهُ يَقُولُ إِنَّهَا بَقَرَةٌ لَّا ذَلُولٌ تُثِيرُ الْأَرْضَ وَلَا
تَسْقِي الْحَرْثَ مُسَلَّمَةٌ لَّا شِيَةَ فِيهَا ۚ قَالُوا الْآنَ جِئْتَ
بِالْحَقِّ ۚ فَذَبَحُوهَا وَمَا كَادُوا يَفْعَلُونَ
Swahili
Akasema: Yeye anasema: Kuwa huyo ni ng'ombe asiye tiwa kazini kulima ardhi wala
kumwagia maji mimea, mzima, hana baka. Wakasema: Sasa umeleta haki. Basi
wakamchinja, na walikaribia kuwa wasifanye hayo.
|
Ayah 2:72 الأية
وَإِذْ قَتَلْتُمْ نَفْسًا فَادَّارَأْتُمْ فِيهَا ۖ وَاللَّهُ مُخْرِجٌ مَّا
كُنتُمْ تَكْتُمُونَ
Swahili
Na mlipo muuwa mtu, kisha mkakhitalifiana kwayo, na Mwenyezi Mungu ni mwenye
kuyatoa hayo mliyo kuwa mkiyaficha.
|
Ayah 2:73 الأية
فَقُلْنَا اضْرِبُوهُ بِبَعْضِهَا ۚ كَذَٰلِكَ يُحْيِي اللَّهُ الْمَوْتَىٰ
وَيُرِيكُمْ آيَاتِهِ لَعَلَّكُمْ تَعْقِلُونَ
Swahili
Tukasema: Mpigeni kwa kipande chake (huyo ng'ombe). Ndivyo hivi Mwenyezi Mungu
huwahuisha wafu; na anakuonyesheni Ishara zake ili mpate kufahamu.
|
Ayah 2:74 الأية
ثُمَّ قَسَتْ قُلُوبُكُم مِّن بَعْدِ ذَٰلِكَ فَهِيَ كَالْحِجَارَةِ أَوْ أَشَدُّ
قَسْوَةً ۚ وَإِنَّ مِنَ الْحِجَارَةِ لَمَا يَتَفَجَّرُ مِنْهُ الْأَنْهَارُ ۚ
وَإِنَّ مِنْهَا لَمَا يَشَّقَّقُ فَيَخْرُجُ مِنْهُ الْمَاءُ ۚ وَإِنَّ مِنْهَا
لَمَا يَهْبِطُ مِنْ خَشْيَةِ اللَّهِ ۗ وَمَا اللَّهُ بِغَافِلٍ عَمَّا
تَعْمَلُونَ
Swahili
Kisha nyoyo zenu zikawa ngumu baada ya hayo, hata zikawa kama mawe au ngumu
zaidi; kwani kuna mawe yanayo timbuka mito, na kuna mengine yanayo pasuka
yakatoka maji ndani yake, na kuna mengine huanguka kwa sababu ya khofu ya
Mwenyezi Mungu. Na Mwenyezi Mungu si mwenye kughafilika na mnayo yafanya.
|
Ayah 2:75 الأية
أَفَتَطْمَعُونَ أَن يُؤْمِنُوا لَكُمْ وَقَدْ كَانَ فَرِيقٌ مِّنْهُمْ يَسْمَعُونَ
كَلَامَ اللَّهِ ثُمَّ يُحَرِّفُونَهُ مِن بَعْدِ مَا عَقَلُوهُ وَهُمْ يَعْلَمُونَ
Swahili
Mnatumai watakuaminini na hali baadhi yao walikuwa wakisikia maneno ya Mwenyezi
Mungu, kisha wakayabadili baada ya kuwa wameyafahamu, na hali wanajua?
|
Ayah 2:76 الأية
وَإِذَا لَقُوا الَّذِينَ آمَنُوا قَالُوا آمَنَّا وَإِذَا خَلَا بَعْضُهُمْ إِلَىٰ
بَعْضٍ قَالُوا أَتُحَدِّثُونَهُم بِمَا فَتَحَ اللَّهُ عَلَيْكُمْ لِيُحَاجُّوكُم
بِهِ عِندَ رَبِّكُمْ ۚ أَفَلَا تَعْقِلُونَ
Swahili
Na wanapo kutana na wale walio amini husema: Tumeamini. Na wanapo kuwa peke yao,
wao kwa wao, husema: Mnawaambia aliyo kufunulieni Mwenyezi Mungu ili wapate
kukuhojieni mbele ya Mola wenu Mlezi? Basi hamfahamu nyinyi?
|
Ayah 2:77 الأية
أَوَلَا يَعْلَمُونَ أَنَّ اللَّهَ يَعْلَمُ مَا يُسِرُّونَ وَمَا يُعْلِنُونَ
Swahili
Hawajui ya kwamba Mwenyezi Mungu anayajua wanayo yaficha na wanayo yatangaza?
|
Ayah 2:78 الأية
وَمِنْهُمْ أُمِّيُّونَ لَا يَعْلَمُونَ الْكِتَابَ إِلَّا أَمَانِيَّ وَإِنْ هُمْ
إِلَّا يَظُنُّونَ
Swahili
Na wako miongoni mwao wasio jua kusoma; hawakijui Kitabu isipo kuwa uwongo wanao
utamani, nao hawana ila ni kudhania tu.
|
Ayah 2:79 الأية
فَوَيْلٌ لِّلَّذِينَ يَكْتُبُونَ الْكِتَابَ بِأَيْدِيهِمْ ثُمَّ يَقُولُونَ
هَٰذَا مِنْ عِندِ اللَّهِ لِيَشْتَرُوا بِهِ ثَمَنًا قَلِيلًا ۖ فَوَيْلٌ لَّهُم
مِّمَّا كَتَبَتْ أَيْدِيهِمْ وَوَيْلٌ لَّهُم مِّمَّا يَكْسِبُونَ
Swahili
Basi ole wao wanao andika kitabu kwa mikono yao, kisha wakasema: Hiki kimetoka
kwa Mwenyezi Mungu, ili wachumie kwacho pato dogo. Basi ole wao kwa yale iliyo
andika mikono yao, na ole wao kwa yale wanayo yachuma.
|
Ayah 2:80 الأية
وَقَالُوا لَن تَمَسَّنَا النَّارُ إِلَّا أَيَّامًا مَّعْدُودَةً ۚ قُلْ
أَتَّخَذْتُمْ عِندَ اللَّهِ عَهْدًا فَلَن يُخْلِفَ اللَّهُ عَهْدَهُ ۖ أَمْ
تَقُولُونَ عَلَى اللَّهِ مَا لَا تَعْلَمُونَ
Swahili
Na walisema: Hautatugusa Moto ila kwa siku chache tu. Sema: Mmechukua ahadi kwa
Mwenyezi Mungu? Kweli Mwenyezi Mungu hatokwenda kinyume na ahadi yake. Au
mnamsingizia Mwenyezi Mungu mambo msiyo yajua?
|
Ayah 2:81 الأية
بَلَىٰ مَن كَسَبَ سَيِّئَةً وَأَحَاطَتْ بِهِ خَطِيئَتُهُ فَأُولَٰئِكَ أَصْحَابُ
النَّارِ ۖ هُمْ فِيهَا خَالِدُونَ
Swahili
Naam, anaye chuma ubaya - na makosa yake yakamzunguka - hao ndio watu wa Motoni;
humo watadumu.
|
Ayah 2:82 الأية
وَالَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ أُولَٰئِكَ أَصْحَابُ الْجَنَّةِ ۖ
هُمْ فِيهَا خَالِدُونَ
Swahili
Na wale walio amini na wakatenda mema, hao ndio watu wa Peponi, humo watadumu.
|
Ayah 2:83 الأية
وَإِذْ أَخَذْنَا مِيثَاقَ بَنِي إِسْرَائِيلَ لَا تَعْبُدُونَ إِلَّا اللَّهَ
وَبِالْوَالِدَيْنِ إِحْسَانًا وَذِي الْقُرْبَىٰ وَالْيَتَامَىٰ وَالْمَسَاكِينِ
وَقُولُوا لِلنَّاسِ حُسْنًا وَأَقِيمُوا الصَّلَاةَ وَآتُوا الزَّكَاةَ ثُمَّ
تَوَلَّيْتُمْ إِلَّا قَلِيلًا مِّنكُمْ وَأَنتُم مُّعْرِضُونَ
Swahili
Na tulipo funga agano na Wana wa Israili: Hamtamuabudu yeyote ila Mwenyezi
Mungu; na muwafanyie wema wazazi na jamaa na mayatima na masikini, na semeni na
watu kwa wema, na shikeni Sala, na toeni Zaka. Kisha mkageuka isipo kuwa
wachache tu katika nyinyi; na nyinyi mnapuuza.
|
Ayah 2:84 الأية
وَإِذْ أَخَذْنَا مِيثَاقَكُمْ لَا تَسْفِكُونَ دِمَاءَكُمْ وَلَا تُخْرِجُونَ
أَنفُسَكُم مِّن دِيَارِكُمْ ثُمَّ أَقْرَرْتُمْ وَأَنتُمْ تَشْهَدُونَ
Swahili
Na tulipo chukua agano lenu kuwa hamtamwaga damu zenu, wala hamtatoana majumbani
mwenu; nanyi mkakubali nanyi mnashuhudia.
|
Ayah 2:85 الأية
ثُمَّ أَنتُمْ هَٰؤُلَاءِ تَقْتُلُونَ أَنفُسَكُمْ وَتُخْرِجُونَ فَرِيقًا مِّنكُم
مِّن دِيَارِهِمْ تَظَاهَرُونَ عَلَيْهِم بِالْإِثْمِ وَالْعُدْوَانِ وَإِن
يَأْتُوكُمْ أُسَارَىٰ تُفَادُوهُمْ وَهُوَ مُحَرَّمٌ عَلَيْكُمْ إِخْرَاجُهُمْ ۚ
أَفَتُؤْمِنُونَ بِبَعْضِ الْكِتَابِ وَتَكْفُرُونَ بِبَعْضٍ ۚ فَمَا جَزَاءُ مَن
يَفْعَلُ ذَٰلِكَ مِنكُمْ إِلَّا خِزْيٌ فِي الْحَيَاةِ الدُّنْيَا ۖ وَيَوْمَ
الْقِيَامَةِ يُرَدُّونَ إِلَىٰ أَشَدِّ الْعَذَابِ ۗ وَمَا اللَّهُ بِغَافِلٍ
عَمَّا تَعْمَلُونَ
Swahili
Kisha nyinyi kwa nyinyi mnauwana, na mnawatoa baadhi yenu majumbani kwao,
mkisaidiana kwa dhambi na uadui. Na wakikujieni mateka mnawakomboa, na hali
kuwatoa mmekatazwa. Je! Mnaamini baadhi ya Kitabu na mnakataa baadhi yake? Basi
hana malipo mwenye kutenda hayo miongoni mwenu ila hizaya katika maisha ya
duniani, na Siku ya Kiyama watapelekwa kwenye adhabu kali kabisa. Na Mwenyezi
Mungu si mwenye kughafilika na yale mnayo yatenda.
|
Ayah 2:86 الأية
أُولَٰئِكَ الَّذِينَ اشْتَرَوُا الْحَيَاةَ الدُّنْيَا بِالْآخِرَةِ ۖ فَلَا
يُخَفَّفُ عَنْهُمُ الْعَذَابُ وَلَا هُمْ يُنصَرُونَ
Swahili
Hao ndio walio nunua uhai wa dunia kwa (uhai wa) Akhera; kwa hivyo
hawatapunguziwa adhabu wala hawatanusuriwa.
|
Ayah 2:87 الأية
وَلَقَدْ آتَيْنَا مُوسَى الْكِتَابَ وَقَفَّيْنَا مِن بَعْدِهِ بِالرُّسُلِ ۖ
وَآتَيْنَا عِيسَى ابْنَ مَرْيَمَ الْبَيِّنَاتِ وَأَيَّدْنَاهُ بِرُوحِ الْقُدُسِ
ۗ أَفَكُلَّمَا جَاءَكُمْ رَسُولٌ بِمَا لَا تَهْوَىٰ أَنفُسُكُمُ اسْتَكْبَرْتُمْ
فَفَرِيقًا كَذَّبْتُمْ وَفَرِيقًا تَقْتُلُونَ
Swahili
Na hakika tulimpa Musa Kitabu na tukafuatisha baada yake Mitume wengine. Na
tukampa Isa, mwana wa Mariamu, hoja zilizo waziwazi, na tukamtia nguvu kwa Roho
Takatifu. Basi kila walipo kufikieni Mitume kwa yale ambayo hayapendwi na nafsi
zenu, mlijivuna; wengine mkawakanusha, na wengine mkawauwa.
|
Ayah 2:88 الأية
وَقَالُوا قُلُوبُنَا غُلْفٌ ۚ بَل لَّعَنَهُمُ اللَّهُ بِكُفْرِهِمْ فَقَلِيلًا
مَّا يُؤْمِنُونَ
Swahili
Na walisema: Nyoyo zetu zimefunikwa. Bali Mwenyezi Mungu amewalaani kwa kufuru
zao: kwa hivyo ni kidogo tu wanayo yaamini.
|
Ayah 2:89 الأية
وَلَمَّا جَاءَهُمْ كِتَابٌ مِّنْ عِندِ اللَّهِ مُصَدِّقٌ لِّمَا مَعَهُمْ
وَكَانُوا مِن قَبْلُ يَسْتَفْتِحُونَ عَلَى الَّذِينَ كَفَرُوا فَلَمَّا جَاءَهُم
مَّا عَرَفُوا كَفَرُوا بِهِ ۚ فَلَعْنَةُ اللَّهِ عَلَى الْكَافِرِينَ
Swahili
Na kilipo wajia Kitabu kitokacho kwa Mwenyezi Mungu kinacho thibitisha waliyo
nayo - na wao walikuwa wakitafutia ushindi kuwashinda makafiri - yalipo wajia
yale waliyo kuwa wakiyajua waliyakanusha. Basi laana ya Mwenyezi Mungu juu ya
wakanushao!
|
Ayah 2:90 الأية
بِئْسَمَا اشْتَرَوْا بِهِ أَنفُسَهُمْ أَن يَكْفُرُوا بِمَا أَنزَلَ اللَّهُ
بَغْيًا أَن يُنَزِّلَ اللَّهُ مِن فَضْلِهِ عَلَىٰ مَن يَشَاءُ مِنْ عِبَادِهِ ۖ
فَبَاءُوا بِغَضَبٍ عَلَىٰ غَضَبٍ ۚ وَلِلْكَافِرِينَ عَذَابٌ مُّهِينٌ
Swahili
Kiovu kweli walicho jiuzia nafsi zao, nacho ni kule kukataa kwao aliyo
yateremsha Mwenyezi Mungu, kwa ajili ya kuona maya kwa kuwa Mwenyezi Mungu
humteremshia fadhila yake amtakaye miongoni mwa waja wake. Basi wamejiletea
wenyewe ghadhabu juu ya ghadhabu. Na makafiri watapata mateso ya kudhalilisha.
|
Ayah 2:91 الأية
وَإِذَا قِيلَ لَهُمْ آمِنُوا بِمَا أَنزَلَ اللَّهُ قَالُوا نُؤْمِنُ بِمَا
أُنزِلَ عَلَيْنَا وَيَكْفُرُونَ بِمَا وَرَاءَهُ وَهُوَ الْحَقُّ مُصَدِّقًا
لِّمَا مَعَهُمْ ۗ قُلْ فَلِمَ تَقْتُلُونَ أَنبِيَاءَ اللَّهِ مِن قَبْلُ إِن
كُنتُم مُّؤْمِنِينَ
Swahili
Na wanapo ambiwa: Yaaminini aliyo yateremsha Mwenyezi Mungu. Wao husema:
Tunaamini tuliyo teremshiwa sisi. Na huyakataa yasiyo kuwa hayo. Na hali ya kuwa
hii ndiyo Haki inayo thibitisha yale waliyo nayo wao. Sema: Mbona mliwauwa
Manabii wa Mwenyezi Mungu hapo zamani ikiwa kweli mlikuwa Waumini?
|
Ayah 2:92 الأية
وَلَقَدْ جَاءَكُم مُّوسَىٰ بِالْبَيِّنَاتِ ثُمَّ اتَّخَذْتُمُ الْعِجْلَ مِن
بَعْدِهِ وَأَنتُمْ ظَالِمُونَ
Swahili
Na alikufikieni Musa na hoja zilizo waziwazi, kisha mkamchukua ndama (kumuabudu)
baada yake, na mkawa wenye kudhulumu.
|
Ayah 2:93 الأية
وَإِذْ أَخَذْنَا مِيثَاقَكُمْ وَرَفَعْنَا فَوْقَكُمُ الطُّورَ خُذُوا مَا
آتَيْنَاكُم بِقُوَّةٍ وَاسْمَعُوا ۖ قَالُوا سَمِعْنَا وَعَصَيْنَا وَأُشْرِبُوا
فِي قُلُوبِهِمُ الْعِجْلَ بِكُفْرِهِمْ ۚ قُلْ بِئْسَمَا يَأْمُرُكُم بِهِ
إِيمَانُكُمْ إِن كُنتُم مُّؤْمِنِينَ
Swahili
Na tulipo chukua ahadi yenu na tukauinua mlima juu yenu (tukakwambieni):
Kamateni kwa nguvu haya tuliyo kupeni na sikieni. Wakasema: Tumesikia na
tumekataa! Na wakanyweshwa nyoyoni mwao (imani ya) ndama kwa kufuru yao. Sema:
Ni uovu mno iliyo kuamrisheni imani yenu ikiwa ni wenye kuamini.
|
Ayah 2:94 الأية
قُلْ إِن كَانَتْ لَكُمُ الدَّارُ الْآخِرَةُ عِندَ اللَّهِ خَالِصَةً مِّن دُونِ
النَّاسِ فَتَمَنَّوُا الْمَوْتَ إِن كُنتُمْ صَادِقِينَ
Swahili
Sema: Ikiwa nyumba ya Akhera iliyoko kwa Mwenyezi Mungu ni yenu tu bila ya watu
wengine, basi tamanini mauti kama nyinyi mnasema kweli.
|
Ayah 2:95 الأية
وَلَن يَتَمَنَّوْهُ أَبَدًا بِمَا قَدَّمَتْ أَيْدِيهِمْ ۗ وَاللَّهُ عَلِيمٌ
بِالظَّالِمِينَ
Swahili
Wala hawatayatamani kamwe kwa sababu ya yale yaliyo tangulizwa na mikono yao; na
Mwenyezi Mungu ni mwenye kuwajua vyema wanao dhulumu.
|
Ayah 2:96 الأية
وَلَتَجِدَنَّهُمْ أَحْرَصَ النَّاسِ عَلَىٰ حَيَاةٍ وَمِنَ الَّذِينَ أَشْرَكُوا ۚ
يَوَدُّ أَحَدُهُمْ لَوْ يُعَمَّرُ أَلْفَ سَنَةٍ وَمَا هُوَ بِمُزَحْزِحِهِ مِنَ
الْعَذَابِ أَن يُعَمَّرَ ۗ وَاللَّهُ بَصِيرٌ بِمَا يَعْمَلُونَ
Swahili
Na hakika utawaona ni wenye kuwashinda watu wote kwa pupa ya kuishi, na kuliko
washirikina. Kila mmoja wao anatamani lau angeli pewa umri wa miaka elfu. Wala
hayo ya kuzidishiwa umri hayamuondoshei adhabu; na Mwenyezi Mungu anayaona
wanayo yatenda.
|
Ayah 2:97 الأية
قُلْ مَن كَانَ عَدُوًّا لِّجِبْرِيلَ فَإِنَّهُ نَزَّلَهُ عَلَىٰ قَلْبِكَ
بِإِذْنِ اللَّهِ مُصَدِّقًا لِّمَا بَيْنَ يَدَيْهِ وَهُدًى وَبُشْرَىٰ
لِلْمُؤْمِنِينَ
Swahili
Sema: Aliye kuwa ni adui wa Jibril, basi huyo ndiye aliye iteremsha Qur'ani
moyoni mwako kwa idhini ya Mwenyezi Mungu, inayo thibitisha yaliyo kuwa kabla
yake, na ni uwongofu na bishara njema kwa Waumini.
|
Ayah 2:98 الأية
مَن كَانَ عَدُوًّا لِّلَّهِ وَمَلَائِكَتِهِ وَرُسُلِهِ وَجِبْرِيلَ وَمِيكَالَ
فَإِنَّ اللَّهَ عَدُوٌّ لِّلْكَافِرِينَ
Swahili
Aliye kuwa adui wa Mwenyezi Mungu na Malaika wake na Mitume wake na Jibril na
Mikail, basi hakika Mwenyezi Mungu ni adui wa makafiri.
|
Ayah 2:99 الأية
وَلَقَدْ أَنزَلْنَا إِلَيْكَ آيَاتٍ بَيِّنَاتٍ ۖ وَمَا يَكْفُرُ بِهَا إِلَّا
الْفَاسِقُونَ
Swahili
Hakika tumekuteremshia Ishara zilizo wazi na hapana wanao zikataa ila wapotovu.
|
Ayah 2:100 الأية
أَوَكُلَّمَا عَاهَدُوا عَهْدًا نَّبَذَهُ فَرِيقٌ مِّنْهُم ۚ بَلْ أَكْثَرُهُمْ
لَا يُؤْمِنُونَ
Swahili
Je! Ati ndio kila wanapo funga ahadi huwapo kikundi miongoni mwao kikaivunja?
Bali wengi wao hawaamini.
|
Ayah 2:101 الأية
وَلَمَّا جَاءَهُمْ رَسُولٌ مِّنْ عِندِ اللَّهِ مُصَدِّقٌ لِّمَا مَعَهُمْ نَبَذَ
فَرِيقٌ مِّنَ الَّذِينَ أُوتُوا الْكِتَابَ كِتَابَ اللَّهِ وَرَاءَ ظُهُورِهِمْ
كَأَنَّهُمْ لَا يَعْلَمُونَ
Swahili
Na alipo wajia Mtume kutoka kwa Mwenyezi Mungu, mwenye kuthibitisha yale waliyo
nayo, kundi moja miongoni mwa wale walio pewa Kitabu lilitupa Kitabu cha
Mwenyezi Mungu hicho nyuma ya migongo yao kama kwamba hawajui.
|
Ayah 2:102 الأية
وَاتَّبَعُوا مَا تَتْلُو الشَّيَاطِينُ عَلَىٰ مُلْكِ سُلَيْمَانَ ۖ وَمَا كَفَرَ
سُلَيْمَانُ وَلَٰكِنَّ الشَّيَاطِينَ كَفَرُوا يُعَلِّمُونَ النَّاسَ السِّحْرَ
وَمَا أُنزِلَ عَلَى الْمَلَكَيْنِ بِبَابِلَ هَارُوتَ وَمَارُوتَ ۚ وَمَا
يُعَلِّمَانِ مِنْ أَحَدٍ حَتَّىٰ يَقُولَا إِنَّمَا نَحْنُ فِتْنَةٌ فَلَا
تَكْفُرْ ۖ فَيَتَعَلَّمُونَ مِنْهُمَا مَا يُفَرِّقُونَ بِهِ بَيْنَ الْمَرْءِ
وَزَوْجِهِ ۚ وَمَا هُم بِضَارِّينَ بِهِ مِنْ أَحَدٍ إِلَّا بِإِذْنِ اللَّهِ ۚ
وَيَتَعَلَّمُونَ مَا يَضُرُّهُمْ وَلَا يَنفَعُهُمْ ۚ وَلَقَدْ عَلِمُوا لَمَنِ
اشْتَرَاهُ مَا لَهُ فِي الْآخِرَةِ مِنْ خَلَاقٍ ۚ وَلَبِئْسَ مَا شَرَوْا بِهِ
أَنفُسَهُمْ ۚ لَوْ كَانُوا يَعْلَمُونَ
Swahili
Na wakafuata yale waliyo zua mashet'ani kuuzulia ufalme wa Su leiman. Na wala
Suleiman hakukufuru, bali mashet'ani ndio walio kufuru, wakiwafundisha watu
uchawi, na yaliyo teremshwa kwa Malaika wawili, Haaruta na Maaruta katika
Baabil. Wala hao hawakumfundisha yeyote mpaka wamwambie: Hakika sisi ni mtihani;
basi usikufuru. Wakajifunza kwa hao wawili yale ya kumfarikisha mtu na mkewe.
Wala hawawezi kumdhuru mtu ila kwa kutaka Mwenyezi Mungu. Na wanajifunza yatayo
wadhuru wala hayawanufaishi. Na hakika wanajua kwamba aliye khiari haya hatakuwa
na fungu lolote katika Akhera. Na hakika ni kiovu mno walicho jiuzia nafsi zao
laiti wangelijua.
|
Ayah 2:103 الأية
وَلَوْ أَنَّهُمْ آمَنُوا وَاتَّقَوْا لَمَثُوبَةٌ مِّنْ عِندِ اللَّهِ خَيْرٌ ۖ
لَّوْ كَانُوا يَعْلَمُونَ
Swahili
Na lau kuwa wangeamini na wakaogopa, bila ya shaka malipo yatokayo kwa Mwenyezi
Mungu yange kuwa bora. Laiti wangeli kuwa wanajua!
|
Ayah 2:104 الأية
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تَقُولُوا رَاعِنَا وَقُولُوا انظُرْنَا
وَاسْمَعُوا ۗ وَلِلْكَافِرِينَ عَذَابٌ أَلِيمٌ
Swahili
Enyi mlio amini! Msiseme: "Raa'ina", na semeni: "Ndhurna". Na sikieni! Na
makafiri watapata adhabu chungu.
|
Ayah 2:105 الأية
مَّا يَوَدُّ الَّذِينَ كَفَرُوا مِنْ أَهْلِ الْكِتَابِ وَلَا الْمُشْرِكِينَ أَن
يُنَزَّلَ عَلَيْكُم مِّنْ خَيْرٍ مِّن رَّبِّكُمْ ۗ وَاللَّهُ يَخْتَصُّ
بِرَحْمَتِهِ مَن يَشَاءُ ۚ وَاللَّهُ ذُو الْفَضْلِ الْعَظِيمِ
Swahili
Walio kufuru miongoni mwa watu wa Kitabu na washirikina hawapendi mteremshiwe
kheri yoyote kutoka kwa Mola wenu Mlezi. Na Mwenyezi Mungu humkusudia kumpa
rehema yake ampendaye. Na Mwenyezi Mungu ni mwenye fadhila kubwa.
|
Ayah 2:106 الأية
مَا نَنسَخْ مِنْ آيَةٍ أَوْ نُنسِهَا نَأْتِ بِخَيْرٍ مِّنْهَا أَوْ مِثْلِهَا ۗ
أَلَمْ تَعْلَمْ أَنَّ اللَّهَ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ
Swahili
Ishara yoyote tunayo ifuta au tunayo isahaulisha tunailetea iliyo bora kuliko
hiyo, au iliyo mfano wake. Hujui kwamba Mwenyezi Mungu ni Muweza wa kila kitu?
|
Ayah 2:107 الأية
أَلَمْ تَعْلَمْ أَنَّ اللَّهَ لَهُ مُلْكُ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ ۗ وَمَا
لَكُم مِّن دُونِ اللَّهِ مِن وَلِيٍّ وَلَا نَصِيرٍ
Swahili
Hujui kwamba Mwenyezi Mungu ana ufalme wa mbingu na ardhi? Nanyi hamna mlinzi
wala msaidizi isipo kuwa Mwenyezi Mungu.
|
Ayah 2:108 الأية
أَمْ تُرِيدُونَ أَن تَسْأَلُوا رَسُولَكُمْ كَمَا سُئِلَ مُوسَىٰ مِن قَبْلُ ۗ
وَمَن يَتَبَدَّلِ الْكُفْرَ بِالْإِيمَانِ فَقَدْ ضَلَّ سَوَاءَ السَّبِيلِ
Swahili
Au mnataka kumwomba Mtume wenu kama alivyo ombwa Musa zamani? Na anaye badilisha
Imani kwa ukafiri bila ya shaka huyo ameipotea njia iliyo sawa.
|
Ayah 2:109 الأية
وَدَّ كَثِيرٌ مِّنْ أَهْلِ الْكِتَابِ لَوْ يَرُدُّونَكُم مِّن بَعْدِ
إِيمَانِكُمْ كُفَّارًا حَسَدًا مِّنْ عِندِ أَنفُسِهِم مِّن بَعْدِ مَا تَبَيَّنَ
لَهُمُ الْحَقُّ ۖ فَاعْفُوا وَاصْفَحُوا حَتَّىٰ يَأْتِيَ اللَّهُ بِأَمْرِهِ ۗ
إِنَّ اللَّهَ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ
Swahili
Wengi miongoni mwa watu wa Kitabu wanatamani lau wange kurudisheni nyinyi muwe
makafiri baada ya kuamini kwenu, kwa ajili ya uhasidi uliomo ndani ya nafsi zao,
baada ya kwisha wapambanukia Haki. Basi sameheni na wachilieni mbali mpaka
Mwenyezi Mungu atapo leta amri yake. Hakika Mwenyezi Mungu ni Muweza wa kila
kitu.
|
Ayah 2:110 الأية
وَأَقِيمُوا الصَّلَاةَ وَآتُوا الزَّكَاةَ ۚ وَمَا تُقَدِّمُوا لِأَنفُسِكُم مِّنْ
خَيْرٍ تَجِدُوهُ عِندَ اللَّهِ ۗ إِنَّ اللَّهَ بِمَا تَعْمَلُونَ بَصِيرٌ
Swahili
Na shikeni Sala na toeni Zaka; na kheri mtakazo jitangulizia nafsi zenu
mtazikuta kwa Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu anayaona mnayo yafanya.
|
Ayah 2:111 الأية
وَقَالُوا لَن يَدْخُلَ الْجَنَّةَ إِلَّا مَن كَانَ هُودًا أَوْ نَصَارَىٰ ۗ
تِلْكَ أَمَانِيُّهُمْ ۗ قُلْ هَاتُوا بُرْهَانَكُمْ إِن كُنتُمْ صَادِقِينَ
Swahili
Na walisema: Hataingia Peponi ila aliyekuwa Yahudi au Mkristo. Hayo ni matamanio
yao. Sema: Leteni ushahidi wenu kama nyinyi ni wasema kweli.
|
Ayah 2:112 الأية
بَلَىٰ مَنْ أَسْلَمَ وَجْهَهُ لِلَّهِ وَهُوَ مُحْسِنٌ فَلَهُ أَجْرُهُ عِندَ
رَبِّهِ وَلَا خَوْفٌ عَلَيْهِمْ وَلَا هُمْ يَحْزَنُونَ
Swahili
Sivyo hivyo! Yeyote anaye elekeza uso wake kwa Mwenyezi Mungu naye ni mtenda
mema, basi ana malipo yake kwa Mola wake Mlezi, wala haitakuwa khofu juu yao
wala hawatahuzunika.
|
Ayah 2:113 الأية
وَقَالَتِ الْيَهُودُ لَيْسَتِ النَّصَارَىٰ عَلَىٰ شَيْءٍ وَقَالَتِ النَّصَارَىٰ
لَيْسَتِ الْيَهُودُ عَلَىٰ شَيْءٍ وَهُمْ يَتْلُونَ الْكِتَابَ ۗ كَذَٰلِكَ قَالَ
الَّذِينَ لَا يَعْلَمُونَ مِثْلَ قَوْلِهِمْ ۚ فَاللَّهُ يَحْكُمُ بَيْنَهُمْ
يَوْمَ الْقِيَامَةِ فِيمَا كَانُوا فِيهِ يَخْتَلِفُونَ
Swahili
Na Mayahudi husema: Wakristo hawana lao jambo. Na Wakristo husema: Mayahudi
hawana lao jambo. Na ilhali wote wanasoma Kitabu hicho hicho (Biblia). Na
kadhaalika walisema wale wasio jua kitu mfano wa kauli yao hii. Basi Mwenyezi
Mungu atahukumu baina yao Siku ya Kiyama katika yale waliyo kuwa
wakikhitilafiana.
|
Ayah 2:114 الأية
وَمَنْ أَظْلَمُ مِمَّن مَّنَعَ مَسَاجِدَ اللَّهِ أَن يُذْكَرَ فِيهَا اسْمُهُ
وَسَعَىٰ فِي خَرَابِهَا ۚ أُولَٰئِكَ مَا كَانَ لَهُمْ أَن يَدْخُلُوهَا إِلَّا
خَائِفِينَ ۚ لَهُمْ فِي الدُّنْيَا خِزْيٌ وَلَهُمْ فِي الْآخِرَةِ عَذَابٌ
عَظِيمٌ
Swahili
Na ni nani dhaalimu mkubwa kuliko yule anaye zuia misikiti ya Mwenyezi Mungu
kutajwa ndani yake jina lake na akajitahidi kuiharibu? Watu hao haitawafalia
kuingia humo ila nao wanaogopa. Duniani watapata hizaya na Akhera watapata
adhabu kubwa.
|
Ayah 2:115 الأية
وَلِلَّهِ الْمَشْرِقُ وَالْمَغْرِبُ ۚ فَأَيْنَمَا تُوَلُّوا فَثَمَّ وَجْهُ
اللَّهِ ۚ إِنَّ اللَّهَ وَاسِعٌ عَلِيمٌ
Swahili
Na mashariki na magharibi ni za Mwenyezi Mungu. Basi kokote mnako elekea, huko
Mwenyezi Mungu yupo. Hakika Mwenyezi Mungu ni mwenye wasaa na Mjuzi.
|
Ayah 2:116 الأية
وَقَالُوا اتَّخَذَ اللَّهُ وَلَدًا ۗ سُبْحَانَهُ ۖ بَل لَّهُ مَا فِي
السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ ۖ كُلٌّ لَّهُ قَانِتُونَ
Swahili
Na ati wanasema: Mwenyezi Mungu ana mwana. Subhanahu! Ametakasika na hayo. Bali
vyote viliomo mbinguni na duniani ni vyake. Vyote vinamt'ii Yeye.
|
Ayah 2:117 الأية
بَدِيعُ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ ۖ وَإِذَا قَضَىٰ أَمْرًا فَإِنَّمَا يَقُولُ
لَهُ كُن فَيَكُونُ
Swahili
Yeye ndiye Muumba wa mbingu na ardhi pasina ruwaza; na anapo taka jambo basi
huliambia tu: Kuwa! Nalo huwa.
|
|