First Ayah 1 الأية الأوليبِسْم ِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ
اقْتَرَبَ لِلنَّاسِ حِسَابُهُمْ وَهُمْ فِي غَفْلَةٍ مُّعْرِضُونَ
Swahili
IMEWAKARIBIA watu hisabu yao, nao wamo katika mghafala wanapuuza.
|
Ayah 21:2 الأية
مَا يَأْتِيهِم مِّن ذِكْرٍ مِّن رَّبِّهِم مُّحْدَثٍ إِلَّا اسْتَمَعُوهُ وَهُمْ
يَلْعَبُونَ
Swahili
Hayawafikilii mawaidha mapya kutoka kwa Mola wao Mlezi ila huyasikiliza na huku
wanafanya mchezo.
|
Ayah 21:3 الأية
لَاهِيَةً قُلُوبُهُمْ ۗ وَأَسَرُّوا النَّجْوَى الَّذِينَ ظَلَمُوا هَلْ هَٰذَا
إِلَّا بَشَرٌ مِّثْلُكُمْ ۖ أَفَتَأْتُونَ السِّحْرَ وَأَنتُمْ تُبْصِرُونَ
Swahili
Zimeghafilika nyoyo zao. Na wale walio dhulumu hunong'onezana kwa siri: Ni nani
ati huyu isipo kuwa ni binaadamu tu kama nyinyi! Mnauwendea uchawi hali nanyi
mnaona?
|
Ayah 21:4 الأية
قَالَ رَبِّي يَعْلَمُ الْقَوْلَ فِي السَّمَاءِ وَالْأَرْضِ ۖ وَهُوَ السَّمِيعُ
الْعَلِيمُ
Swahili
Alisema: Mola wangu Mlezi anayajua yasemwayo mbinguni na katika ardhi. Na Yeye
ni Mwenye kusikia Mwenye kujua.
|
Ayah 21:5 الأية
بَلْ قَالُوا أَضْغَاثُ أَحْلَامٍ بَلِ افْتَرَاهُ بَلْ هُوَ شَاعِرٌ فَلْيَأْتِنَا
بِآيَةٍ كَمَا أُرْسِلَ الْأَوَّلُونَ
Swahili
Lakini wao walisema: Hizo ni ndoto za ovyo ovyo, bali amezizua tu, bali huyo ni
mtunga mashairi. Basi atuletee miujiza kama walivyo tumwa wale wa mwanzo.
|
Ayah 21:6 الأية
مَا آمَنَتْ قَبْلَهُم مِّن قَرْيَةٍ أَهْلَكْنَاهَا ۖ أَفَهُمْ يُؤْمِنُونَ
Swahili
Hawakuamini kabla yao watu wa mji tulio uangamiza. Basi, je, wataamini hawa?
|
Ayah 21:7 الأية
وَمَا أَرْسَلْنَا قَبْلَكَ إِلَّا رِجَالًا نُّوحِي إِلَيْهِمْ ۖ فَاسْأَلُوا
أَهْلَ الذِّكْرِ إِن كُنتُمْ لَا تَعْلَمُونَ
Swahili
Na kabla yako hatukuwatuma ila watu wanaume tulio wapa wahyi (ufunuo). Basi
waulizeni wenye ilimu ikiwa nyinyi hamjui.
|
Ayah 21:8 الأية
وَمَا جَعَلْنَاهُمْ جَسَدًا لَّا يَأْكُلُونَ الطَّعَامَ وَمَا كَانُوا خَالِدِينَ
Swahili
Wala hatukuwafanya miili isiyo kula chakula, wala hawakuwa wenye kuishi milele.
|
Ayah 21:9 الأية
ثُمَّ صَدَقْنَاهُمُ الْوَعْدَ فَأَنجَيْنَاهُمْ وَمَن نَّشَاءُ وَأَهْلَكْنَا
الْمُسْرِفِينَ
Swahili
Kisha tukawatimizia miadi, na tukawaokoa wao na tulio wataka, na tukawateketeza
walio pita mipaka.
|
Ayah 21:10 الأية
لَقَدْ أَنزَلْنَا إِلَيْكُمْ كِتَابًا فِيهِ ذِكْرُكُمْ ۖ أَفَلَا تَعْقِلُونَ
Swahili
Na hakika tumekuteremshieni Kitabu ambacho ndani yake yamo makumbusho yenu. Je!
Hamzingatii?
|
Ayah 21:11 الأية
وَكَمْ قَصَمْنَا مِن قَرْيَةٍ كَانَتْ ظَالِمَةً وَأَنشَأْنَا بَعْدَهَا قَوْمًا
آخَرِينَ
Swahili
Na mingapi katika miji iliyo kuwa ikidhulumu tumeiteketeza, na tukawasimamisha
baada yao watu wengine.
|
Ayah 21:12 الأية
فَلَمَّا أَحَسُّوا بَأْسَنَا إِذَا هُم مِّنْهَا يَرْكُضُونَ
Swahili
Basi walipo ihisi adhabu yetu, mara wakaanza kukimbia.
|
Ayah 21:13 الأية
لَا تَرْكُضُوا وَارْجِعُوا إِلَىٰ مَا أُتْرِفْتُمْ فِيهِ وَمَسَاكِنِكُمْ
لَعَلَّكُمْ تُسْأَلُونَ
Swahili
Msikimbie! Na rejeeni kwenye zile zile starehe zenu, na maskani zenu, mpate
kusailiwa!
|
Ayah 21:14 الأية
قَالُوا يَا وَيْلَنَا إِنَّا كُنَّا ظَالِمِينَ
Swahili
Wakasema: Ole wetu! Hakika sisi tulikuwa madhaalimu.
|
Ayah 21:15 الأية
فَمَا زَالَت تِّلْكَ دَعْوَاهُمْ حَتَّىٰ جَعَلْنَاهُمْ حَصِيدًا خَامِدِينَ
Swahili
Hakikuacha hicho kuwa kilio chao mpaka tukawafanya kama walio fyekwa,
wamezimika.
|
Ayah 21:16 الأية
وَمَا خَلَقْنَا السَّمَاءَ وَالْأَرْضَ وَمَا بَيْنَهُمَا لَاعِبِينَ
Swahili
Na hatukuziumba mbingu na ardhi na vilivyo baina yao kwa mchezo.
|
Ayah 21:17 الأية
لَوْ أَرَدْنَا أَن نَّتَّخِذَ لَهْوًا لَّاتَّخَذْنَاهُ مِن لَّدُنَّا إِن كُنَّا
فَاعِلِينَ
Swahili
Kama tungeli taka kufanya mchezo tunge jifanyia Sisi wenyewe, lau kwamba tungeli
kuwa ni wafanyao mchezo.
|
Ayah 21:18 الأية
بَلْ نَقْذِفُ بِالْحَقِّ عَلَى الْبَاطِلِ فَيَدْمَغُهُ فَإِذَا هُوَ زَاهِقٌ ۚ
وَلَكُمُ الْوَيْلُ مِمَّا تَصِفُونَ
Swahili
Bali tunaitupa kweli juu ya uwongo ikauvunja na mara ukatoweka. Na ole wenu kwa
mnayo yazua.
|
Ayah 21:19 الأية
وَلَهُ مَن فِي السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ ۚ وَمَنْ عِندَهُ لَا يَسْتَكْبِرُونَ
عَنْ عِبَادَتِهِ وَلَا يَسْتَحْسِرُونَ
Swahili
Na ni vyake Yeye tu Mwenyezi Mungu vilivyomo mbinguni na katika ardhi. Na
walioko kwake hawafanyi kiburi wakaacha kumuabudu, wala hawachoki.
|
Ayah 21:20 الأية
يُسَبِّحُونَ اللَّيْلَ وَالنَّهَارَ لَا يَفْتُرُونَ
Swahili
Wanamtakasa usiku na mchana, wala hawanyong'onyei.
|
Ayah 21:21 الأية
أَمِ اتَّخَذُوا آلِهَةً مِّنَ الْأَرْضِ هُمْ يُنشِرُونَ
Swahili
Au wamepata miungu katika ardhi inayo fufua?
|
Ayah 21:22 الأية
لَوْ كَانَ فِيهِمَا آلِهَةٌ إِلَّا اللَّهُ لَفَسَدَتَا ۚ فَسُبْحَانَ اللَّهِ
رَبِّ الْعَرْشِ عَمَّا يَصِفُونَ
Swahili
Lau wangeli kuwamo humo miungu wengine isipo kuwa Mwenyezi Mungu basi bila ya
shaka hizo mbingu na ardhi zingeli fisidika. Subahana 'Llah Ametakasika Mwenyezi
Mungu, Bwana wa A'rshi (Kiti cha Enzi), na hayo wanayo yazua.
|
Ayah 21:23 الأية
لَا يُسْأَلُ عَمَّا يَفْعَلُ وَهُمْ يُسْأَلُونَ
Swahili
Yeye hahojiwi kwa ayatendayo, na wao ndio wanao hojiwa kwa wayatendayo.
|
Ayah 21:24 الأية
أَمِ اتَّخَذُوا مِن دُونِهِ آلِهَةً ۖ قُلْ هَاتُوا بُرْهَانَكُمْ ۖ هَٰذَا ذِكْرُ
مَن مَّعِيَ وَذِكْرُ مَن قَبْلِي ۗ بَلْ أَكْثَرُهُمْ لَا يَعْلَمُونَ الْحَقَّ ۖ
فَهُم مُّعْرِضُونَ
Swahili
Au wanawaabudu miungu mingine badala yake? Sema: Leteni ushahidi wenu! Haya ni
ukumbusho wa hawa walio nami, na ukumbusho wa walio kabla yangu. Lakini wengi
wao hawaijui kweli, na kwa hivyo wanapuuza.
|
Ayah 21:25 الأية
وَمَا أَرْسَلْنَا مِن قَبْلِكَ مِن رَّسُولٍ إِلَّا نُوحِي إِلَيْهِ أَنَّهُ لَا
إِلَٰهَ إِلَّا أَنَا فَاعْبُدُونِ
Swahili
Na hatukumtuma kabla yako Mtume yeyote ila tulimfunulia ya kwamba hapana mungu
isipo kuwa Mimi. Basi niabuduni Mimi tu.
|
Ayah 21:26 الأية
وَقَالُوا اتَّخَذَ الرَّحْمَٰنُ وَلَدًا ۗ سُبْحَانَهُ ۚ بَلْ عِبَادٌ
مُّكْرَمُونَ
Swahili
Na wanasema: Arrahman, Mwingi wa Rehema, ana mwana! Subhanahu, Ametakasika na
hayo! Bali hao (wanao waita wana) ni watumwa walio tukuzwa.
|
Ayah 21:27 الأية
لَا يَسْبِقُونَهُ بِالْقَوْلِ وَهُم بِأَمْرِهِ يَعْمَلُونَ
Swahili
Hawamtangulii kwa neno, nao wanafanya amri zake.
|
Ayah 21:28 الأية
يَعْلَمُ مَا بَيْنَ أَيْدِيهِمْ وَمَا خَلْفَهُمْ وَلَا يَشْفَعُونَ إِلَّا لِمَنِ
ارْتَضَىٰ وَهُم مِّنْ خَشْيَتِهِ مُشْفِقُونَ
Swahili
Anayajua yaliyo mbele yao na yaliyo nyuma yao. Wala hawamwombei yeyote ila yule
anaye mridhia Yeye, nao kwa ajili ya kumwogopa wananyenyekea.
|
Ayah 21:29 الأية
وَمَن يَقُلْ مِنْهُمْ إِنِّي إِلَٰهٌ مِّن دُونِهِ فَذَٰلِكَ نَجْزِيهِ جَهَنَّمَ
ۚ كَذَٰلِكَ نَجْزِي الظَّالِمِينَ
Swahili
Na yeyote kati yao atakaye sema: Mimi ni mungu, badala yake, basi huyo tutamlipa
malipo yake Jahannamu. Hivyo ndivyo tuwalipavyo wenye kudhulumu.
|
Ayah 21:30 الأية
أَوَلَمْ يَرَ الَّذِينَ كَفَرُوا أَنَّ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضَ كَانَتَا
رَتْقًا فَفَتَقْنَاهُمَا ۖ وَجَعَلْنَا مِنَ الْمَاءِ كُلَّ شَيْءٍ حَيٍّ ۖ
أَفَلَا يُؤْمِنُونَ
Swahili
Je! Hao walio kufuru hawakuona kwamba mbingu na ardhi zilikuwa zimeambatana,
kisha Sisi tukazibabandua? Na tukajaalia kwa maji kila kilicho hai? Basi je,
hawaamini?
|
Ayah 21:31 الأية
وَجَعَلْنَا فِي الْأَرْضِ رَوَاسِيَ أَن تَمِيدَ بِهِمْ وَجَعَلْنَا فِيهَا
فِجَاجًا سُبُلًا لَّعَلَّهُمْ يَهْتَدُونَ
Swahili
Na tukaweka katika ardhi milima iliyo thibiti ili isiwayumbishe, na tukaweka
humo njia pana ili wapate kuongoka.
|
Ayah 21:32 الأية
وَجَعَلْنَا السَّمَاءَ سَقْفًا مَّحْفُوظًا ۖ وَهُمْ عَنْ آيَاتِهَا مُعْرِضُونَ
Swahili
Na tukaifanya mbingu kuwa dari iliyo hifadhiwa, lakini wanazipuuza Ishara zake.
|
Ayah 21:33 الأية
وَهُوَ الَّذِي خَلَقَ اللَّيْلَ وَالنَّهَارَ وَالشَّمْسَ وَالْقَمَرَ ۖ كُلٌّ فِي
فَلَكٍ يَسْبَحُونَ
Swahili
Na Yeye ndiye aliye umba usiku na mchana na jua na mwezi, vyote katika anga
vinaogelea.
|
Ayah 21:34 الأية
وَمَا جَعَلْنَا لِبَشَرٍ مِّن قَبْلِكَ الْخُلْدَ ۖ أَفَإِن مِّتَّ فَهُمُ
الْخَالِدُونَ
Swahili
Nasi hatukumjaalia mwanaadamu yeyote kabla yako kuwa na maisha ya milele. Basi
je! Ukifa wewe, wao wataishi milele?
|
Ayah 21:35 الأية
كُلُّ نَفْسٍ ذَائِقَةُ الْمَوْتِ ۗ وَنَبْلُوكُم بِالشَّرِّ وَالْخَيْرِ فِتْنَةً
ۖ وَإِلَيْنَا تُرْجَعُونَ
Swahili
Kila nafsi itaonja mauti; na tunakujaribuni kwa mtihani wa shari na kheri. Na
kwetu Sisi mtarejeshwa.
|
Ayah 21:36 الأية
وَإِذَا رَآكَ الَّذِينَ كَفَرُوا إِن يَتَّخِذُونَكَ إِلَّا هُزُوًا أَهَٰذَا
الَّذِي يَذْكُرُ آلِهَتَكُمْ وَهُم بِذِكْرِ الرَّحْمَٰنِ هُمْ كَافِرُونَ
Swahili
Na wakikuona walio kufuru hawakufanyi wewe ila ni kitu cha maskhara tu,
(wakisema): Je! Ndiye huyu anaye itaja miungu yenu? Na hali wao wanakataa
kumkumbuka Arrahman, Mwingi wa Rehema!
|
Ayah 21:37 الأية
خُلِقَ الْإِنسَانُ مِنْ عَجَلٍ ۚ سَأُرِيكُمْ آيَاتِي فَلَا تَسْتَعْجِلُونِ
Swahili
Mwanaadamu ameumbwa na haraka. Nitakuonyesheni Ishara zangu. Basi msinihimize.
|
Ayah 21:38 الأية
وَيَقُولُونَ مَتَىٰ هَٰذَا الْوَعْدُ إِن كُنتُمْ صَادِقِينَ
Swahili
Na wanasema: Ahadi hii itatokea lini, ikiwa nyinyi mnasema kweli?
|
Ayah 21:39 الأية
لَوْ يَعْلَمُ الَّذِينَ كَفَرُوا حِينَ لَا يَكُفُّونَ عَن وُجُوهِهِمُ النَّارَ
وَلَا عَن ظُهُورِهِمْ وَلَا هُمْ يُنصَرُونَ
Swahili
Lau wangeli jua wale walio kufuru wakati ambao hawatauzuia Moto kwenye nyuso zao
wala migongo yao, na wala hawatanusuriwa!
|
Ayah 21:40 الأية
بَلْ تَأْتِيهِم بَغْتَةً فَتَبْهَتُهُمْ فَلَا يَسْتَطِيعُونَ رَدَّهَا وَلَا هُمْ
يُنظَرُونَ
Swahili
Bali utawafikia kwa ghafla, na utawashitua na wala hawataweza kuurudisha, wala
hawatapewa muhula!
|
Ayah 21:41 الأية
وَلَقَدِ اسْتُهْزِئَ بِرُسُلٍ مِّن قَبْلِكَ فَحَاقَ بِالَّذِينَ سَخِرُوا مِنْهُم
مَّا كَانُوا بِهِ يَسْتَهْزِئُونَ
Swahili
Na Mitume walio kabla yako walikwisha dhihakiwa. Kwa hivyo wale walio wafanyia
maskhara yaliwafika yale waliyo kuwa wakiyafanyia dhihaka.
|
Ayah 21:42 الأية
قُلْ مَن يَكْلَؤُكُم بِاللَّيْلِ وَالنَّهَارِ مِنَ الرَّحْمَٰنِ ۗ بَلْ هُمْ عَن
ذِكْرِ رَبِّهِم مُّعْرِضُونَ
Swahili
Sema: Nani anaye kulindeni usiku na mchana na Arrahmani Mwingi wa Rehema? Bali
wao wanapuuza kumkumbuka Mola wao Mlezi.
|
Ayah 21:43 الأية
أَمْ لَهُمْ آلِهَةٌ تَمْنَعُهُم مِّن دُونِنَا ۚ لَا يَسْتَطِيعُونَ نَصْرَ
أَنفُسِهِمْ وَلَا هُم مِّنَّا يُصْحَبُونَ
Swahili
Au wao wanao miungu watao weza kuwakinga nasi? Hao hawawezi kujinusuru nafsi
zao, wala hawatalindwa nasi!
|
Ayah 21:44 الأية
بَلْ مَتَّعْنَا هَٰؤُلَاءِ وَآبَاءَهُمْ حَتَّىٰ طَالَ عَلَيْهِمُ الْعُمُرُ ۗ
أَفَلَا يَرَوْنَ أَنَّا نَأْتِي الْأَرْضَ نَنقُصُهَا مِنْ أَطْرَافِهَا ۚ
أَفَهُمُ الْغَالِبُونَ
Swahili
Bali tuliwastarehesha hawa na baba zao mpaka umri ukawa mrefu kwao. Je, hawaoni
ya kwamba Sisi tunaifikia ardhi tukiipunguza ncha zake? Basi je! Hao ni wenye
kushinda?
|
Ayah 21:45 الأية
قُلْ إِنَّمَا أُنذِرُكُم بِالْوَحْيِ ۚ وَلَا يَسْمَعُ الصُّمُّ الدُّعَاءَ إِذَا
مَا يُنذَرُونَ
Swahili
Sema: Mimi nakuonyeni kwa Wahyi. Na viziwi hawasikii wito wanapo onywa.
|
Ayah 21:46 الأية
وَلَئِن مَّسَّتْهُمْ نَفْحَةٌ مِّنْ عَذَابِ رَبِّكَ لَيَقُولُنَّ يَا وَيْلَنَا
إِنَّا كُنَّا ظَالِمِينَ
Swahili
Na wanapo guswa na mpulizo mmoja tu wa adhabu itokayo kwa Mola wako Mlezi, bila
ya shaka wao husema: Ole wetu! Hakika tulikuwa wenye kudhulumu.
|
Ayah 21:47 الأية
وَنَضَعُ الْمَوَازِينَ الْقِسْطَ لِيَوْمِ الْقِيَامَةِ فَلَا تُظْلَمُ نَفْسٌ
شَيْئًا ۖ وَإِن كَانَ مِثْقَالَ حَبَّةٍ مِّنْ خَرْدَلٍ أَتَيْنَا بِهَا ۗ
وَكَفَىٰ بِنَا حَاسِبِينَ
Swahili
Nasi tutaweka mizani za uadilifu kwa Siku ya Kiyama. Basi nafsi haitadhulumiwa
kitu chochote. Hata ikiwa ni uzito wa chembe ya khardali tutaileta. Nasi
tunatosha kuwa washika hisabu.
|
Ayah 21:48 الأية
وَلَقَدْ آتَيْنَا مُوسَىٰ وَهَارُونَ الْفُرْقَانَ وَضِيَاءً وَذِكْرًا
لِّلْمُتَّقِينَ
Swahili
Na kwa yakini tuliwapa Musa na Haaruni kipambanuzi, na mwangaza, na makumbusho
kwa wachamngu,
|
Ayah 21:49 الأية
الَّذِينَ يَخْشَوْنَ رَبَّهُم بِالْغَيْبِ وَهُم مِّنَ السَّاعَةِ مُشْفِقُونَ
Swahili
Ambao wanamkhofu Mola wao Mlezi faraghani, na wanaiogopa Saa ya Kiyama.
|
Ayah 21:50 الأية
وَهَٰذَا ذِكْرٌ مُّبَارَكٌ أَنزَلْنَاهُ ۚ أَفَأَنتُمْ لَهُ مُنكِرُونَ
Swahili
Na haya ni makumbusho yaliyo barikiwa, tuliyo yateremsha. Basi je! Mnayakataa?
|
Ayah 21:51 الأية
وَلَقَدْ آتَيْنَا إِبْرَاهِيمَ رُشْدَهُ مِن قَبْلُ وَكُنَّا بِهِ عَالِمِينَ
Swahili
Na hakika tulikwisha mpa Ibrahim uwongofu wake zamani, na tulikuwa tunamjua.
|
Ayah 21:52 الأية
إِذْ قَالَ لِأَبِيهِ وَقَوْمِهِ مَا هَٰذِهِ التَّمَاثِيلُ الَّتِي أَنتُمْ لَهَا
عَاكِفُونَ
Swahili
Alipo mwambia baba yake na watu wake: Ni nini haya masanamu mnayo yashughulikia
kuyaabudu?
|
Ayah 21:53 الأية
قَالُوا وَجَدْنَا آبَاءَنَا لَهَا عَابِدِينَ
Swahili
Wakasema: Tumewakuta baba zetu wakiyaabudu.
|
Ayah 21:54 الأية
قَالَ لَقَدْ كُنتُمْ أَنتُمْ وَآبَاؤُكُمْ فِي ضَلَالٍ مُّبِينٍ
Swahili
Akasema: Bila ya shaka nyinyi na baba zenu mmekuwa katika upotofu ulio dhaahiri.
|
Ayah 21:55 الأية
قَالُوا أَجِئْتَنَا بِالْحَقِّ أَمْ أَنتَ مِنَ اللَّاعِبِينَ
Swahili
Wakasema: Je! Umetujia kwa maneno ya kweli au wewe ni katika wachezao tu?
|
Ayah 21:56 الأية
قَالَ بَل رَّبُّكُمْ رَبُّ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ الَّذِي فَطَرَهُنَّ وَأَنَا
عَلَىٰ ذَٰلِكُم مِّنَ الشَّاهِدِينَ
Swahili
Akasema: Bali Mola wenu Mlezi ni Mola Mlezi wa mbingu na ardhi ambaye ndiye
aliye ziumba. Na mimi ni katika wenye kuyashuhudia hayo.
|
Ayah 21:57 الأية
وَتَاللَّهِ لَأَكِيدَنَّ أَصْنَامَكُم بَعْدَ أَن تُوَلُّوا مُدْبِرِينَ
Swahili
Na Wallahi! Nitayafanyia vitimbi masanamu yenu haya baada ya mkisha geuka kwenda
zenu.
|
Ayah 21:58 الأية
فَجَعَلَهُمْ جُذَاذًا إِلَّا كَبِيرًا لَّهُمْ لَعَلَّهُمْ إِلَيْهِ يَرْجِعُونَ
Swahili
Basi akayavunja vipande vipande, ila kubwa lao, ili wao walirudie.
|
Ayah 21:59 الأية
قَالُوا مَن فَعَلَ هَٰذَا بِآلِهَتِنَا إِنَّهُ لَمِنَ الظَّالِمِينَ
Swahili
Wakasema: Nani aliye ifanyia haya miungu yetu? Hakika huyu ni katika walio
dhulumu.
|
Ayah 21:60 الأية
قَالُوا سَمِعْنَا فَتًى يَذْكُرُهُمْ يُقَالُ لَهُ إِبْرَاهِيمُ
Swahili
Wakasema: Tumemsikia kijana mmoja akiwataja. Anaitwa Ibrahim.
|
Ayah 21:61 الأية
قَالُوا فَأْتُوا بِهِ عَلَىٰ أَعْيُنِ النَّاسِ لَعَلَّهُمْ يَشْهَدُونَ
Swahili
Wakasema: Mleteni mbele ya macho ya watu, wapate kumshuhudia!
|
Ayah 21:62 الأية
قَالُوا أَأَنتَ فَعَلْتَ هَٰذَا بِآلِهَتِنَا يَا إِبْرَاهِيمُ
Swahili
Wakasema: Je! Wewe umeifanyia haya miungu yetu, ewe Ibrahim?
|
Ayah 21:63 الأية
قَالَ بَلْ فَعَلَهُ كَبِيرُهُمْ هَٰذَا فَاسْأَلُوهُمْ إِن كَانُوا يَنطِقُونَ
Swahili
Akasema: Bali amefanya hayo huyu mkubwa wao. Basi waulizeni ikiwa wanaweza
kutamka.
|
Ayah 21:64 الأية
فَرَجَعُوا إِلَىٰ أَنفُسِهِمْ فَقَالُوا إِنَّكُمْ أَنتُمُ الظَّالِمُونَ
Swahili
Basi wakajirudi nafsi zao, wakasema: Hakika nyinyi mlikuwa madhaalimu!
|
Ayah 21:65 الأية
ثُمَّ نُكِسُوا عَلَىٰ رُءُوسِهِمْ لَقَدْ عَلِمْتَ مَا هَٰؤُلَاءِ يَنطِقُونَ
Swahili
Kisha wakarejea kwenye ule ule upotovu wao wakasema: Wewe unajua kwamba hawa
hawesemi.
|
Ayah 21:66 الأية
قَالَ أَفَتَعْبُدُونَ مِن دُونِ اللَّهِ مَا لَا يَنفَعُكُمْ شَيْئًا وَلَا
يَضُرُّكُمْ
Swahili
Akasema: Basi nyinyi mnawaabudu asiye kuwa Mwenyezi Mungu wasio kufaini kitu
wala kukudhuruni?
|
Ayah 21:67 الأية
أُفٍّ لَّكُمْ وَلِمَا تَعْبُدُونَ مِن دُونِ اللَّهِ ۖ أَفَلَا تَعْقِلُونَ
Swahili
Aibu yenu nyinyi na hivyo mnavyo viabudu badala ya Mwenyezi Mungu! Basi nyinyi
hamtii akilini?
|
Ayah 21:68 الأية
قَالُوا حَرِّقُوهُ وَانصُرُوا آلِهَتَكُمْ إِن كُنتُمْ فَاعِلِينَ
Swahili
Wakasema: Mchomeni moto, na muinusuru miungu yenu, ikiwa nyinyi ni watendao
jambo!
|
Ayah 21:69 الأية
قُلْنَا يَا نَارُ كُونِي بَرْدًا وَسَلَامًا عَلَىٰ إِبْرَاهِيمَ
Swahili
Sisi tukasema: Ewe moto! Kuwa baridi na salama kwa Ibrahim!
|
Ayah 21:70 الأية
وَأَرَادُوا بِهِ كَيْدًا فَجَعَلْنَاهُمُ الْأَخْسَرِينَ
Swahili
Wao walimkusudia maovu, lakini Sisi tukawafanya wao ndio walio khasiri.
|
Ayah 21:71 الأية
وَنَجَّيْنَاهُ وَلُوطًا إِلَى الْأَرْضِ الَّتِي بَارَكْنَا فِيهَا لِلْعَالَمِينَ
Swahili
Na tukamwokoa yeye na Luut'i tukawapeleka kwenye nchi tulio ibariki kwa ajili ya
walimwengu wote.
|
Ayah 21:72 الأية
وَوَهَبْنَا لَهُ إِسْحَاقَ وَيَعْقُوبَ نَافِلَةً ۖ وَكُلًّا جَعَلْنَا صَالِحِينَ
Swahili
Naye tukampa Is-haq, na Yaaqub kuwa ni ziada. Na wote tukawajaalia wawe watu
wema.
|
Ayah 21:73 الأية
وَجَعَلْنَاهُمْ أَئِمَّةً يَهْدُونَ بِأَمْرِنَا وَأَوْحَيْنَا إِلَيْهِمْ فِعْلَ
الْخَيْرَاتِ وَإِقَامَ الصَّلَاةِ وَإِيتَاءَ الزَّكَاةِ ۖ وَكَانُوا لَنَا
عَابِدِينَ
Swahili
Na tukawafanya maimamu wakiongoa watu kwa amri yetu. Na tukawafunulia watende
kheri, na washike Sala, na watoe Zaka; na walikuwa wanatuabudu Sisi tu.
|
Ayah 21:74 الأية
وَلُوطًا آتَيْنَاهُ حُكْمًا وَعِلْمًا وَنَجَّيْنَاهُ مِنَ الْقَرْيَةِ الَّتِي
كَانَت تَّعْمَلُ الْخَبَائِثَ ۗ إِنَّهُمْ كَانُوا قَوْمَ سَوْءٍ فَاسِقِينَ
Swahili
Na Luut'i tukampa hukumu na ilimu na tukamwokoa na ule mji ulio kuwa ukifanya
maovu. Hakika hao walikuwa watu wabaya, wachafu.
|
Ayah 21:75 الأية
وَأَدْخَلْنَاهُ فِي رَحْمَتِنَا ۖ إِنَّهُ مِنَ الصَّالِحِينَ
Swahili
Na tukamuingiza katika rehema yetu. Hakika yeye ni miongoni mwa watenda mema.
|
Ayah 21:76 الأية
وَنُوحًا إِذْ نَادَىٰ مِن قَبْلُ فَاسْتَجَبْنَا لَهُ فَنَجَّيْنَاهُ وَأَهْلَهُ
مِنَ الْكَرْبِ الْعَظِيمِ
Swahili
Na Nuhu alipo ita zamani, nasi tukamuitikia, na tukamwokoa yeye na watu wake
kutokana na shida kubwa.
|
Ayah 21:77 الأية
وَنَصَرْنَاهُ مِنَ الْقَوْمِ الَّذِينَ كَذَّبُوا بِآيَاتِنَا ۚ إِنَّهُمْ كَانُوا
قَوْمَ سَوْءٍ فَأَغْرَقْنَاهُمْ أَجْمَعِينَ
Swahili
Na tukamnusuru na watu walio zikanusha Ishara zetu. Hakika hao walikuwa watu
wabaya. Basi tukawazamisha wote.
|
Ayah 21:78 الأية
وَدَاوُودَ وَسُلَيْمَانَ إِذْ يَحْكُمَانِ فِي الْحَرْثِ إِذْ نَفَشَتْ فِيهِ
غَنَمُ الْقَوْمِ وَكُنَّا لِحُكْمِهِمْ شَاهِدِينَ
Swahili
Na Daud na Suleiman walipo kata hukumu katika kadhiya ya konde walipo lisha humo
mbuzi wa watu usiku. Na Sisi tulikuwa wenye kushuhudia hukumu yao hiyo.
|
Ayah 21:79 الأية
فَفَهَّمْنَاهَا سُلَيْمَانَ ۚ وَكُلًّا آتَيْنَا حُكْمًا وَعِلْمًا ۚ وَسَخَّرْنَا
مَعَ دَاوُودَ الْجِبَالَ يُسَبِّحْنَ وَالطَّيْرَ ۚ وَكُنَّا فَاعِلِينَ
Swahili
Tukamfahamisha Suleiman. Na kila mmoja wao tulimpa hukumu na ilimu. Na
tuliifanya milima na ndege kuwa pamoja na Daud imnyenyekee na imtakase Mwenyezi
Mungu. Na Sisi ndio tulio fanya hayo.
|
Ayah 21:80 الأية
وَعَلَّمْنَاهُ صَنْعَةَ لَبُوسٍ لَّكُمْ لِتُحْصِنَكُم مِّن بَأْسِكُمْ ۖ فَهَلْ
أَنتُمْ شَاكِرُونَ
Swahili
Na tukamfundisha kuunda mavazi ya vita kwa ajili yenu ili yakuhifadhini katika
kupigana kwenu. Je! Mtakuwa wenye kushukuru?
|
Ayah 21:81 الأية
وَلِسُلَيْمَانَ الرِّيحَ عَاصِفَةً تَجْرِي بِأَمْرِهِ إِلَى الْأَرْضِ الَّتِي
بَارَكْنَا فِيهَا ۚ وَكُنَّا بِكُلِّ شَيْءٍ عَالِمِينَ
Swahili
Na tukamsahilishia Suleiman upepo wa kimbunga wendao kwa amri yake kwenye ardhi
tuliyo ibarikia. Na Sisi ndio tunao jua kila kitu.
|
Ayah 21:82 الأية
وَمِنَ الشَّيَاطِينِ مَن يَغُوصُونَ لَهُ وَيَعْمَلُونَ عَمَلًا دُونَ ذَٰلِكَ ۖ
وَكُنَّا لَهُمْ حَافِظِينَ
Swahili
Na pia mashet'ani wanao mpigia mbizi na kufanya kazi nyenginezo. Na Sisi
tulikuwa walinzi wao.
|
Ayah 21:83 الأية
وَأَيُّوبَ إِذْ نَادَىٰ رَبَّهُ أَنِّي مَسَّنِيَ الضُّرُّ وَأَنتَ أَرْحَمُ
الرَّاحِمِينَ
Swahili
Na Ayyubu, alipo mwita Mola wake Mlezi, akasema: Mimi yamenipata madhara. Na
Wewe ndiye unaye rehemu kuliko wote wanao rehemu.
|
Ayah 21:84 الأية
فَاسْتَجَبْنَا لَهُ فَكَشَفْنَا مَا بِهِ مِن ضُرٍّ ۖ وَآتَيْنَاهُ أَهْلَهُ
وَمِثْلَهُم مَّعَهُمْ رَحْمَةً مِّنْ عِندِنَا وَذِكْرَىٰ لِلْعَابِدِينَ
Swahili
Basi tukamwitikia, na tukamwondolea madhara aliyo kuwa nayo, na tukampa watu
wake na mfano wao pamoja nao kuwa ni rehema inayo toka kwetu, na ukumbusho kwa
wafanyao ibada.
|
Ayah 21:85 الأية
وَإِسْمَاعِيلَ وَإِدْرِيسَ وَذَا الْكِفْلِ ۖ كُلٌّ مِّنَ الصَّابِرِينَ
Swahili
Na Ismail, na Idris, na Dhulkifli - wote walikuwa miongoni mwa wanao subiri.
|
Ayah 21:86 الأية
وَأَدْخَلْنَاهُمْ فِي رَحْمَتِنَا ۖ إِنَّهُم مِّنَ الصَّالِحِينَ
Swahili
Na tukawaingiza katika rehema yetu. Hakika wao walikuwa katika watu wema.
|
Ayah 21:87 الأية
وَذَا النُّونِ إِذ ذَّهَبَ مُغَاضِبًا فَظَنَّ أَن لَّن نَّقْدِرَ عَلَيْهِ
فَنَادَىٰ فِي الظُّلُمَاتِ أَن لَّا إِلَٰهَ إِلَّا أَنتَ سُبْحَانَكَ إِنِّي
كُنتُ مِنَ الظَّالِمِينَ
Swahili
Na Dhun-Nun alipoondoka hali ameghadhibika, na akadhani ya kwamba hatutakuwa na
uwezo juu yake. Basi aliita katika giza: Hapana mungu isipo kuwa Wewe Subhanaka
Uliye takasika. Hakika mimi nilikuwa miongoni mwa wenye kudhulumu.
|
Ayah 21:88 الأية
فَاسْتَجَبْنَا لَهُ وَنَجَّيْنَاهُ مِنَ الْغَمِّ ۚ وَكَذَٰلِكَ نُنجِي
الْمُؤْمِنِينَ
Swahili
Basi tukamwitikia na tukamwokoa kutokana na dhiki. Na hivyo ndivyo tunavyo
waokoa Waumini.
|
Ayah 21:89 الأية
وَزَكَرِيَّا إِذْ نَادَىٰ رَبَّهُ رَبِّ لَا تَذَرْنِي فَرْدًا وَأَنتَ خَيْرُ
الْوَارِثِينَ
Swahili
Na Zakariya alipo mwita Mola wake Mlezi: Mola wangu Mlezi! Usiniache peke yangu,
na Wewe ndiye Mbora wa wanao rithi.
|
Ayah 21:90 الأية
فَاسْتَجَبْنَا لَهُ وَوَهَبْنَا لَهُ يَحْيَىٰ وَأَصْلَحْنَا لَهُ زَوْجَهُ ۚ
إِنَّهُمْ كَانُوا يُسَارِعُونَ فِي الْخَيْرَاتِ وَيَدْعُونَنَا رَغَبًا وَرَهَبًا
ۖ وَكَانُوا لَنَا خَاشِعِينَ
Swahili
Basi tukamwitikia, na tukampa Yahya na tukamponyeshea mkewe. Hakika wao walikuwa
wepesi wa kutenda mema, na wakituomba kwa shauku na khofu. Nao walikuwa
wakitunyenyekea.
|
Ayah 21:91 الأية
وَالَّتِي أَحْصَنَتْ فَرْجَهَا فَنَفَخْنَا فِيهَا مِن رُّوحِنَا وَجَعَلْنَاهَا
وَابْنَهَا آيَةً لِّلْعَالَمِينَ
Swahili
Na mwanamke aliye linda uke wake, na tukampulizia katika roho yetu, na
tukamfanya yeye na mwanawe kuwa ni Ishara kwa walimwengu.
|
Ayah 21:92 الأية
إِنَّ هَٰذِهِ أُمَّتُكُمْ أُمَّةً وَاحِدَةً وَأَنَا رَبُّكُمْ فَاعْبُدُونِ
Swahili
Kwa hakika huu umma wenu ni umma mmoja, na Mimi ni Mola wenu Mlezi. Kwa hivyo
niabuduni Mimi.
|
Ayah 21:93 الأية
وَتَقَطَّعُوا أَمْرَهُم بَيْنَهُمْ ۖ كُلٌّ إِلَيْنَا رَاجِعُونَ
Swahili
Nao wakalikata jambo lao hili mapande mapande baina yao. Wote watarudi kwetu.
|
Ayah 21:94 الأية
فَمَن يَعْمَلْ مِنَ الصَّالِحَاتِ وَهُوَ مُؤْمِنٌ فَلَا كُفْرَانَ لِسَعْيِهِ
وَإِنَّا لَهُ كَاتِبُونَ
Swahili
Na atendaye mema naye ni Muumini basi haitakataliwa juhudi yake. Na hakika Sisi
tunamwandikia.
|
Ayah 21:95 الأية
وَحَرَامٌ عَلَىٰ قَرْيَةٍ أَهْلَكْنَاهَا أَنَّهُمْ لَا يَرْجِعُونَ
Swahili
Na haiwi kwa wana-mji tulio uangamiza, ya kwamba hawatarejea,
|
Ayah 21:96 الأية
حَتَّىٰ إِذَا فُتِحَتْ يَأْجُوجُ وَمَأْجُوجُ وَهُم مِّن كُلِّ حَدَبٍ يَنسِلُونَ
Swahili
Mpaka watapo funguliwa Juju na Maajuju wakawa wanateremka kutoka kila mlima;
|
Ayah 21:97 الأية
وَاقْتَرَبَ الْوَعْدُ الْحَقُّ فَإِذَا هِيَ شَاخِصَةٌ أَبْصَارُ الَّذِينَ
كَفَرُوا يَا وَيْلَنَا قَدْ كُنَّا فِي غَفْلَةٍ مِّنْ هَٰذَا بَلْ كُنَّا
ظَالِمِينَ
Swahili
Na miadi ya haki ikakaribia. Hapo ndipo yatapo kodoka macho ya walio kufuru (na
watasema:) Ole wetu! Bila ya shaka tulikuwa tumeghafilika na haya, bali tulikuwa
wenye kudhulumu.
|
Ayah 21:98 الأية
إِنَّكُمْ وَمَا تَعْبُدُونَ مِن دُونِ اللَّهِ حَصَبُ جَهَنَّمَ أَنتُمْ لَهَا
وَارِدُونَ
Swahili
Hakika nyinyi na hao mnao waabudu badala ya Mwenyezi Mungu ni kuni za Jahannamu;
huko mtaingia tu.
|
Ayah 21:99 الأية
لَوْ كَانَ هَٰؤُلَاءِ آلِهَةً مَّا وَرَدُوهَا ۖ وَكُلٌّ فِيهَا خَالِدُونَ
Swahili
Lau kuwa hawa ni miungu, wasingeli ingia. Na wote watadumu humo.
|
Ayah 21:100 الأية
لَهُمْ فِيهَا زَفِيرٌ وَهُمْ فِيهَا لَا يَسْمَعُونَ
Swahili
Lao wao humo ni kupiga mayowe, na wala hawatasikia (jenginelo).
|
Ayah 21:101 الأية
إِنَّ الَّذِينَ سَبَقَتْ لَهُم مِّنَّا الْحُسْنَىٰ أُولَٰئِكَ عَنْهَا
مُبْعَدُونَ
Swahili
Ama wale ambao wema wetu umewatangulia, hao watatenganishwa na hayo.
|
Ayah 21:102 الأية
لَا يَسْمَعُونَ حَسِيسَهَا ۖ وَهُمْ فِي مَا اشْتَهَتْ أَنفُسُهُمْ خَالِدُونَ
Swahili
Hawatausikia mvumo wake, na wao watadumu katika yale zinayo yatamani nafsi zao.
|
Ayah 21:103 الأية
لَا يَحْزُنُهُمُ الْفَزَعُ الْأَكْبَرُ وَتَتَلَقَّاهُمُ الْمَلَائِكَةُ هَٰذَا
يَوْمُكُمُ الَّذِي كُنتُمْ تُوعَدُونَ
Swahili
Hicho Kitisho Kikubwa hakito wahuzunisha. Na Malaika watawapokea (kwa
kuwaambia): Hii ndiyo Siku yenu mliyo kuwa mkiahidiwa!
|
Ayah 21:104 الأية
يَوْمَ نَطْوِي السَّمَاءَ كَطَيِّ السِّجِلِّ لِلْكُتُبِ ۚ كَمَا بَدَأْنَا
أَوَّلَ خَلْقٍ نُّعِيدُهُ ۚ وَعْدًا عَلَيْنَا ۚ إِنَّا كُنَّا فَاعِلِينَ
Swahili
Siku tutakapo zikunja mbingu kama mkunjo wa karatasi za vitabu. Kama tulivyo
anza umbo la mwanzo tutalirudisha tena. Ni ahadi iliyo juu yetu. Hakika Sisi ni
watendao.
|
Ayah 21:105 الأية
وَلَقَدْ كَتَبْنَا فِي الزَّبُورِ مِن بَعْدِ الذِّكْرِ أَنَّ الْأَرْضَ يَرِثُهَا
عِبَادِيَ الصَّالِحُونَ
Swahili
Na hakika tulikwisha andika katika Zaburi baada ya Kumbukumbu, ya kwamba nchi
watairithi waja wangu walio wema.
|
Ayah 21:106 الأية
إِنَّ فِي هَٰذَا لَبَلَاغًا لِّقَوْمٍ عَابِدِينَ
Swahili
Hakika katika haya yapo mawaidha kwa watu wafanyao ibada.
|
Ayah 21:107 الأية
وَمَا أَرْسَلْنَاكَ إِلَّا رَحْمَةً لِّلْعَالَمِينَ
Swahili
Nasi hatukukutuma ila uwe ni Rehema kwa walimwengu wote.
|
Ayah 21:108 الأية
قُلْ إِنَّمَا يُوحَىٰ إِلَيَّ أَنَّمَا إِلَٰهُكُمْ إِلَٰهٌ وَاحِدٌ ۖ فَهَلْ
أَنتُم مُّسْلِمُونَ
Swahili
Sema: Hakika imefunuliwa kwangu ya kwamba hakika Mungu wenu ni Mungu Mmoja tu.
Je! Mmesilimu?
|
Ayah 21:109 الأية
فَإِن تَوَلَّوْا فَقُلْ آذَنتُكُمْ عَلَىٰ سَوَاءٍ ۖ وَإِنْ أَدْرِي أَقَرِيبٌ أَم
بَعِيدٌ مَّا تُوعَدُونَ
Swahili
Na kama wakigeuka, basi sema: Nimekutangazieni sawa sawa, wala sijui yako karibu
au mbali hayo mliyo ahidiwa.
|
Ayah 21:110 الأية
إِنَّهُ يَعْلَمُ الْجَهْرَ مِنَ الْقَوْلِ وَيَعْلَمُ مَا تَكْتُمُونَ
Swahili
Hakika Yeye anajua kauli ya dhaahiri na anajua myafichayo.
|
Ayah 21:111 الأية
وَإِنْ أَدْرِي لَعَلَّهُ فِتْنَةٌ لَّكُمْ وَمَتَاعٌ إِلَىٰ حِينٍ
Swahili
Wala sijui pengine huu ni mtihani tu kwenu na starehe mpaka muda kidogo.
|
Ayah 21:112 الأية
قَالَ رَبِّ احْكُم بِالْحَقِّ ۗ وَرَبُّنَا الرَّحْمَٰنُ الْمُسْتَعَانُ عَلَىٰ
مَا تَصِفُونَ
Swahili
Sema: Mola wangu Mlezi! Hukumu kwa haki. Na Mola wetu Mlezi ni Mwingi wa Rehema,
aombwaye msaada juu ya mnayo yazua.
|
©
EsinIslam.Com Designed & produced by The Awqaf London. Please pray for us
|