« Prev

26. Surah Ash-Shu'arâ' سورة الشعراء

Next »



First Ayah   1   الأية الأولي
بِسْم ِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ
طسم
Swahili
 
T'aa Siin Miim. (T'.S.M.)

Ayah   26:2   الأية
تِلْكَ آيَاتُ الْكِتَابِ الْمُبِينِ
Swahili
 
Hizi ni Aya za Kitabu kinacho bainisha.

Ayah   26:3   الأية
لَعَلَّكَ بَاخِعٌ نَّفْسَكَ أَلَّا يَكُونُوا مُؤْمِنِينَ
Swahili
 
Huenda labda ukajikera nafsi yako kwa kuwa hawawi Waumini.

Ayah   26:4   الأية
إِن نَّشَأْ نُنَزِّلْ عَلَيْهِم مِّنَ السَّمَاءِ آيَةً فَظَلَّتْ أَعْنَاقُهُمْ لَهَا خَاضِعِينَ
Swahili
 
Tunge penda tungeli wateremshia kutoka mbinguni Ishara zikanyenyekea shingo zao.

Ayah   26:5   الأية
وَمَا يَأْتِيهِم مِّن ذِكْرٍ مِّنَ الرَّحْمَٰنِ مُحْدَثٍ إِلَّا كَانُوا عَنْهُ مُعْرِضِينَ
Swahili
 
Wala hauwafikii ukumbusho mpya kutoka kwa Arrahman ila wao hujitenga nao.

Ayah   26:6   الأية
فَقَدْ كَذَّبُوا فَسَيَأْتِيهِمْ أَنبَاءُ مَا كَانُوا بِهِ يَسْتَهْزِئُونَ
Swahili
 
Kwa yakini wamekanusha; kwa hivyo zitakuja wafikia khabari za yale waliyo kuwa wakiyafanyia mzaha.

Ayah   26:7   الأية
أَوَلَمْ يَرَوْا إِلَى الْأَرْضِ كَمْ أَنبَتْنَا فِيهَا مِن كُلِّ زَوْجٍ كَرِيمٍ
Swahili
 
Je! Hawakuiona ardhi, mimea mingapi tumeiotesha humo, ya kila namna nzuri?

Ayah   26:8   الأية
إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَةً ۖ وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ
Swahili
 
Hakika katika haya zipo Ishara. Lakini wengi wao hawakuwa wenye kuamini.

Ayah   26:9   الأية
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ الْعَزِيزُ الرَّحِيمُ
Swahili
 
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Yeye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.

Ayah   26:10   الأية
وَإِذْ نَادَىٰ رَبُّكَ مُوسَىٰ أَنِ ائْتِ الْقَوْمَ الظَّالِمِينَ
Swahili
 
Na Mola wako Mlezi, alipo mwita Musa, akamwambia: Fika kwa watu madhaalimu,

Ayah   26:11   الأية
قَوْمَ فِرْعَوْنَ ۚ أَلَا يَتَّقُونَ
Swahili
 
Watu wa Firauni. Hawaogopi?

Ayah   26:12   الأية
قَالَ رَبِّ إِنِّي أَخَافُ أَن يُكَذِّبُونِ
Swahili
 
Akasema: Hakika mimi nachelea wasinikanushe.

Ayah   26:13   الأية
وَيَضِيقُ صَدْرِي وَلَا يَنطَلِقُ لِسَانِي فَأَرْسِلْ إِلَىٰ هَارُونَ
Swahili
 
Na kifua changu kina dhiki, na ulimi wangu haukunjuki vyema. Basi mtumie ujumbe Harun.

Ayah   26:14   الأية
وَلَهُمْ عَلَيَّ ذَنبٌ فَأَخَافُ أَن يَقْتُلُونِ
Swahili
 
Na wao wana kisasi juu yangu, kwa hivyo naogopa wasije kuniuwa.

Ayah   26:15   الأية
قَالَ كَلَّا ۖ فَاذْهَبَا بِآيَاتِنَا ۖ إِنَّا مَعَكُم مُّسْتَمِعُونَ
Swahili
 
Akasema: Siyo hivyo kabisa! Nendeni na miujiza yetu. Hakika Sisi tu pamoja nanyi, tunasikiliza.

Ayah   26:16   الأية
فَأْتِيَا فِرْعَوْنَ فَقُولَا إِنَّا رَسُولُ رَبِّ الْعَالَمِينَ
Swahili
 
Basi mfikieni Firauni na mwambieni: Hakika sisi ni Mitume wa Mola Mlezi wa walimwengu wote.

Ayah   26:17   الأية
أَنْ أَرْسِلْ مَعَنَا بَنِي إِسْرَائِيلَ
Swahili
 
Waachilie Wana wa Israili wende nasi.

Ayah   26:18   الأية
قَالَ أَلَمْ نُرَبِّكَ فِينَا وَلِيدًا وَلَبِثْتَ فِينَا مِنْ عُمُرِكَ سِنِينَ
Swahili
 
(Firauni) akasema: Sisi hatukukulea wewe utotoni, na ukakaa kwetu katika umri wako miaka mingi?

Ayah   26:19   الأية
وَفَعَلْتَ فَعْلَتَكَ الَّتِي فَعَلْتَ وَأَنتَ مِنَ الْكَافِرِينَ
Swahili
 
Na ukatenda kitendo chako ulicho tenda, nawe ukawa miongoni mwa wasio na shukrani?

Ayah   26:20   الأية
قَالَ فَعَلْتُهَا إِذًا وَأَنَا مِنَ الضَّالِّينَ
Swahili
 
(Musa) akasema: Nilitenda hayo hapo nilipo kuwa miongoni mwa wale walio potea.

Ayah   26:21   الأية
فَفَرَرْتُ مِنكُمْ لَمَّا خِفْتُكُمْ فَوَهَبَ لِي رَبِّي حُكْمًا وَجَعَلَنِي مِنَ الْمُرْسَلِينَ
Swahili
 
Basi nikakukimbieni nilipo kuogopeni, tena Mola wangu Mlezi akanitunukia hukumu, na akanijaalia niwe miongoni mwa Mitume.

Ayah   26:22   الأية
وَتِلْكَ نِعْمَةٌ تَمُنُّهَا عَلَيَّ أَنْ عَبَّدتَّ بَنِي إِسْرَائِيلَ
Swahili
 
Na hiyo ndiyo neema ya kunisumbulia, na wewe umewatia utumwani Wana wa Israili?

Ayah   26:23   الأية
قَالَ فِرْعَوْنُ وَمَا رَبُّ الْعَالَمِينَ
Swahili
 
Firauni akasema: Na nani huyo Mola Mlezi wa walimwengu wote?

Ayah   26:24   الأية
قَالَ رَبُّ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَمَا بَيْنَهُمَا ۖ إِن كُنتُم مُّوقِنِينَ
Swahili
 
Akasema: Ndiye Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, na viliomo baina yao, ikiwa nyinyi ni wenye yakini.

Ayah   26:25   الأية
قَالَ لِمَنْ حَوْلَهُ أَلَا تَسْتَمِعُونَ
Swahili
 
(Firauni) akawaambia walio mzunguka: Hamsikilizi?

Ayah   26:26   الأية
قَالَ رَبُّكُمْ وَرَبُّ آبَائِكُمُ الْأَوَّلِينَ
Swahili
 
(Musa) akasema: Ndiye Mola wenu Mlezi, na Mola Mlezi wa baba zenu wa kwanza.

Ayah   26:27   الأية
قَالَ إِنَّ رَسُولَكُمُ الَّذِي أُرْسِلَ إِلَيْكُمْ لَمَجْنُونٌ
Swahili
 
(Firauni) akasema: Hakika huyu Mtume wenu aliye tumwa kwenu ni mwendawazimu.

Ayah   26:28   الأية
قَالَ رَبُّ الْمَشْرِقِ وَالْمَغْرِبِ وَمَا بَيْنَهُمَا ۖ إِن كُنتُمْ تَعْقِلُونَ
Swahili
 
(Musa) akasema: Ndiye Mola Mlezi wa Mashariki na Magharibi na viliomo baina yao, ikiwa nyinyi mnatia akilini.

Ayah   26:29   الأية
قَالَ لَئِنِ اتَّخَذْتَ إِلَٰهًا غَيْرِي لَأَجْعَلَنَّكَ مِنَ الْمَسْجُونِينَ
Swahili
 
(Firauni) akasema: Ukimfuata mungu mwengine asiye kuwa mimi, basi bila ya shaka nitakufunga gerezani.

Ayah   26:30   الأية
قَالَ أَوَلَوْ جِئْتُكَ بِشَيْءٍ مُّبِينٍ
Swahili
 
Akasema: Je! Ijapo kuwa nitakuletea kitu cha kubainisha wazi?

Ayah   26:31   الأية
قَالَ فَأْتِ بِهِ إِن كُنتَ مِنَ الصَّادِقِينَ
Swahili
 
Akasema: Kilete basi, kama wewe ni katika wasemao kweli.

Ayah   26:32   الأية
فَأَلْقَىٰ عَصَاهُ فَإِذَا هِيَ ثُعْبَانٌ مُّبِينٌ
Swahili
 
Basi akaitupa fimbo yake, mara ikawa nyoka wa kuonekana dhaahiri.

Ayah   26:33   الأية
وَنَزَعَ يَدَهُ فَإِذَا هِيَ بَيْضَاءُ لِلنَّاظِرِينَ
Swahili
 
Na akautoa mkono wake, na mara ukawa mweupe kwa watazamao.

Ayah   26:34   الأية
قَالَ لِلْمَلَإِ حَوْلَهُ إِنَّ هَٰذَا لَسَاحِرٌ عَلِيمٌ
Swahili
 
(Firauni) akawaambia waheshimiwa walio mzunguka: Hakika huyu ni mchawi mtaalamu.

Ayah   26:35   الأية
يُرِيدُ أَن يُخْرِجَكُم مِّنْ أَرْضِكُم بِسِحْرِهِ فَمَاذَا تَأْمُرُونَ
Swahili
 
Anataka kukutoeni katika nchi yenu kwa uchawi wake. Basi mna shauri gani?

Ayah   26:36   الأية
قَالُوا أَرْجِهْ وَأَخَاهُ وَابْعَثْ فِي الْمَدَائِنِ حَاشِرِينَ
Swahili
 
Wakasema: Mpe muda yeye na nduguye na uwatume mijini wapigao mbiu ya mgambo.

Ayah   26:37   الأية
يَأْتُوكَ بِكُلِّ سَحَّارٍ عَلِيمٍ
Swahili
 
Wakuletee kila mchawi bingwa mtaalamu.

Ayah   26:38   الأية
فَجُمِعَ السَّحَرَةُ لِمِيقَاتِ يَوْمٍ مَّعْلُومٍ
Swahili
 
Basi wakakusanywa wachawi wakati na siku maalumu.

Ayah   26:39   الأية
وَقِيلَ لِلنَّاسِ هَلْ أَنتُم مُّجْتَمِعُونَ
Swahili
 
Na watu wakaambiwa: Je! Mtakusanyika?

Ayah   26:40   الأية
لَعَلَّنَا نَتَّبِعُ السَّحَرَةَ إِن كَانُوا هُمُ الْغَالِبِينَ
Swahili
 
Huenda tutawafuata wachawi wakiwa wao ndio watakao shinda.

Ayah   26:41   الأية
فَلَمَّا جَاءَ السَّحَرَةُ قَالُوا لِفِرْعَوْنَ أَئِنَّ لَنَا لَأَجْرًا إِن كُنَّا نَحْنُ الْغَالِبِينَ
Swahili
 
Basi walipo kuja wachawi wakamwambia Firauni: Je! Tutapata ujira tukiwa sisi ndio tulio shinda?

Ayah   26:42   الأية
قَالَ نَعَمْ وَإِنَّكُمْ إِذًا لَّمِنَ الْمُقَرَّبِينَ
Swahili
 
Naam! Na hakika mtakuwa katika watu wa mbele.

Ayah   26:43   الأية
قَالَ لَهُم مُّوسَىٰ أَلْقُوا مَا أَنتُم مُّلْقُونَ
Swahili
 
Musa akwaambia: Tupeni mnavyo taka kutupa.

Ayah   26:44   الأية
فَأَلْقَوْا حِبَالَهُمْ وَعِصِيَّهُمْ وَقَالُوا بِعِزَّةِ فِرْعَوْنَ إِنَّا لَنَحْنُ الْغَالِبُونَ
Swahili
 
Basi wakatupa kamba zao na fimbo zao, na wakasema: Kwa nguvu za Firauni hakika sisi hapana shaka ni wenye kushinda.

Ayah   26:45   الأية
فَأَلْقَىٰ مُوسَىٰ عَصَاهُ فَإِذَا هِيَ تَلْقَفُ مَا يَأْفِكُونَ
Swahili
 
Musa tena akatupa fimbo yake, nayo mara ikavimeza walivyo vizua.

Ayah   26:46   الأية
فَأُلْقِيَ السَّحَرَةُ سَاجِدِينَ
Swahili
 
Hapo wachawi walipinduka wakasujudu.

Ayah   26:47   الأية
قَالُوا آمَنَّا بِرَبِّ الْعَالَمِينَ
Swahili
 
Wakasema: Tunamuamini Mola Mlezi wa walimwengu wote.

Ayah   26:48   الأية
رَبِّ مُوسَىٰ وَهَارُونَ
Swahili
 
Mola Mlezi wa Musa na Harun.

Ayah   26:49   الأية
قَالَ آمَنتُمْ لَهُ قَبْلَ أَنْ آذَنَ لَكُمْ ۖ إِنَّهُ لَكَبِيرُكُمُ الَّذِي عَلَّمَكُمُ السِّحْرَ فَلَسَوْفَ تَعْلَمُونَ ۚ لَأُقَطِّعَنَّ أَيْدِيَكُمْ وَأَرْجُلَكُم مِّنْ خِلَافٍ وَلَأُصَلِّبَنَّكُمْ أَجْمَعِينَ
Swahili
 
(Firauni) akasema: Je! Mmemuamini kabla sijakuruhusuni? Bila ya shaka yeye basi ndiye mkubwa wenu aliye kufunzeni uchawi. Basi mtakuja jua! Nitakata mikono yenu na miguu yenu kwa kutafautisha. Na nitakubandikeni misalabani nyote.

Ayah   26:50   الأية
قَالُوا لَا ضَيْرَ ۖ إِنَّا إِلَىٰ رَبِّنَا مُنقَلِبُونَ
Swahili
 
Wakasema: Haidhuru, kwani sisi ni wenye kurejea kwa Mola wetu Mlezi.

Ayah   26:51   الأية
إِنَّا نَطْمَعُ أَن يَغْفِرَ لَنَا رَبُّنَا خَطَايَانَا أَن كُنَّا أَوَّلَ الْمُؤْمِنِينَ
Swahili
 
Hakika sisi tunatumai Mola wetu Mlezi atatusamehe makosa yetu, kwa kuwa ndio wa kwanza wa kuamini.

Ayah   26:52   الأية
وَأَوْحَيْنَا إِلَىٰ مُوسَىٰ أَنْ أَسْرِ بِعِبَادِي إِنَّكُم مُّتَّبَعُونَ
Swahili
 
Na tulimuamrisha Musa kwa wahyi: Nenda na waja wangu wakati wa usiku. Kwa hakika mtafuatwa.

Ayah   26:53   الأية
فَأَرْسَلَ فِرْعَوْنُ فِي الْمَدَائِنِ حَاشِرِينَ
Swahili
 
Basi Firauni akawatuma mijini wapiga mbiu za mgambo.

Ayah   26:54   الأية
إِنَّ هَٰؤُلَاءِ لَشِرْذِمَةٌ قَلِيلُونَ
Swahili
 
(Wakieneza): Hakika hawa ni kikundi kidogo.

Ayah   26:55   الأية
وَإِنَّهُمْ لَنَا لَغَائِظُونَ
Swahili
 
Nao wanatuudhi.

Ayah   26:56   الأية
وَإِنَّا لَجَمِيعٌ حَاذِرُونَ
Swahili
 
Na sisi ni wengi, wenye kuchukua hadhari.

Ayah   26:57   الأية
فَأَخْرَجْنَاهُم مِّن جَنَّاتٍ وَعُيُونٍ
Swahili
 
Basi tukawatoa katika mabustani na chemchem,

Ayah   26:58   الأية
وَكُنُوزٍ وَمَقَامٍ كَرِيمٍ
Swahili
 
Na makhazina, na vyeo vya hishima,

Ayah   26:59   الأية
كَذَٰلِكَ وَأَوْرَثْنَاهَا بَنِي إِسْرَائِيلَ
Swahili
 
Kadhaalika; na tukawarithisha hayo Wana wa Israili.

Ayah   26:60   الأية
فَأَتْبَعُوهُم مُّشْرِقِينَ
Swahili
 
Basi wakawafuata lilipo chomoza jua.

Ayah   26:61   الأية
فَلَمَّا تَرَاءَى الْجَمْعَانِ قَالَ أَصْحَابُ مُوسَىٰ إِنَّا لَمُدْرَكُونَ
Swahili
 
Na yalipo onana majeshi mawili haya, watu wa Musa wakasema: Hakika sisi bila ya shaka tumepatikana!

Ayah   26:62   الأية
قَالَ كَلَّا ۖ إِنَّ مَعِيَ رَبِّي سَيَهْدِينِ
Swahili
 
(Musa) akasema: Hasha! Hakika yu pamoja nami Mola wangu Mlezi. Yeye ataniongoa!

Ayah   26:63   الأية
فَأَوْحَيْنَا إِلَىٰ مُوسَىٰ أَنِ اضْرِب بِّعَصَاكَ الْبَحْرَ ۖ فَانفَلَقَ فَكَانَ كُلُّ فِرْقٍ كَالطَّوْدِ الْعَظِيمِ
Swahili
 
Tulimletea wahyi Musa tukamwambia: Piga bahari kwa fimbo yako. Basi ikatengana, na kila sehemu ikawa kama mlima mkubwa.

Ayah   26:64   الأية
وَأَزْلَفْنَا ثَمَّ الْآخَرِينَ
Swahili
 
Na tukawajongeza hapo wale wengine.

Ayah   26:65   الأية
وَأَنجَيْنَا مُوسَىٰ وَمَن مَّعَهُ أَجْمَعِينَ
Swahili
 
Tukawaokoa Musa na walio kuwa pamoja naye wote.

Ayah   26:66   الأية
ثُمَّ أَغْرَقْنَا الْآخَرِينَ
Swahili
 
Kisha tukawazamisha hao wengine.

Ayah   26:67   الأية
إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَةً ۖ وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ
Swahili
 
Hakika bila ya shaka katika hayo ipo Ishara; lakini wengi wao si katika wenye kuamini.

Ayah   26:68   الأية
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ الْعَزِيزُ الرَّحِيمُ
Swahili
 
Na kwa hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.

Ayah   26:69   الأية
وَاتْلُ عَلَيْهِمْ نَبَأَ إِبْرَاهِيمَ
Swahili
 
Na wasomee khabari za Ibrahim.

Ayah   26:70   الأية
إِذْ قَالَ لِأَبِيهِ وَقَوْمِهِ مَا تَعْبُدُونَ
Swahili
 
Alipo mwambia baba yake na kaumu yake: Mnaabudu nini?

Ayah   26:71   الأية
قَالُوا نَعْبُدُ أَصْنَامًا فَنَظَلُّ لَهَا عَاكِفِينَ
Swahili
 
Wakasema: Tunaabudu masanamu, daima tunayanyenyekea.

Ayah   26:72   الأية
قَالَ هَلْ يَسْمَعُونَكُمْ إِذْ تَدْعُونَ
Swahili
 
Akasema: Je! Yanakusikieni mnapo yaita?

Ayah   26:73   الأية
أَوْ يَنفَعُونَكُمْ أَوْ يَضُرُّونَ
Swahili
 
Au yanakufaeni, au yanakudhuruni?

Ayah   26:74   الأية
قَالُوا بَلْ وَجَدْنَا آبَاءَنَا كَذَٰلِكَ يَفْعَلُونَ
Swahili
 
Wakasema: Bali tumewakuta baba zetu wakifanya hivyo hivyo.

Ayah   26:75   الأية
قَالَ أَفَرَأَيْتُم مَّا كُنتُمْ تَعْبُدُونَ
Swahili
 
Je! Mmewaona hawa mnao waabudu-

Ayah   26:76   الأية
أَنتُمْ وَآبَاؤُكُمُ الْأَقْدَمُونَ
Swahili
 
Nyinyi na baba zenu wa zamani?

Ayah   26:77   الأية
فَإِنَّهُمْ عَدُوٌّ لِّي إِلَّا رَبَّ الْعَالَمِينَ
Swahili
 
Kwani hakika hao ni adui zangu, isipo kuwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.

Ayah   26:78   الأية
الَّذِي خَلَقَنِي فَهُوَ يَهْدِينِ
Swahili
 
Ambaye ndiye aliye niumba, na Yeye ndiye ananiongoa,

Ayah   26:79   الأية
وَالَّذِي هُوَ يُطْعِمُنِي وَيَسْقِينِ
Swahili
 
Na ambaye ndiye ananilisha na kuninywesha.

Ayah   26:80   الأية
وَإِذَا مَرِضْتُ فَهُوَ يَشْفِينِ
Swahili
 
Na ninapo ugua ni Yeye ndiye anaye niponesha.

Ayah   26:81   الأية
وَالَّذِي يُمِيتُنِي ثُمَّ يُحْيِينِ
Swahili
 
Na ambaye atanifisha, na kisha atanihuisha.

Ayah   26:82   الأية
وَالَّذِي أَطْمَعُ أَن يَغْفِرَ لِي خَطِيئَتِي يَوْمَ الدِّينِ
Swahili
 
Na ambaye ndiye ninaye mtumai kunisamehe makosa yangu Siku ya Malipo.

Ayah   26:83   الأية
رَبِّ هَبْ لِي حُكْمًا وَأَلْحِقْنِي بِالصَّالِحِينَ
Swahili
 
Mola wangu Mlezi! Nitunukie hukumu na uniunganishe na watendao mema.

Ayah   26:84   الأية
وَاجْعَل لِّي لِسَانَ صِدْقٍ فِي الْآخِرِينَ
Swahili
 
Na unijaalie nitajwe kwa wema na watu watakao kuja baadaye.

Ayah   26:85   الأية
وَاجْعَلْنِي مِن وَرَثَةِ جَنَّةِ النَّعِيمِ
Swahili
 
Na unijaalie katika warithi wa Bustani za neema.

Ayah   26:86   الأية
وَاغْفِرْ لِأَبِي إِنَّهُ كَانَ مِنَ الضَّالِّينَ
Swahili
 
Na umsamehe baba yangu, kwani hakika alikuwa miongoni mwa wapotovu.

Ayah   26:87   الأية
وَلَا تُخْزِنِي يَوْمَ يُبْعَثُونَ
Swahili
 
Wala usinihizi Siku watapo fufuliwa.

Ayah   26:88   الأية
يَوْمَ لَا يَنفَعُ مَالٌ وَلَا بَنُونَ
Swahili
 
Siku ambayo kwamba mali hayato faa kitu wala wana.

Ayah   26:89   الأية
إِلَّا مَنْ أَتَى اللَّهَ بِقَلْبٍ سَلِيمٍ
Swahili
 
Isipo kuwa mwenye kumjia Mwenyezi Mungu na moyo safi.

Ayah   26:90   الأية
وَأُزْلِفَتِ الْجَنَّةُ لِلْمُتَّقِينَ
Swahili
 
Na Pepo itasogezwa kwa wachamngu.

Ayah   26:91   الأية
وَبُرِّزَتِ الْجَحِيمُ لِلْغَاوِينَ
Swahili
 
Na Jahannamu itadhihirishwa kwa wapotovu.

Ayah   26:92   الأية
وَقِيلَ لَهُمْ أَيْنَ مَا كُنتُمْ تَعْبُدُونَ
Swahili
 
Na wataambiwa: Wako wapi mlio kuwa mkiwaabudu

Ayah   26:93   الأية
مِن دُونِ اللَّهِ هَلْ يَنصُرُونَكُمْ أَوْ يَنتَصِرُونَ
Swahili
 
Badala ya Mwenyezi Mungu? Je! Wanakusaidieni, au wanajisaidia wenyewe?

Ayah   26:94   الأية
فَكُبْكِبُوا فِيهَا هُمْ وَالْغَاوُونَ
Swahili
 
Basi watavurumizwa humo wao na hao wakosefu,

Ayah   26:95   الأية
وَجُنُودُ إِبْلِيسَ أَجْمَعُونَ
Swahili
 
Na majeshi ya Ibilisi yote.

Ayah   26:96   الأية
قَالُوا وَهُمْ فِيهَا يَخْتَصِمُونَ
Swahili
 
Watasema, na hali ya kuwa wanazozana humo:

Ayah   26:97   الأية
تَاللَّهِ إِن كُنَّا لَفِي ضَلَالٍ مُّبِينٍ
Swahili
 
Wallahi! Kwa yakini tulikuwa katika upotovu ulio dhaahiri,

Ayah   26:98   الأية
إِذْ نُسَوِّيكُم بِرَبِّ الْعَالَمِينَ
Swahili
 
Tulipo kufanyeni ni sawa na Mola Mlezi wa walimwengu wote.

Ayah   26:99   الأية
وَمَا أَضَلَّنَا إِلَّا الْمُجْرِمُونَ
Swahili
 
Na hawakutupoteza ila wale wakosefu.

Ayah   26:100   الأية
فَمَا لَنَا مِن شَافِعِينَ
Swahili
 
Basi hatuna waombezi.

Ayah   26:101   الأية
وَلَا صَدِيقٍ حَمِيمٍ
Swahili
 
Wala rafiki wa dhati.

Ayah   26:102   الأية
فَلَوْ أَنَّ لَنَا كَرَّةً فَنَكُونَ مِنَ الْمُؤْمِنِينَ
Swahili
 
Laiti tungeli pata kurejea tena tungeli kuwa katika Waumini.

Ayah   26:103   الأية
إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَةً ۖ وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ
Swahili
 
Hakika katika haya ipo Ishara, lakini wengi wao hawakuwa wenye kuamini.

Ayah   26:104   الأية
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ الْعَزِيزُ الرَّحِيمُ
Swahili
 
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.

Ayah   26:105   الأية
كَذَّبَتْ قَوْمُ نُوحٍ الْمُرْسَلِينَ
Swahili
 
Kaumu ya Nuhu waliwakadhibisha Mitume.

Ayah   26:106   الأية
إِذْ قَالَ لَهُمْ أَخُوهُمْ نُوحٌ أَلَا تَتَّقُونَ
Swahili
 
Alipo waambia ndugu yao, Nuhu: Je! Hamchimngu?

Ayah   26:107   الأية
إِنِّي لَكُمْ رَسُولٌ أَمِينٌ
Swahili
 
Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu.

Ayah   26:108   الأية
فَاتَّقُوا اللَّهَ وَأَطِيعُونِ
Swahili
 
Basi Mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini mimi.

Ayah   26:109   الأية
وَمَا أَسْأَلُكُمْ عَلَيْهِ مِنْ أَجْرٍ ۖ إِنْ أَجْرِيَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ الْعَالَمِينَ
Swahili
 
Na sikutakini juu yake ujira, kwani ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.

Ayah   26:110   الأية
فَاتَّقُوا اللَّهَ وَأَطِيعُونِ
Swahili
 
Basi Mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini mimi.

Ayah   26:111   الأية
قَالُوا أَنُؤْمِنُ لَكَ وَاتَّبَعَكَ الْأَرْذَلُونَ
Swahili
 
Wakasema: Je! Tukuamini wewe, hali wanao kufuata ni watu wa chini?

Ayah   26:112   الأية
قَالَ وَمَا عِلْمِي بِمَا كَانُوا يَعْمَلُونَ
Swahili
 
Akasema: Nayajuaje waliyo kuwa wakiyafanya?

Ayah   26:113   الأية
إِنْ حِسَابُهُمْ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّي ۖ لَوْ تَشْعُرُونَ
Swahili
 
Hisabu yao haiko ila kwa Mola wao Mlezi, laiti mngeli tambua!

Ayah   26:114   الأية
وَمَا أَنَا بِطَارِدِ الْمُؤْمِنِينَ
Swahili
 
Wala mimi si wa kuwafukuza Waumini.

Ayah   26:115   الأية
إِنْ أَنَا إِلَّا نَذِيرٌ مُّبِينٌ
Swahili
 
Mimi si cho chote ila ni Mwonyaji wa dhaahiri shaahiri.

Ayah   26:116   الأية
قَالُوا لَئِن لَّمْ تَنتَهِ يَا نُوحُ لَتَكُونَنَّ مِنَ الْمَرْجُومِينَ
Swahili
 
Wakasema: Ikiwa huachi, ewe Nuhu, bila ya shaka utapigwa mawe.

Ayah   26:117   الأية
قَالَ رَبِّ إِنَّ قَوْمِي كَذَّبُونِ
Swahili
 
Akasema: Mola wangu Mlezi! Hakika watu wangu wamenikanusha.

Ayah   26:118   الأية
فَافْتَحْ بَيْنِي وَبَيْنَهُمْ فَتْحًا وَنَجِّنِي وَمَن مَّعِيَ مِنَ الْمُؤْمِنِينَ
Swahili
 
Basi hukumu baina yangu na wao kwa hukumu yako, na uniokoe mimi na walio pamoja nami, Waumini.

Ayah   26:119   الأية
فَأَنجَيْنَاهُ وَمَن مَّعَهُ فِي الْفُلْكِ الْمَشْحُونِ
Swahili
 
Kwa hivyo tukamwokoa yeye na walio kuwa pamoja naye katika marikebu iliyo sheheni.

Ayah   26:120   الأية
ثُمَّ أَغْرَقْنَا بَعْدُ الْبَاقِينَ
Swahili
 
Kisha tukawazamisha baadaye walio bakia.

Ayah   26:121   الأية
إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَةً ۖ وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ
Swahili
 
Hakika katika haya ipo Ishara, lakini si wengi wao walio kuwa Waumini.

Ayah   26:122   الأية
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ الْعَزِيزُ الرَّحِيمُ
Swahili
 
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Yeye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.

Ayah   26:123   الأية
كَذَّبَتْ عَادٌ الْمُرْسَلِينَ
Swahili
 
Kina A'd waliwakanusha Mitume.

Ayah   26:124   الأية
إِذْ قَالَ لَهُمْ أَخُوهُمْ هُودٌ أَلَا تَتَّقُونَ
Swahili
 
Alipo waambia ndugu yao, Hud: Je! Hamchimngu?

Ayah   26:125   الأية
إِنِّي لَكُمْ رَسُولٌ أَمِينٌ
Swahili
 
Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu.

Ayah   26:126   الأية
فَاتَّقُوا اللَّهَ وَأَطِيعُونِ
Swahili
 
Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini mimi.

Ayah   26:127   الأية
وَمَا أَسْأَلُكُمْ عَلَيْهِ مِنْ أَجْرٍ ۖ إِنْ أَجْرِيَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ الْعَالَمِينَ
Swahili
 
Wala sikutakeni juu yake ujira, kwani ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.

Ayah   26:128   الأية
أَتَبْنُونَ بِكُلِّ رِيعٍ آيَةً تَعْبَثُونَ
Swahili
 
Je! Mnajenga juu ya kila mnyanyuko kumbusho la kufanyia upuuzi?

Ayah   26:129   الأية
وَتَتَّخِذُونَ مَصَانِعَ لَعَلَّكُمْ تَخْلُدُونَ
Swahili
 
Na mnajenga majengo ya fakhari kama kwamba mtaishi milele!

Ayah   26:130   الأية
وَإِذَا بَطَشْتُم بَطَشْتُمْ جَبَّارِينَ
Swahili
 
Na mnapo tumia nguvu mnatumia nguvu kwa ujabari.

Ayah   26:131   الأية
فَاتَّقُوا اللَّهَ وَأَطِيعُونِ
Swahili
 
Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini.

Ayah   26:132   الأية
وَاتَّقُوا الَّذِي أَمَدَّكُم بِمَا تَعْلَمُونَ
Swahili
 
Na mcheni aliye kupeni haya mnayo yajua.

Ayah   26:133   الأية
أَمَدَّكُم بِأَنْعَامٍ وَبَنِينَ
Swahili
 
Amekupeni wanyama wa kufuga na wana.

Ayah   26:134   الأية
وَجَنَّاتٍ وَعُيُونٍ
Swahili
 
Na mabustani na chemchem.

Ayah   26:135   الأية
إِنِّي أَخَافُ عَلَيْكُمْ عَذَابَ يَوْمٍ عَظِيمٍ
Swahili
 
Hakika mimi ninakukhofieni adhabu ya Siku Kubwa.

Ayah   26:136   الأية
قَالُوا سَوَاءٌ عَلَيْنَا أَوَعَظْتَ أَمْ لَمْ تَكُن مِّنَ الْوَاعِظِينَ
Swahili
 
Wakasema: Ni mamoja kwetu, ukitupa mawaidha au hukuwa miongoni mwa watoao mawaidha.

Ayah   26:137   الأية
إِنْ هَٰذَا إِلَّا خُلُقُ الْأَوَّلِينَ
Swahili
 
Haya si chochote ila ni mtindo wa watu wa tokea zamani.

Ayah   26:138   الأية
وَمَا نَحْنُ بِمُعَذَّبِينَ
Swahili
 
Wala sisi hatutaadhibiwa.

Ayah   26:139   الأية
فَكَذَّبُوهُ فَأَهْلَكْنَاهُمْ ۗ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَةً ۖ وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ
Swahili
 
Wakamkanusha; nasi tukawaangamiza. Hakika bila ya shaka katika haya ipo Ishara. Lakini hawakuwa wengi wao wenye kuamini.

Ayah   26:140   الأية
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ الْعَزِيزُ الرَّحِيمُ
Swahili
 
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.

Ayah   26:141   الأية
كَذَّبَتْ ثَمُودُ الْمُرْسَلِينَ
Swahili
 
Kina Thamud waliwakanusha Mitume.

Ayah   26:142   الأية
إِذْ قَالَ لَهُمْ أَخُوهُمْ صَالِحٌ أَلَا تَتَّقُونَ
Swahili
 
Alipo waambia ndugu yao Saleh: Je! Hamumchimngu?

Ayah   26:143   الأية
إِنِّي لَكُمْ رَسُولٌ أَمِينٌ
Swahili
 
Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu.

Ayah   26:144   الأية
فَاتَّقُوا اللَّهَ وَأَطِيعُونِ
Swahili
 
Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini.

Ayah   26:145   الأية
وَمَا أَسْأَلُكُمْ عَلَيْهِ مِنْ أَجْرٍ ۖ إِنْ أَجْرِيَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ الْعَالَمِينَ
Swahili
 
Wala sikutakini ujira juu yake. Ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.

Ayah   26:146   الأية
أَتُتْرَكُونَ فِي مَا هَاهُنَا آمِنِينَ
Swahili
 
Je! Mtaachwa salama usalimina katika haya yaliyopo hapa?

Ayah   26:147   الأية
فِي جَنَّاتٍ وَعُيُونٍ
Swahili
 
Katika mabustani, na chemchem?

Ayah   26:148   الأية
وَزُرُوعٍ وَنَخْلٍ طَلْعُهَا هَضِيمٌ
Swahili
 
Na konde na mitende yenye makole yaliyo wiva.

Ayah   26:149   الأية
وَتَنْحِتُونَ مِنَ الْجِبَالِ بُيُوتًا فَارِهِينَ
Swahili
 
Na mnachonga milimani majumba kwa ustadi.

Ayah   26:150   الأية
فَاتَّقُوا اللَّهَ وَأَطِيعُونِ
Swahili
 
Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini mimi.

Ayah   26:151   الأية
وَلَا تُطِيعُوا أَمْرَ الْمُسْرِفِينَ
Swahili
 
Wala msit'ii amri za walio pindukia mipaka,

Ayah   26:152   الأية
الَّذِينَ يُفْسِدُونَ فِي الْأَرْضِ وَلَا يُصْلِحُونَ
Swahili
 
Ambao wanafanya ufisadi katika nchi, wala hawatengenezi.

Ayah   26:153   الأية
قَالُوا إِنَّمَا أَنتَ مِنَ الْمُسَحَّرِينَ
Swahili
 
Wakasema: Hakika wewe ni miongoni mwa walio rogwa.

Ayah   26:154   الأية
مَا أَنتَ إِلَّا بَشَرٌ مِّثْلُنَا فَأْتِ بِآيَةٍ إِن كُنتَ مِنَ الصَّادِقِينَ
Swahili
 
Wewe si chochote ila ni mtu kama sisi. Basi lete Ishara ukiwa wewe ni miongoni mwa wasemao kweli.

Ayah   26:155   الأية
قَالَ هَٰذِهِ نَاقَةٌ لَّهَا شِرْبٌ وَلَكُمْ شِرْبُ يَوْمٍ مَّعْلُومٍ
Swahili
 
Akasema: Huyu ngamia jike; awe na zamu yake ya kunywa, na nyinyi muwe na zamu yenu ya kunywa katika siku maalumu.

Ayah   26:156   الأية
وَلَا تَمَسُّوهَا بِسُوءٍ فَيَأْخُذَكُمْ عَذَابُ يَوْمٍ عَظِيمٍ
Swahili
 
Wala msimguse kwa uwovu, isije ikakushikeni adhabu ya Siku Kubwa.

Ayah   26:157   الأية
فَعَقَرُوهَا فَأَصْبَحُوا نَادِمِينَ
Swahili
 
Lakini wakamuuwa, na wakawa wenye kujuta.

Ayah   26:158   الأية
فَأَخَذَهُمُ الْعَذَابُ ۗ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَةً ۖ وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ
Swahili
 
Basi ikawapata adhabu. Hakika katika hayo ipo Ishara. Lakini hawakuwa wengi wao wenye kuamini.

Ayah   26:159   الأية
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ الْعَزِيزُ الرَّحِيمُ
Swahili
 
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.

Ayah   26:160   الأية
كَذَّبَتْ قَوْمُ لُوطٍ الْمُرْسَلِينَ
Swahili
 
Watu wa Lut'i waliwakanusha Mitume.

Ayah   26:161   الأية
إِذْ قَالَ لَهُمْ أَخُوهُمْ لُوطٌ أَلَا تَتَّقُونَ
Swahili
 
Alipo waambia ndugu yao, Lut'i: Je! Hamumchimngu?

Ayah   26:162   الأية
إِنِّي لَكُمْ رَسُولٌ أَمِينٌ
Swahili
 
Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu kwenu.

Ayah   26:163   الأية
فَاتَّقُوا اللَّهَ وَأَطِيعُونِ
Swahili
 
Basi mcheni Mwenyezi Mungu na nit'iini mimi.

Ayah   26:164   الأية
وَمَا أَسْأَلُكُمْ عَلَيْهِ مِنْ أَجْرٍ ۖ إِنْ أَجْرِيَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ الْعَالَمِينَ
Swahili
 
Wala mimi sikutakini ujira juu yake; ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.

Ayah   26:165   الأية
أَتَأْتُونَ الذُّكْرَانَ مِنَ الْعَالَمِينَ
Swahili
 
Je! Katika viumbe vyote mnawaingilia wanaume?

Ayah   26:166   الأية
وَتَذَرُونَ مَا خَلَقَ لَكُمْ رَبُّكُم مِّنْ أَزْوَاجِكُم ۚ بَلْ أَنتُمْ قَوْمٌ عَادُونَ
Swahili
 
Na mnaacha alicho kuumbieni Mola wenu Mlezi katika wake zenu? Ama kweli nyinyi ni watu mnao ruka mipaka!

Ayah   26:167   الأية
قَالُوا لَئِن لَّمْ تَنتَهِ يَا لُوطُ لَتَكُونَنَّ مِنَ الْمُخْرَجِينَ
Swahili
 
Wakasema: Ewe Lut'i! Usipo acha, hapana shaka utakuwa miongoni mwa wanao tolewa mji!

Ayah   26:168   الأية
قَالَ إِنِّي لِعَمَلِكُم مِّنَ الْقَالِينَ
Swahili
 
Akasema: Hakika mimi ni katika wanao kichukia hichi kitendo chenu.

Ayah   26:169   الأية
رَبِّ نَجِّنِي وَأَهْلِي مِمَّا يَعْمَلُونَ
Swahili
 
Mola wangu Mlezi! Niokoe mimi na ahali zangu na haya wayatendayo.

Ayah   26:170   الأية
فَنَجَّيْنَاهُ وَأَهْلَهُ أَجْمَعِينَ
Swahili
 
Basi tukamwokoa yeye na ahali zake wote,

Ayah   26:171   الأية
إِلَّا عَجُوزًا فِي الْغَابِرِينَ
Swahili
 
Isipo kuwa kikongwe katika walio kaa nyuma.

Ayah   26:172   الأية
ثُمَّ دَمَّرْنَا الْآخَرِينَ
Swahili
 
Kisha tukawaangamiza wale wengine.

Ayah   26:173   الأية
وَأَمْطَرْنَا عَلَيْهِم مَّطَرًا ۖ فَسَاءَ مَطَرُ الْمُنذَرِينَ
Swahili
 
Na tukawanyeshea mvua, basi ni ovu mno mvua ya waliyo onywa.

Ayah   26:174   الأية
إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَةً ۖ وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ
Swahili
 
Hakika katika hayo ipo Ishara. Na hawakuwa wengi wao wenye kuamini.

Ayah   26:175   الأية
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ الْعَزِيزُ الرَّحِيمُ
Swahili
 
Na hakika Mola wako Mlezi bila ya shaka ndiye Mwenye nguvu, Mwenye kurehemu.

Ayah   26:176   الأية
كَذَّبَ أَصْحَابُ الْأَيْكَةِ الْمُرْسَلِينَ
Swahili
 
Watu wa Machakani waliwakanusha Mitume.

Ayah   26:177   الأية
إِذْ قَالَ لَهُمْ شُعَيْبٌ أَلَا تَتَّقُونَ
Swahili
 
Shuaibu alipo waambia: Je! Hamfanyi mkamchamngu?

Ayah   26:178   الأية
إِنِّي لَكُمْ رَسُولٌ أَمِينٌ
Swahili
 
Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu.

Ayah   26:179   الأية
فَاتَّقُوا اللَّهَ وَأَطِيعُونِ
Swahili
 
Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini mimi.

Ayah   26:180   الأية
وَمَا أَسْأَلُكُمْ عَلَيْهِ مِنْ أَجْرٍ ۖ إِنْ أَجْرِيَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ الْعَالَمِينَ
Swahili
 
Wala sikutakini ujira juu yake. Ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.

Ayah   26:181   الأية
أَوْفُوا الْكَيْلَ وَلَا تَكُونُوا مِنَ الْمُخْسِرِينَ
Swahili
 
Timizeni kipimo sawa sawa, wala msiwe katika wanao punja.

Ayah   26:182   الأية
وَزِنُوا بِالْقِسْطَاسِ الْمُسْتَقِيمِ
Swahili
 
Na pimeni kwa haki iliyo nyooka;

Ayah   26:183   الأية
وَلَا تَبْخَسُوا النَّاسَ أَشْيَاءَهُمْ وَلَا تَعْثَوْا فِي الْأَرْضِ مُفْسِدِينَ
Swahili
 
Wala msiwapunje watu vitu vyao, wala msifanye jeuri kwa ufisadi.

Ayah   26:184   الأية
وَاتَّقُوا الَّذِي خَلَقَكُمْ وَالْجِبِلَّةَ الْأَوَّلِينَ
Swahili
 
Na mcheni aliye kuumbeni nyinyi na vizazi vilivyo tangulia.

Ayah   26:185   الأية
قَالُوا إِنَّمَا أَنتَ مِنَ الْمُسَحَّرِينَ
Swahili
 
Wakasema: Hakika wewe ni katika walio rogwa.

Ayah   26:186   الأية
وَمَا أَنتَ إِلَّا بَشَرٌ مِّثْلُنَا وَإِن نَّظُنُّكَ لَمِنَ الْكَاذِبِينَ
Swahili
 
Na wewe si chochote ila ni mtu tu kama sisi, na kwa yakini tunakuona wewe ni katika waongo.

Ayah   26:187   الأية
فَأَسْقِطْ عَلَيْنَا كِسَفًا مِّنَ السَّمَاءِ إِن كُنتَ مِنَ الصَّادِقِينَ
Swahili
 
Hebu tuangushie vipande kutoka mbinguni ikiwa wewe ni miongoni mwa wasemao kweli.

Ayah   26:188   الأية
قَالَ رَبِّي أَعْلَمُ بِمَا تَعْمَلُونَ
Swahili
 
Akasema: Mola wangu Mlezi anajua zaidi mnayo yatenda.

Ayah   26:189   الأية
فَكَذَّبُوهُ فَأَخَذَهُمْ عَذَابُ يَوْمِ الظُّلَّةِ ۚ إِنَّهُ كَانَ عَذَابَ يَوْمٍ عَظِيمٍ
Swahili
 
Basi walimkanusha, na ikawashika adhabu ya siku ya kivuli. Hakika hiyo ilikuwa adhabu ya siku kubwa.

Ayah   26:190   الأية
إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَةً ۖ وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ
Swahili
 
Hakika katika hayo ipo Ishara, lakini hawakuwa wengi wao wenye kuamini.

Ayah   26:191   الأية
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ الْعَزِيزُ الرَّحِيمُ
Swahili
 
Na hakika Mola wako Mlezi bila ya shaka ndiye Yeye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.

Ayah   26:192   الأية
وَإِنَّهُ لَتَنزِيلُ رَبِّ الْعَالَمِينَ
Swahili
 
Na bila ya shaka hii ni Uteremsho wa Mola Mlezi wa walimwengu wote.

Ayah   26:193   الأية
نَزَلَ بِهِ الرُّوحُ الْأَمِينُ
Swahili
 
Ameuteremsha Roho muaminifu,

Ayah   26:194   الأية
عَلَىٰ قَلْبِكَ لِتَكُونَ مِنَ الْمُنذِرِينَ
Swahili
 
Juu ya moyo wako, ili uwe katika Waonyaji,

Ayah   26:195   الأية
بِلِسَانٍ عَرَبِيٍّ مُّبِينٍ
Swahili
 
Kwa ulimi wa Kiarabu ulio wazi.

Ayah   26:196   الأية
وَإِنَّهُ لَفِي زُبُرِ الْأَوَّلِينَ
Swahili
 
Na hakika bila ya shaka haya yamo katika Vitabu vya kale.

Ayah   26:197   الأية
أَوَلَمْ يَكُن لَّهُمْ آيَةً أَن يَعْلَمَهُ عُلَمَاءُ بَنِي إِسْرَائِيلَ
Swahili
 
Je! Haikuwa kwao ni Ishara kwamba wanayajua haya wanazuoni wa Wana wa Israili?

Ayah   26:198   الأية
وَلَوْ نَزَّلْنَاهُ عَلَىٰ بَعْضِ الْأَعْجَمِينَ
Swahili
 
Na lau kuwa tungeli iteremsha juu ya mmoja wa wasio kuwa Waarabu,

Ayah   26:199   الأية
فَقَرَأَهُ عَلَيْهِم مَّا كَانُوا بِهِ مُؤْمِنِينَ
Swahili
 
Na akawasomea, wasingeli kuwa wenye kuamini.

Ayah   26:200   الأية
كَذَٰلِكَ سَلَكْنَاهُ فِي قُلُوبِ الْمُجْرِمِينَ
Swahili
 
Namna hivi tunaingiza katika nyoyo za wakosefu.

Ayah   26:201   الأية
لَا يُؤْمِنُونَ بِهِ حَتَّىٰ يَرَوُا الْعَذَابَ الْأَلِيمَ
Swahili
 
Hawataiamini mpaka waione adhabu chungu.

Ayah   26:202   الأية
فَيَأْتِيَهُم بَغْتَةً وَهُمْ لَا يَشْعُرُونَ
Swahili
 
Basi itawafikia kwa ghafla, na hali hawana khabari.

Ayah   26:203   الأية
فَيَقُولُوا هَلْ نَحْنُ مُنظَرُونَ
Swahili
 
Na watasema: Je, tutapewa muhula?

Ayah   26:204   الأية
أَفَبِعَذَابِنَا يَسْتَعْجِلُونَ
Swahili
 
Basi, je, wanaihimiza adhabu yetu?

Ayah   26:205   الأية
أَفَرَأَيْتَ إِن مَّتَّعْنَاهُمْ سِنِينَ
Swahili
 
Waonaje kama tukiwastarehesha kwa miaka,

Ayah   26:206   الأية
ثُمَّ جَاءَهُم مَّا كَانُوا يُوعَدُونَ
Swahili
 
Kisha yakawafikia waliyo kuwa wakiahidiwa,

Ayah   26:207   الأية
مَا أَغْنَىٰ عَنْهُم مَّا كَانُوا يُمَتَّعُونَ
Swahili
 
Yatawafaa nini yale waliyo stareheshewa?

Ayah   26:208   الأية
وَمَا أَهْلَكْنَا مِن قَرْيَةٍ إِلَّا لَهَا مُنذِرُونَ
Swahili
 
Wala hatukuangamiza mji wo wote ila ulikuwa na waonyaji -

Ayah   26:209   الأية
ذِكْرَىٰ وَمَا كُنَّا ظَالِمِينَ
Swahili
 
Kuwa ni ukumbusho. Wala Sisi hatukuwa wenye kudhulumu.

Ayah   26:210   الأية
وَمَا تَنَزَّلَتْ بِهِ الشَّيَاطِينُ
Swahili
 
Wala Mashet'ani hawakuteremka nayo,

Ayah   26:211   الأية
وَمَا يَنبَغِي لَهُمْ وَمَا يَسْتَطِيعُونَ
Swahili
 
Wala haitakiwi kwao, na wala hawawezi.

Ayah   26:212   الأية
إِنَّهُمْ عَنِ السَّمْعِ لَمَعْزُولُونَ
Swahili
 
Hakika hao wametengwa na kusikia.

Ayah   26:213   الأية
فَلَا تَدْعُ مَعَ اللَّهِ إِلَٰهًا آخَرَ فَتَكُونَ مِنَ الْمُعَذَّبِينَ
Swahili
 
Basi usimwombe mungu mwingine pamoja na Mwenyezi Mungu ukawa miongoni mwa watakao adhibiwa.

Ayah   26:214   الأية
وَأَنذِرْ عَشِيرَتَكَ الْأَقْرَبِينَ
Swahili
 
Na uwaonye jamaa zako walio karibu nawe.

Ayah   26:215   الأية
وَاخْفِضْ جَنَاحَكَ لِمَنِ اتَّبَعَكَ مِنَ الْمُؤْمِنِينَ
Swahili
 
Na watwae kwa upole wanao kufuata miongoni mwa Waumini.

Ayah   26:216   الأية
فَإِنْ عَصَوْكَ فَقُلْ إِنِّي بَرِيءٌ مِّمَّا تَعْمَلُونَ
Swahili
 
Na ikiwa watakuasi basi sema: Mimi najitenga mbali na hayo mnayo yatenda.

Ayah   26:217   الأية
وَتَوَكَّلْ عَلَى الْعَزِيزِ الرَّحِيمِ
Swahili
 
Na umtegemee Mtukufu Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.

Ayah   26:218   الأية
الَّذِي يَرَاكَ حِينَ تَقُومُ
Swahili
 
Ambaye anakuona unapo simama,

Ayah   26:219   الأية
وَتَقَلُّبَكَ فِي السَّاجِدِينَ
Swahili
 
Na mageuko yako kati ya wanao sujudu.

Ayah   26:220   الأية
إِنَّهُ هُوَ السَّمِيعُ الْعَلِيمُ
Swahili
 
Hakika Yeye ndiye Mwenye kusikia Mwenye kujua.

Ayah   26:221   الأية
هَلْ أُنَبِّئُكُمْ عَلَىٰ مَن تَنَزَّلُ الشَّيَاطِينُ
Swahili
 
Je! Nikwambieni nani wanawashukia Mashet'ani?

Ayah   26:222   الأية
تَنَزَّلُ عَلَىٰ كُلِّ أَفَّاكٍ أَثِيمٍ
Swahili
 
Wanamshukia kila mzushi mkubwa mwingi wa dhambi.

Ayah   26:223   الأية
يُلْقُونَ السَّمْعَ وَأَكْثَرُهُمْ كَاذِبُونَ
Swahili
 
Wanawapelekea yale wanayo yasikia; na wengi wao ni waongo.

Ayah   26:224   الأية
وَالشُّعَرَاءُ يَتَّبِعُهُمُ الْغَاوُونَ
Swahili
 
Na watungaji mashairi ni wapotofu ndio wanawafuata.

Ayah   26:225   الأية
أَلَمْ تَرَ أَنَّهُمْ فِي كُلِّ وَادٍ يَهِيمُونَ
Swahili
 
Je! Huwaoni kwamba wao wanatangatanga katika kila bonde?

Ayah   26:226   الأية
وَأَنَّهُمْ يَقُولُونَ مَا لَا يَفْعَلُونَ
Swahili
 
Na kwamba wao husema wasiyo yatenda?

Ayah   26:227   الأية
إِلَّا الَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ وَذَكَرُوا اللَّهَ كَثِيرًا وَانتَصَرُوا مِن بَعْدِ مَا ظُلِمُوا ۗ وَسَيَعْلَمُ الَّذِينَ ظَلَمُوا أَيَّ مُنقَلَبٍ يَنقَلِبُونَ
Swahili
 
Isipo kuwa wale walio amini, na wakatenda mema, na wakamkumbuka Mwenyezi Mungu kwa wingi, na wakajitetea wanapo dhulumiwa. Na wanao dhulumu watakuja jua mgeuko gani watakao geuka.
 


© EsinIslam.Com Designed & produced by The Awqaf London. Please pray for us