First Ayah 1 الأية الأوليبِسْم ِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ
طسم
Swahili
T'aa Siin Miim. (T'.S.M.)
|
Ayah 26:2 الأية
تِلْكَ آيَاتُ الْكِتَابِ الْمُبِينِ
Swahili
Hizi ni Aya za Kitabu kinacho bainisha.
|
Ayah 26:3 الأية
لَعَلَّكَ بَاخِعٌ نَّفْسَكَ أَلَّا يَكُونُوا مُؤْمِنِينَ
Swahili
Huenda labda ukajikera nafsi yako kwa kuwa hawawi Waumini.
|
Ayah 26:4 الأية
إِن نَّشَأْ نُنَزِّلْ عَلَيْهِم مِّنَ السَّمَاءِ آيَةً فَظَلَّتْ أَعْنَاقُهُمْ
لَهَا خَاضِعِينَ
Swahili
Tunge penda tungeli wateremshia kutoka mbinguni Ishara zikanyenyekea shingo zao.
|
Ayah 26:5 الأية
وَمَا يَأْتِيهِم مِّن ذِكْرٍ مِّنَ الرَّحْمَٰنِ مُحْدَثٍ إِلَّا كَانُوا عَنْهُ
مُعْرِضِينَ
Swahili
Wala hauwafikii ukumbusho mpya kutoka kwa Arrahman ila wao hujitenga nao.
|
Ayah 26:6 الأية
فَقَدْ كَذَّبُوا فَسَيَأْتِيهِمْ أَنبَاءُ مَا كَانُوا بِهِ يَسْتَهْزِئُونَ
Swahili
Kwa yakini wamekanusha; kwa hivyo zitakuja wafikia khabari za yale waliyo kuwa
wakiyafanyia mzaha.
|
Ayah 26:7 الأية
أَوَلَمْ يَرَوْا إِلَى الْأَرْضِ كَمْ أَنبَتْنَا فِيهَا مِن كُلِّ زَوْجٍ كَرِيمٍ
Swahili
Je! Hawakuiona ardhi, mimea mingapi tumeiotesha humo, ya kila namna nzuri?
|
Ayah 26:8 الأية
إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَةً ۖ وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ
Swahili
Hakika katika haya zipo Ishara. Lakini wengi wao hawakuwa wenye kuamini.
|
Ayah 26:9 الأية
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ الْعَزِيزُ الرَّحِيمُ
Swahili
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Yeye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.
|
Ayah 26:10 الأية
وَإِذْ نَادَىٰ رَبُّكَ مُوسَىٰ أَنِ ائْتِ الْقَوْمَ الظَّالِمِينَ
Swahili
Na Mola wako Mlezi, alipo mwita Musa, akamwambia: Fika kwa watu madhaalimu,
|
Ayah 26:11 الأية
قَوْمَ فِرْعَوْنَ ۚ أَلَا يَتَّقُونَ
Swahili
Watu wa Firauni. Hawaogopi?
|
Ayah 26:12 الأية
قَالَ رَبِّ إِنِّي أَخَافُ أَن يُكَذِّبُونِ
Swahili
Akasema: Hakika mimi nachelea wasinikanushe.
|
Ayah 26:13 الأية
وَيَضِيقُ صَدْرِي وَلَا يَنطَلِقُ لِسَانِي فَأَرْسِلْ إِلَىٰ هَارُونَ
Swahili
Na kifua changu kina dhiki, na ulimi wangu haukunjuki vyema. Basi mtumie ujumbe
Harun.
|
Ayah 26:14 الأية
وَلَهُمْ عَلَيَّ ذَنبٌ فَأَخَافُ أَن يَقْتُلُونِ
Swahili
Na wao wana kisasi juu yangu, kwa hivyo naogopa wasije kuniuwa.
|
Ayah 26:15 الأية
قَالَ كَلَّا ۖ فَاذْهَبَا بِآيَاتِنَا ۖ إِنَّا مَعَكُم مُّسْتَمِعُونَ
Swahili
Akasema: Siyo hivyo kabisa! Nendeni na miujiza yetu. Hakika Sisi tu pamoja
nanyi, tunasikiliza.
|
Ayah 26:16 الأية
فَأْتِيَا فِرْعَوْنَ فَقُولَا إِنَّا رَسُولُ رَبِّ الْعَالَمِينَ
Swahili
Basi mfikieni Firauni na mwambieni: Hakika sisi ni Mitume wa Mola Mlezi wa
walimwengu wote.
|
Ayah 26:17 الأية
أَنْ أَرْسِلْ مَعَنَا بَنِي إِسْرَائِيلَ
Swahili
Waachilie Wana wa Israili wende nasi.
|
Ayah 26:18 الأية
قَالَ أَلَمْ نُرَبِّكَ فِينَا وَلِيدًا وَلَبِثْتَ فِينَا مِنْ عُمُرِكَ سِنِينَ
Swahili
(Firauni) akasema: Sisi hatukukulea wewe utotoni, na ukakaa kwetu katika umri
wako miaka mingi?
|
Ayah 26:19 الأية
وَفَعَلْتَ فَعْلَتَكَ الَّتِي فَعَلْتَ وَأَنتَ مِنَ الْكَافِرِينَ
Swahili
Na ukatenda kitendo chako ulicho tenda, nawe ukawa miongoni mwa wasio na
shukrani?
|
Ayah 26:20 الأية
قَالَ فَعَلْتُهَا إِذًا وَأَنَا مِنَ الضَّالِّينَ
Swahili
(Musa) akasema: Nilitenda hayo hapo nilipo kuwa miongoni mwa wale walio potea.
|
Ayah 26:21 الأية
فَفَرَرْتُ مِنكُمْ لَمَّا خِفْتُكُمْ فَوَهَبَ لِي رَبِّي حُكْمًا وَجَعَلَنِي
مِنَ الْمُرْسَلِينَ
Swahili
Basi nikakukimbieni nilipo kuogopeni, tena Mola wangu Mlezi akanitunukia hukumu,
na akanijaalia niwe miongoni mwa Mitume.
|
Ayah 26:22 الأية
وَتِلْكَ نِعْمَةٌ تَمُنُّهَا عَلَيَّ أَنْ عَبَّدتَّ بَنِي إِسْرَائِيلَ
Swahili
Na hiyo ndiyo neema ya kunisumbulia, na wewe umewatia utumwani Wana wa Israili?
|
Ayah 26:23 الأية
قَالَ فِرْعَوْنُ وَمَا رَبُّ الْعَالَمِينَ
Swahili
Firauni akasema: Na nani huyo Mola Mlezi wa walimwengu wote?
|
Ayah 26:24 الأية
قَالَ رَبُّ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَمَا بَيْنَهُمَا ۖ إِن كُنتُم مُّوقِنِينَ
Swahili
Akasema: Ndiye Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, na viliomo baina yao, ikiwa nyinyi
ni wenye yakini.
|
Ayah 26:25 الأية
قَالَ لِمَنْ حَوْلَهُ أَلَا تَسْتَمِعُونَ
Swahili
(Firauni) akawaambia walio mzunguka: Hamsikilizi?
|
Ayah 26:26 الأية
قَالَ رَبُّكُمْ وَرَبُّ آبَائِكُمُ الْأَوَّلِينَ
Swahili
(Musa) akasema: Ndiye Mola wenu Mlezi, na Mola Mlezi wa baba zenu wa kwanza.
|
Ayah 26:27 الأية
قَالَ إِنَّ رَسُولَكُمُ الَّذِي أُرْسِلَ إِلَيْكُمْ لَمَجْنُونٌ
Swahili
(Firauni) akasema: Hakika huyu Mtume wenu aliye tumwa kwenu ni mwendawazimu.
|
Ayah 26:28 الأية
قَالَ رَبُّ الْمَشْرِقِ وَالْمَغْرِبِ وَمَا بَيْنَهُمَا ۖ إِن كُنتُمْ
تَعْقِلُونَ
Swahili
(Musa) akasema: Ndiye Mola Mlezi wa Mashariki na Magharibi na viliomo baina yao,
ikiwa nyinyi mnatia akilini.
|
Ayah 26:29 الأية
قَالَ لَئِنِ اتَّخَذْتَ إِلَٰهًا غَيْرِي لَأَجْعَلَنَّكَ مِنَ الْمَسْجُونِينَ
Swahili
(Firauni) akasema: Ukimfuata mungu mwengine asiye kuwa mimi, basi bila ya shaka
nitakufunga gerezani.
|
Ayah 26:30 الأية
قَالَ أَوَلَوْ جِئْتُكَ بِشَيْءٍ مُّبِينٍ
Swahili
Akasema: Je! Ijapo kuwa nitakuletea kitu cha kubainisha wazi?
|
Ayah 26:31 الأية
قَالَ فَأْتِ بِهِ إِن كُنتَ مِنَ الصَّادِقِينَ
Swahili
Akasema: Kilete basi, kama wewe ni katika wasemao kweli.
|
Ayah 26:32 الأية
فَأَلْقَىٰ عَصَاهُ فَإِذَا هِيَ ثُعْبَانٌ مُّبِينٌ
Swahili
Basi akaitupa fimbo yake, mara ikawa nyoka wa kuonekana dhaahiri.
|
Ayah 26:33 الأية
وَنَزَعَ يَدَهُ فَإِذَا هِيَ بَيْضَاءُ لِلنَّاظِرِينَ
Swahili
Na akautoa mkono wake, na mara ukawa mweupe kwa watazamao.
|
Ayah 26:34 الأية
قَالَ لِلْمَلَإِ حَوْلَهُ إِنَّ هَٰذَا لَسَاحِرٌ عَلِيمٌ
Swahili
(Firauni) akawaambia waheshimiwa walio mzunguka: Hakika huyu ni mchawi mtaalamu.
|
Ayah 26:35 الأية
يُرِيدُ أَن يُخْرِجَكُم مِّنْ أَرْضِكُم بِسِحْرِهِ فَمَاذَا تَأْمُرُونَ
Swahili
Anataka kukutoeni katika nchi yenu kwa uchawi wake. Basi mna shauri gani?
|
Ayah 26:36 الأية
قَالُوا أَرْجِهْ وَأَخَاهُ وَابْعَثْ فِي الْمَدَائِنِ حَاشِرِينَ
Swahili
Wakasema: Mpe muda yeye na nduguye na uwatume mijini wapigao mbiu ya mgambo.
|
Ayah 26:37 الأية
يَأْتُوكَ بِكُلِّ سَحَّارٍ عَلِيمٍ
Swahili
Wakuletee kila mchawi bingwa mtaalamu.
|
Ayah 26:38 الأية
فَجُمِعَ السَّحَرَةُ لِمِيقَاتِ يَوْمٍ مَّعْلُومٍ
Swahili
Basi wakakusanywa wachawi wakati na siku maalumu.
|
Ayah 26:39 الأية
وَقِيلَ لِلنَّاسِ هَلْ أَنتُم مُّجْتَمِعُونَ
Swahili
Na watu wakaambiwa: Je! Mtakusanyika?
|
Ayah 26:40 الأية
لَعَلَّنَا نَتَّبِعُ السَّحَرَةَ إِن كَانُوا هُمُ الْغَالِبِينَ
Swahili
Huenda tutawafuata wachawi wakiwa wao ndio watakao shinda.
|
Ayah 26:41 الأية
فَلَمَّا جَاءَ السَّحَرَةُ قَالُوا لِفِرْعَوْنَ أَئِنَّ لَنَا لَأَجْرًا إِن
كُنَّا نَحْنُ الْغَالِبِينَ
Swahili
Basi walipo kuja wachawi wakamwambia Firauni: Je! Tutapata ujira tukiwa sisi
ndio tulio shinda?
|
Ayah 26:42 الأية
قَالَ نَعَمْ وَإِنَّكُمْ إِذًا لَّمِنَ الْمُقَرَّبِينَ
Swahili
Naam! Na hakika mtakuwa katika watu wa mbele.
|
Ayah 26:43 الأية
قَالَ لَهُم مُّوسَىٰ أَلْقُوا مَا أَنتُم مُّلْقُونَ
Swahili
Musa akwaambia: Tupeni mnavyo taka kutupa.
|
Ayah 26:44 الأية
فَأَلْقَوْا حِبَالَهُمْ وَعِصِيَّهُمْ وَقَالُوا بِعِزَّةِ فِرْعَوْنَ إِنَّا
لَنَحْنُ الْغَالِبُونَ
Swahili
Basi wakatupa kamba zao na fimbo zao, na wakasema: Kwa nguvu za Firauni hakika
sisi hapana shaka ni wenye kushinda.
|
Ayah 26:45 الأية
فَأَلْقَىٰ مُوسَىٰ عَصَاهُ فَإِذَا هِيَ تَلْقَفُ مَا يَأْفِكُونَ
Swahili
Musa tena akatupa fimbo yake, nayo mara ikavimeza walivyo vizua.
|
Ayah 26:46 الأية
فَأُلْقِيَ السَّحَرَةُ سَاجِدِينَ
Swahili
Hapo wachawi walipinduka wakasujudu.
|
Ayah 26:47 الأية
قَالُوا آمَنَّا بِرَبِّ الْعَالَمِينَ
Swahili
Wakasema: Tunamuamini Mola Mlezi wa walimwengu wote.
|
Ayah 26:48 الأية
رَبِّ مُوسَىٰ وَهَارُونَ
Swahili
Mola Mlezi wa Musa na Harun.
|
Ayah 26:49 الأية
قَالَ آمَنتُمْ لَهُ قَبْلَ أَنْ آذَنَ لَكُمْ ۖ إِنَّهُ لَكَبِيرُكُمُ الَّذِي
عَلَّمَكُمُ السِّحْرَ فَلَسَوْفَ تَعْلَمُونَ ۚ لَأُقَطِّعَنَّ أَيْدِيَكُمْ
وَأَرْجُلَكُم مِّنْ خِلَافٍ وَلَأُصَلِّبَنَّكُمْ أَجْمَعِينَ
Swahili
(Firauni) akasema: Je! Mmemuamini kabla sijakuruhusuni? Bila ya shaka yeye basi
ndiye mkubwa wenu aliye kufunzeni uchawi. Basi mtakuja jua! Nitakata mikono yenu
na miguu yenu kwa kutafautisha. Na nitakubandikeni misalabani nyote.
|
Ayah 26:50 الأية
قَالُوا لَا ضَيْرَ ۖ إِنَّا إِلَىٰ رَبِّنَا مُنقَلِبُونَ
Swahili
Wakasema: Haidhuru, kwani sisi ni wenye kurejea kwa Mola wetu Mlezi.
|
Ayah 26:51 الأية
إِنَّا نَطْمَعُ أَن يَغْفِرَ لَنَا رَبُّنَا خَطَايَانَا أَن كُنَّا أَوَّلَ
الْمُؤْمِنِينَ
Swahili
Hakika sisi tunatumai Mola wetu Mlezi atatusamehe makosa yetu, kwa kuwa ndio wa
kwanza wa kuamini.
|
Ayah 26:52 الأية
وَأَوْحَيْنَا إِلَىٰ مُوسَىٰ أَنْ أَسْرِ بِعِبَادِي إِنَّكُم مُّتَّبَعُونَ
Swahili
Na tulimuamrisha Musa kwa wahyi: Nenda na waja wangu wakati wa usiku. Kwa hakika
mtafuatwa.
|
Ayah 26:53 الأية
فَأَرْسَلَ فِرْعَوْنُ فِي الْمَدَائِنِ حَاشِرِينَ
Swahili
Basi Firauni akawatuma mijini wapiga mbiu za mgambo.
|
Ayah 26:54 الأية
إِنَّ هَٰؤُلَاءِ لَشِرْذِمَةٌ قَلِيلُونَ
Swahili
(Wakieneza): Hakika hawa ni kikundi kidogo.
|
Ayah 26:55 الأية
وَإِنَّهُمْ لَنَا لَغَائِظُونَ
Swahili
Nao wanatuudhi.
|
Ayah 26:56 الأية
وَإِنَّا لَجَمِيعٌ حَاذِرُونَ
Swahili
Na sisi ni wengi, wenye kuchukua hadhari.
|
Ayah 26:57 الأية
فَأَخْرَجْنَاهُم مِّن جَنَّاتٍ وَعُيُونٍ
Swahili
Basi tukawatoa katika mabustani na chemchem,
|
Ayah 26:58 الأية
وَكُنُوزٍ وَمَقَامٍ كَرِيمٍ
Swahili
Na makhazina, na vyeo vya hishima,
|
Ayah 26:59 الأية
كَذَٰلِكَ وَأَوْرَثْنَاهَا بَنِي إِسْرَائِيلَ
Swahili
Kadhaalika; na tukawarithisha hayo Wana wa Israili.
|
Ayah 26:60 الأية
فَأَتْبَعُوهُم مُّشْرِقِينَ
Swahili
Basi wakawafuata lilipo chomoza jua.
|
Ayah 26:61 الأية
فَلَمَّا تَرَاءَى الْجَمْعَانِ قَالَ أَصْحَابُ مُوسَىٰ إِنَّا لَمُدْرَكُونَ
Swahili
Na yalipo onana majeshi mawili haya, watu wa Musa wakasema: Hakika sisi bila ya
shaka tumepatikana!
|
Ayah 26:62 الأية
قَالَ كَلَّا ۖ إِنَّ مَعِيَ رَبِّي سَيَهْدِينِ
Swahili
(Musa) akasema: Hasha! Hakika yu pamoja nami Mola wangu Mlezi. Yeye ataniongoa!
|
Ayah 26:63 الأية
فَأَوْحَيْنَا إِلَىٰ مُوسَىٰ أَنِ اضْرِب بِّعَصَاكَ الْبَحْرَ ۖ فَانفَلَقَ
فَكَانَ كُلُّ فِرْقٍ كَالطَّوْدِ الْعَظِيمِ
Swahili
Tulimletea wahyi Musa tukamwambia: Piga bahari kwa fimbo yako. Basi ikatengana,
na kila sehemu ikawa kama mlima mkubwa.
|
Ayah 26:64 الأية
وَأَزْلَفْنَا ثَمَّ الْآخَرِينَ
Swahili
Na tukawajongeza hapo wale wengine.
|
Ayah 26:65 الأية
وَأَنجَيْنَا مُوسَىٰ وَمَن مَّعَهُ أَجْمَعِينَ
Swahili
Tukawaokoa Musa na walio kuwa pamoja naye wote.
|
Ayah 26:66 الأية
ثُمَّ أَغْرَقْنَا الْآخَرِينَ
Swahili
Kisha tukawazamisha hao wengine.
|
Ayah 26:67 الأية
إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَةً ۖ وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ
Swahili
Hakika bila ya shaka katika hayo ipo Ishara; lakini wengi wao si katika wenye
kuamini.
|
Ayah 26:68 الأية
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ الْعَزِيزُ الرَّحِيمُ
Swahili
Na kwa hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.
|
Ayah 26:69 الأية
وَاتْلُ عَلَيْهِمْ نَبَأَ إِبْرَاهِيمَ
Swahili
Na wasomee khabari za Ibrahim.
|
Ayah 26:70 الأية
إِذْ قَالَ لِأَبِيهِ وَقَوْمِهِ مَا تَعْبُدُونَ
Swahili
Alipo mwambia baba yake na kaumu yake: Mnaabudu nini?
|
Ayah 26:71 الأية
قَالُوا نَعْبُدُ أَصْنَامًا فَنَظَلُّ لَهَا عَاكِفِينَ
Swahili
Wakasema: Tunaabudu masanamu, daima tunayanyenyekea.
|
Ayah 26:72 الأية
قَالَ هَلْ يَسْمَعُونَكُمْ إِذْ تَدْعُونَ
Swahili
Akasema: Je! Yanakusikieni mnapo yaita?
|
Ayah 26:73 الأية
أَوْ يَنفَعُونَكُمْ أَوْ يَضُرُّونَ
Swahili
Au yanakufaeni, au yanakudhuruni?
|
Ayah 26:74 الأية
قَالُوا بَلْ وَجَدْنَا آبَاءَنَا كَذَٰلِكَ يَفْعَلُونَ
Swahili
Wakasema: Bali tumewakuta baba zetu wakifanya hivyo hivyo.
|
Ayah 26:75 الأية
قَالَ أَفَرَأَيْتُم مَّا كُنتُمْ تَعْبُدُونَ
Swahili
Je! Mmewaona hawa mnao waabudu-
|
Ayah 26:76 الأية
أَنتُمْ وَآبَاؤُكُمُ الْأَقْدَمُونَ
Swahili
Nyinyi na baba zenu wa zamani?
|
Ayah 26:77 الأية
فَإِنَّهُمْ عَدُوٌّ لِّي إِلَّا رَبَّ الْعَالَمِينَ
Swahili
Kwani hakika hao ni adui zangu, isipo kuwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
|
Ayah 26:78 الأية
الَّذِي خَلَقَنِي فَهُوَ يَهْدِينِ
Swahili
Ambaye ndiye aliye niumba, na Yeye ndiye ananiongoa,
|
Ayah 26:79 الأية
وَالَّذِي هُوَ يُطْعِمُنِي وَيَسْقِينِ
Swahili
Na ambaye ndiye ananilisha na kuninywesha.
|
Ayah 26:80 الأية
وَإِذَا مَرِضْتُ فَهُوَ يَشْفِينِ
Swahili
Na ninapo ugua ni Yeye ndiye anaye niponesha.
|
Ayah 26:81 الأية
وَالَّذِي يُمِيتُنِي ثُمَّ يُحْيِينِ
Swahili
Na ambaye atanifisha, na kisha atanihuisha.
|
Ayah 26:82 الأية
وَالَّذِي أَطْمَعُ أَن يَغْفِرَ لِي خَطِيئَتِي يَوْمَ الدِّينِ
Swahili
Na ambaye ndiye ninaye mtumai kunisamehe makosa yangu Siku ya Malipo.
|
Ayah 26:83 الأية
رَبِّ هَبْ لِي حُكْمًا وَأَلْحِقْنِي بِالصَّالِحِينَ
Swahili
Mola wangu Mlezi! Nitunukie hukumu na uniunganishe na watendao mema.
|
Ayah 26:84 الأية
وَاجْعَل لِّي لِسَانَ صِدْقٍ فِي الْآخِرِينَ
Swahili
Na unijaalie nitajwe kwa wema na watu watakao kuja baadaye.
|
Ayah 26:85 الأية
وَاجْعَلْنِي مِن وَرَثَةِ جَنَّةِ النَّعِيمِ
Swahili
Na unijaalie katika warithi wa Bustani za neema.
|
Ayah 26:86 الأية
وَاغْفِرْ لِأَبِي إِنَّهُ كَانَ مِنَ الضَّالِّينَ
Swahili
Na umsamehe baba yangu, kwani hakika alikuwa miongoni mwa wapotovu.
|
Ayah 26:87 الأية
وَلَا تُخْزِنِي يَوْمَ يُبْعَثُونَ
Swahili
Wala usinihizi Siku watapo fufuliwa.
|
Ayah 26:88 الأية
يَوْمَ لَا يَنفَعُ مَالٌ وَلَا بَنُونَ
Swahili
Siku ambayo kwamba mali hayato faa kitu wala wana.
|
Ayah 26:89 الأية
إِلَّا مَنْ أَتَى اللَّهَ بِقَلْبٍ سَلِيمٍ
Swahili
Isipo kuwa mwenye kumjia Mwenyezi Mungu na moyo safi.
|
Ayah 26:90 الأية
وَأُزْلِفَتِ الْجَنَّةُ لِلْمُتَّقِينَ
Swahili
Na Pepo itasogezwa kwa wachamngu.
|
Ayah 26:91 الأية
وَبُرِّزَتِ الْجَحِيمُ لِلْغَاوِينَ
Swahili
Na Jahannamu itadhihirishwa kwa wapotovu.
|
Ayah 26:92 الأية
وَقِيلَ لَهُمْ أَيْنَ مَا كُنتُمْ تَعْبُدُونَ
Swahili
Na wataambiwa: Wako wapi mlio kuwa mkiwaabudu
|
Ayah 26:93 الأية
مِن دُونِ اللَّهِ هَلْ يَنصُرُونَكُمْ أَوْ يَنتَصِرُونَ
Swahili
Badala ya Mwenyezi Mungu? Je! Wanakusaidieni, au wanajisaidia wenyewe?
|
Ayah 26:94 الأية
فَكُبْكِبُوا فِيهَا هُمْ وَالْغَاوُونَ
Swahili
Basi watavurumizwa humo wao na hao wakosefu,
|
Ayah 26:95 الأية
وَجُنُودُ إِبْلِيسَ أَجْمَعُونَ
Swahili
Na majeshi ya Ibilisi yote.
|
Ayah 26:96 الأية
قَالُوا وَهُمْ فِيهَا يَخْتَصِمُونَ
Swahili
Watasema, na hali ya kuwa wanazozana humo:
|
Ayah 26:97 الأية
تَاللَّهِ إِن كُنَّا لَفِي ضَلَالٍ مُّبِينٍ
Swahili
Wallahi! Kwa yakini tulikuwa katika upotovu ulio dhaahiri,
|
Ayah 26:98 الأية
إِذْ نُسَوِّيكُم بِرَبِّ الْعَالَمِينَ
Swahili
Tulipo kufanyeni ni sawa na Mola Mlezi wa walimwengu wote.
|
Ayah 26:99 الأية
وَمَا أَضَلَّنَا إِلَّا الْمُجْرِمُونَ
Swahili
Na hawakutupoteza ila wale wakosefu.
|
Ayah 26:100 الأية
فَمَا لَنَا مِن شَافِعِينَ
Swahili
Basi hatuna waombezi.
|
Ayah 26:101 الأية
وَلَا صَدِيقٍ حَمِيمٍ
Swahili
Wala rafiki wa dhati.
|
Ayah 26:102 الأية
فَلَوْ أَنَّ لَنَا كَرَّةً فَنَكُونَ مِنَ الْمُؤْمِنِينَ
Swahili
Laiti tungeli pata kurejea tena tungeli kuwa katika Waumini.
|
Ayah 26:103 الأية
إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَةً ۖ وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ
Swahili
Hakika katika haya ipo Ishara, lakini wengi wao hawakuwa wenye kuamini.
|
Ayah 26:104 الأية
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ الْعَزِيزُ الرَّحِيمُ
Swahili
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.
|
Ayah 26:105 الأية
كَذَّبَتْ قَوْمُ نُوحٍ الْمُرْسَلِينَ
Swahili
Kaumu ya Nuhu waliwakadhibisha Mitume.
|
Ayah 26:106 الأية
إِذْ قَالَ لَهُمْ أَخُوهُمْ نُوحٌ أَلَا تَتَّقُونَ
Swahili
Alipo waambia ndugu yao, Nuhu: Je! Hamchimngu?
|
Ayah 26:107 الأية
إِنِّي لَكُمْ رَسُولٌ أَمِينٌ
Swahili
Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu.
|
Ayah 26:108 الأية
فَاتَّقُوا اللَّهَ وَأَطِيعُونِ
Swahili
Basi Mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini mimi.
|
Ayah 26:109 الأية
وَمَا أَسْأَلُكُمْ عَلَيْهِ مِنْ أَجْرٍ ۖ إِنْ أَجْرِيَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ
الْعَالَمِينَ
Swahili
Na sikutakini juu yake ujira, kwani ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa
walimwengu wote.
|
Ayah 26:110 الأية
فَاتَّقُوا اللَّهَ وَأَطِيعُونِ
Swahili
Basi Mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini mimi.
|
Ayah 26:111 الأية
قَالُوا أَنُؤْمِنُ لَكَ وَاتَّبَعَكَ الْأَرْذَلُونَ
Swahili
Wakasema: Je! Tukuamini wewe, hali wanao kufuata ni watu wa chini?
|
Ayah 26:112 الأية
قَالَ وَمَا عِلْمِي بِمَا كَانُوا يَعْمَلُونَ
Swahili
Akasema: Nayajuaje waliyo kuwa wakiyafanya?
|
Ayah 26:113 الأية
إِنْ حِسَابُهُمْ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّي ۖ لَوْ تَشْعُرُونَ
Swahili
Hisabu yao haiko ila kwa Mola wao Mlezi, laiti mngeli tambua!
|
Ayah 26:114 الأية
وَمَا أَنَا بِطَارِدِ الْمُؤْمِنِينَ
Swahili
Wala mimi si wa kuwafukuza Waumini.
|
Ayah 26:115 الأية
إِنْ أَنَا إِلَّا نَذِيرٌ مُّبِينٌ
Swahili
Mimi si cho chote ila ni Mwonyaji wa dhaahiri shaahiri.
|
Ayah 26:116 الأية
قَالُوا لَئِن لَّمْ تَنتَهِ يَا نُوحُ لَتَكُونَنَّ مِنَ الْمَرْجُومِينَ
Swahili
Wakasema: Ikiwa huachi, ewe Nuhu, bila ya shaka utapigwa mawe.
|
Ayah 26:117 الأية
قَالَ رَبِّ إِنَّ قَوْمِي كَذَّبُونِ
Swahili
Akasema: Mola wangu Mlezi! Hakika watu wangu wamenikanusha.
|
|