First Ayah 1 الأية الأوليبِسْم ِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ
الم
Swahili
Alif Lam Mim (A.L.M.)
|
Ayah 29:2 الأية
أَحَسِبَ النَّاسُ أَن يُتْرَكُوا أَن يَقُولُوا آمَنَّا وَهُمْ لَا يُفْتَنُونَ
Swahili
Je! Wanadhani watu wataachwa kwa kuwa wanasema: Tumeamini. Nao wasijaribiwe?
|
Ayah 29:3 الأية
وَلَقَدْ فَتَنَّا الَّذِينَ مِن قَبْلِهِمْ ۖ فَلَيَعْلَمَنَّ اللَّهُ الَّذِينَ
صَدَقُوا وَلَيَعْلَمَنَّ الْكَاذِبِينَ
Swahili
Hakika tuliwajaribu walio kuwa kabla yao, na kwa yakini Mwenyezi Mungu
atawatambulisha walio wa kweli na atawatambulisha walio waongo.
|
Ayah 29:4 الأية
أَمْ حَسِبَ الَّذِينَ يَعْمَلُونَ السَّيِّئَاتِ أَن يَسْبِقُونَا ۚ سَاءَ مَا
يَحْكُمُونَ
Swahili
Au wanadhani wanao tenda maovu kwamba watatushinda? Hukumu mbaya hiyo wanayo
hukumu.
|
Ayah 29:5 الأية
مَن كَانَ يَرْجُو لِقَاءَ اللَّهِ فَإِنَّ أَجَلَ اللَّهِ لَآتٍ ۚ وَهُوَ
السَّمِيعُ الْعَلِيمُ
Swahili
Mwenye kutaraji kukutana na Mwenyezi Mungu, basi hakika miadi ya Mwenyezi Mungu
itafika bila ya shaka. Naye ni Mwenye kusikia, Mwenye kujua.
|
Ayah 29:6 الأية
وَمَن جَاهَدَ فَإِنَّمَا يُجَاهِدُ لِنَفْسِهِ ۚ إِنَّ اللَّهَ لَغَنِيٌّ عَنِ
الْعَالَمِينَ
Swahili
Na anaye fanya juhudi basi bila ya shaka anafanya juhudi kwa ajili ya nafsi
yake. Hakika Mwenyezi Mungu si mhitaji wa walimwengu.
|
Ayah 29:7 الأية
وَالَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ لَنُكَفِّرَنَّ عَنْهُمْ
سَيِّئَاتِهِمْ وَلَنَجْزِيَنَّهُمْ أَحْسَنَ الَّذِي كَانُوا يَعْمَلُونَ
Swahili
Na walio amini na wakatenda mema, kwa yakini tutawafutia makosa yao, na
tutawalipa bora ya waliyo kuwa wakiyatenda.
|
Ayah 29:8 الأية
وَوَصَّيْنَا الْإِنسَانَ بِوَالِدَيْهِ حُسْنًا ۖ وَإِن جَاهَدَاكَ لِتُشْرِكَ بِي
مَا لَيْسَ لَكَ بِهِ عِلْمٌ فَلَا تُطِعْهُمَا ۚ إِلَيَّ مَرْجِعُكُمْ
فَأُنَبِّئُكُم بِمَا كُنتُمْ تَعْمَلُونَ
Swahili
Na tumemuusia mwanaadamu kuwafanyia wema wazazi wake. Na ikiwa watakushikilia
unishirikishe Mimi na usiyo kuwa na ujuzi nayo, basi usiwat'ii. Kwangu Mimi ndio
marejeo yenu, na nitakwambieni mliyo kuwa mkiyatenda.
|
Ayah 29:9 الأية
وَالَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ لَنُدْخِلَنَّهُمْ فِي الصَّالِحِينَ
Swahili
Na walio amini na wakatenda mema, bila ya shaka tutawatia miongoni mwa watu
wema.
|
Ayah 29:10 الأية
وَمِنَ النَّاسِ مَن يَقُولُ آمَنَّا بِاللَّهِ فَإِذَا أُوذِيَ فِي اللَّهِ جَعَلَ
فِتْنَةَ النَّاسِ كَعَذَابِ اللَّهِ وَلَئِن جَاءَ نَصْرٌ مِّن رَّبِّكَ
لَيَقُولُنَّ إِنَّا كُنَّا مَعَكُمْ ۚ أَوَلَيْسَ اللَّهُ بِأَعْلَمَ بِمَا فِي
صُدُورِ الْعَالَمِينَ
Swahili
Na katika watu wapo wanao sema: Tumemuamini Mwenyezi Mungu. Lakini wanapo pewa
maudhi kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, wanayafanya mateso ya watu kama ni adhabu ya
Mwenyezi Mungu. Na inapo kuja nusura kutoka kwa Mola wako Mlezi husema: Hakika
sisi tulikuwa pamoja nanyi. Kwani Mwenyezi Mungu hayajui yaliomo vifuani mwa
walimwengu?
|
Ayah 29:11 الأية
وَلَيَعْلَمَنَّ اللَّهُ الَّذِينَ آمَنُوا وَلَيَعْلَمَنَّ الْمُنَافِقِينَ
Swahili
Na hapana shaka Mwenyezi Mungu atawatambulisha walio amini, na atawatambulisha
wanaafiki.
|
Ayah 29:12 الأية
وَقَالَ الَّذِينَ كَفَرُوا لِلَّذِينَ آمَنُوا اتَّبِعُوا سَبِيلَنَا وَلْنَحْمِلْ
خَطَايَاكُمْ وَمَا هُم بِحَامِلِينَ مِنْ خَطَايَاهُم مِّن شَيْءٍ ۖ إِنَّهُمْ
لَكَاذِبُونَ
Swahili
Na walio kufuru waliwaambia walio amini: Fuateni njia yetu, nasi tutayabeba
makosa yenu. Wala wao hawatabeba katika makosa yao chochote kile. Hakika hao ni
waongo.
|
Ayah 29:13 الأية
وَلَيَحْمِلُنَّ أَثْقَالَهُمْ وَأَثْقَالًا مَّعَ أَثْقَالِهِمْ ۖ وَلَيُسْأَلُنَّ
يَوْمَ الْقِيَامَةِ عَمَّا كَانُوا يَفْتَرُونَ
Swahili
Na hapana shaka wataibeba mizigo yao na mizigo mingine pamoja na mizigo yao. Na
kwa yakini wataulizwa Siku ya Kiyama juu ya waliyo kuwa wakiyazua.
|
Ayah 29:14 الأية
وَلَقَدْ أَرْسَلْنَا نُوحًا إِلَىٰ قَوْمِهِ فَلَبِثَ فِيهِمْ أَلْفَ سَنَةٍ
إِلَّا خَمْسِينَ عَامًا فَأَخَذَهُمُ الطُّوفَانُ وَهُمْ ظَالِمُونَ
Swahili
Na hakika tulimtuma Nuhu kwa watu wake, na akakaa nao miaka elfu kasoro miaka
khamsini. Basi tufani liliwachukua, nao ni madhaalimu.
|
Ayah 29:15 الأية
فَأَنجَيْنَاهُ وَأَصْحَابَ السَّفِينَةِ وَجَعَلْنَاهَا آيَةً لِّلْعَالَمِينَ
Swahili
Nasi tukamwokoa yeye na wenziwe wa katika safina, na tukaifanya kuwa ni Ishara
kwa walimwengu wote.
|
Ayah 29:16 الأية
وَإِبْرَاهِيمَ إِذْ قَالَ لِقَوْمِهِ اعْبُدُوا اللَّهَ وَاتَّقُوهُ ۖ ذَٰلِكُمْ
خَيْرٌ لَّكُمْ إِن كُنتُمْ تَعْلَمُونَ
Swahili
Na Ibrahim pale alipo waambia watu wake: Muabuduni Mwenyezi Mungu, na mcheni
Yeye. Hiyo ndiyo kheri yenu, ikiwa nyinyi mnajua.
|
Ayah 29:17 الأية
إِنَّمَا تَعْبُدُونَ مِن دُونِ اللَّهِ أَوْثَانًا وَتَخْلُقُونَ إِفْكًا ۚ إِنَّ
الَّذِينَ تَعْبُدُونَ مِن دُونِ اللَّهِ لَا يَمْلِكُونَ لَكُمْ رِزْقًا
فَابْتَغُوا عِندَ اللَّهِ الرِّزْقَ وَاعْبُدُوهُ وَاشْكُرُوا لَهُ ۖ إِلَيْهِ
تُرْجَعُونَ
Swahili
Hakika nyinyi mnaabudu masanamu badala ya Mwenyezi Mungu, na mnazua uzushi.
Hakika hao mnao waabudu badala ya Mwenyezi Mungu hawakumilikiini riziki yoyote.
Takeni riziki kwa Mwenyezi Mungu, na mumuabudu Yeye, na mumshukuru Yeye. Kwake
Yeye ndio mtarudishwa.
|
Ayah 29:18 الأية
وَإِن تُكَذِّبُوا فَقَدْ كَذَّبَ أُمَمٌ مِّن قَبْلِكُمْ ۖ وَمَا عَلَى الرَّسُولِ
إِلَّا الْبَلَاغُ الْمُبِينُ
Swahili
Na mkikadhibisha, basi kaumu kadhaa wa kadhaa za kabla yenu zilikwisha
kadhibisha. Na si juu ya Mtume ila kufikisha Ujumbe waziwazi.
|
Ayah 29:19 الأية
أَوَلَمْ يَرَوْا كَيْفَ يُبْدِئُ اللَّهُ الْخَلْقَ ثُمَّ يُعِيدُهُ ۚ إِنَّ
ذَٰلِكَ عَلَى اللَّهِ يَسِيرٌ
Swahili
Je! Wao hawaoni jinsi Mwenyezi Mungu anavyo anzisha uumbaji, na kisha akarudisha
tena. Hakika hayo kwa Mwenyezi Mungu ni mepesi.
|
Ayah 29:20 الأية
قُلْ سِيرُوا فِي الْأَرْضِ فَانظُرُوا كَيْفَ بَدَأَ الْخَلْقَ ۚ ثُمَّ اللَّهُ
يُنشِئُ النَّشْأَةَ الْآخِرَةَ ۚ إِنَّ اللَّهَ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ
Swahili
Sema: Tembeeni katika ardhi na tazameni jinsi alivyo anzisha uumbaji; kisha
Mwenyezi Mungu ndiye anaye umba umbo la baadaye. Hakika Mwenyezi Mungu ni Muweza
juu ya kila kitu.
|
Ayah 29:21 الأية
يُعَذِّبُ مَن يَشَاءُ وَيَرْحَمُ مَن يَشَاءُ ۖ وَإِلَيْهِ تُقْلَبُونَ
Swahili
Humuadhibu amtakaye, na humrehemu amtakaye. Na kwake Yeye mtapelekwa.
|
Ayah 29:22 الأية
وَمَا أَنتُم بِمُعْجِزِينَ فِي الْأَرْضِ وَلَا فِي السَّمَاءِ ۖ وَمَا لَكُم مِّن
دُونِ اللَّهِ مِن وَلِيٍّ وَلَا نَصِيرٍ
Swahili
Na nyinyi si wenye kushinda katika ardhi wala katika mbingu. Wala nyinyi hamna
mlinzi wala msaidizi isipo kuwa Mwenyezi Mungu.
|
Ayah 29:23 الأية
وَالَّذِينَ كَفَرُوا بِآيَاتِ اللَّهِ وَلِقَائِهِ أُولَٰئِكَ يَئِسُوا مِن
رَّحْمَتِي وَأُولَٰئِكَ لَهُمْ عَذَابٌ أَلِيمٌ
Swahili
Na walio zikanusha Ishara za Mwenyezi Mungu na kukutana naye, hao ndio wenye
kukata tamaa na rehema yangu, na hao ndio wenye kupata adhabu chungu.
|
Ayah 29:24 الأية
فَمَا كَانَ جَوَابَ قَوْمِهِ إِلَّا أَن قَالُوا اقْتُلُوهُ أَوْ حَرِّقُوهُ
فَأَنجَاهُ اللَّهُ مِنَ النَّارِ ۚ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَاتٍ لِّقَوْمٍ
يُؤْمِنُونَ
Swahili
Basi haikuwa jawabu ya watu wake ila ni kusema: Muuweni au mchomeni moto!
Mwenyezi Mungu akamwokoa na moto. Hakika katika hayo zipo Ishara kwa watu wanao
amini.
|
Ayah 29:25 الأية
وَقَالَ إِنَّمَا اتَّخَذْتُم مِّن دُونِ اللَّهِ أَوْثَانًا مَّوَدَّةَ بَيْنِكُمْ
فِي الْحَيَاةِ الدُّنْيَا ۖ ثُمَّ يَوْمَ الْقِيَامَةِ يَكْفُرُ بَعْضُكُم
بِبَعْضٍ وَيَلْعَنُ بَعْضُكُم بَعْضًا وَمَأْوَاكُمُ النَّارُ وَمَا لَكُم مِّن
نَّاصِرِينَ
Swahili
Na alisema: Hakika nyinyi mmeyashika masanamu badala ya Mwenyezi Mungu kwa
mapenzi yaliyo baina yenu katika uhai wa duniani. Kisha Siku ya Kiyama
mtakataana nyinyi kwa nyinyi, na mtalaaniana nyinyi kwa nyinyi. Na makaazi yenu
ni Motoni. Wala hamtapata wa kukunusuruni.
|
Ayah 29:26 الأية
فَآمَنَ لَهُ لُوطٌ ۘ وَقَالَ إِنِّي مُهَاجِرٌ إِلَىٰ رَبِّي ۖ إِنَّهُ هُوَ
الْعَزِيزُ الْحَكِيمُ
Swahili
Lut'i akamuamini, na akasema: Mimi nahamia kwa Mola wangu Mlezi. Hakika Yeye
ndiye Mwenye nguvu, Mwenye hikima.
|
Ayah 29:27 الأية
وَوَهَبْنَا لَهُ إِسْحَاقَ وَيَعْقُوبَ وَجَعَلْنَا فِي ذُرِّيَّتِهِ النُّبُوَّةَ
وَالْكِتَابَ وَآتَيْنَاهُ أَجْرَهُ فِي الدُّنْيَا ۖ وَإِنَّهُ فِي الْآخِرَةِ
لَمِنَ الصَّالِحِينَ
Swahili
Na tulimtunukia (Ibrahim) Is-haq na Yaa'qub. Na tukajaalia katika dhuriya zake
Unabii na Kitabu, na tukampa ujira wake katika dunia; naye hakika katika Akhera
bila ya shaka ni katika watu wema.
|
Ayah 29:28 الأية
وَلُوطًا إِذْ قَالَ لِقَوْمِهِ إِنَّكُمْ لَتَأْتُونَ الْفَاحِشَةَ مَا سَبَقَكُم
بِهَا مِنْ أَحَدٍ مِّنَ الْعَالَمِينَ
Swahili
Na pale Lut'i alipo waambia watu wake: Hakika nyinyi mnafanya uchafu, ambao
hapana mmoja katika walimwengu aliye kutangulieni kwa hayo.
|
Ayah 29:29 الأية
أَئِنَّكُمْ لَتَأْتُونَ الرِّجَالَ وَتَقْطَعُونَ السَّبِيلَ وَتَأْتُونَ فِي
نَادِيكُمُ الْمُنكَرَ ۖ فَمَا كَانَ جَوَابَ قَوْمِهِ إِلَّا أَن قَالُوا ائْتِنَا
بِعَذَابِ اللَّهِ إِن كُنتَ مِنَ الصَّادِقِينَ
Swahili
Je! Nyinyi mnawaingilia wanaume, na mnaikata njia? Na katika mikutano yenu
mnafanya maovu? Basi haikuwa jawabu ya watu wake isipo kuwa kusema: Tuletee hiyo
adhabu ya Mwenyezi Mungu ikiwa wewe ni katika wasemao kweli.
|
Ayah 29:30 الأية
قَالَ رَبِّ انصُرْنِي عَلَى الْقَوْمِ الْمُفْسِدِينَ
Swahili
Akasema: Ewe Mola wangu Mlezi! Ninusuru na watu mafisadi hawa!
|
Ayah 29:31 الأية
وَلَمَّا جَاءَتْ رُسُلُنَا إِبْرَاهِيمَ بِالْبُشْرَىٰ قَالُوا إِنَّا مُهْلِكُو
أَهْلِ هَٰذِهِ الْقَرْيَةِ ۖ إِنَّ أَهْلَهَا كَانُوا ظَالِمِينَ
Swahili
Na wajumbe wetu walipo mjia Ibrahim na bishara, walisema: Hakika sisi hapana
shaka tutawahiliki watu wa mji huu, kwani watu wake hakika wamekuwa madhaalimu.
|
Ayah 29:32 الأية
قَالَ إِنَّ فِيهَا لُوطًا ۚ قَالُوا نَحْنُ أَعْلَمُ بِمَن فِيهَا ۖ
لَنُنَجِّيَنَّهُ وَأَهْلَهُ إِلَّا امْرَأَتَهُ كَانَتْ مِنَ الْغَابِرِينَ
Swahili
Akasema: Hakika humo yumo Lut'i. Wao wakasema: Sisi tunajua zaidi nani yumo
humo. Hapana shaka tutamwokoa yeye na ahali zake, isipo kuwa mkewe aliye
miongoni mwa watao kaa nyuma.
|
Ayah 29:33 الأية
وَلَمَّا أَن جَاءَتْ رُسُلُنَا لُوطًا سِيءَ بِهِمْ وَضَاقَ بِهِمْ ذَرْعًا
وَقَالُوا لَا تَخَفْ وَلَا تَحْزَنْ ۖ إِنَّا مُنَجُّوكَ وَأَهْلَكَ إِلَّا
امْرَأَتَكَ كَانَتْ مِنَ الْغَابِرِينَ
Swahili
Na wajumbe wetu walipo mfikia Lut'i, alihuzunika kwa ajili yao, na moyo uliona
dhiki kwa ajili yao. Wakasema: Usiogope, wala usihuzunike. Hakika sisi
tutakuokoa wewe na ahali zako, ila mkeo aliye miongoni mwa watao kaa nyuma.
|
Ayah 29:34 الأية
إِنَّا مُنزِلُونَ عَلَىٰ أَهْلِ هَٰذِهِ الْقَرْيَةِ رِجْزًا مِّنَ السَّمَاءِ
بِمَا كَانُوا يَفْسُقُونَ
Swahili
Kwa yakini sisi tutawateremshia watu wa mji huu adhabu kutoka mbinguni kwa
sababu ya uchafu wanao ufanya.
|
Ayah 29:35 الأية
وَلَقَد تَّرَكْنَا مِنْهَا آيَةً بَيِّنَةً لِّقَوْمٍ يَعْقِلُونَ
Swahili
Na tumeacha katika mji huo Ishara ilio wazi kwa watu wanao tumia akili zao.
|
Ayah 29:36 الأية
وَإِلَىٰ مَدْيَنَ أَخَاهُمْ شُعَيْبًا فَقَالَ يَا قَوْمِ اعْبُدُوا اللَّهَ
وَارْجُوا الْيَوْمَ الْآخِرَ وَلَا تَعْثَوْا فِي الْأَرْضِ مُفْسِدِينَ
Swahili
Na kwa Madyana tulimtuma ndugu yao Shuaibu, naye akasema: Enyi watu wangu!
Muabuduni Mwenyezi Mungu na iogopeni Siku ya Akhera, wala msende katika ardhi
mkifisidi.
|
Ayah 29:37 الأية
فَكَذَّبُوهُ فَأَخَذَتْهُمُ الرَّجْفَةُ فَأَصْبَحُوا فِي دَارِهِمْ جَاثِمِينَ
Swahili
Lakini walimkanusha basi ukawatwaa mtikiso wa ardhi, wakapambazukiwa ndani ya
nyumba zao nao wamefudikia.
|
Ayah 29:38 الأية
وَعَادًا وَثَمُودَ وَقَد تَّبَيَّنَ لَكُم مِّن مَّسَاكِنِهِمْ ۖ وَزَيَّنَ لَهُمُ
الشَّيْطَانُ أَعْمَالَهُمْ فَصَدَّهُمْ عَنِ السَّبِيلِ وَكَانُوا مُسْتَبْصِرِينَ
Swahili
Na pia kina A'di na Thamud. Nanyi yamekwisha kubainikieni kutokana na maskani
zao. Na Shet'ani aliwapambia vitendo vyao, na akawazuilia Njia, na hali walikuwa
wenye kuona.
|
Ayah 29:39 الأية
وَقَارُونَ وَفِرْعَوْنَ وَهَامَانَ ۖ وَلَقَدْ جَاءَهُم مُّوسَىٰ بِالْبَيِّنَاتِ
فَاسْتَكْبَرُوا فِي الْأَرْضِ وَمَا كَانُوا سَابِقِينَ
Swahili
Na pia Qaruni na Firauni na Hamana! Na Musa aliwajia kwa Ishara waziwazi, lakini
walijivuna katika nchi, wala hawakuweza kushinda.
|
Ayah 29:40 الأية
فَكُلًّا أَخَذْنَا بِذَنبِهِ ۖ فَمِنْهُم مَّنْ أَرْسَلْنَا عَلَيْهِ حَاصِبًا
وَمِنْهُم مَّنْ أَخَذَتْهُ الصَّيْحَةُ وَمِنْهُم مَّنْ خَسَفْنَا بِهِ الْأَرْضَ
وَمِنْهُم مَّنْ أَغْرَقْنَا ۚ وَمَا كَانَ اللَّهُ لِيَظْلِمَهُمْ وَلَٰكِن
كَانُوا أَنفُسَهُمْ يَظْلِمُونَ
Swahili
Basi kila mmoja tulimtesa kwa mujibu wa makosa yake. Kati yao wapo tulio
wapelekea kimbunga cha changarawe; na kati yao wapo walio nyakuliwa na ukelele;
na kati yao wapo ambao tulio wadidimiza katika ardhi; na kati yao wapo tulio
wazamisha. Wala Mwenyezi Mungu hakuwa mwenye kuwadhulumu, lakini walikuwa
wenyewe wakijidhulumu nafsi zao.
|
Ayah 29:41 الأية
مَثَلُ الَّذِينَ اتَّخَذُوا مِن دُونِ اللَّهِ أَوْلِيَاءَ كَمَثَلِ الْعَنكَبُوتِ
اتَّخَذَتْ بَيْتًا ۖ وَإِنَّ أَوْهَنَ الْبُيُوتِ لَبَيْتُ الْعَنكَبُوتِ ۖ لَوْ
كَانُوا يَعْلَمُونَ
Swahili
Mfano wa walio wafanya walinzi badala ya Mwenyezi Mungu, ni mfano wa buibui
alivyo jitandia nyumba. Na hakika nyumba dhaifu mno kuliko zote ni jumba la
buibui, laiti kuwa wanajua.
|
Ayah 29:42 الأية
إِنَّ اللَّهَ يَعْلَمُ مَا يَدْعُونَ مِن دُونِهِ مِن شَيْءٍ ۚ وَهُوَ الْعَزِيزُ
الْحَكِيمُ
Swahili
Kwa hakika Mwenyezi Mungu anajua kila kitu wanacho kiomba badala yake Yeye. Na
Yeye ndiye Mtukufu Mwenye nguvu Mwenye hikima.
|
Ayah 29:43 الأية
وَتِلْكَ الْأَمْثَالُ نَضْرِبُهَا لِلنَّاسِ ۖ وَمَا يَعْقِلُهَا إِلَّا
الْعَالِمُونَ
Swahili
Na hiyo ni mifano tunawapigia watu, na hawaifahamu ila wenye ilimu.
|
Ayah 29:44 الأية
خَلَقَ اللَّهُ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضَ بِالْحَقِّ ۚ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَةً
لِّلْمُؤْمِنِينَ
Swahili
Mwenyezi Mungu ameumba mbingu na ardhi kwa Haki. Kwa hakika katika hayo ipo
Ishara kwa Waumini.
|
Ayah 29:45 الأية
اتْلُ مَا أُوحِيَ إِلَيْكَ مِنَ الْكِتَابِ وَأَقِمِ الصَّلَاةَ ۖ إِنَّ
الصَّلَاةَ تَنْهَىٰ عَنِ الْفَحْشَاءِ وَالْمُنكَرِ ۗ وَلَذِكْرُ اللَّهِ أَكْبَرُ
ۗ وَاللَّهُ يَعْلَمُ مَا تَصْنَعُونَ
Swahili
SOMA uliyo funuliwa katika Kitabu, na ushike Sala. Hakika Sala inazuilia mambo
machafu na maovu. Na kwa yakini kumdhukuru Mwenyezi Mungu ndilo jambo kubwa
kabisa. Na Mwenyezi Mungu anayajua mnayo yatenda.
|
Ayah 29:46 الأية
وَلَا تُجَادِلُوا أَهْلَ الْكِتَابِ إِلَّا بِالَّتِي هِيَ أَحْسَنُ إِلَّا
الَّذِينَ ظَلَمُوا مِنْهُمْ ۖ وَقُولُوا آمَنَّا بِالَّذِي أُنزِلَ إِلَيْنَا
وَأُنزِلَ إِلَيْكُمْ وَإِلَٰهُنَا وَإِلَٰهُكُمْ وَاحِدٌ وَنَحْنُ لَهُ
مُسْلِمُونَ
Swahili
Wala msijadiliane na Watu wa Kitabu ila kwa njia iliyo nzuri kabisa, isipo kuwa
wale walio dhulumu miongoni mwao. Na semeni: Tumeyaamini yaliyo teremshwa kwetu
na yaliyo teremshwa kwenu. Na Mungu wetu na Mungu wenu ni Mmoja. Na sisi ni
wenye kusilimu kwake.
|
Ayah 29:47 الأية
وَكَذَٰلِكَ أَنزَلْنَا إِلَيْكَ الْكِتَابَ ۚ فَالَّذِينَ آتَيْنَاهُمُ الْكِتَابَ
يُؤْمِنُونَ بِهِ ۖ وَمِنْ هَٰؤُلَاءِ مَن يُؤْمِنُ بِهِ ۚ وَمَا يَجْحَدُ
بِآيَاتِنَا إِلَّا الْكَافِرُونَ
Swahili
Na namna hivi tumekuteremshia Kitabu (cha Qur'ani). Basi wale tulio wapa Kitabu
(cha Biblia) wataiamini (Qur'ani), na miongoni mwa hawa (washirikina) wapo
watakao iamini. Na hawazikatai Ishara zetu isipo kuwa makafiri.
|
Ayah 29:48 الأية
وَمَا كُنتَ تَتْلُو مِن قَبْلِهِ مِن كِتَابٍ وَلَا تَخُطُّهُ بِيَمِينِكَ ۖ إِذًا
لَّارْتَابَ الْمُبْطِلُونَ
Swahili
Na wewe hukuwa kabla yake unasoma kitabu chochote, wala hukukiandika kwa mkono
wako wa kulia. Ingeli kuwa hivyo wangeli fanya shaka wavunjifu.
|
Ayah 29:49 الأية
بَلْ هُوَ آيَاتٌ بَيِّنَاتٌ فِي صُدُورِ الَّذِينَ أُوتُوا الْعِلْمَ ۚ وَمَا
يَجْحَدُ بِآيَاتِنَا إِلَّا الظَّالِمُونَ
Swahili
Bali hii (Qur'ani) ni Ishara zilizo wazi katika vifua vya walio pewa ilimu. Na
hawazikatai Ishara zetu isipo kuwa wenye kudhulumu.
|
Ayah 29:50 الأية
وَقَالُوا لَوْلَا أُنزِلَ عَلَيْهِ آيَاتٌ مِّن رَّبِّهِ ۖ قُلْ إِنَّمَا
الْآيَاتُ عِندَ اللَّهِ وَإِنَّمَا أَنَا نَذِيرٌ مُّبِينٌ
Swahili
Na walisema: Mbona hakuteremshiwa Ishara kutoka kwa Mola wake Mlezi? Sema:
Ishara ziko kwake Mwenyezi Mungu; ama mimi kwa hakika ni mwonyaji mwenye
kubainisha tu.
|
Ayah 29:51 الأية
أَوَلَمْ يَكْفِهِمْ أَنَّا أَنزَلْنَا عَلَيْكَ الْكِتَابَ يُتْلَىٰ عَلَيْهِمْ ۚ
إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَرَحْمَةً وَذِكْرَىٰ لِقَوْمٍ يُؤْمِنُونَ
Swahili
Je! Kwani hayakuwatosha ya kwamba tumekuteremshia Kitabu hiki wanacho somewa?
Hakika katika hayo zipo rehema na mawaidha kwa watu wanao amini.
|
Ayah 29:52 الأية
قُلْ كَفَىٰ بِاللَّهِ بَيْنِي وَبَيْنَكُمْ شَهِيدًا ۖ يَعْلَمُ مَا فِي
السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ ۗ وَالَّذِينَ آمَنُوا بِالْبَاطِلِ وَكَفَرُوا
بِاللَّهِ أُولَٰئِكَ هُمُ الْخَاسِرُونَ
Swahili
Sema: Mwenyezi Mungu anatosha kuwa ni Shahidi baina yangu na nyinyi. Anayajua
yaliomo katika mbingu na ardhi. Na wale wanao amini upotovu na wakamkataa
Mwenyezi Mungu, hao ndio walio khasiri.
|
Ayah 29:53 الأية
وَيَسْتَعْجِلُونَكَ بِالْعَذَابِ ۚ وَلَوْلَا أَجَلٌ مُّسَمًّى لَّجَاءَهُمُ
الْعَذَابُ وَلَيَأْتِيَنَّهُم بَغْتَةً وَهُمْ لَا يَشْعُرُونَ
Swahili
Na wanakuhimiza waletewe adhabu kwa haraka. Na lau kuwa hapana wakati maalumu
ulio wekwa, basi adhabu ingeli wajia, na ingeli watokea kwa ghafla, na hali wao
hawana khabari.
|
Ayah 29:54 الأية
يَسْتَعْجِلُونَكَ بِالْعَذَابِ وَإِنَّ جَهَنَّمَ لَمُحِيطَةٌ بِالْكَافِرِينَ
Swahili
Wanakuhimiza waletewe adhabu kwa haraka, na hali Jahannamu kwa hakika
imewazunguka makafiri!
|
Ayah 29:55 الأية
يَوْمَ يَغْشَاهُمُ الْعَذَابُ مِن فَوْقِهِمْ وَمِن تَحْتِ أَرْجُلِهِمْ وَيَقُولُ
ذُوقُوا مَا كُنتُمْ تَعْمَلُونَ
Swahili
Siku itapo wafunika adhabu hiyo kutoka juu yao na chini ya miguu yao, na
atasema: Onjeni hayo mliyo kuwa mkiyatenda!
|
Ayah 29:56 الأية
يَا عِبَادِيَ الَّذِينَ آمَنُوا إِنَّ أَرْضِي وَاسِعَةٌ فَإِيَّايَ فَاعْبُدُونِ
Swahili
Enyi waja wangu mlio amini! Kwa hakika ardhi yangu ina wasaa. Basi niabuduni
Mimi peke yangu.
|
Ayah 29:57 الأية
كُلُّ نَفْسٍ ذَائِقَةُ الْمَوْتِ ۖ ثُمَّ إِلَيْنَا تُرْجَعُونَ
Swahili
Kila nafsi itaonja mauti. Kisha mtarudishwa kwetu.
|
Ayah 29:58 الأية
وَالَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ لَنُبَوِّئَنَّهُم مِّنَ الْجَنَّةِ
غُرَفًا تَجْرِي مِن تَحْتِهَا الْأَنْهَارُ خَالِدِينَ فِيهَا ۚ نِعْمَ أَجْرُ
الْعَامِلِينَ
Swahili
Na ambao wameamini na wakatenda mema, bila ya shaka tutawaweka katika maghorofa
ya Peponi yenye kupitiwa chini yake mito, wakidumu humo. Ni mwema ulioje huo
ujira wa watendao,
|
Ayah 29:59 الأية
الَّذِينَ صَبَرُوا وَعَلَىٰ رَبِّهِمْ يَتَوَكَّلُونَ
Swahili
Ambao walisubiri, na wakamtegemea Mola wao Mlezi.
|
Ayah 29:60 الأية
وَكَأَيِّن مِّن دَابَّةٍ لَّا تَحْمِلُ رِزْقَهَا اللَّهُ يَرْزُقُهَا
وَإِيَّاكُمْ ۚ وَهُوَ السَّمِيعُ الْعَلِيمُ
Swahili
Na wanyama wangapi hawawezi kujimilikia riziki zao! Mwenyezi Mungu anawaruzuku
hao na nyinyi pia. Na Yeye ndiye Mwenye kusikia Mwenye kujua.
|
Ayah 29:61 الأية
وَلَئِن سَأَلْتَهُم مَّنْ خَلَقَ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضَ وَسَخَّرَ الشَّمْسَ
وَالْقَمَرَ لَيَقُولُنَّ اللَّهُ ۖ فَأَنَّىٰ يُؤْفَكُونَ
Swahili
Na ukiwauliza; Nani aliye umba mbingu na ardhi na akafanya jua na mwezi kuti'ii
amri yake? Bila ya shaka, watasema: Mwenyezi Mungu. Wapi basi wanako geuzwa?
|
Ayah 29:62 الأية
اللَّهُ يَبْسُطُ الرِّزْقَ لِمَن يَشَاءُ مِنْ عِبَادِهِ وَيَقْدِرُ لَهُ ۚ إِنَّ
اللَّهَ بِكُلِّ شَيْءٍ عَلِيمٌ
Swahili
Mwenyezi Mungu humkunjulia, na humdhikishia, riziki amtakaye katika waja wake.
Kwa hakika Mwenyezi Mungu ni Mjuzi wa kila kitu.
|
Ayah 29:63 الأية
وَلَئِن سَأَلْتَهُم مَّن نَّزَّلَ مِنَ السَّمَاءِ مَاءً فَأَحْيَا بِهِ الْأَرْضَ
مِن بَعْدِ مَوْتِهَا لَيَقُولُنَّ اللَّهُ ۚ قُلِ الْحَمْدُ لِلَّهِ ۚ بَلْ
أَكْثَرُهُمْ لَا يَعْقِلُونَ
Swahili
Na ukiwauliza: Ni nani anaye teremsha maji kutoka mbinguni, na akaihuisha ardhi
baada ya kufa kwake? Bila ya shaka watasema: Ni Mwenyezi Mungu. Sema: Alhamdu
Lillahi, Sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu. Bali wengi katika wao hawafahamu.
|
Ayah 29:64 الأية
وَمَا هَٰذِهِ الْحَيَاةُ الدُّنْيَا إِلَّا لَهْوٌ وَلَعِبٌ ۚ وَإِنَّ الدَّارَ
الْآخِرَةَ لَهِيَ الْحَيَوَانُ ۚ لَوْ كَانُوا يَعْلَمُونَ
Swahili
Na haya maisha ya dunia si chochote ila ni pumbao na mchezo. Na nyumba ya Akhera
ndiyo maisha khasa; laiti wangeli kuwa wanajua!
|
Ayah 29:65 الأية
فَإِذَا رَكِبُوا فِي الْفُلْكِ دَعَوُا اللَّهَ مُخْلِصِينَ لَهُ الدِّينَ
فَلَمَّا نَجَّاهُمْ إِلَى الْبَرِّ إِذَا هُمْ يُشْرِكُونَ
Swahili
Na wanapo panda katika marikebu, humwomba Mwenyezi Mungu kwa kumsafia ut'iifu.
Lakini anapo wavua wakafika nchi kavu, mara wanamshirikisha.
|
Ayah 29:66 الأية
لِيَكْفُرُوا بِمَا آتَيْنَاهُمْ وَلِيَتَمَتَّعُوا ۖ فَسَوْفَ يَعْلَمُونَ
Swahili
Wapate kuyakanya tuliyo wapa, na wajistareheshe. Lakini watakuja jua!
|
Ayah 29:67 الأية
أَوَلَمْ يَرَوْا أَنَّا جَعَلْنَا حَرَمًا آمِنًا وَيُتَخَطَّفُ النَّاسُ مِنْ
حَوْلِهِمْ ۚ أَفَبِالْبَاطِلِ يُؤْمِنُونَ وَبِنِعْمَةِ اللَّهِ يَكْفُرُونَ
Swahili
Je! Hawaoni ya kwamba tumeifanya nchi takatifu ina amani, na hali watu wengine
wananyakuliwa kote kwa majirani zao? Je! Wanaamini upotovu, na neema za Mwenyezi
Mungu wanazikataa?
|
Ayah 29:68 الأية
وَمَنْ أَظْلَمُ مِمَّنِ افْتَرَىٰ عَلَى اللَّهِ كَذِبًا أَوْ كَذَّبَ بِالْحَقِّ
لَمَّا جَاءَهُ ۚ أَلَيْسَ فِي جَهَنَّمَ مَثْوًى لِّلْكَافِرِينَ
Swahili
Na nani dhaalimu mkubwa kuliko yule anaye mzulia uwongo Mwenyezi Mungu au anaye
kanusha Haki inapo mjia? Je! Si katika Jahannamu ndio yatakuwa makaazi ya
makafiri?
|
Ayah 29:69 الأية
وَالَّذِينَ جَاهَدُوا فِينَا لَنَهْدِيَنَّهُمْ سُبُلَنَا ۚ وَإِنَّ اللَّهَ
لَمَعَ الْمُحْسِنِينَ
Swahili
Na wanao fanya juhudi kwa ajili yetu, Sisi tutawaongoa kwenye njia zetu. Na
hakika Mwenyezi Mungu yu pamoja na watu wema.
|
©
EsinIslam.Com Designed & produced by The Awqaf London. Please pray for us
|