First Ayah 1 الأية الأوليبِسْم ِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ
الْحَمْدُ لِلَّهِ فَاطِرِ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ جَاعِلِ الْمَلَائِكَةِ
رُسُلًا أُولِي أَجْنِحَةٍ مَّثْنَىٰ وَثُلَاثَ وَرُبَاعَ ۚ يَزِيدُ فِي الْخَلْقِ
مَا يَشَاءُ ۚ إِنَّ اللَّهَ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ
Swahili
Sifa zote njema ni za Mwenyezi Mungu, Muumba wa mbingu na ardhi, aliye wafanya
Malaika kuwa wajumbe wenye mbawa, mbili-mbili, na tatu- tatu, na nne-nne.
Huzidisha katika kuumba apendavyo. Hakika Mwenyezi Mungu ni Muweza juu ya kila
kitu.
|
Ayah 35:2 الأية
مَّا يَفْتَحِ اللَّهُ لِلنَّاسِ مِن رَّحْمَةٍ فَلَا مُمْسِكَ لَهَا ۖ وَمَا
يُمْسِكْ فَلَا مُرْسِلَ لَهُ مِن بَعْدِهِ ۚ وَهُوَ الْعَزِيزُ الْحَكِيمُ
Swahili
Rehema ambayo Mwenyezi Mungu anawafungulia watu hapana wa kuizuia. Na anayo
izuia hapana wa kuipeleka isipo kuwa Yeye. Naye ndiye Mwenye nguvu, Mwenye
hikima.
|
Ayah 35:3 الأية
يَا أَيُّهَا النَّاسُ اذْكُرُوا نِعْمَتَ اللَّهِ عَلَيْكُمْ ۚ هَلْ مِنْ خَالِقٍ
غَيْرُ اللَّهِ يَرْزُقُكُم مِّنَ السَّمَاءِ وَالْأَرْضِ ۚ لَا إِلَٰهَ إِلَّا
هُوَ ۖ فَأَنَّىٰ تُؤْفَكُونَ
Swahili
Enyi watu! Kumbukeni neema za Mwenyezi Mungu juu yenu. Ati yupo muumba mwengine
asiye kuwa Mwenyezi Mungu anaye kupeni riziki kutoka mbinguni na kwenye ardhi?
Hapana mungu ila Yeye tu. Basi wapi mnako geuzwa?
|
Ayah 35:4 الأية
وَإِن يُكَذِّبُوكَ فَقَدْ كُذِّبَتْ رُسُلٌ مِّن قَبْلِكَ ۚ وَإِلَى اللَّهِ
تُرْجَعُ الْأُمُورُ
Swahili
Na wakikukanusha, basi walikwisha kanushwa Mitume kabla yako. Na mambo yote
yatarudishwa kwa Mwenyezi Mungu.
|
Ayah 35:5 الأية
يَا أَيُّهَا النَّاسُ إِنَّ وَعْدَ اللَّهِ حَقٌّ ۖ فَلَا تَغُرَّنَّكُمُ
الْحَيَاةُ الدُّنْيَا ۖ وَلَا يَغُرَّنَّكُم بِاللَّهِ الْغَرُورُ
Swahili
Enyi watu! Hakika ahadi ya Mwenyezi Mungu ni ya kweli. Basi yasikudanganyeni
maisha ya dunia, wala mdanganyifu asikudanganyeni juu ya Mwenyezi Mungu.
|
Ayah 35:6 الأية
إِنَّ الشَّيْطَانَ لَكُمْ عَدُوٌّ فَاتَّخِذُوهُ عَدُوًّا ۚ إِنَّمَا يَدْعُو
حِزْبَهُ لِيَكُونُوا مِنْ أَصْحَابِ السَّعِيرِ
Swahili
Hakika Shet'ani ni adui yenu, basi mfanyeni kuwa ni adui. Kwani yeye analiita
kundi lake liwe katika watu wa Motoni.
|
Ayah 35:7 الأية
الَّذِينَ كَفَرُوا لَهُمْ عَذَابٌ شَدِيدٌ ۖ وَالَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا
الصَّالِحَاتِ لَهُم مَّغْفِرَةٌ وَأَجْرٌ كَبِيرٌ
Swahili
Walio kufuru watakuwa na adhabu kali; na walio amini na wakatenda mema watapata
msamaha na ujira mkubwa.
|
Ayah 35:8 الأية
أَفَمَن زُيِّنَ لَهُ سُوءُ عَمَلِهِ فَرَآهُ حَسَنًا ۖ فَإِنَّ اللَّهَ يُضِلُّ
مَن يَشَاءُ وَيَهْدِي مَن يَشَاءُ ۖ فَلَا تَذْهَبْ نَفْسُكَ عَلَيْهِمْ حَسَرَاتٍ
ۚ إِنَّ اللَّهَ عَلِيمٌ بِمَا يَصْنَعُونَ
Swahili
Je! Yule aliye pambiwa a'mali zake mbaya na akaziona ni njema - basi hakika
Mwenyezi Mungu humwacha akapotea amtakaye, na humwongoa amtakaye. Basi nafsi
yako isijihiliki kwa kuwasikitikia. Hakika Mwenyezi Mungu anajua wanayo yafanya.
|
Ayah 35:9 الأية
وَاللَّهُ الَّذِي أَرْسَلَ الرِّيَاحَ فَتُثِيرُ سَحَابًا فَسُقْنَاهُ إِلَىٰ
بَلَدٍ مَّيِّتٍ فَأَحْيَيْنَا بِهِ الْأَرْضَ بَعْدَ مَوْتِهَا ۚ كَذَٰلِكَ
النُّشُورُ
Swahili
Na Mwenyezi Mungu ndiye anaye zituma Pepo ziyatimue mawingu, nasi tukayafikisha
kwenye nchi iliyo kufa, tukaifufua ardhi baada ya kufa kwake. Ndivyo kama hivyo
kutakavyo kuwa kufufuliwa.
|
Ayah 35:10 الأية
مَن كَانَ يُرِيدُ الْعِزَّةَ فَلِلَّهِ الْعِزَّةُ جَمِيعًا ۚ إِلَيْهِ يَصْعَدُ
الْكَلِمُ الطَّيِّبُ وَالْعَمَلُ الصَّالِحُ يَرْفَعُهُ ۚ وَالَّذِينَ يَمْكُرُونَ
السَّيِّئَاتِ لَهُمْ عَذَابٌ شَدِيدٌ ۖ وَمَكْرُ أُولَٰئِكَ هُوَ يَبُورُ
Swahili
Mwenye kutaka utukufu basi utukufu wote uko kwa Mwenyezi Mungu. Kwake Yeye
hupanda neno zuri, na a'mali njema Yeye huitukuza. Na wanao panga vitimbi vya
maovu watapata adhabu kali. Na vitimbi vya hao vitaondokea patupu.
|
Ayah 35:11 الأية
وَاللَّهُ خَلَقَكُم مِّن تُرَابٍ ثُمَّ مِن نُّطْفَةٍ ثُمَّ جَعَلَكُمْ أَزْوَاجًا
ۚ وَمَا تَحْمِلُ مِنْ أُنثَىٰ وَلَا تَضَعُ إِلَّا بِعِلْمِهِ ۚ وَمَا يُعَمَّرُ
مِن مُّعَمَّرٍ وَلَا يُنقَصُ مِنْ عُمُرِهِ إِلَّا فِي كِتَابٍ ۚ إِنَّ ذَٰلِكَ
عَلَى اللَّهِ يَسِيرٌ
Swahili
Na Mwenyezi Mungu amekuumbeni kutokana na udongo. Kisha kwa tone la manii. Kisha
akakufanyeni mwanamume na mwanamke. Na mwanamke yeyote hachukui mimba, wala
hazai, ila kwa ilimu yake. Na wala hapewi umri mwenye umri mrefu, wala
hapunguziwi katika umri wake, ila yamo hayo katika Kitabu. Hakika hayo ni mepesi
kwa Mwenyezi Mungu.
|
Ayah 35:12 الأية
وَمَا يَسْتَوِي الْبَحْرَانِ هَٰذَا عَذْبٌ فُرَاتٌ سَائِغٌ شَرَابُهُ وَهَٰذَا
مِلْحٌ أُجَاجٌ ۖ وَمِن كُلٍّ تَأْكُلُونَ لَحْمًا طَرِيًّا وَتَسْتَخْرِجُونَ
حِلْيَةً تَلْبَسُونَهَا ۖ وَتَرَى الْفُلْكَ فِيهِ مَوَاخِرَ لِتَبْتَغُوا مِن
فَضْلِهِ وَلَعَلَّكُمْ تَشْكُرُونَ
Swahili
Na bahari mbili haziwi sawa; haya ni matamu yenye ladha, mazuri kunywa. Na haya
ni ya chumvi, machungu. Na kutokana na bahari zote mnakula nyama mpya (isiyo
chacha). Na mnatoa mapambo mnayo yavaa. Na unaona ndani yake marikebu zinakata
maji ili mtafute fadhila zake, na ili mpate kushukuru.
|
Ayah 35:13 الأية
يُولِجُ اللَّيْلَ فِي النَّهَارِ وَيُولِجُ النَّهَارَ فِي اللَّيْلِ وَسَخَّرَ
الشَّمْسَ وَالْقَمَرَ كُلٌّ يَجْرِي لِأَجَلٍ مُّسَمًّى ۚ ذَٰلِكُمُ اللَّهُ
رَبُّكُمْ لَهُ الْمُلْكُ ۚ وَالَّذِينَ تَدْعُونَ مِن دُونِهِ مَا يَمْلِكُونَ مِن
قِطْمِيرٍ
Swahili
Anauingiza usiku katika mchana, na anauingiza mchana katika usiku. Na amelifanya
jua na mwezi kutumikia. Kila kimojapo kinakwenda kwa muda maalumu. Huyo ndiye
Mwenyezi Mungu Mola wenu Mlezi. Ufalme ni wake. Na hao mnao waomba badala yake
hawamiliki hata ugozi wa kokwa ya tende.
|
Ayah 35:14 الأية
إِن تَدْعُوهُمْ لَا يَسْمَعُوا دُعَاءَكُمْ وَلَوْ سَمِعُوا مَا اسْتَجَابُوا
لَكُمْ ۖ وَيَوْمَ الْقِيَامَةِ يَكْفُرُونَ بِشِرْكِكُمْ ۚ وَلَا يُنَبِّئُكَ
مِثْلُ خَبِيرٍ
Swahili
Mkiwaomba hawasikii maombi yenu; na hata wakisikia hawakujibuni. Na Siku ya
Kiyama watakataa ushirikina wenu. Na hapana atakaye kupa khabari vilivyo kama
Yeye Mwenye khabari.
|
Ayah 35:15 الأية
يَا أَيُّهَا النَّاسُ أَنتُمُ الْفُقَرَاءُ إِلَى اللَّهِ ۖ وَاللَّهُ هُوَ
الْغَنِيُّ الْحَمِيدُ
Swahili
Enyi watu! Nyinyi ndio wenye haja kwa Mwenyezi Mungu, na Mwenyezi Mungu ndiye
Mwenye kujitosha, Msifiwa.
|
Ayah 35:16 الأية
إِن يَشَأْ يُذْهِبْكُمْ وَيَأْتِ بِخَلْقٍ جَدِيدٍ
Swahili
Akitaka atakuondoeni na alete viumbe vipya.
|
Ayah 35:17 الأية
وَمَا ذَٰلِكَ عَلَى اللَّهِ بِعَزِيزٍ
Swahili
Na hilo si gumu kwa Mwenyezi Mungu.
|
Ayah 35:18 الأية
وَلَا تَزِرُ وَازِرَةٌ وِزْرَ أُخْرَىٰ ۚ وَإِن تَدْعُ مُثْقَلَةٌ إِلَىٰ
حِمْلِهَا لَا يُحْمَلْ مِنْهُ شَيْءٌ وَلَوْ كَانَ ذَا قُرْبَىٰ ۗ إِنَّمَا
تُنذِرُ الَّذِينَ يَخْشَوْنَ رَبَّهُم بِالْغَيْبِ وَأَقَامُوا الصَّلَاةَ ۚ وَمَن
تَزَكَّىٰ فَإِنَّمَا يَتَزَكَّىٰ لِنَفْسِهِ ۚ وَإِلَى اللَّهِ الْمَصِيرُ
Swahili
Na mbebaji habebi mzigo wa mwingine. Na aliye topewa na mzigo wake akiomba
uchukuliwe hautachukuliwa hata kidogo, na angamwomba jamaa yake. Hakika wewe
unawaonya wale wanao mcha Mola wao Mlezi kwa ghaibu, na wanashika Sala. Na anaye
jitakasa, basi anajitakasa kwa ajili ya nafsi yake. Na marejeo ni kwa Mwenyezi
Mungu.
|
Ayah 35:19 الأية
وَمَا يَسْتَوِي الْأَعْمَىٰ وَالْبَصِيرُ
Swahili
Na kipofu na mwenye kuona hawalingani.
|
Ayah 35:20 الأية
وَلَا الظُّلُمَاتُ وَلَا النُّورُ
Swahili
Wala giza na mwangaza.
|
Ayah 35:21 الأية
وَلَا الظِّلُّ وَلَا الْحَرُورُ
Swahili
Wala kivuli na joto.
|
Ayah 35:22 الأية
وَمَا يَسْتَوِي الْأَحْيَاءُ وَلَا الْأَمْوَاتُ ۚ إِنَّ اللَّهَ يُسْمِعُ مَن
يَشَاءُ ۖ وَمَا أَنتَ بِمُسْمِعٍ مَّن فِي الْقُبُورِ
Swahili
Wala hawalingani walio hai na maiti. Hakika Mwenyezi Mungu humsikilizisha
amtakaye. Wala wewe si wa kuwasikilizisha walio makaburini.
|
Ayah 35:23 الأية
إِنْ أَنتَ إِلَّا نَذِيرٌ
Swahili
Hukuwa wewe ila ni mwonyaji.
|
Ayah 35:24 الأية
إِنَّا أَرْسَلْنَاكَ بِالْحَقِّ بَشِيرًا وَنَذِيرًا ۚ وَإِن مِّنْ أُمَّةٍ إِلَّا
خَلَا فِيهَا نَذِيرٌ
Swahili
Hakika Sisi tumekutuma wewe kwa Haki, kuwa ni mbashiri na mwonyaji. Na hapana
umma wowote ila ulipata mwonyaji kati yao.
|
Ayah 35:25 الأية
وَإِن يُكَذِّبُوكَ فَقَدْ كَذَّبَ الَّذِينَ مِن قَبْلِهِمْ جَاءَتْهُمْ رُسُلُهُم
بِالْبَيِّنَاتِ وَبِالزُّبُرِ وَبِالْكِتَابِ الْمُنِيرِ
Swahili
Na wakikukanusha basi walikwisha wakanusha walio kuwa kabla yao. Mitume wao
waliwajia kwa dalili wazi wazi na kwa maandiko na Kitabu chenye nuru.
|
Ayah 35:26 الأية
ثُمَّ أَخَذْتُ الَّذِينَ كَفَرُوا ۖ فَكَيْفَ كَانَ نَكِيرِ
Swahili
Kisha nikawakamata walio kufuru. Basi kuchukia kwangu kulikuwaje?
|
Ayah 35:27 الأية
أَلَمْ تَرَ أَنَّ اللَّهَ أَنزَلَ مِنَ السَّمَاءِ مَاءً فَأَخْرَجْنَا بِهِ
ثَمَرَاتٍ مُّخْتَلِفًا أَلْوَانُهَا ۚ وَمِنَ الْجِبَالِ جُدَدٌ بِيضٌ وَحُمْرٌ
مُّخْتَلِفٌ أَلْوَانُهَا وَغَرَابِيبُ سُودٌ
Swahili
Je! Huoni kwamba Mwenyezi Mungu ameteremsha maji kutoka mbinguni, na kwayo
tumeyatoa matunda yenye rangi mbali mbali. Na katika milima imo mistari myeupe
na myekundu yenye rangi mbali mbali, na myeusi sana.
|
Ayah 35:28 الأية
وَمِنَ النَّاسِ وَالدَّوَابِّ وَالْأَنْعَامِ مُخْتَلِفٌ أَلْوَانُهُ كَذَٰلِكَ ۗ
إِنَّمَا يَخْشَى اللَّهَ مِنْ عِبَادِهِ الْعُلَمَاءُ ۗ إِنَّ اللَّهَ عَزِيزٌ
غَفُورٌ
Swahili
Na katika watu, na wanyama, na mifugo, pia rangi zao zinakhitalifiana. Kwa
hakika wanao mcha Mwenyezi Mungu miongoni mwa waja wake ni wanazuoni. Hakika
Mwenyezi Mungu ni Mwenye nguvu, Mwenye kusamehe.
|
Ayah 35:29 الأية
إِنَّ الَّذِينَ يَتْلُونَ كِتَابَ اللَّهِ وَأَقَامُوا الصَّلَاةَ وَأَنفَقُوا
مِمَّا رَزَقْنَاهُمْ سِرًّا وَعَلَانِيَةً يَرْجُونَ تِجَارَةً لَّن تَبُورَ
Swahili
Hakika wale wanao soma Kitabu cha Mwenyezi Mungu, na wakashika Sala, na wakatoa
kwa siri na kwa dhaahiri katika tulivyo waruzuku, hao hutaraji biashara isiyo
bwaga.
|
Ayah 35:30 الأية
لِيُوَفِّيَهُمْ أُجُورَهُمْ وَيَزِيدَهُم مِّن فَضْلِهِ ۚ إِنَّهُ غَفُورٌ شَكُورٌ
Swahili
Ili Yeye awalipe ujira wao kwa ukamilifu, na awazidishie kutokana na fadhila
zake. Hakika Yeye ni Mwenye kusamehe Mwenye shukrani.
|
Ayah 35:31 الأية
وَالَّذِي أَوْحَيْنَا إِلَيْكَ مِنَ الْكِتَابِ هُوَ الْحَقُّ مُصَدِّقًا لِّمَا
بَيْنَ يَدَيْهِ ۗ إِنَّ اللَّهَ بِعِبَادِهِ لَخَبِيرٌ بَصِيرٌ
Swahili
Na hayo tuliyo kufunulia kutoka Kitabuni ni Kweli yenye kusadikisha yaliyo kuwa
kabla yake. Hakika Mwenyezi Mungu kwa waja wake ni Mwenye khabari na Mwenye
kuona.
|
Ayah 35:32 الأية
ثُمَّ أَوْرَثْنَا الْكِتَابَ الَّذِينَ اصْطَفَيْنَا مِنْ عِبَادِنَا ۖ فَمِنْهُمْ
ظَالِمٌ لِّنَفْسِهِ وَمِنْهُم مُّقْتَصِدٌ وَمِنْهُمْ سَابِقٌ بِالْخَيْرَاتِ
بِإِذْنِ اللَّهِ ۚ ذَٰلِكَ هُوَ الْفَضْلُ الْكَبِيرُ
Swahili
Kisha tumewarithisha Kitabu hao ambao tuliwateuwa miongoni mwa waja wetu. Kati
yao yupo aliye jidhulumu nafsi yake, na yupo wa katikati, na yupo aliye tangulia
katika mambo ya kheri, kwa idhini ya Mwenyezi Mungu. Hiyo ndiyo fadhila kuu.
|
Ayah 35:33 الأية
جَنَّاتُ عَدْنٍ يَدْخُلُونَهَا يُحَلَّوْنَ فِيهَا مِنْ أَسَاوِرَ مِن ذَهَبٍ
وَلُؤْلُؤًا ۖ وَلِبَاسُهُمْ فِيهَا حَرِيرٌ
Swahili
Mabustani ya milele watayaingia. Huko watavikwa vikuku vya dhahabu, na lulu, na
nguo zao humo ni za hariri.
|
Ayah 35:34 الأية
وَقَالُوا الْحَمْدُ لِلَّهِ الَّذِي أَذْهَبَ عَنَّا الْحَزَنَ ۖ إِنَّ رَبَّنَا
لَغَفُورٌ شَكُورٌ
Swahili
Na watasema: Alhamdulillahi, Sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu aliye
tuondolea huzuni zote. Hakika Mola wetu Mlezi bila ya shaka ni Mwenye kusamehe,
Mwenye shukrani.
|
Ayah 35:35 الأية
الَّذِي أَحَلَّنَا دَارَ الْمُقَامَةِ مِن فَضْلِهِ لَا يَمَسُّنَا فِيهَا نَصَبٌ
وَلَا يَمَسُّنَا فِيهَا لُغُوبٌ
Swahili
Ambaye kwa fadhila yake ametuweka makao ya kukaa daima; humu haitugusi taabu
wala humu hakutugusi kuchoka.
|
Ayah 35:36 الأية
وَالَّذِينَ كَفَرُوا لَهُمْ نَارُ جَهَنَّمَ لَا يُقْضَىٰ عَلَيْهِمْ فَيَمُوتُوا
وَلَا يُخَفَّفُ عَنْهُم مِّنْ عَذَابِهَا ۚ كَذَٰلِكَ نَجْزِي كُلَّ كَفُورٍ
Swahili
Na walio kufuru watakuwa na Moto wa Jahannamu, hawahukumiwi wakafa, wala
hawatapunguziwa adhabu yake. Hivyo ndivyo tunavyo mlipa kila mwenye kuzidi
ukafiri.
|
Ayah 35:37 الأية
وَهُمْ يَصْطَرِخُونَ فِيهَا رَبَّنَا أَخْرِجْنَا نَعْمَلْ صَالِحًا غَيْرَ
الَّذِي كُنَّا نَعْمَلُ ۚ أَوَلَمْ نُعَمِّرْكُم مَّا يَتَذَكَّرُ فِيهِ مَن
تَذَكَّرَ وَجَاءَكُمُ النَّذِيرُ ۖ فَذُوقُوا فَمَا لِلظَّالِمِينَ مِن نَّصِيرٍ
Swahili
Na humo watapiga makelele: Mola wetu Mlezi! Tutoe tufanye mema sio yale tuliyo
kuwa tukiyafanya. Kwani hatukukupeni umri wa kutosha kukumbuka mwenye kukumbuka?
Na akakujieni Mwonyaji? Basi onjeni! Kwani walio dhulumu hawana wa kuwanusuru.
|
Ayah 35:38 الأية
إِنَّ اللَّهَ عَالِمُ غَيْبِ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ ۚ إِنَّهُ عَلِيمٌ بِذَاتِ
الصُّدُورِ
Swahili
Kwa hakika Mwenyezi Mungu ni Mjuzi wa siri za mbinguni na ardhi. Hakika Yeye ni
Mjuzi wa yaliomo vifuani.
|
Ayah 35:39 الأية
هُوَ الَّذِي جَعَلَكُمْ خَلَائِفَ فِي الْأَرْضِ ۚ فَمَن كَفَرَ فَعَلَيْهِ
كُفْرُهُ ۖ وَلَا يَزِيدُ الْكَافِرِينَ كُفْرُهُمْ عِندَ رَبِّهِمْ إِلَّا مَقْتًا
ۖ وَلَا يَزِيدُ الْكَافِرِينَ كُفْرُهُمْ إِلَّا خَسَارًا
Swahili
Yeye ndiye aliye kufanyeni manaibu katika ardhi. Na anaye kufuru, basi kufuru
yake ni juu yake; na kufuru za makafiri haziwazidishii kwa Mola wao Mlezi ila
kuchukiwa. Wala kufuru za makafiri haziwazidishii ila khasara.
|
Ayah 35:40 الأية
قُلْ أَرَأَيْتُمْ شُرَكَاءَكُمُ الَّذِينَ تَدْعُونَ مِن دُونِ اللَّهِ أَرُونِي
مَاذَا خَلَقُوا مِنَ الْأَرْضِ أَمْ لَهُمْ شِرْكٌ فِي السَّمَاوَاتِ أَمْ
آتَيْنَاهُمْ كِتَابًا فَهُمْ عَلَىٰ بَيِّنَتٍ مِّنْهُ ۚ بَلْ إِن يَعِدُ
الظَّالِمُونَ بَعْضُهُم بَعْضًا إِلَّا غُرُورًا
Swahili
Sema: Mnawaona hawa miungu wenu wa kishirikina mnao waomba badala ya Mwenyezi
Mungu! Nionyesheni wameumba sehemu gani katika ardhi? Au wana ushirika wowote
katika mbingu? Au tumewapa Kitabu nao kwa hicho wakawa na hoja zilizo wazi?
Lakini madhaalimu hawaahidiani wao kwa wao ila udanganyifu tu.
|
Ayah 35:41 الأية
إِنَّ اللَّهَ يُمْسِكُ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضَ أَن تَزُولَا ۚ وَلَئِن زَالَتَا
إِنْ أَمْسَكَهُمَا مِنْ أَحَدٍ مِّن بَعْدِهِ ۚ إِنَّهُ كَانَ حَلِيمًا غَفُورًا
Swahili
Hakika Mwenyezi Mungu ndiye anaye zuilia mbingu na ardhi zisiondoke. Na
zikiondoka hapana yeyote wa kuzizuia isipo kuwa Yeye. Hakika Yeye ni Mpole
Mwenye kusamehe.
|
Ayah 35:42 الأية
وَأَقْسَمُوا بِاللَّهِ جَهْدَ أَيْمَانِهِمْ لَئِن جَاءَهُمْ نَذِيرٌ
لَّيَكُونُنَّ أَهْدَىٰ مِنْ إِحْدَى الْأُمَمِ ۖ فَلَمَّا جَاءَهُمْ نَذِيرٌ مَّا
زَادَهُمْ إِلَّا نُفُورًا
Swahili
Na waliapa kwa Mwenyezi Mungu ukomo wa kuapa kwao, kwamba akiwajia mwonyaji bila
ya shaka watakuwa waongofu zaidi kuliko taifa jingine lolote. Lakini alipo wajia
mwonyaji hakuwazidishia ila kuikimbia hiyo Haki,
|
Ayah 35:43 الأية
اسْتِكْبَارًا فِي الْأَرْضِ وَمَكْرَ السَّيِّئِ ۚ وَلَا يَحِيقُ الْمَكْرُ
السَّيِّئُ إِلَّا بِأَهْلِهِ ۚ فَهَلْ يَنظُرُونَ إِلَّا سُنَّتَ الْأَوَّلِينَ ۚ
فَلَن تَجِدَ لِسُنَّتِ اللَّهِ تَبْدِيلًا ۖ وَلَن تَجِدَ لِسُنَّتِ اللَّهِ
تَحْوِيلًا
Swahili
Kwa kutakabari kwao katika nchi, na kufanya vitimbi vya uovu. Na vitimbi viovu
havimsibu ila mwenyewe aliye vifanya. Hebu hawangojei yalio wasibu watu wa kale?
Basi hutapata mabadiliko katika mtindo wa Mwenyezi Mungu. Wala hutapata mageuko
katika mwendo wa Mwenyezi Mungu.
|
Ayah 35:44 الأية
أَوَلَمْ يَسِيرُوا فِي الْأَرْضِ فَيَنظُرُوا كَيْفَ كَانَ عَاقِبَةُ الَّذِينَ
مِن قَبْلِهِمْ وَكَانُوا أَشَدَّ مِنْهُمْ قُوَّةً ۚ وَمَا كَانَ اللَّهُ
لِيُعْجِزَهُ مِن شَيْءٍ فِي السَّمَاوَاتِ وَلَا فِي الْأَرْضِ ۚ إِنَّهُ كَانَ
عَلِيمًا قَدِيرًا
Swahili
Je! Hawakusafiri katika ardhi wakaona vipi ulikuwa mwisho wa walio kuwa kabla
yao? Na hao walikuwa wana nguvu zaidi kuliko wao. Na hapana kitu kinacho weza
kumshinda Mwenyezi Mungu mbinguni wala katika ardhi. Hakika Yeye ni Mwenye
kujua, Mwenye uweza.
|
Ayah 35:45 الأية
وَلَوْ يُؤَاخِذُ اللَّهُ النَّاسَ بِمَا كَسَبُوا مَا تَرَكَ عَلَىٰ ظَهْرِهَا مِن
دَابَّةٍ وَلَٰكِن يُؤَخِّرُهُمْ إِلَىٰ أَجَلٍ مُّسَمًّى ۖ فَإِذَا جَاءَ
أَجَلُهُمْ فَإِنَّ اللَّهَ كَانَ بِعِبَادِهِ بَصِيرًا
Swahili
Na lau kuwa Mwenyezi Mungu angeli wachukulia watu kwa waliyo yachuma, basi
asingeli muacha juu ya ardhi hata mnyama mmoja. Lakini Yeye anawachukulia mpaka
ufike muda maalumu. Basi ukifika muda wao basi hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye
kuwaona waja wake baraabara.
|
©
EsinIslam.Com Designed & produced by The Awqaf London. Please pray for us
|