« Prev

68. Surah Al-Qalam سورة القلم

Next »



First Ayah   1   الأية الأولي
بِسْم ِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ
ن ۚ وَالْقَلَمِ وَمَا يَسْطُرُونَ
Swahili
 
Nuun. Naapa kwa kalamu na yale wayaandikayo,

Ayah   68:2   الأية
مَا أَنتَ بِنِعْمَةِ رَبِّكَ بِمَجْنُونٍ
Swahili
 
Kwa neema ya Mola wako Mlezi wewe si mwendawazimu.

Ayah   68:3   الأية
وَإِنَّ لَكَ لَأَجْرًا غَيْرَ مَمْنُونٍ
Swahili
 
Na kwa hakika wewe una malipo yasiyo katika.

Ayah   68:4   الأية
وَإِنَّكَ لَعَلَىٰ خُلُقٍ عَظِيمٍ
Swahili
 
Na hakika wewe una tabia tukufu.

Ayah   68:5   الأية
فَسَتُبْصِرُ وَيُبْصِرُونَ
Swahili
 
Karibu utaona, na wao wataona,

Ayah   68:6   الأية
بِأَييِّكُمُ الْمَفْتُونُ
Swahili
 
Ni nani kati yenu aliye pandwa na wazimu.

Ayah   68:7   الأية
إِنَّ رَبَّكَ هُوَ أَعْلَمُ بِمَن ضَلَّ عَن سَبِيلِهِ وَهُوَ أَعْلَمُ بِالْمُهْتَدِينَ
Swahili
 
Hakika Mola wako Mlezi ndiye Yeye ajuaye zaidi nani aliye ipotea Njia yake, na Yeye ndiye anaye wajua zaidi walio ongoka.

Ayah   68:8   الأية
فَلَا تُطِعِ الْمُكَذِّبِينَ
Swahili
 
Basi usiwat'ii wanao kadhibisha.

Ayah   68:9   الأية
وَدُّوا لَوْ تُدْهِنُ فَيُدْهِنُونَ
Swahili
 
Wanatamani lau unge lainisha ili nao wakulainishie.

Ayah   68:10   الأية
وَلَا تُطِعْ كُلَّ حَلَّافٍ مَّهِينٍ
Swahili
 
Wala usimt'ii kila mwingi wa kuapa wa kudharauliwa,

Ayah   68:11   الأية
هَمَّازٍ مَّشَّاءٍ بِنَمِيمٍ
Swahili
 
Mtapitapi, apitaye akifitini,

Ayah   68:12   الأية
مَّنَّاعٍ لِّلْخَيْرِ مُعْتَدٍ أَثِيمٍ
Swahili
 
Mwenye kuzuia kheri, dhaalimu, mwingi wa madhambi,

Ayah   68:13   الأية
عُتُلٍّ بَعْدَ ذَٰلِكَ زَنِيمٍ
Swahili
 
Mkavu, na juu ya hayo, mshari, amejipachika tu.

Ayah   68:14   الأية
أَن كَانَ ذَا مَالٍ وَبَنِينَ
Swahili
 
Ati kwa kuwa ana mali na watoto!

Ayah   68:15   الأية
إِذَا تُتْلَىٰ عَلَيْهِ آيَاتُنَا قَالَ أَسَاطِيرُ الْأَوَّلِينَ
Swahili
 
Anapo somewa Aya zetu, husema: Hizi ni simulizi za uwongo za watu wa zamani!

Ayah   68:16   الأية
سَنَسِمُهُ عَلَى الْخُرْطُومِ
Swahili
 
Tutamtia kovu juu ya pua yake.

Ayah   68:17   الأية
إِنَّا بَلَوْنَاهُمْ كَمَا بَلَوْنَا أَصْحَابَ الْجَنَّةِ إِذْ أَقْسَمُوا لَيَصْرِمُنَّهَا مُصْبِحِينَ
Swahili
 
Hakika tumewajaribu hawa kama tulivyo wajaribu wale wenye shamba, walipo apa kwamba watayavuna mazao yake itakapo kuwa asubuhi.

Ayah   68:18   الأية
وَلَا يَسْتَثْنُونَ
Swahili
 
Wala hawakusema: Mungu akipenda!

Ayah   68:19   الأية
فَطَافَ عَلَيْهَا طَائِفٌ مِّن رَّبِّكَ وَهُمْ نَائِمُونَ
Swahili
 
Basi lilitokea tukio juu yake kutoka kwa Mola wako Mlezi, nao wamelala!

Ayah   68:20   الأية
فَأَصْبَحَتْ كَالصَّرِيمِ
Swahili
 
Likawa kama usiku wa giza.

Ayah   68:21   الأية
فَتَنَادَوْا مُصْبِحِينَ
Swahili
 
Asubuhi wakaitana.

Ayah   68:22   الأية
أَنِ اغْدُوا عَلَىٰ حَرْثِكُمْ إِن كُنتُمْ صَارِمِينَ
Swahili
 
Ya kwamba nendeni kondeni mwenu ikiwa mnataka kuvuna.

Ayah   68:23   الأية
فَانطَلَقُوا وَهُمْ يَتَخَافَتُونَ
Swahili
 
Basi walikwenda na huku wakinong'onezana,

Ayah   68:24   الأية
أَن لَّا يَدْخُلَنَّهَا الْيَوْمَ عَلَيْكُم مِّسْكِينٌ
Swahili
 
Ya kuwa leo hata masikini mmoja asikuingilieni.

Ayah   68:25   الأية
وَغَدَوْا عَلَىٰ حَرْدٍ قَادِرِينَ
Swahili
 
Na walikwenda asubuhi, nao wameshikilia azimio hilo.

Ayah   68:26   الأية
فَلَمَّا رَأَوْهَا قَالُوا إِنَّا لَضَالُّونَ
Swahili
 
Basi walipo liona, wakasema: Hakika tumepotea!

Ayah   68:27   الأية
بَلْ نَحْنُ مَحْرُومُونَ
Swahili
 
Bali tumenyimwa!

Ayah   68:28   الأية
قَالَ أَوْسَطُهُمْ أَلَمْ أَقُل لَّكُمْ لَوْلَا تُسَبِّحُونَ
Swahili
 
Mbora wao akasema: Sikukwambieni, kwa nini hamumtakasi Mwenyezi Mungu?

Ayah   68:29   الأية
قَالُوا سُبْحَانَ رَبِّنَا إِنَّا كُنَّا ظَالِمِينَ
Swahili
 
Wakasema: Ametakasika Mola wetu Mlezi! Hakika sisi tulikuwa wenye kudhulumu.

Ayah   68:30   الأية
فَأَقْبَلَ بَعْضُهُمْ عَلَىٰ بَعْضٍ يَتَلَاوَمُونَ
Swahili
 
Basi wakakabiliana kulaumiana wao kwa wao.

Ayah   68:31   الأية
قَالُوا يَا وَيْلَنَا إِنَّا كُنَّا طَاغِينَ
Swahili
 
Wakasema: Ole wetu! Tulikuwa tumeikiuka mipaka!

Ayah   68:32   الأية
عَسَىٰ رَبُّنَا أَن يُبْدِلَنَا خَيْرًا مِّنْهَا إِنَّا إِلَىٰ رَبِّنَا رَاغِبُونَ
Swahili
 
Asaa Mola wetu Mlezi akatubadilishia lilio bora kuliko hili. Hakika sisi ni wenye kurejea kwa Mola wetu Mlezi.

Ayah   68:33   الأية
كَذَٰلِكَ الْعَذَابُ ۖ وَلَعَذَابُ الْآخِرَةِ أَكْبَرُ ۚ لَوْ كَانُوا يَعْلَمُونَ
Swahili
 
Namna hivi yanakuwa mateso, na bila ya shaka mateso ya Akhera ni makubwa zaidi, laiti wangeli jua!

Ayah   68:34   الأية
إِنَّ لِلْمُتَّقِينَ عِندَ رَبِّهِمْ جَنَّاتِ النَّعِيمِ
Swahili
 
Hakika wachamngu watakuwa na Bustani za neema kwa Mola wao Mlezi.

Ayah   68:35   الأية
أَفَنَجْعَلُ الْمُسْلِمِينَ كَالْمُجْرِمِينَ
Swahili
 
Kwani tutawafanya Waislamu kama wakosefu?

Ayah   68:36   الأية
مَا لَكُمْ كَيْفَ تَحْكُمُونَ
Swahili
 
Mna nini? Mnahukumu vipi?

Ayah   68:37   الأية
أَمْ لَكُمْ كِتَابٌ فِيهِ تَدْرُسُونَ
Swahili
 
Au mnacho kitabu ambacho ndani yake mnasoma?

Ayah   68:38   الأية
إِنَّ لَكُمْ فِيهِ لَمَا تَخَيَّرُونَ
Swahili
 
Kuwa mtapata humo mnayo yapenda?

Ayah   68:39   الأية
أَمْ لَكُمْ أَيْمَانٌ عَلَيْنَا بَالِغَةٌ إِلَىٰ يَوْمِ الْقِيَامَةِ ۙ إِنَّ لَكُمْ لَمَا تَحْكُمُونَ
Swahili
 
Au mnazo ahadi za viapo juu yetu za kufika Siku ya Kiyama ya kuwa hakika mtapata kila mnayo jihukumia?

Ayah   68:40   الأية
سَلْهُمْ أَيُّهُم بِذَٰلِكَ زَعِيمٌ
Swahili
 
Waulize: Ni nani miongoni mwao dhamini wa haya?

Ayah   68:41   الأية
أَمْ لَهُمْ شُرَكَاءُ فَلْيَأْتُوا بِشُرَكَائِهِمْ إِن كَانُوا صَادِقِينَ
Swahili
 
Au wanao washirika? Basi wawalete washirika wao wakiwa wanasema kweli.

Ayah   68:42   الأية
يَوْمَ يُكْشَفُ عَن سَاقٍ وَيُدْعَوْنَ إِلَى السُّجُودِ فَلَا يَسْتَطِيعُونَ
Swahili
 
Siku utakapo wekwa wazi mundi, na wataitwa kusujudu, lakini hawataweza,

Ayah   68:43   الأية
خَاشِعَةً أَبْصَارُهُمْ تَرْهَقُهُمْ ذِلَّةٌ ۖ وَقَدْ كَانُوا يُدْعَوْنَ إِلَى السُّجُودِ وَهُمْ سَالِمُونَ
Swahili
 
Macho yao yatainama chini, fedheha itawafunika. Na hakika walikuwa wakiitwa wasujudu walipo kuwa wazima -

Ayah   68:44   الأية
فَذَرْنِي وَمَن يُكَذِّبُ بِهَٰذَا الْحَدِيثِ ۖ سَنَسْتَدْرِجُهُم مِّنْ حَيْثُ لَا يَعْلَمُونَ
Swahili
 
Basi niache na wanao kadhibisha maneno haya! Tutawavutia kidogo kidogo kwa mahali wasipo pajua.

Ayah   68:45   الأية
وَأُمْلِي لَهُمْ ۚ إِنَّ كَيْدِي مَتِينٌ
Swahili
 
Na ninawapururia muhula; hakika hila zangu ni imara.

Ayah   68:46   الأية
أَمْ تَسْأَلُهُمْ أَجْرًا فَهُم مِّن مَّغْرَمٍ مُّثْقَلُونَ
Swahili
 
Au unawaomba ujira, na wao wanaemewa na gharama hiyo?

Ayah   68:47   الأية
أَمْ عِندَهُمُ الْغَيْبُ فَهُمْ يَكْتُبُونَ
Swahili
 
Au iko kwao siri, basi wao wanaiandika?

Ayah   68:48   الأية
فَاصْبِرْ لِحُكْمِ رَبِّكَ وَلَا تَكُن كَصَاحِبِ الْحُوتِ إِذْ نَادَىٰ وَهُوَ مَكْظُومٌ
Swahili
 
Basi ingojee hukumu ya Mola wako Mlezi, wala usiwe kama mmezwa na samaki, alipo nadi naye kazongwa.

Ayah   68:49   الأية
لَّوْلَا أَن تَدَارَكَهُ نِعْمَةٌ مِّن رَّبِّهِ لَنُبِذَ بِالْعَرَاءِ وَهُوَ مَذْمُومٌ
Swahili
 
Kama isingeli mfikia neema kutoka kwa Mola wake Mlezi, bila ya shaka angeli tupwa ufukweni naye ni mwenye kulaumiwa.

Ayah   68:50   الأية
فَاجْتَبَاهُ رَبُّهُ فَجَعَلَهُ مِنَ الصَّالِحِينَ
Swahili
 
Lakini Mola wake Mlezi alimteua na akamfanya miongoni mwa watu wema.

Ayah   68:51   الأية
وَإِن يَكَادُ الَّذِينَ كَفَرُوا لَيُزْلِقُونَكَ بِأَبْصَارِهِمْ لَمَّا سَمِعُوا الذِّكْرَ وَيَقُولُونَ إِنَّهُ لَمَجْنُونٌ
Swahili
 
Na walio kufuru hukaribia kukutelezesha kwa macho yao, wanapo sikia mawaidha, na wanasema: Hakika yeye ni mwendawazimu.

Ayah   68:52   الأية
وَمَا هُوَ إِلَّا ذِكْرٌ لِّلْعَالَمِينَ
Swahili
 
Na hayakuwa haya, ila ni ukumbusho kwa walimwengu wote.
 


© EsinIslam.Com Designed & produced by The Awqaf London. Please pray for us