« Prev

81. Surah At-Takwîr سورة التكوير

Next »



First Ayah   1   الأية الأولي
بِسْم ِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ
إِذَا الشَّمْسُ كُوِّرَتْ
Swahili
 
Jua litakapo kunjwa,

Ayah   81:2   الأية
وَإِذَا النُّجُومُ انكَدَرَتْ
Swahili
 
Na nyota zikazimwa,

Ayah   81:3   الأية
وَإِذَا الْجِبَالُ سُيِّرَتْ
Swahili
 
Na milima ikaondolewa,

Ayah   81:4   الأية
وَإِذَا الْعِشَارُ عُطِّلَتْ
Swahili
 
Na ngamia wenye mimba pevu watakapo achwa wasishughulikiwe,

Ayah   81:5   الأية
وَإِذَا الْوُحُوشُ حُشِرَتْ
Swahili
 
Na wanyama wa mwituni wakakusanywa,

Ayah   81:6   الأية
وَإِذَا الْبِحَارُ سُجِّرَتْ
Swahili
 
Na bahari zikawaka moto,

Ayah   81:7   الأية
وَإِذَا النُّفُوسُ زُوِّجَتْ
Swahili
 
Na nafsi zikaunganishwa,

Ayah   81:8   الأية
وَإِذَا الْمَوْءُودَةُ سُئِلَتْ
Swahili
 
Na msichana aliye zikwa hai atapo ulizwa,

Ayah   81:9   الأية
بِأَيِّ ذَنبٍ قُتِلَتْ
Swahili
 
Kwa kosa gani aliuliwa?

Ayah   81:10   الأية
وَإِذَا الصُّحُفُ نُشِرَتْ
Swahili
 
Na madaftari yatakapo enezwa,

Ayah   81:11   الأية
وَإِذَا السَّمَاءُ كُشِطَتْ
Swahili
 
Na mbingu itapo tanduliwa,

Ayah   81:12   الأية
وَإِذَا الْجَحِيمُ سُعِّرَتْ
Swahili
 
Na Jahannamu itapo chochewa,

Ayah   81:13   الأية
وَإِذَا الْجَنَّةُ أُزْلِفَتْ
Swahili
 
Na Pepo ikasogezwa,

Ayah   81:14   الأية
عَلِمَتْ نَفْسٌ مَّا أَحْضَرَتْ
Swahili
 
Kila nafsi itajua ilicho kihudhurisha.

Ayah   81:15   الأية
فَلَا أُقْسِمُ بِالْخُنَّسِ
Swahili
 
Naapa kwa nyota zinapo rejea nyuma,

Ayah   81:16   الأية
الْجَوَارِ الْكُنَّسِ
Swahili
 
Zinazo kwenda, kisha zikajificha,

Ayah   81:17   الأية
وَاللَّيْلِ إِذَا عَسْعَسَ
Swahili
 
Na kwa usiku unapo pungua,

Ayah   81:18   الأية
وَالصُّبْحِ إِذَا تَنَفَّسَ
Swahili
 
Na kwa asubuhi inapo pambazuka,

Ayah   81:19   الأية
إِنَّهُ لَقَوْلُ رَسُولٍ كَرِيمٍ
Swahili
 
Kwamba hakika bila ya shaka hii ni kauli ya Mjumbe mtukufu,

Ayah   81:20   الأية
ذِي قُوَّةٍ عِندَ ذِي الْعَرْشِ مَكِينٍ
Swahili
 
Mwenye nguvu na mwenye cheo kwa huyo Mwenye Kiti cha Enzi,

Ayah   81:21   الأية
مُّطَاعٍ ثَمَّ أَمِينٍ
Swahili
 
Anaye t'iiwa, tena muaminifu.

Ayah   81:22   الأية
وَمَا صَاحِبُكُم بِمَجْنُونٍ
Swahili
 
Na wala huyu mwenzenu hana wazimu.

Ayah   81:23   الأية
وَلَقَدْ رَآهُ بِالْأُفُقِ الْمُبِينِ
Swahili
 
Na hakika yeye alimwona kwenye upeo wa macho ulio safi.

Ayah   81:24   الأية
وَمَا هُوَ عَلَى الْغَيْبِ بِضَنِينٍ
Swahili
 
Wala yeye si bakhili kwa mambo ya ghaibu.

Ayah   81:25   الأية
وَمَا هُوَ بِقَوْلِ شَيْطَانٍ رَّجِيمٍ
Swahili
 
Wala hii si kauli ya Shetani maluuni.

Ayah   81:26   الأية
فَأَيْنَ تَذْهَبُونَ
Swahili
 
Basi mnakwenda wapi?

Ayah   81:27   الأية
إِنْ هُوَ إِلَّا ذِكْرٌ لِّلْعَالَمِينَ
Swahili
 
Haikuwa hii ila ni ukumbusho kwa walimwengu wote.

Ayah   81:28   الأية
لِمَن شَاءَ مِنكُمْ أَن يَسْتَقِيمَ
Swahili
 
Kwa yule miongoni mwenu anaye taka kwenda sawa.

Ayah   81:29   الأية
وَمَا تَشَاءُونَ إِلَّا أَن يَشَاءَ اللَّهُ رَبُّ الْعَالَمِينَ
Swahili
 
Wala nyinyi hamtataka isipo kuwa atake Mwenyezi Mungu Mola Mlezi wa walimwengu wote.
 


© EsinIslam.Com Designed & produced by The Awqaf London. Please pray for us