« Prev
81. Surah At-Takwîr سورة التكوير
Next »
First Ayah 1 الأية الأوليبِسْم ِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ
إِذَا الشَّمْسُ كُوِّرَتْ
Swahili
Jua litakapo kunjwa,
|
Ayah 81:2 الأية
وَإِذَا النُّجُومُ انكَدَرَتْ
Swahili
Na nyota zikazimwa,
|
Ayah 81:3 الأية
وَإِذَا الْجِبَالُ سُيِّرَتْ
Swahili
Na milima ikaondolewa,
|
Ayah 81:4 الأية
وَإِذَا الْعِشَارُ عُطِّلَتْ
Swahili
Na ngamia wenye mimba pevu watakapo achwa wasishughulikiwe,
|
Ayah 81:5 الأية
وَإِذَا الْوُحُوشُ حُشِرَتْ
Swahili
Na wanyama wa mwituni wakakusanywa,
|
Ayah 81:6 الأية
وَإِذَا الْبِحَارُ سُجِّرَتْ
Swahili
Na bahari zikawaka moto,
|
Ayah 81:7 الأية
وَإِذَا النُّفُوسُ زُوِّجَتْ
Swahili
Na nafsi zikaunganishwa,
|
Ayah 81:8 الأية
وَإِذَا الْمَوْءُودَةُ سُئِلَتْ
Swahili
Na msichana aliye zikwa hai atapo ulizwa,
|
Ayah 81:9 الأية
بِأَيِّ ذَنبٍ قُتِلَتْ
Swahili
Kwa kosa gani aliuliwa?
|
Ayah 81:10 الأية
وَإِذَا الصُّحُفُ نُشِرَتْ
Swahili
Na madaftari yatakapo enezwa,
|
Ayah 81:11 الأية
وَإِذَا السَّمَاءُ كُشِطَتْ
Swahili
Na mbingu itapo tanduliwa,
|
Ayah 81:12 الأية
وَإِذَا الْجَحِيمُ سُعِّرَتْ
Swahili
Na Jahannamu itapo chochewa,
|
Ayah 81:13 الأية
وَإِذَا الْجَنَّةُ أُزْلِفَتْ
Swahili
Na Pepo ikasogezwa,
|
Ayah 81:14 الأية
عَلِمَتْ نَفْسٌ مَّا أَحْضَرَتْ
Swahili
Kila nafsi itajua ilicho kihudhurisha.
|
Ayah 81:15 الأية
فَلَا أُقْسِمُ بِالْخُنَّسِ
Swahili
Naapa kwa nyota zinapo rejea nyuma,
|
Ayah 81:16 الأية
الْجَوَارِ الْكُنَّسِ
Swahili
Zinazo kwenda, kisha zikajificha,
|
Ayah 81:17 الأية
وَاللَّيْلِ إِذَا عَسْعَسَ
Swahili
Na kwa usiku unapo pungua,
|
Ayah 81:18 الأية
وَالصُّبْحِ إِذَا تَنَفَّسَ
Swahili
Na kwa asubuhi inapo pambazuka,
|
Ayah 81:19 الأية
إِنَّهُ لَقَوْلُ رَسُولٍ كَرِيمٍ
Swahili
Kwamba hakika bila ya shaka hii ni kauli ya Mjumbe mtukufu,
|
Ayah 81:20 الأية
ذِي قُوَّةٍ عِندَ ذِي الْعَرْشِ مَكِينٍ
Swahili
Mwenye nguvu na mwenye cheo kwa huyo Mwenye Kiti cha Enzi,
|
Ayah 81:21 الأية
مُّطَاعٍ ثَمَّ أَمِينٍ
Swahili
Anaye t'iiwa, tena muaminifu.
|
Ayah 81:22 الأية
وَمَا صَاحِبُكُم بِمَجْنُونٍ
Swahili
Na wala huyu mwenzenu hana wazimu.
|
Ayah 81:23 الأية
وَلَقَدْ رَآهُ بِالْأُفُقِ الْمُبِينِ
Swahili
Na hakika yeye alimwona kwenye upeo wa macho ulio safi.
|
Ayah 81:24 الأية
وَمَا هُوَ عَلَى الْغَيْبِ بِضَنِينٍ
Swahili
Wala yeye si bakhili kwa mambo ya ghaibu.
|
Ayah 81:25 الأية
وَمَا هُوَ بِقَوْلِ شَيْطَانٍ رَّجِيمٍ
Swahili
Wala hii si kauli ya Shetani maluuni.
|
Ayah 81:26 الأية
فَأَيْنَ تَذْهَبُونَ
Swahili
Basi mnakwenda wapi?
|
Ayah 81:27 الأية
إِنْ هُوَ إِلَّا ذِكْرٌ لِّلْعَالَمِينَ
Swahili
Haikuwa hii ila ni ukumbusho kwa walimwengu wote.
|
Ayah 81:28 الأية
لِمَن شَاءَ مِنكُمْ أَن يَسْتَقِيمَ
Swahili
Kwa yule miongoni mwenu anaye taka kwenda sawa.
|
Ayah 81:29 الأية
وَمَا تَشَاءُونَ إِلَّا أَن يَشَاءَ اللَّهُ رَبُّ الْعَالَمِينَ
Swahili
Wala nyinyi hamtataka isipo kuwa atake Mwenyezi Mungu Mola Mlezi wa walimwengu
wote.
|
©
EsinIslam.Com Designed & produced by The Awqaf London. Please pray for us
|
|