1st Ayah 1 الأية ١الأوليبِسْم ِ اللهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ
طسم
Ta-seen-meem
Swahili
T'aa Siin Miim. (T'.S.M.)
|
Ayah 26:2 الأية
تِلْكَ آيَاتُ الْكِتَابِ الْمُبِينِ
Tilka ayatu alkitabialmubeen
Swahili
Hizi ni Aya za Kitabu kinacho bainisha.
|
Ayah 26:3 الأية
لَعَلَّكَ بَاخِعٌ نَّفْسَكَ أَلَّا يَكُونُوا مُؤْمِنِينَ
LaAAallaka bakhiAAun nafsaka allayakoonoo mu/mineen
Swahili
Huenda labda ukajikera nafsi yako kwa kuwa hawawi Waumini.
|
Ayah 26:4 الأية
إِن نَّشَأْ نُنَزِّلْ عَلَيْهِم مِّنَ السَّمَاءِ آيَةً فَظَلَّتْ أَعْنَاقُهُمْ
لَهَا خَاضِعِينَ
In nasha/ nunazzil AAalayhim mina assama-iayatan fathallat aAAnaquhum
lahakhadiAAeen
Swahili
Tunge penda tungeli wateremshia kutoka mbinguni Ishara zikanyenyekea shingo zao.
|
Ayah 26:5 الأية
وَمَا يَأْتِيهِم مِّن ذِكْرٍ مِّنَ الرَّحْمَٰنِ مُحْدَثٍ إِلَّا كَانُوا عَنْهُ
مُعْرِضِينَ
Wama ya/teehim min thikrin minaarrahmani muhdathin illa kanooAAanhu muAArideen
Swahili
Wala hauwafikii ukumbusho mpya kutoka kwa Arrahman ila wao hujitenga nao.
|
Ayah 26:6 الأية
فَقَدْ كَذَّبُوا فَسَيَأْتِيهِمْ أَنبَاءُ مَا كَانُوا بِهِ يَسْتَهْزِئُونَ
Faqad kaththaboo fasaya/teehim anbaoma kanoo bihi yastahzi-oon
Swahili
Kwa yakini wamekanusha; kwa hivyo zitakuja wafikia khabari za yale waliyo kuwa
wakiyafanyia mzaha.
|
Ayah 26:7 الأية
أَوَلَمْ يَرَوْا إِلَى الْأَرْضِ كَمْ أَنبَتْنَا فِيهَا مِن كُلِّ زَوْجٍ كَرِيمٍ
Awa lam yaraw ila al-ardi kamanbatna feeha min kulli zawjin kareem
Swahili
Je! Hawakuiona ardhi, mimea mingapi tumeiotesha humo, ya kila namna nzuri?
|
Ayah 26:8 الأية
إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَةً ۖ وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ
Inna fee thalika laayatan wamakana aktharuhum mu/mineen
Swahili
Hakika katika haya zipo Ishara. Lakini wengi wao hawakuwa wenye kuamini.
|
Ayah 26:9 الأية
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ الْعَزِيزُ الرَّحِيمُ
Wa-inna rabbaka lahuwa alAAazeezu arraheem
Swahili
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Yeye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.
|
Ayah 26:10 الأية
وَإِذْ نَادَىٰ رَبُّكَ مُوسَىٰ أَنِ ائْتِ الْقَوْمَ الظَّالِمِينَ
Wa-ith nada rabbukamoosa ani i/ti alqawma aththalimeen
Swahili
Na Mola wako Mlezi, alipo mwita Musa, akamwambia: Fika kwa watu madhaalimu,
|
Ayah 26:11 الأية
قَوْمَ فِرْعَوْنَ ۚ أَلَا يَتَّقُونَ
Qawma firAAawna ala yattaqoon
Swahili
Watu wa Firauni. Hawaogopi?
|
Ayah 26:12 الأية
قَالَ رَبِّ إِنِّي أَخَافُ أَن يُكَذِّبُونِ
Qala rabbi innee akhafu anyukaththiboon
Swahili
Akasema: Hakika mimi nachelea wasinikanushe.
|
Ayah 26:13 الأية
وَيَضِيقُ صَدْرِي وَلَا يَنطَلِقُ لِسَانِي فَأَرْسِلْ إِلَىٰ هَارُونَ
Wayadeequ sadree walayantaliqu lisanee faarsil ila haroon
Swahili
Na kifua changu kina dhiki, na ulimi wangu haukunjuki vyema. Basi mtumie ujumbe
Harun.
|
Ayah 26:14 الأية
وَلَهُمْ عَلَيَّ ذَنبٌ فَأَخَافُ أَن يَقْتُلُونِ
Walahum AAalayya thanbun faakhafuan yaqtuloon
Swahili
Na wao wana kisasi juu yangu, kwa hivyo naogopa wasije kuniuwa.
|
Ayah 26:15 الأية
قَالَ كَلَّا ۖ فَاذْهَبَا بِآيَاتِنَا ۖ إِنَّا مَعَكُم مُّسْتَمِعُونَ
Qala kalla fathhababi-ayatina inna maAAakum mustamiAAoon
Swahili
Akasema: Siyo hivyo kabisa! Nendeni na miujiza yetu. Hakika Sisi tu pamoja
nanyi, tunasikiliza.
|
Ayah 26:16 الأية
فَأْتِيَا فِرْعَوْنَ فَقُولَا إِنَّا رَسُولُ رَبِّ الْعَالَمِينَ
Fa/tiya firAAawna faqoola innarasoolu rabbi alAAalameen
Swahili
Basi mfikieni Firauni na mwambieni: Hakika sisi ni Mitume wa Mola Mlezi wa
walimwengu wote.
|
Ayah 26:17 الأية
أَنْ أَرْسِلْ مَعَنَا بَنِي إِسْرَائِيلَ
An arsil maAAana banee isra-eel
Swahili
Waachilie Wana wa Israili wende nasi.
|
Ayah 26:18 الأية
قَالَ أَلَمْ نُرَبِّكَ فِينَا وَلِيدًا وَلَبِثْتَ فِينَا مِنْ عُمُرِكَ سِنِينَ
Qala alam nurabbika feenawaleedan walabithta feena min AAumurika sineen
Swahili
(Firauni) akasema: Sisi hatukukulea wewe utotoni, na ukakaa kwetu katika umri
wako miaka mingi?
|
Ayah 26:19 الأية
وَفَعَلْتَ فَعْلَتَكَ الَّتِي فَعَلْتَ وَأَنتَ مِنَ الْكَافِرِينَ
WafaAAalta faAAlataka allatee faAAaltawaanta mina alkafireen
Swahili
Na ukatenda kitendo chako ulicho tenda, nawe ukawa miongoni mwa wasio na
shukrani?
|
Ayah 26:20 الأية
قَالَ فَعَلْتُهَا إِذًا وَأَنَا مِنَ الضَّالِّينَ
Qala faAAaltuha ithanwaana mina addalleen
Swahili
(Musa) akasema: Nilitenda hayo hapo nilipo kuwa miongoni mwa wale walio potea.
|
Ayah 26:21 الأية
فَفَرَرْتُ مِنكُمْ لَمَّا خِفْتُكُمْ فَوَهَبَ لِي رَبِّي حُكْمًا وَجَعَلَنِي
مِنَ الْمُرْسَلِينَ
Fafarartu minkum lamma khiftukumfawahaba lee rabbee hukman wajaAAalanee mina
almursaleen
Swahili
Basi nikakukimbieni nilipo kuogopeni, tena Mola wangu Mlezi akanitunukia hukumu,
na akanijaalia niwe miongoni mwa Mitume.
|
Ayah 26:22 الأية
وَتِلْكَ نِعْمَةٌ تَمُنُّهَا عَلَيَّ أَنْ عَبَّدتَّ بَنِي إِسْرَائِيلَ
Watilka niAAmatun tamunnuha AAalayyaan AAabbadta banee isra-eel
Swahili
Na hiyo ndiyo neema ya kunisumbulia, na wewe umewatia utumwani Wana wa Israili?
|
Ayah 26:23 الأية
قَالَ فِرْعَوْنُ وَمَا رَبُّ الْعَالَمِينَ
Qala firAAawnu wama rabbu alAAalameen
Swahili
Firauni akasema: Na nani huyo Mola Mlezi wa walimwengu wote?
|
Ayah 26:24 الأية
قَالَ رَبُّ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَمَا بَيْنَهُمَا ۖ إِن كُنتُم مُّوقِنِينَ
Qala rabbu assamawatiwal-ardi wama baynahuma in kuntummooqineen
Swahili
Akasema: Ndiye Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, na viliomo baina yao, ikiwa nyinyi
ni wenye yakini.
|
Ayah 26:25 الأية
قَالَ لِمَنْ حَوْلَهُ أَلَا تَسْتَمِعُونَ
Qala liman hawlahu alatastamiAAoon
Swahili
(Firauni) akawaambia walio mzunguka: Hamsikilizi?
|
Ayah 26:26 الأية
قَالَ رَبُّكُمْ وَرَبُّ آبَائِكُمُ الْأَوَّلِينَ
Qala rabbukum warabbu aba-ikumual-awwaleen
Swahili
(Musa) akasema: Ndiye Mola wenu Mlezi, na Mola Mlezi wa baba zenu wa kwanza.
|
Ayah 26:27 الأية
قَالَ إِنَّ رَسُولَكُمُ الَّذِي أُرْسِلَ إِلَيْكُمْ لَمَجْنُونٌ
Qala inna rasoolakumu allatheeorsila ilaykum lamajnoon
Swahili
(Firauni) akasema: Hakika huyu Mtume wenu aliye tumwa kwenu ni mwendawazimu.
|
Ayah 26:28 الأية
قَالَ رَبُّ الْمَشْرِقِ وَالْمَغْرِبِ وَمَا بَيْنَهُمَا ۖ إِن كُنتُمْ
تَعْقِلُونَ
Qala rabbu almashriqi walmaghribiwama baynahuma in kuntum taAAqiloon
Swahili
(Musa) akasema: Ndiye Mola Mlezi wa Mashariki na Magharibi na viliomo baina yao,
ikiwa nyinyi mnatia akilini.
|
Ayah 26:29 الأية
قَالَ لَئِنِ اتَّخَذْتَ إِلَٰهًا غَيْرِي لَأَجْعَلَنَّكَ مِنَ الْمَسْجُونِينَ
Qala la-ini ittakhathta ilahanghayree laajAAalannaka mina almasjooneen
Swahili
(Firauni) akasema: Ukimfuata mungu mwengine asiye kuwa mimi, basi bila ya shaka
nitakufunga gerezani.
|
Ayah 26:30 الأية
قَالَ أَوَلَوْ جِئْتُكَ بِشَيْءٍ مُّبِينٍ
Qala awa law ji/tuka bishay-in mubeen
Swahili
Akasema: Je! Ijapo kuwa nitakuletea kitu cha kubainisha wazi?
|
Ayah 26:31 الأية
قَالَ فَأْتِ بِهِ إِن كُنتَ مِنَ الصَّادِقِينَ
Qala fa/ti bihi in kunta mina assadiqeen
Swahili
Akasema: Kilete basi, kama wewe ni katika wasemao kweli.
|
Ayah 26:32 الأية
فَأَلْقَىٰ عَصَاهُ فَإِذَا هِيَ ثُعْبَانٌ مُّبِينٌ
Faalqa AAasahu fa-ithahiya thuAAbanun mubeen
Swahili
Basi akaitupa fimbo yake, mara ikawa nyoka wa kuonekana dhaahiri.
|
Ayah 26:33 الأية
وَنَزَعَ يَدَهُ فَإِذَا هِيَ بَيْضَاءُ لِلنَّاظِرِينَ
WanazaAAa yadahu fa-itha hiya baydaolinnathireen
Swahili
Na akautoa mkono wake, na mara ukawa mweupe kwa watazamao.
|
Ayah 26:34 الأية
قَالَ لِلْمَلَإِ حَوْلَهُ إِنَّ هَٰذَا لَسَاحِرٌ عَلِيمٌ
Qala lilmala-i hawlahu inna hathalasahirun AAaleem
Swahili
(Firauni) akawaambia waheshimiwa walio mzunguka: Hakika huyu ni mchawi mtaalamu.
|
Ayah 26:35 الأية
يُرِيدُ أَن يُخْرِجَكُم مِّنْ أَرْضِكُم بِسِحْرِهِ فَمَاذَا تَأْمُرُونَ
Yureedu an yukhrijakum min ardikumbisihrihi famatha ta/muroon
Swahili
Anataka kukutoeni katika nchi yenu kwa uchawi wake. Basi mna shauri gani?
|
Ayah 26:36 الأية
قَالُوا أَرْجِهْ وَأَخَاهُ وَابْعَثْ فِي الْمَدَائِنِ حَاشِرِينَ
Qaloo arjih waakhahu wabAAathfee almada-ini hashireen
Swahili
Wakasema: Mpe muda yeye na nduguye na uwatume mijini wapigao mbiu ya mgambo.
|
Ayah 26:37 الأية
يَأْتُوكَ بِكُلِّ سَحَّارٍ عَلِيمٍ
Ya/tooka bikulli sahharin AAaleem
Swahili
Wakuletee kila mchawi bingwa mtaalamu.
|
Ayah 26:38 الأية
فَجُمِعَ السَّحَرَةُ لِمِيقَاتِ يَوْمٍ مَّعْلُومٍ
FajumiAAa assaharatu limeeqatiyawmin maAAloom
Swahili
Basi wakakusanywa wachawi wakati na siku maalumu.
|
Ayah 26:39 الأية
وَقِيلَ لِلنَّاسِ هَلْ أَنتُم مُّجْتَمِعُونَ
Waqeela linnasi hal antummujtamiAAoon
Swahili
Na watu wakaambiwa: Je! Mtakusanyika?
|
Ayah 26:40 الأية
لَعَلَّنَا نَتَّبِعُ السَّحَرَةَ إِن كَانُوا هُمُ الْغَالِبِينَ
LaAAallana nattabiAAu assaharatain kanoo humu alghalibeen
Swahili
Huenda tutawafuata wachawi wakiwa wao ndio watakao shinda.
|
Ayah 26:41 الأية
فَلَمَّا جَاءَ السَّحَرَةُ قَالُوا لِفِرْعَوْنَ أَئِنَّ لَنَا لَأَجْرًا إِن
كُنَّا نَحْنُ الْغَالِبِينَ
Falamma jaa assaharatuqaloo lifirAAawna a-inna lana laajran in kunnanahnu
alghalibeen
Swahili
Basi walipo kuja wachawi wakamwambia Firauni: Je! Tutapata ujira tukiwa sisi
ndio tulio shinda?
|
Ayah 26:42 الأية
قَالَ نَعَمْ وَإِنَّكُمْ إِذًا لَّمِنَ الْمُقَرَّبِينَ
Qala naAAam wa-innakum ithanlamina almuqarrabeen
Swahili
Naam! Na hakika mtakuwa katika watu wa mbele.
|
Ayah 26:43 الأية
قَالَ لَهُم مُّوسَىٰ أَلْقُوا مَا أَنتُم مُّلْقُونَ
Qala lahum moosa alqoo maantum mulqoon
Swahili
Musa akwaambia: Tupeni mnavyo taka kutupa.
|
Ayah 26:44 الأية
فَأَلْقَوْا حِبَالَهُمْ وَعِصِيَّهُمْ وَقَالُوا بِعِزَّةِ فِرْعَوْنَ إِنَّا
لَنَحْنُ الْغَالِبُونَ
Faalqaw hibalahum waAAisiyyahumwaqaloo biAAizzati firAAawna inna
lanahnualghaliboon
Swahili
Basi wakatupa kamba zao na fimbo zao, na wakasema: Kwa nguvu za Firauni hakika
sisi hapana shaka ni wenye kushinda.
|
Ayah 26:45 الأية
فَأَلْقَىٰ مُوسَىٰ عَصَاهُ فَإِذَا هِيَ تَلْقَفُ مَا يَأْفِكُونَ
Faalqa moosa AAasahufa-itha hiya talqafu ma ya/fikoon
Swahili
Musa tena akatupa fimbo yake, nayo mara ikavimeza walivyo vizua.
|
Ayah 26:46 الأية
فَأُلْقِيَ السَّحَرَةُ سَاجِدِينَ
Faolqiya assaharatu sajideen
Swahili
Hapo wachawi walipinduka wakasujudu.
|
Ayah 26:47 الأية
قَالُوا آمَنَّا بِرَبِّ الْعَالَمِينَ
Qaloo amanna birabbialAAalameen
Swahili
Wakasema: Tunamuamini Mola Mlezi wa walimwengu wote.
|
Ayah 26:48 الأية
رَبِّ مُوسَىٰ وَهَارُونَ
Rabbi moosa waharoon
Swahili
Mola Mlezi wa Musa na Harun.
|
Ayah 26:49 الأية
قَالَ آمَنتُمْ لَهُ قَبْلَ أَنْ آذَنَ لَكُمْ ۖ إِنَّهُ لَكَبِيرُكُمُ الَّذِي
عَلَّمَكُمُ السِّحْرَ فَلَسَوْفَ تَعْلَمُونَ ۚ لَأُقَطِّعَنَّ أَيْدِيَكُمْ
وَأَرْجُلَكُم مِّنْ خِلَافٍ وَلَأُصَلِّبَنَّكُمْ أَجْمَعِينَ
Qala amantum lahu qabla an athanalakum innahu lakabeerukumu allathee
AAallamakumu assihrafalasawfa taAAlamoona laoqattiAAanna aydiyakum
waarjulakummin khilafin walaosallibannakum ajmaAAeen
Swahili
(Firauni) akasema: Je! Mmemuamini kabla sijakuruhusuni? Bila ya shaka yeye basi
ndiye mkubwa wenu aliye kufunzeni uchawi. Basi mtakuja jua! Nitakata mikono yenu
na miguu yenu kwa kutafautisha. Na nitakubandikeni misalabani nyote.
|
Ayah 26:50 الأية
قَالُوا لَا ضَيْرَ ۖ إِنَّا إِلَىٰ رَبِّنَا مُنقَلِبُونَ
Qaloo la dayra innaila rabbina munqaliboon
Swahili
Wakasema: Haidhuru, kwani sisi ni wenye kurejea kwa Mola wetu Mlezi.
|
Ayah 26:51 الأية
إِنَّا نَطْمَعُ أَن يَغْفِرَ لَنَا رَبُّنَا خَطَايَانَا أَن كُنَّا أَوَّلَ
الْمُؤْمِنِينَ
Inna natmaAAu an yaghfira lanarabbuna khatayana an kunnaawwala almu/mineen
Swahili
Hakika sisi tunatumai Mola wetu Mlezi atatusamehe makosa yetu, kwa kuwa ndio wa
kwanza wa kuamini.
|
Ayah 26:52 الأية
وَأَوْحَيْنَا إِلَىٰ مُوسَىٰ أَنْ أَسْرِ بِعِبَادِي إِنَّكُم مُّتَّبَعُونَ
Waawhayna ila moosaan asri biAAibadee innakum muttabaAAoon
Swahili
Na tulimuamrisha Musa kwa wahyi: Nenda na waja wangu wakati wa usiku. Kwa hakika
mtafuatwa.
|
Ayah 26:53 الأية
فَأَرْسَلَ فِرْعَوْنُ فِي الْمَدَائِنِ حَاشِرِينَ
Faarsala firAAawnu fee almada-ini hashireen
Swahili
Basi Firauni akawatuma mijini wapiga mbiu za mgambo.
|
Ayah 26:54 الأية
إِنَّ هَٰؤُلَاءِ لَشِرْذِمَةٌ قَلِيلُونَ
Inna haola-i lashirthimatunqaleeloon
Swahili
(Wakieneza): Hakika hawa ni kikundi kidogo.
|
Ayah 26:55 الأية
وَإِنَّهُمْ لَنَا لَغَائِظُونَ
Wa-innahum lana lagha-ithoon
Swahili
Nao wanatuudhi.
|
Ayah 26:56 الأية
وَإِنَّا لَجَمِيعٌ حَاذِرُونَ
Wa-inna lajameeAAun hathiroon
Swahili
Na sisi ni wengi, wenye kuchukua hadhari.
|
Ayah 26:57 الأية
فَأَخْرَجْنَاهُم مِّن جَنَّاتٍ وَعُيُونٍ
Faakhrajnahum min jannatinwaAAuyoon
Swahili
Basi tukawatoa katika mabustani na chemchem,
|
Ayah 26:58 الأية
وَكُنُوزٍ وَمَقَامٍ كَرِيمٍ
Wakunoozin wamaqamin kareem
Swahili
Na makhazina, na vyeo vya hishima,
|
Ayah 26:59 الأية
كَذَٰلِكَ وَأَوْرَثْنَاهَا بَنِي إِسْرَائِيلَ
Kathalika waawrathnahabanee isra-eel
Swahili
Kadhaalika; na tukawarithisha hayo Wana wa Israili.
|
Ayah 26:60 الأية
فَأَتْبَعُوهُم مُّشْرِقِينَ
FaatbaAAoohum mushriqeen
Swahili
Basi wakawafuata lilipo chomoza jua.
|
Ayah 26:61 الأية
فَلَمَّا تَرَاءَى الْجَمْعَانِ قَالَ أَصْحَابُ مُوسَىٰ إِنَّا لَمُدْرَكُونَ
Falamma taraa aljamAAaniqala as-habu moosa innalamudrakoon
Swahili
Na yalipo onana majeshi mawili haya, watu wa Musa wakasema: Hakika sisi bila ya
shaka tumepatikana!
|
Ayah 26:62 الأية
قَالَ كَلَّا ۖ إِنَّ مَعِيَ رَبِّي سَيَهْدِينِ
Qala kalla inna maAAiya rabbeesayahdeen
Swahili
(Musa) akasema: Hasha! Hakika yu pamoja nami Mola wangu Mlezi. Yeye ataniongoa!
|
Ayah 26:63 الأية
فَأَوْحَيْنَا إِلَىٰ مُوسَىٰ أَنِ اضْرِب بِّعَصَاكَ الْبَحْرَ ۖ فَانفَلَقَ
فَكَانَ كُلُّ فِرْقٍ كَالطَّوْدِ الْعَظِيمِ
Faawhayna ila moosaani idrib biAAasaka albahra fanfalaqafakana kullu firqin
kattawdi alAAatheem
Swahili
Tulimletea wahyi Musa tukamwambia: Piga bahari kwa fimbo yako. Basi ikatengana,
na kila sehemu ikawa kama mlima mkubwa.
|
Ayah 26:64 الأية
وَأَزْلَفْنَا ثَمَّ الْآخَرِينَ
Waazlafna thamma al-akhareen
Swahili
Na tukawajongeza hapo wale wengine.
|
Ayah 26:65 الأية
وَأَنجَيْنَا مُوسَىٰ وَمَن مَّعَهُ أَجْمَعِينَ
Waanjayna moosa waman maAAahuajmaAAeen
Swahili
Tukawaokoa Musa na walio kuwa pamoja naye wote.
|
Ayah 26:66 الأية
ثُمَّ أَغْرَقْنَا الْآخَرِينَ
Thumma aghraqna al-akhareen
Swahili
Kisha tukawazamisha hao wengine.
|
Ayah 26:67 الأية
إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَةً ۖ وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ
Inna fee thalika laayatan wamakana aktharuhum mu/mineen
Swahili
Hakika bila ya shaka katika hayo ipo Ishara; lakini wengi wao si katika wenye
kuamini.
|
Ayah 26:68 الأية
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ الْعَزِيزُ الرَّحِيمُ
Wa-inna rabbaka lahuwa alAAazeezu arraheem
Swahili
Na kwa hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.
|
Ayah 26:69 الأية
وَاتْلُ عَلَيْهِمْ نَبَأَ إِبْرَاهِيمَ
Watlu AAalayhim nabaa ibraheem
Swahili
Na wasomee khabari za Ibrahim.
|
Ayah 26:70 الأية
إِذْ قَالَ لِأَبِيهِ وَقَوْمِهِ مَا تَعْبُدُونَ
Ith qala li-abeehi waqawmihi mataAAbudoon
Swahili
Alipo mwambia baba yake na kaumu yake: Mnaabudu nini?
|
Ayah 26:71 الأية
قَالُوا نَعْبُدُ أَصْنَامًا فَنَظَلُّ لَهَا عَاكِفِينَ
Qaloo naAAbudu asnamanfanathallu laha AAakifeen
Swahili
Wakasema: Tunaabudu masanamu, daima tunayanyenyekea.
|
Ayah 26:72 الأية
قَالَ هَلْ يَسْمَعُونَكُمْ إِذْ تَدْعُونَ
Qala hal yasmaAAoonakum ithtadAAoon
Swahili
Akasema: Je! Yanakusikieni mnapo yaita?
|
Ayah 26:73 الأية
أَوْ يَنفَعُونَكُمْ أَوْ يَضُرُّونَ
Aw yanfaAAoonakum aw yadurroon
Swahili
Au yanakufaeni, au yanakudhuruni?
|
Ayah 26:74 الأية
قَالُوا بَلْ وَجَدْنَا آبَاءَنَا كَذَٰلِكَ يَفْعَلُونَ
Qaloo bal wajadna abaanakathalika yafAAaloon
Swahili
Wakasema: Bali tumewakuta baba zetu wakifanya hivyo hivyo.
|
Ayah 26:75 الأية
قَالَ أَفَرَأَيْتُم مَّا كُنتُمْ تَعْبُدُونَ
Qala afaraaytum ma kuntumtaAAbudoon
Swahili
Je! Mmewaona hawa mnao waabudu-
|
Ayah 26:76 الأية
أَنتُمْ وَآبَاؤُكُمُ الْأَقْدَمُونَ
Antum waabaokumu al-aqdamoon
Swahili
Nyinyi na baba zenu wa zamani?
|
Ayah 26:77 الأية
فَإِنَّهُمْ عَدُوٌّ لِّي إِلَّا رَبَّ الْعَالَمِينَ
Fa-innahum AAaduwwun lee illa rabbaalAAalameen
Swahili
Kwani hakika hao ni adui zangu, isipo kuwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
|
Ayah 26:78 الأية
الَّذِي خَلَقَنِي فَهُوَ يَهْدِينِ
Allathee khalaqanee fahuwa yahdeen
Swahili
Ambaye ndiye aliye niumba, na Yeye ndiye ananiongoa,
|
Ayah 26:79 الأية
وَالَّذِي هُوَ يُطْعِمُنِي وَيَسْقِينِ
Wallathee huwa yutAAimuneewayasqeen
Swahili
Na ambaye ndiye ananilisha na kuninywesha.
|
Ayah 26:80 الأية
وَإِذَا مَرِضْتُ فَهُوَ يَشْفِينِ
Wa-itha maridtu fahuwayashfeen
Swahili
Na ninapo ugua ni Yeye ndiye anaye niponesha.
|
Ayah 26:81 الأية
وَالَّذِي يُمِيتُنِي ثُمَّ يُحْيِينِ
Wallathee yumeetunee thummayuhyeen
Swahili
Na ambaye atanifisha, na kisha atanihuisha.
|
Ayah 26:82 الأية
وَالَّذِي أَطْمَعُ أَن يَغْفِرَ لِي خَطِيئَتِي يَوْمَ الدِّينِ
Wallathee atmaAAu anyaghfira lee khatee-atee yawma addeen
Swahili
Na ambaye ndiye ninaye mtumai kunisamehe makosa yangu Siku ya Malipo.
|
Ayah 26:83 الأية
رَبِّ هَبْ لِي حُكْمًا وَأَلْحِقْنِي بِالصَّالِحِينَ
Rabbi hab lee hukman waalhiqneebissaliheen
Swahili
Mola wangu Mlezi! Nitunukie hukumu na uniunganishe na watendao mema.
|
Ayah 26:84 الأية
وَاجْعَل لِّي لِسَانَ صِدْقٍ فِي الْآخِرِينَ
WajAAal lee lisana sidqinfee al-akhireen
Swahili
Na unijaalie nitajwe kwa wema na watu watakao kuja baadaye.
|
Ayah 26:85 الأية
وَاجْعَلْنِي مِن وَرَثَةِ جَنَّةِ النَّعِيمِ
WajAAalnee min warathati jannati annaAAeem
Swahili
Na unijaalie katika warithi wa Bustani za neema.
|
Ayah 26:86 الأية
وَاغْفِرْ لِأَبِي إِنَّهُ كَانَ مِنَ الضَّالِّينَ
Waghfir li-abee innahu kanamina addalleen
Swahili
Na umsamehe baba yangu, kwani hakika alikuwa miongoni mwa wapotovu.
|
Ayah 26:87 الأية
وَلَا تُخْزِنِي يَوْمَ يُبْعَثُونَ
Wala tukhzinee yawma yubAAathoon
Swahili
Wala usinihizi Siku watapo fufuliwa.
|
Ayah 26:88 الأية
يَوْمَ لَا يَنفَعُ مَالٌ وَلَا بَنُونَ
Yawma la yanfaAAu malun walabanoon
Swahili
Siku ambayo kwamba mali hayato faa kitu wala wana.
|
Ayah 26:89 الأية
إِلَّا مَنْ أَتَى اللهَ بِقَلْبٍ سَلِيمٍ
Illa man ata Allahabiqalbin saleem
Swahili
Isipo kuwa mwenye kumjia Mwenyezi Mungu na moyo safi.
|
Ayah 26:90 الأية
وَأُزْلِفَتِ الْجَنَّةُ لِلْمُتَّقِينَ
Waozlifati aljannatu lilmuttaqeen
Swahili
Na Pepo itasogezwa kwa wachamngu.
|
Ayah 26:91 الأية
وَبُرِّزَتِ الْجَحِيمُ لِلْغَاوِينَ
Waburrizati aljaheemu lilghaween
Swahili
Na Jahannamu itadhihirishwa kwa wapotovu.
|
Ayah 26:92 الأية
وَقِيلَ لَهُمْ أَيْنَ مَا كُنتُمْ تَعْبُدُونَ
Waqeela lahum ayna ma kuntumtaAAbudoon
Swahili
Na wataambiwa: Wako wapi mlio kuwa mkiwaabudu
|
Ayah 26:93 الأية
مِن دُونِ اللهِ هَلْ يَنصُرُونَكُمْ أَوْ يَنتَصِرُونَ
Min dooni Allahi hal yansuroonakumaw yantasiroon
Swahili
Badala ya Mwenyezi Mungu? Je! Wanakusaidieni, au wanajisaidia wenyewe?
|
Ayah 26:94 الأية
فَكُبْكِبُوا فِيهَا هُمْ وَالْغَاوُونَ
Fakubkiboo feeha hum walghawoon
Swahili
Basi watavurumizwa humo wao na hao wakosefu,
|
Ayah 26:95 الأية
وَجُنُودُ إِبْلِيسَ أَجْمَعُونَ
Wajunoodu ibleesa ajmaAAoon
Swahili
Na majeshi ya Ibilisi yote.
|
Ayah 26:96 الأية
قَالُوا وَهُمْ فِيهَا يَخْتَصِمُونَ
Qaloo wahum feeha yakhtasimoon
Swahili
Watasema, na hali ya kuwa wanazozana humo:
|
Ayah 26:97 الأية
تَاللهِ إِن كُنَّا لَفِي ضَلَالٍ مُّبِينٍ
Tallahi in kunna lafeedalalin mubeen
Swahili
Wallahi! Kwa yakini tulikuwa katika upotovu ulio dhaahiri,
|
Ayah 26:98 الأية
إِذْ نُسَوِّيكُم بِرَبِّ الْعَالَمِينَ
Ith nusawweekum birabbi alAAalameen
Swahili
Tulipo kufanyeni ni sawa na Mola Mlezi wa walimwengu wote.
|
Ayah 26:99 الأية
وَمَا أَضَلَّنَا إِلَّا الْمُجْرِمُونَ
Wama adallana illaalmujrimoon
Swahili
Na hawakutupoteza ila wale wakosefu.
|
Ayah 26:100 الأية
فَمَا لَنَا مِن شَافِعِينَ
Fama lana min shafiAAeen
Swahili
Basi hatuna waombezi.
|
Ayah 26:101 الأية
وَلَا صَدِيقٍ حَمِيمٍ
Wala sadeeqin hameem
Swahili
Wala rafiki wa dhati.
|
Ayah 26:102 الأية
فَلَوْ أَنَّ لَنَا كَرَّةً فَنَكُونَ مِنَ الْمُؤْمِنِينَ
Falaw anna lana karratan fanakoonamina almu/mineen
Swahili
Laiti tungeli pata kurejea tena tungeli kuwa katika Waumini.
|
Ayah 26:103 الأية
إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَةً ۖ وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ
Inna fee thalika laayatan wamakana aktharuhum mu/mineen
Swahili
Hakika katika haya ipo Ishara, lakini wengi wao hawakuwa wenye kuamini.
|
Ayah 26:104 الأية
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ الْعَزِيزُ الرَّحِيمُ
Wa-inna rabbaka lahuwa alAAazeezu arraheem
Swahili
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.
|
Ayah 26:105 الأية
كَذَّبَتْ قَوْمُ نُوحٍ الْمُرْسَلِينَ
Kaththabat qawmu noohinalmursaleen
Swahili
Kaumu ya Nuhu waliwakadhibisha Mitume.
|
Ayah 26:106 الأية
إِذْ قَالَ لَهُمْ أَخُوهُمْ نُوحٌ أَلَا تَتَّقُونَ
Ith qala lahum akhoohum noohunala tattaqoon
Swahili
Alipo waambia ndugu yao, Nuhu: Je! Hamchimngu?
|
Ayah 26:107 الأية
إِنِّي لَكُمْ رَسُولٌ أَمِينٌ
Innee lakum rasoolun ameen
Swahili
Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu.
|
Ayah 26:108 الأية
فَاتَّقُوا اللهَ وَأَطِيعُونِ
Fattaqoo Allaha waateeAAoon
Swahili
Basi Mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini mimi.
|
Ayah 26:109 الأية
وَمَا أَسْأَلُكُمْ عَلَيْهِ مِنْ أَجْرٍ ۖ إِنْ أَجْرِيَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ
الْعَالَمِينَ
Wama as-alukum AAalayhi min ajrin inajriya illa AAala rabbi alAAalameen
Swahili
Na sikutakini juu yake ujira, kwani ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa
walimwengu wote.
|
Ayah 26:110 الأية
فَاتَّقُوا اللهَ وَأَطِيعُونِ
Fattaqoo Allaha waateeAAoon
Swahili
Basi Mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini mimi.
|
Ayah 26:111 الأية
قَالُوا أَنُؤْمِنُ لَكَ وَاتَّبَعَكَ الْأَرْذَلُونَ
Qaloo anu/minu laka wattabaAAakaal-arthaloon
Swahili
Wakasema: Je! Tukuamini wewe, hali wanao kufuata ni watu wa chini?
|
Ayah 26:112 الأية
قَالَ وَمَا عِلْمِي بِمَا كَانُوا يَعْمَلُونَ
Qala wama AAilmee bimakanoo yaAAmaloon
Swahili
Akasema: Nayajuaje waliyo kuwa wakiyafanya?
|
Ayah 26:113 الأية
إِنْ حِسَابُهُمْ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّي ۖ لَوْ تَشْعُرُونَ
In hisabuhum illa AAalarabbee law tashAAuroon
Swahili
Hisabu yao haiko ila kwa Mola wao Mlezi, laiti mngeli tambua!
|
Ayah 26:114 الأية
وَمَا أَنَا بِطَارِدِ الْمُؤْمِنِينَ
Wama ana bitaridialmu/mineen
Swahili
Wala mimi si wa kuwafukuza Waumini.
|
Ayah 26:115 الأية
إِنْ أَنَا إِلَّا نَذِيرٌ مُّبِينٌ
In ana illa natheerunmubeen
Swahili
Mimi si cho chote ila ni Mwonyaji wa dhaahiri shaahiri.
|
Ayah 26:116 الأية
قَالُوا لَئِن لَّمْ تَنتَهِ يَا نُوحُ لَتَكُونَنَّ مِنَ الْمَرْجُومِينَ
Qaloo la-in lam tantahi yanoohu latakoonanna mina almarjoomeen
Swahili
Wakasema: Ikiwa huachi, ewe Nuhu, bila ya shaka utapigwa mawe.
|
Ayah 26:117 الأية
قَالَ رَبِّ إِنَّ قَوْمِي كَذَّبُونِ
Qala rabbi inna qawmee kaththaboon
Swahili
Akasema: Mola wangu Mlezi! Hakika watu wangu wamenikanusha.
|
Ayah 26:118 الأية
فَافْتَحْ بَيْنِي وَبَيْنَهُمْ فَتْحًا وَنَجِّنِي وَمَن مَّعِيَ مِنَ
الْمُؤْمِنِينَ
Faftah baynee wabaynahum fathanwanajjinee waman maAAiya mina almu/mineen
Swahili
Basi hukumu baina yangu na wao kwa hukumu yako, na uniokoe mimi na walio pamoja
nami, Waumini.
|
Ayah 26:119 الأية
فَأَنجَيْنَاهُ وَمَن مَّعَهُ فِي الْفُلْكِ الْمَشْحُونِ
Faanjaynahu waman maAAahu feealfulki almashhoon
Swahili
Kwa hivyo tukamwokoa yeye na walio kuwa pamoja naye katika marikebu iliyo
sheheni.
|
|