1st Ayah 1 الأية ١الأوليبِسْم ِ اللهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ
يَا أَيُّهَا النَّبِيُّ لِمَ تُحَرِّمُ مَا أَحَلَّ اللهُ لَكَ ۖ تَبْتَغِي
مَرْضَاتَ أَزْوَاجِكَ ۚ وَاللهُ غَفُورٌ رَّحِيمٌ
Ya ayyuha annabiyyulima tuharrimu ma ahalla Allahu lakatabtaghee mardata
azwajika wallahughafoorun raheem
Swahili
Ewe Nabii! Kwa nini unaharimisha alicho kuhalilishia Mwenyezi Mungu? Unatafuta
kuwaridhi wake zako. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusamehe, Mwenye kurehemu.
|
Ayah 66:2 الأية
قَدْ فَرَضَ اللهُ لَكُمْ تَحِلَّةَ أَيْمَانِكُمْ ۚ وَاللهُ مَوْلَاكُمْ ۖ
وَهُوَ الْعَلِيمُ الْحَكِيمُ
Qad farada Allahu lakum tahillataaymanikum wallahu mawlakum wahuwaalAAaleemu
alhakeem
Swahili
Hakika Mwenyezi Mungu kakupeni Sharia ya kufungua viapo vyenu, na Mwenyezi Mungu
ni Mola wenu. Na Yeye ni Mwenye kujua, Mwenye hikima.
|
Ayah 66:3 الأية
وَإِذْ أَسَرَّ النَّبِيُّ إِلَىٰ بَعْضِ أَزْوَاجِهِ حَدِيثًا فَلَمَّا نَبَّأَتْ
بِهِ وَأَظْهَرَهُ اللهُ عَلَيْهِ عَرَّفَ بَعْضَهُ وَأَعْرَضَ عَن بَعْضٍ ۖ
فَلَمَّا نَبَّأَهَا بِهِ قَالَتْ مَنْ أَنبَأَكَ هَٰذَا ۖ قَالَ نَبَّأَنِيَ
الْعَلِيمُ الْخَبِيرُ
Wa-ith asarra annabiyyu ilabaAAdi azwajihi hadeethan falammanabbaat bihi
waathharahu Allahu AAalayhiAAarrafa baAAdahu waaAArada AAan baAAdinfalamma
nabbaaha bihi qalat man anbaaka hathaqala nabbaaniya alAAaleemu alkhabeer
Swahili
Na Nabii alipo mwambia mmoja wa wake zake jambo la siri. Basi alipo litangaza
yule mke, na Mwenyezi Mungu akamdhihirishia Mtume, alimjuvya sehemu na akaacha
sehemu nyengine. Alipo mwambia hayo, huyo mke akasema: Nani aliye kwambia haya?
Mtume akasema: Kaniambia Mjuzi Mwenye khabari zote!
|
Ayah 66:4 الأية
إِن تَتُوبَا إِلَى اللهِ فَقَدْ صَغَتْ قُلُوبُكُمَا ۖ وَإِن تَظَاهَرَا
عَلَيْهِ فَإِنَّ اللهَ هُوَ مَوْلَاهُ وَجِبْرِيلُ وَصَالِحُ الْمُؤْمِنِينَ ۖ
وَالْمَلَائِكَةُ بَعْدَ ذَٰلِكَ ظَهِيرٌ
In tatooba ila Allahifaqad saghat quloobukuma wa-in tathaharaAAalayhi fa-inna
Allaha huwa mawlahu wajibreelu wasalihualmu/mineena walmala-ikatu baAAda thalika
thaheer
Swahili
Kama nyinyi wawili hamkutubia kwa Mwenyezi Mungu, basi nyoyo zenu zimekwisha
elekea huko. Na mkisaidiana dhidi yake (Mtume), basi hakika Mwenyezi Mungu ndiye
kipenzi chake, na Jibrili, na Waumini wema, na zaidi ya hayo Malaika pia
watasaidia.
|
Ayah 66:5 الأية
عَسَىٰ رَبُّهُ إِن طَلَّقَكُنَّ أَن يُبْدِلَهُ أَزْوَاجًا خَيْرًا مِّنكُنَّ
مُسْلِمَاتٍ مُّؤْمِنَاتٍ قَانِتَاتٍ تَائِبَاتٍ عَابِدَاتٍ سَائِحَاتٍ ثَيِّبَاتٍ
وَأَبْكَارًا
AAasa rabbuhu in tallaqakunnaan yubdilahu azwajan khayran minkunna
muslimatinmu/minatin qanitatin ta-ibatinAAabidatin sa-ihatin thayyibatinwaabkara
Swahili
Asaa Mola wake Mlezi, akikupeni talaka, akampa wake wengine badala yenu nyinyi,
walio bora kuliko nyinyi, wanynyekevu, Waumini, wat'awa, walio tubu, wenye
kushika ibada, wafanyao kheri, wajane na wanawari.
|
Ayah 66:6 الأية
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا قُوا أَنفُسَكُمْ وَأَهْلِيكُمْ نَارًا وَقُودُهَا
النَّاسُ وَالْحِجَارَةُ عَلَيْهَا مَلَائِكَةٌ غِلَاظٌ شِدَادٌ لَّا يَعْصُونَ
اللهَ مَا أَمَرَهُمْ وَيَفْعَلُونَ مَا يُؤْمَرُونَ
Ya ayyuha allatheena amanooqoo anfusakum waahleekum naran waqooduha
annasuwalhijaratu AAalayha mala-ikatunghilathun shidadun la yaAAsoonaAllaha ma
amarahum wayafAAaloona mayu/maroon
Swahili
Enyi mlio amini! Jilindeni nafsi zenu na ahali zenu na Moto ambao kuni zake ni
watu na mawe. Wanausimamia Malaika wakali, wenye nguvu, hawamuasi Mwenyezi Mungu
kwa anayo waamrisha, na wanatenda wanayo amrishwa.
|
Ayah 66:7 الأية
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ كَفَرُوا لَا تَعْتَذِرُوا الْيَوْمَ ۖ إِنَّمَا تُجْزَوْنَ
مَا كُنتُمْ تَعْمَلُونَ
Ya ayyuha allatheenakafaroo la taAAtathiroo alyawma innamatujzawna ma kuntum
taAAmaloon
Swahili
Enyi mlio kufuru! Msilete udhuru leo. Hakika mnalipwa mliyo kuwa mkiyatenda.
|
Ayah 66:8 الأية
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا تُوبُوا إِلَى اللهِ تَوْبَةً نَّصُوحًا عَسَىٰ
رَبُّكُمْ أَن يُكَفِّرَ عَنكُمْ سَيِّئَاتِكُمْ وَيُدْخِلَكُمْ جَنَّاتٍ تَجْرِي
مِن تَحْتِهَا الْأَنْهَارُ يَوْمَ لَا يُخْزِي اللهُ النَّبِيَّ وَالَّذِينَ
آمَنُوا مَعَهُ ۖ نُورُهُمْ يَسْعَىٰ بَيْنَ أَيْدِيهِمْ وَبِأَيْمَانِهِمْ
يَقُولُونَ رَبَّنَا أَتْمِمْ لَنَا نُورَنَا وَاغْفِرْ لَنَا ۖ إِنَّكَ عَلَىٰ
كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ
Ya ayyuha allatheena amanootooboo ila Allahi tawbatan nasoohanAAasa rabbukum an
yukaffira AAankum sayyi-atikumwayudkhilakum jannatin tajree min tahtihaal-anharu
yawma la yukhzee Allahu annabiyyawallatheena amanoo maAAahu nooruhum yasAAabayna
aydeehim wabi-aymanihim yaqooloona rabbanaatmim lana noorana waghfir lanainnaka
AAala kulli shay-in qadeer
Swahili
Enyi mlio amini! Tubuni kwa Mwenyezi Mungu toba iliyo ya kweli! Asaa Mola wenu
Mlezi akakufutieni maovu yenu na akakuingizeni katika Pepo zipitazo mito kati
yake, siku ambayo Mwenyezi Mungu hatamdhalilisha Nabii na walio amini pamoja
naye. Nuru yao inakwenda mbele yao na pande zao za kulia, na huku wanasema: Mola
wetu Mlezi! Tutimilizie nuru yetu, na utughufirie! Hakika Wewe ni Mwenye uweza
juu ya kila kitu.
|
Ayah 66:9 الأية
يَا أَيُّهَا النَّبِيُّ جَاهِدِ الْكُفَّارَ وَالْمُنَافِقِينَ وَاغْلُظْ
عَلَيْهِمْ ۚ وَمَأْوَاهُمْ جَهَنَّمُ ۖ وَبِئْسَ الْمَصِيرُ
Ya ayyuha annabiyyu jahidialkuffara walmunafiqeena waghluthAAalayhim wama/wahum
jahannamu wabi/sa almaseer
Swahili
Ewe Nabii! Pambana na makafiri na wanaafiki, na kuwa mgumu kwao! Na makaazi yao
ni Jahannamu. Na hayo ni marejeo mabaya.
|
Ayah 66:10 الأية
ضَرَبَ اللهُ مَثَلًا لِّلَّذِينَ كَفَرُوا امْرَأَتَ نُوحٍ وَامْرَأَتَ لُوطٍ ۖ
كَانَتَا تَحْتَ عَبْدَيْنِ مِنْ عِبَادِنَا صَالِحَيْنِ فَخَانَتَاهُمَا فَلَمْ
يُغْنِيَا عَنْهُمَا مِنَ اللهِ شَيْئًا وَقِيلَ ادْخُلَا النَّارَ مَعَ
الدَّاخِلِينَ
Daraba Allahu mathalan lillatheenakafaroo imraata noohin wamraata lootin
kanatatahta AAabdayni min AAibadina salihaynifakhanatahuma falam yughniya
AAanhumamina Allahi shay-an waqeela odkhula annaramaAAa addakhileen
Swahili
Mwenyezi Mungu amewapigia mfano walio kufuru: mke wa Nuhu na mke wa Lut'i.
Walikuwa chini ya waja wetu wema wawili miongoni mwa waja wetu. Lakini
wakawakhuni waume zao, nao wasiwafae kitu. Na ikasemwa: Ingieni Motoni pamoja na
wanao ingia!
|
Ayah 66:11 الأية
وَضَرَبَ اللهُ مَثَلًا لِّلَّذِينَ آمَنُوا امْرَأَتَ فِرْعَوْنَ إِذْ قَالَتْ
رَبِّ ابْنِ لِي عِندَكَ بَيْتًا فِي الْجَنَّةِ وَنَجِّنِي مِن فِرْعَوْنَ
وَعَمَلِهِ وَنَجِّنِي مِنَ الْقَوْمِ الظَّالِمِينَ
Wadaraba Allahu mathalan lillatheenaamanoo imraata firAAawna ith qalat rabbiibni
lee AAindaka baytan fee aljannati wanajjinee min firAAawnawaAAamalihi wanajjinee
mina alqawmi aththalimeen
Swahili
Na Mwenyezi Mungu amewapigia mfano walio amini - mkewe Firauni, alipo sema: Mola
wangu Mlezi! Nijengee kwako nyumba Peponi, na uniokoe na Firauni na vitendo
vyake, na uniokoe na watu madhaalimu.
|
Ayah 66:12 الأية
وَمَرْيَمَ ابْنَتَ عِمْرَانَ الَّتِي أَحْصَنَتْ فَرْجَهَا فَنَفَخْنَا فِيهِ مِن
رُّوحِنَا وَصَدَّقَتْ بِكَلِمَاتِ رَبِّهَا وَكُتُبِهِ وَكَانَتْ مِنَ
الْقَانِتِينَ
Wamaryama ibnata AAimrana allatee ahsanatfarjaha fanafakhna feehi min
roohinawasaddaqat bikalimati rabbiha wakutubihi wakanatmina alqaniteen
Swahili
Na Mariamu binti wa Imrani, aliye linda ubikira wake, na tukampulizia humo
kutoka roho yetu, na akayasadiki maneno ya Mola wake Mlezi na Vitabu vyake, na
alikuwa miongoni mwa wat'iifu.
|
©
EsinIslam.Com Designed & produced by The Awqaf London. Please pray for us
|