1st Ayah 1 الأية ١الأوليبِسْم ِ اللهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ
ن ۚ وَالْقَلَمِ وَمَا يَسْطُرُونَ
Noon walqalami wama yasturoon
Swahili
Nuun. Naapa kwa kalamu na yale wayaandikayo,
|
Ayah 68:2 الأية
مَا أَنتَ بِنِعْمَةِ رَبِّكَ بِمَجْنُونٍ
Ma anta biniAAmati rabbika bimajnoon
Swahili
Kwa neema ya Mola wako Mlezi wewe si mwendawazimu.
|
Ayah 68:3 الأية
وَإِنَّ لَكَ لَأَجْرًا غَيْرَ مَمْنُونٍ
Wa-inna laka laajran ghayra mamnoon
Swahili
Na kwa hakika wewe una malipo yasiyo katika.
|
Ayah 68:4 الأية
وَإِنَّكَ لَعَلَىٰ خُلُقٍ عَظِيمٍ
Wa-innaka laAAala khuluqin AAatheem
Swahili
Na hakika wewe una tabia tukufu.
|
Ayah 68:5 الأية
فَسَتُبْصِرُ وَيُبْصِرُونَ
Fasatubsiru wayubsiroon
Swahili
Karibu utaona, na wao wataona,
|
Ayah 68:6 الأية
بِأَييِّكُمُ الْمَفْتُونُ
Bi-ayyikumu almaftoon
Swahili
Ni nani kati yenu aliye pandwa na wazimu.
|
Ayah 68:7 الأية
إِنَّ رَبَّكَ هُوَ أَعْلَمُ بِمَن ضَلَّ عَن سَبِيلِهِ وَهُوَ أَعْلَمُ
بِالْمُهْتَدِينَ
Inna rabbaka huwa aAAlamu biman dallaAAan sabeelihi wahuwa aAAlamu bilmuhtadeen
Swahili
Hakika Mola wako Mlezi ndiye Yeye ajuaye zaidi nani aliye ipotea Njia yake, na
Yeye ndiye anaye wajua zaidi walio ongoka.
|
Ayah 68:8 الأية
فَلَا تُطِعِ الْمُكَذِّبِينَ
Fala tutiAAi almukaththibeen
Swahili
Basi usiwat'ii wanao kadhibisha.
|
Ayah 68:9 الأية
وَدُّوا لَوْ تُدْهِنُ فَيُدْهِنُونَ
Waddoo law tudhinu fayudhinoon
Swahili
Wanatamani lau unge lainisha ili nao wakulainishie.
|
Ayah 68:10 الأية
وَلَا تُطِعْ كُلَّ حَلَّافٍ مَّهِينٍ
Wala tutiAA kulla hallafinmaheen
Swahili
Wala usimt'ii kila mwingi wa kuapa wa kudharauliwa,
|
Ayah 68:11 الأية
هَمَّازٍ مَّشَّاءٍ بِنَمِيمٍ
Hammazin mashsha-in binameem
Swahili
Mtapitapi, apitaye akifitini,
|
Ayah 68:12 الأية
مَّنَّاعٍ لِّلْخَيْرِ مُعْتَدٍ أَثِيمٍ
MannaAAin lilkhayri muAAtadin atheem
Swahili
Mwenye kuzuia kheri, dhaalimu, mwingi wa madhambi,
|
Ayah 68:13 الأية
عُتُلٍّ بَعْدَ ذَٰلِكَ زَنِيمٍ
AAutullin baAAda thalika zaneem
Swahili
Mkavu, na juu ya hayo, mshari, amejipachika tu.
|
Ayah 68:14 الأية
أَن كَانَ ذَا مَالٍ وَبَنِينَ
An kana tha malinwabaneen
Swahili
Ati kwa kuwa ana mali na watoto!
|
Ayah 68:15 الأية
إِذَا تُتْلَىٰ عَلَيْهِ آيَاتُنَا قَالَ أَسَاطِيرُ الْأَوَّلِينَ
Itha tutla AAalayhi ayatunaqala asateeru al-awwaleen
Swahili
Anapo somewa Aya zetu, husema: Hizi ni simulizi za uwongo za watu wa zamani!
|
Ayah 68:16 الأية
سَنَسِمُهُ عَلَى الْخُرْطُومِ
Sanasimuhu AAala alkhurtoom
Swahili
Tutamtia kovu juu ya pua yake.
|
Ayah 68:17 الأية
إِنَّا بَلَوْنَاهُمْ كَمَا بَلَوْنَا أَصْحَابَ الْجَنَّةِ إِذْ أَقْسَمُوا
لَيَصْرِمُنَّهَا مُصْبِحِينَ
Inna balawnahum kamabalawna as-haba aljannati ith aqsamoolayasrimunnaha
musbiheen
Swahili
Hakika tumewajaribu hawa kama tulivyo wajaribu wale wenye shamba, walipo apa
kwamba watayavuna mazao yake itakapo kuwa asubuhi.
|
Ayah 68:18 الأية
وَلَا يَسْتَثْنُونَ
Wala yastathnoon
Swahili
Wala hawakusema: Mungu akipenda!
|
Ayah 68:19 الأية
فَطَافَ عَلَيْهَا طَائِفٌ مِّن رَّبِّكَ وَهُمْ نَائِمُونَ
Fatafa AAalayha ta-ifunmin rabbika wahum na-imoon
Swahili
Basi lilitokea tukio juu yake kutoka kwa Mola wako Mlezi, nao wamelala!
|
Ayah 68:20 الأية
فَأَصْبَحَتْ كَالصَّرِيمِ
Faasbahat kassareem
Swahili
Likawa kama usiku wa giza.
|
Ayah 68:21 الأية
فَتَنَادَوْا مُصْبِحِينَ
Fatanadaw musbiheen
Swahili
Asubuhi wakaitana.
|
Ayah 68:22 الأية
أَنِ اغْدُوا عَلَىٰ حَرْثِكُمْ إِن كُنتُمْ صَارِمِينَ
Ani ighdoo AAala harthikum inkuntum sarimeen
Swahili
Ya kwamba nendeni kondeni mwenu ikiwa mnataka kuvuna.
|
Ayah 68:23 الأية
فَانطَلَقُوا وَهُمْ يَتَخَافَتُونَ
Fantalaqoo wahum yatakhafatoon
Swahili
Basi walikwenda na huku wakinong'onezana,
|
Ayah 68:24 الأية
أَن لَّا يَدْخُلَنَّهَا الْيَوْمَ عَلَيْكُم مِّسْكِينٌ
An la yadkhulannaha alyawmaAAalaykum miskeen
Swahili
Ya kuwa leo hata masikini mmoja asikuingilieni.
|
Ayah 68:25 الأية
وَغَدَوْا عَلَىٰ حَرْدٍ قَادِرِينَ
Waghadaw AAala hardin qadireen
Swahili
Na walikwenda asubuhi, nao wameshikilia azimio hilo.
|
Ayah 68:26 الأية
فَلَمَّا رَأَوْهَا قَالُوا إِنَّا لَضَالُّونَ
Falamma raawha qalooinna ladalloon
Swahili
Basi walipo liona, wakasema: Hakika tumepotea!
|
Ayah 68:27 الأية
بَلْ نَحْنُ مَحْرُومُونَ
Bal nahnu mahroomoon
Swahili
Bali tumenyimwa!
|
Ayah 68:28 الأية
قَالَ أَوْسَطُهُمْ أَلَمْ أَقُل لَّكُمْ لَوْلَا تُسَبِّحُونَ
Qala awsatuhum alam aqul lakumlawla tusabbihoon
Swahili
Mbora wao akasema: Sikukwambieni, kwa nini hamumtakasi Mwenyezi Mungu?
|
Ayah 68:29 الأية
قَالُوا سُبْحَانَ رَبِّنَا إِنَّا كُنَّا ظَالِمِينَ
Qaloo subhana rabbinainna kunna thalimeen
Swahili
Wakasema: Ametakasika Mola wetu Mlezi! Hakika sisi tulikuwa wenye kudhulumu.
|
Ayah 68:30 الأية
فَأَقْبَلَ بَعْضُهُمْ عَلَىٰ بَعْضٍ يَتَلَاوَمُونَ
Faaqbala baAAduhum AAala baAAdinyatalawamoon
Swahili
Basi wakakabiliana kulaumiana wao kwa wao.
|
Ayah 68:31 الأية
قَالُوا يَا وَيْلَنَا إِنَّا كُنَّا طَاغِينَ
Qaloo ya waylana innakunna tagheen
Swahili
Wakasema: Ole wetu! Tulikuwa tumeikiuka mipaka!
|
Ayah 68:32 الأية
عَسَىٰ رَبُّنَا أَن يُبْدِلَنَا خَيْرًا مِّنْهَا إِنَّا إِلَىٰ رَبِّنَا
رَاغِبُونَ
AAasa rabbuna an yubdilanakhayran minha inna ila rabbina raghiboon
Swahili
Asaa Mola wetu Mlezi akatubadilishia lilio bora kuliko hili. Hakika sisi ni
wenye kurejea kwa Mola wetu Mlezi.
|
Ayah 68:33 الأية
كَذَٰلِكَ الْعَذَابُ ۖ وَلَعَذَابُ الْآخِرَةِ أَكْبَرُ ۚ لَوْ كَانُوا
يَعْلَمُونَ
Kathalika alAAathabu walaAAathabual-akhirati akbaru law kanoo yaAAlamoon
Swahili
Namna hivi yanakuwa mateso, na bila ya shaka mateso ya Akhera ni makubwa zaidi,
laiti wangeli jua!
|
Ayah 68:34 الأية
إِنَّ لِلْمُتَّقِينَ عِندَ رَبِّهِمْ جَنَّاتِ النَّعِيمِ
Inna lilmuttaqeena AAinda rabbihim jannatiannaAAeem
Swahili
Hakika wachamngu watakuwa na Bustani za neema kwa Mola wao Mlezi.
|
Ayah 68:35 الأية
أَفَنَجْعَلُ الْمُسْلِمِينَ كَالْمُجْرِمِينَ
AfanajAAalu almuslimeena kalmujrimeen
Swahili
Kwani tutawafanya Waislamu kama wakosefu?
|
Ayah 68:36 الأية
مَا لَكُمْ كَيْفَ تَحْكُمُونَ
Ma lakum kayfa tahkumoon
Swahili
Mna nini? Mnahukumu vipi?
|
Ayah 68:37 الأية
أَمْ لَكُمْ كِتَابٌ فِيهِ تَدْرُسُونَ
Am lakum kitabun feehi tadrusoon
Swahili
Au mnacho kitabu ambacho ndani yake mnasoma?
|
Ayah 68:38 الأية
إِنَّ لَكُمْ فِيهِ لَمَا تَخَيَّرُونَ
Inna lakum feehi lama takhayyaroon
Swahili
Kuwa mtapata humo mnayo yapenda?
|
Ayah 68:39 الأية
أَمْ لَكُمْ أَيْمَانٌ عَلَيْنَا بَالِغَةٌ إِلَىٰ يَوْمِ الْقِيَامَةِ ۙ إِنَّ
لَكُمْ لَمَا تَحْكُمُونَ
Am lakum aymanun AAalayna balighatunila yawmi alqiyamati inna lakum lama
tahkumoon
Swahili
Au mnazo ahadi za viapo juu yetu za kufika Siku ya Kiyama ya kuwa hakika mtapata
kila mnayo jihukumia?
|
Ayah 68:40 الأية
سَلْهُمْ أَيُّهُم بِذَٰلِكَ زَعِيمٌ
Salhum ayyuhum bithalika zaAAeem
Swahili
Waulize: Ni nani miongoni mwao dhamini wa haya?
|
Ayah 68:41 الأية
أَمْ لَهُمْ شُرَكَاءُ فَلْيَأْتُوا بِشُرَكَائِهِمْ إِن كَانُوا صَادِقِينَ
Am lahum shurakao falya/too bishuraka-ihimin kanoo sadiqeen
Swahili
Au wanao washirika? Basi wawalete washirika wao wakiwa wanasema kweli.
|
Ayah 68:42 الأية
يَوْمَ يُكْشَفُ عَن سَاقٍ وَيُدْعَوْنَ إِلَى السُّجُودِ فَلَا يَسْتَطِيعُونَ
Yawma yukshafu AAan saqin wayudAAawnaila assujoodi fala yastateeAAoon
Swahili
Siku utakapo wekwa wazi mundi, na wataitwa kusujudu, lakini hawataweza,
|
Ayah 68:43 الأية
خَاشِعَةً أَبْصَارُهُمْ تَرْهَقُهُمْ ذِلَّةٌ ۖ وَقَدْ كَانُوا يُدْعَوْنَ إِلَى
السُّجُودِ وَهُمْ سَالِمُونَ
KhashiAAatan absaruhumtarhaquhum thillatun waqad kanoo yudAAawna ilaassujoodi
wahum salimoon
Swahili
Macho yao yatainama chini, fedheha itawafunika. Na hakika walikuwa wakiitwa
wasujudu walipo kuwa wazima -
|
Ayah 68:44 الأية
فَذَرْنِي وَمَن يُكَذِّبُ بِهَٰذَا الْحَدِيثِ ۖ سَنَسْتَدْرِجُهُم مِّنْ حَيْثُ
لَا يَعْلَمُونَ
Fatharnee waman yukaththibubihatha alhadeethi sanastadrijuhum min haythula
yaAAlamoon
Swahili
Basi niache na wanao kadhibisha maneno haya! Tutawavutia kidogo kidogo kwa
mahali wasipo pajua.
|
Ayah 68:45 الأية
وَأُمْلِي لَهُمْ ۚ إِنَّ كَيْدِي مَتِينٌ
Waomlee lahum inna kaydee mateen
Swahili
Na ninawapururia muhula; hakika hila zangu ni imara.
|
Ayah 68:46 الأية
أَمْ تَسْأَلُهُمْ أَجْرًا فَهُم مِّن مَّغْرَمٍ مُّثْقَلُونَ
Am tas-aluhum ajran fahum min maghraminmuthqaloon
Swahili
Au unawaomba ujira, na wao wanaemewa na gharama hiyo?
|
Ayah 68:47 الأية
أَمْ عِندَهُمُ الْغَيْبُ فَهُمْ يَكْتُبُونَ
Am AAindahumu alghaybu fahum yaktuboon
Swahili
Au iko kwao siri, basi wao wanaiandika?
|
Ayah 68:48 الأية
فَاصْبِرْ لِحُكْمِ رَبِّكَ وَلَا تَكُن كَصَاحِبِ الْحُوتِ إِذْ نَادَىٰ وَهُوَ
مَكْظُومٌ
Fasbir lihukmi rabbikawala takun kasahibi alhooti ith nadawahuwa makthoom
Swahili
Basi ingojee hukumu ya Mola wako Mlezi, wala usiwe kama mmezwa na samaki, alipo
nadi naye kazongwa.
|
Ayah 68:49 الأية
لَّوْلَا أَن تَدَارَكَهُ نِعْمَةٌ مِّن رَّبِّهِ لَنُبِذَ بِالْعَرَاءِ وَهُوَ
مَذْمُومٌ
Lawla an tadarakahu niAAmatunmin rabbihi lanubitha bilAAara-i wahuwa mathmoom
Swahili
Kama isingeli mfikia neema kutoka kwa Mola wake Mlezi, bila ya shaka angeli
tupwa ufukweni naye ni mwenye kulaumiwa.
|
Ayah 68:50 الأية
فَاجْتَبَاهُ رَبُّهُ فَجَعَلَهُ مِنَ الصَّالِحِينَ
Fajtabahu rabbuhu fajaAAalahumina assaliheen
Swahili
Lakini Mola wake Mlezi alimteua na akamfanya miongoni mwa watu wema.
|
Ayah 68:51 الأية
وَإِن يَكَادُ الَّذِينَ كَفَرُوا لَيُزْلِقُونَكَ بِأَبْصَارِهِمْ لَمَّا سَمِعُوا
الذِّكْرَ وَيَقُولُونَ إِنَّهُ لَمَجْنُونٌ
Wa-in yakadu allatheenakafaroo layuzliqoonaka bi-absarihim lamma
samiAAooaththikra wayaqooloona innahu lamajnoon
Swahili
Na walio kufuru hukaribia kukutelezesha kwa macho yao, wanapo sikia mawaidha, na
wanasema: Hakika yeye ni mwendawazimu.
|
Ayah 68:52 الأية
وَمَا هُوَ إِلَّا ذِكْرٌ لِّلْعَالَمِينَ
Wama huwa illa thikrunlilAAalameen
Swahili
Na hayakuwa haya, ila ni ukumbusho kwa walimwengu wote.
|
©
EsinIslam.Com Designed & produced by The Awqaf London. Please pray for us
|