Prev  

68. Surah Al-Qalam سورة القلم

  Next  



1st Ayah  1  الأية ١الأولي
بِسْم ِ اللهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ
ن ۚ وَالْقَلَمِ وَمَا يَسْطُرُونَ
Noon walqalami wama yasturoon

Swahili
 
Nuun. Naapa kwa kalamu na yale wayaandikayo,

Ayah  68:2  الأية
مَا أَنتَ بِنِعْمَةِ رَبِّكَ بِمَجْنُونٍ
Ma anta biniAAmati rabbika bimajnoon

Swahili
 
Kwa neema ya Mola wako Mlezi wewe si mwendawazimu.

Ayah  68:3  الأية
وَإِنَّ لَكَ لَأَجْرًا غَيْرَ مَمْنُونٍ
Wa-inna laka laajran ghayra mamnoon

Swahili
 
Na kwa hakika wewe una malipo yasiyo katika.

Ayah  68:4  الأية
وَإِنَّكَ لَعَلَىٰ خُلُقٍ عَظِيمٍ
Wa-innaka laAAala khuluqin AAatheem

Swahili
 
Na hakika wewe una tabia tukufu.

Ayah  68:5  الأية
فَسَتُبْصِرُ وَيُبْصِرُونَ
Fasatubsiru wayubsiroon

Swahili
 
Karibu utaona, na wao wataona,

Ayah  68:6  الأية
بِأَييِّكُمُ الْمَفْتُونُ
Bi-ayyikumu almaftoon

Swahili
 
Ni nani kati yenu aliye pandwa na wazimu.

Ayah  68:7  الأية
إِنَّ رَبَّكَ هُوَ أَعْلَمُ بِمَن ضَلَّ عَن سَبِيلِهِ وَهُوَ أَعْلَمُ بِالْمُهْتَدِينَ
Inna rabbaka huwa aAAlamu biman dallaAAan sabeelihi wahuwa aAAlamu bilmuhtadeen

Swahili
 
Hakika Mola wako Mlezi ndiye Yeye ajuaye zaidi nani aliye ipotea Njia yake, na Yeye ndiye anaye wajua zaidi walio ongoka.

Ayah  68:8  الأية
فَلَا تُطِعِ الْمُكَذِّبِينَ
Fala tutiAAi almukaththibeen

Swahili
 
Basi usiwat'ii wanao kadhibisha.

Ayah  68:9  الأية
وَدُّوا لَوْ تُدْهِنُ فَيُدْهِنُونَ
Waddoo law tudhinu fayudhinoon

Swahili
 
Wanatamani lau unge lainisha ili nao wakulainishie.

Ayah  68:10  الأية
وَلَا تُطِعْ كُلَّ حَلَّافٍ مَّهِينٍ
Wala tutiAA kulla hallafinmaheen

Swahili
 
Wala usimt'ii kila mwingi wa kuapa wa kudharauliwa,

Ayah  68:11  الأية
هَمَّازٍ مَّشَّاءٍ بِنَمِيمٍ
Hammazin mashsha-in binameem

Swahili
 
Mtapitapi, apitaye akifitini,

Ayah  68:12  الأية
مَّنَّاعٍ لِّلْخَيْرِ مُعْتَدٍ أَثِيمٍ
MannaAAin lilkhayri muAAtadin atheem

Swahili
 
Mwenye kuzuia kheri, dhaalimu, mwingi wa madhambi,

Ayah  68:13  الأية
عُتُلٍّ بَعْدَ ذَٰلِكَ زَنِيمٍ
AAutullin baAAda thalika zaneem

Swahili
 
Mkavu, na juu ya hayo, mshari, amejipachika tu.

Ayah  68:14  الأية
أَن كَانَ ذَا مَالٍ وَبَنِينَ
An kana tha malinwabaneen

Swahili
 
Ati kwa kuwa ana mali na watoto!

Ayah  68:15  الأية
إِذَا تُتْلَىٰ عَلَيْهِ آيَاتُنَا قَالَ أَسَاطِيرُ الْأَوَّلِينَ
Itha tutla AAalayhi ayatunaqala asateeru al-awwaleen

Swahili
 
Anapo somewa Aya zetu, husema: Hizi ni simulizi za uwongo za watu wa zamani!

Ayah  68:16  الأية
سَنَسِمُهُ عَلَى الْخُرْطُومِ
Sanasimuhu AAala alkhurtoom

Swahili
 
Tutamtia kovu juu ya pua yake.

Ayah  68:17  الأية
إِنَّا بَلَوْنَاهُمْ كَمَا بَلَوْنَا أَصْحَابَ الْجَنَّةِ إِذْ أَقْسَمُوا لَيَصْرِمُنَّهَا مُصْبِحِينَ
Inna balawnahum kamabalawna as-haba aljannati ith aqsamoolayasrimunnaha musbiheen

Swahili
 
Hakika tumewajaribu hawa kama tulivyo wajaribu wale wenye shamba, walipo apa kwamba watayavuna mazao yake itakapo kuwa asubuhi.

Ayah  68:18  الأية
وَلَا يَسْتَثْنُونَ
Wala yastathnoon

Swahili
 
Wala hawakusema: Mungu akipenda!

Ayah  68:19  الأية
فَطَافَ عَلَيْهَا طَائِفٌ مِّن رَّبِّكَ وَهُمْ نَائِمُونَ
Fatafa AAalayha ta-ifunmin rabbika wahum na-imoon

Swahili
 
Basi lilitokea tukio juu yake kutoka kwa Mola wako Mlezi, nao wamelala!

Ayah  68:20  الأية
فَأَصْبَحَتْ كَالصَّرِيمِ
Faasbahat kassareem

Swahili
 
Likawa kama usiku wa giza.

Ayah  68:21  الأية
فَتَنَادَوْا مُصْبِحِينَ
Fatanadaw musbiheen

Swahili
 
Asubuhi wakaitana.

Ayah  68:22  الأية
أَنِ اغْدُوا عَلَىٰ حَرْثِكُمْ إِن كُنتُمْ صَارِمِينَ
Ani ighdoo AAala harthikum inkuntum sarimeen

Swahili
 
Ya kwamba nendeni kondeni mwenu ikiwa mnataka kuvuna.

Ayah  68:23  الأية
فَانطَلَقُوا وَهُمْ يَتَخَافَتُونَ
Fantalaqoo wahum yatakhafatoon

Swahili
 
Basi walikwenda na huku wakinong'onezana,

Ayah  68:24  الأية
أَن لَّا يَدْخُلَنَّهَا الْيَوْمَ عَلَيْكُم مِّسْكِينٌ
An la yadkhulannaha alyawmaAAalaykum miskeen

Swahili
 
Ya kuwa leo hata masikini mmoja asikuingilieni.

Ayah  68:25  الأية
وَغَدَوْا عَلَىٰ حَرْدٍ قَادِرِينَ
Waghadaw AAala hardin qadireen

Swahili
 
Na walikwenda asubuhi, nao wameshikilia azimio hilo.

Ayah  68:26  الأية
فَلَمَّا رَأَوْهَا قَالُوا إِنَّا لَضَالُّونَ
Falamma raawha qalooinna ladalloon

Swahili
 
Basi walipo liona, wakasema: Hakika tumepotea!

Ayah  68:27  الأية
بَلْ نَحْنُ مَحْرُومُونَ
Bal nahnu mahroomoon

Swahili
 
Bali tumenyimwa!

Ayah  68:28  الأية
قَالَ أَوْسَطُهُمْ أَلَمْ أَقُل لَّكُمْ لَوْلَا تُسَبِّحُونَ
Qala awsatuhum alam aqul lakumlawla tusabbihoon

Swahili
 
Mbora wao akasema: Sikukwambieni, kwa nini hamumtakasi Mwenyezi Mungu?

Ayah  68:29  الأية
قَالُوا سُبْحَانَ رَبِّنَا إِنَّا كُنَّا ظَالِمِينَ
Qaloo subhana rabbinainna kunna thalimeen

Swahili
 
Wakasema: Ametakasika Mola wetu Mlezi! Hakika sisi tulikuwa wenye kudhulumu.

Ayah  68:30  الأية
فَأَقْبَلَ بَعْضُهُمْ عَلَىٰ بَعْضٍ يَتَلَاوَمُونَ
Faaqbala baAAduhum AAala baAAdinyatalawamoon

Swahili
 
Basi wakakabiliana kulaumiana wao kwa wao.

Ayah  68:31  الأية
قَالُوا يَا وَيْلَنَا إِنَّا كُنَّا طَاغِينَ
Qaloo ya waylana innakunna tagheen

Swahili
 
Wakasema: Ole wetu! Tulikuwa tumeikiuka mipaka!

Ayah  68:32  الأية
عَسَىٰ رَبُّنَا أَن يُبْدِلَنَا خَيْرًا مِّنْهَا إِنَّا إِلَىٰ رَبِّنَا رَاغِبُونَ
AAasa rabbuna an yubdilanakhayran minha inna ila rabbina raghiboon

Swahili
 
Asaa Mola wetu Mlezi akatubadilishia lilio bora kuliko hili. Hakika sisi ni wenye kurejea kwa Mola wetu Mlezi.

Ayah  68:33  الأية
كَذَٰلِكَ الْعَذَابُ ۖ وَلَعَذَابُ الْآخِرَةِ أَكْبَرُ ۚ لَوْ كَانُوا يَعْلَمُونَ
Kathalika alAAathabu walaAAathabual-akhirati akbaru law kanoo yaAAlamoon

Swahili
 
Namna hivi yanakuwa mateso, na bila ya shaka mateso ya Akhera ni makubwa zaidi, laiti wangeli jua!

Ayah  68:34  الأية
إِنَّ لِلْمُتَّقِينَ عِندَ رَبِّهِمْ جَنَّاتِ النَّعِيمِ
Inna lilmuttaqeena AAinda rabbihim jannatiannaAAeem

Swahili
 
Hakika wachamngu watakuwa na Bustani za neema kwa Mola wao Mlezi.

Ayah  68:35  الأية
أَفَنَجْعَلُ الْمُسْلِمِينَ كَالْمُجْرِمِينَ
AfanajAAalu almuslimeena kalmujrimeen

Swahili
 
Kwani tutawafanya Waislamu kama wakosefu?

Ayah  68:36  الأية
مَا لَكُمْ كَيْفَ تَحْكُمُونَ
Ma lakum kayfa tahkumoon

Swahili
 
Mna nini? Mnahukumu vipi?

Ayah  68:37  الأية
أَمْ لَكُمْ كِتَابٌ فِيهِ تَدْرُسُونَ
Am lakum kitabun feehi tadrusoon

Swahili
 
Au mnacho kitabu ambacho ndani yake mnasoma?

Ayah  68:38  الأية
إِنَّ لَكُمْ فِيهِ لَمَا تَخَيَّرُونَ
Inna lakum feehi lama takhayyaroon

Swahili
 
Kuwa mtapata humo mnayo yapenda?

Ayah  68:39  الأية
أَمْ لَكُمْ أَيْمَانٌ عَلَيْنَا بَالِغَةٌ إِلَىٰ يَوْمِ الْقِيَامَةِ ۙ إِنَّ لَكُمْ لَمَا تَحْكُمُونَ
Am lakum aymanun AAalayna balighatunila yawmi alqiyamati inna lakum lama tahkumoon

Swahili
 
Au mnazo ahadi za viapo juu yetu za kufika Siku ya Kiyama ya kuwa hakika mtapata kila mnayo jihukumia?

Ayah  68:40  الأية
سَلْهُمْ أَيُّهُم بِذَٰلِكَ زَعِيمٌ
Salhum ayyuhum bithalika zaAAeem

Swahili
 
Waulize: Ni nani miongoni mwao dhamini wa haya?

Ayah  68:41  الأية
أَمْ لَهُمْ شُرَكَاءُ فَلْيَأْتُوا بِشُرَكَائِهِمْ إِن كَانُوا صَادِقِينَ
Am lahum shurakao falya/too bishuraka-ihimin kanoo sadiqeen

Swahili
 
Au wanao washirika? Basi wawalete washirika wao wakiwa wanasema kweli.

Ayah  68:42  الأية
يَوْمَ يُكْشَفُ عَن سَاقٍ وَيُدْعَوْنَ إِلَى السُّجُودِ فَلَا يَسْتَطِيعُونَ
Yawma yukshafu AAan saqin wayudAAawnaila assujoodi fala yastateeAAoon

Swahili
 
Siku utakapo wekwa wazi mundi, na wataitwa kusujudu, lakini hawataweza,

Ayah  68:43  الأية
خَاشِعَةً أَبْصَارُهُمْ تَرْهَقُهُمْ ذِلَّةٌ ۖ وَقَدْ كَانُوا يُدْعَوْنَ إِلَى السُّجُودِ وَهُمْ سَالِمُونَ
KhashiAAatan absaruhumtarhaquhum thillatun waqad kanoo yudAAawna ilaassujoodi wahum salimoon

Swahili
 
Macho yao yatainama chini, fedheha itawafunika. Na hakika walikuwa wakiitwa wasujudu walipo kuwa wazima -

Ayah  68:44  الأية
فَذَرْنِي وَمَن يُكَذِّبُ بِهَٰذَا الْحَدِيثِ ۖ سَنَسْتَدْرِجُهُم مِّنْ حَيْثُ لَا يَعْلَمُونَ
Fatharnee waman yukaththibubihatha alhadeethi sanastadrijuhum min haythula yaAAlamoon

Swahili
 
Basi niache na wanao kadhibisha maneno haya! Tutawavutia kidogo kidogo kwa mahali wasipo pajua.

Ayah  68:45  الأية
وَأُمْلِي لَهُمْ ۚ إِنَّ كَيْدِي مَتِينٌ
Waomlee lahum inna kaydee mateen

Swahili
 
Na ninawapururia muhula; hakika hila zangu ni imara.

Ayah  68:46  الأية
أَمْ تَسْأَلُهُمْ أَجْرًا فَهُم مِّن مَّغْرَمٍ مُّثْقَلُونَ
Am tas-aluhum ajran fahum min maghraminmuthqaloon

Swahili
 
Au unawaomba ujira, na wao wanaemewa na gharama hiyo?

Ayah  68:47  الأية
أَمْ عِندَهُمُ الْغَيْبُ فَهُمْ يَكْتُبُونَ
Am AAindahumu alghaybu fahum yaktuboon

Swahili
 
Au iko kwao siri, basi wao wanaiandika?

Ayah  68:48  الأية
فَاصْبِرْ لِحُكْمِ رَبِّكَ وَلَا تَكُن كَصَاحِبِ الْحُوتِ إِذْ نَادَىٰ وَهُوَ مَكْظُومٌ
Fasbir lihukmi rabbikawala takun kasahibi alhooti ith nadawahuwa makthoom

Swahili
 
Basi ingojee hukumu ya Mola wako Mlezi, wala usiwe kama mmezwa na samaki, alipo nadi naye kazongwa.

Ayah  68:49  الأية
لَّوْلَا أَن تَدَارَكَهُ نِعْمَةٌ مِّن رَّبِّهِ لَنُبِذَ بِالْعَرَاءِ وَهُوَ مَذْمُومٌ
Lawla an tadarakahu niAAmatunmin rabbihi lanubitha bilAAara-i wahuwa mathmoom

Swahili
 
Kama isingeli mfikia neema kutoka kwa Mola wake Mlezi, bila ya shaka angeli tupwa ufukweni naye ni mwenye kulaumiwa.

Ayah  68:50  الأية
فَاجْتَبَاهُ رَبُّهُ فَجَعَلَهُ مِنَ الصَّالِحِينَ
Fajtabahu rabbuhu fajaAAalahumina assaliheen

Swahili
 
Lakini Mola wake Mlezi alimteua na akamfanya miongoni mwa watu wema.

Ayah  68:51  الأية
وَإِن يَكَادُ الَّذِينَ كَفَرُوا لَيُزْلِقُونَكَ بِأَبْصَارِهِمْ لَمَّا سَمِعُوا الذِّكْرَ وَيَقُولُونَ إِنَّهُ لَمَجْنُونٌ
Wa-in yakadu allatheenakafaroo layuzliqoonaka bi-absarihim lamma samiAAooaththikra wayaqooloona innahu lamajnoon

Swahili
 
Na walio kufuru hukaribia kukutelezesha kwa macho yao, wanapo sikia mawaidha, na wanasema: Hakika yeye ni mwendawazimu.

Ayah  68:52  الأية
وَمَا هُوَ إِلَّا ذِكْرٌ لِّلْعَالَمِينَ
Wama huwa illa thikrunlilAAalameen

Swahili
 
Na hayakuwa haya, ila ni ukumbusho kwa walimwengu wote.
 


© EsinIslam.Com Designed & produced by The Awqaf London. Please pray for us