Prev  

74. Surah Al-Muddaththir سورة المدّثر

  Next  



1st Ayah  1  الأية ١الأولي
بِسْم ِ اللهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ
يَا أَيُّهَا الْمُدَّثِّرُ
Ya ayyuha almuddaththir

Swahili
 
Ewe uliye jigubika!

Ayah  74:2  الأية
قُمْ فَأَنذِرْ
Qum faanthir

Swahili
 
Simama uonye!

Ayah  74:3  الأية
وَرَبَّكَ فَكَبِّرْ
Warabbaka fakabbir

Swahili
 
Na Mola wako Mlezi mtukuze!

Ayah  74:4  الأية
وَثِيَابَكَ فَطَهِّرْ
Wathiyabaka fatahhir

Swahili
 
Na nguo zako, zisafishe.

Ayah  74:5  الأية
وَالرُّجْزَ فَاهْجُرْ
Warrujza fahjur

Swahili
 
Na yaliyo machafu yahame!

Ayah  74:6  الأية
وَلَا تَمْنُن تَسْتَكْثِرُ
Wala tamnun tastakthir

Swahili
 
Wala usitoe kwa kutaraji kuzidishiwa.

Ayah  74:7  الأية
وَلِرَبِّكَ فَاصْبِرْ
Walirabbika fasbir

Swahili
 
Na kwa ajili ya Mola wako Mlezi, subiri!

Ayah  74:8  الأية
فَإِذَا نُقِرَ فِي النَّاقُورِ
Fa-itha nuqira fee annaqoor

Swahili
 
Basi litapo pulizwa barugumu,

Ayah  74:9  الأية
فَذَٰلِكَ يَوْمَئِذٍ يَوْمٌ عَسِيرٌ
Fathalika yawma-ithin yawmunAAaseer

Swahili
 
Siku hiyo, basi, itakuwa siku ngumu.

Ayah  74:10  الأية
عَلَى الْكَافِرِينَ غَيْرُ يَسِيرٍ
AAala alkafireena ghayruyaseer

Swahili
 
Kwa makafiri haitakuwa nyepesi.

Ayah  74:11  الأية
ذَرْنِي وَمَنْ خَلَقْتُ وَحِيدًا
Tharnee waman khalaqtu waheeda

Swahili
 
Niache peke yangu na niliye muumba;

Ayah  74:12  الأية
وَجَعَلْتُ لَهُ مَالًا مَّمْدُودًا
WajaAAaltu lahu malan mamdooda

Swahili
 
Na nikamjaalia awe na mali mengi,

Ayah  74:13  الأية
وَبَنِينَ شُهُودًا
Wabaneena shuhooda

Swahili
 
Na wana wanao onekana,

Ayah  74:14  الأية
وَمَهَّدتُّ لَهُ تَمْهِيدًا
Wamahhadtu lahu tamheeda

Swahili
 
Na nikamtgenezea mambo vizuri kabisa.

Ayah  74:15  الأية
ثُمَّ يَطْمَعُ أَنْ أَزِيدَ
Thumma yatmaAAu an azeed

Swahili
 
Kisha anatumai nimzidishie!

Ayah  74:16  الأية
كَلَّا ۖ إِنَّهُ كَانَ لِآيَاتِنَا عَنِيدًا
Kalla innahu kana li-ayatinaAAaneeda

Swahili
 
Hasha! Kwani hakika yeye alikuwa akizifanyia inadi Aya zetu!

Ayah  74:17  الأية
سَأُرْهِقُهُ صَعُودًا
Saorhiquhu saAAooda

Swahili
 
Nitamtesa kwa mateso yasio wezekana.

Ayah  74:18  الأية
إِنَّهُ فَكَّرَ وَقَدَّرَ
Innahu fakkara waqaddar

Swahili
 
Kwani hakika yeye alifikiri na akapima.

Ayah  74:19  الأية
فَقُتِلَ كَيْفَ قَدَّرَ
Faqutila kayfa qaddar

Swahili
 
Basi ameangamia! Vipi alivyo pima!

Ayah  74:20  الأية
ثُمَّ قُتِلَ كَيْفَ قَدَّرَ
Thumma qutila kayfa qaddar

Swahili
 
Tena ameangamia! Vipi alivyo pima!

Ayah  74:21  الأية
ثُمَّ نَظَرَ
Thumma nathar

Swahili
 
Kisha akatazama,

Ayah  74:22  الأية
ثُمَّ عَبَسَ وَبَسَرَ
Thumma AAabasa wabasar

Swahili
 
Kisha akakunja kipaji, na akanuna.

Ayah  74:23  الأية
ثُمَّ أَدْبَرَ وَاسْتَكْبَرَ
Thumma adbara wastakbar

Swahili
 
Kisha akaipa kisogo haki, na akatakabari.

Ayah  74:24  الأية
فَقَالَ إِنْ هَٰذَا إِلَّا سِحْرٌ يُؤْثَرُ
Faqala in hatha illa sihrunyu/thar

Swahili
 
Na akasema: Haya si chochote ila ni uchawi ulio nukuliwa.

Ayah  74:25  الأية
إِنْ هَٰذَا إِلَّا قَوْلُ الْبَشَرِ
In hatha illa qawlu albashar

Swahili
 
Haya si chochote ila kauli ya binaadamu.

Ayah  74:26  الأية
سَأُصْلِيهِ سَقَرَ
Saosleehi saqar

Swahili
 
Nitakuja mtia kwenye Moto wa Saqar.

Ayah  74:27  الأية
وَمَا أَدْرَاكَ مَا سَقَرُ
Wama adraka ma saqar

Swahili
 
Na nini kitakujuulisha ni nini huo Moto wa Saqar?

Ayah  74:28  الأية
لَا تُبْقِي وَلَا تَذَرُ
La tubqee wala tathar

Swahili
 
Haubakishi wala hausazi.

Ayah  74:29  الأية
لَوَّاحَةٌ لِّلْبَشَرِ
Lawwahatun lilbashar

Swahili
 
Unababua ngozi iwe nyeusi.

Ayah  74:30  الأية
عَلَيْهَا تِسْعَةَ عَشَرَ
AAalayha tisAAata AAashar

Swahili
 
Juu yake wapo kumi na tisa.

Ayah  74:31  الأية
وَمَا جَعَلْنَا أَصْحَابَ النَّارِ إِلَّا مَلَائِكَةً ۙ وَمَا جَعَلْنَا عِدَّتَهُمْ إِلَّا فِتْنَةً لِّلَّذِينَ كَفَرُوا لِيَسْتَيْقِنَ الَّذِينَ أُوتُوا الْكِتَابَ وَيَزْدَادَ الَّذِينَ آمَنُوا إِيمَانًا ۙ وَلَا يَرْتَابَ الَّذِينَ أُوتُوا الْكِتَابَ وَالْمُؤْمِنُونَ ۙ وَلِيَقُولَ الَّذِينَ فِي قُلُوبِهِم مَّرَضٌ وَالْكَافِرُونَ مَاذَا أَرَادَ اللهُ بِهَٰذَا مَثَلًا ۚ كَذَٰلِكَ يُضِلُّ اللهُ مَن يَشَاءُ وَيَهْدِي مَن يَشَاءُ ۚ وَمَا يَعْلَمُ جُنُودَ رَبِّكَ إِلَّا هُوَ ۚ وَمَا هِيَ إِلَّا ذِكْرَىٰ لِلْبَشَرِ
Wama jaAAalna as-habaannari illa mala-ikatan wamajaAAalna AAiddatahum illa fitnatan lillatheenakafaroo liyastayqina allatheena ootoo alkitabawayazdada allatheena amanoo eemananwala yartaba allatheena ootoo alkitabawalmu/minoona waliyaqoola allatheena feequloobihim maradun walkafiroona mathaarada Allahu bihatha mathalan kathalikayudillu Allahu man yashao wayahdee man yashaowama yaAAlamu junooda rabbika illa huwa wamahiya illa thikra lilbashar

Swahili
 
Na hatukuwafanya walinzi wa Motoni ila ni Malaika, wala hatukuifanya idadi yao hiyo ila kuwatatanisha walio kufuru, wapate kuwa na yakini walio pewa Kitabu, na wazidi Imani wale walio amini, wala wasiwe na shaka walio pewa Kitabu na Waumini, na wapate kusema wenye maradhi katika nyoyo zao na makafiri: Mwenyezi Mungu amekusudia nini kwa mfano huu? Ndio kama hivyo Mwenyezi Mungu humwacha apotee amtakaye, na humwongoa amtakaye. Na hapana yeyote anaye jua majeshi ya Mola wako Mlezi ila Yeye tu. Na haya si chochote ila ni ukumbusho kwa binaadamu.

Ayah  74:32  الأية
كَلَّا وَالْقَمَرِ
Kalla walqamar

Swahili
 
Hasha! Naapa kwa mwezi!

Ayah  74:33  الأية
وَاللَّيْلِ إِذْ أَدْبَرَ
Wallayli ith adbar

Swahili
 
Na kwa usiku unapo kucha!

Ayah  74:34  الأية
وَالصُّبْحِ إِذَا أَسْفَرَ
Wassubhi ithaasfar

Swahili
 
Na kwa asubuhi inapo pambazuka!

Ayah  74:35  الأية
إِنَّهَا لَإِحْدَى الْكُبَرِ
Innaha la-ihda alkubar

Swahili
 
Hakika huo Moto ni katika mambo yaliyo makubwa kabisa!

Ayah  74:36  الأية
نَذِيرًا لِّلْبَشَرِ
Natheeran lilbashar

Swahili
 
Ni onyo kwa binaadamu,

Ayah  74:37  الأية
لِمَن شَاءَ مِنكُمْ أَن يَتَقَدَّمَ أَوْ يَتَأَخَّرَ
Liman shaa minkum an yataqaddama awyataakhkhar

Swahili
 
Kwa anaye taka miongoni mwenu kutangulia au kuchelewa.

Ayah  74:38  الأية
كُلُّ نَفْسٍ بِمَا كَسَبَتْ رَهِينَةٌ
Kullu nafsin bima kasabat raheena

Swahili
 
Kila nafsi imo rahanini kwa mabaya iliyo yachuma.

Ayah  74:39  الأية
إِلَّا أَصْحَابَ الْيَمِينِ
Illa as-haba alyameen

Swahili
 
Isipo kuwa watu wa kuliani.

Ayah  74:40  الأية
فِي جَنَّاتٍ يَتَسَاءَلُونَ
Fee jannatin yatasaaloon

Swahili
 
Hao watakuwa katika Mabustani, wawe wanaulizana

Ayah  74:41  الأية
عَنِ الْمُجْرِمِينَ
AAani almujrimeen

Swahili
 
Khabari za wakosefu:

Ayah  74:42  الأية
مَا سَلَكَكُمْ فِي سَقَرَ
Ma salakakum fee saqar

Swahili
 
Ni nini kilicho kupelekeni Motoni?

Ayah  74:43  الأية
قَالُوا لَمْ نَكُ مِنَ الْمُصَلِّينَ
Qaloo lam naku mina almusalleen

Swahili
 
Waseme: Hatukuwa miongoni walio kuwa wakisali.

Ayah  74:44  الأية
وَلَمْ نَكُ نُطْعِمُ الْمِسْكِينَ
Walam naku nutAAimu almiskeen

Swahili
 
Wala hatukuwa tukiwalisha masikini.

Ayah  74:45  الأية
وَكُنَّا نَخُوضُ مَعَ الْخَائِضِينَ
Wakunna nakhoodu maAAa alkha-ideen

Swahili
 
Na tulikuwa tukizama pamoja na walio zama katika maovu.

Ayah  74:46  الأية
وَكُنَّا نُكَذِّبُ بِيَوْمِ الدِّينِ
Wakunna nukaththibu biyawmi addeen

Swahili
 
Na tulikuwa tukiikanusha siku ya malipo.

Ayah  74:47  الأية
حَتَّىٰ أَتَانَا الْيَقِينُ
Hatta atanaalyaqeen

Swahili
 
Mpaka yakini ilipo tufikia.

Ayah  74:48  الأية
فَمَا تَنفَعُهُمْ شَفَاعَةُ الشَّافِعِينَ
Fama tanfaAAuhum shafaAAatu ashshafiAAeen

Swahili
 
Basi hautawafaa kitu uombezi wa waombezi.

Ayah  74:49  الأية
فَمَا لَهُمْ عَنِ التَّذْكِرَةِ مُعْرِضِينَ
Fama lahum AAani attathkiratimuAArideen

Swahili
 
Basi wana nini hata wanapuuza onyo hili?

Ayah  74:50  الأية
كَأَنَّهُمْ حُمُرٌ مُّسْتَنفِرَةٌ
Kaannahum humurun mustanfira

Swahili
 
Kama kwamba wao ni mapunda walio timuliwa,

Ayah  74:51  الأية
فَرَّتْ مِن قَسْوَرَةٍ
Farrat min qaswara

Swahili
 
Wanao mkimbia simba!

Ayah  74:52  الأية
بَلْ يُرِيدُ كُلُّ امْرِئٍ مِّنْهُمْ أَن يُؤْتَىٰ صُحُفًا مُّنَشَّرَةً
Bal yureedu kullu imri-in minhum an yu/tasuhufan munashshara

Swahili
 
Ati kila mmoja katika wao anataka apewe nyaraka zilizo funuliwa.

Ayah  74:53  الأية
كَلَّا ۖ بَل لَّا يَخَافُونَ الْآخِرَةَ
Kalla bal la yakhafoonaal-akhira

Swahili
 
Hasha! Kwani wao hawaiogopi Akhera?

Ayah  74:54  الأية
كَلَّا إِنَّهُ تَذْكِرَةٌ
Kalla innahu tathkira

Swahili
 
Hasha! Kwa hakika huu ni ukumbusho!

Ayah  74:55  الأية
فَمَن شَاءَ ذَكَرَهُ
Faman shaa thakarah

Swahili
 
Basi anaye taka atakumbuka.

Ayah  74:56  الأية
وَمَا يَذْكُرُونَ إِلَّا أَن يَشَاءَ اللهُ ۚ هُوَ أَهْلُ التَّقْوَىٰ وَأَهْلُ الْمَغْفِرَةِ
Wama yathkuroona illaan yashaa Allahu huwa ahlu attaqwawaahlu almaghfirat

Swahili
 
Na hawatakumbuka isipo kuwa Mwenyezi Mungu atake. Uchamngu ni kwake Yeye, na msamaha ni wake Yeye.
 


© EsinIslam.Com Designed & produced by The Awqaf London. Please pray for us