Prev  

78. Surah An-Naba' سورة النبأ

  Next  



1st Ayah  1  الأية ١الأولي
بِسْم ِ اللهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ
عَمَّ يَتَسَاءَلُونَ
AAamma yatasaaloon

Swahili
 
WANAULIZANA nini?

Ayah  78:2  الأية
عَنِ النَّبَإِ الْعَظِيمِ
AAani annaba-i alAAatheem

Swahili
 
Ile khabari kuu,

Ayah  78:3  الأية
الَّذِي هُمْ فِيهِ مُخْتَلِفُونَ
Allathee hum feehi mukhtalifoon

Swahili
 
Ambayo kwayo wanakhitalifiana.

Ayah  78:4  الأية
كَلَّا سَيَعْلَمُونَ
Kalla sayaAAlamoon

Swahili
 
La! Karibu watakuja jua.

Ayah  78:5  الأية
ثُمَّ كَلَّا سَيَعْلَمُونَ
Thumma kalla sayaAAlamoon

Swahili
 
Tena la! Karibu watakuja jua.

Ayah  78:6  الأية
أَلَمْ نَجْعَلِ الْأَرْضَ مِهَادًا
Alam najAAali al-arda mihada

Swahili
 
Kwani hatukuifanya ardhi kama tandiko?

Ayah  78:7  الأية
وَالْجِبَالَ أَوْتَادًا
Waljibala awtada

Swahili
 
Na milima kama vigingi?

Ayah  78:8  الأية
وَخَلَقْنَاكُمْ أَزْوَاجًا
Wakhalaqnakum azwaja

Swahili
 
Na tukakuumbeni kwa jozi?

Ayah  78:9  الأية
وَجَعَلْنَا نَوْمَكُمْ سُبَاتًا
WajaAAalna nawmakum subata

Swahili
 
Na tukakufanya kulala kwenu ni mapumziko?

Ayah  78:10  الأية
وَجَعَلْنَا اللَّيْلَ لِبَاسًا
WajaAAalna allayla libasa

Swahili
 
Na tukaufanya usiku ni nguo?

Ayah  78:11  الأية
وَجَعَلْنَا النَّهَارَ مَعَاشًا
WajaAAalna annaharamaAAasha

Swahili
 
Na tukaufanya mchana ni wa kuchumia maisha?

Ayah  78:12  الأية
وَبَنَيْنَا فَوْقَكُمْ سَبْعًا شِدَادًا
Wabanayna fawqakum sabAAan shidada

Swahili
 
Na tukajenga juu yenu saba zenye nguvu?

Ayah  78:13  الأية
وَجَعَلْنَا سِرَاجًا وَهَّاجًا
WajaAAalna sirajan wahhaja

Swahili
 
Na tukaifanya taa yenye mwanga na joto;

Ayah  78:14  الأية
وَأَنزَلْنَا مِنَ الْمُعْصِرَاتِ مَاءً ثَجَّاجًا
Waanzalna mina almuAAsiratimaan thajjaja

Swahili
 
Na tukateremsha maji yanayo anguka kwa kasi kutoka mawinguni,

Ayah  78:15  الأية
لِّنُخْرِجَ بِهِ حَبًّا وَنَبَاتًا
Linukhrija bihi habban wanabata

Swahili
 
Ili tutoe kwayo nafaka na mimea,

Ayah  78:16  الأية
وَجَنَّاتٍ أَلْفَافًا
Wajannatin alfafa

Swahili
 
Na mabustani yenye miti iliyo kamatana.

Ayah  78:17  الأية
إِنَّ يَوْمَ الْفَصْلِ كَانَ مِيقَاتًا
Inna yawma alfasli kana meeqata

Swahili
 
Hakika siku ya uamuzi imewekewa wakati wake,

Ayah  78:18  الأية
يَوْمَ يُنفَخُ فِي الصُّورِ فَتَأْتُونَ أَفْوَاجًا
Yawma yunfakhu fee assoorifata/toona afwaja

Swahili
 
Siku litapo pulizwa barugumu, nanyi mtakuja kwa makundi,

Ayah  78:19  الأية
وَفُتِحَتِ السَّمَاءُ فَكَانَتْ أَبْوَابًا
Wafutihati assamao fakanatabwaba

Swahili
 
Na mbingu zitafunguliwa, ziwe milango,

Ayah  78:20  الأية
وَسُيِّرَتِ الْجِبَالُ فَكَانَتْ سَرَابًا
Wasuyyirati aljibalu fakanatsaraba

Swahili
 
Na milima itaondolewa na itakuwa kama sarabi.

Ayah  78:21  الأية
إِنَّ جَهَنَّمَ كَانَتْ مِرْصَادًا
Inna jahannama kanat mirsada

Swahili
 
Hakika Jahannamu inangojea!

Ayah  78:22  الأية
لِّلطَّاغِينَ مَآبًا
Littagheena maaba

Swahili
 
Kwa walio asi ndio makaazi yao,

Ayah  78:23  الأية
لَّابِثِينَ فِيهَا أَحْقَابًا
Labitheena feeha ahqaba

Swahili
 
Wakae humo karne baada ya karne,

Ayah  78:24  الأية
لَّا يَذُوقُونَ فِيهَا بَرْدًا وَلَا شَرَابًا
La yathooqoona feehabardan wala sharaba

Swahili
 
Hawataonja humo chochote kibaridi wala kinywaji,

Ayah  78:25  الأية
إِلَّا حَمِيمًا وَغَسَّاقًا
Illa hameeman waghassaqa

Swahili
 
Ila maji yamoto sana na usaha,

Ayah  78:26  الأية
جَزَاءً وِفَاقًا
Jazaan wifaqa

Swahili
 
Ndio jaza muwafaka.

Ayah  78:27  الأية
إِنَّهُمْ كَانُوا لَا يَرْجُونَ حِسَابًا
Innahum kanoo la yarjoona hisaba

Swahili
 
Hakika hao hawakuwa wakitaraji kuwa kuna hisabu.

Ayah  78:28  الأية
وَكَذَّبُوا بِآيَاتِنَا كِذَّابًا
Wakaththaboo bi-ayatinakiththaba

Swahili
 
Na wakikanusha Aya zetu kwa nguvu.

Ayah  78:29  الأية
وَكُلَّ شَيْءٍ أَحْصَيْنَاهُ كِتَابًا
Wakulla shay-in ahsaynahu kitaba

Swahili
 
Na kila kitu Sisi tumekidhibiti kwa kukiandika.

Ayah  78:30  الأية
فَذُوقُوا فَلَن نَّزِيدَكُمْ إِلَّا عَذَابًا
Fathooqoo falan nazeedakum illaAAathaba

Swahili
 
Basi onjeni! Nasi hatutakuzidishieni ila adhabu!

Ayah  78:31  الأية
إِنَّ لِلْمُتَّقِينَ مَفَازًا
Inna lilmuttaqeena mafaza

Swahili
 
Hakika wachamngu wanastahiki kufuzu,

Ayah  78:32  الأية
حَدَائِقَ وَأَعْنَابًا
Hada-iqa waaAAnaba

Swahili
 
Mabustani na mizabibu,

Ayah  78:33  الأية
وَكَوَاعِبَ أَتْرَابًا
WakawaAAiba atraba

Swahili
 
Na wake walio lingana nao,

Ayah  78:34  الأية
وَكَأْسًا دِهَاقًا
Waka/san dihaqa

Swahili
 
Na bilauri zilizo jaa,

Ayah  78:35  الأية
لَّا يَسْمَعُونَ فِيهَا لَغْوًا وَلَا كِذَّابًا
La yasmaAAoona feeha laghwanwala kiththaba

Swahili
 
Hawatasikia humo upuuzi wala uwongo -

Ayah  78:36  الأية
جَزَاءً مِّن رَّبِّكَ عَطَاءً حِسَابًا
Jazaan min rabbika AAataan hisaba

Swahili
 
Malipo kutoka kwa Mola wako Mlezi, kipawa cha kutosha.

Ayah  78:37  الأية
رَّبِّ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَمَا بَيْنَهُمَا الرَّحْمَٰنِ ۖ لَا يَمْلِكُونَ مِنْهُ خِطَابًا
Rabbi assamawati wal-ardiwama baynahuma arrahmani layamlikoona minhu khitaba

Swahili
 
Mola Mlezi wa mbingu na ardhi na vilio baina yao, Arrahman, Mwingi wa rehema; hawamiliki usemi mbele yake!

Ayah  78:38  الأية
يَوْمَ يَقُومُ الرُّوحُ وَالْمَلَائِكَةُ صَفًّا ۖ لَّا يَتَكَلَّمُونَ إِلَّا مَنْ أَذِنَ لَهُ الرَّحْمَٰنُ وَقَالَ صَوَابًا
Yawma yaqoomu arroohu walmala-ikatusaffan la yatakallamoona illa man athinalahu arrahmanu waqala sawaba

Swahili
 
Siku atakapo simama Roho na Malaika kwa safu. Hawatasema ila Mwingi wa rehema aliye mruhusu, na atasema yaliyo sawa tu.

Ayah  78:39  الأية
ذَٰلِكَ الْيَوْمُ الْحَقُّ ۖ فَمَن شَاءَ اتَّخَذَ إِلَىٰ رَبِّهِ مَآبًا
Thalika alyawmu alhaqqu famanshaa ittakhatha ila rabbihi maaba

Swahili
 
Hiyo ndiyo Siku ya haki. Basi anaye taka na ashike njia arejee kwa Mola wake Mlezi.

Ayah  78:40  الأية
إِنَّا أَنذَرْنَاكُمْ عَذَابًا قَرِيبًا يَوْمَ يَنظُرُ الْمَرْءُ مَا قَدَّمَتْ يَدَاهُ وَيَقُولُ الْكَافِرُ يَا لَيْتَنِي كُنتُ تُرَابًا
Inna antharnakum AAathabanqareeban yawma yanthuru almaro ma qaddamatyadahu wayaqoolu alkafiru ya laytanee kuntuturaba

Swahili
 
Hakika tumekuhadharisheni adhabu iliyo karibu kufika; Siku ambayo mtu atakapo ona yaliyo tangulizwa na mikono yake; na kafiri atasema: Laiti ningeli kuwa udongo!
 


© EsinIslam.Com Designed & produced by The Awqaf London. Please pray for us