1st Ayah 1 الأية ١الأوليبِسْم ِ اللهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ
عَمَّ يَتَسَاءَلُونَ
AAamma yatasaaloon
Swahili
WANAULIZANA nini?
|
Ayah 78:2 الأية
عَنِ النَّبَإِ الْعَظِيمِ
AAani annaba-i alAAatheem
Swahili
Ile khabari kuu,
|
Ayah 78:3 الأية
الَّذِي هُمْ فِيهِ مُخْتَلِفُونَ
Allathee hum feehi mukhtalifoon
Swahili
Ambayo kwayo wanakhitalifiana.
|
Ayah 78:4 الأية
كَلَّا سَيَعْلَمُونَ
Kalla sayaAAlamoon
Swahili
La! Karibu watakuja jua.
|
Ayah 78:5 الأية
ثُمَّ كَلَّا سَيَعْلَمُونَ
Thumma kalla sayaAAlamoon
Swahili
Tena la! Karibu watakuja jua.
|
Ayah 78:6 الأية
أَلَمْ نَجْعَلِ الْأَرْضَ مِهَادًا
Alam najAAali al-arda mihada
Swahili
Kwani hatukuifanya ardhi kama tandiko?
|
Ayah 78:7 الأية
وَالْجِبَالَ أَوْتَادًا
Waljibala awtada
Swahili
Na milima kama vigingi?
|
Ayah 78:8 الأية
وَخَلَقْنَاكُمْ أَزْوَاجًا
Wakhalaqnakum azwaja
Swahili
Na tukakuumbeni kwa jozi?
|
Ayah 78:9 الأية
وَجَعَلْنَا نَوْمَكُمْ سُبَاتًا
WajaAAalna nawmakum subata
Swahili
Na tukakufanya kulala kwenu ni mapumziko?
|
Ayah 78:10 الأية
وَجَعَلْنَا اللَّيْلَ لِبَاسًا
WajaAAalna allayla libasa
Swahili
Na tukaufanya usiku ni nguo?
|
Ayah 78:11 الأية
وَجَعَلْنَا النَّهَارَ مَعَاشًا
WajaAAalna annaharamaAAasha
Swahili
Na tukaufanya mchana ni wa kuchumia maisha?
|
Ayah 78:12 الأية
وَبَنَيْنَا فَوْقَكُمْ سَبْعًا شِدَادًا
Wabanayna fawqakum sabAAan shidada
Swahili
Na tukajenga juu yenu saba zenye nguvu?
|
Ayah 78:13 الأية
وَجَعَلْنَا سِرَاجًا وَهَّاجًا
WajaAAalna sirajan wahhaja
Swahili
Na tukaifanya taa yenye mwanga na joto;
|
Ayah 78:14 الأية
وَأَنزَلْنَا مِنَ الْمُعْصِرَاتِ مَاءً ثَجَّاجًا
Waanzalna mina almuAAsiratimaan thajjaja
Swahili
Na tukateremsha maji yanayo anguka kwa kasi kutoka mawinguni,
|
Ayah 78:15 الأية
لِّنُخْرِجَ بِهِ حَبًّا وَنَبَاتًا
Linukhrija bihi habban wanabata
Swahili
Ili tutoe kwayo nafaka na mimea,
|
Ayah 78:16 الأية
وَجَنَّاتٍ أَلْفَافًا
Wajannatin alfafa
Swahili
Na mabustani yenye miti iliyo kamatana.
|
Ayah 78:17 الأية
إِنَّ يَوْمَ الْفَصْلِ كَانَ مِيقَاتًا
Inna yawma alfasli kana meeqata
Swahili
Hakika siku ya uamuzi imewekewa wakati wake,
|
Ayah 78:18 الأية
يَوْمَ يُنفَخُ فِي الصُّورِ فَتَأْتُونَ أَفْوَاجًا
Yawma yunfakhu fee assoorifata/toona afwaja
Swahili
Siku litapo pulizwa barugumu, nanyi mtakuja kwa makundi,
|
Ayah 78:19 الأية
وَفُتِحَتِ السَّمَاءُ فَكَانَتْ أَبْوَابًا
Wafutihati assamao fakanatabwaba
Swahili
Na mbingu zitafunguliwa, ziwe milango,
|
Ayah 78:20 الأية
وَسُيِّرَتِ الْجِبَالُ فَكَانَتْ سَرَابًا
Wasuyyirati aljibalu fakanatsaraba
Swahili
Na milima itaondolewa na itakuwa kama sarabi.
|
Ayah 78:21 الأية
إِنَّ جَهَنَّمَ كَانَتْ مِرْصَادًا
Inna jahannama kanat mirsada
Swahili
Hakika Jahannamu inangojea!
|
Ayah 78:22 الأية
لِّلطَّاغِينَ مَآبًا
Littagheena maaba
Swahili
Kwa walio asi ndio makaazi yao,
|
Ayah 78:23 الأية
لَّابِثِينَ فِيهَا أَحْقَابًا
Labitheena feeha ahqaba
Swahili
Wakae humo karne baada ya karne,
|
Ayah 78:24 الأية
لَّا يَذُوقُونَ فِيهَا بَرْدًا وَلَا شَرَابًا
La yathooqoona feehabardan wala sharaba
Swahili
Hawataonja humo chochote kibaridi wala kinywaji,
|
Ayah 78:25 الأية
إِلَّا حَمِيمًا وَغَسَّاقًا
Illa hameeman waghassaqa
Swahili
Ila maji yamoto sana na usaha,
|
Ayah 78:26 الأية
جَزَاءً وِفَاقًا
Jazaan wifaqa
Swahili
Ndio jaza muwafaka.
|
Ayah 78:27 الأية
إِنَّهُمْ كَانُوا لَا يَرْجُونَ حِسَابًا
Innahum kanoo la yarjoona hisaba
Swahili
Hakika hao hawakuwa wakitaraji kuwa kuna hisabu.
|
Ayah 78:28 الأية
وَكَذَّبُوا بِآيَاتِنَا كِذَّابًا
Wakaththaboo bi-ayatinakiththaba
Swahili
Na wakikanusha Aya zetu kwa nguvu.
|
Ayah 78:29 الأية
وَكُلَّ شَيْءٍ أَحْصَيْنَاهُ كِتَابًا
Wakulla shay-in ahsaynahu kitaba
Swahili
Na kila kitu Sisi tumekidhibiti kwa kukiandika.
|
Ayah 78:30 الأية
فَذُوقُوا فَلَن نَّزِيدَكُمْ إِلَّا عَذَابًا
Fathooqoo falan nazeedakum illaAAathaba
Swahili
Basi onjeni! Nasi hatutakuzidishieni ila adhabu!
|
Ayah 78:31 الأية
إِنَّ لِلْمُتَّقِينَ مَفَازًا
Inna lilmuttaqeena mafaza
Swahili
Hakika wachamngu wanastahiki kufuzu,
|
Ayah 78:32 الأية
حَدَائِقَ وَأَعْنَابًا
Hada-iqa waaAAnaba
Swahili
Mabustani na mizabibu,
|
Ayah 78:33 الأية
وَكَوَاعِبَ أَتْرَابًا
WakawaAAiba atraba
Swahili
Na wake walio lingana nao,
|
Ayah 78:34 الأية
وَكَأْسًا دِهَاقًا
Waka/san dihaqa
Swahili
Na bilauri zilizo jaa,
|
Ayah 78:35 الأية
لَّا يَسْمَعُونَ فِيهَا لَغْوًا وَلَا كِذَّابًا
La yasmaAAoona feeha laghwanwala kiththaba
Swahili
Hawatasikia humo upuuzi wala uwongo -
|
Ayah 78:36 الأية
جَزَاءً مِّن رَّبِّكَ عَطَاءً حِسَابًا
Jazaan min rabbika AAataan hisaba
Swahili
Malipo kutoka kwa Mola wako Mlezi, kipawa cha kutosha.
|
Ayah 78:37 الأية
رَّبِّ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَمَا بَيْنَهُمَا الرَّحْمَٰنِ ۖ لَا
يَمْلِكُونَ مِنْهُ خِطَابًا
Rabbi assamawati wal-ardiwama baynahuma arrahmani layamlikoona minhu khitaba
Swahili
Mola Mlezi wa mbingu na ardhi na vilio baina yao, Arrahman, Mwingi wa rehema;
hawamiliki usemi mbele yake!
|
Ayah 78:38 الأية
يَوْمَ يَقُومُ الرُّوحُ وَالْمَلَائِكَةُ صَفًّا ۖ لَّا يَتَكَلَّمُونَ إِلَّا
مَنْ أَذِنَ لَهُ الرَّحْمَٰنُ وَقَالَ صَوَابًا
Yawma yaqoomu arroohu walmala-ikatusaffan la yatakallamoona illa man athinalahu
arrahmanu waqala sawaba
Swahili
Siku atakapo simama Roho na Malaika kwa safu. Hawatasema ila Mwingi wa rehema
aliye mruhusu, na atasema yaliyo sawa tu.
|
Ayah 78:39 الأية
ذَٰلِكَ الْيَوْمُ الْحَقُّ ۖ فَمَن شَاءَ اتَّخَذَ إِلَىٰ رَبِّهِ مَآبًا
Thalika alyawmu alhaqqu famanshaa ittakhatha ila rabbihi maaba
Swahili
Hiyo ndiyo Siku ya haki. Basi anaye taka na ashike njia arejee kwa Mola wake
Mlezi.
|
Ayah 78:40 الأية
إِنَّا أَنذَرْنَاكُمْ عَذَابًا قَرِيبًا يَوْمَ يَنظُرُ الْمَرْءُ مَا قَدَّمَتْ
يَدَاهُ وَيَقُولُ الْكَافِرُ يَا لَيْتَنِي كُنتُ تُرَابًا
Inna antharnakum AAathabanqareeban yawma yanthuru almaro ma qaddamatyadahu
wayaqoolu alkafiru ya laytanee kuntuturaba
Swahili
Hakika tumekuhadharisheni adhabu iliyo karibu kufika; Siku ambayo mtu atakapo
ona yaliyo tangulizwa na mikono yake; na kafiri atasema: Laiti ningeli kuwa
udongo!
|
©
EsinIslam.Com Designed & produced by The Awqaf London. Please pray for us
|