« Prev
82. Surah Al-Infitâr سورة الإنفطار
Next »
First Ayah 1 الأية الأوليبِسْم ِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ
إِذَا السَّمَاءُ انفَطَرَتْ
Swahili
Mbingu itapo chanika,
|
Ayah 82:2 الأية
وَإِذَا الْكَوَاكِبُ انتَثَرَتْ
Swahili
Na nyota zitapo tawanyika,
|
Ayah 82:3 الأية
وَإِذَا الْبِحَارُ فُجِّرَتْ
Swahili
Na bahari zitakapo pasuliwa,
|
Ayah 82:4 الأية
وَإِذَا الْقُبُورُ بُعْثِرَتْ
Swahili
Na makaburi yatapo fukuliwa,
|
Ayah 82:5 الأية
عَلِمَتْ نَفْسٌ مَّا قَدَّمَتْ وَأَخَّرَتْ
Swahili
Hapo kila nafsi itajua ilicho tanguliza, na ilicho bakisha nyuma.
|
Ayah 82:6 الأية
يَا أَيُّهَا الْإِنسَانُ مَا غَرَّكَ بِرَبِّكَ الْكَرِيمِ
Swahili
Ewe mwanaadamu! Nini kilicho kughuri ukamwacha Mola wako Mlezi Mtukufu?
|
Ayah 82:7 الأية
الَّذِي خَلَقَكَ فَسَوَّاكَ فَعَدَلَكَ
Swahili
Aliye kuumba, akakuweka sawa, akakunyoosha,
|
Ayah 82:8 الأية
فِي أَيِّ صُورَةٍ مَّا شَاءَ رَكَّبَكَ
Swahili
Katika sura yoyote aliyo ipenda akakujenga.
|
Ayah 82:9 الأية
كَلَّا بَلْ تُكَذِّبُونَ بِالدِّينِ
Swahili
Sivyo hivyo! Bali nyinyi mnaikanusha Siku ya Malipo.
|
Ayah 82:10 الأية
وَإِنَّ عَلَيْكُمْ لَحَافِظِينَ
Swahili
Na hakika bila ya shaka wapo walinzi juu yenu,
|
Ayah 82:11 الأية
كِرَامًا كَاتِبِينَ
Swahili
Waandishi wenye hishima,
|
Ayah 82:12 الأية
يَعْلَمُونَ مَا تَفْعَلُونَ
Swahili
Wanayajua mnayo yatenda.
|
Ayah 82:13 الأية
إِنَّ الْأَبْرَارَ لَفِي نَعِيمٍ
Swahili
Hakika wema bila ya shaka watakuwa katika neema,
|
Ayah 82:14 الأية
وَإِنَّ الْفُجَّارَ لَفِي جَحِيمٍ
Swahili
Na hakika waovu bila ya shaka watakuwa Motoni;
|
Ayah 82:15 الأية
يَصْلَوْنَهَا يَوْمَ الدِّينِ
Swahili
Wataingia humo Siku ya Malipo.
|
Ayah 82:16 الأية
وَمَا هُمْ عَنْهَا بِغَائِبِينَ
Swahili
Na hawatoacha kuwamo humo.
|
Ayah 82:17 الأية
وَمَا أَدْرَاكَ مَا يَوْمُ الدِّينِ
Swahili
Na nini kitakacho kujuulisha Siku ya Malipo ni siku gani?
|
Ayah 82:18 الأية
ثُمَّ مَا أَدْرَاكَ مَا يَوْمُ الدِّينِ
Swahili
Tena nini kitakacho kujuulisha Siku ya Malipo ni siku gani?
|
Ayah 82:19 الأية
يَوْمَ لَا تَمْلِكُ نَفْسٌ لِّنَفْسٍ شَيْئًا ۖ وَالْأَمْرُ يَوْمَئِذٍ لِّلَّهِ
Swahili
Siku ambayo nafsi haitakuwa na madaraka yoyote juu ya nafsi; na amri yote siku
hiyo ni ya Mwenyezi Mungu tu.
|
©
EsinIslam.Com Designed & produced by The Awqaf London. Please pray for us
|
|