« Prev

82. Surah Al-Infitâr سورة الإنفطار

Next »



First Ayah   1   الأية الأولي
بِسْم ِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ
إِذَا السَّمَاءُ انفَطَرَتْ
Swahili
 
Mbingu itapo chanika,

Ayah   82:2   الأية
وَإِذَا الْكَوَاكِبُ انتَثَرَتْ
Swahili
 
Na nyota zitapo tawanyika,

Ayah   82:3   الأية
وَإِذَا الْبِحَارُ فُجِّرَتْ
Swahili
 
Na bahari zitakapo pasuliwa,

Ayah   82:4   الأية
وَإِذَا الْقُبُورُ بُعْثِرَتْ
Swahili
 
Na makaburi yatapo fukuliwa,

Ayah   82:5   الأية
عَلِمَتْ نَفْسٌ مَّا قَدَّمَتْ وَأَخَّرَتْ
Swahili
 
Hapo kila nafsi itajua ilicho tanguliza, na ilicho bakisha nyuma.

Ayah   82:6   الأية
يَا أَيُّهَا الْإِنسَانُ مَا غَرَّكَ بِرَبِّكَ الْكَرِيمِ
Swahili
 
Ewe mwanaadamu! Nini kilicho kughuri ukamwacha Mola wako Mlezi Mtukufu?

Ayah   82:7   الأية
الَّذِي خَلَقَكَ فَسَوَّاكَ فَعَدَلَكَ
Swahili
 
Aliye kuumba, akakuweka sawa, akakunyoosha,

Ayah   82:8   الأية
فِي أَيِّ صُورَةٍ مَّا شَاءَ رَكَّبَكَ
Swahili
 
Katika sura yoyote aliyo ipenda akakujenga.

Ayah   82:9   الأية
كَلَّا بَلْ تُكَذِّبُونَ بِالدِّينِ
Swahili
 
Sivyo hivyo! Bali nyinyi mnaikanusha Siku ya Malipo.

Ayah   82:10   الأية
وَإِنَّ عَلَيْكُمْ لَحَافِظِينَ
Swahili
 
Na hakika bila ya shaka wapo walinzi juu yenu,

Ayah   82:11   الأية
كِرَامًا كَاتِبِينَ
Swahili
 
Waandishi wenye hishima,

Ayah   82:12   الأية
يَعْلَمُونَ مَا تَفْعَلُونَ
Swahili
 
Wanayajua mnayo yatenda.

Ayah   82:13   الأية
إِنَّ الْأَبْرَارَ لَفِي نَعِيمٍ
Swahili
 
Hakika wema bila ya shaka watakuwa katika neema,

Ayah   82:14   الأية
وَإِنَّ الْفُجَّارَ لَفِي جَحِيمٍ
Swahili
 
Na hakika waovu bila ya shaka watakuwa Motoni;

Ayah   82:15   الأية
يَصْلَوْنَهَا يَوْمَ الدِّينِ
Swahili
 
Wataingia humo Siku ya Malipo.

Ayah   82:16   الأية
وَمَا هُمْ عَنْهَا بِغَائِبِينَ
Swahili
 
Na hawatoacha kuwamo humo.

Ayah   82:17   الأية
وَمَا أَدْرَاكَ مَا يَوْمُ الدِّينِ
Swahili
 
Na nini kitakacho kujuulisha Siku ya Malipo ni siku gani?

Ayah   82:18   الأية
ثُمَّ مَا أَدْرَاكَ مَا يَوْمُ الدِّينِ
Swahili
 
Tena nini kitakacho kujuulisha Siku ya Malipo ni siku gani?

Ayah   82:19   الأية
يَوْمَ لَا تَمْلِكُ نَفْسٌ لِّنَفْسٍ شَيْئًا ۖ وَالْأَمْرُ يَوْمَئِذٍ لِّلَّهِ
Swahili
 
Siku ambayo nafsi haitakuwa na madaraka yoyote juu ya nafsi; na amri yote siku hiyo ni ya Mwenyezi Mungu tu.
 


© EsinIslam.Com Designed & produced by The Awqaf London. Please pray for us