Prev  

51. Surah Az-Zâriyât سورة الذاريات

  Next  



Ayah  51:1  الأية
    +/- -/+  
بِسْم ِ اللهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ

Ayah  51:2  الأية
    +/- -/+  

Ayah  51:3  الأية
    +/- -/+  

Ayah  51:4  الأية
    +/- -/+  

Ayah  51:5  الأية
    +/- -/+  

Ayah  51:6  الأية
    +/- -/+  

Ayah  51:7  الأية
    +/- -/+  

Ayah  51:8  الأية
    +/- -/+  
إِنَّكُمْ لَفِي قَوْلٍ مُّخْتَلِفٍ
Swahili
 
Hakika nyinyi bila ya shaka mmo katika kauli inayo khitalifiana.

Ayah  51:9  الأية
    +/- -/+  

Ayah  51:10  الأية
    +/- -/+  

Ayah  51:11  الأية
    +/- -/+  

Ayah  51:12  الأية
    +/- -/+  
يَسْأَلُونَ أَيَّانَ يَوْمُ الدِّينِ
Swahili
 
Wanauliza: Ni lini hiyo siku ya malipo?

Ayah  51:13  الأية
    +/- -/+  
يَوْمَ هُمْ عَلَى النَّارِ يُفْتَنُونَ
Swahili
 
Hiyo ni siku watakayo adhibiwa Motoni.

Ayah  51:14  الأية
    +/- -/+  
ذُوقُوا فِتْنَتَكُمْ هَٰذَا الَّذِي كُنتُم بِهِ تَسْتَعْجِلُونَ
Swahili
 
Onjeni adhabu yenu! Haya ndiyo mliyo kuwa mkiyahimiza.

Ayah  51:15  الأية
    +/- -/+  
إِنَّ الْمُتَّقِينَ فِي جَنَّاتٍ وَعُيُونٍ
Swahili
 
Hakika wachamngu watakuwa katika Mabustani na chemchem.

Ayah  51:16  الأية
    +/- -/+  
آخِذِينَ مَا آتَاهُمْ رَبُّهُمْ ۚ إِنَّهُمْ كَانُوا قَبْلَ ذَٰلِكَ مُحْسِنِينَ
Swahili
 
Wanapokea aliyo wapa Mola wao Mlezi. Kwa hakika hao walikuwa kabla ya haya wakifanya mema.

Ayah  51:17  الأية
    +/- -/+  
كَانُوا قَلِيلًا مِّنَ اللَّيْلِ مَا يَهْجَعُونَ
Swahili
 
Walikuwa wakilala kidogo tu usiku.

Ayah  51:18  الأية
    +/- -/+  
وَبِالْأَسْحَارِ هُمْ يَسْتَغْفِرُونَ
Swahili
 
Na kabla ya alfajiri wakiomba maghfira.

Ayah  51:19  الأية
    +/- -/+  
وَفِي أَمْوَالِهِمْ حَقٌّ لِّلسَّائِلِ وَالْمَحْرُومِ
Swahili
 
Na katika mali yao ipo haki ya mwenye kuomba na asiye omba.

Ayah  51:20  الأية
    +/- -/+  
وَفِي الْأَرْضِ آيَاتٌ لِّلْمُوقِنِينَ
Swahili
 
Na katika ardhi zipo Ishara kwa wenye yakini.

Ayah  51:21  الأية
    +/- -/+  
وَفِي أَنفُسِكُمْ ۚ أَفَلَا تُبْصِرُونَ
Swahili
 
Na pia katika nafsi zenu - Je! Hamwoni?

Ayah  51:22  الأية
    +/- -/+  
وَفِي السَّمَاءِ رِزْقُكُمْ وَمَا تُوعَدُونَ
Swahili
 
Na katika mbingu ziko riziki zenu na mliyo ahidiwa.

Ayah  51:23  الأية
    +/- -/+  
فَوَرَبِّ السَّمَاءِ وَالْأَرْضِ إِنَّهُ لَحَقٌّ مِّثْلَ مَا أَنَّكُمْ تَنطِقُونَ
Swahili
 
Basi naapa kwa Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, hakika haya ni kweli kama ilivyo kweli kuwa nyinyi mnasema.

Ayah  51:24  الأية
    +/- -/+  
هَلْ أَتَاكَ حَدِيثُ ضَيْفِ إِبْرَاهِيمَ الْمُكْرَمِينَ
Swahili
 
Je! Imekufikia hadithi ya wageni wa Ibrahim wanao hishimiwa?

Ayah  51:25  الأية
    +/- -/+  
إِذْ دَخَلُوا عَلَيْهِ فَقَالُوا سَلَامًا ۖ قَالَ سَلَامٌ قَوْمٌ مُّنكَرُونَ
Swahili
 
Walipo ingia kwake wakasema: Salama! Na yeye akasema: Salama! Nyinyi ni watu nisio kujueni.

Ayah  51:26  الأية
    +/- -/+  
فَرَاغَ إِلَىٰ أَهْلِهِ فَجَاءَ بِعِجْلٍ سَمِينٍ
Swahili
 
Akenda kwa ahali yake na akaja na ndama aliye nona.

Ayah  51:27  الأية
    +/- -/+  
فَقَرَّبَهُ إِلَيْهِمْ قَالَ أَلَا تَأْكُلُونَ
Swahili
 
Akawakaribisha, akasema: Mbona hamli?

Ayah  51:28  الأية
    +/- -/+  
فَأَوْجَسَ مِنْهُمْ خِيفَةً ۖ قَالُوا لَا تَخَفْ ۖ وَبَشَّرُوهُ بِغُلَامٍ عَلِيمٍ
Swahili
 
Akahisi kuwaogopa katika nafsi yake. Wakasema: Usiwe na khofu, nao wakambashiria kupata kijana mwenye ilimu.

Ayah  51:29  الأية
    +/- -/+  
فَأَقْبَلَتِ امْرَأَتُهُ فِي صَرَّةٍ فَصَكَّتْ وَجْهَهَا وَقَالَتْ عَجُوزٌ عَقِيمٌ
Swahili
 
Ndipo mkewe akawaelekea, na huku anasema na akijipiga usoni kwa mastaajabu, na kusema: Mimi ni kikongwe na tasa!

Ayah  51:30  الأية
    +/- -/+  
قَالُوا كَذَٰلِكِ قَالَ رَبُّكِ ۖ إِنَّهُ هُوَ الْحَكِيمُ الْعَلِيمُ
Swahili
 
Wakasema: Ndivyo vivyo hivyo alivyo sema Mola wako Mlezi. Hakika Yeye ni Mwenye hikima na Mwenye kujua.

Ayah  51:31  الأية
    +/- -/+  
قَالَ فَمَا خَطْبُكُمْ أَيُّهَا الْمُرْسَلُونَ
Swahili
 
AKASEMA: Basi ujumbe wenu ni nini, enyi mlio tumwa?

Ayah  51:32  الأية
    +/- -/+  
قَالُوا إِنَّا أُرْسِلْنَا إِلَىٰ قَوْمٍ مُّجْرِمِينَ
Swahili
 
Wakasema: Hakika sisi tumetumwa kwa watu wakosefu,

Ayah  51:33  الأية
    +/- -/+  
لِنُرْسِلَ عَلَيْهِمْ حِجَارَةً مِّن طِينٍ
Swahili
 
Tuwatupie mawe ya udongo,

Ayah  51:34  الأية
    +/- -/+  
مُّسَوَّمَةً عِندَ رَبِّكَ لِلْمُسْرِفِينَ
Swahili
 
Yaliyo tiwa alama kutoka kwa Mola wako Mlezi kwa ajili ya wanao pindukia mipaka.

Ayah  51:35  الأية
    +/- -/+  
فَأَخْرَجْنَا مَن كَانَ فِيهَا مِنَ الْمُؤْمِنِينَ
Swahili
 
Kwa hivyo tutawatoa katika hao wale walio amini.

Ayah  51:36  الأية
    +/- -/+  
فَمَا وَجَدْنَا فِيهَا غَيْرَ بَيْتٍ مِّنَ الْمُسْلِمِينَ
Swahili
 
Lakini hatukupata humo ila nyumba moja tu yenye Waislamu!

Ayah  51:37  الأية
    +/- -/+  
وَتَرَكْنَا فِيهَا آيَةً لِّلَّذِينَ يَخَافُونَ الْعَذَابَ الْأَلِيمَ
Swahili
 
Na tukaacha humo Ishara kwa ajili ya wanao iogopa adhabu chungu.

Ayah  51:38  الأية
    +/- -/+  
وَفِي مُوسَىٰ إِذْ أَرْسَلْنَاهُ إِلَىٰ فِرْعَوْنَ بِسُلْطَانٍ مُّبِينٍ
Swahili
 
Na katika khabari za Musa, tulipo mtuma kwa Firauni na hoja wazi.

Ayah  51:39  الأية
    +/- -/+  
فَتَوَلَّىٰ بِرُكْنِهِ وَقَالَ سَاحِرٌ أَوْ مَجْنُونٌ
Swahili
 
Lakini alipuuza kwa sababu ya nguvu zake na akasema: Huyu ni mchawi au mwendawazimu!

Ayah  51:40  الأية
    +/- -/+  
فَأَخَذْنَاهُ وَجُنُودَهُ فَنَبَذْنَاهُمْ فِي الْيَمِّ وَهُوَ مُلِيمٌ
Swahili
 
Basi tukamkamata yeye na majeshi yake na tukawatupa baharini, na yeye ndiye wa kulaumiwa.

Ayah  51:41  الأية
    +/- -/+  
وَفِي عَادٍ إِذْ أَرْسَلْنَا عَلَيْهِمُ الرِّيحَ الْعَقِيمَ
Swahili
 
Na katika khabari za A'di tulipo wapelekea upepo wa kukata uzazi.

Ayah  51:42  الأية
    +/- -/+  
مَا تَذَرُ مِن شَيْءٍ أَتَتْ عَلَيْهِ إِلَّا جَعَلَتْهُ كَالرَّمِيمِ
Swahili
 
Haukuacha chochote ulicho kifikia ila ulikifanya kama kilio nyambuka.

Ayah  51:43  الأية
    +/- -/+  
وَفِي ثَمُودَ إِذْ قِيلَ لَهُمْ تَمَتَّعُوا حَتَّىٰ حِينٍ
Swahili
 
Na katika khabari za Thamudi walipo ambiwa: Jifurahisheni kwa muda mdogo tu.

Ayah  51:44  الأية
    +/- -/+  
فَعَتَوْا عَنْ أَمْرِ رَبِّهِمْ فَأَخَذَتْهُمُ الصَّاعِقَةُ وَهُمْ يَنظُرُونَ
Swahili
 
Wakaasi amri ya Mola wao Mlezi. Basi uliwanyakua moto wa radi nao wanaona.

Ayah  51:45  الأية
    +/- -/+  
فَمَا اسْتَطَاعُوا مِن قِيَامٍ وَمَا كَانُوا مُنتَصِرِينَ
Swahili
 
Basi hawakuweza kusimama wala hawakuwa wenye kujitetea.

Ayah  51:46  الأية
    +/- -/+  
وَقَوْمَ نُوحٍ مِّن قَبْلُ ۖ إِنَّهُمْ كَانُوا قَوْمًا فَاسِقِينَ
Swahili
 
Na kaumu ya Nuhu hapo mbele. Hakika hao walikuwa watu wapotovu.

Ayah  51:47  الأية
    +/- -/+  
وَالسَّمَاءَ بَنَيْنَاهَا بِأَيْدٍ وَإِنَّا لَمُوسِعُونَ
Swahili
 
Na mbingu tumezifanya kwa nguvu na uwezo na hakika Sisi bila ya shaka ndio twenye uwezo wa kuzitanua.

Ayah  51:48  الأية
    +/- -/+  
وَالْأَرْضَ فَرَشْنَاهَا فَنِعْمَ الْمَاهِدُونَ
Swahili
 
Na ardhi tumeitandaza; basi watandazaji wazuri namna gani Sisi!

Ayah  51:49  الأية
    +/- -/+  
وَمِن كُلِّ شَيْءٍ خَلَقْنَا زَوْجَيْنِ لَعَلَّكُمْ تَذَكَّرُونَ
Swahili
 
Na katika kila kitu tumeumba kwa jozi ili mzingatie.

Ayah  51:50  الأية
    +/- -/+  
فَفِرُّوا إِلَى اللهِ ۖ إِنِّي لَكُم مِّنْهُ نَذِيرٌ مُّبِينٌ
Swahili
 
Basi kimbilieni kwa Mwenyezi Mungu, hakika mimi ni mwonyaji kwenu wa kubainisha nitokae kwake.

Ayah  51:51  الأية
    +/- -/+  
وَلَا تَجْعَلُوا مَعَ اللهِ إِلَٰهًا آخَرَ ۖ إِنِّي لَكُم مِّنْهُ نَذِيرٌ مُّبِينٌ
Swahili
 
Wala msifanye kuwa kuna mungu mwengine pamoja na Mwenyezi Mungu. Hakika mimi ni mwonyaji kwenu wa kubainisha nitokae kwake.

Ayah  51:52  الأية
    +/- -/+  
كَذَٰلِكَ مَا أَتَى الَّذِينَ مِن قَبْلِهِم مِّن رَّسُولٍ إِلَّا قَالُوا سَاحِرٌ أَوْ مَجْنُونٌ
Swahili
 
Basi ndio hivyo hivyo, hakuwajia kabla yao Mtume ila walisema: Huyu ni mchawi au mwendawazimu.

Ayah  51:53  الأية
    +/- -/+  
أَتَوَاصَوْا بِهِ ۚ بَلْ هُمْ قَوْمٌ طَاغُونَ
Swahili
 
Je! Wameambizana kwa haya? Bali hawa ni watu waasi.

Ayah  51:54  الأية
    +/- -/+  
فَتَوَلَّ عَنْهُمْ فَمَا أَنتَ بِمَلُومٍ
Swahili
 
Basi waachilie mbali, nawe hulaumiwi.

Ayah  51:55  الأية
    +/- -/+  
وَذَكِّرْ فَإِنَّ الذِّكْرَىٰ تَنفَعُ الْمُؤْمِنِينَ
Swahili
 
Na kumbusha, kwani ukumbusho huwafaa Waumini.

Ayah  51:56  الأية
    +/- -/+  
وَمَا خَلَقْتُ الْجِنَّ وَالْإِنسَ إِلَّا لِيَعْبُدُونِ
Swahili
 
Nami sikuwaumba majini na watu ila waniabudu Mimi.

Ayah  51:57  الأية
    +/- -/+  
مَا أُرِيدُ مِنْهُم مِّن رِّزْقٍ وَمَا أُرِيدُ أَن يُطْعِمُونِ
Swahili
 
Na sitaki kwao riziki, wala sitaki wanilishe.

Ayah  51:58  الأية
    +/- -/+  
إِنَّ اللهَ هُوَ الرَّزَّاقُ ذُو الْقُوَّةِ الْمَتِينُ
Swahili
 
Hakika Mwenyezi Mungu ndiye Mwenye kuruzuku, Mwenye nguvu, Madhubuti.

Ayah  51:59  الأية
    +/- -/+  
فَإِنَّ لِلَّذِينَ ظَلَمُوا ذَنُوبًا مِّثْلَ ذَنُوبِ أَصْحَابِهِمْ فَلَا يَسْتَعْجِلُونِ
Swahili
 
Hakika walio dhulumu wana fungu lao la adhabu kama fungu la wenzao. Basi wasinihimize.

Ayah  51:60  الأية
    +/- -/+  
فَوَيْلٌ لِّلَّذِينَ كَفَرُوا مِن يَوْمِهِمُ الَّذِي يُوعَدُونَ
Swahili
 
Ole wao walio ikanusha siku yao waliyo ahidiwa.
 


© EsinIslam.Com Designed & produced by The Awqaf London. Please pray for us