« Prev

71. Surah Nûh سورة نوح

Next »



First Ayah   1   الأية الأولي
بِسْم ِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ
إِنَّا أَرْسَلْنَا نُوحًا إِلَىٰ قَوْمِهِ أَنْ أَنذِرْ قَوْمَكَ مِن قَبْلِ أَن يَأْتِيَهُمْ عَذَابٌ أَلِيمٌ
Swahili
 
Hakika Sisi tulimtuma Nuh'u kwa watu wake: Uwaonye kaumu yako kabla ya kuwafikia adhabu chungu.

Ayah   71:2   الأية
قَالَ يَا قَوْمِ إِنِّي لَكُمْ نَذِيرٌ مُّبِينٌ
Swahili
 
Akasema: Enyi watu wangu! Kwa hakika mimi ni mwonyaji wa dhaahiri kwenu,

Ayah   71:3   الأية
أَنِ اعْبُدُوا اللَّهَ وَاتَّقُوهُ وَأَطِيعُونِ
Swahili
 
Ya kwamba mumuabudu Mwenyezi Mungu, na mumche Yeye, na mumt'ii.

Ayah   71:4   الأية
يَغْفِرْ لَكُم مِّن ذُنُوبِكُمْ وَيُؤَخِّرْكُمْ إِلَىٰ أَجَلٍ مُّسَمًّى ۚ إِنَّ أَجَلَ اللَّهِ إِذَا جَاءَ لَا يُؤَخَّرُ ۖ لَوْ كُنتُمْ تَعْلَمُونَ
Swahili
 
Atakughufirieni madhambi yenu, na atakuakhirisheni mpaka muda ulio wekwa. Hakika muda wa Mwenyezi Mungu utapo fika haucheleweshwi. Laiti mngejua!

Ayah   71:5   الأية
قَالَ رَبِّ إِنِّي دَعَوْتُ قَوْمِي لَيْلًا وَنَهَارًا
Swahili
 
Akasema: Ee Mola wangu Mlezi! Hakika mimi nimewaita watu wangu usiku na mchana,

Ayah   71:6   الأية
فَلَمْ يَزِدْهُمْ دُعَائِي إِلَّا فِرَارًا
Swahili
 
Lakini wito wangu haukuwazidisha ila kukimbia.

Ayah   71:7   الأية
وَإِنِّي كُلَّمَا دَعَوْتُهُمْ لِتَغْفِرَ لَهُمْ جَعَلُوا أَصَابِعَهُمْ فِي آذَانِهِمْ وَاسْتَغْشَوْا ثِيَابَهُمْ وَأَصَرُّوا وَاسْتَكْبَرُوا اسْتِكْبَارًا
Swahili
 
Na hakika mimi kila nilipo waita ili upate kuwaghufiria, walijiziba masikio yao kwa vidole vyao, na wakajigubika nguo zao, na wakakamia, na wakatakabari vikubwa mno!

Ayah   71:8   الأية
ثُمَّ إِنِّي دَعَوْتُهُمْ جِهَارًا
Swahili
 
Tena niliwaita kwa uwazi,

Ayah   71:9   الأية
ثُمَّ إِنِّي أَعْلَنتُ لَهُمْ وَأَسْرَرْتُ لَهُمْ إِسْرَارًا
Swahili
 
Kisha nikawatangazia kwa kelele, tena nikasema nao kwa siri.

Ayah   71:10   الأية
فَقُلْتُ اسْتَغْفِرُوا رَبَّكُمْ إِنَّهُ كَانَ غَفَّارًا
Swahili
 
Nikasema: Ombeni msamaha kwa Mola wenu Mlezi; hakika Yeye ni Mwingi wa kusamehe.

Ayah   71:11   الأية
يُرْسِلِ السَّمَاءَ عَلَيْكُم مِّدْرَارًا
Swahili
 
Atakuleteeni mvua inyeshe mfululizo.

Ayah   71:12   الأية
وَيُمْدِدْكُم بِأَمْوَالٍ وَبَنِينَ وَيَجْعَل لَّكُمْ جَنَّاتٍ وَيَجْعَل لَّكُمْ أَنْهَارًا
Swahili
 
Na atakupeni mali na wana, na atakupeni mabustani na atakufanyieni mito.

Ayah   71:13   الأية
مَّا لَكُمْ لَا تَرْجُونَ لِلَّهِ وَقَارًا
Swahili
 
Mna nini hamweki heshima ya Mwenyezi Mungu?

Ayah   71:14   الأية
وَقَدْ خَلَقَكُمْ أَطْوَارًا
Swahili
 
Na hali Yeye kakuumbeni daraja baada ya daraja?

Ayah   71:15   الأية
أَلَمْ تَرَوْا كَيْفَ خَلَقَ اللَّهُ سَبْعَ سَمَاوَاتٍ طِبَاقًا
Swahili
 
Kwani hamwoni jinsi Mwenyezi Mungu alivyo ziumba mbingu saba kwa matabaka?

Ayah   71:16   الأية
وَجَعَلَ الْقَمَرَ فِيهِنَّ نُورًا وَجَعَلَ الشَّمْسَ سِرَاجًا
Swahili
 
Na akaufanya mwezi ndani yake uwe nuru, na akalifanya jua kuwa taa?

Ayah   71:17   الأية
وَاللَّهُ أَنبَتَكُم مِّنَ الْأَرْضِ نَبَاتًا
Swahili
 
Na Mwenyezi Mungu amekuotesheni katika ardhi kama mimea.

Ayah   71:18   الأية
ثُمَّ يُعِيدُكُمْ فِيهَا وَيُخْرِجُكُمْ إِخْرَاجًا
Swahili
 
Kisha atakurudsheni humo na atakutoeni tena.

Ayah   71:19   الأية
وَاللَّهُ جَعَلَ لَكُمُ الْأَرْضَ بِسَاطًا
Swahili
 
Na Mwenyezi Mungu amekukunjulieni ardhi kama busati.

Ayah   71:20   الأية
لِّتَسْلُكُوا مِنْهَا سُبُلًا فِجَاجًا
Swahili
 
Ili mtembee humo katika njia zilizo pana.

Ayah   71:21   الأية
قَالَ نُوحٌ رَّبِّ إِنَّهُمْ عَصَوْنِي وَاتَّبَعُوا مَن لَّمْ يَزِدْهُ مَالُهُ وَوَلَدُهُ إِلَّا خَسَارًا
Swahili
 
Nuh'u akasema: Mola wangu Mlezi! Hakika hao wameniasi, na wamemfuata yule ambaye mali yake na wanawe hawakumzidishia ila khasara.

Ayah   71:22   الأية
وَمَكَرُوا مَكْرًا كُبَّارًا
Swahili
 
Na wakapanga vitimbi vikubwa.

Ayah   71:23   الأية
وَقَالُوا لَا تَذَرُنَّ آلِهَتَكُمْ وَلَا تَذَرُنَّ وَدًّا وَلَا سُوَاعًا وَلَا يَغُوثَ وَيَعُوقَ وَنَسْرًا
Swahili
 
Na wakasema: Msiwaache miungu yenu, wala msimwache Wadda wala Suwaa' wala Yaghutha, wala Yau'qa, wala Nasra.

Ayah   71:24   الأية
وَقَدْ أَضَلُّوا كَثِيرًا ۖ وَلَا تَزِدِ الظَّالِمِينَ إِلَّا ضَلَالًا
Swahili
 
Na hao walikwisha wapoteza wengi, wala usiwazidishie walio dhulumu ila kupotea.

Ayah   71:25   الأية
مِّمَّا خَطِيئَاتِهِمْ أُغْرِقُوا فَأُدْخِلُوا نَارًا فَلَمْ يَجِدُوا لَهُم مِّن دُونِ اللَّهِ أَنصَارًا
Swahili
 
Basi kwa ajili ya makosa yao waligharikishwa wakaingizwa Motoni, wala hawakuwapata wa kuwanusuru badala ya Mwenyezi Mungu.

Ayah   71:26   الأية
وَقَالَ نُوحٌ رَّبِّ لَا تَذَرْ عَلَى الْأَرْضِ مِنَ الْكَافِرِينَ دَيَّارًا
Swahili
 
Na Nuh'u akasema: Mola wangu Mlezi! Usimwache juu ya ardhi mkaazi wake yeyote katika makafiri!

Ayah   71:27   الأية
إِنَّكَ إِن تَذَرْهُمْ يُضِلُّوا عِبَادَكَ وَلَا يَلِدُوا إِلَّا فَاجِرًا كَفَّارًا
Swahili
 
Hakika ukiwaacha watawapoteza waja wako, wala wao hawatazaa ila waovu makafiri.

Ayah   71:28   الأية
رَّبِّ اغْفِرْ لِي وَلِوَالِدَيَّ وَلِمَن دَخَلَ بَيْتِيَ مُؤْمِنًا وَلِلْمُؤْمِنِينَ وَالْمُؤْمِنَاتِ وَلَا تَزِدِ الظَّالِمِينَ إِلَّا تَبَارًا
Swahili
 
Mola wangu Mlezi! Nighufirie mimi na wazazi wangu, na kila aliye ingia nyumbani mwangu kuwa ni mwenye kuamini, na Waumini wote wanaume, na Waumini wanawake. Na wala usiwazidishie walio dhulumu ila kupotea.
 


© EsinIslam.Com Designed & produced by The Awqaf London. Please pray for us