Prev  

54. Surah Al-Qamar سورة القمر

  Next  



Ayah  54:1  الأية
    +/- -/+  
بِسْم ِ اللهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ
اقْتَرَبَتِ السَّاعَةُ وَانشَقَّ الْقَمَرُ
Swahili
 
Saa imekaribia, na mwezi umepasuka!

Ayah  54:2  الأية
    +/- -/+  
وَإِن يَرَوْا آيَةً يُعْرِضُوا وَيَقُولُوا سِحْرٌ مُّسْتَمِرٌّ
Swahili
 
Na wakiona Ishara hugeuka upande na husema: Huu uchawi tu unazidi kuendelea.

Ayah  54:3  الأية
    +/- -/+  
وَكَذَّبُوا وَاتَّبَعُوا أَهْوَاءَهُمْ ۚ وَكُلُّ أَمْرٍ مُّسْتَقِرٌّ
Swahili
 
Na wamekanusha na wamefuata matamanio yao. Na kila jambo ni lenye kuthibiti.

Ayah  54:4  الأية
    +/- -/+  
وَلَقَدْ جَاءَهُم مِّنَ الْأَنبَاءِ مَا فِيهِ مُزْدَجَرٌ
Swahili
 
Na bila ya shaka zimewajia khabari zenye makaripio.

Ayah  54:5  الأية
    +/- -/+  
حِكْمَةٌ بَالِغَةٌ ۖ فَمَا تُغْنِ النُّذُرُ
Swahili
 
Hikima kaamili; lakini maonyo hayafai kitu!

Ayah  54:6  الأية
    +/- -/+  
فَتَوَلَّ عَنْهُمْ ۘ يَوْمَ يَدْعُ الدَّاعِ إِلَىٰ شَيْءٍ نُّكُرٍ
Swahili
 
Basi jiepushe nao. Siku atakapo ita mwitaji kuliendea jambo linalo chusha;

Ayah  54:7  الأية
    +/- -/+  
خُشَّعًا أَبْصَارُهُمْ يَخْرُجُونَ مِنَ الْأَجْدَاثِ كَأَنَّهُمْ جَرَادٌ مُّنتَشِرٌ
Swahili
 
Macho yao yatainama; watatoka makaburini kama nzige walio tawanyika,

Ayah  54:8  الأية
    +/- -/+  
مُّهْطِعِينَ إِلَى الدَّاعِ ۖ يَقُولُ الْكَافِرُونَ هَٰذَا يَوْمٌ عَسِرٌ
Swahili
 
Wanamkimbilia mwitaji, na makafiri wanasema: Hii ni siku ngumu.

Ayah  54:9  الأية
    +/- -/+  
كَذَّبَتْ قَبْلَهُمْ قَوْمُ نُوحٍ فَكَذَّبُوا عَبْدَنَا وَقَالُوا مَجْنُونٌ وَازْدُجِرَ
Swahili
 
Kabla yao kaumu ya Nuhu walikanusha; wakamkanusha mja wetu, na wakasema ni mwendawazimu, na akakaripiwa.

Ayah  54:10  الأية
    +/- -/+  
فَدَعَا رَبَّهُ أَنِّي مَغْلُوبٌ فَانتَصِرْ
Swahili
 
Basi akamwomba Mola wake Mlezi akasema: Kwa hakika mimi nimeshindwa, basi ninusuru!

Ayah  54:11  الأية
    +/- -/+  
فَفَتَحْنَا أَبْوَابَ السَّمَاءِ بِمَاءٍ مُّنْهَمِرٍ
Swahili
 
Basi tukaifungua milango ya mbingu kwa maji yanayo miminika.

Ayah  54:12  الأية
    +/- -/+  
وَفَجَّرْنَا الْأَرْضَ عُيُونًا فَالْتَقَى الْمَاءُ عَلَىٰ أَمْرٍ قَدْ قُدِرَ
Swahili
 
Na tukazipasua ardhi kwa chemchem, yakakutana maji kwa jambo lilio kadiriwa.

Ayah  54:13  الأية
    +/- -/+  
وَحَمَلْنَاهُ عَلَىٰ ذَاتِ أَلْوَاحٍ وَدُسُرٍ
Swahili
 
Na tukamchukua kwenye safina ya mbao na kamba.

Ayah  54:14  الأية
    +/- -/+  
تَجْرِي بِأَعْيُنِنَا جَزَاءً لِّمَن كَانَ كُفِرَ
Swahili
 
Ikawa inakwenda kwa nadhari yetu, kuwa ni malipo kwa alivyo kuwa amekanushwa.

Ayah  54:15  الأية
    +/- -/+  
وَلَقَد تَّرَكْنَاهَا آيَةً فَهَلْ مِن مُّدَّكِرٍ
Swahili
 
Na bila ya shaka tuliiacha iwe ni Ishara. Lakini je, yupo anaye kumbuka?

Ayah  54:16  الأية
    +/- -/+  
فَكَيْفَ كَانَ عَذَابِي وَنُذُرِ
Swahili
 
Basi ilikuwaje adhabu yangu, na maonyo yangu.

Ayah  54:17  الأية
    +/- -/+  
وَلَقَدْ يَسَّرْنَا الْقُرْآنَ لِلذِّكْرِ فَهَلْ مِن مُّدَّكِرٍ
Swahili
 
Na bila ya shaka Sisi tumeifanya Qur'ani iwe nyepesi kufahamika. Lakini yupo anaye kumbuka?

Ayah  54:18  الأية
    +/- -/+  
كَذَّبَتْ عَادٌ فَكَيْفَ كَانَ عَذَابِي وَنُذُرِ
Swahili
 
Kina A'di walikanusha. Basi ilikuwaje adhabu yangu na maonyo yangu?

Ayah  54:19  الأية
    +/- -/+  
إِنَّا أَرْسَلْنَا عَلَيْهِمْ رِيحًا صَرْصَرًا فِي يَوْمِ نَحْسٍ مُّسْتَمِرٍّ
Swahili
 
Hakika Sisi tuliwapelekea upepo wa kimbunga katika siku korofi mfululizo,

Ayah  54:20  الأية
    +/- -/+  
تَنزِعُ النَّاسَ كَأَنَّهُمْ أَعْجَازُ نَخْلٍ مُّنقَعِرٍ
Swahili
 
Ukiwang'oa watu kama vigogo vya mitende vilio ng'olewa.

Ayah  54:21  الأية
    +/- -/+  
فَكَيْفَ كَانَ عَذَابِي وَنُذُرِ
Swahili
 
Basi ilikuwaje adhabu yangu na maonyo yangu?

Ayah  54:22  الأية
    +/- -/+  
وَلَقَدْ يَسَّرْنَا الْقُرْآنَ لِلذِّكْرِ فَهَلْ مِن مُّدَّكِرٍ
Swahili
 
Na bila ya shaka Sisi tumeifanya Qur'ani nyepesi kufahamika; lakini yupo anaye kumbuka?

Ayah  54:23  الأية
    +/- -/+  

Ayah  54:24  الأية
    +/- -/+  
فَقَالُوا أَبَشَرًا مِّنَّا وَاحِدًا نَّتَّبِعُهُ إِنَّا إِذًا لَّفِي ضَلَالٍ وَسُعُرٍ
Swahili
 
Wakasema: Ati tumfuate binaadamu mmoja katika sisi? Basi hivyo sisi tutakuwa katika upotofu na kichaa!

Ayah  54:25  الأية
    +/- -/+  
أَأُلْقِيَ الذِّكْرُ عَلَيْهِ مِن بَيْنِنَا بَلْ هُوَ كَذَّابٌ أَشِرٌ
Swahili
 
Ni yeye tu aliye teremshiwa huo ukumbusho kati yetu sote? Bali huyu ni mwongo mwenye kiburi!

Ayah  54:26  الأية
    +/- -/+  
سَيَعْلَمُونَ غَدًا مَّنِ الْكَذَّابُ الْأَشِرُ
Swahili
 
Kesho watajua ni nani huyo mwongo mwenye kiburi.

Ayah  54:27  الأية
    +/- -/+  
إِنَّا مُرْسِلُو النَّاقَةِ فِتْنَةً لَّهُمْ فَارْتَقِبْهُمْ وَاصْطَبِرْ
Swahili
 
Hakika Sisi tutawapelekea ngamia jike ili kuwajaribu, basi watazame tu na ustahamili.

Ayah  54:28  الأية
    +/- -/+  
وَنَبِّئْهُمْ أَنَّ الْمَاءَ قِسْمَةٌ بَيْنَهُمْ ۖ كُلُّ شِرْبٍ مُّحْتَضَرٌ
Swahili
 
Na waambie kwamba maji yatagawanywa baina yao; kila sehemu ya maji itahudhuriwa na aliye khusika.

Ayah  54:29  الأية
    +/- -/+  
فَنَادَوْا صَاحِبَهُمْ فَتَعَاطَىٰ فَعَقَرَ
Swahili
 
Basi wakamwita mtu wao akaja akamchinja.

Ayah  54:30  الأية
    +/- -/+  
فَكَيْفَ كَانَ عَذَابِي وَنُذُرِ
Swahili
 
Basi ilikuwaje adhabu yangu na maonyo yangu!

Ayah  54:31  الأية
    +/- -/+  
إِنَّا أَرْسَلْنَا عَلَيْهِمْ صَيْحَةً وَاحِدَةً فَكَانُوا كَهَشِيمِ الْمُحْتَظِرِ
Swahili
 
Hakika Sisi tuliwapelekea ukelele mmoja tu, wakawa kama mabuwa ya kujengea uwa.

Ayah  54:32  الأية
    +/- -/+  
وَلَقَدْ يَسَّرْنَا الْقُرْآنَ لِلذِّكْرِ فَهَلْ مِن مُّدَّكِرٍ
Swahili
 
Na bila ya shaka Sisi tumeifanya Qur'ani iwe nyepesi kwa kukumbuka, lakini yupo akumbukaye?

Ayah  54:33  الأية
    +/- -/+  
كَذَّبَتْ قَوْمُ لُوطٍ بِالنُّذُرِ
Swahili
 
Kaumu Lut'i nao waliwakadhibisha Waonyaji.

Ayah  54:34  الأية
    +/- -/+  
إِنَّا أَرْسَلْنَا عَلَيْهِمْ حَاصِبًا إِلَّا آلَ لُوطٍ ۖ نَّجَّيْنَاهُم بِسَحَرٍ
Swahili
 
Hakika Sisi tukawapelekea kimbunga cha vijiwe, isipo kuwa wafuasi wa Lut'i. Hao tuliwaokoa karibu na alfajiri.

Ayah  54:35  الأية
    +/- -/+  
نِّعْمَةً مِّنْ عِندِنَا ۚ كَذَٰلِكَ نَجْزِي مَن شَكَرَ
Swahili
 
Kwa neema inayo toka kwetu. Hivyo ndivyo tumlipavyo anaye shukuru.

Ayah  54:36  الأية
    +/- -/+  
وَلَقَدْ أَنذَرَهُم بَطْشَتَنَا فَتَمَارَوْا بِالنُّذُرِ
Swahili
 
Na hakika yeye aliwaonya adhabu yetu; lakini wao waliyatilia shaka hayo maonyo.

Ayah  54:37  الأية
    +/- -/+  
وَلَقَدْ رَاوَدُوهُ عَن ضَيْفِهِ فَطَمَسْنَا أَعْيُنَهُمْ فَذُوقُوا عَذَابِي وَنُذُرِ
Swahili
 
Na walimtaka awape wageni wake. Tukayapofua macho yao, na tukawaambia: Onjeni basi adhabu na maonyo yangu!

Ayah  54:38  الأية
    +/- -/+  
وَلَقَدْ صَبَّحَهُم بُكْرَةً عَذَابٌ مُّسْتَقِرٌّ
Swahili
 
Na iliwafikia wakati wa asubuhi adhabu yangu ya kuendelea.

Ayah  54:39  الأية
    +/- -/+  

Ayah  54:40  الأية
    +/- -/+  
وَلَقَدْ يَسَّرْنَا الْقُرْآنَ لِلذِّكْرِ فَهَلْ مِن مُّدَّكِرٍ
Swahili
 
Na hakika tumeisahilisha Qur'ani kuikumbuka. Lakini yupo anaye kumbuka?

Ayah  54:41  الأية
    +/- -/+  
وَلَقَدْ جَاءَ آلَ فِرْعَوْنَ النُّذُرُ
Swahili
 
Na Waonyaji waliwafikia watu wa Firauni.

Ayah  54:42  الأية
    +/- -/+  
كَذَّبُوا بِآيَاتِنَا كُلِّهَا فَأَخَذْنَاهُمْ أَخْذَ عَزِيزٍ مُّقْتَدِرٍ
Swahili
 
Walizikadhibisha Ishara zetu zote, nasi tukawashika kama anavyo shika Mwenye nguvu Mwenye uweza.

Ayah  54:43  الأية
    +/- -/+  
أَكُفَّارُكُمْ خَيْرٌ مِّنْ أُولَٰئِكُمْ أَمْ لَكُم بَرَاءَةٌ فِي الزُّبُرِ
Swahili
 
Je! Makafiri wenu ni bora kuliko hao, au yameandikwa vitabuni kuwa nyinyi hamtiwi makosani?

Ayah  54:44  الأية
    +/- -/+  
أَمْ يَقُولُونَ نَحْنُ جَمِيعٌ مُّنتَصِرٌ
Swahili
 
Au ndio wanasema: Sisi ni wengi tutashinda tu.

Ayah  54:45  الأية
    +/- -/+  
سَيُهْزَمُ الْجَمْعُ وَيُوَلُّونَ الدُّبُرَ
Swahili
 
Wingi wao huu utashindwa, na wao watasukumwa nyuma.

Ayah  54:46  الأية
    +/- -/+  
بَلِ السَّاعَةُ مَوْعِدُهُمْ وَالسَّاعَةُ أَدْهَىٰ وَأَمَرُّ
Swahili
 
Bali Saa ya Kiyama ndio miadi yao, na Saa hiyo ni nzito zaidi na chungu zaidi.

Ayah  54:47  الأية
    +/- -/+  
إِنَّ الْمُجْرِمِينَ فِي ضَلَالٍ وَسُعُرٍ
Swahili
 
Hakika wakosefu wamo katika upotofu na wazimu.

Ayah  54:48  الأية
    +/- -/+  
يَوْمَ يُسْحَبُونَ فِي النَّارِ عَلَىٰ وُجُوهِهِمْ ذُوقُوا مَسَّ سَقَرَ
Swahili
 
Siku watakapo kokotwa Motoni kifudifudi waambiwe: Onjeni mguso wa Jahannamu!

Ayah  54:49  الأية
    +/- -/+  
إِنَّا كُلَّ شَيْءٍ خَلَقْنَاهُ بِقَدَرٍ
Swahili
 
Kwa hakika Sisi tumekiumba kila kitu kwa kipimo.

Ayah  54:50  الأية
    +/- -/+  
وَمَا أَمْرُنَا إِلَّا وَاحِدَةٌ كَلَمْحٍ بِالْبَصَرِ
Swahili
 
Na amri yetu haikuwa ila ni moja tu, kama kupepesa jicho.

Ayah  54:51  الأية
    +/- -/+  
وَلَقَدْ أَهْلَكْنَا أَشْيَاعَكُمْ فَهَلْ مِن مُّدَّكِرٍ
Swahili
 
Na bila ya shaka tumekwisha waangamiza wenzenu. Lakini yupo anaye kumbuka?

Ayah  54:52  الأية
    +/- -/+  
وَكُلُّ شَيْءٍ فَعَلُوهُ فِي الزُّبُرِ
Swahili
 
Na kila jambo walilo lifanya limo vitabuni.

Ayah  54:53  الأية
    +/- -/+  
وَكُلُّ صَغِيرٍ وَكَبِيرٍ مُّسْتَطَرٌ
Swahili
 
Na kila kidogo na kikubwa kimeandikwa.

Ayah  54:54  الأية
    +/- -/+  
إِنَّ الْمُتَّقِينَ فِي جَنَّاتٍ وَنَهَرٍ
Swahili
 
Hakika wachamngu watakuwa katika Mabustani na mito.

Ayah  54:55  الأية
    +/- -/+  
فِي مَقْعَدِ صِدْقٍ عِندَ مَلِيكٍ مُّقْتَدِرٍ
Swahili
 
Katika makalio ya haki kwa Mfalme Mwenye uweza.
 


© EsinIslam.Com Designed & produced by The Awqaf London. Please pray for us