First Ayah 1 الأية الأوليبِسْم ِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ
الرَّحْمَٰنُ
Swahili
Arrah'man, Mwingi wa Rehema
|
Ayah 55:2 الأية
عَلَّمَ الْقُرْآنَ
Swahili
Amefundisha Qur'ani.
|
Ayah 55:3 الأية
خَلَقَ الْإِنسَانَ
Swahili
Amemuumba mwanaadamu,
|
Ayah 55:4 الأية
عَلَّمَهُ الْبَيَانَ
Swahili
Akamfundisha kubaini.
|
Ayah 55:5 الأية
الشَّمْسُ وَالْقَمَرُ بِحُسْبَانٍ
Swahili
Jua na mwezi huenda kwa hisabu.
|
Ayah 55:6 الأية
وَالنَّجْمُ وَالشَّجَرُ يَسْجُدَانِ
Swahili
Na mimea yenye kutambaa, na miti, inanyenyekea.
|
Ayah 55:7 الأية
وَالسَّمَاءَ رَفَعَهَا وَوَضَعَ الْمِيزَانَ
Swahili
Na mbingu ameziinua, na ameweka mizani,
|
Ayah 55:8 الأية
أَلَّا تَطْغَوْا فِي الْمِيزَانِ
Swahili
Ili msidhulumu katika mizani.
|
Ayah 55:9 الأية
وَأَقِيمُوا الْوَزْنَ بِالْقِسْطِ وَلَا تُخْسِرُوا الْمِيزَانَ
Swahili
Na wekeni mizani kwa haki, wala msipunje katika mizani.
|
Ayah 55:10 الأية
وَالْأَرْضَ وَضَعَهَا لِلْأَنَامِ
Swahili
Na ardhi ameiweka kwa ajili ya viumbe.
|
Ayah 55:11 الأية
فِيهَا فَاكِهَةٌ وَالنَّخْلُ ذَاتُ الْأَكْمَامِ
Swahili
Humo yamo matunda na mitende yenye mafumba.
|
Ayah 55:12 الأية
وَالْحَبُّ ذُو الْعَصْفِ وَالرَّيْحَانُ
Swahili
Na nafaka zenye makapi, na rehani.
|
Ayah 55:13 الأية
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Swahili
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
|
Ayah 55:14 الأية
خَلَقَ الْإِنسَانَ مِن صَلْصَالٍ كَالْفَخَّارِ
Swahili
Amemuumba mtu kwa udongo wa kinamo..
|
Ayah 55:15 الأية
وَخَلَقَ الْجَانَّ مِن مَّارِجٍ مِّن نَّارٍ
Swahili
Na akawaumba majini kwa ulimi wa moto.
|
Ayah 55:16 الأية
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Swahili
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
|
Ayah 55:17 الأية
رَبُّ الْمَشْرِقَيْنِ وَرَبُّ الْمَغْرِبَيْنِ
Swahili
Mola Mlezi wa mashariki mbili na wa magharibi mbili.
|
Ayah 55:18 الأية
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Swahili
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
|
Ayah 55:19 الأية
مَرَجَ الْبَحْرَيْنِ يَلْتَقِيَانِ
Swahili
Anaziendesha bahari mbili zikutane;
|
Ayah 55:20 الأية
بَيْنَهُمَا بَرْزَخٌ لَّا يَبْغِيَانِ
Swahili
Baina yao kipo kizuizi, zisiingiliane.
|
Ayah 55:21 الأية
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Swahili
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
|
Ayah 55:22 الأية
يَخْرُجُ مِنْهُمَا اللُّؤْلُؤُ وَالْمَرْجَانُ
Swahili
Katika hizo bahari mbili zinatoka lulu na marijani.
|
Ayah 55:23 الأية
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Swahili
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
|
Ayah 55:24 الأية
وَلَهُ الْجَوَارِ الْمُنشَآتُ فِي الْبَحْرِ كَالْأَعْلَامِ
Swahili
Na ni vyake Yeye hivi viendavyo baharini vilivyo undwa kama vilima.
|
Ayah 55:25 الأية
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Swahili
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
|
Ayah 55:26 الأية
كُلُّ مَنْ عَلَيْهَا فَانٍ
Swahili
Kila kilioko juu yake kitatoweka.
|
Ayah 55:27 الأية
وَيَبْقَىٰ وَجْهُ رَبِّكَ ذُو الْجَلَالِ وَالْإِكْرَامِ
Swahili
Na atabakia Mwenyewe Mola wako Mlezi Mwenye utukufu na ukarimu.
|
Ayah 55:28 الأية
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Swahili
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
|
Ayah 55:29 الأية
يَسْأَلُهُ مَن فِي السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ ۚ كُلَّ يَوْمٍ هُوَ فِي شَأْنٍ
Swahili
Vinamwomba Yeye vilivyomo katika mbingu na ardhi. Kila siku Yeye yumo katika
mambo.
|
Ayah 55:30 الأية
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Swahili
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
|
Ayah 55:31 الأية
سَنَفْرُغُ لَكُمْ أَيُّهَ الثَّقَلَانِ
Swahili
Tutakuhisabuni enyi makundi mawili.
|
Ayah 55:32 الأية
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Swahili
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
|
Ayah 55:33 الأية
يَا مَعْشَرَ الْجِنِّ وَالْإِنسِ إِنِ اسْتَطَعْتُمْ أَن تَنفُذُوا مِنْ أَقْطَارِ
السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ فَانفُذُوا ۚ لَا تَنفُذُونَ إِلَّا بِسُلْطَانٍ
Swahili
Enyi makundi ya majini na watu! Mkiweza kupenya kwenye mbingu na ardhi, basi
penyeni! Hamtapenya ila kwa kupewa madaraka.
|
Ayah 55:34 الأية
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Swahili
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
|
Ayah 55:35 الأية
يُرْسَلُ عَلَيْكُمَا شُوَاظٌ مِّن نَّارٍ وَنُحَاسٌ فَلَا تَنتَصِرَانِ
Swahili
Mtapelekewa muwako wa moto na shaba; wala hamtashinda.
|
Ayah 55:36 الأية
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Swahili
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
|
Ayah 55:37 الأية
فَإِذَا انشَقَّتِ السَّمَاءُ فَكَانَتْ وَرْدَةً كَالدِّهَانِ
Swahili
Itakapo pasuka mbingu ikawa nyekundu kama mafuta.
|
Ayah 55:38 الأية
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Swahili
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
|
Ayah 55:39 الأية
فَيَوْمَئِذٍ لَّا يُسْأَلُ عَن ذَنبِهِ إِنسٌ وَلَا جَانٌّ
Swahili
Siku hiyo hataulizwa dhambi zake mtu wala jini.
|
Ayah 55:40 الأية
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Swahili
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
|
Ayah 55:41 الأية
يُعْرَفُ الْمُجْرِمُونَ بِسِيمَاهُمْ فَيُؤْخَذُ بِالنَّوَاصِي وَالْأَقْدَامِ
Swahili
Watajuulikana wakosefu kwa alama zao, basi watashikwa kwa nywele zao za utosini
na kwa miguu.
|
Ayah 55:42 الأية
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Swahili
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
|
Ayah 55:43 الأية
هَٰذِهِ جَهَنَّمُ الَّتِي يُكَذِّبُ بِهَا الْمُجْرِمُونَ
Swahili
Hii ndiyo Jahannamu ambayo wakosefu wakiikanusha.
|
Ayah 55:44 الأية
يَطُوفُونَ بَيْنَهَا وَبَيْنَ حَمِيمٍ آنٍ
Swahili
Watakuwa wakizunguka baina ya hiyo na maji ya moto yanayo chemka.
|
Ayah 55:45 الأية
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Swahili
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
|
Ayah 55:46 الأية
وَلِمَنْ خَافَ مَقَامَ رَبِّهِ جَنَّتَانِ
Swahili
Na mwenye kuogopa kusimamishwa mbele ya Mola wake Mlezi atapata Bustani mbili.
|
Ayah 55:47 الأية
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Swahili
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
|
Ayah 55:48 الأية
ذَوَاتَا أَفْنَانٍ
Swahili
Bustani zenye matawi yaliyo tanda.
|
Ayah 55:49 الأية
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Swahili
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
|
Ayah 55:50 الأية
فِيهِمَا عَيْنَانِ تَجْرِيَانِ
Swahili
Ndani yake zimo chemchem mbili zinazo pita.
|
Ayah 55:51 الأية
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Swahili
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
|
Ayah 55:52 الأية
فِيهِمَا مِن كُلِّ فَاكِهَةٍ زَوْجَانِ
Swahili
Humo katika kila matunda zimo namna mbili.
|
Ayah 55:53 الأية
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Swahili
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
|
Ayah 55:54 الأية
مُتَّكِئِينَ عَلَىٰ فُرُشٍ بَطَائِنُهَا مِنْ إِسْتَبْرَقٍ ۚ وَجَنَى
الْجَنَّتَيْنِ دَانٍ
Swahili
Wawe wameegemea matandiko yenye bit'ana ya hariri nzito; na matunda ya Bustani
hizo yapo karibu.
|
Ayah 55:55 الأية
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Swahili
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
|
Ayah 55:56 الأية
فِيهِنَّ قَاصِرَاتُ الطَّرْفِ لَمْ يَطْمِثْهُنَّ إِنسٌ قَبْلَهُمْ وَلَا جَانٌّ
Swahili
Humo watakuwamo wanawake watulizao macho yao; hajawagusa mtu kabla yao wala
jini.
|
Ayah 55:57 الأية
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Swahili
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
|
Ayah 55:58 الأية
كَأَنَّهُنَّ الْيَاقُوتُ وَالْمَرْجَانُ
Swahili
Kama kwamba wao ni yakuti na marijani.
|
Ayah 55:59 الأية
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Swahili
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha.
|
Ayah 55:60 الأية
هَلْ جَزَاءُ الْإِحْسَانِ إِلَّا الْإِحْسَانُ
Swahili
Ati yaweza kuwa malipo ya ihsani ila ihsani?
|
Ayah 55:61 الأية
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Swahili
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
|
Ayah 55:62 الأية
وَمِن دُونِهِمَا جَنَّتَانِ
Swahili
Na zaidi ya hizo zipo Bustani nyengine mbili.
|
Ayah 55:63 الأية
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Swahili
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
|
Ayah 55:64 الأية
مُدْهَامَّتَانِ
Swahili
Za kijani kibivu.
|
Ayah 55:65 الأية
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Swahili
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
|
Ayah 55:66 الأية
فِيهِمَا عَيْنَانِ نَضَّاخَتَانِ
Swahili
Na chemchem mbili zinazo furika.
|
Ayah 55:67 الأية
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Swahili
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
|
Ayah 55:68 الأية
فِيهِمَا فَاكِهَةٌ وَنَخْلٌ وَرُمَّانٌ
Swahili
Imo humo miti ya matunda, na mitende na mikomamanga.
|
Ayah 55:69 الأية
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Swahili
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
|
Ayah 55:70 الأية
فِيهِنَّ خَيْرَاتٌ حِسَانٌ
Swahili
Humo wamo wanawake wema wazuri.
|
Ayah 55:71 الأية
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Swahili
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
|
Ayah 55:72 الأية
حُورٌ مَّقْصُورَاتٌ فِي الْخِيَامِ
Swahili
Wanawake wazuri wanao tawishwa katika makhema.
|
Ayah 55:73 الأية
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Swahili
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
|
Ayah 55:74 الأية
لَمْ يَطْمِثْهُنَّ إِنسٌ قَبْلَهُمْ وَلَا جَانٌّ
Swahili
Hajawagusa mtu wala jini kabla yao.
|
Ayah 55:75 الأية
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Swahili
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
|
Ayah 55:76 الأية
مُتَّكِئِينَ عَلَىٰ رَفْرَفٍ خُضْرٍ وَعَبْقَرِيٍّ حِسَانٍ
Swahili
Wameegemea juu ya matakia ya kijani na mazulia mazuri.
|
Ayah 55:77 الأية
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Swahili
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
|
Ayah 55:78 الأية
تَبَارَكَ اسْمُ رَبِّكَ ذِي الْجَلَالِ وَالْإِكْرَامِ
Swahili
Limetukuka jina la Mola wako Mlezi Mwenye utukufu na ukarimu.
|
©
EsinIslam.Com Designed & produced by The Awqaf London. Please pray for us
|