Prev  

15. Surah Al-Hijr سورة الحجر

  Next  



Ayah  15:1  الأية
    +/- -/+  
بِسْم ِ اللهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ
الر ۚ تِلْكَ آيَاتُ الْكِتَابِ وَقُرْآنٍ مُّبِينٍ
Swahili
 
Alif Lam Ra. (A.L.R). Hizi ni Aya za Kitabu na Qur'ani inayo bainisha.

Ayah  15:2  الأية
    +/- -/+  
رُّبَمَا يَوَدُّ الَّذِينَ كَفَرُوا لَوْ كَانُوا مُسْلِمِينَ
Swahili
 
HUENDA ikawa walio kufuru wakatamani wange kuwa Waislamu.

Ayah  15:3  الأية
    +/- -/+  
ذَرْهُمْ يَأْكُلُوا وَيَتَمَتَّعُوا وَيُلْهِهِمُ الْأَمَلُ ۖ فَسَوْفَ يَعْلَمُونَ
Swahili
 
Waache wale, na wastarehe, na iwazuge tamaa. Watakuja jua.

Ayah  15:4  الأية
    +/- -/+  
وَمَا أَهْلَكْنَا مِن قَرْيَةٍ إِلَّا وَلَهَا كِتَابٌ مَّعْلُومٌ
Swahili
 
Na hatukuuangamiza mji wowote ule ila ulikuwa na muda wake maalumu.

Ayah  15:5  الأية
    +/- -/+  
مَّا تَسْبِقُ مِنْ أُمَّةٍ أَجَلَهَا وَمَا يَسْتَأْخِرُونَ
Swahili
 
Hawawezi watu wowote kuitangulia ajali yao, wala kuchelewa.

Ayah  15:6  الأية
    +/- -/+  
وَقَالُوا يَا أَيُّهَا الَّذِي نُزِّلَ عَلَيْهِ الذِّكْرُ إِنَّكَ لَمَجْنُونٌ
Swahili
 
Na walisema: Ewe uliyeteremshiwa Ukumbusho! Hakika wewe ni mwendawazimu.

Ayah  15:7  الأية
    +/- -/+  
لَّوْ مَا تَأْتِينَا بِالْمَلَائِكَةِ إِن كُنتَ مِنَ الصَّادِقِينَ
Swahili
 
Mbona hutuletei Malaika ikiwa wewe ni miongoni mwa wasemao kweli?

Ayah  15:8  الأية
    +/- -/+  
مَا نُنَزِّلُ الْمَلَائِكَةَ إِلَّا بِالْحَقِّ وَمَا كَانُوا إِذًا مُّنظَرِينَ
Swahili
 
Sisi hatuwateremshi Malaika ila kwa sababu ya haki, na hapo hawatapewa muhula.

Ayah  15:9  الأية
    +/- -/+  
إِنَّا نَحْنُ نَزَّلْنَا الذِّكْرَ وَإِنَّا لَهُ لَحَافِظُونَ
Swahili
 
Hakika Sisi ndio tulio teremsha Ukumbusho huu, na hakika Sisi ndio tutao ulinda.

Ayah  15:10  الأية
    +/- -/+  
وَلَقَدْ أَرْسَلْنَا مِن قَبْلِكَ فِي شِيَعِ الْأَوَّلِينَ
Swahili
 
Na hakika tulikwisha watumia Mitume mataifa ya mwanzo.

Ayah  15:11  الأية
    +/- -/+  
وَمَا يَأْتِيهِم مِّن رَّسُولٍ إِلَّا كَانُوا بِهِ يَسْتَهْزِئُونَ
Swahili
 
Na hakuwafikia Mtume ila walimkejeli.

Ayah  15:12  الأية
    +/- -/+  
كَذَٰلِكَ نَسْلُكُهُ فِي قُلُوبِ الْمُجْرِمِينَ
Swahili
 
Na kama hivi ndivyo tunavyo ingiza katika nyoyo za wakosefu.

Ayah  15:13  الأية
    +/- -/+  
لَا يُؤْمِنُونَ بِهِ ۖ وَقَدْ خَلَتْ سُنَّةُ الْأَوَّلِينَ
Swahili
 
Hawayaamini haya, na hali ya kuwa umekwisha wapitia mfano wa watu wa kale.

Ayah  15:14  الأية
    +/- -/+  
وَلَوْ فَتَحْنَا عَلَيْهِم بَابًا مِّنَ السَّمَاءِ فَظَلُّوا فِيهِ يَعْرُجُونَ
Swahili
 
Na lau tungeli wafungulia mlango wa mbingu, wakawa wanapanda,

Ayah  15:15  الأية
    +/- -/+  
لَقَالُوا إِنَّمَا سُكِّرَتْ أَبْصَارُنَا بَلْ نَحْنُ قَوْمٌ مَّسْحُورُونَ
Swahili
 
Basi wangeli sema: Macho yetu yamelevywa, bali sisi wenyewe tumerogwa.

Ayah  15:16  الأية
    +/- -/+  
وَلَقَدْ جَعَلْنَا فِي السَّمَاءِ بُرُوجًا وَزَيَّنَّاهَا لِلنَّاظِرِينَ
Swahili
 
Na hakika tumeweka katika mbingu vituo vya sayari, na tumezipamba kwa wenye kuangalia.

Ayah  15:17  الأية
    +/- -/+  
وَحَفِظْنَاهَا مِن كُلِّ شَيْطَانٍ رَّجِيمٍ
Swahili
 
Na tumezilinda na kila shetani afukuzwaye.

Ayah  15:18  الأية
    +/- -/+  
إِلَّا مَنِ اسْتَرَقَ السَّمْعَ فَأَتْبَعَهُ شِهَابٌ مُّبِينٌ
Swahili
 
Isipo kuwa mwenye kusikiliza kwa kuibia, naye hufuatwa na kijinga cha moto kinacho onekana.

Ayah  15:19  الأية
    +/- -/+  
وَالْأَرْضَ مَدَدْنَاهَا وَأَلْقَيْنَا فِيهَا رَوَاسِيَ وَأَنبَتْنَا فِيهَا مِن كُلِّ شَيْءٍ مَّوْزُونٍ
Swahili
 
Na ardhi tumeitandaza na humo tumeweka milima, na tumeotesha kila kitu kwa kiasi chake.

Ayah  15:20  الأية
    +/- -/+  
وَجَعَلْنَا لَكُمْ فِيهَا مَعَايِشَ وَمَن لَّسْتُمْ لَهُ بِرَازِقِينَ
Swahili
 
Na tumekujaalieni humo vitu vya maisha yenu, na ya hao ambao nyinyi sio wenye kuwaruzuku.

Ayah  15:21  الأية
    +/- -/+  
وَإِن مِّن شَيْءٍ إِلَّا عِندَنَا خَزَائِنُهُ وَمَا نُنَزِّلُهُ إِلَّا بِقَدَرٍ مَّعْلُومٍ
Swahili
 
Na hakuna chochote ila asili yake inatokana na Sisi; wala hatukiteremshi ila kwa kipimo maalumu.

Ayah  15:22  الأية
    +/- -/+  
وَأَرْسَلْنَا الرِّيَاحَ لَوَاقِحَ فَأَنزَلْنَا مِنَ السَّمَاءِ مَاءً فَأَسْقَيْنَاكُمُوهُ وَمَا أَنتُمْ لَهُ بِخَازِنِينَ
Swahili
 
Na tunazipeleka pepo za kupandishia, na tunateremsha kutoka mbinguni maji, kisha tukakunywesheni maji hayo. Wala si nyinyi mnayo yaweka.

Ayah  15:23  الأية
    +/- -/+  
وَإِنَّا لَنَحْنُ نُحْيِي وَنُمِيتُ وَنَحْنُ الْوَارِثُونَ
Swahili
 
Na Sisi ndio tunao huisha na tunao fisha. Na Sisi ndio Warithi.

Ayah  15:24  الأية
    +/- -/+  
وَلَقَدْ عَلِمْنَا الْمُسْتَقْدِمِينَ مِنكُمْ وَلَقَدْ عَلِمْنَا الْمُسْتَأْخِرِينَ
Swahili
 
Na tunawajua walio tangulia katika nyinyi, na tunawajua walio taakhari.

Ayah  15:25  الأية
    +/- -/+  
وَإِنَّ رَبَّكَ هُوَ يَحْشُرُهُمْ ۚ إِنَّهُ حَكِيمٌ عَلِيمٌ
Swahili
 
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye atakaye wakusanya. Hakika Yeye ni Mwenye hikima na Mjuzi.

Ayah  15:26  الأية
    +/- -/+  
وَلَقَدْ خَلَقْنَا الْإِنسَانَ مِن صَلْصَالٍ مِّنْ حَمَإٍ مَّسْنُونٍ
Swahili
 
Na tulimuumba mtu kwa udongo unao toa sauti, unao tokana na matope yaliyo tiwa sura.

Ayah  15:27  الأية
    +/- -/+  
وَالْجَانَّ خَلَقْنَاهُ مِن قَبْلُ مِن نَّارِ السَّمُومِ
Swahili
 
Na majini tuliwaumba kabla kwa moto wa upepo umoto.

Ayah  15:28  الأية
    +/- -/+  
وَإِذْ قَالَ رَبُّكَ لِلْمَلَائِكَةِ إِنِّي خَالِقٌ بَشَرًا مِّن صَلْصَالٍ مِّنْ حَمَإٍ مَّسْنُونٍ
Swahili
 
Na Mola wako Mlezi alipo waambia Malaika: Hakika Mimi nitamuumba mtu kwa udongo unao toa sauti, unao tokana na matope yaliyo tiwa sura.

Ayah  15:29  الأية
    +/- -/+  
فَإِذَا سَوَّيْتُهُ وَنَفَخْتُ فِيهِ مِن رُّوحِي فَقَعُوا لَهُ سَاجِدِينَ
Swahili
 
Basi nitakapo mkamilisha na nikampulizia roho yangu, basi mumwangukie kumsujudia.

Ayah  15:30  الأية
    +/- -/+  
فَسَجَدَ الْمَلَائِكَةُ كُلُّهُمْ أَجْمَعُونَ
Swahili
 
Basi Malaika wote pamoja walimsujudia,

Ayah  15:31  الأية
    +/- -/+  
إِلَّا إِبْلِيسَ أَبَىٰ أَن يَكُونَ مَعَ السَّاجِدِينَ
Swahili
 
Isipo kuwa Iblisi. Yeye alikataa kuwa pamoja na walio sujudu.

Ayah  15:32  الأية
    +/- -/+  
قَالَ يَا إِبْلِيسُ مَا لَكَ أَلَّا تَكُونَ مَعَ السَّاجِدِينَ
Swahili
 
(Mwenyezi Mungu) akasema: Ewe Iblisi! Una nini hata hukuwa pamoja na walio sujudu?

Ayah  15:33  الأية
    +/- -/+  
قَالَ لَمْ أَكُن لِّأَسْجُدَ لِبَشَرٍ خَلَقْتَهُ مِن صَلْصَالٍ مِّنْ حَمَإٍ مَّسْنُونٍ
Swahili
 
Akasema: Haiwi mimi nimsujudie mtu uliye muumba kwa udongo unao toa sauti, unao tokana na matope yenye sura.

Ayah  15:34  الأية
    +/- -/+  
قَالَ فَاخْرُجْ مِنْهَا فَإِنَّكَ رَجِيمٌ
Swahili
 
(Mwenyezi Mungu) akasema: Basi toka humo, kwani hakika wewe ni maluuni!

Ayah  15:35  الأية
    +/- -/+  
وَإِنَّ عَلَيْكَ اللَّعْنَةَ إِلَىٰ يَوْمِ الدِّينِ
Swahili
 
Na hakika juu yako ipo laana mpaka Siku ya Malipo.

Ayah  15:36  الأية
    +/- -/+  
قَالَ رَبِّ فَأَنظِرْنِي إِلَىٰ يَوْمِ يُبْعَثُونَ
Swahili
 
Akasema (Iblisi): Mola wangu Mlezi! Nipe muhula mpaka siku watapo fufuliwa.

Ayah  15:37  الأية
    +/- -/+  
قَالَ فَإِنَّكَ مِنَ الْمُنظَرِينَ
Swahili
 
(Mwenyezi Mungu) akasema: Hakika wewe ni katika walio pewa muhula

Ayah  15:38  الأية
    +/- -/+  

Ayah  15:39  الأية
    +/- -/+  
قَالَ رَبِّ بِمَا أَغْوَيْتَنِي لَأُزَيِّنَنَّ لَهُمْ فِي الْأَرْضِ وَلَأُغْوِيَنَّهُمْ أَجْمَعِينَ
Swahili
 
Akasema: Mola wangu Mlezi! Ilivyo kuwa umenitia makosani, basi nahakikisha nitawazaini hapa duniani na nitawapoteza wote,

Ayah  15:40  الأية
    +/- -/+  

Ayah  15:41  الأية
    +/- -/+  
قَالَ هَٰذَا صِرَاطٌ عَلَيَّ مُسْتَقِيمٌ
Swahili
 
Akasema: Hii Njia ya kujia kwangu Iliyo Nyooka.

Ayah  15:42  الأية
    +/- -/+  
إِنَّ عِبَادِي لَيْسَ لَكَ عَلَيْهِمْ سُلْطَانٌ إِلَّا مَنِ اتَّبَعَكَ مِنَ الْغَاوِينَ
Swahili
 
Hakika waja wangu, wewe hutakuwa na mamlaka juu yao, isipo kuwa wale wapotofu walio kufuata.

Ayah  15:43  الأية
    +/- -/+  
وَإِنَّ جَهَنَّمَ لَمَوْعِدُهُمْ أَجْمَعِينَ
Swahili
 
Na bila shaka Jahannamu ndipo pahali pao walipo ahidiwa wote.

Ayah  15:44  الأية
    +/- -/+  
لَهَا سَبْعَةُ أَبْوَابٍ لِّكُلِّ بَابٍ مِّنْهُمْ جُزْءٌ مَّقْسُومٌ
Swahili
 
Ina milango saba; na kwa kila mlango iko sehemu walio tengewa.

Ayah  15:45  الأية
    +/- -/+  
إِنَّ الْمُتَّقِينَ فِي جَنَّاتٍ وَعُيُونٍ
Swahili
 
Hakika wachamngu watakuwa katika Mabustani na chemchem.

Ayah  15:46  الأية
    +/- -/+  

Ayah  15:47  الأية
    +/- -/+  
وَنَزَعْنَا مَا فِي صُدُورِهِم مِّنْ غِلٍّ إِخْوَانًا عَلَىٰ سُرُرٍ مُّتَقَابِلِينَ
Swahili
 
Na tutaondoa chuki iliyo kuwamo vifuani mwao, wawe ndugu juu ya viti vya enzi wameelekeana.

Ayah  15:48  الأية
    +/- -/+  
لَا يَمَسُّهُمْ فِيهَا نَصَبٌ وَمَا هُم مِّنْهَا بِمُخْرَجِينَ
Swahili
 
Humo hayatawagusa machofu, wala hawatatolewa humo.

Ayah  15:49  الأية
    +/- -/+  
نَبِّئْ عِبَادِي أَنِّي أَنَا الْغَفُورُ الرَّحِيمُ
Swahili
 
Waambie waja wangu ya kwamba Mimi ndiye Mwenye kusamehe, Mwenye kurehemu.

Ayah  15:50  الأية
    +/- -/+  
وَأَنَّ عَذَابِي هُوَ الْعَذَابُ الْأَلِيمُ
Swahili
 
Na kwamba adhabu yangu ndio adhabu iliyo chungu!

Ayah  15:51  الأية
    +/- -/+  
وَنَبِّئْهُمْ عَن ضَيْفِ إِبْرَاهِيمَ
Swahili
 
Na uwape khabari za wageni wa Ibrahim.

Ayah  15:52  الأية
    +/- -/+  
إِذْ دَخَلُوا عَلَيْهِ فَقَالُوا سَلَامًا قَالَ إِنَّا مِنكُمْ وَجِلُونَ
Swahili
 
Walipo ingia kwake na wakasema: Salama! Yeye akasema: Hakika sisi tunakuogopeni.

Ayah  15:53  الأية
    +/- -/+  
قَالُوا لَا تَوْجَلْ إِنَّا نُبَشِّرُكَ بِغُلَامٍ عَلِيمٍ
Swahili
 
Wakasema: Usiogope. Sisi tunakubashiria kijana mwenye ujuzi.

Ayah  15:54  الأية
    +/- -/+  
قَالَ أَبَشَّرْتُمُونِي عَلَىٰ أَن مَّسَّنِيَ الْكِبَرُ فَبِمَ تُبَشِّرُونَ
Swahili
 
Akasema: Mnanibashiria nami uzee umenishika! Basi kwa njia gani mnanibashiria?

Ayah  15:55  الأية
    +/- -/+  
قَالُوا بَشَّرْنَاكَ بِالْحَقِّ فَلَا تَكُن مِّنَ الْقَانِطِينَ
Swahili
 
Wakasema: Tunakubashiria kwa haki; basi usiwe miongoni mwa wanao kata tamaa.

Ayah  15:56  الأية
    +/- -/+  
قَالَ وَمَن يَقْنَطُ مِن رَّحْمَةِ رَبِّهِ إِلَّا الضَّالُّونَ
Swahili
 
Akasema: Na nani anaye kata tamaa na rehema ya Mola wake Mlezi ila wale walio potea?

Ayah  15:57  الأية
    +/- -/+  
قَالَ فَمَا خَطْبُكُمْ أَيُّهَا الْمُرْسَلُونَ
Swahili
 
Akasema: Hebu nini amri yenu, enyi wajumbe?

Ayah  15:58  الأية
    +/- -/+  
قَالُوا إِنَّا أُرْسِلْنَا إِلَىٰ قَوْمٍ مُّجْرِمِينَ
Swahili
 
Wakasema: Hakika sisi tumetumwa kwa kaumu ya wakosefu!

Ayah  15:59  الأية
    +/- -/+  
إِلَّا آلَ لُوطٍ إِنَّا لَمُنَجُّوهُمْ أَجْمَعِينَ
Swahili
 
Isipo kuwa walio mfuata Luut'i. Bila ya shaka sisi tutawaokoa hao wote.

Ayah  15:60  الأية
    +/- -/+  
إِلَّا امْرَأَتَهُ قَدَّرْنَا ۙ إِنَّهَا لَمِنَ الْغَابِرِينَ
Swahili
 
Ila mkewe. Tunakadiria huyo atakuwa miongoni watao bakia nyuma.

Ayah  15:61  الأية
    +/- -/+  
فَلَمَّا جَاءَ آلَ لُوطٍ الْمُرْسَلُونَ
Swahili
 
Basi wale wajumbe walipo fika kwa Luut'i,

Ayah  15:62  الأية
    +/- -/+  
قَالَ إِنَّكُمْ قَوْمٌ مُّنكَرُونَ
Swahili
 
Alisema (Luut'i): Hakika nyinyi ni watu msio juulikana.

Ayah  15:63  الأية
    +/- -/+  
قَالُوا بَلْ جِئْنَاكَ بِمَا كَانُوا فِيهِ يَمْتَرُونَ
Swahili
 
Wakasema: Bali sisi tumekuletea yale waliyo kuwa wakiyafanyia shaka.

Ayah  15:64  الأية
    +/- -/+  
وَأَتَيْنَاكَ بِالْحَقِّ وَإِنَّا لَصَادِقُونَ
Swahili
 
Na tumefika kwako kwa Haki, na hakika sisi tunasema kweli.

Ayah  15:65  الأية
    +/- -/+  
فَأَسْرِ بِأَهْلِكَ بِقِطْعٍ مِّنَ اللَّيْلِ وَاتَّبِعْ أَدْبَارَهُمْ وَلَا يَلْتَفِتْ مِنكُمْ أَحَدٌ وَامْضُوا حَيْثُ تُؤْمَرُونَ
Swahili
 
Basi ondoka na ahli zako usiku ungalipo, nawe ufuate nyuma yao, wala yeyote kati yenu asigeuke nyuma. Na mwende mnapo amrishwa.

Ayah  15:66  الأية
    +/- -/+  
وَقَضَيْنَا إِلَيْهِ ذَٰلِكَ الْأَمْرَ أَنَّ دَابِرَ هَٰؤُلَاءِ مَقْطُوعٌ مُّصْبِحِينَ
Swahili
 
Na tukamfunulia hukumu hiyo, ya kwamba hata wa mwisho wao hao ikifika asubuhi atakuwa kesha katiliwa mbali.

Ayah  15:67  الأية
    +/- -/+  
وَجَاءَ أَهْلُ الْمَدِينَةِ يَسْتَبْشِرُونَ
Swahili
 
Na wakaja watu wa mji ule nao furahani.

Ayah  15:68  الأية
    +/- -/+  
قَالَ إِنَّ هَٰؤُلَاءِ ضَيْفِي فَلَا تَفْضَحُونِ
Swahili
 
Akasema: Hakika hawa wageni wangu, basi msinifedheheshe.

Ayah  15:69  الأية
    +/- -/+  

Ayah  15:70  الأية
    +/- -/+  
قَالُوا أَوَلَمْ نَنْهَكَ عَنِ الْعَالَمِينَ
Swahili
 
Wakasema: Sisi hatukukukataza usimkaribishe yeyote?

Ayah  15:71  الأية
    +/- -/+  
قَالَ هَٰؤُلَاءِ بَنَاتِي إِن كُنتُمْ فَاعِلِينَ
Swahili
 
Akasema: Hawa binti zangu, ikiwa nyinyi ni watendaji.

Ayah  15:72  الأية
    +/- -/+  
لَعَمْرُكَ إِنَّهُمْ لَفِي سَكْرَتِهِمْ يَعْمَهُونَ
Swahili
 
Naapa kwa umri wako! Hakika hao walikuwa katika ulevi wao, wakihangaika ovyo.

Ayah  15:73  الأية
    +/- -/+  
فَأَخَذَتْهُمُ الصَّيْحَةُ مُشْرِقِينَ
Swahili
 
Ukelele ukawatwaa wakipambaukiwa.

Ayah  15:74  الأية
    +/- -/+  
فَجَعَلْنَا عَالِيَهَا سَافِلَهَا وَأَمْطَرْنَا عَلَيْهِمْ حِجَارَةً مِّن سِجِّيلٍ
Swahili
 
Na tukaigeuza nchi juu chini, na tukawanyeshea mvua ya mawe ya udongo wa Motoni.

Ayah  15:75  الأية
    +/- -/+  
إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَاتٍ لِّلْمُتَوَسِّمِينَ
Swahili
 
Hakika katika hayo zipo ishara kwa waaguzi.

Ayah  15:76  الأية
    +/- -/+  

Ayah  15:77  الأية
    +/- -/+  
إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَةً لِّلْمُؤْمِنِينَ
Swahili
 
Hakika katika hayo ipo ishara kwa Waumini.

Ayah  15:78  الأية
    +/- -/+  
وَإِن كَانَ أَصْحَابُ الْأَيْكَةِ لَظَالِمِينَ
Swahili
 
Na hakika watu wa Kichakani walikuwa wenye kudhulumu.

Ayah  15:79  الأية
    +/- -/+  
فَانتَقَمْنَا مِنْهُمْ وَإِنَّهُمَا لَبِإِمَامٍ مُّبِينٍ
Swahili
 
Kwa hivyo tukawaadhibu. Na nchi mbili hizi ziko kwenye njia ilio wazi.

Ayah  15:80  الأية
    +/- -/+  
وَلَقَدْ كَذَّبَ أَصْحَابُ الْحِجْرِ الْمُرْسَلِينَ
Swahili
 
Na bila ya shaka wakaazi wa Hijr waliwakanusha Mitume.

Ayah  15:81  الأية
    +/- -/+  
وَآتَيْنَاهُمْ آيَاتِنَا فَكَانُوا عَنْهَا مُعْرِضِينَ
Swahili
 
Na tuliwapa ishara zetu, nao wakazipuuza.

Ayah  15:82  الأية
    +/- -/+  
وَكَانُوا يَنْحِتُونَ مِنَ الْجِبَالِ بُيُوتًا آمِنِينَ
Swahili
 
Nao walikuwa wakichonga majumba katika milima kwa amani.

Ayah  15:83  الأية
    +/- -/+  
فَأَخَذَتْهُمُ الصَّيْحَةُ مُصْبِحِينَ
Swahili
 
Basi ukelele ukawatwaa asubuhi.

Ayah  15:84  الأية
    +/- -/+  
فَمَا أَغْنَىٰ عَنْهُم مَّا كَانُوا يَكْسِبُونَ
Swahili
 
Hayakuwafaa waliyo kuwa wakiyachuma.

Ayah  15:85  الأية
    +/- -/+  
وَمَا خَلَقْنَا السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضَ وَمَا بَيْنَهُمَا إِلَّا بِالْحَقِّ ۗ وَإِنَّ السَّاعَةَ لَآتِيَةٌ ۖ فَاصْفَحِ الصَّفْحَ الْجَمِيلَ
Swahili
 
Na hatukuziumba mbingu na ardhi na vilivyomo ndani yake ila kwa ajili ya Haki. Na hakika Kiyama kitafika. Basi samehe msamaha mzuri.

Ayah  15:86  الأية
    +/- -/+  
إِنَّ رَبَّكَ هُوَ الْخَلَّاقُ الْعَلِيمُ
Swahili
 
Hakika Mola wako Mlezi ndiye Muumbaji Mjuzi.

Ayah  15:87  الأية
    +/- -/+  
وَلَقَدْ آتَيْنَاكَ سَبْعًا مِّنَ الْمَثَانِي وَالْقُرْآنَ الْعَظِيمَ
Swahili
 
Na tumekupa Aya saba zinazo somwa mara kwa mara, na Qur'ani Tukufu.

Ayah  15:88  الأية
    +/- -/+  
لَا تَمُدَّنَّ عَيْنَيْكَ إِلَىٰ مَا مَتَّعْنَا بِهِ أَزْوَاجًا مِّنْهُمْ وَلَا تَحْزَنْ عَلَيْهِمْ وَاخْفِضْ جَنَاحَكَ لِلْمُؤْمِنِينَ
Swahili
 
Usivitumbulie macho yako vitu tulivyo waneemesha makundi fulani kati yao, wala usiwahuzunikie. Na wainamishie bawa lako (la huruma) Waumini.

Ayah  15:89  الأية
    +/- -/+  
وَقُلْ إِنِّي أَنَا النَّذِيرُ الْمُبِينُ
Swahili
 
Na sema: Hakika mimi ni mwonyaji mwenye kubainisha.

Ayah  15:90  الأية
    +/- -/+  
كَمَا أَنزَلْنَا عَلَى الْمُقْتَسِمِينَ
Swahili
 
Kama hivyo tuliwateremshia walio gawa,

Ayah  15:91  الأية
    +/- -/+  
الَّذِينَ جَعَلُوا الْقُرْآنَ عِضِينَ
Swahili
 
Ambao wakaifanya Qur'ani vipande vipande.

Ayah  15:92  الأية
    +/- -/+  
فَوَرَبِّكَ لَنَسْأَلَنَّهُمْ أَجْمَعِينَ
Swahili
 
Basi Naapa kwa Mola wako Mlezi! Tutawahoji wote,

Ayah  15:93  الأية
    +/- -/+  

Ayah  15:94  الأية
    +/- -/+  
فَاصْدَعْ بِمَا تُؤْمَرُ وَأَعْرِضْ عَنِ الْمُشْرِكِينَ
Swahili
 
Basi wewe yatangaze uliyo amrishwa, na jitenge na washirikina.

Ayah  15:95  الأية
    +/- -/+  
إِنَّا كَفَيْنَاكَ الْمُسْتَهْزِئِينَ
Swahili
 
Hakika Sisi tunatosha kukukinga na wanao kejeli.

Ayah  15:96  الأية
    +/- -/+  
الَّذِينَ يَجْعَلُونَ مَعَ اللهِ إِلَٰهًا آخَرَ ۚ فَسَوْفَ يَعْلَمُونَ
Swahili
 
Hao wanao fanya kuwa pamoja na Mwenyezi Mungu yupo mungu mwingine. Basi, watakuja jua!

Ayah  15:97  الأية
    +/- -/+  
وَلَقَدْ نَعْلَمُ أَنَّكَ يَضِيقُ صَدْرُكَ بِمَا يَقُولُونَ
Swahili
 
Na Sisi tunajua kwa hakika kuwa wewe kifua chako kinaona dhiki kwa hayo wayasemayo.

Ayah  15:98  الأية
    +/- -/+  
فَسَبِّحْ بِحَمْدِ رَبِّكَ وَكُن مِّنَ السَّاجِدِينَ
Swahili
 
Basi mtakase Mola wako Mlezi kwa kumhimidi, na uwe miongoni wanao msujudia.

Ayah  15:99  الأية
    +/- -/+  
وَاعْبُدْ رَبَّكَ حَتَّىٰ يَأْتِيَكَ الْيَقِينُ
Swahili
 
Na muabudu Mola wako Mlezi mpaka ikufikie Yakini.
 


© EsinIslam.Com Designed & produced by The Awqaf London. Please pray for us