First Ayah 1 الأية الأوليبِسْم ِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ
إِنَّا فَتَحْنَا لَكَ فَتْحًا مُّبِينًا
Swahili
Hakika tumekufungulia Ushindi wa dhaahiri
|
Ayah 48:2 الأية
لِّيَغْفِرَ لَكَ اللَّهُ مَا تَقَدَّمَ مِن ذَنبِكَ وَمَا تَأَخَّرَ وَيُتِمَّ
نِعْمَتَهُ عَلَيْكَ وَيَهْدِيَكَ صِرَاطًا مُّسْتَقِيمًا
Swahili
Ili Mwenyezi Mungu akusamehe makosa yako yaliyo tangulia na yajayo, na
akutimizie neema zake, na akuongoe katika Njia Iliyo Nyooka,
|
Ayah 48:3 الأية
وَيَنصُرَكَ اللَّهُ نَصْرًا عَزِيزًا
Swahili
Na Mwenyezi Mungu akunusuru nusura yenye nguvu -
|
Ayah 48:4 الأية
هُوَ الَّذِي أَنزَلَ السَّكِينَةَ فِي قُلُوبِ الْمُؤْمِنِينَ لِيَزْدَادُوا
إِيمَانًا مَّعَ إِيمَانِهِمْ ۗ وَلِلَّهِ جُنُودُ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ ۚ
وَكَانَ اللَّهُ عَلِيمًا حَكِيمًا
Swahili
Yeye ndiye aliye teremsha utulivu katika nyoyo za Waumini ili wazidi Imani juu
ya Imani yao. Na Mwenyezi Mungu ndiye mwenye majeshi ya mbingu na ardhi. Na
Mwenyezi Mungu ni Mwenye ujuzi, Mwenye hikima -
|
Ayah 48:5 الأية
لِّيُدْخِلَ الْمُؤْمِنِينَ وَالْمُؤْمِنَاتِ جَنَّاتٍ تَجْرِي مِن تَحْتِهَا
الْأَنْهَارُ خَالِدِينَ فِيهَا وَيُكَفِّرَ عَنْهُمْ سَيِّئَاتِهِمْ ۚ وَكَانَ
ذَٰلِكَ عِندَ اللَّهِ فَوْزًا عَظِيمًا
Swahili
Ili awaingize Waumini wanaume na Waumini wanawake katika Bustani zipitazo mito
kati yake, wadumu humo, na awafutie makosa yao. Na huko ndiko kufuzu kukubwa
mbele ya Mwenyezi Mungu.
|
Ayah 48:6 الأية
وَيُعَذِّبَ الْمُنَافِقِينَ وَالْمُنَافِقَاتِ وَالْمُشْرِكِينَ وَالْمُشْرِكَاتِ
الظَّانِّينَ بِاللَّهِ ظَنَّ السَّوْءِ ۚ عَلَيْهِمْ دَائِرَةُ السَّوْءِ ۖ
وَغَضِبَ اللَّهُ عَلَيْهِمْ وَلَعَنَهُمْ وَأَعَدَّ لَهُمْ جَهَنَّمَ ۖ وَسَاءَتْ
مَصِيرًا
Swahili
Na awape adhabu wanaafiki wanaume na wanaafiki wanawake, na washirikina wanaume
na washirikina wanawake, wanao mdhania Mwenyezi Mungu dhana mbaya. Utawafikia
mgeuko mbaya, na Mwenyezi Mungu awakasirikie, na awalaani, na awaandalie
Jahannamu. Na hayo ni marudio maovu kabisa.
|
Ayah 48:7 الأية
وَلِلَّهِ جُنُودُ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ ۚ وَكَانَ اللَّهُ عَزِيزًا حَكِيمًا
Swahili
Na Mwenyezi Mungu ana majeshi ya mbingu na ardhi. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye
nguvu, Mwenye hikima.
|
Ayah 48:8 الأية
إِنَّا أَرْسَلْنَاكَ شَاهِدًا وَمُبَشِّرًا وَنَذِيرًا
Swahili
Hakika tumekutuma wewe uwe Shahidi, na Mbashiri, na Mwonyaji,
|
Ayah 48:9 الأية
لِّتُؤْمِنُوا بِاللَّهِ وَرَسُولِهِ وَتُعَزِّرُوهُ وَتُوَقِّرُوهُ وَتُسَبِّحُوهُ
بُكْرَةً وَأَصِيلًا
Swahili
Ili mumuamini Mwenyezi Mungu na Mtume wake, na mumsaidie, na mumhishimu, na
mumtakase asubuhi na jioni.
|
Ayah 48:10 الأية
إِنَّ الَّذِينَ يُبَايِعُونَكَ إِنَّمَا يُبَايِعُونَ اللَّهَ يَدُ اللَّهِ فَوْقَ
أَيْدِيهِمْ ۚ فَمَن نَّكَثَ فَإِنَّمَا يَنكُثُ عَلَىٰ نَفْسِهِ ۖ وَمَنْ أَوْفَىٰ
بِمَا عَاهَدَ عَلَيْهُ اللَّهَ فَسَيُؤْتِيهِ أَجْرًا عَظِيمًا
Swahili
Bila ya shaka wanao fungamana nawe, kwa hakika wanafungamana na Mwenyezi Mungu.
Mkono wa Mwenyezi Mungu uko juu ya mikono yao. Basi avunjaye ahadi hizi anavunja
kwa kuidhuru nafsi yake; na anaye tekeleza aliyo muahadi Mwenyezi Mungu,
Mwenyezi Mungu atamlipa ujira mkubwa.
|
Ayah 48:11 الأية
سَيَقُولُ لَكَ الْمُخَلَّفُونَ مِنَ الْأَعْرَابِ شَغَلَتْنَا أَمْوَالُنَا
وَأَهْلُونَا فَاسْتَغْفِرْ لَنَا ۚ يَقُولُونَ بِأَلْسِنَتِهِم مَّا لَيْسَ فِي
قُلُوبِهِمْ ۚ قُلْ فَمَن يَمْلِكُ لَكُم مِّنَ اللَّهِ شَيْئًا إِنْ أَرَادَ
بِكُمْ ضَرًّا أَوْ أَرَادَ بِكُمْ نَفْعًا ۚ بَلْ كَانَ اللَّهُ بِمَا تَعْمَلُونَ
خَبِيرًا
Swahili
Watakuambia mabedui walio baki nyuma: Yametushughulisha mali yetu na ahali zetu,
basi tuombee msamaha. Wanasema kwa ndimi zao yasiyo kuwamo katika nyoyo zao.
Sema: Ni nani awezaye kukusaidieni chochote kwa Mwenyezi Mungu akitaka Yeye
kukudhuruni au akitaka kukunufaisheni? Bali Mwenyezi Mungu anazo khabari za
mnayo yatenda.
|
Ayah 48:12 الأية
بَلْ ظَنَنتُمْ أَن لَّن يَنقَلِبَ الرَّسُولُ وَالْمُؤْمِنُونَ إِلَىٰ أَهْلِيهِمْ
أَبَدًا وَزُيِّنَ ذَٰلِكَ فِي قُلُوبِكُمْ وَظَنَنتُمْ ظَنَّ السَّوْءِ وَكُنتُمْ
قَوْمًا بُورًا
Swahili
Lakini mlidhani kwamba Mtume na Waumini hawatarudi kabisa kwa ahali zao, na
mkapambiwa hayo katika nyoyo zenu, na mkadhania dhana mbaya, na mkawa watu wanao
angamia.
|
Ayah 48:13 الأية
وَمَن لَّمْ يُؤْمِن بِاللَّهِ وَرَسُولِهِ فَإِنَّا أَعْتَدْنَا لِلْكَافِرِينَ
سَعِيرًا
Swahili
Na asiye muamini Mwenyezi Mungu na Mtume wake, basi kwa hakika Sisi
tumewaandalia makafiri Moto mkali.
|
Ayah 48:14 الأية
وَلِلَّهِ مُلْكُ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ ۚ يَغْفِرُ لِمَن يَشَاءُ وَيُعَذِّبُ
مَن يَشَاءُ ۚ وَكَانَ اللَّهُ غَفُورًا رَّحِيمًا
Swahili
Na Mwenyezi Mungu ndiye mwenye ufalme wa mbingu na ardhi. Humsamehe amtakaye, na
humuadhibu amtakaye. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusamehe, Mwenye kurehemu.
|
Ayah 48:15 الأية
سَيَقُولُ الْمُخَلَّفُونَ إِذَا انطَلَقْتُمْ إِلَىٰ مَغَانِمَ لِتَأْخُذُوهَا
ذَرُونَا نَتَّبِعْكُمْ ۖ يُرِيدُونَ أَن يُبَدِّلُوا كَلَامَ اللَّهِ ۚ قُل لَّن
تَتَّبِعُونَا كَذَٰلِكُمْ قَالَ اللَّهُ مِن قَبْلُ ۖ فَسَيَقُولُونَ بَلْ
تَحْسُدُونَنَا ۚ بَلْ كَانُوا لَا يَفْقَهُونَ إِلَّا قَلِيلًا
Swahili
Walio baki nyuma watasema: Mtapo kwenda kuchukua ngawira, tuacheni tukufuateni!
Wanataka kuyabadili maneno ya Mwenyezi Mungu. Sema: Hamtatufuata kabisa.
Mwenyezi Mungu alikwisha sema kama hivi zamani. Hapo watasema: Bali nyinyi
mnatuhusudu. Siyo, bali walikuwa hawafahamu ila kidogo.
|
Ayah 48:16 الأية
قُل لِّلْمُخَلَّفِينَ مِنَ الْأَعْرَابِ سَتُدْعَوْنَ إِلَىٰ قَوْمٍ أُولِي بَأْسٍ
شَدِيدٍ تُقَاتِلُونَهُمْ أَوْ يُسْلِمُونَ ۖ فَإِن تُطِيعُوا يُؤْتِكُمُ اللَّهُ
أَجْرًا حَسَنًا ۖ وَإِن تَتَوَلَّوْا كَمَا تَوَلَّيْتُم مِّن قَبْلُ
يُعَذِّبْكُمْ عَذَابًا أَلِيمًا
Swahili
Waambie walio achwa nyuma katika mabedui: Mtakuja itwa kwenda pigana na watu
wakali kwa vita, mpigane nao au wasalimu amri. Basi mkimt'ii, Mwenyezi Mungu
atakupeni ujira mzuri. Na mkigeuka kama mlivyo geuka kwanza, atakuadhibuni kwa
adhabu iliyo chungu.
|
Ayah 48:17 الأية
لَّيْسَ عَلَى الْأَعْمَىٰ حَرَجٌ وَلَا عَلَى الْأَعْرَجِ حَرَجٌ وَلَا عَلَى
الْمَرِيضِ حَرَجٌ ۗ وَمَن يُطِعِ اللَّهَ وَرَسُولَهُ يُدْخِلْهُ جَنَّاتٍ تَجْرِي
مِن تَحْتِهَا الْأَنْهَارُ ۖ وَمَن يَتَوَلَّ يُعَذِّبْهُ عَذَابًا أَلِيمًا
Swahili
Kipofu hana lawama, wala kiguru hana lawama, wala mgonjwa hana lawama. Na mwenye
kumt'ii Mwenyezi Mungu na Mtume wake, atamuingiza katika Mabustani yapitayo mito
kati yake. Na atakaye geuka upande atamuadhibu kwa adhabu chungu.
|
Ayah 48:18 الأية
لَّقَدْ رَضِيَ اللَّهُ عَنِ الْمُؤْمِنِينَ إِذْ يُبَايِعُونَكَ تَحْتَ
الشَّجَرَةِ فَعَلِمَ مَا فِي قُلُوبِهِمْ فَأَنزَلَ السَّكِينَةَ عَلَيْهِمْ
وَأَثَابَهُمْ فَتْحًا قَرِيبًا
Swahili
Kwa hakika Mwenyezi Mungu amewapa radhi Waumini walipo fungamana nawe chini ya
mti, na alijua yaliyomo nyoyoni mwao. Basi akateremsha utulivu juu yao, na
akawalipa kwa Ushindi wa karibu.
|
Ayah 48:19 الأية
وَمَغَانِمَ كَثِيرَةً يَأْخُذُونَهَا ۗ وَكَانَ اللَّهُ عَزِيزًا حَكِيمًا
Swahili
Na ngawira nyingi watakazo zichukua. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye nguvu, Mwenye
hikima.
|
Ayah 48:20 الأية
وَعَدَكُمُ اللَّهُ مَغَانِمَ كَثِيرَةً تَأْخُذُونَهَا فَعَجَّلَ لَكُمْ هَٰذِهِ
وَكَفَّ أَيْدِيَ النَّاسِ عَنكُمْ وَلِتَكُونَ آيَةً لِّلْمُؤْمِنِينَ
وَيَهْدِيَكُمْ صِرَاطًا مُّسْتَقِيمًا
Swahili
Mwenyezi Mungu anakuahidini ngawira nyingi mtakazo zichukua, basi
amekutangulizieni hizi kwanza, na akaizuia mikono ya watu isikufikieni, na ili
hayo yawe ni Ishara kwa Waumini, na akakuongozeni Njia Iliyo Nyooka.
|
Ayah 48:21 الأية
وَأُخْرَىٰ لَمْ تَقْدِرُوا عَلَيْهَا قَدْ أَحَاطَ اللَّهُ بِهَا ۚ وَكَانَ
اللَّهُ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرًا
Swahili
Na mengine hamwezi kuyapata bado, Mwenyezi Mungu amekwisha yazingia. Na Mwenyezi
Mungu ni Muweza wa kila kitu.
|
Ayah 48:22 الأية
وَلَوْ قَاتَلَكُمُ الَّذِينَ كَفَرُوا لَوَلَّوُا الْأَدْبَارَ ثُمَّ لَا
يَجِدُونَ وَلِيًّا وَلَا نَصِيرًا
Swahili
Na lau makafiri wangeli pigana nanyi basi bila ya shaka wangeli geuza migongo,
kisha wasingeli pata mlinzi wala msaidizi.
|
Ayah 48:23 الأية
سُنَّةَ اللَّهِ الَّتِي قَدْ خَلَتْ مِن قَبْلُ ۖ وَلَن تَجِدَ لِسُنَّةِ اللَّهِ
تَبْدِيلًا
Swahili
Huo ndio mwendo wa Mwenyezi Mungu ulio kwisha pita zamani, wala hutapata
mabadiliko katika mwendo wa Mwenyezi Mungu.
|
Ayah 48:24 الأية
وَهُوَ الَّذِي كَفَّ أَيْدِيَهُمْ عَنكُمْ وَأَيْدِيَكُمْ عَنْهُم بِبَطْنِ
مَكَّةَ مِن بَعْدِ أَنْ أَظْفَرَكُمْ عَلَيْهِمْ ۚ وَكَانَ اللَّهُ بِمَا
تَعْمَلُونَ بَصِيرًا
Swahili
Na Yeye ndiye aliyeizuia mikono yao kwenu, na mikono yenu kwao, katika bonde la
Makka baada ya kukupeni Ushindi juu yao. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kuyaona
myatendayo.
|
Ayah 48:25 الأية
هُمُ الَّذِينَ كَفَرُوا وَصَدُّوكُمْ عَنِ الْمَسْجِدِ الْحَرَامِ وَالْهَدْيَ
مَعْكُوفًا أَن يَبْلُغَ مَحِلَّهُ ۚ وَلَوْلَا رِجَالٌ مُّؤْمِنُونَ وَنِسَاءٌ
مُّؤْمِنَاتٌ لَّمْ تَعْلَمُوهُمْ أَن تَطَئُوهُمْ فَتُصِيبَكُم مِّنْهُم
مَّعَرَّةٌ بِغَيْرِ عِلْمٍ ۖ لِّيُدْخِلَ اللَّهُ فِي رَحْمَتِهِ مَن يَشَاءُ ۚ
لَوْ تَزَيَّلُوا لَعَذَّبْنَا الَّذِينَ كَفَرُوا مِنْهُمْ عَذَابًا أَلِيمًا
Swahili
Hao ndio walio kufuru na wakakuzuieni msiingie Msikiti Mtakatifu, na
wakawazuilia dhabihu kufika mahala pao. Na lau si wanaume Waumini na wanawake
Waumini msio wajua mkawasaga na mkaingia makosani kutokana nao bila ya kujua
...Mwenyezi Mungu (amefanya haya) ili amuingize amtakaye katika rehema yake. Lau
wangeli tengana bila ya shaka tungeli waadhibu walio kufuru kwa adhabu chungu.
|
Ayah 48:26 الأية
إِذْ جَعَلَ الَّذِينَ كَفَرُوا فِي قُلُوبِهِمُ الْحَمِيَّةَ حَمِيَّةَ
الْجَاهِلِيَّةِ فَأَنزَلَ اللَّهُ سَكِينَتَهُ عَلَىٰ رَسُولِهِ وَعَلَى
الْمُؤْمِنِينَ وَأَلْزَمَهُمْ كَلِمَةَ التَّقْوَىٰ وَكَانُوا أَحَقَّ بِهَا
وَأَهْلَهَا ۚ وَكَانَ اللَّهُ بِكُلِّ شَيْءٍ عَلِيمًا
Swahili
Pale walio kufuru walipo tia katika nyoyo zao hasira, hasira za kijinga,
Mwenyezi Mungu aliteremsha utulivu juu ya Mtume wake na juu ya Waumini, na
akawalazimisha neno la kuchamngu. Na wao walikuwa ndio wenye haki nalo na wenye
kustahili. Na Mwenyezi Mungu ni Mjuzi wa kila kitu.
|
Ayah 48:27 الأية
لَّقَدْ صَدَقَ اللَّهُ رَسُولَهُ الرُّؤْيَا بِالْحَقِّ ۖ لَتَدْخُلُنَّ
الْمَسْجِدَ الْحَرَامَ إِن شَاءَ اللَّهُ آمِنِينَ مُحَلِّقِينَ رُءُوسَكُمْ
وَمُقَصِّرِينَ لَا تَخَافُونَ ۖ فَعَلِمَ مَا لَمْ تَعْلَمُوا فَجَعَلَ مِن دُونِ
ذَٰلِكَ فَتْحًا قَرِيبًا
Swahili
Hakika Mwenyezi Mungu amemtimizia Mtume wake ndoto ya haki. Bila ya shaka nyinyi
mtauingia Msikiti Mtakatifu, Inshallah, kwa amani, na hali mmenyoa vichwa vyenu
na mmepunguza nywele. Hamtakuwa na khofu. Yeye anajua msiyo yajua. Basi
atakupeni kabla ya haya Ushindi karibuni.
|
Ayah 48:28 الأية
هُوَ الَّذِي أَرْسَلَ رَسُولَهُ بِالْهُدَىٰ وَدِينِ الْحَقِّ لِيُظْهِرَهُ عَلَى
الدِّينِ كُلِّهِ ۚ وَكَفَىٰ بِاللَّهِ شَهِيدًا
Swahili
Yeye ndiye aliye mtuma Mtume wake kwa uwongofu na Dini ya Haki, ili aitukuze juu
ya dini zote. Na Mwenyezi Mungu anatosha kuwa Shahidi.
|
Ayah 48:29 الأية
مُّحَمَّدٌ رَّسُولُ اللَّهِ ۚ وَالَّذِينَ مَعَهُ أَشِدَّاءُ عَلَى الْكُفَّارِ
رُحَمَاءُ بَيْنَهُمْ ۖ تَرَاهُمْ رُكَّعًا سُجَّدًا يَبْتَغُونَ فَضْلًا مِّنَ
اللَّهِ وَرِضْوَانًا ۖ سِيمَاهُمْ فِي وُجُوهِهِم مِّنْ أَثَرِ السُّجُودِ ۚ
ذَٰلِكَ مَثَلُهُمْ فِي التَّوْرَاةِ ۚ وَمَثَلُهُمْ فِي الْإِنجِيلِ كَزَرْعٍ
أَخْرَجَ شَطْأَهُ فَآزَرَهُ فَاسْتَغْلَظَ فَاسْتَوَىٰ عَلَىٰ سُوقِهِ يُعْجِبُ
الزُّرَّاعَ لِيَغِيظَ بِهِمُ الْكُفَّارَ ۗ وَعَدَ اللَّهُ الَّذِينَ آمَنُوا
وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ مِنْهُم مَّغْفِرَةً وَأَجْرًا عَظِيمًا
Swahili
Muhammad ni Mtume wa Mwenyezi Mungu. Na walio pamoja naye wana nguvu mbele ya
makafiri, na wanahurumiana wao kwa wao. Utawaona wakiinama na kusujudu
wakitafuta fadhila na radhi za Mwenyezi Mungu. Alama zao zi katika nyuso zao,
kwa athari ya kusujudu. Huu ndio mfano wao katika Taurati. Na mfano wao katika
Injili ni kama mmea ulio toa chipukizi lake, kisha ukalitia nguvu, ukawa mnene,
ukasimama sawa juu ya ubuwa wake, ukawafurahisha wakulima, ili kuwakasirisha kwa
ajili yao makafiri. Mwenyezi Mungu amewaahidi walio amini na wakatenda mema
katika wao msamaha na ujira mkubwa.
|
©
EsinIslam.Com Designed & produced by The Awqaf London. Please pray for us
|