First Ayah 1 الأية الأوليبِسْم ِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ
Ayah 44:2 الأية
وَالْكِتَابِ الْمُبِينِ
Swahili
Naapa kwa Kitabu kinacho bainisha,
|
Ayah 44:3 الأية
إِنَّا أَنزَلْنَاهُ فِي لَيْلَةٍ مُّبَارَكَةٍ ۚ إِنَّا كُنَّا مُنذِرِينَ
Swahili
Hakika tumekiteremsha katika usiku ulio barikiwa. Hakika Sisi ni Waonyaji.
|
Ayah 44:4 الأية
فِيهَا يُفْرَقُ كُلُّ أَمْرٍ حَكِيمٍ
Swahili
Katika usiku huu hubainishwa kila jambo la hikima,
|
Ayah 44:5 الأية
أَمْرًا مِّنْ عِندِنَا ۚ إِنَّا كُنَّا مُرْسِلِينَ
Swahili
Jambo litokalo kwetu. Hakika Sisi ndio wenye kutuma.
|
Ayah 44:6 الأية
رَحْمَةً مِّن رَّبِّكَ ۚ إِنَّهُ هُوَ السَّمِيعُ الْعَلِيمُ
Swahili
Ni rehema itokayo kwa Mola wako Mlezi. Hakika Yeye ni Mwenye kusikia Mwenye
kujua.
|
Ayah 44:7 الأية
رَبِّ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَمَا بَيْنَهُمَا ۖ إِن كُنتُم مُّوقِنِينَ
Swahili
Mola Mlezi wa mbingu na ardhi na vilio baina yao, ikiwa nyinyi mna yakini.
|
Ayah 44:8 الأية
لَا إِلَٰهَ إِلَّا هُوَ يُحْيِي وَيُمِيتُ ۖ رَبُّكُمْ وَرَبُّ آبَائِكُمُ
الْأَوَّلِينَ
Swahili
Hakuna mungu ila Yeye; anahuisha na anafisha- Mola Mlezi wenu na Mola Mlezi wa
baba zenu wa mwanzo.
|
Ayah 44:9 الأية
بَلْ هُمْ فِي شَكٍّ يَلْعَبُونَ
Swahili
Lakini wao wanacheza katika shaka.
|
Ayah 44:10 الأية
فَارْتَقِبْ يَوْمَ تَأْتِي السَّمَاءُ بِدُخَانٍ مُّبِينٍ
Swahili
Basi ingoje siku ambayo mbingu zitakapo leta moshi ulio dhaahiri,
|
Ayah 44:11 الأية
يَغْشَى النَّاسَ ۖ هَٰذَا عَذَابٌ أَلِيمٌ
Swahili
Utakao wafunika watu: Hii ni adhabu chungu!
|
Ayah 44:12 الأية
رَّبَّنَا اكْشِفْ عَنَّا الْعَذَابَ إِنَّا مُؤْمِنُونَ
Swahili
Mola wetu Mlezi! Tuondolee adhabu hii. Hakika tutaamini.
|
Ayah 44:13 الأية
أَنَّىٰ لَهُمُ الذِّكْرَىٰ وَقَدْ جَاءَهُمْ رَسُولٌ مُّبِينٌ
Swahili
Nini faida ya kukumbuka kwao? Na alikwisha wafikia Mtume mwenye kubainisha.
|
Ayah 44:14 الأية
ثُمَّ تَوَلَّوْا عَنْهُ وَقَالُوا مُعَلَّمٌ مَّجْنُونٌ
Swahili
Na wao wakamgeuzia uso, na wakasema: Huyu amefunzwa, naye ni mwendawazimu.
|
Ayah 44:15 الأية
إِنَّا كَاشِفُو الْعَذَابِ قَلِيلًا ۚ إِنَّكُمْ عَائِدُونَ
Swahili
Hakika sisi tutaiondoa adhabu kidogo, lakini nyinyi kwa yakini mtarejea vile
vile!
|
Ayah 44:16 الأية
يَوْمَ نَبْطِشُ الْبَطْشَةَ الْكُبْرَىٰ إِنَّا مُنتَقِمُونَ
Swahili
Siku tutayo yashambulia mashambulio makubwa, bila ya shaka Sisi ni wenye kutesa.
|
Ayah 44:17 الأية
وَلَقَدْ فَتَنَّا قَبْلَهُمْ قَوْمَ فِرْعَوْنَ وَجَاءَهُمْ رَسُولٌ كَرِيمٌ
Swahili
Na hakika kabla ya hawa tuliwafanyia mtihani watu wa Firauni, na aliwafikia
Mtume Mtukufu.
|
Ayah 44:18 الأية
أَنْ أَدُّوا إِلَيَّ عِبَادَ اللَّهِ ۖ إِنِّي لَكُمْ رَسُولٌ أَمِينٌ
Swahili
Akasema: Nipeni waja wa Mwenyezi Mungu; kwa hakika mimi kwenu ni Mtume
Muaminifu.
|
Ayah 44:19 الأية
وَأَن لَّا تَعْلُوا عَلَى اللَّهِ ۖ إِنِّي آتِيكُم بِسُلْطَانٍ مُّبِينٍ
Swahili
Na msimfanyie kiburi Mwenyezi Mungu; hakika mimi nitakuleteeni uthibitisho ulio
wazi.
|
Ayah 44:20 الأية
وَإِنِّي عُذْتُ بِرَبِّي وَرَبِّكُمْ أَن تَرْجُمُونِ
Swahili
Nami najikinga kwa Mola wangu Mlezi na ndiye Mola wenu Mlezi pia, ili msinipige
mawe.
|
Ayah 44:21 الأية
وَإِن لَّمْ تُؤْمِنُوا لِي فَاعْتَزِلُونِ
Swahili
Na ikiwa hamniamini, basi jitengeni nami.
|
Ayah 44:22 الأية
فَدَعَا رَبَّهُ أَنَّ هَٰؤُلَاءِ قَوْمٌ مُّجْرِمُونَ
Swahili
Ndipo akamwomba Mola wake Mlezi: Hakika watu hawa ni wakosefu.
|
Ayah 44:23 الأية
فَأَسْرِ بِعِبَادِي لَيْلًا إِنَّكُم مُّتَّبَعُونَ
Swahili
Mwenyezi Mungu akasema: Basi nenda na waja wangu usiku. Kwa yakini mtafuatwa.
|
Ayah 44:24 الأية
وَاتْرُكِ الْبَحْرَ رَهْوًا ۖ إِنَّهُمْ جُندٌ مُّغْرَقُونَ
Swahili
Na iache bahari vivyo hivyo imeachana, hakika wao hao ni jeshi litakalo
zamishwa.
|
Ayah 44:25 الأية
كَمْ تَرَكُوا مِن جَنَّاتٍ وَعُيُونٍ
Swahili
Mabustani mangapi, na chemchem ngapi waliziacha!
|
Ayah 44:26 الأية
وَزُرُوعٍ وَمَقَامٍ كَرِيمٍ
Swahili
Na mimea na vyeo vitukufu!
|
Ayah 44:27 الأية
وَنَعْمَةٍ كَانُوا فِيهَا فَاكِهِينَ
Swahili
Na neema walizo kuwa wakijistareheshea!
|
Ayah 44:28 الأية
كَذَٰلِكَ ۖ وَأَوْرَثْنَاهَا قَوْمًا آخَرِينَ
Swahili
Ndio hivyo! Na tukawarithisha haya watu wenginewe.
|
Ayah 44:29 الأية
فَمَا بَكَتْ عَلَيْهِمُ السَّمَاءُ وَالْأَرْضُ وَمَا كَانُوا مُنظَرِينَ
Swahili
La mbingu wala ardhi hazikuwalilia, wala hawakupewa muhula.
|
Ayah 44:30 الأية
وَلَقَدْ نَجَّيْنَا بَنِي إِسْرَائِيلَ مِنَ الْعَذَابِ الْمُهِينِ
Swahili
Na bila ya shaka tuliwaokoa Wana wa Israili katika adhabu ya kuwadhalilisha,
|
Ayah 44:31 الأية
مِن فِرْعَوْنَ ۚ إِنَّهُ كَانَ عَالِيًا مِّنَ الْمُسْرِفِينَ
Swahili
Ya Firauni. Hakika yeye alikuwa jeuri katika wenye kupindukia mipaka.
|
Ayah 44:32 الأية
وَلَقَدِ اخْتَرْنَاهُمْ عَلَىٰ عِلْمٍ عَلَى الْعَالَمِينَ
Swahili
Na tuliwakhiari kwa ujuzi wetu kuliko walimwengu wenginewe.
|
Ayah 44:33 الأية
وَآتَيْنَاهُم مِّنَ الْآيَاتِ مَا فِيهِ بَلَاءٌ مُّبِينٌ
Swahili
Na tukawapa katika ishara zenye majaribio yaliyo wazi.
|
Ayah 44:34 الأية
إِنَّ هَٰؤُلَاءِ لَيَقُولُونَ
Swahili
Hakika hawa wanasema:
|
Ayah 44:35 الأية
إِنْ هِيَ إِلَّا مَوْتَتُنَا الْأُولَىٰ وَمَا نَحْنُ بِمُنشَرِينَ
Swahili
Hapana ila kufa kwetu mara ya kwanza tu, wala sisi hatufufuliwi.
|
Ayah 44:36 الأية
فَأْتُوا بِآبَائِنَا إِن كُنتُمْ صَادِقِينَ
Swahili
Basi warudisheni baba zetu, ikiwa nyinyi mnasema kweli.
|
Ayah 44:37 الأية
أَهُمْ خَيْرٌ أَمْ قَوْمُ تُبَّعٍ وَالَّذِينَ مِن قَبْلِهِمْ ۚ أَهْلَكْنَاهُمْ ۖ
إِنَّهُمْ كَانُوا مُجْرِمِينَ
Swahili
Je! Ni wao bora au watu wa Tubbaa' na walio kuwa kabla yao? Tuliwaangamiza.
Hakika hao walikuwa wakosefu.
|
Ayah 44:38 الأية
وَمَا خَلَقْنَا السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضَ وَمَا بَيْنَهُمَا لَاعِبِينَ
Swahili
Na hatukuziumba mbingu na ardhi na vilivyomo baina yake kwa mchezo.
|
Ayah 44:39 الأية
مَا خَلَقْنَاهُمَا إِلَّا بِالْحَقِّ وَلَٰكِنَّ أَكْثَرَهُمْ لَا يَعْلَمُونَ
Swahili
Hatukuviumba hivyo ila kwa Haki, lakini wengi wao hawajui.
|
Ayah 44:40 الأية
إِنَّ يَوْمَ الْفَصْلِ مِيقَاتُهُمْ أَجْمَعِينَ
Swahili
Hakika siku ya Uamuzi ni wakati ulio wekwa kwa wao wote.
|
Ayah 44:41 الأية
يَوْمَ لَا يُغْنِي مَوْلًى عَن مَّوْلًى شَيْئًا وَلَا هُمْ يُنصَرُونَ
Swahili
Siku ambayo rafiki hatamfaa rafiki yake kwa chochote, wala hawatanusuriwa.
|
Ayah 44:42 الأية
إِلَّا مَن رَّحِمَ اللَّهُ ۚ إِنَّهُ هُوَ الْعَزِيزُ الرَّحِيمُ
Swahili
Isipo kuwa atakaye mrehemu Mwenyezi Mungu. Hakika Yeye ndiye Mwenye nguvu,
Mwenye kurehemu.
|
Ayah 44:43 الأية
إِنَّ شَجَرَتَ الزَّقُّومِ
Swahili
Hakika Mti wa Zaqqum,
|
Ayah 44:44 الأية
طَعَامُ الْأَثِيمِ
Swahili
Ni chakula cha mwenye dhambi.
|
Ayah 44:45 الأية
كَالْمُهْلِ يَغْلِي فِي الْبُطُونِ
Swahili
Kama shaba iliyo yayushwa, hutokota matumboni
|
Ayah 44:46 الأية
كَغَلْيِ الْحَمِيمِ
Swahili
Kama kutokota kwa maji ya moto.
|
Ayah 44:47 الأية
خُذُوهُ فَاعْتِلُوهُ إِلَىٰ سَوَاءِ الْجَحِيمِ
Swahili
(Itasemwa:) Mkamateni na mtupeni katikati ya Jahannamu!
|
Ayah 44:48 الأية
ثُمَّ صُبُّوا فَوْقَ رَأْسِهِ مِنْ عَذَابِ الْحَمِيمِ
Swahili
Kisha mmwagieni juu ya kichwa chake adhabu ya maji yanayo chemka.
|
Ayah 44:49 الأية
ذُقْ إِنَّكَ أَنتَ الْعَزِيزُ الْكَرِيمُ
Swahili
Onja! Ati wewe ndiye mwenye nguvu, mtukufu!
|
Ayah 44:50 الأية
إِنَّ هَٰذَا مَا كُنتُم بِهِ تَمْتَرُونَ
Swahili
Hakika haya ndiyo mliyo kuwa mkiyatilia shaka.
|
Ayah 44:51 الأية
إِنَّ الْمُتَّقِينَ فِي مَقَامٍ أَمِينٍ
Swahili
Hakika wachamngu watakuwa katika mahali pa amani,
|
Ayah 44:52 الأية
فِي جَنَّاتٍ وَعُيُونٍ
Swahili
Katika mabustani na chemchem,
|
Ayah 44:53 الأية
يَلْبَسُونَ مِن سُندُسٍ وَإِسْتَبْرَقٍ مُّتَقَابِلِينَ
Swahili
Watavaa hariri nyepesi na hariri nzito wakikabiliana,
|
Ayah 44:54 الأية
كَذَٰلِكَ وَزَوَّجْنَاهُم بِحُورٍ عِينٍ
Swahili
Hivi ndivyo itakavyo kuwa, na tutawaoza mahurilaini.
|
Ayah 44:55 الأية
يَدْعُونَ فِيهَا بِكُلِّ فَاكِهَةٍ آمِنِينَ
Swahili
Humo watataka kila aina ya matunda, na wakae kwa amani.
|
Ayah 44:56 الأية
لَا يَذُوقُونَ فِيهَا الْمَوْتَ إِلَّا الْمَوْتَةَ الْأُولَىٰ ۖ وَوَقَاهُمْ
عَذَابَ الْجَحِيمِ
Swahili
Humo hawataonja mauti ila mauti yale ya kwanza, na (Mwenyezi Mungu) atawalinda
na adhabu ya Jahannamu,
|
Ayah 44:57 الأية
فَضْلًا مِّن رَّبِّكَ ۚ ذَٰلِكَ هُوَ الْفَوْزُ الْعَظِيمُ
Swahili
Kuwa ni fadhila zitokazo kwa Mola wako Mlezi. Huko ndiko kufuzu kukubwa.
|
Ayah 44:58 الأية
فَإِنَّمَا يَسَّرْنَاهُ بِلِسَانِكَ لَعَلَّهُمْ يَتَذَكَّرُونَ
Swahili
Basi tumeifanya nyepesi hii Qur'ani kwa ulimi wako, ili wapate kukumbuka.
|
Ayah 44:59 الأية
فَارْتَقِبْ إِنَّهُم مُّرْتَقِبُونَ
Swahili
Ngoja tu, na wao wangoje pia.
|
©
EsinIslam.Com Designed & produced by The Awqaf London. Please pray for us
|