Prev  

73. Surah Al-Muzzammil سورة المزّمّل

  Next  



Ayah  73:1  الأية
    +/- -/+  
بِسْم ِ اللهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ

Ayah  73:2  الأية
    +/- -/+  

Ayah  73:3  الأية
    +/- -/+  

Ayah  73:4  الأية
    +/- -/+  
أَوْ زِدْ عَلَيْهِ وَرَتِّلِ الْقُرْآنَ تَرْتِيلًا
Swahili
 
Au izidishe - na soma Qur'ani kwa utaratibu na utungo.

Ayah  73:5  الأية
    +/- -/+  
إِنَّا سَنُلْقِي عَلَيْكَ قَوْلًا ثَقِيلًا
Swahili
 
Hakika Sisi tutakuteremshia kauli nzito.

Ayah  73:6  الأية
    +/- -/+  
إِنَّ نَاشِئَةَ اللَّيْلِ هِيَ أَشَدُّ وَطْئًا وَأَقْوَمُ قِيلًا
Swahili
 
Hakika kuamka usiku kunawafikiana zaidi na moyo, na maneno yake yanatua zaidi.

Ayah  73:7  الأية
    +/- -/+  
إِنَّ لَكَ فِي النَّهَارِ سَبْحًا طَوِيلًا
Swahili
 
Kwani hakika mchana una shughuli nyingi.

Ayah  73:8  الأية
    +/- -/+  
وَاذْكُرِ اسْمَ رَبِّكَ وَتَبَتَّلْ إِلَيْهِ تَبْتِيلًا
Swahili
 
Na lidhukuru jina la Mola wako Mlezi, na ujitolee kwake kwa ukamilifu.

Ayah  73:9  الأية
    +/- -/+  
رَّبُّ الْمَشْرِقِ وَالْمَغْرِبِ لَا إِلَٰهَ إِلَّا هُوَ فَاتَّخِذْهُ وَكِيلًا
Swahili
 
Mola Mlezi wa mashariki na magharibi, hapana mungu isipo kuwa Yeye, basi mfanye kuwa Mtegemewa wako.

Ayah  73:10  الأية
    +/- -/+  
وَاصْبِرْ عَلَىٰ مَا يَقُولُونَ وَاهْجُرْهُمْ هَجْرًا جَمِيلًا
Swahili
 
Na vumilia hayo wayasemayo, na jitenge nao kwa vizuri.

Ayah  73:11  الأية
    +/- -/+  
وَذَرْنِي وَالْمُكَذِّبِينَ أُولِي النَّعْمَةِ وَمَهِّلْهُمْ قَلِيلًا
Swahili
 
Na niache Mimi na hao wanao kanusha, walio neemeka; na wape muhula kidogo!

Ayah  73:12  الأية
    +/- -/+  
إِنَّ لَدَيْنَا أَنكَالًا وَجَحِيمًا
Swahili
 
Hakika Sisi tunazo pingu nzito na Moto unao waka kwa ukali kabisa!

Ayah  73:13  الأية
    +/- -/+  
وَطَعَامًا ذَا غُصَّةٍ وَعَذَابًا أَلِيمًا
Swahili
 
Na chakula kinacho kwama kooni, na adhabu inayo umiza.

Ayah  73:14  الأية
    +/- -/+  
يَوْمَ تَرْجُفُ الْأَرْضُ وَالْجِبَالُ وَكَانَتِ الْجِبَالُ كَثِيبًا مَّهِيلًا
Swahili
 
Siku ambayo ardhi itatikiswa na milima pia, na milima itakuwa kama tifutifu la mchanga!

Ayah  73:15  الأية
    +/- -/+  
إِنَّا أَرْسَلْنَا إِلَيْكُمْ رَسُولًا شَاهِدًا عَلَيْكُمْ كَمَا أَرْسَلْنَا إِلَىٰ فِرْعَوْنَ رَسُولًا
Swahili
 
Hakika Sisi tumemtuma kwenu Mtume aliye shahidi juu yenu, kama tulivyo mtuma Mtume kwa Firauni.

Ayah  73:16  الأية
    +/- -/+  
فَعَصَىٰ فِرْعَوْنُ الرَّسُولَ فَأَخَذْنَاهُ أَخْذًا وَبِيلًا
Swahili
 
Lakini Firauni alimuasi huyo Mtume, basi tukamshika mshiko wa mateso.

Ayah  73:17  الأية
    +/- -/+  
فَكَيْفَ تَتَّقُونَ إِن كَفَرْتُمْ يَوْمًا يَجْعَلُ الْوِلْدَانَ شِيبًا
Swahili
 
Basi nyinyi mkikufuru, mtawezaje kujikinga na Siku ambayo itawafanya watoto wadogo waote mvi?

Ayah  73:18  الأية
    +/- -/+  
السَّمَاءُ مُنفَطِرٌ بِهِ ۚ كَانَ وَعْدُهُ مَفْعُولًا
Swahili
 
Hapo mbingu zitapasuka! Ahadi yake itakuwa imetekelezwa.

Ayah  73:19  الأية
    +/- -/+  
إِنَّ هَٰذِهِ تَذْكِرَةٌ ۖ فَمَن شَاءَ اتَّخَذَ إِلَىٰ رَبِّهِ سَبِيلًا
Swahili
 
Kwa hakika hili ni kumbusho. Mwenye kutaka atashika njia ya kwendea kwa Mola wake Mlezi.

Ayah  73:20  الأية
    +/- -/+  
إِنَّ رَبَّكَ يَعْلَمُ أَنَّكَ تَقُومُ أَدْنَىٰ مِن ثُلُثَيِ اللَّيْلِ وَنِصْفَهُ وَثُلُثَهُ وَطَائِفَةٌ مِّنَ الَّذِينَ مَعَكَ ۚ وَاللهُ يُقَدِّرُ اللَّيْلَ وَالنَّهَارَ ۚ عَلِمَ أَن لَّن تُحْصُوهُ فَتَابَ عَلَيْكُمْ ۖ فَاقْرَءُوا مَا تَيَسَّرَ مِنَ الْقُرْآنِ ۚ عَلِمَ أَن سَيَكُونُ مِنكُم مَّرْضَىٰ ۙ وَآخَرُونَ يَضْرِبُونَ فِي الْأَرْضِ يَبْتَغُونَ مِن فَضْلِ اللهِ ۙ وَآخَرُونَ يُقَاتِلُونَ فِي سَبِيلِ اللهِ ۖ فَاقْرَءُوا مَا تَيَسَّرَ مِنْهُ ۚ وَأَقِيمُوا الصَّلَاةَ وَآتُوا الزَّكَاةَ وَأَقْرِضُوا اللهَ قَرْضًا حَسَنًا ۚ وَمَا تُقَدِّمُوا لِأَنفُسِكُم مِّنْ خَيْرٍ تَجِدُوهُ عِندَ اللهِ هُوَ خَيْرًا وَأَعْظَمَ أَجْرًا ۚ وَاسْتَغْفِرُوا اللهَ ۖ إِنَّ اللهَ غَفُورٌ رَّحِيمٌ
Swahili
 
Hakika Mola wako Mlezi anajua ya kuwa hakika wewe unakesha karibu na thuluthi mbili za usiku, na nusu yake, na thuluthi yake. Na baadhi ya watu walio pamoja nawe kadhaalika. Na Mwenyezi Mungu ndiye anaye ukadiria usiku na mchana. Anajua kuwa hamwezi kuweka hisabu, basi amekusameheni. Basi someni kilicho chepesi katika Qur'ani. Anajua ya kuwa baadhi yenu watakuwa wagonjwa, na wengine wanasafiri katika ardhi wakitafuta fadhila ya Mwenyezi Mungu, na wengine wanapigana katika Njia ya Mwenyezi Mungu. Kwa hivyo someni kilicho chepesi humo, na mshike Sala, na toeni Zaka, na mkopesheni Mwenyezi Mungu mkopo mwema. Na kheri yoyote mnayo itanguliza kwa ajili ya nafsi zenu mtaikuta kwa Mwenyezi Mungu, imekuwa bora zaidi, na ina thawabu kubwa sana. Na mtakeni msamaha Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusamehe Mwenye kurehemu.
 


© EsinIslam.Com Designed & produced by The Awqaf London. Please pray for us