« Prev
80. Surah 'Abasa سورة عبس
Next »
First Ayah 1 الأية الأوليبِسْم ِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ
عَبَسَ وَتَوَلَّىٰ
Swahili
Alikunja kipaji na akageuka,
|
Ayah 80:2 الأية
أَن جَاءَهُ الْأَعْمَىٰ
Swahili
Kwa sababu alimjia kipofu!
|
Ayah 80:3 الأية
وَمَا يُدْرِيكَ لَعَلَّهُ يَزَّكَّىٰ
Swahili
Na nini kitakujuulisha pengine yeye atatakasika?
|
Ayah 80:4 الأية
أَوْ يَذَّكَّرُ فَتَنفَعَهُ الذِّكْرَىٰ
Swahili
Au atawaidhika, na mawaidha yamfae?
|
Ayah 80:5 الأية
أَمَّا مَنِ اسْتَغْنَىٰ
Swahili
Ama ajionaye hana haja,
|
Ayah 80:6 الأية
فَأَنتَ لَهُ تَصَدَّىٰ
Swahili
Wewe ndio unamshughulikia?
|
Ayah 80:7 الأية
وَمَا عَلَيْكَ أَلَّا يَزَّكَّىٰ
Swahili
Na si juu yako kama hakutakasika.
|
Ayah 80:8 الأية
وَأَمَّا مَن جَاءَكَ يَسْعَىٰ
Swahili
Ama anaye kujia kwa juhudi,
|
Ayah 80:9 الأية
وَهُوَ يَخْشَىٰ
Swahili
Naye anaogopa,
|
Ayah 80:10 الأية
فَأَنتَ عَنْهُ تَلَهَّىٰ
Swahili
Ndio wewe unampuuza?
|
Ayah 80:11 الأية
كَلَّا إِنَّهَا تَذْكِرَةٌ
Swahili
Sivyo hivyo! Huku ni kukumbushana.
|
Ayah 80:12 الأية
فَمَن شَاءَ ذَكَرَهُ
Swahili
Basi anaye penda akumbuke.
|
Ayah 80:13 الأية
فِي صُحُفٍ مُّكَرَّمَةٍ
Swahili
Yamo katika kurasa zilizo hishimiwa,
|
Ayah 80:14 الأية
مَّرْفُوعَةٍ مُّطَهَّرَةٍ
Swahili
Zilizo inuliwa, zilizo takaswa.
|
Ayah 80:15 الأية
بِأَيْدِي سَفَرَةٍ
Swahili
Zimo mikononi mwa Malaika waandishi,
|
Ayah 80:16 الأية
كِرَامٍ بَرَرَةٍ
Swahili
Watukufu, wema.
|
Ayah 80:17 الأية
قُتِلَ الْإِنسَانُ مَا أَكْفَرَهُ
Swahili
Ameangamia mwanaadamu! Nini kinacho mkufurisha?
|
Ayah 80:18 الأية
مِنْ أَيِّ شَيْءٍ خَلَقَهُ
Swahili
Kwa kitu gani amemuumba?
|
Ayah 80:19 الأية
مِن نُّطْفَةٍ خَلَقَهُ فَقَدَّرَهُ
Swahili
Kwa tone la manii, akamuumba na akamkadiria.
|
Ayah 80:20 الأية
ثُمَّ السَّبِيلَ يَسَّرَهُ
Swahili
Kisha akamsahilishia njia.
|
Ayah 80:21 الأية
ثُمَّ أَمَاتَهُ فَأَقْبَرَهُ
Swahili
Kisha akamfisha, akamtia kaburini.
|
Ayah 80:22 الأية
ثُمَّ إِذَا شَاءَ أَنشَرَهُ
Swahili
Kisha apendapo atamfufua.
|
Ayah 80:23 الأية
كَلَّا لَمَّا يَقْضِ مَا أَمَرَهُ
Swahili
La! Hajamaliza aliyo muamuru.
|
Ayah 80:24 الأية
فَلْيَنظُرِ الْإِنسَانُ إِلَىٰ طَعَامِهِ
Swahili
Hebu mtu na atazame chakula chake.
|
Ayah 80:25 الأية
أَنَّا صَبَبْنَا الْمَاءَ صَبًّا
Swahili
Hakika Sisi tumemimina maji kwa nguvu,
|
Ayah 80:26 الأية
ثُمَّ شَقَقْنَا الْأَرْضَ شَقًّا
Swahili
Tena tukaipasua pasua ardhi kwa nguvu,
|
Ayah 80:27 الأية
فَأَنبَتْنَا فِيهَا حَبًّا
Swahili
Kisha tukaotesha humo nafaka,
|
Ayah 80:28 الأية
وَعِنَبًا وَقَضْبًا
Swahili
Na zabibu, na mimea ya majani,
|
Ayah 80:29 الأية
وَزَيْتُونًا وَنَخْلًا
Swahili
Na mizaituni, na mitende,
|
Ayah 80:30 الأية
وَحَدَائِقَ غُلْبًا
Swahili
Na bustani zenye miti iliyo songana baraabara,
|
Ayah 80:31 الأية
وَفَاكِهَةً وَأَبًّا
Swahili
Na matunda, na malisho ya wanyama;
|
Ayah 80:32 الأية
مَّتَاعًا لَّكُمْ وَلِأَنْعَامِكُمْ
Swahili
Kwa manufaa yenu na mifugo yenu.
|
Ayah 80:33 الأية
فَإِذَا جَاءَتِ الصَّاخَّةُ
Swahili
Basi utakapo kuja ukelele,
|
Ayah 80:34 الأية
يَوْمَ يَفِرُّ الْمَرْءُ مِنْ أَخِيهِ
Swahili
Siku ambayo mtu atamkimbia nduguye,
|
Ayah 80:35 الأية
وَأُمِّهِ وَأَبِيهِ
Swahili
Na mamaye na babaye,
|
Ayah 80:36 الأية
وَصَاحِبَتِهِ وَبَنِيهِ
Swahili
Na mkewe na wanawe -
|
Ayah 80:37 الأية
لِكُلِّ امْرِئٍ مِّنْهُمْ يَوْمَئِذٍ شَأْنٌ يُغْنِيهِ
Swahili
Kila mtu miongoni mwao siku hiyo atakuwa na lake la kumtosha.
|
Ayah 80:38 الأية
وُجُوهٌ يَوْمَئِذٍ مُّسْفِرَةٌ
Swahili
Siku hiyo ziko nyuso zitazo nawiri,
|
Ayah 80:39 الأية
ضَاحِكَةٌ مُّسْتَبْشِرَةٌ
Swahili
Zitacheka, zitachangamka;
|
Ayah 80:40 الأية
وَوُجُوهٌ يَوْمَئِذٍ عَلَيْهَا غَبَرَةٌ
Swahili
Na nyuso siku hiyo zitakuwa na mavumbi,
|
Ayah 80:41 الأية
تَرْهَقُهَا قَتَرَةٌ
Swahili
Giza totoro litazifunika,
|
Ayah 80:42 الأية
أُولَٰئِكَ هُمُ الْكَفَرَةُ الْفَجَرَةُ
Swahili
Hao ndio makafiri watenda maovu.
|
©
EsinIslam.Com Designed & produced by The Awqaf London. Please pray for us
|
|