« Prev

80. Surah 'Abasa سورة عبس

Next »



First Ayah   1   الأية الأولي
بِسْم ِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ
عَبَسَ وَتَوَلَّىٰ
Swahili
 
Alikunja kipaji na akageuka,

Ayah   80:2   الأية
أَن جَاءَهُ الْأَعْمَىٰ
Swahili
 
Kwa sababu alimjia kipofu!

Ayah   80:3   الأية
وَمَا يُدْرِيكَ لَعَلَّهُ يَزَّكَّىٰ
Swahili
 
Na nini kitakujuulisha pengine yeye atatakasika?

Ayah   80:4   الأية
أَوْ يَذَّكَّرُ فَتَنفَعَهُ الذِّكْرَىٰ
Swahili
 
Au atawaidhika, na mawaidha yamfae?

Ayah   80:5   الأية
أَمَّا مَنِ اسْتَغْنَىٰ
Swahili
 
Ama ajionaye hana haja,

Ayah   80:6   الأية
فَأَنتَ لَهُ تَصَدَّىٰ
Swahili
 
Wewe ndio unamshughulikia?

Ayah   80:7   الأية
وَمَا عَلَيْكَ أَلَّا يَزَّكَّىٰ
Swahili
 
Na si juu yako kama hakutakasika.

Ayah   80:8   الأية
وَأَمَّا مَن جَاءَكَ يَسْعَىٰ
Swahili
 
Ama anaye kujia kwa juhudi,

Ayah   80:9   الأية
وَهُوَ يَخْشَىٰ
Swahili
 
Naye anaogopa,

Ayah   80:10   الأية
فَأَنتَ عَنْهُ تَلَهَّىٰ
Swahili
 
Ndio wewe unampuuza?

Ayah   80:11   الأية
كَلَّا إِنَّهَا تَذْكِرَةٌ
Swahili
 
Sivyo hivyo! Huku ni kukumbushana.

Ayah   80:12   الأية
فَمَن شَاءَ ذَكَرَهُ
Swahili
 
Basi anaye penda akumbuke.

Ayah   80:13   الأية
فِي صُحُفٍ مُّكَرَّمَةٍ
Swahili
 
Yamo katika kurasa zilizo hishimiwa,

Ayah   80:14   الأية
مَّرْفُوعَةٍ مُّطَهَّرَةٍ
Swahili
 
Zilizo inuliwa, zilizo takaswa.

Ayah   80:15   الأية
بِأَيْدِي سَفَرَةٍ
Swahili
 
Zimo mikononi mwa Malaika waandishi,

Ayah   80:16   الأية
كِرَامٍ بَرَرَةٍ
Swahili
 
Watukufu, wema.

Ayah   80:17   الأية
قُتِلَ الْإِنسَانُ مَا أَكْفَرَهُ
Swahili
 
Ameangamia mwanaadamu! Nini kinacho mkufurisha?

Ayah   80:18   الأية
مِنْ أَيِّ شَيْءٍ خَلَقَهُ
Swahili
 
Kwa kitu gani amemuumba?

Ayah   80:19   الأية
مِن نُّطْفَةٍ خَلَقَهُ فَقَدَّرَهُ
Swahili
 
Kwa tone la manii, akamuumba na akamkadiria.

Ayah   80:20   الأية
ثُمَّ السَّبِيلَ يَسَّرَهُ
Swahili
 
Kisha akamsahilishia njia.

Ayah   80:21   الأية
ثُمَّ أَمَاتَهُ فَأَقْبَرَهُ
Swahili
 
Kisha akamfisha, akamtia kaburini.

Ayah   80:22   الأية
ثُمَّ إِذَا شَاءَ أَنشَرَهُ
Swahili
 
Kisha apendapo atamfufua.

Ayah   80:23   الأية
كَلَّا لَمَّا يَقْضِ مَا أَمَرَهُ
Swahili
 
La! Hajamaliza aliyo muamuru.

Ayah   80:24   الأية
فَلْيَنظُرِ الْإِنسَانُ إِلَىٰ طَعَامِهِ
Swahili
 
Hebu mtu na atazame chakula chake.

Ayah   80:25   الأية
أَنَّا صَبَبْنَا الْمَاءَ صَبًّا
Swahili
 
Hakika Sisi tumemimina maji kwa nguvu,

Ayah   80:26   الأية
ثُمَّ شَقَقْنَا الْأَرْضَ شَقًّا
Swahili
 
Tena tukaipasua pasua ardhi kwa nguvu,

Ayah   80:27   الأية
فَأَنبَتْنَا فِيهَا حَبًّا
Swahili
 
Kisha tukaotesha humo nafaka,

Ayah   80:28   الأية
وَعِنَبًا وَقَضْبًا
Swahili
 
Na zabibu, na mimea ya majani,

Ayah   80:29   الأية
وَزَيْتُونًا وَنَخْلًا
Swahili
 
Na mizaituni, na mitende,

Ayah   80:30   الأية
وَحَدَائِقَ غُلْبًا
Swahili
 
Na bustani zenye miti iliyo songana baraabara,

Ayah   80:31   الأية
وَفَاكِهَةً وَأَبًّا
Swahili
 
Na matunda, na malisho ya wanyama;

Ayah   80:32   الأية
مَّتَاعًا لَّكُمْ وَلِأَنْعَامِكُمْ
Swahili
 
Kwa manufaa yenu na mifugo yenu.

Ayah   80:33   الأية
فَإِذَا جَاءَتِ الصَّاخَّةُ
Swahili
 
Basi utakapo kuja ukelele,

Ayah   80:34   الأية
يَوْمَ يَفِرُّ الْمَرْءُ مِنْ أَخِيهِ
Swahili
 
Siku ambayo mtu atamkimbia nduguye,

Ayah   80:35   الأية
وَأُمِّهِ وَأَبِيهِ
Swahili
 
Na mamaye na babaye,

Ayah   80:36   الأية
وَصَاحِبَتِهِ وَبَنِيهِ
Swahili
 
Na mkewe na wanawe -

Ayah   80:37   الأية
لِكُلِّ امْرِئٍ مِّنْهُمْ يَوْمَئِذٍ شَأْنٌ يُغْنِيهِ
Swahili
 
Kila mtu miongoni mwao siku hiyo atakuwa na lake la kumtosha.

Ayah   80:38   الأية
وُجُوهٌ يَوْمَئِذٍ مُّسْفِرَةٌ
Swahili
 
Siku hiyo ziko nyuso zitazo nawiri,

Ayah   80:39   الأية
ضَاحِكَةٌ مُّسْتَبْشِرَةٌ
Swahili
 
Zitacheka, zitachangamka;

Ayah   80:40   الأية
وَوُجُوهٌ يَوْمَئِذٍ عَلَيْهَا غَبَرَةٌ
Swahili
 
Na nyuso siku hiyo zitakuwa na mavumbi,

Ayah   80:41   الأية
تَرْهَقُهَا قَتَرَةٌ
Swahili
 
Giza totoro litazifunika,

Ayah   80:42   الأية
أُولَٰئِكَ هُمُ الْكَفَرَةُ الْفَجَرَةُ
Swahili
 
Hao ndio makafiri watenda maovu.
 


© EsinIslam.Com Designed & produced by The Awqaf London. Please pray for us