« Prev

37. Surah As-Sâffât سورة الصافات

Next »



First Ayah   1   الأية الأولي
بِسْم ِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ
وَالصَّافَّاتِ صَفًّا
Swahili
 
Naapa kwa wanao jipanga kwa safu.

Ayah   37:2   الأية
فَالزَّاجِرَاتِ زَجْرًا
Swahili
 
Na kwa wenye kukataza mabaya.

Ayah   37:3   الأية
فَالتَّالِيَاتِ ذِكْرًا
Swahili
 
Na kwa wenye kusoma Ukumbusho.

Ayah   37:4   الأية
إِنَّ إِلَٰهَكُمْ لَوَاحِدٌ
Swahili
 
Hakika Mungu wenu bila ya shaka ni Mmoja.

Ayah   37:5   الأية
رَّبُّ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَمَا بَيْنَهُمَا وَرَبُّ الْمَشَارِقِ
Swahili
 
Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, na yaliyomo kati yao, na ni Mola Mlezi wa mashariki zote.

Ayah   37:6   الأية
إِنَّا زَيَّنَّا السَّمَاءَ الدُّنْيَا بِزِينَةٍ الْكَوَاكِبِ
Swahili
 
Hakika Sisi tumeipamba mbingu ya karibu kwa pambo la nyota.

Ayah   37:7   الأية
وَحِفْظًا مِّن كُلِّ شَيْطَانٍ مَّارِدٍ
Swahili
 
Na kulinda na kila shet'ani a'si.

Ayah   37:8   الأية
لَّا يَسَّمَّعُونَ إِلَى الْمَلَإِ الْأَعْلَىٰ وَيُقْذَفُونَ مِن كُلِّ جَانِبٍ
Swahili
 
Wasiweze kuwasikiliza viumbe watukufu. Na wanafukuzwa huko kila upande.

Ayah   37:9   الأية
دُحُورًا ۖ وَلَهُمْ عَذَابٌ وَاصِبٌ
Swahili
 
Wakifurushwa. Na wanayo adhabu ya kudumu.

Ayah   37:10   الأية
إِلَّا مَنْ خَطِفَ الْخَطْفَةَ فَأَتْبَعَهُ شِهَابٌ ثَاقِبٌ
Swahili
 
Isipo kuwa anaye nyakua kitu kidogo, na mara humfwatia kimondo kinacho ng'ara.

Ayah   37:11   الأية
فَاسْتَفْتِهِمْ أَهُمْ أَشَدُّ خَلْقًا أَم مَّنْ خَلَقْنَا ۚ إِنَّا خَلَقْنَاهُم مِّن طِينٍ لَّازِبٍ
Swahili
 
Hebu waulize: Je! Wao ni wenye umbo gumu zaidi au hao wengine tulio waumba. Hakika Sisi tuliwaumba wao kwa udongo unao nata.

Ayah   37:12   الأية
بَلْ عَجِبْتَ وَيَسْخَرُونَ
Swahili
 
Bali unastaajabu, na wao wanafanya maskhara.

Ayah   37:13   الأية
وَإِذَا ذُكِّرُوا لَا يَذْكُرُونَ
Swahili
 
Na wanapo kumbushwa hawakumbuki.

Ayah   37:14   الأية
وَإِذَا رَأَوْا آيَةً يَسْتَسْخِرُونَ
Swahili
 
Na wanapo ona Ishara, wanafanya maskhara.

Ayah   37:15   الأية
وَقَالُوا إِنْ هَٰذَا إِلَّا سِحْرٌ مُّبِينٌ
Swahili
 
Na husema: Haya si chochote ila ni uchawi tu ulio dhaahiri.

Ayah   37:16   الأية
أَإِذَا مِتْنَا وَكُنَّا تُرَابًا وَعِظَامًا أَإِنَّا لَمَبْعُوثُونَ
Swahili
 
Ati tukisha kufa na tukawa udongo na mifupa ndio kweli tutafufuliwa?

Ayah   37:17   الأية
أَوَآبَاؤُنَا الْأَوَّلُونَ
Swahili
 
Hata baba zetu wa zamani?

Ayah   37:18   الأية
قُلْ نَعَمْ وَأَنتُمْ دَاخِرُونَ
Swahili
 
Sema: Naam! Hali nanyi ni madhalili.

Ayah   37:19   الأية
فَإِنَّمَا هِيَ زَجْرَةٌ وَاحِدَةٌ فَإِذَا هُمْ يَنظُرُونَ
Swahili
 
Huko utapigwa ukelele mmoja tu! Na hapo ndio wataona!

Ayah   37:20   الأية
وَقَالُوا يَا وَيْلَنَا هَٰذَا يَوْمُ الدِّينِ
Swahili
 
Watasema: Ole wetu! Hii ndiyo Siku ya Malipo.

Ayah   37:21   الأية
هَٰذَا يَوْمُ الْفَصْلِ الَّذِي كُنتُم بِهِ تُكَذِّبُونَ
Swahili
 
Hii ndiyo Siku ya Hukumu mliyo kuwa mkiikadhibisha.

Ayah   37:22   الأية
احْشُرُوا الَّذِينَ ظَلَمُوا وَأَزْوَاجَهُمْ وَمَا كَانُوا يَعْبُدُونَ
Swahili
 
Wakusanyeni walio dhulumu, na wake zao, na hao walio kuwa wakiwaabudu -

Ayah   37:23   الأية
مِن دُونِ اللَّهِ فَاهْدُوهُمْ إِلَىٰ صِرَاطِ الْجَحِيمِ
Swahili
 
Badala ya Mwenyezi Mungu. Waongozeni njia ya Jahannamu!

Ayah   37:24   الأية
وَقِفُوهُمْ ۖ إِنَّهُم مَّسْئُولُونَ
Swahili
 
Na wasimamisheni. Hakika hao watasailiwa:

Ayah   37:25   الأية
مَا لَكُمْ لَا تَنَاصَرُونَ
Swahili
 
Mna nini? Mbona hamsaidiani?

Ayah   37:26   الأية
بَلْ هُمُ الْيَوْمَ مُسْتَسْلِمُونَ
Swahili
 
Bali hii leo, watasalimu amri.

Ayah   37:27   الأية
وَأَقْبَلَ بَعْضُهُمْ عَلَىٰ بَعْضٍ يَتَسَاءَلُونَ
Swahili
 
Watakabiliana wao kwa wao kuulizana.

Ayah   37:28   الأية
قَالُوا إِنَّكُمْ كُنتُمْ تَأْتُونَنَا عَنِ الْيَمِينِ
Swahili
 
Watasema: Kwa hakika nyinyi mlikuwa mkitujia upande wa kulia.

Ayah   37:29   الأية
قَالُوا بَل لَّمْ تَكُونُوا مُؤْمِنِينَ
Swahili
 
Watasema (wakubwa): Bali nyinyi wenyewe hamkuwa Waumini.

Ayah   37:30   الأية
وَمَا كَانَ لَنَا عَلَيْكُم مِّن سُلْطَانٍ ۖ بَلْ كُنتُمْ قَوْمًا طَاغِينَ
Swahili
 
Sisi hatukuwa na mamlaka juu yenu, bali nyinyi wenyewe mlikuwa wapotovu.

Ayah   37:31   الأية
فَحَقَّ عَلَيْنَا قَوْلُ رَبِّنَا ۖ إِنَّا لَذَائِقُونَ
Swahili
 
Basi hukumu ya Mola wetu Mlezi imekwisha tuthibitikia. Hakika bila ya shaka tutaonja tu adhabu.

Ayah   37:32   الأية
فَأَغْوَيْنَاكُمْ إِنَّا كُنَّا غَاوِينَ
Swahili
 
Tulikupotezeni kwa sababu sisi wenyewe tulikuwa wapotovu.

Ayah   37:33   الأية
فَإِنَّهُمْ يَوْمَئِذٍ فِي الْعَذَابِ مُشْتَرِكُونَ
Swahili
 
Basi wao kwa hakika siku hiyo watashirikiana katika adhabu pamoja.

Ayah   37:34   الأية
إِنَّا كَذَٰلِكَ نَفْعَلُ بِالْمُجْرِمِينَ
Swahili
 
Hivyo ndivyo tutakavyo wafanyia wakosefu.

Ayah   37:35   الأية
إِنَّهُمْ كَانُوا إِذَا قِيلَ لَهُمْ لَا إِلَٰهَ إِلَّا اللَّهُ يَسْتَكْبِرُونَ
Swahili
 
Wao walipo kuwa wakiambiwa La ilaha illa 'Llahu Hapana mungu ila Mwenyezi Mungu tu, wakijivuna.

Ayah   37:36   الأية
وَيَقُولُونَ أَئِنَّا لَتَارِكُو آلِهَتِنَا لِشَاعِرٍ مَّجْنُونٍ
Swahili
 
Na wakisema: Hivyo sisi tuiache miungu yetu kwa ajili ya huyu mtunga mashairi mwendawazimu?

Ayah   37:37   الأية
بَلْ جَاءَ بِالْحَقِّ وَصَدَّقَ الْمُرْسَلِينَ
Swahili
 
Bali huyu amekuja kwa Haki, na amewasadikisha Mitume.

Ayah   37:38   الأية
إِنَّكُمْ لَذَائِقُو الْعَذَابِ الْأَلِيمِ
Swahili
 
Hakika nyinyi bila ya shaka mtaionja adhabu chungu.

Ayah   37:39   الأية
وَمَا تُجْزَوْنَ إِلَّا مَا كُنتُمْ تَعْمَلُونَ
Swahili
 
Wala hamlipwi ila hayo mliyo kuwa mkiyafanya.

Ayah   37:40   الأية
إِلَّا عِبَادَ اللَّهِ الْمُخْلَصِينَ
Swahili
 
Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio khitariwa.

Ayah   37:41   الأية
أُولَٰئِكَ لَهُمْ رِزْقٌ مَّعْلُومٌ
Swahili
 
Hao ndio watakao pata riziki maalumu,

Ayah   37:42   الأية
فَوَاكِهُ ۖ وَهُم مُّكْرَمُونَ
Swahili
 
Matunda, nao watahishimiwa.

Ayah   37:43   الأية
فِي جَنَّاتِ النَّعِيمِ
Swahili
 
Katika Bustani za neema.

Ayah   37:44   الأية
عَلَىٰ سُرُرٍ مُّتَقَابِلِينَ
Swahili
 
Wako juu ya viti wamekabiliana.

Ayah   37:45   الأية
يُطَافُ عَلَيْهِم بِكَأْسٍ مِّن مَّعِينٍ
Swahili
 
Wanazungushiwa kikombe chenye kinywaji cha chemchem

Ayah   37:46   الأية
بَيْضَاءَ لَذَّةٍ لِّلشَّارِبِينَ
Swahili
 
Kinywaji cheupe, kitamu kwa wanywao.

Ayah   37:47   الأية
لَا فِيهَا غَوْلٌ وَلَا هُمْ عَنْهَا يُنزَفُونَ
Swahili
 
Hakina madhara, wala hakiwaleweshi.

Ayah   37:48   الأية
وَعِندَهُمْ قَاصِرَاتُ الطَّرْفِ عِينٌ
Swahili
 
Na watakuwa nao wanawake wenye macho ya staha mazuri.

Ayah   37:49   الأية
كَأَنَّهُنَّ بَيْضٌ مَّكْنُونٌ
Swahili
 
Hao wanawake kama mayai yaliyo hifadhika.

Ayah   37:50   الأية
فَأَقْبَلَ بَعْضُهُمْ عَلَىٰ بَعْضٍ يَتَسَاءَلُونَ
Swahili
 
Waingie kuulizana wenyewe kwa wenyewe.

Ayah   37:51   الأية
قَالَ قَائِلٌ مِّنْهُمْ إِنِّي كَانَ لِي قَرِينٌ
Swahili
 
Aseme msemaji mmoja miongoni mwao: Hakika mimi nalikuwa na rafiki

Ayah   37:52   الأية
يَقُولُ أَإِنَّكَ لَمِنَ الْمُصَدِّقِينَ
Swahili
 
Aliye kuwa akinambia: Hivyo wewe ni katika wanao sadiki

Ayah   37:53   الأية
أَإِذَا مِتْنَا وَكُنَّا تُرَابًا وَعِظَامًا أَإِنَّا لَمَدِينُونَ
Swahili
 
Ati tukisha kufa tukawa udongo na mafupa, ndio tutalipwa na kuhisabiwa?

Ayah   37:54   الأية
قَالَ هَلْ أَنتُم مُّطَّلِعُونَ
Swahili
 
Atasema: Je! Nyie mnawaona?

Ayah   37:55   الأية
فَاطَّلَعَ فَرَآهُ فِي سَوَاءِ الْجَحِيمِ
Swahili
 
Basi atachungulia amwone katikati ya Jahannamu.

Ayah   37:56   الأية
قَالَ تَاللَّهِ إِن كِدتَّ لَتُرْدِينِ
Swahili
 
Atasema: Wallahi! Ulikaribia kunipoteza.

Ayah   37:57   الأية
وَلَوْلَا نِعْمَةُ رَبِّي لَكُنتُ مِنَ الْمُحْضَرِينَ
Swahili
 
Na lau kuwa si neema ya Mola wangu Mlezi bila ya shaka ningeli kuwa miongoni mwa walio hudhurishwa.

Ayah   37:58   الأية
أَفَمَا نَحْنُ بِمَيِّتِينَ
Swahili
 
Je! Sisi hatutakufa,

Ayah   37:59   الأية
إِلَّا مَوْتَتَنَا الْأُولَىٰ وَمَا نَحْنُ بِمُعَذَّبِينَ
Swahili
 
Isipo kuwa kifo chetu cha kwanza? Wala sisi hatutaadhibiwa.

Ayah   37:60   الأية
إِنَّ هَٰذَا لَهُوَ الْفَوْزُ الْعَظِيمُ
Swahili
 
Hakika huku bila ya shaka ndiko kufuzu kukubwa.

Ayah   37:61   الأية
لِمِثْلِ هَٰذَا فَلْيَعْمَلِ الْعَامِلُونَ
Swahili
 
Kwa mfano wa haya nawatende watendao.

Ayah   37:62   الأية
أَذَٰلِكَ خَيْرٌ نُّزُلًا أَمْ شَجَرَةُ الزَّقُّومِ
Swahili
 
Je! Kukaribishwa hivi si ndio bora, au mti wa Zaqqum?

Ayah   37:63   الأية
إِنَّا جَعَلْنَاهَا فِتْنَةً لِّلظَّالِمِينَ
Swahili
 
Hakika Sisi tumeufanya huo kuwa ni mateso kwa walio dhulumu.

Ayah   37:64   الأية
إِنَّهَا شَجَرَةٌ تَخْرُجُ فِي أَصْلِ الْجَحِيمِ
Swahili
 
Hakika huo ni mti unao toka katikati ya Jahannamu.

Ayah   37:65   الأية
طَلْعُهَا كَأَنَّهُ رُءُوسُ الشَّيَاطِينِ
Swahili
 
Mashada ya matunda yake kama kwamba vichwa vya mashet'ani.

Ayah   37:66   الأية
فَإِنَّهُمْ لَآكِلُونَ مِنْهَا فَمَالِئُونَ مِنْهَا الْبُطُونَ
Swahili
 
Basi hakika bila ya shaka hao watayala hayo, na wajaze matumbo.

Ayah   37:67   الأية
ثُمَّ إِنَّ لَهُمْ عَلَيْهَا لَشَوْبًا مِّنْ حَمِيمٍ
Swahili
 
Kisha juu yake wanyweshwe mchanganyo wa maji yamoto yaliyo chemka.

Ayah   37:68   الأية
ثُمَّ إِنَّ مَرْجِعَهُمْ لَإِلَى الْجَحِيمِ
Swahili
 
Kisha hakika marejeo yao bila ya shaka yatakuwa kwenye Jahannamu.

Ayah   37:69   الأية
إِنَّهُمْ أَلْفَوْا آبَاءَهُمْ ضَالِّينَ
Swahili
 
Hakika waliwakuta baba zao wamepotea.

Ayah   37:70   الأية
فَهُمْ عَلَىٰ آثَارِهِمْ يُهْرَعُونَ
Swahili
 
Na wao wakafanya haraka kufuata nyayo zao.

Ayah   37:71   الأية
وَلَقَدْ ضَلَّ قَبْلَهُمْ أَكْثَرُ الْأَوَّلِينَ
Swahili
 
Na bila ya shaka walikwisha potea kabla yao wengi wa watu wa zamani.

Ayah   37:72   الأية
وَلَقَدْ أَرْسَلْنَا فِيهِم مُّنذِرِينَ
Swahili
 
Na Sisi hakika tuliwapelekea waonyaji.

Ayah   37:73   الأية
فَانظُرْ كَيْفَ كَانَ عَاقِبَةُ الْمُنذَرِينَ
Swahili
 
Basi hebu angalia ulikuwaje mwisho wa walio onywa.

Ayah   37:74   الأية
إِلَّا عِبَادَ اللَّهِ الْمُخْلَصِينَ
Swahili
 
Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio khitariwa.

Ayah   37:75   الأية
وَلَقَدْ نَادَانَا نُوحٌ فَلَنِعْمَ الْمُجِيبُونَ
Swahili
 
Na hakika Nuhu alitwita, na Sisi ni bora wa waitikiaji.

Ayah   37:76   الأية
وَنَجَّيْنَاهُ وَأَهْلَهُ مِنَ الْكَرْبِ الْعَظِيمِ
Swahili
 
Na tulimwokoa yeye na ahali zake kutokana na msiba mkubwa.

Ayah   37:77   الأية
وَجَعَلْنَا ذُرِّيَّتَهُ هُمُ الْبَاقِينَ
Swahili
 
Na tuliwajaalia dhuriya zake ndio wenye kubakia.

Ayah   37:78   الأية
وَتَرَكْنَا عَلَيْهِ فِي الْآخِرِينَ
Swahili
 
Na tukamwachia (sifa njema) kwa walio kuja baadaye.

Ayah   37:79   الأية
سَلَامٌ عَلَىٰ نُوحٍ فِي الْعَالَمِينَ
Swahili
 
Iwe salama kwa Nuhu ulimwenguni kote!

Ayah   37:80   الأية
إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجْزِي الْمُحْسِنِينَ
Swahili
 
Kwa hakika hivi ndivyo tunavyo walipa wanao fanya mema.

Ayah   37:81   الأية
إِنَّهُ مِنْ عِبَادِنَا الْمُؤْمِنِينَ
Swahili
 
Hakika yeye ni katika waja wetu walio amini.

Ayah   37:82   الأية
ثُمَّ أَغْرَقْنَا الْآخَرِينَ
Swahili
 
Kisha tukawazamisha wale wengine.

Ayah   37:83   الأية
وَإِنَّ مِن شِيعَتِهِ لَإِبْرَاهِيمَ
Swahili
 
Na hakika Ibrahim alikuwa katika kundi lake,

Ayah   37:84   الأية
إِذْ جَاءَ رَبَّهُ بِقَلْبٍ سَلِيمٍ
Swahili
 
Alipo mjia Mola wake Mlezi kwa moyo mzima.

Ayah   37:85   الأية
إِذْ قَالَ لِأَبِيهِ وَقَوْمِهِ مَاذَا تَعْبُدُونَ
Swahili
 
Alimwambia baba yake na watu wake: Mnaabudu nini?

Ayah   37:86   الأية
أَئِفْكًا آلِهَةً دُونَ اللَّهِ تُرِيدُونَ
Swahili
 
Kwa kuzua tu mnataka miungu mingine badala ya Mwenyezi Mungu?

Ayah   37:87   الأية
فَمَا ظَنُّكُم بِرَبِّ الْعَالَمِينَ
Swahili
 
Mnamdhania nini Mola Mlezi wa walimwengu wote?

Ayah   37:88   الأية
فَنَظَرَ نَظْرَةً فِي النُّجُومِ
Swahili
 
Kisha akapiga jicho kutazama nyota.

Ayah   37:89   الأية
فَقَالَ إِنِّي سَقِيمٌ
Swahili
 
Akasema: Hakika mimi ni mgonjwa!

Ayah   37:90   الأية
فَتَوَلَّوْا عَنْهُ مُدْبِرِينَ
Swahili
 
Nao wakamwacha, wakampa kisogo.

Ayah   37:91   الأية
فَرَاغَ إِلَىٰ آلِهَتِهِمْ فَقَالَ أَلَا تَأْكُلُونَ
Swahili
 
Basi akaiendea miungu yao kwa siri, akaiambia: Mbona hamli?

Ayah   37:92   الأية
مَا لَكُمْ لَا تَنطِقُونَ
Swahili
 
Mna nini hata hamsemi?

Ayah   37:93   الأية
فَرَاغَ عَلَيْهِمْ ضَرْبًا بِالْيَمِينِ
Swahili
 
Kisha akaigeukia kuipiga kwa mkono wa kulia.

Ayah   37:94   الأية
فَأَقْبَلُوا إِلَيْهِ يَزِفُّونَ
Swahili
 
Basi wakamjia upesi upesi.

Ayah   37:95   الأية
قَالَ أَتَعْبُدُونَ مَا تَنْحِتُونَ
Swahili
 
Akasema: Hivyo mnaviabudu vitu mnavyo vichonga wenyewe?

Ayah   37:96   الأية
وَاللَّهُ خَلَقَكُمْ وَمَا تَعْمَلُونَ
Swahili
 
Na hali Mwenyezi Mungu ndiye aliye kuumbeni nyinyi na hivyo mnavyo vifanya!

Ayah   37:97   الأية
قَالُوا ابْنُوا لَهُ بُنْيَانًا فَأَلْقُوهُ فِي الْجَحِيمِ
Swahili
 
Wakasema: Mjengeeni jengo, na kisha mtupeni motoni humo!

Ayah   37:98   الأية
فَأَرَادُوا بِهِ كَيْدًا فَجَعَلْنَاهُمُ الْأَسْفَلِينَ
Swahili
 
Basi walitaka kumfanyia vitimbi, lakini tukawafanya wao ndio wa chini.

Ayah   37:99   الأية
وَقَالَ إِنِّي ذَاهِبٌ إِلَىٰ رَبِّي سَيَهْدِينِ
Swahili
 
Na akasema: Hakika mimi nahama, nakwenda kwa Mola wangu Mlezi; Yeye ataniongoa.

Ayah   37:100   الأية
رَبِّ هَبْ لِي مِنَ الصَّالِحِينَ
Swahili
 
Ewe Mola wangu Mlezi! Nitunukie aliye miongoni mwa watenda mema.

Ayah   37:101   الأية
فَبَشَّرْنَاهُ بِغُلَامٍ حَلِيمٍ
Swahili
 
Basi tukambashiria mwana aliye mpole.

Ayah   37:102   الأية
فَلَمَّا بَلَغَ مَعَهُ السَّعْيَ قَالَ يَا بُنَيَّ إِنِّي أَرَىٰ فِي الْمَنَامِ أَنِّي أَذْبَحُكَ فَانظُرْ مَاذَا تَرَىٰ ۚ قَالَ يَا أَبَتِ افْعَلْ مَا تُؤْمَرُ ۖ سَتَجِدُنِي إِن شَاءَ اللَّهُ مِنَ الصَّابِرِينَ
Swahili
 
Basi alipo fika makamo ya kwenda na kurudi pamoja naye, alimwambia: Ewe mwanangu! Hakika mimi nimeona usingizini kuwa ninakuchinja. Basi angalia wewe, waonaje? Akasema: Ewe baba yangu! Tenda unavyo amrishwa, utanikuta mimi, Inshallah, katika wanao subiri.

Ayah   37:103   الأية
فَلَمَّا أَسْلَمَا وَتَلَّهُ لِلْجَبِينِ
Swahili
 
Basi wote wawili walipo jisalimisha, na akamlaza juu ya kipaji.

Ayah   37:104   الأية
وَنَادَيْنَاهُ أَن يَا إِبْرَاهِيمُ
Swahili
 
Tulimwita: Ewe Ibrahim!

Ayah   37:105   الأية
قَدْ صَدَّقْتَ الرُّؤْيَا ۚ إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجْزِي الْمُحْسِنِينَ
Swahili
 
Umekwisha itimiliza ndoto. Hakika hivi ndivyo tunavyo walipa wanao tenda mema.

Ayah   37:106   الأية
إِنَّ هَٰذَا لَهُوَ الْبَلَاءُ الْمُبِينُ
Swahili
 
Hakika haya ni majaribio yaliyo dhaahiri.

Ayah   37:107   الأية
وَفَدَيْنَاهُ بِذِبْحٍ عَظِيمٍ
Swahili
 
Basi tukamtolea fidia kwa dhabihu mtukufu.

Ayah   37:108   الأية
وَتَرَكْنَا عَلَيْهِ فِي الْآخِرِينَ
Swahili
 
Na tukamwachia (sifa njema) kwa watu walio kuja baadaye.

Ayah   37:109   الأية
سَلَامٌ عَلَىٰ إِبْرَاهِيمَ
Swahili
 
Iwe salama kwa Ibrahim!

Ayah   37:110   الأية
كَذَٰلِكَ نَجْزِي الْمُحْسِنِينَ
Swahili
 
Hivi ndivyo tunavyo walipa wanao fanya mema.

Ayah   37:111   الأية
إِنَّهُ مِنْ عِبَادِنَا الْمُؤْمِنِينَ
Swahili
 
Hakika yeye ni katika waja wetu walio amini.

Ayah   37:112   الأية
وَبَشَّرْنَاهُ بِإِسْحَاقَ نَبِيًّا مِّنَ الصَّالِحِينَ
Swahili
 
Na tukambashiria kuzaliwa Is-haqa, naye ni Nabii miongoni mwa watu wema.

Ayah   37:113   الأية
وَبَارَكْنَا عَلَيْهِ وَعَلَىٰ إِسْحَاقَ ۚ وَمِن ذُرِّيَّتِهِمَا مُحْسِنٌ وَظَالِمٌ لِّنَفْسِهِ مُبِينٌ
Swahili
 
Na tukambarikia yeye na Is-haqa. Na miongoni mwa dhuriya zao walitokea wema na wenye kudhulumu nafsi zao waziwazi.

Ayah   37:114   الأية
وَلَقَدْ مَنَنَّا عَلَىٰ مُوسَىٰ وَهَارُونَ
Swahili
 
Na kwa hakika tuliwafanyia hisani Musa na Haruni.

Ayah   37:115   الأية
وَنَجَّيْنَاهُمَا وَقَوْمَهُمَا مِنَ الْكَرْبِ الْعَظِيمِ
Swahili
 
Na tukawaokoa wao na watu wao kutokana na dhiki kubwa.

Ayah   37:116   الأية
وَنَصَرْنَاهُمْ فَكَانُوا هُمُ الْغَالِبِينَ
Swahili
 
Na tukawanusuru; na wakawa wao ndio wenye kushinda.

Ayah   37:117   الأية
وَآتَيْنَاهُمَا الْكِتَابَ الْمُسْتَبِينَ
Swahili
 
Na tukawapa wawili hao Kitabu kinacho bainisha.

Ayah   37:118   الأية
وَهَدَيْنَاهُمَا الصِّرَاطَ الْمُسْتَقِيمَ
Swahili
 
Na tukawaongoa kwenye Njia Iliyo Nyooka.

Ayah   37:119   الأية
وَتَرَكْنَا عَلَيْهِمَا فِي الْآخِرِينَ
Swahili
 
Na tukawaachia (sifa njema) katika watu walio kuja baadaye.

Ayah   37:120   الأية
سَلَامٌ عَلَىٰ مُوسَىٰ وَهَارُونَ
Swahili
 
Iwe salama kwa Musa na Haruni!

Ayah   37:121   الأية
إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجْزِي الْمُحْسِنِينَ
Swahili
 
Hakika hivyo ndivyo tunavyo walipa walio wema.

Ayah   37:122   الأية
إِنَّهُمَا مِنْ عِبَادِنَا الْمُؤْمِنِينَ
Swahili
 
Hakika wawili hao ni katika waja wetu walio amini.

Ayah   37:123   الأية
وَإِنَّ إِلْيَاسَ لَمِنَ الْمُرْسَلِينَ
Swahili
 
Na hakika Ilyas bila ya shaka alikuwa miongoni mwa Mitume.

Ayah   37:124   الأية
إِذْ قَالَ لِقَوْمِهِ أَلَا تَتَّقُونَ
Swahili
 
Alipo waambia watu wake: Hamwogopi?

Ayah   37:125   الأية
أَتَدْعُونَ بَعْلًا وَتَذَرُونَ أَحْسَنَ الْخَالِقِينَ
Swahili
 
Mnamwomba Baa'li na mnamwacha Mbora wa waumbaji,

Ayah   37:126   الأية
اللَّهَ رَبَّكُمْ وَرَبَّ آبَائِكُمُ الْأَوَّلِينَ
Swahili
 
Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wenu na Mola Mlezi wa baba zenu wa zamani?

Ayah   37:127   الأية
فَكَذَّبُوهُ فَإِنَّهُمْ لَمُحْضَرُونَ
Swahili
 
Wakamkadhibisha. Basi kwa hakika watahudhurishwa;

Ayah   37:128   الأية
إِلَّا عِبَادَ اللَّهِ الْمُخْلَصِينَ
Swahili
 
Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio safishwa.

Ayah   37:129   الأية
وَتَرَكْنَا عَلَيْهِ فِي الْآخِرِينَ
Swahili
 
Na tumemwachia (sifa nzuri) kwa walio kuja baadaye.

Ayah   37:130   الأية
سَلَامٌ عَلَىٰ إِلْ يَاسِينَ
Swahili
 
Iwe salama kwa Ilyas.

Ayah   37:131   الأية
إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجْزِي الْمُحْسِنِينَ
Swahili
 
Hakika hivyo ndivyo tunavyo walipa walio wema.

Ayah   37:132   الأية
إِنَّهُ مِنْ عِبَادِنَا الْمُؤْمِنِينَ
Swahili
 
Hakika yeye ni katika waja wetu walio amini.

Ayah   37:133   الأية
وَإِنَّ لُوطًا لَّمِنَ الْمُرْسَلِينَ
Swahili
 
Na hakika Lut'i bila ya shaka ni miongoni mwa Mitume.

Ayah   37:134   الأية
إِذْ نَجَّيْنَاهُ وَأَهْلَهُ أَجْمَعِينَ
Swahili
 
Tulipo mwokoa yeye na ahali zake wote,

Ayah   37:135   الأية
إِلَّا عَجُوزًا فِي الْغَابِرِينَ
Swahili
 
Isipo kuwa mwanamke mkongwe katika wale walio bakia nyuma.

Ayah   37:136   الأية
ثُمَّ دَمَّرْنَا الْآخَرِينَ
Swahili
 
Kisha tukawaangamiza wale wengineo.

Ayah   37:137   الأية
وَإِنَّكُمْ لَتَمُرُّونَ عَلَيْهِم مُّصْبِحِينَ
Swahili
 
Na hakika nyinyi mnawapitia wakati wa asubuhi,

Ayah   37:138   الأية
وَبِاللَّيْلِ ۗ أَفَلَا تَعْقِلُونَ
Swahili
 
Na usiku. Basi je! Hamyatii akilini?

Ayah   37:139   الأية
وَإِنَّ يُونُسَ لَمِنَ الْمُرْسَلِينَ
Swahili
 
Na hakika Yunus alikuwa miongoni mwa Mitume.

Ayah   37:140   الأية
إِذْ أَبَقَ إِلَى الْفُلْكِ الْمَشْحُونِ
Swahili
 
Alipo kimbia katika jahazi lilio sheheni.

Ayah   37:141   الأية
فَسَاهَمَ فَكَانَ مِنَ الْمُدْحَضِينَ
Swahili
 
Akaingia katika kupigiwa kura, na akawa katika walio shindwa.

Ayah   37:142   الأية
فَالْتَقَمَهُ الْحُوتُ وَهُوَ مُلِيمٌ
Swahili
 
Samaki akammeza hali ya kuwa ni mwenye kulaumiwa.

Ayah   37:143   الأية
فَلَوْلَا أَنَّهُ كَانَ مِنَ الْمُسَبِّحِينَ
Swahili
 
Na ingeli kuwa hakuwa katika wanao mtakasa Mwenyezi Mungu,

Ayah   37:144   الأية
لَلَبِثَ فِي بَطْنِهِ إِلَىٰ يَوْمِ يُبْعَثُونَ
Swahili
 
Bila ya shaka angeli kaa ndani yake mpaka siku ya kufufuliwa.

Ayah   37:145   الأية
فَنَبَذْنَاهُ بِالْعَرَاءِ وَهُوَ سَقِيمٌ
Swahili
 
Lakini tulimtupa ufukweni patupu, hali yu mgonjwa.

Ayah   37:146   الأية
وَأَنبَتْنَا عَلَيْهِ شَجَرَةً مِّن يَقْطِينٍ
Swahili
 
Na tukauotesha juu yake mmea wa kabila ya mung'unye.

Ayah   37:147   الأية
وَأَرْسَلْنَاهُ إِلَىٰ مِائَةِ أَلْفٍ أَوْ يَزِيدُونَ
Swahili
 
Na tulimtuma kwa watu laki moja au zaidi.

Ayah   37:148   الأية
فَآمَنُوا فَمَتَّعْنَاهُمْ إِلَىٰ حِينٍ
Swahili
 
Basi wakaamini, na tukawastarehesha kwa muda.

Ayah   37:149   الأية
فَاسْتَفْتِهِمْ أَلِرَبِّكَ الْبَنَاتُ وَلَهُمُ الْبَنُونَ
Swahili
 
Basi waulize: Ati Mola wako Mlezi ndiye mwenye watoto wa kike, na wao wanao watoto wa kiume?

Ayah   37:150   الأية
أَمْ خَلَقْنَا الْمَلَائِكَةَ إِنَاثًا وَهُمْ شَاهِدُونَ
Swahili
 
Au tumewaumba Malaika kuwa ni wanawake, na wao wakashuhudia?

Ayah   37:151   الأية
أَلَا إِنَّهُم مِّنْ إِفْكِهِمْ لَيَقُولُونَ
Swahili
 
Ati ni kwa uzushi wao ndio wanasema:

Ayah   37:152   الأية
وَلَدَ اللَّهُ وَإِنَّهُمْ لَكَاذِبُونَ
Swahili
 
Mwenyezi Mungu amezaa! Ama hakika bila ya shaka hao ni waongo!

Ayah   37:153   الأية
أَصْطَفَى الْبَنَاتِ عَلَى الْبَنِينَ
Swahili
 
Ati amekhiari watoto wa kike kuliko wanaume?

Ayah   37:154   الأية
مَا لَكُمْ كَيْفَ تَحْكُمُونَ
Swahili
 
Mna nini? Mnahukumu vipi nyinyi?

Ayah   37:155   الأية
أَفَلَا تَذَكَّرُونَ
Swahili
 
Hamkumbuki?

Ayah   37:156   الأية
أَمْ لَكُمْ سُلْطَانٌ مُّبِينٌ
Swahili
 
Au mnayo hoja iliyo wazi?

Ayah   37:157   الأية
فَأْتُوا بِكِتَابِكُمْ إِن كُنتُمْ صَادِقِينَ
Swahili
 
Basi leteni Kitabu chenu kama mnasema kweli.

Ayah   37:158   الأية
وَجَعَلُوا بَيْنَهُ وَبَيْنَ الْجِنَّةِ نَسَبًا ۚ وَلَقَدْ عَلِمَتِ الْجِنَّةُ إِنَّهُمْ لَمُحْضَرُونَ
Swahili
 
Na wameweka makhusiano ya nasaba baina yake na majini; na majini wamekwisha jua bila ya shaka kuwa wao watahudhurishwa.

Ayah   37:159   الأية
سُبْحَانَ اللَّهِ عَمَّا يَصِفُونَ
Swahili
 
Subhana 'Llah Ametakasika Mwenyezi Mungu na hayo wanayo msingizia.

Ayah   37:160   الأية
إِلَّا عِبَادَ اللَّهِ الْمُخْلَصِينَ
Swahili
 
Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio safishwa.

Ayah   37:161   الأية
فَإِنَّكُمْ وَمَا تَعْبُدُونَ
Swahili
 
Basi hakika nyinyi na mnao waabudu

Ayah   37:162   الأية
مَا أَنتُمْ عَلَيْهِ بِفَاتِنِينَ
Swahili
 
Hamwezi kuwapoteza

Ayah   37:163   الأية
إِلَّا مَنْ هُوَ صَالِ الْجَحِيمِ
Swahili
 
Isipo kuwa yule atakaye ingia Motoni.

Ayah   37:164   الأية
وَمَا مِنَّا إِلَّا لَهُ مَقَامٌ مَّعْلُومٌ
Swahili
 
Na hapana katika sisi ila anapo mahali pake maalumu.

Ayah   37:165   الأية
وَإِنَّا لَنَحْنُ الصَّافُّونَ
Swahili
 
Na hakika bila ya shaka sisi ndio wajipangao safu.

Ayah   37:166   الأية
وَإِنَّا لَنَحْنُ الْمُسَبِّحُونَ
Swahili
 
Na hakika sisi ndio wenye kusabihi kutakasa.

Ayah   37:167   الأية
وَإِن كَانُوا لَيَقُولُونَ
Swahili
 
Na walikuwapo walio kuwa wakisema:

Ayah   37:168   الأية
لَوْ أَنَّ عِندَنَا ذِكْرًا مِّنَ الْأَوَّلِينَ
Swahili
 
Tungeli kuwa na Ukumbusho kama wa watu wa zamani,

Ayah   37:169   الأية
لَكُنَّا عِبَادَ اللَّهِ الْمُخْلَصِينَ
Swahili
 
Bila ya shaka tungeli kuwa ni waja wa Mwenyezi Mungu wenye ikhlasi.

Ayah   37:170   الأية
فَكَفَرُوا بِهِ ۖ فَسَوْفَ يَعْلَمُونَ
Swahili
 
Lakini waliukataa. Basi watakuja jua.

Ayah   37:171   الأية
وَلَقَدْ سَبَقَتْ كَلِمَتُنَا لِعِبَادِنَا الْمُرْسَلِينَ
Swahili
 
Na bila ya shaka neno letu lilikwisha tangulia kwa waja wetu walio tumwa.

Ayah   37:172   الأية
إِنَّهُمْ لَهُمُ الْمَنصُورُونَ
Swahili
 
Ya kuwa wao bila ya shaka ndio watakao nusuriwa.

Ayah   37:173   الأية
وَإِنَّ جُندَنَا لَهُمُ الْغَالِبُونَ
Swahili
 
Na kwamba jeshi letu ndilo litakalo shinda.

Ayah   37:174   الأية
فَتَوَلَّ عَنْهُمْ حَتَّىٰ حِينٍ
Swahili
 
Basi waachilie mbali kwa muda.

Ayah   37:175   الأية
وَأَبْصِرْهُمْ فَسَوْفَ يُبْصِرُونَ
Swahili
 
Na watazame, nao wataona.

Ayah   37:176   الأية
أَفَبِعَذَابِنَا يَسْتَعْجِلُونَ
Swahili
 
Je! Wanaihimiza adhabu yetu?

Ayah   37:177   الأية
فَإِذَا نَزَلَ بِسَاحَتِهِمْ فَسَاءَ صَبَاحُ الْمُنذَرِينَ
Swahili
 
Basi itakapo shuka uwanjani kwao, itakuwa asubuhi mbaya kwa walio onywa.

Ayah   37:178   الأية
وَتَوَلَّ عَنْهُمْ حَتَّىٰ حِينٍ
Swahili
 
Na waache kwa muda.

Ayah   37:179   الأية
وَأَبْصِرْ فَسَوْفَ يُبْصِرُونَ
Swahili
 
Na tazama, na wao wataona.

Ayah   37:180   الأية
سُبْحَانَ رَبِّكَ رَبِّ الْعِزَّةِ عَمَّا يَصِفُونَ
Swahili
 
Subhana Rabbi'l'Izzat Ametakasika Mola Mlezi Mwenye enzi na yale wanayo mzulia.

Ayah   37:181   الأية
وَسَلَامٌ عَلَى الْمُرْسَلِينَ
Swahili
 
Na Salamu juu ya Mitume.

Ayah   37:182   الأية
وَالْحَمْدُ لِلَّهِ رَبِّ الْعَالَمِينَ
Swahili
 
Na sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu Mola Mlezi wa walimwengu wote.
 


© EsinIslam.Com Designed & produced by The Awqaf London. Please pray for us