First Ayah 1 الأية الأوليبِسْم ِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ
وَالصَّافَّاتِ صَفًّا
Swahili
Naapa kwa wanao jipanga kwa safu.
|
Ayah 37:2 الأية
فَالزَّاجِرَاتِ زَجْرًا
Swahili
Na kwa wenye kukataza mabaya.
|
Ayah 37:3 الأية
فَالتَّالِيَاتِ ذِكْرًا
Swahili
Na kwa wenye kusoma Ukumbusho.
|
Ayah 37:4 الأية
إِنَّ إِلَٰهَكُمْ لَوَاحِدٌ
Swahili
Hakika Mungu wenu bila ya shaka ni Mmoja.
|
Ayah 37:5 الأية
رَّبُّ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَمَا بَيْنَهُمَا وَرَبُّ الْمَشَارِقِ
Swahili
Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, na yaliyomo kati yao, na ni Mola Mlezi wa
mashariki zote.
|
Ayah 37:6 الأية
إِنَّا زَيَّنَّا السَّمَاءَ الدُّنْيَا بِزِينَةٍ الْكَوَاكِبِ
Swahili
Hakika Sisi tumeipamba mbingu ya karibu kwa pambo la nyota.
|
Ayah 37:7 الأية
وَحِفْظًا مِّن كُلِّ شَيْطَانٍ مَّارِدٍ
Swahili
Na kulinda na kila shet'ani a'si.
|
Ayah 37:8 الأية
لَّا يَسَّمَّعُونَ إِلَى الْمَلَإِ الْأَعْلَىٰ وَيُقْذَفُونَ مِن كُلِّ جَانِبٍ
Swahili
Wasiweze kuwasikiliza viumbe watukufu. Na wanafukuzwa huko kila upande.
|
Ayah 37:9 الأية
دُحُورًا ۖ وَلَهُمْ عَذَابٌ وَاصِبٌ
Swahili
Wakifurushwa. Na wanayo adhabu ya kudumu.
|
Ayah 37:10 الأية
إِلَّا مَنْ خَطِفَ الْخَطْفَةَ فَأَتْبَعَهُ شِهَابٌ ثَاقِبٌ
Swahili
Isipo kuwa anaye nyakua kitu kidogo, na mara humfwatia kimondo kinacho ng'ara.
|
Ayah 37:11 الأية
فَاسْتَفْتِهِمْ أَهُمْ أَشَدُّ خَلْقًا أَم مَّنْ خَلَقْنَا ۚ إِنَّا خَلَقْنَاهُم
مِّن طِينٍ لَّازِبٍ
Swahili
Hebu waulize: Je! Wao ni wenye umbo gumu zaidi au hao wengine tulio waumba.
Hakika Sisi tuliwaumba wao kwa udongo unao nata.
|
Ayah 37:12 الأية
بَلْ عَجِبْتَ وَيَسْخَرُونَ
Swahili
Bali unastaajabu, na wao wanafanya maskhara.
|
Ayah 37:13 الأية
وَإِذَا ذُكِّرُوا لَا يَذْكُرُونَ
Swahili
Na wanapo kumbushwa hawakumbuki.
|
Ayah 37:14 الأية
وَإِذَا رَأَوْا آيَةً يَسْتَسْخِرُونَ
Swahili
Na wanapo ona Ishara, wanafanya maskhara.
|
Ayah 37:15 الأية
وَقَالُوا إِنْ هَٰذَا إِلَّا سِحْرٌ مُّبِينٌ
Swahili
Na husema: Haya si chochote ila ni uchawi tu ulio dhaahiri.
|
Ayah 37:16 الأية
أَإِذَا مِتْنَا وَكُنَّا تُرَابًا وَعِظَامًا أَإِنَّا لَمَبْعُوثُونَ
Swahili
Ati tukisha kufa na tukawa udongo na mifupa ndio kweli tutafufuliwa?
|
Ayah 37:17 الأية
أَوَآبَاؤُنَا الْأَوَّلُونَ
Swahili
Hata baba zetu wa zamani?
|
Ayah 37:18 الأية
قُلْ نَعَمْ وَأَنتُمْ دَاخِرُونَ
Swahili
Sema: Naam! Hali nanyi ni madhalili.
|
Ayah 37:19 الأية
فَإِنَّمَا هِيَ زَجْرَةٌ وَاحِدَةٌ فَإِذَا هُمْ يَنظُرُونَ
Swahili
Huko utapigwa ukelele mmoja tu! Na hapo ndio wataona!
|
Ayah 37:20 الأية
وَقَالُوا يَا وَيْلَنَا هَٰذَا يَوْمُ الدِّينِ
Swahili
Watasema: Ole wetu! Hii ndiyo Siku ya Malipo.
|
Ayah 37:21 الأية
هَٰذَا يَوْمُ الْفَصْلِ الَّذِي كُنتُم بِهِ تُكَذِّبُونَ
Swahili
Hii ndiyo Siku ya Hukumu mliyo kuwa mkiikadhibisha.
|
Ayah 37:22 الأية
احْشُرُوا الَّذِينَ ظَلَمُوا وَأَزْوَاجَهُمْ وَمَا كَانُوا يَعْبُدُونَ
Swahili
Wakusanyeni walio dhulumu, na wake zao, na hao walio kuwa wakiwaabudu -
|
Ayah 37:23 الأية
مِن دُونِ اللَّهِ فَاهْدُوهُمْ إِلَىٰ صِرَاطِ الْجَحِيمِ
Swahili
Badala ya Mwenyezi Mungu. Waongozeni njia ya Jahannamu!
|
Ayah 37:24 الأية
وَقِفُوهُمْ ۖ إِنَّهُم مَّسْئُولُونَ
Swahili
Na wasimamisheni. Hakika hao watasailiwa:
|
Ayah 37:25 الأية
مَا لَكُمْ لَا تَنَاصَرُونَ
Swahili
Mna nini? Mbona hamsaidiani?
|
Ayah 37:26 الأية
بَلْ هُمُ الْيَوْمَ مُسْتَسْلِمُونَ
Swahili
Bali hii leo, watasalimu amri.
|
Ayah 37:27 الأية
وَأَقْبَلَ بَعْضُهُمْ عَلَىٰ بَعْضٍ يَتَسَاءَلُونَ
Swahili
Watakabiliana wao kwa wao kuulizana.
|
Ayah 37:28 الأية
قَالُوا إِنَّكُمْ كُنتُمْ تَأْتُونَنَا عَنِ الْيَمِينِ
Swahili
Watasema: Kwa hakika nyinyi mlikuwa mkitujia upande wa kulia.
|
Ayah 37:29 الأية
قَالُوا بَل لَّمْ تَكُونُوا مُؤْمِنِينَ
Swahili
Watasema (wakubwa): Bali nyinyi wenyewe hamkuwa Waumini.
|
Ayah 37:30 الأية
وَمَا كَانَ لَنَا عَلَيْكُم مِّن سُلْطَانٍ ۖ بَلْ كُنتُمْ قَوْمًا طَاغِينَ
Swahili
Sisi hatukuwa na mamlaka juu yenu, bali nyinyi wenyewe mlikuwa wapotovu.
|
Ayah 37:31 الأية
فَحَقَّ عَلَيْنَا قَوْلُ رَبِّنَا ۖ إِنَّا لَذَائِقُونَ
Swahili
Basi hukumu ya Mola wetu Mlezi imekwisha tuthibitikia. Hakika bila ya shaka
tutaonja tu adhabu.
|
Ayah 37:32 الأية
فَأَغْوَيْنَاكُمْ إِنَّا كُنَّا غَاوِينَ
Swahili
Tulikupotezeni kwa sababu sisi wenyewe tulikuwa wapotovu.
|
Ayah 37:33 الأية
فَإِنَّهُمْ يَوْمَئِذٍ فِي الْعَذَابِ مُشْتَرِكُونَ
Swahili
Basi wao kwa hakika siku hiyo watashirikiana katika adhabu pamoja.
|
Ayah 37:34 الأية
إِنَّا كَذَٰلِكَ نَفْعَلُ بِالْمُجْرِمِينَ
Swahili
Hivyo ndivyo tutakavyo wafanyia wakosefu.
|
Ayah 37:35 الأية
إِنَّهُمْ كَانُوا إِذَا قِيلَ لَهُمْ لَا إِلَٰهَ إِلَّا اللَّهُ يَسْتَكْبِرُونَ
Swahili
Wao walipo kuwa wakiambiwa La ilaha illa 'Llahu Hapana mungu ila Mwenyezi Mungu
tu, wakijivuna.
|
Ayah 37:36 الأية
وَيَقُولُونَ أَئِنَّا لَتَارِكُو آلِهَتِنَا لِشَاعِرٍ مَّجْنُونٍ
Swahili
Na wakisema: Hivyo sisi tuiache miungu yetu kwa ajili ya huyu mtunga mashairi
mwendawazimu?
|
Ayah 37:37 الأية
بَلْ جَاءَ بِالْحَقِّ وَصَدَّقَ الْمُرْسَلِينَ
Swahili
Bali huyu amekuja kwa Haki, na amewasadikisha Mitume.
|
Ayah 37:38 الأية
إِنَّكُمْ لَذَائِقُو الْعَذَابِ الْأَلِيمِ
Swahili
Hakika nyinyi bila ya shaka mtaionja adhabu chungu.
|
Ayah 37:39 الأية
وَمَا تُجْزَوْنَ إِلَّا مَا كُنتُمْ تَعْمَلُونَ
Swahili
Wala hamlipwi ila hayo mliyo kuwa mkiyafanya.
|
Ayah 37:40 الأية
إِلَّا عِبَادَ اللَّهِ الْمُخْلَصِينَ
Swahili
Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio khitariwa.
|
Ayah 37:41 الأية
أُولَٰئِكَ لَهُمْ رِزْقٌ مَّعْلُومٌ
Swahili
Hao ndio watakao pata riziki maalumu,
|
Ayah 37:42 الأية
فَوَاكِهُ ۖ وَهُم مُّكْرَمُونَ
Swahili
Matunda, nao watahishimiwa.
|
Ayah 37:43 الأية
فِي جَنَّاتِ النَّعِيمِ
Swahili
Katika Bustani za neema.
|
Ayah 37:44 الأية
عَلَىٰ سُرُرٍ مُّتَقَابِلِينَ
Swahili
Wako juu ya viti wamekabiliana.
|
Ayah 37:45 الأية
يُطَافُ عَلَيْهِم بِكَأْسٍ مِّن مَّعِينٍ
Swahili
Wanazungushiwa kikombe chenye kinywaji cha chemchem
|
Ayah 37:46 الأية
بَيْضَاءَ لَذَّةٍ لِّلشَّارِبِينَ
Swahili
Kinywaji cheupe, kitamu kwa wanywao.
|
Ayah 37:47 الأية
لَا فِيهَا غَوْلٌ وَلَا هُمْ عَنْهَا يُنزَفُونَ
Swahili
Hakina madhara, wala hakiwaleweshi.
|
Ayah 37:48 الأية
وَعِندَهُمْ قَاصِرَاتُ الطَّرْفِ عِينٌ
Swahili
Na watakuwa nao wanawake wenye macho ya staha mazuri.
|
Ayah 37:49 الأية
كَأَنَّهُنَّ بَيْضٌ مَّكْنُونٌ
Swahili
Hao wanawake kama mayai yaliyo hifadhika.
|
Ayah 37:50 الأية
فَأَقْبَلَ بَعْضُهُمْ عَلَىٰ بَعْضٍ يَتَسَاءَلُونَ
Swahili
Waingie kuulizana wenyewe kwa wenyewe.
|
Ayah 37:51 الأية
قَالَ قَائِلٌ مِّنْهُمْ إِنِّي كَانَ لِي قَرِينٌ
Swahili
Aseme msemaji mmoja miongoni mwao: Hakika mimi nalikuwa na rafiki
|
Ayah 37:52 الأية
يَقُولُ أَإِنَّكَ لَمِنَ الْمُصَدِّقِينَ
Swahili
Aliye kuwa akinambia: Hivyo wewe ni katika wanao sadiki
|
Ayah 37:53 الأية
أَإِذَا مِتْنَا وَكُنَّا تُرَابًا وَعِظَامًا أَإِنَّا لَمَدِينُونَ
Swahili
Ati tukisha kufa tukawa udongo na mafupa, ndio tutalipwa na kuhisabiwa?
|
Ayah 37:54 الأية
قَالَ هَلْ أَنتُم مُّطَّلِعُونَ
Swahili
Atasema: Je! Nyie mnawaona?
|
Ayah 37:55 الأية
فَاطَّلَعَ فَرَآهُ فِي سَوَاءِ الْجَحِيمِ
Swahili
Basi atachungulia amwone katikati ya Jahannamu.
|
Ayah 37:56 الأية
قَالَ تَاللَّهِ إِن كِدتَّ لَتُرْدِينِ
Swahili
Atasema: Wallahi! Ulikaribia kunipoteza.
|
Ayah 37:57 الأية
وَلَوْلَا نِعْمَةُ رَبِّي لَكُنتُ مِنَ الْمُحْضَرِينَ
Swahili
Na lau kuwa si neema ya Mola wangu Mlezi bila ya shaka ningeli kuwa miongoni mwa
walio hudhurishwa.
|
Ayah 37:58 الأية
أَفَمَا نَحْنُ بِمَيِّتِينَ
Swahili
Je! Sisi hatutakufa,
|
Ayah 37:59 الأية
إِلَّا مَوْتَتَنَا الْأُولَىٰ وَمَا نَحْنُ بِمُعَذَّبِينَ
Swahili
Isipo kuwa kifo chetu cha kwanza? Wala sisi hatutaadhibiwa.
|
Ayah 37:60 الأية
إِنَّ هَٰذَا لَهُوَ الْفَوْزُ الْعَظِيمُ
Swahili
Hakika huku bila ya shaka ndiko kufuzu kukubwa.
|
Ayah 37:61 الأية
لِمِثْلِ هَٰذَا فَلْيَعْمَلِ الْعَامِلُونَ
Swahili
Kwa mfano wa haya nawatende watendao.
|
Ayah 37:62 الأية
أَذَٰلِكَ خَيْرٌ نُّزُلًا أَمْ شَجَرَةُ الزَّقُّومِ
Swahili
Je! Kukaribishwa hivi si ndio bora, au mti wa Zaqqum?
|
Ayah 37:63 الأية
إِنَّا جَعَلْنَاهَا فِتْنَةً لِّلظَّالِمِينَ
Swahili
Hakika Sisi tumeufanya huo kuwa ni mateso kwa walio dhulumu.
|
Ayah 37:64 الأية
إِنَّهَا شَجَرَةٌ تَخْرُجُ فِي أَصْلِ الْجَحِيمِ
Swahili
Hakika huo ni mti unao toka katikati ya Jahannamu.
|
Ayah 37:65 الأية
طَلْعُهَا كَأَنَّهُ رُءُوسُ الشَّيَاطِينِ
Swahili
Mashada ya matunda yake kama kwamba vichwa vya mashet'ani.
|
Ayah 37:66 الأية
فَإِنَّهُمْ لَآكِلُونَ مِنْهَا فَمَالِئُونَ مِنْهَا الْبُطُونَ
Swahili
Basi hakika bila ya shaka hao watayala hayo, na wajaze matumbo.
|
Ayah 37:67 الأية
ثُمَّ إِنَّ لَهُمْ عَلَيْهَا لَشَوْبًا مِّنْ حَمِيمٍ
Swahili
Kisha juu yake wanyweshwe mchanganyo wa maji yamoto yaliyo chemka.
|
Ayah 37:68 الأية
ثُمَّ إِنَّ مَرْجِعَهُمْ لَإِلَى الْجَحِيمِ
Swahili
Kisha hakika marejeo yao bila ya shaka yatakuwa kwenye Jahannamu.
|
Ayah 37:69 الأية
إِنَّهُمْ أَلْفَوْا آبَاءَهُمْ ضَالِّينَ
Swahili
Hakika waliwakuta baba zao wamepotea.
|
Ayah 37:70 الأية
فَهُمْ عَلَىٰ آثَارِهِمْ يُهْرَعُونَ
Swahili
Na wao wakafanya haraka kufuata nyayo zao.
|
Ayah 37:71 الأية
وَلَقَدْ ضَلَّ قَبْلَهُمْ أَكْثَرُ الْأَوَّلِينَ
Swahili
Na bila ya shaka walikwisha potea kabla yao wengi wa watu wa zamani.
|
Ayah 37:72 الأية
وَلَقَدْ أَرْسَلْنَا فِيهِم مُّنذِرِينَ
Swahili
Na Sisi hakika tuliwapelekea waonyaji.
|
Ayah 37:73 الأية
فَانظُرْ كَيْفَ كَانَ عَاقِبَةُ الْمُنذَرِينَ
Swahili
Basi hebu angalia ulikuwaje mwisho wa walio onywa.
|
Ayah 37:74 الأية
إِلَّا عِبَادَ اللَّهِ الْمُخْلَصِينَ
Swahili
Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio khitariwa.
|
Ayah 37:75 الأية
وَلَقَدْ نَادَانَا نُوحٌ فَلَنِعْمَ الْمُجِيبُونَ
Swahili
Na hakika Nuhu alitwita, na Sisi ni bora wa waitikiaji.
|
Ayah 37:76 الأية
وَنَجَّيْنَاهُ وَأَهْلَهُ مِنَ الْكَرْبِ الْعَظِيمِ
Swahili
Na tulimwokoa yeye na ahali zake kutokana na msiba mkubwa.
|
Ayah 37:77 الأية
وَجَعَلْنَا ذُرِّيَّتَهُ هُمُ الْبَاقِينَ
Swahili
Na tuliwajaalia dhuriya zake ndio wenye kubakia.
|
Ayah 37:78 الأية
وَتَرَكْنَا عَلَيْهِ فِي الْآخِرِينَ
Swahili
Na tukamwachia (sifa njema) kwa walio kuja baadaye.
|
Ayah 37:79 الأية
سَلَامٌ عَلَىٰ نُوحٍ فِي الْعَالَمِينَ
Swahili
Iwe salama kwa Nuhu ulimwenguni kote!
|
Ayah 37:80 الأية
إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجْزِي الْمُحْسِنِينَ
Swahili
Kwa hakika hivi ndivyo tunavyo walipa wanao fanya mema.
|
Ayah 37:81 الأية
إِنَّهُ مِنْ عِبَادِنَا الْمُؤْمِنِينَ
Swahili
Hakika yeye ni katika waja wetu walio amini.
|
Ayah 37:82 الأية
ثُمَّ أَغْرَقْنَا الْآخَرِينَ
Swahili
Kisha tukawazamisha wale wengine.
|
Ayah 37:83 الأية
وَإِنَّ مِن شِيعَتِهِ لَإِبْرَاهِيمَ
Swahili
Na hakika Ibrahim alikuwa katika kundi lake,
|
Ayah 37:84 الأية
إِذْ جَاءَ رَبَّهُ بِقَلْبٍ سَلِيمٍ
Swahili
Alipo mjia Mola wake Mlezi kwa moyo mzima.
|
Ayah 37:85 الأية
إِذْ قَالَ لِأَبِيهِ وَقَوْمِهِ مَاذَا تَعْبُدُونَ
Swahili
Alimwambia baba yake na watu wake: Mnaabudu nini?
|
Ayah 37:86 الأية
أَئِفْكًا آلِهَةً دُونَ اللَّهِ تُرِيدُونَ
Swahili
Kwa kuzua tu mnataka miungu mingine badala ya Mwenyezi Mungu?
|
Ayah 37:87 الأية
فَمَا ظَنُّكُم بِرَبِّ الْعَالَمِينَ
Swahili
Mnamdhania nini Mola Mlezi wa walimwengu wote?
|
Ayah 37:88 الأية
فَنَظَرَ نَظْرَةً فِي النُّجُومِ
Swahili
Kisha akapiga jicho kutazama nyota.
|
Ayah 37:89 الأية
فَقَالَ إِنِّي سَقِيمٌ
Swahili
Akasema: Hakika mimi ni mgonjwa!
|
Ayah 37:90 الأية
فَتَوَلَّوْا عَنْهُ مُدْبِرِينَ
Swahili
Nao wakamwacha, wakampa kisogo.
|
Ayah 37:91 الأية
فَرَاغَ إِلَىٰ آلِهَتِهِمْ فَقَالَ أَلَا تَأْكُلُونَ
Swahili
Basi akaiendea miungu yao kwa siri, akaiambia: Mbona hamli?
|
Ayah 37:92 الأية
مَا لَكُمْ لَا تَنطِقُونَ
Swahili
Mna nini hata hamsemi?
|
Ayah 37:93 الأية
فَرَاغَ عَلَيْهِمْ ضَرْبًا بِالْيَمِينِ
Swahili
Kisha akaigeukia kuipiga kwa mkono wa kulia.
|
Ayah 37:94 الأية
فَأَقْبَلُوا إِلَيْهِ يَزِفُّونَ
Swahili
Basi wakamjia upesi upesi.
|
Ayah 37:95 الأية
قَالَ أَتَعْبُدُونَ مَا تَنْحِتُونَ
Swahili
Akasema: Hivyo mnaviabudu vitu mnavyo vichonga wenyewe?
|
Ayah 37:96 الأية
وَاللَّهُ خَلَقَكُمْ وَمَا تَعْمَلُونَ
Swahili
Na hali Mwenyezi Mungu ndiye aliye kuumbeni nyinyi na hivyo mnavyo vifanya!
|
Ayah 37:97 الأية
قَالُوا ابْنُوا لَهُ بُنْيَانًا فَأَلْقُوهُ فِي الْجَحِيمِ
Swahili
Wakasema: Mjengeeni jengo, na kisha mtupeni motoni humo!
|
Ayah 37:98 الأية
فَأَرَادُوا بِهِ كَيْدًا فَجَعَلْنَاهُمُ الْأَسْفَلِينَ
Swahili
Basi walitaka kumfanyia vitimbi, lakini tukawafanya wao ndio wa chini.
|
Ayah 37:99 الأية
وَقَالَ إِنِّي ذَاهِبٌ إِلَىٰ رَبِّي سَيَهْدِينِ
Swahili
Na akasema: Hakika mimi nahama, nakwenda kwa Mola wangu Mlezi; Yeye ataniongoa.
|
Ayah 37:100 الأية
رَبِّ هَبْ لِي مِنَ الصَّالِحِينَ
Swahili
Ewe Mola wangu Mlezi! Nitunukie aliye miongoni mwa watenda mema.
|
Ayah 37:101 الأية
فَبَشَّرْنَاهُ بِغُلَامٍ حَلِيمٍ
Swahili
Basi tukambashiria mwana aliye mpole.
|
Ayah 37:102 الأية
فَلَمَّا بَلَغَ مَعَهُ السَّعْيَ قَالَ يَا بُنَيَّ إِنِّي أَرَىٰ فِي الْمَنَامِ
أَنِّي أَذْبَحُكَ فَانظُرْ مَاذَا تَرَىٰ ۚ قَالَ يَا أَبَتِ افْعَلْ مَا تُؤْمَرُ
ۖ سَتَجِدُنِي إِن شَاءَ اللَّهُ مِنَ الصَّابِرِينَ
Swahili
Basi alipo fika makamo ya kwenda na kurudi pamoja naye, alimwambia: Ewe
mwanangu! Hakika mimi nimeona usingizini kuwa ninakuchinja. Basi angalia wewe,
waonaje? Akasema: Ewe baba yangu! Tenda unavyo amrishwa, utanikuta mimi,
Inshallah, katika wanao subiri.
|
Ayah 37:103 الأية
فَلَمَّا أَسْلَمَا وَتَلَّهُ لِلْجَبِينِ
Swahili
Basi wote wawili walipo jisalimisha, na akamlaza juu ya kipaji.
|
Ayah 37:104 الأية
وَنَادَيْنَاهُ أَن يَا إِبْرَاهِيمُ
Swahili
Tulimwita: Ewe Ibrahim!
|
Ayah 37:105 الأية
قَدْ صَدَّقْتَ الرُّؤْيَا ۚ إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجْزِي الْمُحْسِنِينَ
Swahili
Umekwisha itimiliza ndoto. Hakika hivi ndivyo tunavyo walipa wanao tenda mema.
|
Ayah 37:106 الأية
إِنَّ هَٰذَا لَهُوَ الْبَلَاءُ الْمُبِينُ
Swahili
Hakika haya ni majaribio yaliyo dhaahiri.
|
Ayah 37:107 الأية
وَفَدَيْنَاهُ بِذِبْحٍ عَظِيمٍ
Swahili
Basi tukamtolea fidia kwa dhabihu mtukufu.
|
Ayah 37:108 الأية
وَتَرَكْنَا عَلَيْهِ فِي الْآخِرِينَ
Swahili
Na tukamwachia (sifa njema) kwa watu walio kuja baadaye.
|
Ayah 37:109 الأية
سَلَامٌ عَلَىٰ إِبْرَاهِيمَ
Swahili
Iwe salama kwa Ibrahim!
|
Ayah 37:110 الأية
كَذَٰلِكَ نَجْزِي الْمُحْسِنِينَ
Swahili
Hivi ndivyo tunavyo walipa wanao fanya mema.
|
Ayah 37:111 الأية
إِنَّهُ مِنْ عِبَادِنَا الْمُؤْمِنِينَ
Swahili
Hakika yeye ni katika waja wetu walio amini.
|
Ayah 37:112 الأية
وَبَشَّرْنَاهُ بِإِسْحَاقَ نَبِيًّا مِّنَ الصَّالِحِينَ
Swahili
Na tukambashiria kuzaliwa Is-haqa, naye ni Nabii miongoni mwa watu wema.
|
Ayah 37:113 الأية
وَبَارَكْنَا عَلَيْهِ وَعَلَىٰ إِسْحَاقَ ۚ وَمِن ذُرِّيَّتِهِمَا مُحْسِنٌ
وَظَالِمٌ لِّنَفْسِهِ مُبِينٌ
Swahili
Na tukambarikia yeye na Is-haqa. Na miongoni mwa dhuriya zao walitokea wema na
wenye kudhulumu nafsi zao waziwazi.
|
Ayah 37:114 الأية
وَلَقَدْ مَنَنَّا عَلَىٰ مُوسَىٰ وَهَارُونَ
Swahili
Na kwa hakika tuliwafanyia hisani Musa na Haruni.
|
Ayah 37:115 الأية
وَنَجَّيْنَاهُمَا وَقَوْمَهُمَا مِنَ الْكَرْبِ الْعَظِيمِ
Swahili
Na tukawaokoa wao na watu wao kutokana na dhiki kubwa.
|
Ayah 37:116 الأية
وَنَصَرْنَاهُمْ فَكَانُوا هُمُ الْغَالِبِينَ
Swahili
Na tukawanusuru; na wakawa wao ndio wenye kushinda.
|
Ayah 37:117 الأية
وَآتَيْنَاهُمَا الْكِتَابَ الْمُسْتَبِينَ
Swahili
Na tukawapa wawili hao Kitabu kinacho bainisha.
|
|